Wednesday, April 19, 2017

UTALII WA BALOON WAWA KIVUTIO KIKUBWA KATIKA HIFADHI YA TAIFA YA SERENETI


Kikapu maalumu kinachotumika katika Baloon kwa ajili ya kubeba watalii kikishushwa katika eneo la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kwa ajili ya Utalii wa Baloon.
Waandaaji wa Baloon wakifanya maandalizi ya kuliandaa Baloon hilo kwa ajili ya kubeba wageni wakati wa maandalizi ya kutalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Rubani wa Baloon linalo milikiwa na Kampuni ya Serengeti Balon Safari  ,Masoud Mohamed akitoa maelekezo kwa crew yake wakati wa maandalizi ya balon hiyo.
Watangazaji wa Kipindi cha Clouds 360 James Tupatupa na Sam Sasali wakiwa mbele ya Baloon wakati liwekewa hewa kabla ya kuanza safari ya utalii.
Baloon likiwekewa hewa .
Sehemu ya ndani ya Baloon ikionekana wakati likijazwa hewa kabla ya kuanza safari.
Baloon ikijazwa hewa kabla ya kuanza safari ya Utalii.
Rubani wa Baloon Masoud Mohamed akiruhusu gesi kwa ajili ya kuchoma Oxygen wakati wakiandaa Baloon kwa ajili ya kuanza safari ya utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Seengeti.
Baadhi ya Wageni wakifurahia jambo na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi ya Taifa ya Serengeti,William Mwakilema walipokuwa wamepanda Baloon kuzunguka katika maeneo mbalimbali ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Rubani wa Baloon ,Masoud Mohamed akiongoza chombo hicho kupita maeneo mbalimbali ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Baadhi ya wageni wakiwemo Wanahabri wakiwa katika kikapu maalum kinachobebwa na Baloon .
Baloon likiwa angani ambapo watalii wamekuwa akifanya utalii huu wa aina yake unaofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Msafara wa Pundamilia ukiwa kwenye uwanda wa nyasi fupi ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.
Muonekanao wa ndani wa Baloon wakati likiwa angani.
Baadhi ya wageni wakiwemo wanahabari walipanda Baloon kwa ajili ya kufanya utalii katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.
AA
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Samia Suluhu Hassan akizungumza na wajumbe wa Kamati tekelezaji za UWT ngazi za Wilaya, Mikoa na Taifa Unguja, huko Afisi Kuu Kisiwandui.
…………
NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR.
JUMUIYA ya Wanawake wa CCM (UWT) wametakiwa  kutumia uwezo, weledi, nguvu na ushawishi waliokuwa nao kisiasa kuhakikisha Chama cha Mapinduzi kinafanikisha  kwa ufanisi  Uchaguzi wa ndani ya Chama ili ipatikane timu imara ya viongozi watakaofanikisha   Ushindi wa Dola katika Uchaguzi Mkuu 2020.
Nasaha hizo zimetolewa na Mjumbe wa Kamati Kuu wa CCM, Mh. Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na Wajumbe wa Kamati Tekelezaji  wa ngazi za Wilaya, Mikoa hadi Taifa
wa UWT, huko Afisi Kuu CCM Kisiwandui Zanzibar alipohitimisha ziara yake ya kuimarisha Chama hicho nchini.
Alifafanua kwamba UWT wanatakiwa kwa mstari wa mbele kuhakikisha kila hatua ya uchaguzi huo inafanyika kwa ufanisi kwa lengo la kupata jopo la viongozi na watendaji waadilifu na wenye uwezo wa kusoma alama za nyakati kisiasa na kijamii.
Pia aliendelea kueleza  kwamba  wanawake wa Umoja huo ni miongoni mwa rasilimali watu wanaotakiwa kukitumikia chama kwa bidii ili kiweze kufikia malengo yake ya  kuendeleza ushindi wa Dola kwa kila uchaguzi mkuu wa kisiasa.
Mh. Ambaye pia ni Makamo wa Pili wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, aliwambia Akina Mama hao kwamba mikakati hiyo itafanyika kwa ufanisi endapo kila mtu ndani ya umoja huo atakuwa tayari kutumia kipaji chake cha kisiasa kuhakikisha analinda na kutetea maslahi ya chama kwa vitendo.
“ Wanawake tutumieni uwezo wetu katika kujenga ushawishi na hamasa kwa kuongeza wanachama wapya watakaokubali kuwa na itikadi ya kweli ya CCM.
Pamoja na mipango yetu ya kuimarisha chama tusisahau kuzidisha umoja na upendo miongoni mwetu kwa kuacha baadhi ya mambo yasiyofaa na tunayohisi hayana maslahi na Chama pamoja na jumuiya yetu”, alisema Mh.Samia na kuongeza kuwa lazima viongozi waliopewa dhamana ndani ya umoja huo wafanye kazi kwa bidii  ili wananchi waendelee kujivunia uwepo wa Chama hicho katika medali za kisisasa Visiwani Zanzibar.
Pamoja na hayo alisisitiza umuhimu wa wanachama wa chama hicho hasa Wazee kuwarithisha watoto wao  miongozo na itikadi za ASP ambayo ni CCM, ili waweze kukua wakiwa katika misingi ya weledi na ukada wa kweli ambazo ni nyenzo zitakazowasaidia pindi watakapokuwa  viongozi wa chama na serikali wa baadae.
Hata hivyo aliwataka viongozi na watendaji kuhakikisha takwimu za wanachama wanazoratibu zinakuwa sahihi ili ziweze kusaidia katika tathimini mbali mbali za kisiasa nchini hasa kabla na baada ya uchaguzi.
Akitoa ufafanuzi juu ya Uchaguzi wa chama unaoendelea kwa hatua ya uchukuaji wa fomu kwa ngazi ya Matawi na mashina, Katibu wa NEC, Idara ya Itikadi na Uenezi CCM Zanzibar, Bi. Waride Bakar Jabu amesema nafasi zinazochukuliwa fomu kwa mtu mmoja ni zile za kiutendaji ambazo ni Katibu na Mwenyekiti lakini nafasi zingine zote zilizobaki zinatakiwa kuchukuliwa fomu zaidi ya mtu mmoja.
 Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa UWT Zanzibar , Bi. Tunu Juma Kondo alisema umoja huo umekuwa ukishiriki ipasavyo katika majukumu mbali mbali ya chama na kuhakikisha yanafanyikana na kukamilika kwa wakati.
Aidha  aliahidi kwamba umoja huo utafanya kila linalowezekana kuhakikisha Uchaguzi ndani ya taasisi hiyo unafanyika vizuri kwa mujibu wa kanuni na miongozo ya Katiba ya CCM ya mwaka 1977 pamoja na marekebisho yake.
Naye  Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Bi. Maudline Cyrus Castico, akitoa ufafanuzi juu ya kesi za udhalilishaji wa kijinzia nchini, alisema kwa sasa wanaendelea na kutoa elimu kwa jamii juu ya kuwa na muamuko wa kutoa ushahidi mahakamani huku wakiandaa mikakati imara ya kusimamia vyombo vya kisheria vitende haki kwa watu wanaofanya uhalifu huo.
Kwa upande wao viongozi mbali mbali wa umoja huo kutoka Mikoa  ya Zanzibar kichama walipewa fursa ya kutoa maoni na ushauri wao, ambao walipendekeza kwamba CCM kupitia idara husika ziendeleze madarasa ya Itikadi kwa vijana mbali mbali ili kupata viongozi wa baadae walioiva kisiasa.
Akizungumza  miongoni mwa waasisi wa ASP, Bi.Asha Simba aliwataka vijana wa Chama hicho kuvaa joho la Vijana wa enzi za ASP waliokomboa  Zanzibar  kutoka katika mikono ya utawala wa kimabavu, na wao wafuate nyayo hizo kuendeleza heshima ya CCM kwa sasa.

No comments :

Post a Comment