KAMISHINA
wa Operesheni na Mafunzo wa jeshi la polisi,
Nsato Marijani, akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Wizara ya
Mambo ya Ndani, wakati akitoa tamko kuhusu operesheni itakayoendeshwa na jeshi
hilo ya kuwasaka wahalifu waliohusika na mauaji ya Askari nane katika msitu wa
Jaribu Mpakani Mkoa wa Pwani juzi. Kushoto ni Msemaji wa Jeshi la Polisi,
Advera Bulimba ''Tunaomba wananchi watusamehe kwa operesheni hii tunayokwenda
kuianza, kwani askari wanane ni wengi sana na hatutakuwa na msalie mtume kwa hili,
wameanza sisi tunamaliza, na jana ilikuwa ni 8 - 4, lakini tukianza nawaambia
mabao yetu yatakuwa ni zaidi yao'';. alisema Marijani Aidha Marijani ametangaza
kuwa eneo hilo ni marufuku waendesha pikipiki kupita zaidi ya saa kumi na moja
jioni. Kaa nasi
(KWA HISANI YA SUFIANI MAFOTO BLOG)
Tarehe
11 Aprili, 2017, Mhe. Balozi Wilson Mutaganywa Kajumula Masilingi
aliwasilisha hati za utambulisho kwa Mhe. Enrique Peña Nieto, Rais wa
Mexico, Ikulu Katika Jiji la Mexico. Hafla hiyo ilishuhudiwa na Mhe.
Luis Videgaray Caso, Waziri wa Mambo ya Nje wa Serikali ya Mexico na mke
wa Mhe. Balozi, Marystella Masilingi. Wakati wa kuwasilisha hati hizo,
Mhe. Balozi alipata fursa ya kuongea na Mhe. Rais wa Mexico na kumpa
salam kutoka kwa Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.
Mhe.
Enrique Peña Nieto, Rais wa Mexico akimpokea Mhe. Balozi Wilson M. K.
Masilingi, Balozi mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Mexico. Katikati akitizama ni Mhe. Luis Videgaray Caso, Waziri wa Mambo
ya Nje wa Mexico.
Mhe.
Enrique Peña Nieto, Rais wa Mexico na Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi,
Balozi mpya wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, nchini Mexico.
Kutoka
kushoto, Mhe. Balozi Wilson M. Masilingi na Mhe. Enrique Peña Nieto,
Rais wa Mexico; Mke wa Balozi Bi. Marystella E. Masilingi na Mhe. Luis
Videgaray, Waziri wa Mambo ya Nje wa Mexico.
Mhe.
Balozi Wilson M. K. Masilingi na Mke wake Bi. Marystella Masilingi
(kulia) na Bi. Swahiba Mndeme, Mkuu wa Utawala wa Ubalozi (kushoto)

No comments :
Post a Comment