Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akiongoza maandamano ya wasanii wa Bongo Move kutoka ofisi
ya mkuu wa mkoa huyo kwenda Kariakoo ambako mkutano mkubwa umefanyika
leo ukiwa na lengo la kuzindua kampeni kabambe ya kupambana na mawakala
wa kuchapisha na kuuza filamu za nje ya nchi zinazoingizwa kinyume cha
utaratibu na sheria huku zikiwa hazilipiwi kodi, Jambo ambali
linafifisha biashara ya filamu za wasanii wa Tanzania kutokana na kuuzwa
kwa bei ya chini ukilinganisha na filamu za nyumbani ambazo zinalipiwa
kila kodi kwa mujibu wa sheria
Makonda amewatahadharisha watu
wote wanaoingiza filamu kutoka nje ya nchi bila kulipa kodi wala huku
wakijua kwamba hawana mikataba ya kusambaza au kuuza kazi za wasanii hao
, amewataka wauzaji wadogo wadogo kujiunga vikundi na kusajiliwa ili
wapewe vitambulisho ili watambulike wakati wanafanya kazi za kuuza kazi
hizo za sanaa zikiwemo Filamu na nyimbo.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie
wakiimba nyimbo za kumshangilia Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Bw. Paul
Makonda wakati wakiwa kwenye maandamano kuelekea Kariakoo ambako
kumefanyika mkutano mkubwa wa uzinduzi wa kampeni ya kuzuia uuzaji wa
kaza za filamu bila kufuata utaratibu na sheria za nchi.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaa Paul Makonda akiwasili katika eneo la mkutano.
Baadhi ya wasanii pamoja na wananchi wakiwa katika mkutano huo.
Waigizaji Kajala Masanja na Dokii wakiwa katika mkutano huo.
Katibu Tawala wa mkoa wa Dar es salaam Theresia Mmbando akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuhutubia.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya wasanii wa Bongo Movie na wananchi wakiwa wamejitokeza kwa wingi katika mkutano huo.
Mkuu wa wilaya ya Ilala Mh Sophia Mjema akizungua katika mkutano huo.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda katikati akimsikiliza Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Bi. Bi. Joyce Fissoo wakati akizungumza katika mkutano huo.
Kamanda Wa Polisi Kanda Maalum ya
Dar es salaam Kamishna Simon Sirro akizungumza katika mkutano huo
ambapo ameonya wale wote wanaouza filamu za Ngono na za kigaidi amesema
hao watapambana na mkono wa dola.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh.
Paul Makonda akizungumza katika mkutano huo na kupiga marufuku uuzaji
na usambazaji wa filamu za nje bila kufuata utaratibu na sheria za nchi
na kuagiza uuzwaji wa filamu za Ngono na za Kigaidi ni marufuku na
atakayekamatwa akiuza atakumbana na mkono wa sheria
No comments :
Post a Comment