Tuesday, March 28, 2017

WAZIRI WA SHERIA NA KATIBA, PROF. KABUDI ARIPOTI OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

ZA 1Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akiangaalia kadi ya Pongezi iliyoasiniwa na watumishi wa wizara mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma
 ZA
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akipokea shada la maua kutoka kwa mtumishi Joyce Mtuma mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma.

ZA 2
WaziriwaKatibanaSheriaMhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana naNaibu Katibu Mkuu Bw. Amon Mpanju mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma
ZA 3
Waziri wa Katiba na SheriaMhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana na Jaji mfawidhi Kanda ya Dodoma Mhe. Mwanaisha Kwariko alipowasili Wizarani mjini Dodoma
ZA 4
WaziriwaKatibanaSheriaMhe. Prof.PalamagambaKabudiakisikilizamaelezombalimbalialipokutananawatendajiwaWizaranaMahakamakatikaukumbiwamikutanoWizaranimjini Dodoma.
WaziriwaKatibanaSheriaProf.PalamagambaKabudiamewasilikatikaOfisizaMakaomakuuyaWizarazilizokondaniya Chuo Kikuu cha Dodoma nakulakiwanawatumishiwaWizarawaliokomakaomakuuyaSerikalimjini Dodoma. Prof Kabudialiapishwatarehe24/03/2017 Ikulujijini Dar Es SalaamkuchukuanafasihiyobaadayaMhe.RaiskufanyamabadilikomadogokwenyeBaraza la MawaaziriambapoDkt. Harrison MwakyembealihamishiwaWizarayaHabari, Utamaduni, SanaanaMichezo.
NjeyaOfisizaWizaraMhe. Prof. PalamagambaKabudialilakiwanaNaibuKatibuMkuu, Bw. AmonMpanju, MkurugenziwaUtawalanaRasilimaliWatuBw. AloyceMwogofi, JajiMfawidhi Kanda ya Dodoma nawafanyakaziwenginewaWizarawaliopoMakaoMakuuyaSerikalimjini Dodoma.

QQ
Mkurugenzi Msaidizi Masuala Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Venance Manori akiwa katika picha ya pamoja na waandaaji wa warsha ya kuwawezesha Maafisa Waandamizi wa Serikali kutoka nchi sita za Afrika katika kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia katika elimu kutoka shirika la Plan International- Tanzania, Global Partnership for Education (GPE), Dubai Cares pamoja na United Nations Girls’ Education Initiative (UNGEI) mara baada ya ufunguzi wa warsha hiyo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
QQ 1
Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Plan International- Tanzania, Jorgen Haldorsen akitoa neno fupi kwa ajili ya kuwakaribisha Maafisa Waandamizi wa Serikali kutoka nchi sita za Afrika katika ufunguzi wa warsha ya kuwawezesha kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia katika elimu. Ufunguzi wa warsha hiyo ulifanyika jana jijini Dar es Salaam.
QQ 2
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa Serikali wanaohusika na elimu kutoka nchi sita za Afrika wakisikiliza hotuba ya Mkurugenzi Msaidizi Masuala Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (hayupo pichani), Venance Manori wakati wa ufunguzi wa warsha ya kuwawezesha maafisa hao katika kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia katika elimu.Warsha hiyo ya siku tatu imefunguliwa jana jijini Dar es Salaam.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Serikali imejipanga kutengeneza mwongozo wa kuwarudisha shuleni wanafunzi waliopata mimba wakiwa masomoni ili kuhakikisha wanapata elimu hadi kufikia ngazi za juu.
Hayo yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi Masuala Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Venance Manori alipokuwa akifungua warsha ya kuwawezesha Maafisa Waandamizi wa Serikali kutoka nchi sita za Afrika katika kutengeneza mipango inayozingatia jinsia katika elimu kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Prof. Joyce Ndalichako.
Manori amesema Serikali ya Tanzania inajitahidi kuzingatia jinsia katika utoaji wa elimu ambapo takwimu zinaonyesha kuwa elimu ya Msingi na Sekondari uwiano wake ni moja kwa moja japo kuwa idadi ya wasichana hupungua kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakumba hivyo lengo la warsha hiyo ni kuwasaidia wadau kuweka mipango ya elimu inayozingatia usawa wa kijinsia.
“Serikali yetu imejipanga kuhakikisha wasichana wanapata elimu hadi ngazi za juu lakini mpango huo unakumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za mimba na ndoa za utotoni hivyo ili kuhakikisha mtoto wa kike anafikia ngazi za juu za elimu tuko kwenye mchakato wa kuandaa mwongozo kwa ajili ya wanafunzi waliopata mimba wakiwa bado wanasoma kupata nafasi ya kuendelea na masomo,”alisema Manori.
Mkurugenzi Msaidizi amezitaja changamoto zingine zinazowapelekea wanafunzi wa kike kuacha shule zikiwemo za umaskini, mazingira rafiki ya kusomea, mila na desturi zinazomkataza msichana kupata nafasi ya kusoma pamoja na kukosa muda wa kujisomea kwa sababu ya kufanya kazi nyingi wanaporudi majumbani.
Manori ametoa rai kwa Watanzania kuelewa kuwa kila mtoto ana haki na wajibu wa kupata elimu bila kujali jinsia pia ameiasa jamii kuacha kuwaozesha wasichana wenye umri chini ya miaka 18 ili waweze kufikia malengo yao waliyojipangia.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Plan International- Tanzania, Jorgen Haldorsen ameahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha mipango ya elimu nchini inaangalia usawa wa kijinsia kwa kuwa ni njia moja wapo itakayochochea maendeleo ya elimu kwa watoto wa kike.
“Warsha hii imeandaliwa kwa ajili ya wadau wote kutoa mawazo yao juu ya changamoto za usawa wa kijinsia zinazoikumba sekta ya elimu pamoja na kuwapa fursa wadau hao kushauriana kuhusu mikakati mbalimbali ya kutatua changamoto hizo ili kuinua sekta ya elimu sio tu kwa Tanzania bali kwa Afrika nzima,”alisema Haldorsen.
Haldorsen ameongeza kuwa mfumo wa elimu umetambua uhusiano uliopo kati ya elimu na usawa wa kijinsia ndio maana wadau wa masuala ya elimu wa Serikali kutoka katika baadhi ya nchi za Afrika wameamua kuungana kwa pamoja kujadili juu ya tathmini, mpangilio na ufuatiliaji wa elimu unayozingatia jinsia.
Tanzania imekua nchi ya kwanza kuendesha warsha hiyo ya siku tatu iliyoshirikisha maafisa waandamizi wa Serikali wanaoshughulikia mipango ya elimu kutoka nchi za Mozambique, Zambia, Malawi, Uganda, Zanzibar na Tanzania Bara.
Imeandaliwa kwa ushirikiano wa shirika la Plan International- Tanzania, Global Partnership for Education (GPE), Dubai Cares pamoja na United Nations Girls’ Education Initiative (UNGEI).


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akipanda mti wa kumbukumbu nyumbani kwa Hayati Edward Moringe Sokoine. Waziri Makamba yuko katika ziara ya kikazi Mkoani Arusha na alitembelea msitu wa Enguiki na Lendikinya kisha alizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara.

 Faida ya Hifadhi endelevu ya Mazingira. Pichani ni eneo la Ngaresero Wilaya ya Meru ambapo kuna uhifadhi mzuri wa mazingira. Hata hivyo eneo hilo limeanza kuvamiwa na wananchi kwa shughuli za kibinadamu na kuhatarisha uhai wake. Waziri Makamba ametembelea eneo hilo na kumtaka Bw. Timoth Leach mmiliki wa Ngaresero Mountain Lodge kufanya ukaguzi wa mazingira mara moja ili kubaina matumizi sahihi ya rasilimali maji. 

 
Mkurugenzi wa Hope Art Factory, Hellen Tegga akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya wanawake ya Ujasiliamali , Ainde Ndanshau yaliyofanyika katika ukumbi wa Milllenium Tower jijini Dar es Salaam.

 
Mkurugenzi wa Hope Art Factory Hellen Tegga akizungumza katika mafunzo ya wanawake juu ya ujasiliamali na kupaza sauti yaliyofanyika Millenium Tower jijini Dar es Salaam.
 
Mratibu wa Mfuko Graca Machel , Manuel Akinyi akitoa mada katika mafunzo ya wanawake juu ya ujasiliamali na kupaza sauti yaliyofanyika Millenium Tower jijini Dar es Salaam.
 
Mkurugenzi wa Hope Art Factory, Hellen Tegga akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya wanawake ya Ujasiliamali , Ainde Ndanshau yaliyofanyika katika ukumbi wa Milllenium Tower jijini Dar es Salaam.

 
Mkurugenzi wa Hope Art Factory ,Hellen Tegga akimkabidhi cheti cha ushiriki wa mafunzo ya wanawake ya Ujasiliamali , Mrcy Mchechu yaliyofanyika katika ukumbi wa Milllenium Tower jijini Dar es Salaam.
 
Washiriki wakiwa katika mafunzo ya wanawake yaliofanyika katika ukumbi wa Milleniumm Tower jijini Dar es Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka, Globu ya Jamii)
 
Picha ya pamoja.

Mtanzania Lilian Danieli mwenye kampuni yake ya NASHONA amefungua duka la nguo za Kitanzania Goldsboro jimbo la North Carolina nchini Marekani. Uzinduzi wa duka hilo ambalo lipo Center Street katikati ya mji huo wa Goldsboro ulifanyika siku Jumamosi March 25, 2017. Anuani kamili ya duka ni 119 Center Street, Goldsboro, NC na simu ya dukani ni 919 947 1273.

Katika duka hilo nguo mbalimbali vitenge toka Tanzania ikiwa asilimia 90 ameshona yeye mwenyewe na baadhi ya vingine kuja toka Tanzania. Duka litakua linafunguliwa siku ya Jumanne mpaka Jumamosi. Picha na Vijimambo Blog na Kwanza Production
Baadhi ya wateja waliokuwepo dukani hapo siku ya uzinduzi wa duka hilo Jumamosi March 25, 2017 Goldsboro, North Carolina nchini Marekani.
Lilian Daniel Kulia akikinja moja ya nguo zilizo nunuliwa na mmoja ya wateja wake siku ya uzinduzi wa duka lake la nguo za kiTanzania lililozinduliwa siku ya Jumamosi Machi 25, 2017.
Kushoto ni Serena Danieli akisaidiana na dada yake Imani Danieli katika kuhakikisha mahesabu ya duka yanaenda sawa.
Lilian Danieli akiwa na mmoja ya wateja wake akiwaonyesha nguo zake na kuwapa maelekezo.
Mmoja ya wateja akilipia kitu alichonunua.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi.



Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ,akimvisha cheo kipya Kamishna wa Uhamiaji Utawala na Fedha,  Edward Peter Chogero  katika hafla iliyofanyika leo Machi 28, 2017 katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Anayeshuhudia ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji Chrispin Ngonyani. Tukio hili linehudhuriwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira  na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi  Hassan Simba Yahaya.


Kamishna mpya wa Uhamiaji Divisheni ya Sheria Hannerole Morgan Manyanga akila kiapo cha Utii mbele ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr.  Anna Peter Makakala katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   na Naibu  Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan Simba Yahaya.


Kamishna wa Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma , Jaji Mstaafu Harold Nsekela (wakwanza kushoto), akiwaongoza  Makamishna wapya wa Uhamiaji kuapa  kiapo cha Maadili ya Viongozi wa  Utumishi wa Umma baada ya Makamishna hao wapya kuvalishwa vyeo vipya katika hafla iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.


Makamishna wapya wa Uhamiaji wakisaini Fomu za Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya Makamishna hao kula kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Utumishi wa Umma, katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.


Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira  akitoa maelekezo kwa Makamishna wapya wa Uhamiaji wakati wa hafla ya kuvikwa Vyeo Vipya   iliyofanyika  leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.



Katibu Mkuu wa Wizara  ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest Rwegasira   akizungumza jambo na Makamishna wapya wa Uhamiaji baada ya kumalizika shughuli ya kuapishwa Makamishna hao  leo katika viwanja vya Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.

No comments :

Post a Comment