Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akiangaalia kadi ya
Pongezi iliyoasiniwa na watumishi wa wizara mara baada ya kuwasili
Wizarani mjini Dodoma
Waziri
wa Katiba na Sheria Mhe. Prof.Palamagamba Kabudi akipokea shada la maua kutoka
kwa mtumishi Joyce Mtuma mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma.
WaziriwaKatibanaSheriaMhe.
Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana naNaibu Katibu Mkuu Bw. Amon
Mpanju mara baada ya kuwasili Wizarani mjini Dodoma
Waziri
wa Katiba na SheriaMhe. Prof.Palamagamba Kabudi akisalimiana na Jaji
mfawidhi Kanda ya Dodoma Mhe. Mwanaisha Kwariko alipowasili Wizarani
mjini Dodoma
WaziriwaKatibanaSheriaMhe.
Prof.PalamagambaKabudiakisikilizamaelezombalimbalialipokutananawatendajiwaWizaranaMahakamakatikaukumbiwamikutanoWizaranimjini
Dodoma.
WaziriwaKatibanaSheriaProf.PalamagambaKabudiamewasilikatikaOfisizaMakaomakuuyaWizarazilizokondaniya
Chuo Kikuu cha Dodoma
nakulakiwanawatumishiwaWizarawaliokomakaomakuuyaSerikalimjini Dodoma.
Prof Kabudialiapishwatarehe24/03/2017 Ikulujijini Dar Es
SalaamkuchukuanafasihiyobaadayaMhe.RaiskufanyamabadilikomadogokwenyeBaraza
la MawaaziriambapoDkt. Harrison MwakyembealihamishiwaWizarayaHabari,
Utamaduni, SanaanaMichezo.
NjeyaOfisizaWizaraMhe.
Prof. PalamagambaKabudialilakiwanaNaibuKatibuMkuu, Bw. AmonMpanju,
MkurugenziwaUtawalanaRasilimaliWatuBw. AloyceMwogofi, JajiMfawidhi Kanda
ya Dodoma nawafanyakaziwenginewaWizarawaliopoMakaoMakuuyaSerikalimjini
Dodoma.
Mkurugenzi
Msaidizi Masuala Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na
Teknolojia, Venance Manori akiwa katika picha ya pamoja na waandaaji wa
warsha ya kuwawezesha Maafisa Waandamizi wa Serikali kutoka nchi sita za
Afrika katika kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia
katika elimu kutoka shirika la Plan International- Tanzania, Global
Partnership for Education (GPE), Dubai Cares pamoja na United Nations
Girls’ Education Initiative (UNGEI) mara baada ya ufunguzi wa warsha
hiyo uliofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
Mkuu wa shirika la Plan International- Tanzania, Jorgen Haldorsen
akitoa neno fupi kwa ajili ya kuwakaribisha Maafisa Waandamizi wa
Serikali kutoka nchi sita za Afrika katika ufunguzi wa warsha ya
kuwawezesha kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia katika
elimu. Ufunguzi wa warsha hiyo ulifanyika jana jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya Maafisa Waandamizi wa Serikali wanaohusika na elimu kutoka nchi sita
za Afrika wakisikiliza hotuba ya Mkurugenzi Msaidizi Masuala Mtambuka
kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia (hayupo pichani), Venance
Manori wakati wa ufunguzi wa warsha ya kuwawezesha maafisa hao katika
kutengeneza mipango inayozingatia usawa wa kijinsia katika elimu.Warsha
hiyo ya siku tatu imefunguliwa jana jijini Dar es Salaam.
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO.
Serikali
imejipanga kutengeneza mwongozo wa kuwarudisha shuleni wanafunzi
waliopata mimba wakiwa masomoni ili kuhakikisha wanapata elimu hadi
kufikia ngazi za juu.
Hayo
yamesemwa jana Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Msaidizi Masuala
Mtambuka kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Venance Manori
alipokuwa akifungua warsha ya kuwawezesha Maafisa Waandamizi wa Serikali
kutoka nchi sita za Afrika katika kutengeneza mipango inayozingatia
jinsia katika elimu kwa niaba ya Waziri wa Wizara hiyo Prof. Joyce
Ndalichako.
Manori
amesema Serikali ya Tanzania inajitahidi kuzingatia jinsia katika
utoaji wa elimu ambapo takwimu zinaonyesha kuwa elimu ya Msingi na
Sekondari uwiano wake ni moja kwa moja japo kuwa idadi ya wasichana
hupungua kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakumba hivyo lengo la
warsha hiyo ni kuwasaidia wadau kuweka mipango ya elimu inayozingatia
usawa wa kijinsia.
“Serikali
yetu imejipanga kuhakikisha wasichana wanapata elimu hadi ngazi za juu
lakini mpango huo unakumbwa na changamoto mbalimbali zikiwemo za mimba
na ndoa za utotoni hivyo ili kuhakikisha mtoto wa kike anafikia ngazi za
juu za elimu tuko kwenye mchakato wa kuandaa mwongozo kwa ajili ya
wanafunzi waliopata mimba wakiwa bado wanasoma kupata nafasi ya
kuendelea na masomo,”alisema Manori.
Mkurugenzi
Msaidizi amezitaja changamoto zingine zinazowapelekea wanafunzi wa kike
kuacha shule zikiwemo za umaskini, mazingira rafiki ya kusomea, mila na
desturi zinazomkataza msichana kupata nafasi ya kusoma pamoja na kukosa
muda wa kujisomea kwa sababu ya kufanya kazi nyingi wanaporudi
majumbani.
Manori
ametoa rai kwa Watanzania kuelewa kuwa kila mtoto ana haki na wajibu wa
kupata elimu bila kujali jinsia pia ameiasa jamii kuacha kuwaozesha
wasichana wenye umri chini ya miaka 18 ili waweze kufikia malengo yao
waliyojipangia.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Plan International- Tanzania,
Jorgen Haldorsen ameahidi kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika
kuhakikisha mipango ya elimu nchini inaangalia usawa wa kijinsia kwa
kuwa ni njia moja wapo itakayochochea maendeleo ya elimu kwa watoto wa
kike.
“Warsha
hii imeandaliwa kwa ajili ya wadau wote kutoa mawazo yao juu ya
changamoto za usawa wa kijinsia zinazoikumba sekta ya elimu pamoja na
kuwapa fursa wadau hao kushauriana kuhusu mikakati mbalimbali ya kutatua
changamoto hizo ili kuinua sekta ya elimu sio tu kwa Tanzania bali kwa
Afrika nzima,”alisema Haldorsen.
Haldorsen
ameongeza kuwa mfumo wa elimu umetambua uhusiano uliopo kati ya elimu
na usawa wa kijinsia ndio maana wadau wa masuala ya elimu wa Serikali
kutoka katika baadhi ya nchi za Afrika wameamua kuungana kwa pamoja
kujadili juu ya tathmini, mpangilio na ufuatiliaji wa elimu
unayozingatia jinsia.
Tanzania
imekua nchi ya kwanza kuendesha warsha hiyo ya siku tatu
iliyoshirikisha maafisa waandamizi wa Serikali wanaoshughulikia mipango
ya elimu kutoka nchi za Mozambique, Zambia, Malawi, Uganda, Zanzibar na
Tanzania Bara.
Imeandaliwa
kwa ushirikiano wa shirika la Plan International- Tanzania, Global
Partnership for Education (GPE), Dubai Cares pamoja na United Nations
Girls’ Education Initiative (UNGEI).
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akipanda mti wa kumbukumbu nyumbani kwa Hayati Edward Moringe Sokoine. Waziri Makamba yuko katika ziara ya kikazi Mkoani Arusha na alitembelea msitu wa Enguiki na Lendikinya kisha alizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara. |
Faida ya Hifadhi endelevu ya Mazingira. Pichani ni eneo la Ngaresero Wilaya ya Meru ambapo kuna uhifadhi mzuri wa mazingira. Hata hivyo eneo hilo limeanza kuvamiwa na wananchi kwa shughuli za kibinadamu na kuhatarisha uhai wake. Waziri Makamba ametembelea eneo hilo na kumtaka Bw. Timoth Leach mmiliki wa Ngaresero Mountain Lodge kufanya ukaguzi wa mazingira mara moja ili kubaina matumizi sahihi ya rasilimali maji.
Mkurugenzi
wa Hope Art Factory Hellen Tegga akizungumza katika mafunzo ya wanawake
juu ya ujasiliamali na kupaza sauti yaliyofanyika Millenium Tower
jijini Dar es Salaam.
Mratibu
wa Mfuko Graca Machel , Manuel Akinyi akitoa mada katika mafunzo ya
wanawake juu ya ujasiliamali na kupaza sauti yaliyofanyika Millenium
Tower jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Hope Art Factory, Hellen Tegga akimkabidhi cheti cha ushiriki wa
mafunzo ya wanawake ya Ujasiliamali , Ainde Ndanshau yaliyofanyika
katika ukumbi wa Milllenium Tower jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi
wa Hope Art Factory ,Hellen Tegga akimkabidhi cheti cha ushiriki wa
mafunzo ya wanawake ya Ujasiliamali , Mrcy Mchechu yaliyofanyika katika
ukumbi wa Milllenium Tower jijini Dar es Salaam.
Washiriki
wakiwa katika mafunzo ya wanawake yaliofanyika katika ukumbi wa
Milleniumm Tower jijini Dar es Salaam. (Picha na Emmanuel Massaka, Globu
ya Jamii)
Picha ya pamoja.
Mtanzania
Lilian Danieli mwenye kampuni yake ya NASHONA amefungua duka la nguo za
Kitanzania Goldsboro jimbo la North Carolina nchini Marekani. Uzinduzi
wa duka hilo ambalo lipo Center Street katikati ya mji huo wa Goldsboro
ulifanyika siku Jumamosi March 25, 2017. Anuani kamili ya duka ni 119
Center Street, Goldsboro, NC na simu ya dukani ni 919 947 1273.
Katika
duka hilo nguo mbalimbali vitenge toka Tanzania ikiwa asilimia 90
ameshona yeye mwenyewe na baadhi ya vingine kuja toka Tanzania. Duka
litakua linafunguliwa siku ya Jumanne mpaka Jumamosi. Picha na Vijimambo
Blog na Kwanza Production
Baadhi
ya wateja waliokuwepo dukani hapo siku ya uzinduzi wa duka hilo
Jumamosi March 25, 2017 Goldsboro, North Carolina nchini Marekani.
Lilian Daniel Kulia akikinja moja ya
nguo zilizo nunuliwa na mmoja ya wateja wake siku ya uzinduzi wa duka
lake la nguo za kiTanzania lililozinduliwa siku ya Jumamosi Machi 25,
2017.
Kushoto ni Serena Danieli akisaidiana na dada yake Imani Danieli katika kuhakikisha mahesabu ya duka yanaenda sawa.
Lilian Danieli akiwa na mmoja ya wateja wake akiwaonyesha nguo zake na kuwapa maelekezo.
Mmoja ya wateja akilipia kitu alichonunua.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi.
Kamishna
Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala ,akimvisha cheo kipya Kamishna wa
Uhamiaji Utawala na Fedha, Edward Peter
Chogero katika hafla iliyofanyika leo Machi 28, 2017 katika
ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Anayeshuhudia
ni Naibu Kamishna wa Uhamiaji Chrispin Ngonyani. Tukio hili linehudhuriwa na
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja Jenerali Projest
Rwegasira na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan Simba Yahaya.
Kamishna
mpya wa Uhamiaji Divisheni ya Sheria Hannerole Morgan Manyanga akila kiapo cha
Utii mbele ya Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dr.
Anna Peter Makakala katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma. Hafla hiyo imehudhuriwa na Katibu Mkuu wa
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Meja
Jenerali Projest Rwegasira na
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Hassan
Simba Yahaya.
Kamishna
wa Tume ya Maadili ya Utumishi wa Umma , Jaji Mstaafu Harold Nsekela (wakwanza
kushoto), akiwaongoza Makamishna wapya
wa Uhamiaji kuapa kiapo cha Maadili ya
Viongozi wa Utumishi wa Umma baada ya Makamishna
hao wapya kuvalishwa vyeo vipya katika
hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano
wa Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Makamishna
wapya wa Uhamiaji wakisaini Fomu za Maadili ya Viongozi wa Umma baada ya Makamishna
hao kula kiapo cha Maadili ya Viongozi wa Utumishi wa Umma, katika hafla iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi
ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira
akitoa maelekezo kwa Makamishna wapya wa Uhamiaji wakati wa hafla ya
kuvikwa Vyeo Vipya iliyofanyika leo katika ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Dodoma.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Meja Jenerali Projest Rwegasira akizungumza jambo na Makamishna wapya wa Uhamiaji
baada ya kumalizika shughuli ya kuapishwa Makamishna hao leo katika viwanja vya Ofisi ya Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Dodoma.
No comments :
Post a Comment