Mwenyekiti wa Dar Jogging, Ramadhan Namkoveka akizungumza wakati wa Tamasha la vikundi vya Jogging Temeke.
Moja ya manjonjo ya wana-jogging wakati wa kufanya mazoezi. Manjonjo hayo uwasaidia kutokufikiria kuchoka.
Mwenyekiti wa Dar Jogging, Ramadhani Namkoveka akiwaongoza wenzake katika mbio hizo.
Wana-Jogging wakipasha viungo kabla ya kuanza kukimbia ‘mdogomdogo’.
Wana-Jogging wakifanya mazoezi
Wana Jogging wakifanya mazoezi.
…………..
Wanachama wa Umoja wa vilabu
vya jogging (Uvijo) umeomba uongozi wa Chama Cha Kuogelea nchini (TSA)
kuandaa mavunzo yamchezo wa kuogelea kwa vijana chipukizi.
Ombi hilo lilitolewa na wanachama
wa umoja huo wakati wa tamasha kubwa la vikundi vya
jogging
lililofanyika hivi karibuni kwenye uwanja wa Mwembe Yanga.
Katika tamasha hilo ambalo
lilianzia uwanja wa Taifa, wamia ya wanachama walisema kuwa ni wakati wa
wao kuanza kujifunza mchezo huo ili kuendeleza mazoezi kwa ajili ya
kuhimarisha afya zao.
Wanachama hao walisema kuwa mchezo
wa kuogelea ni mzuri kwa ajili ya mazoezi ya mwili kwani uwezesha
viungo vyote kutumika wakati wa mazoezi.
Mwenyekiti wa Dar Jogging,
Ramadhan Namkoveka ambaye pia ni katibu mkuu wa TSA alipokea ombi hilo
na kuahidi kulifisha kwa viongozi wenzake kwa akjili ya kutoewa maamuzi.
Wakati huo huo; Uvijo imeanzisha mkakati wa kuviinua kwa uchumi vikundi wanachama wake.
Mkoveka alisema kuwa kuanzia sasa
Uvijo ikitoa msaada wa fedha vilabu wanachama kwa lengo la kuendesha
miradi yao ya klabu, kukuza sekta ya michezo kwenye mazoezi na vifaa na
pamoja na kukuza upatikanaji wa ajira ndani ya vilabu rafiki vya uvijo.
Hii ni mara pili ndani ya
umoja huu ambapo mwaka jana waliweza kuichangia klabu ya Dar Jogging
kiasi kama kilichochangwa mwaka huu.
Vilabu wanachama wa Uvijo ni Dar
Jogging, Dovya Jogging, Tupo Jogging, Barafu Jogging, Mzimuni Jogging,
Tunajenga Jogging, Wasafi Jogging na Temeke Family.
Tamasha hilo lilifanikiwa kwa
msaada wa Times FM Radio, Ndanda Spring water, pamoja na huduma ya
kwanza ikitolewa na G1 Security ambao walitoa madaktari pamoja na
Ambulance.
No comments :
Post a Comment