Habari kuhusu kifo cha diwani wa
kata ya Kijichi Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam Tausi Milanzi
zimekuwa zikisambaa kwa kasi kwenye mitandao ya kijamii jambo
lililopelekea Mtembezi Media Group kutafuta ukweli wa jambo hilo.
Mtembezi ilimtafuta diwani huyo
kwa njia ya simu ya kiganjani na kuzungumza nae ambapo amekanusha uwepo
wa taarifa hizo na kueleza kuwa yeye ni mzima wa afya na anaendelea na
shughuli zake kama kawaida na kuwataka wananchi wake waendelee kumuunga
mkono na kupuuza uvumi huo.
Pia amehaidi kuwafikisha katika
vyombo vya sheria wote wanaosambaza taarifa hizo kwa ni matumizi mabaya
ya mtandao na ni kinyume na sheria ya mitandao ya hapa nchini.
No comments :
Post a Comment