Na.Alex Mathias
Timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’
imeshindi mchezo wa pili Mfululizo wa Mechi za Kirafiki baada ya
kuwatandika majirani zao Burundi magoli 2-1 mchezo uliopigwa kwenye
dimba la Taifa jijini Dar es salaam.
Wakicheza bila Nahodha wao Mbwana
Samatta aliyeondoka leo na kurejea Ubelgiji kujiunga
na timu yake ya KRC
Genk,alikuwa winga hatari kwa sasa Simon Msuva aliifungia Stars dakika
ya 20 shuti la moja kwa moja akipokea pasi ya Ibrahim Ajibu.
Hadi mapumziko Stars walikuwa
mbele kwa goli moja hilo huku Vijana wa Mayanga wakicheza Mpira wa
kuonana na wachezaji kuweza kutulia japo kosa kosa zilikuwa nyingi
kupitia kwa Msuva.
Kipindi cha pili, mshambuliaji
Laudit Mavugo akatumia makosa ya mchezaji mwenzake wa Simba, beki Abdi
Banda kuifungia bao la kusawazisha Burundi.
Mavugo aliutokea mpira uliompita Banda na kwenda kumtungua kipa wa Yanga, Deo Munishi ‘Dida’ dakika ya 53.
Pamoja na Burundi kusaka bao la pili kwa juhudi, lakini walijikuta wakifungwa wao na kulala 2-1.
Pamoja na Burundi kusaka bao la pili kwa juhudi, lakini walijikuta wakifungwa wao na kulala 2-1.
Chipukizi, Mbaraka Yussuf Abeid
ameanza vyema soka ya kimataifa baada ya kutokea benchi na kuifungia bao
la ushindi Tanzania ikiilaza 2-1 Burundi katika mchezo wa kirafiki
jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mchezaji huyo wa Kagera Sugar ya Bukoba, alifunga bao hilo dakika ya 77 baada ya kupokea pasi ya Simon Msuva mbele kidogo ya mstari unaogawa Uwanja na kujivuta hadi ndani ya boksi kabla ya kufumua shuti lililogonga mwamba na kurudi, akauwahi na kufunga bao zuri.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Shomary Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Salim Mbonde, Himid Mao, Muzamil Yassin/Jonas Mkude, Salum Abubakr ‘Sure Boy’/Said Ndemla, Ibrahim Hajib/Shiza Kichuya, Farid Mussa/Mbaraka Yussuf na Simon Msuva.
Burundi; Jonathan Nahimana, Gael Duhayindavya, Rashid Harerimana, Omary Moussa, David Nshirimimana/Eric Ndoyirobija, Youssouf Ndayishimiye, Tresor Ndikumana, Jean Ndarusanze/Franck Barirengako, Laudit Mavugo, Kiza Fataki/Moustapha Selemani na Djuma Nzeyimana/Sudi Ntirwaza.
Mchezaji huyo wa Kagera Sugar ya Bukoba, alifunga bao hilo dakika ya 77 baada ya kupokea pasi ya Simon Msuva mbele kidogo ya mstari unaogawa Uwanja na kujivuta hadi ndani ya boksi kabla ya kufumua shuti lililogonga mwamba na kurudi, akauwahi na kufunga bao zuri.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Deo Munishi ‘Dida’, Shomary Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Salim Mbonde, Himid Mao, Muzamil Yassin/Jonas Mkude, Salum Abubakr ‘Sure Boy’/Said Ndemla, Ibrahim Hajib/Shiza Kichuya, Farid Mussa/Mbaraka Yussuf na Simon Msuva.
Burundi; Jonathan Nahimana, Gael Duhayindavya, Rashid Harerimana, Omary Moussa, David Nshirimimana/Eric Ndoyirobija, Youssouf Ndayishimiye, Tresor Ndikumana, Jean Ndarusanze/Franck Barirengako, Laudit Mavugo, Kiza Fataki/Moustapha Selemani na Djuma Nzeyimana/Sudi Ntirwaza.
No comments :
Post a Comment