Tuesday, February 21, 2017

Viongozi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wakutana na wadau wa Sekta ya Filamu kujadili kuhusu Sera ya Filamu


NAP1
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kushoto) akizungumza na wadau wa sekta ya filamu (hawapo pichani) wakati wa kikao cha wadau kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura na Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Nuru Millao
NAP2
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akifafanua jambo wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya filamu kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam.
NAP3
Mtayarishaji na msambazaji wa filamu nchini Bibi. Rose Urio akichangia mada wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya filamu kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam.
NAP4
Katibu Mtendaji Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey Mngereza akitolea ufafanuzi maoni yaliyotolewa wakati wa kikao cha wadau wa sekta ya filamu kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam.
NAP5
Mkurugenzi wa Sera na Mipango kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Petro Ryatuu akizungumza na wadau wa sekta ya filamu (hawapo pichani) wakati wa kikao cha wadau kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam.
NAP6
Baadhi ya wadau wa sekta ya filamu wakisikiliza hoja zilizokua zikiendelea kutolewa wakati wa kikao cha wadau kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam.
NAP7
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (wanne kulia) katika picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa sekta ya filamu walioshiriki katika kikao cha wadau kuzungumzia sera ya filamu leo Jijini Dar es Salaam. Watatu kulia ni Naibu Waziri Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Annastazia Wambura, watano kulia ni Katibu Mkuu Wizara hiyo Prof. Elisante Ole Gabriel na wapili kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bibi. Nuru Millao
Picha na: Genofeva Matemu WHUSM

No comments :

Post a Comment