Ujumbe kutoka kampuni ya Ishara Consulting wakitembelea maeneo mbalimbali ya kiwanda
Moja ya paneli ya kuzalisha umeme wa nishati ya jua katika kiwanda cha Mbeya
Meneja
wa Kiwanda cha bia cha TBL Mbeya, Waziri Jemedari (aliyeshika simu)
akiwaonyesha namna anavyopata taarifa zote muhimu za utendaji kazi wa
kiwanda hicho kupitia simu yake ya mkononi ujumbe kutoka kampuni ya Ishara Consulting Ltd walipofanya ziara ya kutembelea kiwanda hicho .
………………………………….
Meneja
Mkuu wa kiwanda cha bia cha Mbeya,Jemedari Waziri,amesema kuwa wakati
Tanzania inajipanga kuwa nchi ya viwanda kuna umuhimu mkubwa kwa viwanda
vilivyo na vipya ambavyo vitajengwa na wawekezaji mbalimbali kuzingatia
kanuni bora za uendeshaji wa viwanda lengo kubwa likiwa ni kupunguza
athari za uharibifu wa mazingira zinazotokana na mchakato wa uzalishaji
katika viwanda.
Jemedari ambaye anaongoza kiwanda hicho ambacho kinashikilia rekodi ya kuwa kiwanda bora cha bia barani Afrika, anasema TBL Mbeya imefanikiwa kupunguza matumizi makubwa ya maji katika mchakato wa uzalishaji kutoka hectolita 6 hadi hectolita 3.2 kwa kila lita moja ya bia inayozalishwa.
Amesema pia kuwa wanafanya uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa zinazopunguza uchafuzi wa hewa
(Carbon Emmision) ambao unapelekea kuwepo mabadiliko ya hali ya hewa
ambayo yanapelekea kuwepo mabadiliko mbalimbali yanayoleta athari kwa
jamii kama vile ukame,upungufu wa maji kutokana na kukauka vyanzo vya
maji.
Baadhi ya hatua za kulinda mazingira ambazo kampuni inaendelea kuzitekeleza alizitaja kuwa ni kutumia
teknolojia zisizochafua hewa wakati wa uzalishaji katika viwanda
vyake,kushiriki kampeni za kupanda miti na utunzaji wa vyanzo vya
maji,kushiriki kampeni za matumizi ya maji kwa umakini kwa kutumia mfumo
unaojulikana kitaalamu kama 5Rs,utakatishaji wa maji taka na kuharibu
taka ngumu na nyepesi kwa kutumia teknolojia za kisasa ambazo ni rafiki
kwa mazingira.
“Katika
kudhihirisha kuwa tumejipanga kuleta teknolojia za kupunguza athari za
uharibu wa mazingira katika uzalishaji katika kiwanda hiki cha Mbeya
tayari tumefunga mitambo ya kuzalisha umeme unaotumia nishati ya umeme
wa jua na katika kipindi cha muda mfupi mtambo huo umeweza kuzalisha
uniti za umeme 15,460 na kupunguza tani za hewa chafu tani 30 na tunategemea kupata mafanikio makubwa zaidi ya kupunguza gharama za matumizi ya umeme na uchafuzi wa hewa“.Alisema Jemedari.
Kuhusiana na suala la upungufu wa maji unaotishia kuikumba dunia kutoka na mabadiliko ya hali ya hewa alisema kampuni inalipa kipaumbele suala hili na inashirikiana na serikali, wadau mbalimbali na wananchi kuhakikisha inaweka mikakati ya kukabiliana nalo ikizingatiwa kuwa moja ya malighafi kubwa katika uzalishaji wa bidhaa zake ni maji.
Jemedari aliongeza kusema kuwa kampuni inaliangalia suala la utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji sio kwa kiwango cha maslahi ya viwanda vyake kupata malighafi tu bali kwa jamii nzima ambapo kampuni inafanyia biashara kwa kuwa sera ya kujenga Dunia Maridhawa inashahabiana Malengo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs) na suala la utunzaji wa mazingira na vyanzo vya maji ni moja ya suala ambalo limepewa umuhimu mkubwa.
Jemedari
alimalizia kwa kusema kuwa Tanzania ya Viwanda inawezekana na sekta hii
itasaidia kukuza uchumi wa nchi kwa haraka bali kitachotakiwa ni
kuhakikisha viwanda vinatumia mifumo bora ya uendeshaji wa viwanda na kuzingatia matumizi ya teknolojia rafiki kwa mazingira katika mchakato wa uzalishaji.
Vilevile
alitoa wito kwa watanzania wote kuzingatia suala la utunzaji wa
mazingira hususani kupanda miti ,kulinda vyanzo vya maji na kutumia maji
kwa umakini.
No comments :
Post a Comment