Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa
Tanzania limeshitushwa na kusikitishwa na taarifa za kutapeliwa wananchi
kuhusu ajira za JWTZ. Hivi karibuni kumezuka kundi la watu wanao jiita
mawakala wa kutafuta vijana wa kujiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi
wa Tanzania na
mara nyingi hutumia majina ya viongozi wa JWTZ kutapeli,
huwataka wananchi hao kuwapa fedha ili kuweza kuwapatia nafasi hizo.
JWTZ linapenda kuwafahamisha
wananchi kuwa nafasi za ajira Jeshini hutangazwa kwa kufuata taratibu za
ajira ambapo JKT imepewa mamlaka ya kuwachukuwa vijana kutoka uraiani
kwa kutoa matangazo ya wito wa vijana wa kujitolea ambapo matangazo hayo
hutolewa hadi ngazi ya wilaya, vijana hao hutakiwa kuwa na nyaraka
mbali mbali zikiwemo za elimu, uraia na nyaraka nyingine kama hizo ili
kukidhi vigezo vya kupatiwa mafunzo ya kijeshi.
Baada ya kumaliza mafunzo hayo
wahitimu hubaki JKT kwa muda wakisubiri vyombo vya ulinzi na usalama
likiwemo JWTZ kutoa ajira kulingana na hitajio la vyombo hivyo. Wananchi
wanatakiwa kufuata taratibu hizo ili kuepuka udanganyifu unaoweza
kusababisha kutapeliwa fedha zao. Jeshi halitahusika na madai yoyote
yatakayotokana na udanganyifu huo.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
No comments :
Post a Comment