Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi akifunga mafunzo
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma yaliyokuwa yakitolewa kwa wafanyakazi wa
Mfuko wa Misitu Tanzania (TFF) ambayo yalifanyika kwa siku nne kwenye
Shule ya Sekondari ya wasichana mjini Kibaha mkoani Pwani.
Wataalam wa bodi hiyo walitoa
mafunzo kuhusu sheria ya ununuzi wa Umma na kanuni zake pamoja na
mabadiliko ya mwaka 2016, Aidha mafunzo yayo yalijadili taratibu za
kuandaa nyaraka za zabuni, taratibu za uchambuzi wa zabuni na
uidhinishaji wa zabuni kwa ujumla wake.
Washiriki wa mafunzo hayo
walikumbuswa majukumu na mipaka ya utendaji wao kama inavyoelekezwa
kwenye sheria na ununuzi wa Umma, Washiriki hao pia walikumbushwa na
kujadili kwa kina wajibu wao katika kuandaa na kutekeleza mikataba ya
ununuzi kwani ndiyo nguzo muhimu katika kutekeleza mikataba ya ununuzi
wa vifaa , huduma na kazi za majenzi
Kaimu Mkurugenzi huyo
aliwakumbushwa wataalamu hao wa Mfuko wa Misitu Tanzania (TFF) kuwa ni
wajibu wao kuwa waadilifu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku
ili kuiweka bodi ya (PSPTB) katika sifa na yenye manufaa kwa taifa.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi akizungumza na
Amosi Kasinza Afisa Mkuu wa Utafiti na Ushauri PSPTB wakati alipowasili
shuleni hapo kwa ajili ya kufunga mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa Fedha na Utawala
(PSPTB) Bw. Paul Bilabaye akifunga mafunzo akitoa mada katika mafunzo
yaliyotolewa na bodi hiyo kwa wataalamu wa Ununuzi na Ugavi kutoka Mfuko
wa Misitu (TFF).
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada mbalimbali katika mafunzo hayo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi akizungumza na
Amosi Kasinza Afisa Mkuu wa Utafiti na Ushauri PSPTB wakifuatilia
mafunzo hayo.
Patricia Manonga Afisa Miradi wa Mfuko wa Misitu akishukuru Uongozi wa bodi ya (PSPTB) kwa kutoa mafunzo hayo.
Dk. Tuli Msuya Katibu Tawala wa
Mfuko wa Misitu Tanzania TFF akishukuru kwa wataalam wa mfuko huo kupata
mafunzo hayo ambayo ni muhimu sana kwao kama wataalam wa Ununuzi na
Ugavi wa Umma.
Mwenyekiti wa Bodi ya Tenda ya
Mfuko wa Misitu Tanzania Bw.Kelvin Mtei akitoa neno la shukurani kwa
bodi ya (PSPTB) kwa kuwapa mafunzo hayo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi akikabidhi cheti
cha kuhitimu mafunzo hao mmoja wa washiriki wa mafunzo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi akisisitiza
jambo wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi pamoja na baadhi
ya wataalam wa Bodi ya PSPTB wakiwa katika picha ya pamoja na
washiriki wa mafunzo hayo.
No comments :
Post a Comment