Mbunge wa Morogoro Mjini Mohamed Abood Azizi (mwenye mavazi mekundu mbele) akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe (kushoto kwake) wakiongoza mamia ya watu waliofiki kushiriki mazoezi ya mwili.
Mkuu
wa Mkoa wa Morogoro (mwenye Truck rangi ya bluu) akiwa katika mazoezi
mepesi Uwanja wa Jamhuri Mjini Morogoro siku ya Jumamosi ya Februari
11,2017. Kushoto kwake ni Mbunge wa jimbo la Morogoro mjini Mohamed
Abood Azizi, na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo.
Kamanda
wa Polisi Mkoa wa Morogoro Urich Matei (katikati) akiwa na viongozi
wengine wa majeshi ya magereza Mkoani humo wakitembea kwa ukakamavu
wakati wa mazoezi ya pamoja Februari 11 mwaka huu.
……………………………………………………………………….
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt.
Steven Kebwe amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo Mhandisi Dkt. John
Ndunguru kuratibu vikundi vingine vya mazoezi na wananchi wengine
Mkoani
Morogoro kujiunga na mazoezi ya viungo yanayofanyika kila Jumamosi ya
pili ya kila mwezi kwa lengo la kuimarisha Afya zao.
Dkt. Kebwe ametoa agizo hilo
mwishoni mwa wiki hii muda mfupi kabla Mkuu huyo kuongoa mamia ya watu
kutoka Taasisi za Umma na watu binafsi waliofika kushiriki mazoezi hayo
na Mkuu huyo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Serikali la kufanya pamoja
mazoezi ili kulinda Afya zao.
Dkt. Kebwe alisema, mazoezi hayo
hayakuanzishwa kwa ajili ya watumishi wa umma pekee bali kwa ajili ya
wananchi wote na lengo lake ni kupunguza magonjwa yasiyoambukizwa kwa
wanannchi wote na kumuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo kuendelea
kuratibu ili kuvipata vikundi au watu wengine kujiunga na mazoezi hayo.
“Lakini RAS, suala hili
lifuatiliwe, kwa mujibu wa waraka kutoka kwa Makamu wa Rais Makatibu
Tawala wa Mikoa ndio wenyeviti wa shughuli hii ya michezo kwa Mkoa
mzima”, Dkt. Kebwe alisema. “kwa hiyo Mwenyekiti, tafadhali simamia ili
watu wengine waendelee kuratibiwa kwa kuwa mazoezi haya siyo kwa ajili
ya watumishi wa umma tu bali kwa watu wote” alisisitiza
Pamoja na wito huo Mkuu huyo wa
Mkoa wa Morogoro ameitahadhalisha jamii kuwa magonjwa yasiyoambukizwa
yanapanda kwa kasi hapa nchini na dawa pekee ya kutibu magonjwa hayo ni
kufanya mazoezi. Ameyataja magonjwa hayo kuwa ni pamoja na shinikizo la
damu, kiharusi, magonjwa ya moyo saratani n.k.
Awali kabla ya kuanza mazoezi
hayo Mkuu wa Mkoa aliwashukuru wote waliofika kushiriki michezo na
kwamba ameridhika na mwitikio huo huku akitaka watu wengi zaidi
waendelee kuitikia wito wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan wa kuungana kufanya mazoezi ya pamoja
kila Jumamosi ya pili ya kila mwezi.
Mazoezi hayo yaliyoanzia katika
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na kuishia Uwanja wa Jamhuri uliopo
katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoroa yalihudhuriwa na viongozi
mbalimbali wa Mkoa huo akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa Mhandisi Daktari
John Nunguru, Kamanda wa Polisi wa Mkoa Urich Onesphori Matei, Mkuu wa
Wilaya ya Morogoro Regina Chonjo na Mbunge wa jimbo la Morogoro Mjini
Mhe. Mohamed Abood Azizi.
No comments :
Post a Comment