Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL Group ) Calvin
Martin (wa pili kulia) Mhandisi wa mitambo wa TBL Group Chrispine
Christopher (Kulia) pamoja na Afisa Uhusiano na Mawasiliano wa mambo ya
nje wa kampuni hiyo Edith Mushi , wakisikiliza maelezo ya Meneja Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa Kampuni ya Toyo Seikan Group Holdings Ltd ya Tokyo Japan( General manager of Business Development) Yashimasa Ito (kushoto).
Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL Group ) Calvin Martin (kushoto) akiwapa maelezo baadhi maofisa wa Kampuni ya Toyo Seikan Group Holdings Ltd ya Tokyo Japan inayojihusisha na uzalishaji wa vifungashia vya bia ,kutoka kulia ni Afisa wa JICA mhandisi Patrick Marwa na Meneja Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa Kampuni ya Toyo Seikan Group Holdings Ltd ya Tokyo Japan Yashimasa Ito
Maofisa kutoka Kampuni ya Toyo Seikan Group Holdings Ltd ya Tokyo Japan inayojihusisha na uzalishaji wa vifungashio wakimsikiliza kwa makini Meneja Uzalishaji wa TBL Group ,(Packaging Manager) Patel Kilovela (Kulia) wakati walipotembelea kiwandani hapo
Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL Group ) Calvin Martin (kushoto) na mhandisi wa Mitambo wa TBL Group Chrispine Christopher (Kulia) wakionyeshwa na Meneja Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa Kampuni ya Toyo Seikan Group Holdings Ltd ya Tokyo Japan (Yashimasa Ito (katikati) moja ya vifungashio vianavyotengenezwa na kampuni yake.
Kampuni
ya Toyo Seikan Group Holding Ltd kutoka nchini Japan imeonyesha dhamira
ya kuwekeza nchini kwa kuzalisha vifungashio vya vinywaji
vilivyotengenezwa kwa teknolojia ya kisasa ya maofisa wa kampuni hiyo
wako nchini kufanya utafiti wa masoko .
Ujumbe wa maofisa wake umetembelea kiwanda cha bia Tanzania (TBL) kwa
ajili ya kujifunza jinsi kinavyofanya kazi ikiwemo kuonyesha
vifungashio vilivyotengeneza kwa teknolojia ya kisasa ambavyo kampuni
hiyo hiyo inazalisha.
Meneja Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa Kampuni hiyo , Yashimasa Ito,ambaye ameongoza ujumbe huo ameelezwa kuvutiwa na hatua kubwa ya kiteknolojia ambayo kampuni ya TBL imefikia katika mchakato wa kuzalisha bia na alisema kuwa wanayo
yadhamira ya kuwekeza nchini na kutengeneza vifungashio kwa kutumia
teknolojia ya kisasa zaidi iwapo watakuwa na uhakika wa kupata masoko ya
kutosha.
Kwa
upande wake Meneja Mkuu wa kiwanda cha TBL cha Ilala,Calvin
Martin,aliueleza ujumbe wa maofisa wa kampuni hiyo mikakati mbalimbali
inayotekelezwa na kampuni kuhakikisha inaenda sambamba na teknolojia za
kisasa zinazotumiwa na viwanda vyote vikubwa vya kutengeneza bia na
vinywaji vingine duniani.
“Tumevutiwa
na dhamira yenu ya kuwekeza nchini kwa kuwa kampuni yetu iko mstari wa
mbele kwenda sambamba na teknolojia na ndio maana viwanda vyetu
vinashikilia rekodi ya kuwa viwanda bora barani Afrika pia bidhaa zetu
zinatamba katika masoko ya kimataifa”.Alisema Calvin.
No comments :
Post a Comment