Kiungo
wa kati wa Manchester United Henrikh Mkhitaryan amemshukuru Jurgen Klop
kwa ushauri wake uliomsaidia kuimarika katika timu yake mpya uwanja wa
Old Trafford.
Mkufunzi huyo wa Liverpool alimshauri mchezaji huyo wakati mgumu walipokuwa katika klabu ya Borussia Dortmund 2013.
Mapema msimu huu Mkhitaryan mwenye umri wa miaka 28 hakucheza kwa muda wa wiki 10 na kukumbuka ushauri aliopewa na Klopp.
”Namshakuru sana Klopp”, alinisaidia kiakili”, aliambia BBC.
Raia huyo wa Armenia alihudumu miaka miwili akimchezea Klopp ambaye alijiunga na Liverpool 2015.
Nilipokuwa Dortmund, nilikuwa na
shikinizo kubwa la kiakili baada ya kushiriki mechi chache ambapo
tulikuwa hatuchezi vyema ,aliongezea Mkhitaryan, ambaye amefunga mara
tano msimu huu.
”Klopp alinionyesha njia,
alinisaidia na kunambia kutovunjika moyo kwa kuwa ufanisi mkubwa ulikuwa
unakuja. Alinisaidia kuwa mchezaji nilivyo”.
SOURCE BBC
No comments :
Post a Comment