Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi
ya Ununuzi na Ugavi wa Umma PSPTB Bw. Godfred Mbanyi , akifungua
semina ya mafunzo ya uongozi na madili kwa wanafunzi wa chuo cha
Biashara cha (CBE) kilichopo jijini Dar es salaam kwa lengo la kupata
viongozi wenye maadili kazini na wenye kufuata kanuni na taratibu za
Ununuzi na Ugavi wa Umma.
Semina hiyo imefanyika leo
katika Ukumbi wa Chuo cha Biashara (CBE) ambapo jumla ya wafunzi 45
walishiriki katika katika mafunzo hayo ya Ugavi na Ununuzi wa Umma.
Akizungumza wakati akifungua
mafunzo hayo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa (PSPTB) Bw. Godfred Mbanyi
amesema , lengo la kuanzisha mafunzo hayo ni kutaka kuwajengea uwezo
katika utendaji wa kazi wenye ubunifu, maadili na Uadilifu ili kuijengea
heshima taaluma ya Ununuzi na Ugavi wa Umma, lakini pia kupata viongozi
wenye kufuata misingi ya taaluma kwa ujumla wake , Kulia katika picha
ni Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB)
Mwezeshaji wa Mafunzo hayo ya
Uongozi yaliyotolewa na Bodi ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB )Zuhura
Sinare Muro akizungumza wakati alipokuwa akitoa mada katika mafunzo hayo
yaliyofanyika leo kwenye chuo cha Biashara CBE.
Baadhi ya wanafunzi wakifuatilia mafunzo hayo.
Mwezeshaji wa Mafunzo hayo ya
Uongozi yaliyotolewa na Bodi ya Ununuzi na Ugavi wa Umma (PSPTB )Zuhura
Sinare Muro akifafanua jambo kwa wanafunzi hao
Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB)na Afisa Mwandamizi wa Masoko na Mahusiano Bi. Shamim Mdee wakiwa katika mafunzo hayo.
Baadhi ya wakufunzi wa mafunzo hayo wakifuatilia jambo.
Kaimu Mkurugenzi
Mtendaji wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi wa Umma PSPTB Bw. Godfred Mbanyi
akimsikiliza Amani Ngonyani Kaimu Mkurugenzi wa Mafunzo (PSPTB)wakati
alipokuwa akitoa shukurani zake mara baada ya Kaimu Mkurugenzi huyo
kufungua semina hiyo
Baadhi ya wanafunzi wakiuliza maswali katika semina hiyo.
Baadhi ya maofisa wa PSPTB wakifuatilia mafunzo yaliyokuwa yakitolewa kwa wanafunzi katika semina hiyo.
No comments :
Post a Comment