Thursday, December 8, 2016

Serikali yakumbana na Changamoto kuu mbili katika kutekelza OGP


6
Na Jonas Kamaleki, Paris
Serikali inakumbwa na changamoto kuu mbili katika kutekeleza Mpango wa Uendeshaji Serikali kwa Uwazi (OGP) ambazo ni kutoa huduma kwa wananchi na kujitathimini yenyewe.
Hii ni kauli ya Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Bw. Aidan Eyakuze aliyoitoa jana jijini Paris, Ufaransa wakati wa mjadala wa jopo la wataalam wa OGP baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Kilele.

“Kutatua changamoto ni pamoja na kufanya kazi na wananchi na kuwasikiliza nini wanataka badala ya  wewe kuwaletea,” alisema Eyakuze.
Aliongeza kuwa lazima kuwepo utoaji wa fursa ya wananchi kujaribu hata ikitokea wakashindwa kutimiza malengo lakini wamepewa nafasi.
Eyakuze alisema katika utekelzaji wa OGP yapo matunda mawili ambayo ni mazungumzo ya kudumu baina Serikali na wananchi pia na mkakati wa kujitathimini. Bila mazungumzo na kujitathini uendeshaji wa Serikali kwa Uwazi hauwezi kutimia, alisisitiza Eyakuze.
Aridudia maneno ya Rais wa Ufaransa, Francois Hollande kuwa demokrasia ikishambuliwa haiwezi kurudi nyuma lazima isonge mbele ili kufikia malengo yaliyowekwa.
Kwa upande wake, Rais Hollande alisema: “Tunataka demokrasia inayoaminika na ya kupambana na rushwa na vitendo viovu katika jamii.”
Aliongeza kuwa ili kupunguza vitendo vya rushwa na kuongeza uwazi katika Serikali, nchi yake imetunga sheria ya kuwalinda watoa taarifa.
“Viongozi wa Serikali ikiwemo wabunge na mawaziri ni lazima kutangaza mali zao kwa ajili ya kudhibiti mianya ya kujilimbikizia mali wakiwa madarakani,” alisema Hollande.
Ili kufanikisha Mpango wa Uendeshaji Serikali kwa Uwazi ni lazima wananchi kushirikiana na Serikali yao, aliongeza Rais Hollande.
Huu ni Mkutano wa Kilele wa 4 ambao umejumuisha mataifa toka pande zote za Dunia ambao ni wanachama wa OGP na wale ambao wanataka kujiunga na Mpango huo. Unafanyika jijini Paris, Ufaransa kwa siku tatu.
Katika siku ya ufunguzi nchi kadha zimejiunga na mango huo. Nchi hizo ni pamoja na Ujerumani, BurkinaFaso, Jamaica, Luxembourg, Pakistan, Ureno na Senegal. Nchi ambazo zinakaribia kujiunga ni Afghanistan, Madagascar na Morocco.
Suala kubwa katika Mkutano huu wa Kilele ni Uwazi na kupambana na rushwa katika Serikali za nchi wanachama. Uwazi unatakiwa katika kutengeneza bajeti za nchi, katika kutoa kandarasi na utoaji wa wa taarifa kwa wananchi kwa uwazi zaidi.

No comments :

Post a Comment