Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya
Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akipokea zawadi za
pampers ambazo zitatumika kwa watoto waliolazwa kutoka kwa Mary Mabano
ambaye mwaka 2008 alifanyiwa upasuaji na madaktari wa Taasisi hiyo na
kuwekewa Valve moja ambayo inamsaidia kupitisha damu vizuri baada ya
upasuaji huo amepona na amejaliwa kupata mtoto mmoja. Siku ya jana
tarehe 28/12/2016 Mary alikuwa anatimiza umri wa miaka 23 na aliamua
kusherehekea siku hiyo na wagonjwa wa moyo.
Mary Mabano akimkabidhi Afisa
Muuguzi Msaidizi ambaye pia ni msimamizi wa wodi namba tatu (3) iliyoko
Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Rogers Kibula zawadi ya sabuni
ya unga ya kufulia ambayo itatumika kwa ajili ya usafi wakati wa
sherehe yake ya kutimiza miaka 23 iliyofanyia jana katika Taasisi hiyo.
Mary alisherehekea siku yake ya kuzaliwa na wagonjwa wa Moyo kwa kuwa
hata yeye mwaka 2008 alifanyiwa upasuaji wa moyo na kuwekewa Valve moja
ambayo inamsaidia kupitisha damu vizuri baada ya upasuaji huo amepona
na amejaliwa kupata mtoto mmoja.
Mary Mabano akiwa katika picha ya
pamoja na Daktari Bingwa wa Moyo ambaye ndiye daktari anaendelea
kumtibu Tulizo Shemu Sanga, baba yake mzazi Mzee Fabian Mabano ambaye
amembeba mjukuu wake mtoto wa Mary aitwaye Faraj Khalid.
Mary Mabano akimlisha keki Mtoto
Jumanne Mndeme ambaye amelazwa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete
(JKCI) kwa ajili ya matibabu ya moyo.
Mary Mabano akimlisha keki
mgonjwa wa Moyo Nasra Hamis ambaye amefanyiwa upasuaji na kuwekewa
Valve ambayo inamsaidia kupitisha damu vizuri katika moyo wake.
Picha ya keki ya Siku ya kuzaliwa Mary Mabano.
Madaktari Bingwa wa Moyo, Wauguzi
, wagonjwa wa Moyo, ndugu, jamaa na marafiki wakiwa katika picha ya
pamoja wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa Mary Mabano ambaye
aliyesherehea siku hiyo na wagonjwa wa Moyo waliolazwa katika Taasisi ya
Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI). Wa tano kutoka kulia ni Mkurugenzi
Mtendaji wa JKCI Prof. Mohamed Janabi.
Mary Mabano akikata keki wakati wa
kusherehekea siku yake ya kuzaliwa huku Madaktari Bingwa wa moyo,
wauguzi, ndugu na jamaa wakishuhudia.
Picha na Anna Nkinda – JKCI
No comments :
Post a Comment