Waziri
wa Afya katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti
wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF, Mhe.Mahmood Thabith
Kombo, akizungumza kwenye Uzinduzi wa Tamasha la Uoneshaji wa Filamu kwa
njia ya Sinema mkoani Geita, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo, Mhe.Nape Nhauye.
Uzinduzi
huo ulifanyika jana katika Ukumbi wa Desire Park Geita ambapo Taasisi
ya Sanaa Na Mazingira ya Kijani Consult Tanzania imeanzisha kampeni ya
kuonesha bure Filamu mbalimbali kwa ajili ya kufikisha elimu kwa umma
ikiwemo elimu ya Utunzaji wa Mazingira (Mabadiliko ya Tabianchi),
Ufugaji wa kuku wa kienyeji, Usalama barabarani, Madawa ya kulevya,
Madhara ya ndoa za utotoni miongoni mwa mambo mengi ya kijamii. Mradi huo umefadhiriwa na ZIFF.
Kutokana
na Mwitikio wa wanatasnia ya Filamu mkoani Geita kuonesha shauku ya
kuwa na Maonesho hayo ya Filamu, Mhe.Kombo alisema mwakani Tamasha la
Kimataifa Zanzibar pia litafanyika mkoani Geita ikiwa ni sehemu ya ZIFF
ni sehemu ya kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa ZIFF.
Na BMG
Mhe.Kombo alisema
mwakani Tamasha la Kimataifa Zanzibar pia litafanyika mkoani Geita ikiwa
ni sehemu ya ZIFF ni sehemu ya kusherehekea miaka 20 tangu kuanzishwa
ZIFF.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu
Tanzania, Bi.Joyce Fessoo, akizungumza kwa niaba ya Serikali kwenye
uzinduzi huo ambapo aliwahakikishia Wanatasnia ya Filamu mkoani Geita na
nchini kwa ujumla kwamba Serikali itahakikisha inaboresha zaidi sanaa
ya filamu ikiwemo kuendelea kutoa mafunzo ya filamu kwa wanatasnia hiyo
ili filamu zinazozalishwa ziwe na ubora.
Aidha alidokeza kwamba Serikali inatoa
baraka zote kuhusiana na Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar, pia
kufanyika mkoani Geita hapo mwakani.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Meja Jenerali
Mstaafu, Ezekiel Kyunga, akizungumza kwenye Uzinduzi wa Uoneshaji wa
Filamu mkoani Geita, ambapo alisisitiza kwamba sanaa ni ajira hivyo
wanatasnia hiyo watumie fursa mbalimbali ikiwemo mafunzo yanayotolewa na
serikali ili kuboresha zaidi kazi zao.
Katibu wa Tamasha la Kimataifa la Filamu
Zanzibar ZIFF, Robert Manondolo, akizungumza kwenye uzinduzi huo ambapo
alibainisha kwamba ZIFF imekuwa ikitoa ufadhiri kwa taasisi mbalimbali
nchini ikiwemo Taasisi ya Kijani Consult kwa lengo la kuziwezesha
kufikisha elimu kwa umma kwa njia ya kuonesha filamu bure na kufikisha
elimu iliyokusudiwa.
Katibu Tawala Wilayani Geita, Thomas
Dimme, akizungumza kwenye uzinduzi wa Tamasha la Uoneshaji wa Filamu
bure mkoani Geita ili kufikisha elimu mbalimbali ikiwemo Ufugaji na
utunzaji wa Mazingira.
Herman Matemu (aliyesimama) ambaye ni Kaimu Afisa Tawala mkoa wa Geita, akisalimia kwenye uzinduzi huo.
Kulia ni Kuka Kahindi ambaye ni Kaimu
Mkurugenzi wa Taasisi ya Sanaa na Mazingira ya Kijani Consult ya mkoani
Geita, akisoma risala kuhusiana na Mradi wa Uoneshaji Filamu Bure mkoani
Geita.
Alisema mradi huo umelenga kutoa chachu
kwa wanajamii kutumia fursa mbalimbali ikiwemo ufugaji kujipatia kipato
badala ya kutegemea shughuli moja kama vile madini. Pia kuwahimiza
kujiepusha na uharibifu wa mazingira. Yote hayo pamoja na mengine
yanafikishwa kwa wananchi kwa njia ya filamu.
Mgeni Rasmi, Waziri wa Afya katika
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Tamasha la
Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF, Mhe.Mahmood Thabith Kombo (kulia)
akipokea taarifa ya mradi wa uoneshaji wa filamu bure mkoani Geita
kutoka kwa Kuka Kahindi ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Sanaa na Mazingira ya Kijani Consult ya mkoani Geita (kushoto).
Mkuu wa idara ya Habari, Kijani Consult
Tanzania, Rose Mweko, akitoa salamu zake kwenye uzinduzi wa mradi wa
kuonesha filamu bure katika maeneo ya wazi mkoani Geita.
Kutoka Kushoto ni Mwakilishi wa Balozi
wa Denimark nchini Tanzania, Dotto Kahindi, Katibu Mtendaji Bodi ya
Filamu Tanzania, Bi.Joyce Fessoo na Mgeni
Rasmi, Waziri wa Afya katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia
ni Mwenyekiti wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF,
Mhe.Mahmood Thabith Kombo, wakifuatilia kwa makini zoezi la uzinduzi wa
mradi wa Kuonesha Filamu bure mkoani Geita ili kufikisha elimu kuhusu
masuala mbalimbali kwa wanajamii.
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye uzinduzi wa mradi wa Kuonesha Filamu bure mkoani Geita
Wageni mbalimbali waliohudhuria uzinduzi huo
Maafisa Habari mkoani Geita wakifuatilia uzinduzi wa mradi wa kuonesha filamu bure mkoani Geita
Wageni mbalimbali wakifuatilia uzinduzi wa mradi wa kuonesha filamu bure mkoani Geita
Wanahabari mkoani Geita wakifuatilia uzinduzi wa mradi wa kuonesha filamu bure mkoani Geita
Wanatasnia wa Filamu mkoani Geita
Burudani za asili mkoani Geita
Burudani za asili zikiendelea
Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Geita
wakifuatilia Uzinduzi wa Mradi wa Uoneshaji wa Filamu bure mkoani humo
ili kufikisha elimu ya masuala mabalimbali ikiwemo uharibifu wa
mazingira pamoja na ufugaji kwa njia ya filamu
Mgeni Rasmi, Waziri
wa Afya katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, ambaye pia ni Mwenyekiti
wa Tamasha la Kimataifa la Filamu Zanzibar ZIFF, Mhe.Mahmood Thabith
Kombo (mwenye kofia) pamoja na
viongozi wengine, wakiwa kwenye picha ya pamoja na watoto walioshiriki
shindano fupi la kucheza muziki kwenye Uzinduzi wa Mradi wa kuonesha
Filamu bure mkoani Geita.
Mgeni Rasmi Mhe.Kombo (mwenye kofia)
pamoja na viongozi wengine, wakiwa kwenye picha ya pamoja na watoto,
Maisala Ibrahimu anayesoma kidato cha pili shule ya Sekondari Kangalala
(ke) na Joshua Tito anayesoma darasa la kwanza shule ya msingi Kivukoni
Geita (Me) ambao walioonesha vipaji vya hali ya juu katika kucheza
muziki.
ZIFF imetoa fursa ya kuwanunulia mavazi
ya shule watoto hao huku pia wakipata fursa ya Kuhudhuria Tamasha la
Kimataifa la Filamu katika Visiwa vya Zanzibar hapo mwakani.
Bonyeza HAPA Kutazama picha za kikao cha Wanatasnia ya Filamu mkoani Geita na Bodi ya Filamu Tanzania.
Wanafunzi waliohitimu na kutunukiwa Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa
Biashara wakishangilia wakati wa Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha
Tumaini Makumira tawi la Dar es Salaam Tudarco yaliyofanyika leo Mwenge,
Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Frederick Shoo, alitunuku jumla ya wahitimu 733. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG}
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Frederick Shoo,akimtunuku Evelyn Wallace Shundi Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara wakati wa Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira tawi la Dar es Salaam Tudarco yaliyofanyika leo Mwenge, Dar es Salaam.
Wahitimu Agnes Nsokolo (kulia) na Asha Kidendei wakiwa na furaha baada ya kuwa miongoni mwa wahitimu 43 waliotunukiwa Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara wakati wa Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira tawi la Dar es Salaam Tudarco yaliyofanyika leo Mwenge, Dar es Salaam.
Evelyn Shundi ambaye ni mfanyakazi wa Ewura akiwa na furaha wakati wa mahafali hayo.
Wahitimu wakivaa kofia baada ya kutukiwa
Mmoja wa wanafunzi akipatiwa cheti wakati wa mahafali hayo
Wakivaa kofia ikiwa ni ishara ya kunukiwa
Wahitimu wakiwa wamekaa baada ya kutunukiwa
Wahitimu wakiwa wamesimama mbele ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wakisubiri kutunukiwa Shahada ya Uzamili
Domina Rwemanyila (kushoto) na Diana Tengia wakiwa na furaha baada ya kutunukiwa Sahada ya Sanaa ya Mawasiliano ya Umma
Ni furaha iliyoje kutunukiwa Shahada ya Uzamili
Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Dk Frederick Shoo na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu waliotunukiwa Sahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara
Wapigapicha wakiwa kazini wakati wa mahafali hayo
Brass Band ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakipiga wimbo wa Taifa wakati wa kuhitimisha mahafali hayo
Julieth (katikati) akiwa na ndugu zake baada ya kuhitimu katika chuo hicho. KWA MAWASILIANO ZAIDI;0715 264202/0754 264203
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Frederick Shoo, alitunuku jumla ya wahitimu 733. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG}
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk Frederick Shoo,akimtunuku Evelyn Wallace Shundi Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara wakati wa Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira tawi la Dar es Salaam Tudarco yaliyofanyika leo Mwenge, Dar es Salaam.
Wahitimu Agnes Nsokolo (kulia) na Asha Kidendei wakiwa na furaha baada ya kuwa miongoni mwa wahitimu 43 waliotunukiwa Shahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara wakati wa Mahafali ya 10 ya Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira tawi la Dar es Salaam Tudarco yaliyofanyika leo Mwenge, Dar es Salaam.
Evelyn Shundi ambaye ni mfanyakazi wa Ewura akiwa na furaha wakati wa mahafali hayo.
Wahitimu wakivaa kofia baada ya kutukiwa
Mmoja wa wanafunzi akipatiwa cheti wakati wa mahafali hayo
Wakivaa kofia ikiwa ni ishara ya kunukiwa
Wahitimu wakiwa wamekaa baada ya kutunukiwa
Wahitimu wakiwa wamesimama mbele ya Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira wakisubiri kutunukiwa Shahada ya Uzamili
Domina Rwemanyila (kushoto) na Diana Tengia wakiwa na furaha baada ya kutunukiwa Sahada ya Sanaa ya Mawasiliano ya Umma
Ni furaha iliyoje kutunukiwa Shahada ya Uzamili
Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Dk Frederick Shoo na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wahitimu waliotunukiwa Sahada ya Uzamili ya Uongozi wa Biashara
Wapigapicha wakiwa kazini wakati wa mahafali hayo
Brass Band ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) wakipiga wimbo wa Taifa wakati wa kuhitimisha mahafali hayo
Julieth (katikati) akiwa na ndugu zake baada ya kuhitimu katika chuo hicho. KWA MAWASILIANO ZAIDI;0715 264202/0754 264203
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Pili ya Kutunuku Shahada na Stashahada za Chuo cha Takwimu Mashariki ya Afrika Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiongozana na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe.Dkt. Philip Mpango (kushoto) pamoja na mkuu wa chuo hicho Prof. Innocent Ngalinda (kulia) kuingia ukumbini pamoja na wahitimu tayari kwa mahafali.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Pili ya Kutunuku Shahada na Stashahada za Chuo cha Takwimu Mashariki ya Afrika Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akifungua mahafali ya pili yaliofanyika chuoni hapo.
Sehemu ya Wahitimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki Mwa Afrika.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Pili ya Kutunuku Shahada na Stashahada za Chuo cha Takwimu Mashariki ya Afrika Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku mmoja wa wahitimu kati ya wahitimu 133 waliohitimu leo na kutunukiwa Shahada na Stashahada.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Pili ya Kutunuku Shahada na Stashahada za Chuo cha Takwimu Mashariki ya Afrika Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Balozi wa Sudan Mhe.Mahgoub Ahmed Sharfi , ambapo mabalozi mbali mbali walihudhuria.
Mgeni Rasmi katika Mahafali ya Pili ya Kutunuku Shahada na Stashahada za Chuo cha Takwimu Mashariki ya Afrika Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja Mabalozi wa nchi mbali mbali waliohudhuria mahafali hayo.
..............................................................
Makamu wa
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amekiri kuwa Wizara,
Idara na taasisi za Serikali zina matumizi madogo ya takwimu sahihi
zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini hali ambayo inachangia kurudisha nyuma shughuli
za upangaji wa maendeleo za wananchi.
Makamu wa
Rais wa Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo leo trh 19-Nov-2016 katika hotuba yake kwenye mahafali ya Pili ya Chuo cha
Takwimu Mashariki mwa Afrika (EASTC)
Jijini Dar es Salaam.
Kutokana na
hali hiyo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu
Hassan ameziagiza wizara, Idara na taasisi za Serikali kuimarisha matumizi ya
takwimu sahihi kwa ajili ya kupanga na kuweka mikakati ya kuwaletea wananchi
maendeleo endelevu.
Makamu wa
Rais ameutaka uongozi wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika uimarishe
ushirikiano na Wakuu wa Takwimu wa Afrika kwa kuhakikisha watakwimu wanaoingia
katika soko la ajira wanafanya kazi zao kwa kufuata misingi ya kisheria na
kanuni zake katika ukokotoaji wa takwimu zinazokubalika kitaifa na kimataifa
ambazo zitawezesha Afrika kupanga maendeleo ya wananchi kwa ufanisi mkubwa.
Amewahimiza
wahitimu wa Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika pindi watakapoanza kufanya
kazi zao wafanye kazi kwa ufanisi na kwa umakini wa hali ya juu ili kutimiza
azma ya kutokomeza kabisa umaskini uliokithiri ifikapo mwaka 2030 katika bara
la Afrika.
“Wito wangu kwa Wizara, Idara na
Taasisi za Serikali kuhakikisha zinaimarisha vitengo vya takwimu kwa kuwaruhusu
maofisa waliopo katika vitengo vyao vya sera na mipango wapate fursa ya
kupatiwa mafunzo elekezi na ya muda mfupi kwa ajili ya kuongeza ujuzi wao wa
kuchambua na kukokotoa takwimu rasmi”
Makamu wa
Rais Samia Suluhu Hassan amesisitiza kuwa hategemei kuona wahitimu walio maliza
masomo yao katika ngazi mbalimbali katika Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika
wamalize soli za viatu kusaka ajira na kwamba Serikali itawawekea mazingira bora
ya kupata ajira haraka.
Kwa upande
wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Philip Mpango amesema Serikali itaendelea
kushirikiana kikamilifu na Ofisi ya Taifa ya Takwimu katika kutumia takwimu
sahihi ambazo zimetolewa na ofisi hiyo katika kupanga shughuli za maendeleo za
taifa.
Katika
mahafali hiyo ya Pili ya Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika, Makamu wa Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewatunuku vyeti
wahitimu 133 katika ngazi za Shahada ya Uzamili ya Takwimu, Shahada ya awali ya
takiwmu na Stashahada ya takwimu kwa wahitimu kutoka nchi Kumi za Afrika ambazo
ni Nigeria,Ghana,Sierra Leon, Ethiopia,Somalia, Uganda, Swaziland, Liberia,
Rwanda na mwenyeji Tanzania.
Washiriki
wa Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani
yaliyotaribiwa na Taasisi ya Doris Mollel wakiwa na bango lenye ujumbe
wa kuadhimisha siku hiyo, iliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar
Novemba 19, 2016. Matembezi hayo yalianzia katika Uwanja wa Amani
kupitia Uwanja wa Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara.
Baadhi
ya viongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakijumuika pamoja
Wadhamini na Waratibu wa Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya
Mtoto Njiti Duniani, wakishiriki Matembezi hayo, yalianzia katika Uwanja
wa Amani kupitia Uwanja wa Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara,
Mjini Unguja, Zanzibar.
Brass
Band ya Chuo cha Mafunzo, Zanzibar ikiongoza Matembezi ya hisani ya
kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Dunian, iliyoadhimishwa kitaifa Mjini
Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016.
Matembezi hayo yalianzia katika Uwanja wa Amani kupitia Uwanja wa
Tumbaku na kuishia Viwanja vya Maisara.
Mkuu
wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania,
Jacqueline Materu akiwa pamoja na Muanzilishi wa Taasisi ya Doris
Mollel, Doris Mollel pamoja na washiriki wengine katika Matembezi ya
hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, yaliyoadhimishwa
kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016.
Mgeni
Rasmi katika hafla ya Matembezi ya hisani ya kuadhimisha Siku ya Mtoto
Njiti Duniani, Naibu Waziri wa Afya wa Zanzibar, Harusi Said Suleiman
akitoa hotuba yake, katika hafla ya Kilele cha siku ya Mtoto Njiti
Duniani, iliyoadhimishwa
kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016. Vodacom ndio Wadhamini
wakuu walioeza kufanyikisha shughuli hiyo. Kulia ni Muanzilishi wa
Taasisi ya Doris Mollel na Mratibu wa Matembezi hayo, Doris Mollel na
kushoto ni Mkuu wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu.
Mkuu
wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania,
Jacqueline Materu akizungumza katika hafla ya Kilele cha siku ya Mtoto
Njiti Duniani, iliyoadhimishwa kitaifa Mjini Unguja, Zanzibar Novemba
19, 2016. Vodacom ndio Wadhamini wakuu walioeza kufanyikisha shughuli
hiyo.
Baadhi
ya Vikundi vya Jogging kutoka maeneo mbalimbali Visiwani Zanzibar,
wakipasha moto misuli mara baada ya kumalizika kwa Matembezi ya hisani
ya kuadhimisha Siku ya Mtoto Njiti Duniani, yaliyoadhimishwa kitaifa
Mjini Unguja, Zanzibar Novemba 19, 2016.
Mshehereshaji wa hafla hiyo, Mishy Bomba akiweka sawa mambo.
Mkuu wa Kitengo ya Uhusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya Vodacom Tanzania, Jacqueline Materu akipokea
No comments :
Post a Comment