SERIKALI imesema kuwa itaendelea na utaratibu wa kuwalipa wastaafu wanaohudumiwa na Wizara ya Fedha na Mipango, pensheni yao kila mwezi kwa mujibu wa sharia ya mafao ya wastaafu Na. 371 badala ya kuwalipa malipo hayo kila baada ya miezi mitatu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha
na Mipango, Bw. DOTTO JAMES amesema kuwa uamuzi huo umetolewa baada ya
kupitia na kujadili mapendekezo ya baadhi ya wastaafu waliofika Makao
Makao Makuu ya Wizara ya Fedha Jijini Da ers salaam mwezi uliopita
wakitaka serikali irejeshe utaratibu wa kuwalipa kila baada ya miezi
mitatu mitatu ili waweze kujikimu kimaisha.
James amesema kuwa Wizara
imepokea maombi kutoka kwa baadhi ya wastaafu kutaka kulipwa kila baada
ya kipindi hicho huku wengine wakitaka kulipwa kila mwezi hatua ambayo
imeifanya Serikali kuamua kulifanyia kazi suala hilo kwa kina na kuahidi
kulitolea uamuzi hapo baadae.
Benny Mwaipaja, Msemaji Wizara ya Fedhana Mipango
No comments :
Post a Comment