Monday, November 28, 2016

BENKI YA UBA YATOA MSAADA WA VIFAA KWA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI MAALUM SHULE YA SEKONDARI PUGU.


 Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA, Peter Makao akiwa meneja wa operesheni wa benki hiyo, Omary, wakikabidhi vitabu kwa wanafunzi, Salum Mohamed na Ramadhani Juma pamoja na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
 Wanafunzi wa shule ya sekondari, Pugu wakishusha sehemu ya magodoro yaliyokabidhiwa na benki ya UBA kwa ajili ya wanafuzni wenye mahitaji maalum shuleni hapo
 Mkurugenzi mkuu wa Benki ya UBA,Piter Makao akiwa meneja operesheni Omary wakikabidhi mafuta ya ngozi kwa kijana mwenye ulemavu wa ngozi ,Daudi Nyangusi na Meneja ufadhili wa eleimu kutoka TEA , Tito Mganwa.
 Wafanyakazi waUnited Bank of Afrika wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wenye ulemavu wa shule ya Sekondari ya wavulana pugu jijini Dar es Salaam
 Afisa masoko wa UBA , Evance Chandarua akimkabidhi begi, Ramadahani Juma

Na  Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Benki ya United Bank of Africa, (UBA), leo imetoa msaada wa viti, Magodoro, Magongo ya kutembelea na vitabu vya kujisomea kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu wa shule ya sekondari ya wavulana, Pugu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa kutoa vifaa hivyo Meneja wa benki hiyo nchini ,Peter Makao, amesema kuwa wamechagua kutoa vifaa hivyo katika shule hiyo kutokana na mahitaji ya wanafunzi hao ambao wamekuwa wakisoma katika mazingira magumu.
“Vitu hivi ambavyo tumevitoa leo vitasaidia kwa kiasi kikubwa kuwapunguzia watoto hawa wenye mahitaji maalum shida zinazowakabili wakati wa kusoma na hivyo kusongwa na mawazo ”Amesema Makao

 Ameto  wito kwa wanafunzi hao kusoma kwa bidii hili waweze kufanikiwa katikamaisha yao na jamii kwa ujumla.
Wanafaunzi wenye ulemavu wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya bwalo la shulehiyo.

No comments :

Post a Comment