Kutoka
kushoto ni Bw. Amishadai Owusu-Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF
AFRICA-Tanzania akisaini mkataba na Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa
Kanda wa AFD Afrika Mashariki.
Kutoka
kushoto ni Bw. Youssef Benrhafiane Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mikopo
na Udhibiti wa BANK OF AFRICA- Tanzania, Bw. Amishadai Owusu- Amoah
Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA- Tanzania, HE Malika Berak, Balozi
wa Ufaransa nchini Tanzania, Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa
AFD Afrika Mashariki na Bw. Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la
viwanda Tanzania.
Tanzania,
22nd Novemba 2016 –Agence Française de Développement (AFD) na BANK OF
AFRICA- Tanzania leo wametia saini mkataba wa makubaliano ya kutoa
mikopo kiasi cha shilingi bilioni 25.67 kusaidia uwekezaji kwenye
nishati mbadala na ufanisi wa nishati.
Makubaliano
hayo, yamewezesha upatikanaji wa zaidi ya dola milioni 11.84 kwa ajili
ya kukopesha miradi mbalimbali iliyojikita katika nishati mbadala au
kuongeza ufanisi wa upatikanaji au matumizi ya nishati hapa nchini
kupitia BANK OF AFRICA.
Mkataba
huo umesainiwa na ndugu Bruno Deprince ambaye ni Mkurugenzi wa Kanda wa
AFD na ndugu Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa
Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA, mbele ya Mheshimiwa Bi Malika Berak,
Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mheshimiwa Mikael Melin Programme,
Meneja katika Ujumbe wa Umoja wa Ulaya kwa Tanzania na Mheshimiwa Thomas
Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la Viwanda nchini (CTI).
Katika
makubaliano hayo, taasisi zote mbili zimethibitisha kushirikiana
kupitia mpango wa SUNREF (Matumizi Endelevu ya Maliasili na Nishati).
Mpango huu bunifu utaiwezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi
na mrefu itakayowavutia sekta ya umma na binafsi kutekeleza miradi
katika nishati mbadala na ufanisi wa nishati, ambayo imekuwa ikipata
changamoto katika upatikanaji wa mikopo.
Mpango
huu ubunifu itawezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na
mrefu klatika viwango vya riba nafuu kulinganisha na viwango vya kawaida
vya kibiashara kwa lengo la kuwawezesha wateja katika sekta binafsi na
umma, kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha za kutekeleza
mpango wa nishati mbadala.
Mikopo
hii inaambatana na msaada wa kiufundi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya
ili kuiunga mkono BANK OF AFRICA lakini pia kuiwezesha benki hiyo
kuongeza uwekezaji katika miradi inayochochea ukijani.
Msaada
wa kiufundi pia utatoa utaalamu kwa wawekezaji na waendelezaji wa
miradi ili kuwajengea uwezo katika kuendeleza nishati mbadala na
kuongeza ufanisi katika matumizi ya nishati. Msaada huu utajumuisha
maeneo yote ya uwekezaji kama maandalizi ya mradi, mchakato mzima wa
uwekezaji pamoja na kujengewa uwezo wa kibenki.
Kwa
upande wa Afrika Mashariki, SUNREF, inakuza mpango wa matumizi ya
nishati zinazotoa gesi chafu kidogo kwa kugharimia uendelezaji wa miradi
ya nishati mbadala na ufanisi katika matumizi ya nishati.
AFD
inazisaidia benki za ndani katika kutambua fursa za uwekezaji katika
nishati mbadala na kutoa mikopo inayochochea hali ya kijani pamoja na
kutengeneza utaratibu mzuri wa ulipaji wa mikopo hiyo unaziofaa pande
husika.
Programu
hii imeundwa ili kuzisaidia biashara ziweze kutumia fursa ya mabadiliko
ya hali ya hewa, pamoja na kuimarisha sekta ya benki kufadhili nishati
mbadala na ufanisi wa nishati. Miradi ya nishati mbadala ni ile
inayozalisha aina yoyote ya nishati (joto, mvuke, nguvu) bila kutoa
nishati yoyote ya mafuta au chanzo chochote cha mionzi, ikiwa ni pamoja
na nishati ya upepo na nishati ya jua.
Mradi
huu utachangia pia kuongeza ufanisi wa nishati na mchango wa nishati
mbadala katika ukuaji wa uchumi nchini,na hivyo kuchangia kupunguza
uzalishaji wa gesi ya kaboni. Mradi huu pia utaziwezesha taasisi na
biashara za kitanzania kupata teknolojia ya kijani pamoja na kuboresha
ufanisi wao na ushindani wa jumla pamoja kuendeleza nishati safi.
Mkakati
wa AFD umejikita katika kusaidia maendeleo endelevu ya kimazingira
kupitia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kutumia nishati
zinazotoa gesi kidogo ya kaboni. Hii ni pamoja na, miongoni mwa mambo
mengine, kuboresha ufanisi wa nishati, kupanua matumizi ya vyanzo vya
nishati safi, na kupunguza uzalishaji wa gesi chafu.
Mzazi Sakina Lembo |
TAARIFA KUHUSU MZAZI KUZUILIWA KUONDOKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI
Kuna taarifa zimezagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili imemzuia mzazi Bi. Sakina Mohammed Lembo kuondoka baada ya kuhudumiwa mpaka alipe kiasi cha shilingi 338,257. Taarifa hizo siyo za kweli mama huyo ameruhusiwa kwenda nyumbani na hajalipa kiasi chochote cha fedha.
Ukweli ni kwamba Hospitali ilikuwa ikikumbana na changamoto ya upungufu wa dawa na vitendanishi vya kuwahudumia akina mama hawa kwani mara nyingi vilikuwa havitoshelezi mahitaji kutokana na wingi wa wagonjwa. Kutokana na tatizo hilo Hospitali iliamua kuanzisha mfuko maalumu wa dawa (drug revolving fund) kwa ajili ya kuwahudumia akina mama wajawazito kwa lengo la kuhakikisha hakuna mama mjamzito anayekosa dawa na huduma nyingine kwa wakati.
Ili kuhakikisha mfuko huu unadumu na kuwa endelevu kwa ajili ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vya kuwahudumia kina mama wanaofika katika hospitali kupata msaada wa kujifungua, Hospitali ilianzisha utaratibu wa kuwaomba akina mama wanaopewa huduma hizi kuchangia kadiri inavyowezekana.
Utaratibu huu unawezesha akina mama kuhudumiwa na kupata dawa zote na vifaa vyote vinavyohitajika kwa wakati na bila bugudha ya kuwataka kwenda kununua nje ya Hospitali kabla ya kuhudumiwa. Kauli mbiu ya Hospitali ni kuwa mama akifika tu anahudumiwa kwanza na uchangiaji unakuja baadaye. Kumekuwa na mwitikio mzuri wa kuchangia kwenye mfuko huu kulingana na uwezo alionao mgonjwa husika.
Ili kuhakikisha kwamba utaratibu huu unaendana na sera ya msamaha, akina mama wanaoshindwa kuchangia mfuko huu wamekuwa wakisamehewa kupitia utaratibu wa msamaha wa Hospitali unaoratibiwa na idara yetu ya ustawi wa jamii. Kwa hiyo hakuna mama anayezuiliwa kuondoka Hospitali kwa sababu ameshindwa kuchangia.
Ieleweke kwamba Hospitali inatumia mfumo wa kieletroniki ambao lazima uoneshe gharama halisi aliyotumia mgonjwa yeyote. Kwa utaratibu huu, mgonjwa halazimishwi kulipia bali ni hiari na ambao hawana uwezo wanapewa huduma zote bure. Mfumo huu unafanya kazi vizuri na toka uanze akina mama wengi wamefurahishwa na huduma zetu na wamekuwa mashuhuda juu ya ubora wa huduma hii. Kutokana na utaratibu huu hakuna jinsi mama yeyote atazuiliwa kwa sababu ya kushindwa kuchangia huduma.
Katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2016/2017, Hospitali iliwahudumia akina mama wajawazito 13,322. Miongoni mwao, akina mama waliokuja kutokea Hospitali za umma walikuwa 7,055 sawa na asilimia 53. Aidha gharama halisi za kuwapa huduma akina mama wenye rufaa 7,055 ilikuwa Tshs. 620.4 milioni. Akina mama waliweza kuchangia Tshs. 250.5 milioni. Kwa hiyo Tshs. 370 milioni sawa na asilimia 60 ziligharimiwa na Hospitali. Kuanzia mwezi Novemba mosi 2016 hadi Leo Novemba 21,2016 Hospitali imetoa msamaha kwa kina mama yenye jumla ya shilingi milioni 198.
Imetolewa na;
Aminiel Aligaesha,
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma,
Hospitali ya Taifa Muhimbili,
Kuna taarifa zimezagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili imemzuia mzazi Bi. Sakina Mohammed Lembo kuondoka baada ya kuhudumiwa mpaka alipe kiasi cha shilingi 338,257. Taarifa hizo siyo za kweli mama huyo ameruhusiwa kwenda nyumbani na hajalipa kiasi chochote cha fedha.
Ukweli ni kwamba Hospitali ilikuwa ikikumbana na changamoto ya upungufu wa dawa na vitendanishi vya kuwahudumia akina mama hawa kwani mara nyingi vilikuwa havitoshelezi mahitaji kutokana na wingi wa wagonjwa. Kutokana na tatizo hilo Hospitali iliamua kuanzisha mfuko maalumu wa dawa (drug revolving fund) kwa ajili ya kuwahudumia akina mama wajawazito kwa lengo la kuhakikisha hakuna mama mjamzito anayekosa dawa na huduma nyingine kwa wakati.
Ili kuhakikisha mfuko huu unadumu na kuwa endelevu kwa ajili ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vya kuwahudumia kina mama wanaofika katika hospitali kupata msaada wa kujifungua, Hospitali ilianzisha utaratibu wa kuwaomba akina mama wanaopewa huduma hizi kuchangia kadiri inavyowezekana.
Utaratibu huu unawezesha akina mama kuhudumiwa na kupata dawa zote na vifaa vyote vinavyohitajika kwa wakati na bila bugudha ya kuwataka kwenda kununua nje ya Hospitali kabla ya kuhudumiwa. Kauli mbiu ya Hospitali ni kuwa mama akifika tu anahudumiwa kwanza na uchangiaji unakuja baadaye. Kumekuwa na mwitikio mzuri wa kuchangia kwenye mfuko huu kulingana na uwezo alionao mgonjwa husika.
Ili kuhakikisha kwamba utaratibu huu unaendana na sera ya msamaha, akina mama wanaoshindwa kuchangia mfuko huu wamekuwa wakisamehewa kupitia utaratibu wa msamaha wa Hospitali unaoratibiwa na idara yetu ya ustawi wa jamii. Kwa hiyo hakuna mama anayezuiliwa kuondoka Hospitali kwa sababu ameshindwa kuchangia.
Ieleweke kwamba Hospitali inatumia mfumo wa kieletroniki ambao lazima uoneshe gharama halisi aliyotumia mgonjwa yeyote. Kwa utaratibu huu, mgonjwa halazimishwi kulipia bali ni hiari na ambao hawana uwezo wanapewa huduma zote bure. Mfumo huu unafanya kazi vizuri na toka uanze akina mama wengi wamefurahishwa na huduma zetu na wamekuwa mashuhuda juu ya ubora wa huduma hii. Kutokana na utaratibu huu hakuna jinsi mama yeyote atazuiliwa kwa sababu ya kushindwa kuchangia huduma.
Katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2016/2017, Hospitali iliwahudumia akina mama wajawazito 13,322. Miongoni mwao, akina mama waliokuja kutokea Hospitali za umma walikuwa 7,055 sawa na asilimia 53. Aidha gharama halisi za kuwapa huduma akina mama wenye rufaa 7,055 ilikuwa Tshs. 620.4 milioni. Akina mama waliweza kuchangia Tshs. 250.5 milioni. Kwa hiyo Tshs. 370 milioni sawa na asilimia 60 ziligharimiwa na Hospitali. Kuanzia mwezi Novemba mosi 2016 hadi Leo Novemba 21,2016 Hospitali imetoa msamaha kwa kina mama yenye jumla ya shilingi milioni 198.
Imetolewa na;
Aminiel Aligaesha,
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma,
Hospitali ya Taifa Muhimbili,
No comments :
Post a Comment