Tuesday, November 22, 2016

BANK OF AFRICA YASAINI MKATABA NA TAASISI YA AFD ILI KUWEZESHA UTOAJI WA MIKOPO YA UWEKEZAJI KWENYE NISHATI MBADALA


Kutoka kushoto ni Bw. Amishadai Owusu-Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA-Tanzania akisaini mkataba na Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki.
Kutoka kushoto ni Bw. Youssef Benrhafiane Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Mikopo na Udhibiti wa BANK OF AFRICA- Tanzania, Bw. Amishadai Owusu- Amoah Mkurugenzi Mtendaji wa BANK OF AFRICA- Tanzania, HE Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Bw. Bruno Deprince Mkurugenzi wa Kanda wa AFD Afrika Mashariki na Bw. Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la viwanda Tanzania.

Tanzania, 22nd Novemba 2016 –Agence Française de Développement (AFD) na BANK OF AFRICA- Tanzania leo wametia saini mkataba wa makubaliano ya kutoa mikopo kiasi cha shilingi bilioni 25.67 kusaidia uwekezaji kwenye nishati mbadala na ufanisi wa nishati.

Makubaliano hayo, yamewezesha upatikanaji wa zaidi ya dola milioni 11.84 kwa ajili ya kukopesha miradi mbalimbali iliyojikita katika nishati mbadala au kuongeza ufanisi wa upatikanaji au matumizi ya nishati hapa nchini kupitia BANK OF AFRICA.

Mkataba huo umesainiwa na ndugu Bruno Deprince ambaye ni Mkurugenzi wa Kanda wa AFD na ndugu Ammishaddai Owusu-Amoah, Mkurugenzi Mtendaji na Afisa Mtendaji Mkuu wa BANK OF AFRICA, mbele ya Mheshimiwa Bi Malika Berak, Balozi wa Ufaransa nchini Tanzania, Mheshimiwa Mikael Melin Programme, Meneja katika Ujumbe wa Umoja wa Ulaya kwa Tanzania na Mheshimiwa Thomas Richard, Mwakilishi wa Shirikisho la Viwanda nchini (CTI).

Katika makubaliano hayo, taasisi zote mbili zimethibitisha kushirikiana kupitia mpango wa SUNREF (Matumizi Endelevu ya Maliasili na Nishati). Mpango huu bunifu utaiwezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu itakayowavutia sekta ya umma na binafsi kutekeleza miradi katika nishati mbadala na ufanisi wa nishati, ambayo imekuwa ikipata changamoto katika upatikanaji wa mikopo.

Mpango huu ubunifu itawezesha BANK OF AFRICA kutoa mikopo ya muda mfupi na mrefu klatika viwango vya riba nafuu kulinganisha na viwango vya kawaida vya kibiashara kwa lengo la kuwawezesha wateja katika sekta binafsi na umma, kuondokana na changamoto ya upatikanaji wa fedha za kutekeleza mpango wa nishati mbadala.

Mikopo hii inaambatana na msaada wa kiufundi unaofadhiliwa na Umoja wa Ulaya ili kuiunga mkono BANK OF AFRICA lakini pia kuiwezesha benki hiyo kuongeza uwekezaji katika miradi inayochochea ukijani.

Msaada wa kiufundi pia utatoa utaalamu kwa wawekezaji na waendelezaji wa miradi ili kuwajengea uwezo katika kuendeleza nishati mbadala na kuongeza ufanisi katika matumizi ya nishati. Msaada huu utajumuisha maeneo yote ya uwekezaji kama maandalizi ya mradi, mchakato mzima wa uwekezaji pamoja na kujengewa uwezo wa kibenki.

Kwa upande wa Afrika Mashariki, SUNREF, inakuza mpango wa matumizi ya nishati zinazotoa gesi chafu kidogo kwa kugharimia uendelezaji wa miradi ya nishati mbadala na ufanisi katika matumizi ya nishati.

AFD inazisaidia benki za ndani katika kutambua fursa za uwekezaji katika nishati mbadala na kutoa mikopo inayochochea hali ya kijani pamoja na kutengeneza utaratibu mzuri wa ulipaji wa mikopo hiyo unaziofaa pande husika.

Programu hii imeundwa ili kuzisaidia biashara ziweze kutumia fursa ya mabadiliko ya hali ya hewa, pamoja na kuimarisha sekta ya benki kufadhili nishati mbadala na ufanisi wa nishati. Miradi ya nishati mbadala ni ile inayozalisha aina yoyote ya nishati (joto, mvuke, nguvu) bila kutoa nishati yoyote ya mafuta au chanzo chochote cha mionzi, ikiwa ni pamoja na nishati ya upepo na nishati ya jua.

Mradi huu utachangia pia kuongeza ufanisi wa nishati na mchango wa nishati mbadala katika ukuaji wa uchumi nchini,na hivyo kuchangia kupunguza uzalishaji wa gesi ya kaboni. Mradi huu pia utaziwezesha taasisi na biashara za kitanzania kupata teknolojia ya kijani pamoja na kuboresha ufanisi wao na ushindani wa jumla pamoja kuendeleza nishati safi.

Mkakati wa AFD umejikita katika kusaidia maendeleo endelevu ya kimazingira kupitia kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kutumia nishati zinazotoa gesi kidogo ya kaboni. Hii ni pamoja na, miongoni mwa mambo mengine, kuboresha ufanisi wa nishati, kupanua matumizi ya vyanzo vya nishati safi, na kupunguza uzalishaji wa gesi chafu.


Mzazi Sakina Lembo
TAARIFA KUHUSU MZAZI KUZUILIWA KUONDOKA HOSPITALI YA TAIFA MUHIMBILI

Kuna taarifa zimezagaa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Hospitali ya Taifa Muhimbili imemzuia mzazi Bi. Sakina Mohammed Lembo kuondoka baada ya kuhudumiwa mpaka alipe kiasi cha shilingi 338,257. Taarifa hizo siyo za kweli mama huyo ameruhusiwa kwenda nyumbani na hajalipa kiasi chochote cha fedha.

Ukweli ni kwamba Hospitali ilikuwa ikikumbana na changamoto ya upungufu wa dawa na vitendanishi vya kuwahudumia akina mama hawa kwani mara nyingi vilikuwa havitoshelezi mahitaji kutokana na wingi wa wagonjwa. Kutokana na tatizo hilo Hospitali iliamua kuanzisha mfuko maalumu wa dawa (drug revolving fund) kwa ajili ya kuwahudumia akina mama wajawazito kwa lengo la kuhakikisha hakuna mama mjamzito anayekosa dawa na huduma nyingine kwa wakati. 

Ili kuhakikisha mfuko huu unadumu na kuwa endelevu kwa ajili ya upatikanaji wa dawa na vifaa tiba vya kuwahudumia kina mama wanaofika katika hospitali kupata msaada wa kujifungua, Hospitali ilianzisha utaratibu wa kuwaomba akina mama wanaopewa huduma hizi kuchangia kadiri inavyowezekana. 

Utaratibu huu unawezesha akina mama kuhudumiwa na kupata dawa zote na vifaa vyote vinavyohitajika kwa wakati na bila bugudha ya kuwataka kwenda kununua nje ya Hospitali kabla ya kuhudumiwa. Kauli mbiu ya Hospitali ni kuwa mama akifika tu anahudumiwa kwanza na uchangiaji unakuja baadaye. Kumekuwa na mwitikio mzuri wa kuchangia kwenye mfuko huu kulingana na uwezo alionao mgonjwa husika. 

Ili kuhakikisha kwamba utaratibu huu unaendana na sera ya msamaha, akina mama wanaoshindwa kuchangia mfuko huu wamekuwa wakisamehewa kupitia utaratibu wa msamaha wa Hospitali unaoratibiwa na idara yetu ya ustawi wa jamii. Kwa hiyo hakuna mama anayezuiliwa kuondoka Hospitali kwa sababu ameshindwa kuchangia. 

Ieleweke kwamba Hospitali inatumia mfumo wa kieletroniki ambao lazima uoneshe gharama halisi aliyotumia mgonjwa yeyote. Kwa utaratibu huu, mgonjwa halazimishwi kulipia bali ni hiari na ambao hawana uwezo wanapewa huduma zote bure. Mfumo huu unafanya kazi vizuri na toka uanze akina mama wengi wamefurahishwa na huduma zetu na wamekuwa mashuhuda juu ya ubora wa huduma hii. Kutokana na utaratibu huu hakuna jinsi mama yeyote atazuiliwa kwa sababu ya kushindwa kuchangia huduma.

Katika robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2016/2017, Hospitali iliwahudumia akina mama wajawazito 13,322. Miongoni mwao, akina mama waliokuja kutokea Hospitali za umma walikuwa 7,055 sawa na asilimia 53. Aidha gharama halisi za kuwapa huduma akina mama wenye rufaa 7,055 ilikuwa Tshs. 620.4 milioni. Akina mama waliweza kuchangia Tshs. 250.5 milioni. Kwa hiyo Tshs. 370 milioni sawa na asilimia 60 ziligharimiwa na Hospitali. Kuanzia mwezi Novemba mosi 2016  hadi Leo Novemba 21,2016 Hospitali imetoa msamaha kwa kina mama yenye jumla ya shilingi milioni 198.

Imetolewa na;
Aminiel Aligaesha,
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma,
Hospitali ya Taifa Muhimbili,

No comments :

Post a Comment