Friday, October 28, 2016

TTCL, HUAWEI WAZINDUA HUDUMA YA TEKNOLOJIA YA 4.5G TANZANIA


Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (katikati) akibonyeza kitufe kuashiria uzinduzi rasmi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Kulia ni Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba na Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Tanzania, Bruth Zhang (kushoto) wakishuhudia.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, anayesimamia Sekta ya Mawasiliano, Profesa Faustine Kamuzora (katikati) akipiga makofi pamoja na Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Huawei Tanzania, Bruth Zhang (kushoto) mara baada ya uzinduzi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano.
Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Bw. Waziri Waziri Kindamba akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa matumizi ya teknolojia ya 4.5G inayotolewa na Kampuni ya Huawei ambayo ni mshirika wa TTCL katika huduma za teknolojia ya Mawasiliano. Hafla hiyo ilifanyika jana katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

MTU MMOJA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NJE YA UBALOZI WA MAREKANI NCHINI KENYA

ILIVYOKUWA KWENYE USIKU WA MSHIKE MSHIKE NA KHADIJA OMAR KOPA JIJINI MWANZA.

Malikia wa Taarabu Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omar Kopa, akitoa burudani kwa wakazi wa Jiji la Mwanza usiku wa kuamkia leo ndani ya Villa Park Resort kwenye show ya Usiku wa Mshike Mshike iliyoandaliwa na 102.5 Lake Fm Mwanza.
Na BMG

Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.
Bi.Khadija Omar Kopa pamoja na bendi yake ya Ogopa Kopa Classic alikonga nyoyo za wakazi wa Jiji la Mwanza.

KUMBUKUMBU YA BABA YETU OMUTWALE PASCHAL RUTAIHWA KAKIZIBA

BENKI YA POSTA YAJENGA CHOO CHA SH.MILIONI 14.5 SHULE YA MSINGI PANDE JIJINI TANGA

 Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Umma wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Noves Moses akizundua Jengo jipya la Choo cha Shule ya Msingi Pande ambalo wamelijenga.
 Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Umma wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Noves Moses pamoja na wageni wengine wakipiga makofi mara baada ya kulizundua jengo hilo
 Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Umma wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), Noves Moses kulia akipongezwa na mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Pande,Mathias Anthony mara baada ya kuzindua Jengo la Choo

RAIS WA PHILIPPINE RODRIGO DUTERTE ASEMA AMEMUAHIDI MUNGU KUACHA LUGHA CHAFU

MAROUANE FELLAINI AKATIZA MITAANI NA MDOGO WAKE ANAYEFANANA NAYE

BALOZI SEIF AFUNGUA MKUTANO WA KIKANDA WA KIMATAIFA WA SEKTA YA MAFUTA NA GESI ASILIA, ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi wa pili kutoka kulia akiwa pamoja na Viongozi waandamizi kabla ya kuufungua Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi na kufanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Park Hyatt Mjini Zanzibar.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia wakimsikiliza Balozi Seif wakati akiufungua Mkutano huo.
Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia wakimsikiliza Balozi Seif wakati akiufungua Mkutano huo.
Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Mkutano wa Kikanda wa Kimataifa wa Siku Mbili unaohusiana na Sekta ya Mafuta na Gesi asilia.
 

UJERUMANI WAIPIGA JEKI SAUTI ZA BUSARA 2017

Mwenyekiti wa Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar Ndg Simai Mohammed Said akitiliana saini ya Makubaliano ya kusaidia Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar na Balozi wa Ujerumani Tanzania Balozi Egon Kochanke, Ujerumani imekubali kuchangia €5000 sawa na shilingi za Kitanzania milioni 12,hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Kitalii ya Park Hyyat Shangani Zanzibar leo. Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar hufanyika kila mwaka katika mwezi wa Febuary na kuhudhuriwa na Wageni mbalimbali wanaotembelea Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tamasha la Sauti za Busara Zanzibar Mhe Simai Mohammed Said, akibadilishana mkataba na Balozi wa Ujerumani Nchini Tanzania Balozi Egon Kochanke, baada kumaliza kutiliana saini ya makubaliano ya kuchangia Tamasha hilo kwa mwaka 2017, hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Park Hyyat Shangani Zanzibar, leo mchana. Kwa hisani ya ZanziNews

No comments :

Post a Comment