Tuesday, October 25, 2016

MABALOZI NCHI 12 ZA JUMUIYA YA ULAYA WAWASILI TANGA KUANGALIA FURSA ZA UWEKEZAJI


Kaimu Meneja wa Bandari wa Bandari Tanga, Hendry Arika, (kushoto) akimtambulisha kiongozi wa Mabalozi wa Jumuiya ya Ulaya wanaowakilisha nchi zao nchi, Roeland Vande Geer kwa Captain Bandari, Endrew Matiria wakati ulipofanya ziara yake Tanga kuangalia fursa za uwekezaji baada ya ujio wa mradi wa Bomba la Mafuta Tanga.
 

Mabalozi 12 kutoka nchi mbalimbali wamefika Tanga kuangalia furasa za uwekezaji kwa kutembelea Bandari ya Tanga, Bohari ya mafuta ya GBP na eneo ambalo litajengwa bombala Mafuta kijiji cha Chongoleani.
Akizungumza katika mkutano na ujumbe huo, Meneja wa Bandari Tanga, Hendry Arika, alisema ujumbe huo umejionea kasi kuelekea ujenzi wa bomba la Mafuta na kuwataka wawekezaji wa ndani kuangalia namna ambavyo nao watawekeza.

Kaimu Meneja Bandari Tanga, Hendry Arika, akiwafahamisha mabalozi wa nchi za Ulaya wanaowakilisha nchi zao nchini wakati walipotembelea Bandari ya Tanga kuangalia fursa za uwekezaji kufuatia ujio wa mradi wa bomba la mafuta Tanga.

MASAUNI AFANYA MAZUNGUMZO NA MWAKILISHI WA UNHCR NCHINI

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akimfafanulia jambo Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (kulia) wakati Mwakilishi huyo alipomtembelea Naibu Waziri ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya kuwahudumia Wakimbizi nchini. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya wakimbizi wa Wizara hiyo, Harrison Mseke. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akimsikiliza Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati alipokuwa anamfafanulia jambo kuhusu masuala ya wakimbizi nchini. Mwakilishi huyo alipomtembelea Naibu Waziri ofisini kwake, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

RAIS AZUNGUMZA NA UONGOZI WA OFISI YA MAKAMO WA PILI

MFUNGWA ALIYEACHIWA KWA MSAMAHA WA RAIS WIKI ILIYOPITA AKAMATWA KWA KUIBA SADAKA

PAMBANO LA ANTHONY JOSHUA NA WLADIMIR KLISTCHKO KUTOFANYIKA MWAKA HUU

Bingwa wa uzito wa juu wa IBF Muingereza, Anthony Joshua, hatopigana tena na Wladimir Klistchko mwaka huu.

Mabondia hao walikuwa wapigane Desemba 10, lakini Klitschko amepata majeraha madogo wakati akifanya mazoezi.

Sasa Joshua atapanda ulingoni Desemba 10 kupigana na David Prince, huku pambano lao na Klitschko likitarajiwa kufanyika mwezi Machi ama Aprili mwakani.
                             Bingwa wa IBF Muingereza Anthony Joshua akiwa na mkanda wake.

DK. SHEIN AZUNGUMZA NA UONGOZI WA WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji wakati wa kikao cha Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,[Picha na Ikulu.] 24/10 /2016.
Baadhi ya Wakurugenzi katika Idara mbali mbali katika Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji wakiwa katika mkutano wa siku moja unaozungumzia Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 uliofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,chini ya mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),[Picha na Ikulu.] 24/10 /2016.
Baadhi ya Wakurugenzi katika Idara mbali mbali za Wizara ya Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji wakiwa katika mkutano wa siku moja unaozungumzia Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika utekelezaji wa robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 uliofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,chini ya mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani),[Picha na Ikulu.] 24/10 /2016.
Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Mhe,Balozi Ali Abeid Karume (katikati) akisoma taarifa ya utekelezaji wa Mpango kazi wa mwaka 2016-2017 katika kikao cha robo mwaka ya kwanza ya Julai-Septemba 2016 kilichofanyika leo Ikulu Mjini Unguja,chini ya mwenyekiti wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (hayupo pichani) (kulia) Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulhamid Yahya Mzee na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe.Mohamed Ahmed Salum,[Picha na Ikulu.] 24/10 /2016.

PROFESA MAGHEMBE AFUNGA MAFUNZO YA ASKARI WANYAMAPORI KITUO MLELE KATAVI

vyeti-1
Waziri wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe akiwahutubia wahitimu wa mafunzo ya ukakamavu ambao ni wahifadhi wa wanyama pori kutoka TANAPA , Mamlaka ya Ngorongoro na TAWA mafunzo yaliofanyika katika kituo cha Mlele Mkoa wa Katavi mafunzo hayo yamewashirikisha wahitimu 69 na yalifungwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof Jumanne Maghembe ambapo alieleza kuwa Serikali itaendelea kulinda maliasili kwa nguvu zote. Picha na Walter Mguluchuma
vyeti-2vyeti01
Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Profesa Jumanne Maghembe akizungumza wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya askari wanyamapori katika kituo cha Mlele mkoani Katavi.
vyeti3
Waziri wa Maliasili na utalii Prof Jumanne Maghembe akikagua gwarid la wahifadhi wanyamapori kutoka TANAPA,TAWA na Mamlaka ya Ngorongoro wakati alipokuwa akifunga mafunzo hayo yaiyofanika katika kituo cha mafunzo mlele Mkoani KATAVI.

MATUKIO MBALIMBALI UFUNGUZI WA MKUTANO WA KIUCHUMI WA KOREA NA AFRIKA MJINI SEOUL, KOREA KUSINI

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akipokea zawadi ya kitabu kinachoelezea njia zilizotumiwa na nchi ya Korea Kusini, kupiha hatua kubwa ya maendeleo, kutoka kwa Afisa Mikopo wa Benki ya Exim ya Korea Kusini, Park Gil Jong, kabla ya kuhudhuria ufunguzi wa mkutano wa tano wa ushirikiano wa Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC), Mjini Seoul, Korea Kusini.
 Mawaziri wa Fedha kutoka nchi 54 za kiafrika wanaoshiriki Mkutano wa Tano wa ushirikiano wa kiuchumi kati ya Korea Kusini na nchi Afrika (KOAFEC) wakiweka alama ya kiganja cha mkono kwenye kibao chenye malighafi maalumu yanayoshika alama za vidole kuonesha ushirikiano na umoja, baada ya kufunguliwa rasmi kwa mkutano huo katika ukumbi wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), akiwa ameshika kibao alichoweka alama ya kiganja chake, kuunga mkono umoja na mshikamano wa nchi za Kiafrika zinazohusiana kiuchumi na Korea Kusini baada ya kufunguliwa kwa mkutano wa Tano wa ushirikiano huo kati ya Korea Kusini na nchi za Afrika (KOAFEC) katika ukumbi wa Grand Intercontinental, Seoul Parnas, Korea Kusini.

MKUTANO UHUSIANO NCHI ZA KOREA NA AFRIKA WAFUNGULIWA SEOUL, KOREA

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb) ( kulia ).

MKUTANO wa Tano wa Ushirikiano kati ya Nchi za Kiafrika na Korea Kusini (Korea-Africa Economic Cooperation (KOAFEC), Umefunguliwa leo Jijini Seoul, Korea Kusini, huku agenda kubwa ikiwa ni kuzungumzia namna nchi za Kiafrika zinavyoweza kutumia kilimo katika muktadha wa maendeleo ya viwanda ili ziweze kujikwamua haraka kiuchumi.

Mkutano wa tano wa KOAFEC mwaka huu umebeba kaulimbiu ya kuibadili Afrika kwa njia kilimo na mpango jumuifu wa watu unaolenga kuimarisha sekta ya fedha kwa njia ya mitandao ya simu” (Transforming Africa’s Agriculture through Industrialization and Inclusive Finance)

No comments :

Post a Comment