Friday, September 9, 2016

Blogs & Opinion


 Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni Dar es Salaam leo mchana, wakati akitoa madai ya kushikiliwa kwa wafuasi wa chama hicho zaidi ya 70 wasiofahamika na wengine 10 katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kujihusisha na masuala ya Umoja wa Kupinga Udikiteta (Ukuta), bila ya kufikishwa mahakamani. Kushoto ni Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene.
 Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya chama hicho Kinondoni Dar es Salaam leo mchana, wakati akitoa madai ya kushikiliwa kwa wafuasi wa chama hicho zaidi ya 70 wasiofahamika na wengine 10 katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za kujihusisha na masuala ya Umoja wa Kupinga Udikiteta (Ukuta). Kulia ni Mwenyekiti Baraza la Umoja wa Vijana Chadema (Bavicha), Patrobas Katambi na kushoto ni Ofisa Habari wa chama hicho, Tumaini Makene.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kinakusudia kufungua maombi katika Mahakama Kuu ya kuiomba mahakama hiyo kuiamuru Polisi kuwafikisha mahakamani watu wanaoshikiliwa katika vituo mbalimbali vya polisi jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo inatokana na chama hicho kudai kuwa kuna watu 10 ambao wanashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) na Kituo cha Oysterbay vya Dar es Salaam kwa zaidi ya wiki mbili bila kupewa dhamana ya polisi au kufikishwa mahakamani.

Kauli hiyo ya Chadema imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu yake yaliyo mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es Salaam leo mchana.

Akifafanua kuhusu Habeas Corpus alisema, ni mamlaka iliyonayo Mahakama Kuu ya kuamuru mamlaka yoyote ya kiserikali inayomshikilia mtu kumpeleka mtu huyo mahakamani.

Lissu alisema, vijana hao walikamatwa katika mikoa mbalimbali kwa makosa aliyodai kuwa ni kujihusisha na haraka za kinachoitwa Umoja wa Kupambana na Udikteta (UKUTA) pamoja na masuala mengine ya kisiasa.

“Kama ikifika Jumanne hawajapelekwa mahakamani au hawajapewa dhamana ya polisi, tutakwenda Mahakama Kuu kufungua maombi ya habeas corpus, imuite IGP au DCI au Ma-RPC au wakuu wa vituo wanakoshikiliwa hao waeleze kwa kwanini wanawashikilia hao watu kwa zaidi ya wiki mbili,” alisema Lissu

Lissu alisema tayari wameshaanza maandalizi ya hati hizo ambazo zitapelekwa Mahakama Kuu ili iweze kuwaita kati ya Mkuu wa Polisi (IGP), Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Makamanda wa Polisi wa Mikoa au Wakuu wa Vituo vya Polisi wanakoshikiliwa watu hao.

Alifafanua kuwa alionana na watu hao ambao wamedai mbali na kushikiliwa lakini pia wamepigwa na kuteswa huku wakidai kuwa wamekuwa wakichukuliwa usiku na kupelekwa katika eneo lililopo Mikocheni ambako wanateshwa na kurudishwa polisi.


Alisema jeshi la polisi linakiuka sheria na haki za binadamu kwa kuwashikilia watu hao kwa muda mrefu bila kuwapa dhamana au kuwafikisha mahakamani kwa ajili ya kusomewa mashitaka.

Mshauri wa Rais Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Balozi Mohamed Ramia Abdiwawa (kushoto) pamoja na Viongozi mbali mbali wa Wizara ya  Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora wakiwa katika mkutano Mpango wa Utekelezaji  wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi  CCM  mwaka 2015-2020,chini ya Mwenyekiti  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(hayupo pichani) katika  ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo Septemba 9, 2016. (PICHA NA IKULU YA ZANZIBAR)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Uongozi wa Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora katika mkutano Mpango wa Utekelezaji  wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi  CCM  mwaka 2015-2020 katika  ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja leo
  Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Mhe,Said Hassan Said (kulia) akiwa na Viongozi wengine wa Wizara ya  Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala Bora   katika mkutano Mpango wa Utekelezaji  wa Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi  CCM  mwaka 2015-2020,chini ya Mwenyekiti  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(hayupo pichani) katika  ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
View More...

No comments :

Post a Comment