Monday, August 22, 2016

RAIS MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA MRADI MKUBWA WA UJENZI WA KIWANDA CHA KUSINDIKA GESI UNAOEN DESHWA NA KAMPUNI YA STAT OIL NORWAY


Rais Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mwakilishi wa Kampuni ya Mafuta ya Stat Oil ya Norway, Bw. Oystein Michelsen Ikulu jijini Dar es Salaam, Agosti 22, 2016, kabla ya kupokea taarifa ya maendeleo ya mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha kusindika gesi asili (LNG Plant) kinachotarajiwa kujengwa katika eneo la Likon'go, Mchinga Mkoani Lindi.



Rais Dkt. John Pombe Magufuli akijadiliana jambo na Meneja Biashara wa Kampuni ya Stat Oil ya Norway Oivind Holm Karlsen (watatu) kutoka kushoto mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Wapili kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Kampuni hiyo, Bw. Oystein Michelsen. (PICHA NA IKULU)




NA MTATIRO J 
1. Akidi ilitimia pande zote, Bara na Zanzibar na mkutano ulimchagua Ndugu. Julius Mtatiro kwa kura takribani 500 kuwa Mwenyekiti wa Kikao, alifuatiwa na Ndugu. Ridhiwani wa Morogoro aliyekuwa na kura takribani 170


Sehemu ya Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani
NA MWANDISHI MAALUM

SHIRIKA la Umeme Tanzania (TANESCO) linaendelea kuwatangazia wateja wake wote wa Wilaya ya Bagamoyo kuwa, kutokana na kukatika kwa waya wa mawasiliano, (Optic Fiber) kati ya Dar es Salaam na Bagamoyo, Ofisi ya Shirika hilo wilayani Bagamoyo bado inashindwa kutoa huduma za kupokea malipo na kuuza LUKU kwa muda mpaka hapo waya huo utakapoungwa.

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Mhe. Bahame Tom Nyanduga akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Mgeni Rasmi, Mhe. Jaji Mkuu wa Zanzibar Mhe. Omar Othman kutoa hotuba yake ya ufunguzi wa
mafunzo ya siku tatu kuhusu Miongozo ya Luanda juu ya taratibu za ukamataji na ushikiliaji wa watuhumiwa kabla ya kufunguliwa mashtaka mjini Unguja, Zanzibar Agosti 22, 2016

Mgeni Rasmi, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Omar Othman Makungu leo akifungua rasmi mafunzo ya siku tatu kuhusu Miongozo ya Luanda juu ya taratibu za ukamataji na ushikiliaji wa watuhumiwa kabla ya kufunguliwa mashtaka. Mafunzo hayo yanafanyika Zanzibar Beach hotel mjini Zanzibar na yanawashirikisha takriban maafisa 50 wa Jeshi la Polisi, Magereza, Vyuo vya Mafunzo, Mahakama na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kutoka Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar.

Mwakilishi kutoka taasisi ya African Policing Civilian Oversight Forum – APCOF, Bi. Louise Edwards

Mgeni Rasmi, Jaji Mkuu wa Zanzibar, Mhe. Omar Othman Makungu (katikati) na Mwenyekiti wa THBUB, Mhe. Bahame Tom Nyanduga (wa pili kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya washiriki wa mafunzo kuhusu Miongozo ya Luanda (Luanda Guidelines on the conditions of arrest, police custody and pre–trial detention in Africa) yaliyoanza leo Zanzibar Beach Hotel mjini Zanzibar. Wengine waliokaa kutoka kushoto ni: Katibu Mtendaji wa THBUB, Bibi Mary Massay, Mwakilishi kutoka taasisi ya African Po

No comments :

Post a Comment