Friday, August 26, 2016

PSPF YAKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA JESHI LA MAGEREZA UKONGA JIJINI DAR ES SALAAM


Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akimkabidhi seemu ya vifaa vya michezo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, Agosti 25, 2016. Vifaa hovyo ni vya michezo ya ngumi, mpira wa miguu na mpira wa pete.

 Afisa Masoko wa PSPF, Magira Werema, (kushoto), akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari.
NA K-VIS BLOG/KHALFAN SAID

MFUKO wa Pensheni wa PSPF, umekabidhi vifaa vya michezo kwa wanamichezo wa Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam na kasha kufuatiwa na PSPF bonanza la michezo ya mpira wa miguu, mpira wa pete, Ngumi na Judo.

Akikabidhi vifaa hivyo vya michezo Agosti 25, 2016, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa Mfuko huo, Abdul Njaidi, alisema, PSPF imeamua kutoa vifaa hivyo ili kuunga mkono juhudi za serikali katika kuinua michezo nchini.
“Nyinyi mkiwa kama sehemu kubwa ya wanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, tunayo furaha kutoa vifaa hivi vya michezo kwani baada ya kutekeleza majukumu mazito ya kitaifa mnahitaji kushiriki michezo ili kujenga afya lakini pia kuinua vipaji vyenu,” alisema na kuongeza,
 “Nichukue fursa hii kuwahamasisha mjiunge na PSPF kwani kuna faida nyingi mtapata kutokana na kutoa mafao mbalimbali yatakayoboresha maisha yenu kama ambavyo kauli mbiu yetu inavyosema, PSPF ni chaguo lako sahihi na kamwe hutajutia uamuzi wako wa kujiunga na Mfuko huu.” Alisisitiza Njaidi.
Akipokea vifaa hivyo kwa niaba ya wanamichezo hao, Mkuu wa Kikosi Maalum cha Magereza-Ukonga, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, aliishukuru PSPF kwa msaada huo wa vifaa vya michezo kwani vitawawezesha wanamichezo hao kushiriki michezo katika mazingira bora ya kiuanamichezo.
Baada ya makabidhiano hayo, wanamichezo hao walionyesha uwezo wao katika michezo ya mpira wa miguu, ngumi, mpira wa pete, na judo.

 Afisa Matekelezo (Compliance), wa PSPF, George Mnasizu, (kushoto), akigawa vipeperushi vyenye maelezo ya kina ya huduma zitolewazo na Mfuko huo kwa baadhi ya wanamichezo wa Jeshi la Magereza
 Njaidi akiwa na Mkuu wa Kikosi hicho, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Kikosi Maalum cha Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Rajabu Nyange Bakari, na wacheza judo wa kikosi hicho wakiwa katika picha ya pamoja na vipeperushi vya PSPF.
 Njaidi akimkabidhi sehemu ya vifaa hicho, Nahodha wa timu ya mpira wa pete (Netball), wa timu ya Magereza Ukonga, Pili Enzi
 Werema akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo kocha wa soka wa timu ya Magereza, Sajenti Hassan Mulego
 Njaidi akikagua timu ya soka ya Magereza Ukonga, ambayo ilimenyana na Kikosi Maalum cha Magereza Dar es Salaam, wakati wa bonanza hilo la michezo
  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza
  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza
  Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza
 Hizi ndio Gloves na flana zilizotolewa kwa wana masumbwi (ngumi)
 Pambano la masumbwi likiendelea
  Pambano la masumbwi likiendelea
 Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, akiwa na Mkuu wa Kikosi Maalum cha Magereza jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, wakati akitoa nasaha kwa wanamichezo kabla ya kuanza kwa bonanza hilo
Nasaha za mgeni rasmi kwa wanamichezo
 Wanamichezo wakishangilia hotuba
 Onyesho la Judo
 Werema akimkabidhi sehemu ya vifaa hivyo vya michezo, Kocha na Afisa Michezo wa Kikosi Maalum cha Magereza Dar es Salaam, Inspekta Francis Tabu
 Soka likiendelea baina ya Kikosi Maalum na timu ya Magereza

Mkuu wa Kikosi Maalum cha Jeshi la Magereza Ukonga jijini Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza, Rajabu Nyange Bakari, akizungumza jambo na maafisa wa PSPF, kutoka kulia, Afisa Matekelezo, (Compliance), George Mnasizu, Afisa Masoko, Magira Werema, Afisa Uhsuiano Mwandamizi, Abdul Njaidi, na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, Maseka Kadala




NA JACQUILINE MRISHO - MAELEZO
HALMASHAURI ya Manispaa ya Temeke  imeandaa operesheni kabambe katika stendi ya Mbagala ili kuhakikisha biashara zote zinafanyika katika maeneo yaliyotengwa na yasiyohatarisha afya ya jamii.
Afisa tawala wa wilaya ya Masasi Lincoln Ben Tamba akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa duka  la tigo wilaya ya Masasi mkoani Mtwara kwa lengo la kusogeza huduma karibu na wananchi kulia kwake ni meneja wa kanda ya kusini wa tigo Nderingo Materu  na na wa kwanza kushoto ni  Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles na anayefuatia ni  Meneja huduma kwa wateja kanda ya Pwani, Isaack Shoo  katika sherehe za ufunguzi zilizofanyika mapema wiki iliyopita wilayani Masasi.
 Mkurugenzi wa Tigo kanda ya Pwani, Goodluck Charles akiongea na wananchi wa Masasi mara baada ya ufunguzi wa duka la tigo Masasi katika hafla ya ufunguzi iliyofanyika katika wilaya ya Masasi mapema iliyopita.





Afisa tawala wa wilaya ya Masasi Lincoln Ben Tamba akihutubia wananchi wa Masasi mara baada ya hafla ya ufunguzi wa duka la tigo wilayani hapo ,mapema wiki iliyopita.




Baadhi ya wafanyakazi wa duka la Tigo Masasi wakifuatilia kwa makini hafla za ufunguzi wa duka la Tigo wilaya ya Masasi mapema wiki iliyopita.

DK.SHEIN AONANANA BALOZI MDOGO WA INDIA

BAHILI ARSENE WENGER AJITUTUMUA NA KUTOA PAUNDI MILIONI 50 KWA USAJILI

WACHIMBAJI MADINI WAMUUA NAIBU WAZIRI WA ULINZI NCHINI BOLOVIA

JACQUELINE MENGI AUNGA MKONO JUHUDI ZA JPM KWA KUKARABATI NA KUNUNU VITABU VYA MAKTABA

JAQ
Mkurugenzi wa Dr.Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi (wa pili kushoto) akiwa ameongoza na Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda (kushoto), Diwani wa Kata ya Mwananyamala, Songoro Mnyonge (wa tatu kushoto) pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kinondoni, Emmanuel Ntenga mara baada ya kuwasili shuleni hapo.
 Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation na Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Msingi Kinondoni ambapo aliwahimiza kusoma kwa bidii vitabu hivyo ili kupanua ufahamu wao zaidi na hata kimasomo pia vitasaidia kuinua viwango vyao vya ufaulu.

 Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa maktaba ya Shule ya Msingi Kinondoni jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi (katikati) pamoja na Diwani wa Kata ya Mwananyamala, Songoro Mnyonge.
 Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda na Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi kwa pamoja wakizundua nembo ya taasisi hiyo.
Mkurugenzi wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation, Miss Tanzania 2000, Bi. Jacqueline Mengi wakipeana mikono na Afisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda.

TUNAIFUATA TOTO AFRICAN LEO

SPIKA WA BARAZA LA WAWAKILISHI, MH. ZUBEIR AHUDHURIA MKUTANO WA CPA MAURITIUS

Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid yuko nchini Mauritius kuhudhuria Mkutano wa 47 wa Umoja wa Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Madola Kanda ya Afirika (CPA African Region).

i

No comments :

Post a Comment