Monday, August 29, 2016

MAKAMU WA RAIS, SAMIA SULUHU HASSAN ZIARANI NCHINI SWAZILAND

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye ardhi ya mji wa Mbabane nchini Swaziland tayari kuhudhuria mkutano wa 36 wa SADC wa Wakuu wa nchi  na Serikali ambao utafanyika tarehe 29 Agosti mjini hapo.
 Sehemu ya Mabinti wa Swaziland wakiimba na kucheza wakati wa mapokezi ya Makamu wa Rais wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na ngoma mbali mbali mjini Mbabane nchini Swaziland.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akizungumza na Waziri wa Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Phiwayinkhosi Mabuza wa Swaziland ambaye pia ni Kaimu Waziri wa Fedha mara baada ya kuwasili kwenye kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Mfalme Mswati III.
                                  ...............................................................

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewasili mjini Mbabane - Swaziland leo kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 36 wa Wakuu wa nchi na serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika- SADC. 
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan atamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika mkutano huo ambao utafanyika tarehe 29 Agosti  2016 ambapo Tanzania inatarajiwa kukabidhiwa nafasi ya Uenyekiti wa Jumuiya hiyo.

Mkutano huo wa 36 wa SADC ni maalum kwa wakuu wa nchi na serikali wanaounda Kamati ya siasa,ulinzi na usalama ambao watajadili kwa kina hali ya siasa na usalama, demokrasia na maombi ya Burundi na Comoro kwa ajili ya kujiunga na SADC.

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan katika  msafara wake amefuatana na Waziri wa Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,Kikanda na Kimataifa Augustine Mahiga, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage na Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Amina Salum Ali.

Simon Msuva wa Timu ya Yanga akiwa katikati akimtoka, Omar Salum kushoto na kufanikiwa kumtoka mlinda mlango wa goli la Lyon, Youthe Rostand

MABINGWA watetezi, Yanga SC wameanza vizuri Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kushinda mabao 3-0 dhidi ya African Lyon Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Pongezi kwa wafungaji wa mabao hayo, viungo Deus David Kaseke aliyefungua pazia  kipindi cha kwanza, Simon Msuva na Juma Mahadhi.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Rajab Mrope wa Ruvuma, Mirambo Tshikungu wa Mbeya na Janeth Balama wa Iringa, hadi mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa bao 1-0.
Bao hilo lilifungwa na Kaseke dakika ya 18, akimalizia pasi ya winga Simon Msuva, ambaye leo alikuwa katika kiwango chake.
 Donald Ngoma wa Timu ya Yanga (jezi 11) katikati akijaribu kuwatoka mabeki ya Lyon, kulia ni Abdul Hilary na namba 26 mgongoni ni Amani Peter
 Wanachama wa Timu ya Yanga wakimpungia mikono SimonMsuva
 Simon Msuva, akiwapungia mikono wanachama na wapenzi waliokuwa wakimpungia mikono katika Uwanja wa Mpira wa Taifa
 Mchezo ulianzia hapa  kutoka kwa Harun Niyonzima kwa kmpatia pasi Simon Msuva kwa kupachika mpira katika nyavu za goli la Afikan Lyon, angalia picha tatu za chini na kufanikiwa kumtoka Kipa wa Lyon
 Simon Msuva wa Timu ya Yanga akiwa katikati akimtoka Omar Salum kushoto na kufanikiwa kumtoka mlinda mlango wa goli la Lyon, Youthe Rostand
 Simon Msuva wa Timu ya Yanga akiwa katikati akimtoka, Omar Salum kushoto na kufanikiwa kumtoka mlinda mlango wa goli la Lyon, Youthe Rostand
  Simon Msuva wa Timu ya Yanga akiwa kulia  akimtoka, Omar Salum na kufanikiwa kumtoka mlinda mlango wa goli la Lyon, Youthe Rostand, hapa mlinda mlango akishuhudia kwa macho mpira unavyo tinga golini, mpira uliopigwa kwa kicha na  Simon Msuva katika mchezo wa Ligi Kuu  Tanzania Bara, mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam
   Simon Msuva kulia akifurahi baada ya kuipatia timu yake goli akiwa na Juma Mahadhi
 Donald Ngoma akiwana Mpira
Wanachama wa Timu ya Simba wakiwa na butwaa kutoamini kinacho tokea Uwanjani hapo. (PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)
Wageniwaalikwa wakipatiwa Supu ya mbuzi ambayo huchemshwa kwa masaa kadhaa bila kuungwa, wakati wa sherehe ya kuchinja Mbuzi, ambayo hufanywa na jamiiya Wakurya ikiwa ni sehemu ya kusherehekea jambo fulani
Kuna Sherehe za aina mbalimbali mkoani Mara. Leo BMG inakujuza juu ya Shereze ya kuchinja Mbuzi ili kutengeneza supu. Hii hufanywa zaidi kwa wanajamii wa kabila la Wakurya mkoani humo.

Sherehe hizi hazina msimu maalumu bali hufanyika kadri familia moja na nyingine ama mtu na mtu walivyokubaliana. Mfano mtoto kumchinjia mzazi wake mbuzi kwa ajili ya supu (umusuri) au dada kumchinjia kaka ama mtu yeyote kulingana na makubaliano yao ambapo inaaminika mtu akiinywa supu hiyo husafisha tumbo.

Huchukuliwa kama Heshima kubwa pindi sherehe za aina hii zinapofanyika katika familia fulani ambapo ndugu, jamaa na marafiki hujumuika pamoja kama picha zinavyoonekana katika sherehe ya Chacha Kuchenga alipoenda kumchinjia mbuzi mdogo wake, Leah Marwa Binagi (Binti Kuchenga).
Na BMG
Supu huandaliwa
Supu hii huchemshwa kwa masaa kadhaa bila kuungwa
Muda wa kunywa supu.
Katika supu hiyo, huchanganywa damu mbichi ili kuongeza ladha
Bonyeza  HAPA Kujua Zaidi.

 Wanyange wa Lete Raha Miss Kinondoni 2016 wakionesha moja ya shoo katika Bonanza walioandaliwa na Mdhamini wao Mkuu Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd lililofanyika ufukwe wa Jangwani Sea Breeze Mbezi jijini Dar es Salaam jana lenye lengo la kuwaweka fiti kabla ya shindano lao litakalofanyikaa Septemba mbili Hoteli ya Denfrances Sinza jijini Dar es Salaam.
 Wanyange hao wakiwa na waandaaji wa shindano hilo litakalofanyika Septemba 2, 2016 Hoteli ya Denfrances iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
 Warembo hao wakiwa wameshika chupa za Windhoek kinywaji kinachosambazwa na kuuzwa Mdhamini wao Mkuu Kampuni ya Mabibo Beer Wine and Spirits Ltd.
 Wanyange hao wakitosti kinywaji hicho
 Mratibu wa Shindano hilo, Rahmat George ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Rahmat Entertainment iliyoandaa shindano hilo, akizungumza na wanahabari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya shindano hilo.
 Mwakilishi wa Kampuni ya Mabibo, Abdallah Ngoma, akizungumzia udhamini shindano hilo na shabaha ya kuandaa bonanza hilo.
 Mshauri wa shindano hilo, Boy George, akizungumza na wanahabari.
 Burudani zikiendelea katika bonanza hilo.
 Wanyange hao wakishiriki kucheza mpira wa mkono kwenye bonanza hilo.
 Wadau wa Windhoek wakicheza soka la ufukweni katika 
bonanza hilo.
 Soka la ufukweni likiendelea.

Mchezo wa kuogelea ukiendelea ndani ya kiota cha Jangwani  Sea Breeze huko Mbezi jijini Dar es Salaam.

Na Dotto Mwaibale

MDHAMINI Mkuu wa Lete Raha Miss Kinondoni 2016 Kampuni ya Mabibo Beer Wines and Spirits Ltd imewaandalia Bonanza wanyange wa shindano hilo ili kuwaweka fiti kuelekea shindano lenyewe litakalofanyika Septemba 2 Ukumbi wa Denfrances uliopo Sinza.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwakilishi wa 
Kampuni hiyo, Abdallah Ngoma alisema wameamua
kuwa andalia bonaza hilo ili kuwafanya wawe fiti kabla
ya kuingia kwenye shindano lenyewe Sptemba 2.

" Katika bonaza hilo warembo hao wameweza kushiriki
mpira wa miguu, mikono na  kucheza" alisema Ngoma.

Mratibu wa shindano hilo Rahmat George alisema maandalizi
 yote yamekwisha kamilika ambapo warembo 20 watapanda
jukwaani kuwania nafasi ya Miss Kinondoni 2016.

Alisema kama kawaida warembo hao watapanda jukwaani 
wakiwa katika vazi la ufukweni, ubunifu na kujibu maswali wata
kayoulizwa na majaji.

George ametumia nafasi hiyo kuwaomba wadau wa 
mashindano hayo kufika kupata burudani safi itakayotolewa na mwanamuziki 
nguri Christian Bela na kikosi cha promosheni cha kampuni ya
Mabibo.

Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji Jumanne Mtaturu akisikiliza Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Kaugere Beatus Kapatya akitoa taarifa juu ya kusimama kwa ujenzi wa Zahanati hiyo.
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza kwa Makini Mkuu wa Wilaya ya ikungi
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi mhe Miraji Jumanne Mtaturu akimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Kijiji cha Kaugeri wakati akitoa maelezo wakati wa kikao cha serikali ya kijiji


Mkurungezi mtendaji wa Asasi ya Fedha Jafari Selemani akisitiza jambo wakati wa ufunguzi wa warsha iliyofanyika katika Chuo cha Kilimanjaro Insitute college  na kuwakutanisha wanavyuo zaidi ya mia 2 hapa jijini Dar es salaam ambapo alitumia fursa hiyo kuwaasa vijana kuwa na tabia ya kuweka akiba na kujiandaa na maisha ya uzee ambapo Moto wa asasi hiyo ni "UHURU WA KIFEDHA NI WAJIBU WAKO " kulia kwake ni mtaalamu wa biashara na mhamasishaji wa vijana Fasili  Boniface   mapema mwishoni wa wiki iliyopita.



Mhamasishaji wa vijana Mussa Mashauri akitoa mada kuhusu Vijana na Utendaji kazi katika warsha hiyo iliyoandaliwa na Asasi ya Fedha iliyofanyika katika chuo na Kilimanjaro Insitute college na kuwakutanisha wanachuo zaidi ya 200 toka chuo cha UDSM,Ustawi wa jamii, Teku , St Joseph na Kilimanjaro Insitute college na kushoto kwake ni Murungezi Mtendaji wa KONCEPT na Mhamasishaji wa Vijana Krantz Mwantepele mapema mwisho wa wiki iliyopita.

Mmoja wa wanachuo waliohudhuria warsha hiyo akiuliza swali kwa mwongoza Mada Musa Mashauri.

Mtaalamu wa Biashara na Mhamasishaji wa vijana Fasili Boniface akiongoza mada kuhusu "Siri za jinsi ya kupata Ajira " katika warsha hiyo iliyoandaliwa na Asasi ya Fedha mapema mwishoni mwa wiki iliyopita katika chuo cha Kilimanjaro Insitute college na kukutanisha wanachuo zaidi ya mia 200 hapa jijini Dar es salaam..

Mkurungezi Mtendaji wa KONCEPT na mhamasishaji wa vijana Krantz Mwantepele akisitiza jambo wakati akiongoza mada kuhusu "Siri za uhuru wa kifedha na fursa ambazo zipo nchini vijana wanaweza kujiajili na kutengeneza thamani kwa  jamii inayowazunguka ,katika warsha iliyofanyika mapema mwishoni mwa wiki iliyopita katika chuo cha Kilimanjaro Insitute college,

Baadhi ya washiriki wa warsha hiyo wakisiliza kwa makini mada toka kwa Mkurungezi  Mtendaji wa Koncept Krantz Mwantepele mapema mwa wiki iliyopita.


Mkurungezi Mtendaji wa Koncept akiongoza washiriki wa warsha hiyo kula kiapo kuwa wanaamini nguvu ya mafanikio ipo ndani yao na ni wajibu wao kutafuta fursa na kutimiza ndoto zao

Mkurungezi wa Asasi ya Fedha Jafari selemani akitoa neno la kufunga warsha hiyo iliyofanyika katika chuo cha kilimanjaro na kukutanisha zaidi mia mbili kutoka vyuo vya UDSM , TEKU, USTAWI WA JAMII , ST JOSEPH NA KILIMANJARO INSITUTE COLLEGE mapema wiki iliyopita katika chuo cha Kilimanjaro Insitute college

No comments :

Post a Comment