Thursday, June 30, 2016

Wawekezaji wazawa wana haki kuwekeza kwenye gesi, mafuta

D1 
Afisa Habari, Mhandisi  Yisambi Shiwa (kushoto) na Mkaguzi wa Madini Mwandamizi Jeremiah Hango (kulia) kutoka Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA), wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kuwahudumia wateja katika  Maonesho ya Kimataifa  ya Saba Saba (Dar es Salaam International  Trade  Fair)  yanayoendelea katika  Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
D2 
Afisa Habari, Mhandisi  Yisambi Shiwa (kulia) kutoka  Wakala wa Ukaguzi wa Madini Nchini (TMAA) akielezea madini ya dhahabu yanavyochenjuliwa kwa mteja aliyeshika sampuni ya madini hayo kwenye banda la TMAA katika maonesho hayo.
D3 
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Phillip Mathayo  (kushoto) akielezea majukumu ya Wizara  kwa mteja aliyetembelea banda  hilo  katika Maonesho ya Kimataifa  ya Saba Saba (Dar es Salaam International  Trade  Fair)  yanayoendelea katika  Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
D5 
Mmoja wa wateja (kushoto) akitoa maoni yake kwenye banda la Shirika la Madini la  Taifa (STAMICO) kwenye Maonesho ya Kimataifa  ya Saba Saba (Dar es Salaam International  Trade  Fair)  yanayoendelea katika  Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.

Ulinzi vituo vya DART kuimarishwa

DARAJANI 
Benjamin Sawe Maelezo
—————————–
Baadhi ya abiria wanaotumia usafiri wa mabasi yaendayo kasi maarufu kama mwendo kasi wameilalamikia kampuni hiyo kwa kushindwa kudhibiti vitendo vya wizi vinavyoendelea katika baadhi ya vituo hivyo.
Bw. Juma Ally mkazi wa Kimara mwisho anasema vitendo hivyo hutokea nyakati za usiku kwa baadhi ya vijana kujifanya nao ni miongoni mwa watumiaji daraja hilo na kupelekea abiria kuibiwa vitu vyao ikiwa ni pamoja na kujeruhiwa.
Aliongezea kuwa walinzi wa kituo hicho wamekuwa wakifanya kazi ya kuwapanga abiria na kusahau majukumu yao ya kulinda usalama wa kituo hicho pamoja na mali zao.
“Tunashangaa hawa walinzi wanaolinda vituo hivi, abiria wamekuwa wakilalamika kila siku kuibiwa nyakati za usiku lakini tunaona abiria wakiendelea kuibiwa sijui wahusika wapo wapi?”Aliuliza Bw. Ally.
Nae Bi. Herrieth Shangaa aliongezea kuwa licha ya vitendo vya wizi vinavyoendelea katika vituo hivyo kuna baadhi ya vitendo vikiwemo vya kujisaidia katika madaraja hayo hivyo kupelekea uchafuzi wa mazingira
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi msimamizi wa vituo hivyo ambae hakutaja kutajwa jina lake amesema kuna baadhi ya vituo ni vikubwa na wanawalinzi wachache hivyo wamejipanga kuongeza ulinzi ikiwa ni pamoja na kufunga mfumo wa kidigitali wa kudhibiti wahalifu
Mradi wa mabasi yaendayo haraka ulioanza rasmi terehe 10, mei, 2016 umeonesha ni jinsi gani kero ya foleni itakavyopungua kwa kuwa mabasi hayo yanatumia njia yake ambayo ni miundombinu  iliyojengwa kwa  gharama kubwa  sana.

siku ya mwisho wa zoezi la kuhakiki silaha

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA
TZ 
TAARIFA YA JESHI LA POLISI KWA VYOMBO VYA HABARI
Ndugu zangu waandishi wa habari,
Leo tarehe 30.6.2016 ndiyo tarehe na siku ya mwisho wa zoezi la kuhakiki silaha. Kwa mujibu wa takwimu za silaha tulizonazo inaonyesha kwamba wapo baadhi ya wamiliki wa silaha ambao hawajatekeleza agizo la kuhakiki silaha wanazozimiliki.
Kufutia hali hiyo, natoa angalizo kwa wale wote ambao hawajahikiki silaha zao kwamba muda wowote kuanzia sasa tutaanza operesheni maalum ya kutafuta silaha ambazo hazijahikikiwa.  Ifahamike kwamba yeyote atakaye kutwa na silaha ambayo haijahakikiwa atachuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo  kupoteza sifa ya kuwa mmiliki halali wa silaha hiyo.
Tunatoa agizo kwa wamiliki binafsi wa maghala ya silaha waziwasilishe silaha hizo pamoja na nyaraka zake katika vituo vya karibu vya Polisi kwa ajili ya uhakiki.
Imetolewa:-
Nsato M. Mssanzya – CP
Kamishina wa Polisi Operesheni na Mafunzo
Makao Makuu ya Polisi

BARAZA LA WAFANYAKAZI MUHIMBILI LAFANYA KIKAO CHAKE CHA 16, WAJUMBE WATAKIWA KUWA MFANO KWA WATUMISHI WENGINE.

M1 
Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Hospitali ya Taifa Muhimbili   Profesa Lawrence Museru  akifungua kikao cha 16 cha Baraza hilo kilichofanyika  leo Juni 30, 2016  katika ukumbi wa NACTE Mikocheni jijini Dar es salaam. Kulia ni Katibu wa Baraza hilo Dk. Kisah Mwambene na kushoto ni Katibu Msaidizi Enezer Msuya.
M2 
Katibu wa TUGHE mkoa Bwana.  Gaudence  Kadyango   akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa mikataba ya hali bora za kazi na faida zake.
M3 
Bwana.  Andrew Mwalwisi  kutoka Tume ya Usuluhishi  -CMA-   akiwasilisha mada  katika kikao cha Baraza la wafanyakazi  wa MNH .
M4Mwenyekiti wa TUGHE  Tawi la Muhimbili Mziwanda Salum Chimwege akiuza swali   kwa viongozi wa Baraza  la MNH  katika kikao hicho  .
M5Mjumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa- MNH -Alex   Samweli  akitoa hoja katika kikao hicho  kilichofayika leo.

SABMiller kuendelea kufanya biashara zenye kuleta manufaa kwa jamii

indexMkurugenzi wa Mazingira wa SABMiller Africa,Muzi Chonko katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
———————————————————–
Na Mwandishi wetu
Kampuni ya kimataifa ya SABMiller inayomiliki viwanda vya kutengeneza vinywaji sehemu mbalimbali duniani itaendelea kufanya biashara zenye mwelekeo wa kubadilisha maisha ya jamii mbalimbali kuwa bora bila kusahau kuzingatia utunzaji wa mazingira.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mazingira wa kampuni hiyo kanda ya Afrika Bw.Muzi Chonco,alipozungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam ambapo alipata wasaa wa kuelezea kanuni zinazoongoza utendaji wa kazi wa kampuni kwa ajili ya kuleta mabadiliko endelevu sehemu zote ilikowekeza duniani.
Chonco alisema kuwa tangu kampuni ianze kutumia kanuni hizo ambazo zinashahabiana na malengo ya umoja wa mataifa tayari mafanikio mbalimbali yameanza kupatikana na yapo matumaini ya kufikia mafanikio makubwa katika siku za usoni.
“Tunapoongelea biashara  endelevu tunamaanisha kuwawezesha wanachi kiuchumi kama ambavyo tumekuwa tukifanya kazi na wakulima kupitia mpango wetu wa Go Farming,kuwakwamua wanawake kiuchumi,kuendeleza wajasiriamali,kutunza vyanzo va maji na kuwekeza katika miradi ya maji bila kusahau utunzaji wa mazingira”.Alisema Chonco.
Alitoa mfano wa kampuni  ya TBL Group ambayo iko chini ya kampuni hiyo kwa jinsi ilivyoweza kufanya uwekezaji ambao umeleta mabadiliko nchini ambapo serikali na taaasisi mbalimbali zinatambua mchango wake kwa kuitunukia tuzo mbalimbali ambazo imekuwa ikishinda mwaka hadi mwaka.
Chonco alizichambua kanuni zinazoongoza kampuni na kuleta mabadiliko kwenye jamii kuwa ni dunia yenye nuru njema,dunia changamfu,dunia imara,dunia iliyo  safi na dunia yenye nguvu kazi.
Alisema wakati umefika kwa wawekezaji mbalimbali kufanya uwekezaji wenye kuleta mabadiliko kwenye jamii badala ya kunufaisha upande mmoja  “uwekezaji unaoleta ajira za kila aina kwa wananchi,unaowawezesha kujipatia mapato kwa kuuza bidhaa kwa kampuni iliyowekeza,kutunza mazingira na kuwapatia wananchi elimu ya utunzaji wa mazingira na vyanzo vva maji,kusaidia makundi mbalimbali kwenye jamii yaliyoachwa nyuma ukizingatiwa kwa vyovyote utaleta mabadiliko”.Alisisitiza.
Alitoa mfano kuwa ukimwezesha mkulima ataweza kupata kipato na kujenga nyumba nzuri ya kuishi,watoto wake kusoma vizuri,familia yake kupata lishe bora na kuongeza pato la familia kwa ujumla na maisha kubadilika kutoka hali duni kuwa bora kama ambavyo imetokea kwa wakulima na makundi mengine yanayoshirikiana na kampuni hiyo sehemu mbalimbali duniani.

Bodaboda waiomba serikali kuwachukulia hatua kali abiria wanaokataa kuvaa helmeti

bodaBoda 
Jonas Kamaleki, Maelezo
——————————
WAAENDESHA pikipiki maarufu kama bodaboda wameiomba serikali kuwachukulia hatua kali abiria wanaokataa kuvaa kofia ngumu (Helmet) ili kutoa fundisho kwa watu wengine wasihatarishe maisha yao.
Akiongea katika mahojiano maalum, mwendesha pikipiki, Nathanael Kiula wa Dar es Salaam amesema kuwa abiria wanaokataa kuvaa helmeti wachukuliwe hatua kali ikiwepo kutozwa faini isiopungua Tsh. 30,000/=  ili liwe fundisho kwa wengine.
“Mimi nina helmeti mbili ya kwangu na abiria lakini abiria wengi hawataki kuvaa helmeti hasa akina mama kwa madai kuwa nywele zao zinaharibika pia wanadai kuwa zina uchafu.”alisema Kiula.
Kiula alisema kuwa elimu itolewe kwa abiria na waendesha pikipiki juu ya umuhimu wa kuvaa helmeti kwani ni kwa manufaa yao wanapopata ajali wasiumie sana au kupoteza maisha na si kwa ajili ya kuwakwepa matrafiki.
Mwendesha pikipiki aliyejitambulisha kwa jina la Isaac William alisema abiria wanaokataa kuvaa helmeti waadhibiwe vikali ili kukomesha tabia hii isiokubalika katika suala zima la usafirishaji.
“Abiria wangu baadhi wanakubali kuvaa helmeti lakini walio wengi hukataa kuzivaa kwa madai kuwa wanaogopa magonjwa ya kuambukizwa kupitia vifaa hivyo,”alisema William.
Naye abiria wa bodaboda ambaye ni mkazi wa Dar es Salaam, Bi Fatuma Abdallah amesema yeye hawezi kuvaa helmeti kwani zinatumiwa na watu wengi hivyo anaogopa kupatwa na magonjwa.
“Siwezi kuvaa mikofia yao kwani inatumiwa na watu wengi huwezijua wana magonjwa ya ngozi kiasi gani, kamwe sintoyavaa ng’o,”alisema Fatuma.
Kwa upande wake Kamanda Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchi, Mohamed Mpinga alisema kuwa uvaaji wa kofia ngumu kwa waendesha pikipiki ni lazima. Anayekaidi amri hiyo hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Kwa upande wake, Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Helmet Vaccine Initiative Tanzania Foundation, Bw. Alpherio  Nchimbi alisema matumizi ya Helmeti hayaepukiki kwa usalama wa mwendesha pikipiki na abiria.
“Kwa umuhimu huo, Taasisi yetu inatoa msaada wa kiufundi kwa Jeshi la Magereza nchini kwa ajili ya uanzishwaji wa kiwanda cha kutengeneza kofia ngumu kwa kufuata viwango vya Shirika la Viwango nchini (TBS) na pia tunatoa elimu kwa bodaboda kuhusu matumizi ya kofia ngumu na madhara yatokanayo na kutovaa kofia hizo kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa kwa ujumla,” alisema Nchimbi.
Kuhusu suala la kuvaa helmeti, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alisema kuwa mwendesha pikipiki na abiria ni lazima wavae helmeti na ifikapo Julai 1, 2016 hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya abiria au mwendesha pikipiki atakayekaidi amri hiyo.
“Nawaambia, hatutamvumilia mtu yeyote, mwendesha pikipiki na abiria asiyevaa helmeti tunawahesabu kuwa wana mpango wa kujiua,”alisema Makonda wakati wa Uzinduzi wa Mpango wa Taifa wa Usalama wa raia wa Jeshi la Polisi.
Suala la kuvaa kofia ngumu au helmeti kwa waendesha pikipiki na biria wao limekuwa likipuuzwa kwa muda mrefu ndio maana serikali ya Mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na Jeshi la polisi wameandaa utaratibu wa kuwafuatilia na kuwachukulia hatua za kisheria kwa ajili ya kunusuru maisha yao. Mpango huu unaanza rasmi tarehe 1, 2016.

SERIKALI YATANGAZA KIAMA CHA WAUZA DAWA NA VIPODOZI HATARI MITANDAONI

TZ 
Na Fatma Salum (MAELEZO)
——————————
Serikali kupitia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) imesema hivi karibuni itaanza msako mkali wa kuwatafuta na kuwakamata wauzaji wa dawa zinazokatazwa pamoja na vipodozi vikali ambao wanajitangaza kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii.
Hayo yamesemwa na Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Umma kutoka TFDA Bi. Gaudensia Simwanza wakati wa mahojiano na mwandishi wa habari hii kuhusu kuibuka kwa watu wanaotangaza  biashara ya dawa na vipodozi ambavyo Serikali imevipiga marufuku.
Akitaja bidhaa hizo Bi. Simwanza alisema ni pamoja na dawa za kuongeza ukubwa wa viungo vya mwili, kupunguza uzito wa mwili na vipodozi vyenye kemikali za kuchubua ngozi bidhaa ambazo zinasababisha madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo ugonjwa wa Saratani.
“Kumezuka wafanyabiashara holela wanaotumia mitandao ya kijamii kama vile Instagram, Facebook, Whatsup Groups na kwengineko  kutangaza biashara ya dawa na vipodozi vyenye kemikali hatari ambavyo vimepigwa marufuku na TFDA hivyo wanaohusika wajiandae, hivi karibuni tutaanza kuwashughulikia.” Alisema Simwanza.
Alibainisha kuwa bidhaa hizo nyingi hazijathibitishwa na kupewa kibali na TFDA hivyo wauzaji wanakiuka Sheria ya Chakula, Dawa na Vipodozi Sura ya 219 inayowataka wafanyabiashara wote wa bidhaa hizo kuzisajili kabla hazijaenda kwa  mtumiaji na kutofanya hivyo ni kwenda kinyume na Sheria.
Alieleza kuwa TFDA kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wameandaa mkakati madhubuti wa kuhakikisha wanawabaini na kuwakamata wafanyabiashara wote wanaouza dawa na vipodozi hivyo kupitia mitandao na kuwachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani au kuwatoza faini.
“Wengi wa wafanyabiashara hao hawaweki anuani za maeneo wanayopatikana na hawana maduka rasmi bali huweka namba za simu za mkononi lakini kwa kutumia vyombo vya dola tutawabaini tu na kuwatia mbaroni.” Alisisitiza Simwanza.
Kwa upande wake Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Bw. Innocent Mungy amewatahadharisha watumiaji wa huduma za mawasiliano hasa matangazo ya biashara kuwa makini na matangazo hayo kwani baadhi ya wafanyabiashara hizo wanaweza kuwa ni watu wenye nia mbaya.
Hivi karibuni kumeibuka wimbi la wafanyabiashara wa dawa mbalimbali pamoja na vipodozi ambao wanajitangaza kupitia mitandao ya kijamii na kuna baadhi ya watu wananunua bidhaa hizo bila ya kuhakikisha usalama wake jambo ambalo ni hatari kwa afya zao.

MAKAMU WA RAIS AFUTURU NA WATOTO YATIMA


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa Nasaha maalum mara baada ya kumaliza kufuturu na watoto Yatima
kwenye viwanja vya Karimjee iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa kipindi television cha Mboni Show.
Mkuu wa Wilaya ya kinondoni Mhe. Ally Hapi (kushoto) akiwa kwenye dua pamoja na wageni waalikwa wengine.
Watoto Yatima wakiswali wakati wa tafrija ya kufuturisha watoto Yatima iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa kipindi cha televisheni cha Mboni Show ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan na kufanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan (kushoto) akisalimiana na Mkuu mpya wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema (kulia)
mwingine pichani ni Mkurugenzi wa kampuni ya Chocolate Princess inayotengeneza kipindi cha television cha Mboni Show Bi. Mboni Masimba  wakati wa tafrija
ya kufuturisha watoto yatima iliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee.
Mkurugenzi wa kampuni ya Chocolate Princess kinachoandaa kipindi cha The Mboni Show akizungumza wakati wa kufuturisha watoto yatima .
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza kwenye tafrija ya kufuturisha Watoto Yatima  iliyoandaliwa na kampuni ya Chocolate Princess inayoandaa na kipindi cha television Mboni Show ambapo mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan .(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Watoto wakipewa juisi wakati wa Tafrij ya Futari.
Naibu Mufti Mkuu Sheikh Hamid Jongo akizungumza kwenye tafrija hiyo.

GAZET LA MTANZANIA LA ZINDUA MWEONEKA MPYA “MTANZANIA LIMEBORESHWA

004
005 
Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya New Habari (2006)Ltd, Absalom Kibanda, akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu uzinduzi wa mwonekano mpya wa Gazeti la Mtanzania lenye kauli mbiu ya “Mtanzania Limeboreshwa”.Kulia ni Mhariri Mtendaji wa  Mtanzania, Dennis Msacky na Meneja Masoko wa kampuni hiyo.
???????????????????????????????????? 
Mhariri wa Gazeti la Mtanzania, Dennis Msacky.akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana. kuhusu uzinduzi wa mwonekano mpya wa Gazeti la Mtanzania lenye kauli mbiu ya “Mtanzania Limeboreshwa”Katikati ni Mhariri Mtendaji Kampuni ya New Habari(2006)Ltd, Absalom Kibanda na Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Michael Bugidira.
Picha na Mpiga Picha Wetu

WAFANYAKAZI WA ABANA WAANDAMANA KUDAI MIL 400 WANAZODAI

ma1Wafanyakazi wa kiwanda cha kuchapisha vitabu cha ABANA Printers ltd,kilichopo kata ya Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani,wakiandamana kudai mishahara na mafao yao wanayodai kwa kipindi cha miaka miwili na nusu ambayo yamefikia mil 400 .
(Picha na Mwamvua Mwinyi) 
———————————————————–
Na Mwamvua Mwinyi,Bagamoyo
WAFANYAKAZI wa kiwanda cha uchapishaji vitabu(ABANA Printers Ltd) kilichopo kata ya Mapinga wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ,wanadai fedha za mishahara na mafao yao kiasi cha sh.mil.400 tangu mwaka 2014 bila mafanikio.
Aidha wafanyakazi hao waiomba serikali ya awamu ya tano kuingilia kati tatizo hilo kwani wameshapigania haki zao kupitia mahakamani ,wizara,idara na vyama vinavyojishughulisha kutetea haki za wafanyakazi lakini hakuna msaada walioupata.
Wameeleza kuwa hadi sasa wanaishi katika maisha magumu  huku wengine wakiwa wamefukuzwa kwenye nyumba walizopanga  na wenzao watatu wamefariki kutokana na ugonjwa wa moyo.
Hayo yamejiri jana baada ya wafanyakazi hao kuchukua hatua ya kufanya maandamano nje ya kiwanda hicho na kisha kumfikishia kilio chao mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi (CCM)Bagamoyo,alhaj Abdul Sharif ili aweze kuwasaidia kulipwa haki zao.
Mwenyekiti wa tawi la chama cha wafanyakazi tawi la ABANA printers Wilbard Ikigo ,alidai kuwa mmiliki wa kampuni hiyo anajigamba kwa kusema serikali ipo mkononi mwake hivyo hawezi kuchukuliwa hatua yoyote.
Alisema ni miaka miwili na nusu sasa tangu watelekezwe na mwajiri wao hali iliyosababisha kuingia katika mgogoro na mmiliki huyo.

No comments :

Post a Comment