Waandishi
wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani wakiwa
tayari wamewasili Kituo cha Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)
kituo cha Korogwe.
Mtaalamu
wa utafiti katika Kituo cha Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR)
kituo cha Korogwe Dkt. Daniel Minja akifafanua jambo kwa baadhi ya
waandishi wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini
Marekani walipotembelea kituoni hapo kujionea namna Tanzania
inavyopambana na ugonjwa wa malaria.
Waandishi
wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani
wakimsikiliza Mtaalamu wa utafiti katika Kituo cha Utafiti wa Magonjwa
ya Binadamu (NIMR) kituo cha Korogwe Dkt. Daniel Minja (hayupo pichani)
walipotembelea kituoni hapo kujionea namna Tanzania inavyopambana na
ugonjwa wa malaria.
Familia
ya Salumu Rashidi wa kijiji cha Masatu kilichopo wilaya ya Korogwe
mkoani Tanga wakiwa na mtoto wao Mohammedi Salimu ambaye ni miongoni mwa
watoto waliopo kwenye mradi wa kudhibiti malaria wilayani huo. Kushoto
ni mama yake Mohammedi Monica Mugunda.
Vijana
wa Jeshi la Kujenga Taifa, (JKT) wakitumbuiza wakati wa zaira ya
waandishi wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini
Marekani walipotembelea zahanati ya Mgambo inayomilikiwa na JKT iliyopo
mkoani Tanga kujionea namna Tanzania inavyopambana na ugonjwa wa
malaria.
(Picha na Eleuteri Mangi, MAELEZO, Tanga)
WABUNGE WENGI WAIBARIKI BAJETI WIZARA YA AFYA
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalim
akihitimisha majumuisho ya makadirio ya Bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka
wa fedha wa 2016/2017, bungeni Dodoma usiku huu.
Waziri Ummy Mwalim akipanga vizuri nyaraka tayari kuhitimisha majadiliano ya makadirio ya bajeti ya wizara hiyo.
Viongozi wa wizara hiyo wakifuatilia majadiliano ya wabunge kuhusu bajeti hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Hamis Kigwangallah akijibu moja ya hoja za wabunge.
Mbunge
wa Viti Maalum, Sophia Mwakagenda (Chadema), Mkoa wa Mbeya, akichangia
hoja wakati wa makadilio ya Bajeti ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa iliyopitishwa bungeni Dodoma
Naibu
Waziri wa Afya, Hamisi Kigwangala akisalimiana na wanafunzi wanaosomea
utabibu katika Chuo Kikuu cha Dodoma waliozuru bunge mjini Dodoma
Continue reading →KATIBU WABUNGE AKUTANA NA WADAU WA HABARI OFISINI KWAKE MJINI DODOMA
Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah akizungumza na wadau wa Habari kutoka Jukwaa la
Wahariri, TMF, Sikika, Baraza la Habari Tanzania, Jukwaa la Katiba na TAMWA.
Wahariri, TMF, Sikika, Baraza la Habari Tanzania, Jukwaa la Katiba na TAMWA.
Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah akimsikiliza Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Bw Deus
Kibamba wakati alipokutana na wadau wa Habari Ofisini kwake.
Kibamba wakati alipokutana na wadau wa Habari Ofisini kwake.
Katibu wa Jukwaa la Wahariri Bw Nevelle Meena akizungumza wakati wa Mkutano kati ya
Katibu wa Bunge na wadau wa Habari.
Katibu wa Bunge na wadau wa Habari.
Katibu wa Bunge Dkt Thomas Kashililah akisalimiana na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Bw Theophil Makunga wakati wa Kikao kati ya Katibu wa Bunge na wadau wa Habari.
Picha na Ofisi ya Bunge
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linafanya uchunguzi juu ya mauaji ya watu saba yaliotokea Wilayani Sengerema.
Kwamba
tarehe 11.05.2016 siku ya jumatano majira ya saa 03:45hrs usiku katika
Kijiji na Kata ya Sima Wilaya ya Sengerema Mkoa wa Mwanza, watu wawili
wasiofahamika majina wakiwa na mapanga walivunja mlango na kuingia
kwenye nyumba ya Mama Eugenia Philipo miaka 60, akiwa amelala na familia
yake na kuwakata mapanga sehemu mbalimbali za miili yao hadi kufariki
papo hapo, Mama mwenye Kaya Bi Eugeni, Mdogo wake, Watoto, pamoja na
watu wengine wawili waliokua wakifanya kazi hapo nyumbani kwao wakitokea
Ngara Mkoani Kagera.
Waliouawa 1. Eugenia Philipo
miaka 60 Mama mwenye Kaya, 2. Maria Philipo miaka 50, mdogo wa Mama
Mwenye Kaya 3.Mabula Makeleja miaka 20 mwanafunzi wa kidato cha nne, 4.
Mkiwa Philipo mika 12, mwanafunzi shule ya msingi 5. Leonard Aloyce
miaka 13 mwanafunzi shule ya msingi sima wote wa familia moja na 6.
Donald miaka 40, pamoja na 7. Samson miaka 23 wakazi wa Ngara waliokuwa
wakifanyakazi hapo nyumbani kwa Bi Eugeni.
Aidha katika utekelezaji wa
mauaji hayo watu hao walianza kuingia kwenye nyumba walipokuwa wamelala
watoto wa familia hiyo pamoja na wafanyakazi, na baada ya kuwakata
mapanga hadi kuwaua waliingia kwenye nyumba ya jirani alipokuwa amelala
Mama mwenye Kaya na mdogo wake Bi Maria na kuwaua vivyo hivyo, kisha
wakaondoka eneo la tukio na kwenda kusiko julikana. Huku watoto wengine
wanne wakinusurika kwenye mauaji hayo baada ya kujificha chini ya uvungu
wa kitanda.
Jeshi la Polisi linawashikilia
watu nane kwa mahojiano dhidi ya mauaji hayo na msako mkali wa kuwasaka
wahusika wengine waliohusika kwa namna yeyote katika mauaji hayo bado
unaendelea. Chanzo cha mauaji hayo bado hakijajulikana, uchunguzi bado
unaendelea. Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linawaomba wananchi wenye
mapenzi mema na nchi yao watusaidie kutupa taarifa za wahusika wa
mauaji hayo ili tuweze kuwakamata.
Imetolewa na:
SACP: AHMED MSANGI
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA
SERIKALI KUTUNGA SERA YA KUSIMAMIA SEKTA NDOGO YA FEDHA NCHINI
NAIBU
Waziri, Wizara ya Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, ameliambia
Bunge Mjini Dodoma, leo tarehe 12 Mei, 2016, kwamba serikali inaandaa
sera ya Taifa ya huduma ndogo za fedha ya mwaka 2016, itakayosimamia na
kutatua changamoto zinazoikabili sekta hiyo
Alisema kuwa sera hiyo
itawasilishwa mbele ya Baraza la Mawaziri hivi karibuni kabla ya
kupelekwa bungeni hatimaye itapatikana sheria ya kusimamia taasisi ndogo
za fedha-microfinance Act, 2016.
“Serikali inatambua changamoto ya
taasisi binafsi za fedha zinazosumbua wananchi, hivyo sheria hiyo
ikitungwa itasaidia kuondoa matatizo hayo” alisisitiza Dkt. Kijaji
Naibu Waziri huyo wa Fedha na
Mipango alikuwa akijibu swali lililoulizwa na Mhe. Rahisa Abdalah Musa
(Viti maalumu), aliyetaka kujua serikali ilikuwa na mpango gani wa
kudhibiti utitiri wa taasisi za fedha pamoja na mabenki ili yalete tija
kwa Taifa kwa kuwakopesha wananchi
Akijibu swali la msingi na
maswali ya nyongeza yaliyoulizwa na Mhe. Faida Mohamed Bakar (Viti
maalumu) aliyetaka kujua mikakati ya serikali ya kuanzisha benki ya
wafanyabiashara wakubwa na wadogo ili kuwawezesha kupata huduma bora,
Dkt. Ashatu Kijaji alisema kuwa serikali haina mpango wowote wa kufanya
hivyo.
Alisema kuwa badala yake serikali
inafanya jitihada za kuimarisha benki zake zilizopo ikiwemo Benki ya
maendeleo ya Kilimo (TADB) na Benki ya Rasilimali (TIB) ili kukidhi
mahitaji ya wafanyabiashara wa kada mbalimbali.
“Serikali imeiboresha kimuundo,
Benki ya Rasilimali (TIB) kwa kuunda kampuni tatu zinazofanyakazi kwa
kujitegemea lakini kwa ushirikiano wa karibu” alisisitiza Dkt. Kijaji
Alizitaja kampuni hizo kuwa ni
TIB Benki ya Maendeleo itakayotoa mikopo ya muda wa kati na mrefu kwa
wafanyabiashara wakubwa na wa kati, TIB Benki ya Biashara
itakayowahudumia wafanyabiashara wakubwa, wa kati na wadogo na TIB
Rasilimali itakayohusika na masuala ya ushauri kwenye Soko la Hisa na
Mitaji la Dar es salaam
“Pamoja na mambo mengine, kampuni
hii inawajibika kuwashauri wafanyabiashara, hususan wa sekta ndogo ya
fedha kupata mitaji kupitia Soko la Hisa la Dar es salaam” aliongeza
Dkt. Kijaji
Dkt. Kijaji alisema kuwa pamoja
na juhudi za serikali za kuboresha benki hizo, ikiwemo Benki ya Posta,
Serikali kupitia Benki Kuu (BOT) inaendelea kuweka mazingira wezeshi
ikiwemo kutunga sheria, kanuni na taratibu za kusaidia nguvu za wananchi
na sekta binafsi kuanzisha benki au taasisi za fedha katika maeneo yao
“Ni matarajio yetu kuwa wananchi
wanatumia fursa ya mazingira mazuri ya uwekezaji yaliyopo nchini
kuwekeza wao wenyewe au kuzishawishi benki za biashara kuanzisha huduma
za kibenki katika maeneo yao” alisema Dkt. Kijaji
Kuhusu ombi la mbunge huyo
kuitaka serikali iingilie kati masuara ya riba zinazotozwa na taasisi za
fedha na kuwaumiza wananchi, Dkt. Kijaji alisema kuwa serikali haiwezi
kudhibiti wala kuingilia jambo hilo.
Alisema kuwa Serikali ilijitoa
katika uendeshaji wa moja kwa moja wa shughuli za kifedha tangu mwaka
1991 ili kuruhusu ushindani huru na kuboresha huduma katika sekta ya
fedha hivyo viwango vya riba na mikopo vinavyotozwa na benki hizo na
taasisi nyingine za fedha zinapangwa kutokana na nguvu ya soko.
Dkt Kijaji alieleza kuwa katika
upangaji wa viwango vya tozo na riba mbalimbali benki na taasisi za
fedha huzingatia gharanma za upatikanaji wa fedha, halikadhalika gharama
za uendeshaji na sifa alizonazo mkopaji”Alisisitiza Dkt Kijaji
Imetolewa na:
Benny Mwaipaja
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Fedha na Mipango
DODOMA
12/5/2016
Waandishi wa habari kutoka taasisi ya Malaria no More wawasili Tanga
Mganga
Mkuu wa Zahanati ya Ithna-Asheri iliyopo jijini Arusha Dkt. Mohammed
Alawi akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka Taasisi ya
“Malaria No More” ya nchini Marekani, ambao wapo nchini kwa ziara ya
siku tano kujionea namna Tanzania inavyopambana na ugonjwa wa malaria.
Mganga
Mkuu wa Zahanati ya Ithna-Asheri iliyopo jijini Arusha Dkt. Mohammed
Alawi akiongea na baadhi ya waandishi wa habari kutoka Taasisi ya
“Malaria No More” ya nchini Marekani, ambao wapo nchini kwa ziara ya
siku tano kujionea namna Tanzania inavyopambana na ugonjwa wa malaria.
Mwandishi
wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani
Lyndsey Wajert akiwa tayari kufanyiwa vipimo vya malaria na Mtaalamu wa
Maabara Apolinary Mushi katika zahanati ya Ithna-Asheri iliyopo jijini
Arusha wakati wa ziara ya waandishi wa Habari hao ambao wapo nchini kwa
ziara ya siku tano kujionea namna Tanzania inavyopambana na ugonjwa wa
malaria.
Mtaalamu
wa Maabara Apolinary Mushi anayefanya kazi katika zahanati ya
Ithna-Asheri iliyopo jijini Arusha akifanya mahojiano na mwandishi wa
habari Katy Migiro wa Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani
wakati wa ziara mkoani Arusha kujionea namna Tanzania inavyopambana na
ugonjwa wa malaria.
Waandishi
wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya nchini Marekani wakiwa
tayari uwanja wa ndege wa Arusha kwa safari ya kuelekea mkoani Tanga.
Eneo
la ukingo wa Bahari ya Hindi mkoani Tanga ambapo karibu na eneo
walipofikia waandishi wa habari kutoka Taasisi ya “Malaria No More” ya
nchini Marekani wakati wa ziara yao mkoani Tanga kujionea namna Tanzania
inavyopambana na ugonjwa wa malaria.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Tanga)
RAIS DKT. MAGUFULI AHUDHURIA SHEREHE ZA UAPISHO WA RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kuwasili
kwenye viwanja vya Kololo jijini Kampala.Picha na IKULU
Rais
wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili
kwenye viwanja hivyo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Rais wa wa Sudani Kusini Salva Kir mara baada ya
kuwasili kwenye viwanja hivyo.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akijadiliana jambo kwa furaha na Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt.
Jakaya Kikwete pamoja na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya
kuapishwa kwa Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni katika viwanja vya
Kololo jijini Kampala Uganda.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili
kwenye Uwanja wa Kololo jijini Kampala kuhudhuria sherehe za uapisho wa
Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri Kaguta Museveni.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya Pili Alhaji Ali Hassani Mwinyi
kwenye viwanja vya Kololo jijini Kampala Uganda. Rais Mstaafu Mwinyi
alihudhuria pia sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri
Kaguta Museveni.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na Rais mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete kwenye
viwanja vya Kololo jijini Kampala Uganda. Rais Mstaafu Kikwete pia
alihudhuria sherehe za uapisho wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Yoweri
Kaguta Museveni.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na viongozi wa mataifa mbalimbali katika viwanja vya Kololo
jijini Kampala.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akisalimiana na mmoja wa viongozi wa dini wa Taifa la Uganda katika
viwanja vya Kololo jijini Kampala.
TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MKUU WA WAKADIRIAJI MAJENZI, AFRIKA UTAKAOFANYIKA MWEZI AGOSTI 2016 JIJINI DAR ES SALAAM
Rais
wa Chama cha Wakadiriaji Majenzi Tanzania (TIQS), Samuel Marwa
(kushoto), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam leo (hawapo
pichani), kuhusu Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano mkuu wa wakadiriaji
majenzi, Afrika utakaofanyika Agosti 2016. Kutoka kulia ni Mjumbe wa
chama hicho, Neema Shabani na Bahati Mbambe.
Rais
wa Chama cha Wakadiriaji Majenzi Tanzania (TIQS), Samuel Marwa
(katikati), akisisitiza jambo katika mkutano huo. Kutoka kushoto ni
Mjumbe wa chama hicho, Joseph Mhonda, Katibu wa chama hicho, Bernard
Ndakidemi, Mjumbe wa Chama hicho, Bahati Mbambe na Mjumbe, Neema Shaban.
Mjumbe wa Chama hicho, Bahati Mbambe (kulia), akisisitiza jambo.
Mjumbe wa Chama hicho, Neema Shabani akisisitiza jambo kwenye mkutano huo.
Mjumbe wa chama hicho, Joseph Mhonda akitoa ufafanuzi kadhaa baada ya waandishi wa habari kuuliza maswali.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
……………………………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale CHAMA Cha WakadiriajiMajengo Tanzania (TIQS) kwa kushirikiana na Chama cha wakadiriaji majenzi Afrika (AAQS), watakuwa wenyeji wa mkutano mkuu wa Wakadiriaji Majenzi wa Afrika utakaofanyika tarehe 18 na 19 Agosti 2016 jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine chama hicho kimemuomba Rais John Magufuli,awape kazi katika miradi ya ujenzi
……………………………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale CHAMA Cha WakadiriajiMajengo Tanzania (TIQS) kwa kushirikiana na Chama cha wakadiriaji majenzi Afrika (AAQS), watakuwa wenyeji wa mkutano mkuu wa Wakadiriaji Majenzi wa Afrika utakaofanyika tarehe 18 na 19 Agosti 2016 jijini Dar es Salaam.
Katika hatua nyingine chama hicho kimemuomba Rais John Magufuli,awape kazi katika miradi ya ujenzi
NAIBU KATIBU MKUU WA WIZARA YA NISHATI NA MADINI FROF. JAMES MDOE AFUNGA MKUTANO WA JOTOARDHI JIJINI DAR ES SALAAM
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia madini,
Prof. James Mdoe ( wa nne kutoka kulia) akisoma hotuba ya ufungaji wa
mkutano wa siku tatu uliokutanisha wataalam wa masuala ya jotoardhi
kutoka katika nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Ethiopia,
Eritrea, Marekani, New Zealand na Djibouti kwa ajili ya kujadili
taarifa ya mtaalam mwelekezi kuhusu utafiti uliofanywa katika Ziwa
Ngozi lililopo mkoani Mbeya ambapo kuna viashiria vya jotoardhi
pamoja na eneo la Kibiro nchini Uganda.
Naibu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia madini,
Prof. James Mdoe (kushoto) akisisitiza jambo wakati alipokuwa akifunga
mkutano huo. Kulia ni Mjiolojia Mkuu kutoka Idara ya Nishati, Wizara ya
Nishati na Madini, Jacob Mayalla.
Sehemu
ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia kwa makini hotuba ya ufungaji
iliyokuwa inatolewa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini
anayeshughulikia madini, Prof. James Mdoe (hayupo pichani)
Tiketi za Bahati Nasibu ya Taifa kuanza kuuzwa mwezi huu
kurugenzi
Mkuu wa Bodi ya Taifa ya Michezo ya Kubahatisha nchini,Abbas Tarimba
(kulia) na wadau wengine wa michezo ya kubahatisha wakisikiliza maelezo
ya Professa Khumalo
…………………………………………………………………………………………………….
TAMKO LA WIZARA KULAANI MAUAJI YA WATU 7 MWANZA
Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto imesikitishwa na
tukio la mauaji ya watu saba wa familia moja waliokatwakatwa mapanga
baada ya kuvamiwa nyumbani, katika kijiji cha Sima wilayani Sengerema,
mkoani Mwanza, siku ya Jumatano usiku.
Wizara inalaani vikali mazingira
ya mauaji ya watu hao wa familia moja, ambapo wauaji walivamia nyumba ya
mama mjane na kumuuwa yeye mwenyewe, na watu wengine sita wakiwemo
watoto watatu.
Erasto T. Ching’oro (Msemaji)
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
12/5/2016
Matukio mengi ya ukatili dhidi yao yamekuwa yakifanyika ama shuleni au nyumbani
Na. Immaculate Makilika, MAELEZO
Utafiti ulofanywa mwaka 2009 na
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kwa kushirikiana na wadau
mbalimbali wa masuala ya watoto hapa nchini ulionyesha kuwa kuna
kiwango kikubwa cha ukatili dhidi ya watoto.




No comments :
Post a Comment