Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha
sehemu mbalimbali wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha kwa njia
ya barabara leo Mei 6, 2016. PICHA NA IKULU
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha
wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Babati Mkoani Manyara waliomsimamisha
wakati akitokea Dodoma kuelekea mjini Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akinunua
karanga kutoka kwa mjasiriamali mara baada ya kuwahutubia mamia ya
wakazi wa Babati mkoani Manyara waliojitokeza katika eneo la Stendi ya
Mabasi ya Babati Mkoani Manyara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiwahutubia na mamia ya wakazi wa Magugu mkoani Manyara wakati
akielekea Mkoani Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na wafanyabiashara wa Stendi ya Mabasi ya Singida wakati alipokuwa
njiania kuelekea Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na wakazi wa Endasak mkoani Manyara wakati akitokea Dodoma kuelekea
Arusha kwa njia ya barabara.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
na wananchi wa Dareda mkoani Manyara waliojitokeza kumsalimia wakati
akitokea Dodoma kuelekea mkoani Arusha. PICHA NA IKULU
OFISI YA RAIS-UTUMISHI YAZUNGUMZIA KUHUSU UTEKELEZAJI WA AHADI YA UADILIFU KWA WATUMISHI WA UMMA
TAMKO LA WIZARA KULAANI MAUAJI YA MAMA NA MTOTO, B/MOYO
Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto inasikitishwa na
inalaani vikali tukio la kuuawa kwa kuchinjwa, mwanamke Oliver Erasto
(23) na mtoto wake Emmanuel (3), wakazi wa eneo la Zinga, kata ya Dunda,
wilayani Bagamoyo, kutokana na wivu wa kimapenzi.
Wizara inakemea maauji hayo,
yanayodaiwa kutekelezwa na Frowin Mbwale mkazi wa Kawe, Dar es salaam,
ambaye ni mme wa marehemu, kwani yamesababisha kukatisha maisha ya mama
na mtoto, katika kipindi ambacho Taifa linahimiza uzingatiaji wa mchango
na haki za wanawake katika maendeleo ya taifa, na mwitikio wa haki ya
kuishi ya Mtoto katika mipango na programu za maendeleo endelevu.
Wizara inasisitiza kutambua kuwa
jukumu la ulinzi na usalama wa wanafamilia liko mikononi mwa kila
mwananchi, hivyo jamii inawajibu wa kusaidia udhibiti wa ukatili na
mauaji katika familia na jamii zetu. Jamii ikiwa na uelewa wa pamoja
katika haki za wanawake na watoto katika jamii, itawezesha kuwekeza
katika haki ya kuishi ya Mtoto, na kuendelea kuwaamini wanawake kwamba
wanaweza kutoa mchango mkubwa wa kuendeleza familia zao, na taifa
likaweza kupiga hatua kufikia maendeleo endelevu.
Wizara inapenda kupongeza Polisi
mkoa wa Pwani na wananchi walitoa taarifa za kuwakamata watuhumiwa wa
mauaji haya, na tunaamini kuwa watakapofikishwa mbele ya vyombo vya
sheria haki itaweza kutendeka.
Wizara inapenda kutoa pole kwa
familia za marehemu hao waliopoteza maisha kwa kuchinjwa na kuawa, na
kuwaombea kuwa na moyo wa subira katika kipindi hiki cha majonzi
makubwa. Wizara inaitaka jamii itambue kuwa hakuna mwenye haki ya
kukatisha uhai wa mtu mwingine, na mwanamke na mtoto anahaki ya
kuthaminiwa utu wake, bila ubaguzi wowote ambao unaweza kukatisha maisha
yao.
Erasto T. Ching’oro (Msemaji)
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee
The Government to issue a quarterly report on maternal death
Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and Children, Ms. Ummy Mwalimu.
…………………………………………………………………………………………….
By Jonas Kamaleki- Maelezo
The Ministry of Health,
Community Development, Gender, Elderly and Children is set to give a
quarterly report on maternal deaths during delivery in order to minimize
mothers’ deaths in the country.
This was revealed by the
Minister for Health, Community Development, Gender, Elderly and
Children, Ms. Ummy Mwalimu at the opening of the Health Women Leaders
Conference in Dar es Salaam. “My ministry will ensure that all District
Councils are providing a quarterly report on the deaths that occur
during delivery.” Said Ummy Mwalimu. These reports according to the
minister will be in line with maternal deaths reduction.
She also said the 5th Phase Government will construct rooms for operations in all health centres countrywide to rescue women’s life at delivery.
On promoting women in the decision making bodies, Ms. Ummy said she will be appointing 30 percent of women in the boards under her ministry. She mentioned such boards as the Tanzania Food and Drug Authority (TFDA), Medical Store Department (MSD) and Pharmacy Board.
On promoting women in the decision making bodies, Ms. Ummy said she will be appointing 30 percent of women in the boards under her ministry. She mentioned such boards as the Tanzania Food and Drug Authority (TFDA), Medical Store Department (MSD) and Pharmacy Board.
She noted that promotion of
women depends largely on the level of education, thus she urged girls to
study hard and perform well in order to acquire higher leadership
positions. “Fifty – fifty in leadership without education is just
politics, so girls you need to be educated so as to be considered in
high ranking leadership positions,” added Ummy Mwalimu.
Meanwhile, the Executive
Chairperson of the Tanzania Commission for AIDS (TACAIDS), Ms. Fatuma
Mrisho urged girls to be busy with studies so as to avoid involving
themselves with love affairs thus concentrating with academic issues.
She further said that when girls are fully engaged with studies they
will be free from HIV/AIDS by about 7 per cent.
Stressing on women empowerment,
the Danish Ambassador in Tanzania, Mr. Einar Hebogård Jensen said women
need to have equal access to education, healthcare, resources and
leadership. He said there was a need to respect and empower them for the
betterment of the community.
This was a pre-conference that will be followed by the largest conference on the health, rights and well-being of girls and women that will take place on 16-19 May 2016 in Copenhagen, Denmark. It will attract more than 5,000 people – world leaders, academics, policy makers, activists, media, royalty, civil society and private sector representatives.
This was a pre-conference that will be followed by the largest conference on the health, rights and well-being of girls and women that will take place on 16-19 May 2016 in Copenhagen, Denmark. It will attract more than 5,000 people – world leaders, academics, policy makers, activists, media, royalty, civil society and private sector representatives.
VIINGILIO MECHI YA YANGA, ESPERANCA
Uongozi wa Young Africans ya Dar es Salaam, umekamilisha
maandalizi yote muhimu ya mchezo dhidi ya GD Sagrada Esperanca ya Angola
wa kufuzu hatua ya makundi Kombe la Shirikisho la Barani Afrika
utakaofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kesho Jumamosi Mei 7, saa
10:00 jioni.
Mchezo huo utakaochezeshwa na waamuzi kutoka Ghana ukisimamiwa na kamishna kutoka Ethiopia.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro ametaja viingilio vya mchezo huo kuwa Jukwaa la VIP “A” kuwa ni Sh 30,000; VIP “B” na “C” Sh 20,000 wakati jukwaa la viti Rangi ya chungwa ni Sh 7,000 wakati mzunguko wa viti vya bluu na kijani ni Sh 5,000.
Kwa mujibu wa Muro, Yanga itawakosa wachezaji mahiri wawili, Donald Ngoma na Thaban Kamusoko ambao watatumia mchezo huo kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano walizoonywa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kushuka kucheza Kombe la Shirikisho.
“Tunawaomba wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yanga tujitokeze kwa wingi kesho kuishangilia timu yetu kwa nguvu na kasi kubwa,” amesema Muro ambaye alitumia nafasi hiyo kutamba kwamba Yanga ilisajili wachezaji 24 kwenye michuano inayoratibiwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).
Mchezo huo utakaochezeshwa na waamuzi kutoka Ghana ukisimamiwa na kamishna kutoka Ethiopia.
Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro ametaja viingilio vya mchezo huo kuwa Jukwaa la VIP “A” kuwa ni Sh 30,000; VIP “B” na “C” Sh 20,000 wakati jukwaa la viti Rangi ya chungwa ni Sh 7,000 wakati mzunguko wa viti vya bluu na kijani ni Sh 5,000.
Kwa mujibu wa Muro, Yanga itawakosa wachezaji mahiri wawili, Donald Ngoma na Thaban Kamusoko ambao watatumia mchezo huo kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano walizoonywa kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kabla ya kushuka kucheza Kombe la Shirikisho.
“Tunawaomba wanachama, wapenzi na mashabiki wa Yanga tujitokeze kwa wingi kesho kuishangilia timu yetu kwa nguvu na kasi kubwa,” amesema Muro ambaye alitumia nafasi hiyo kutamba kwamba Yanga ilisajili wachezaji 24 kwenye michuano inayoratibiwa na Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF).
FIFA YAILIMA FAINI SIMBA, YAPANGA KUISHUSHA DARAJA
Kamati ya idara hiyo iliyokutana
na Aprili 20, 2016 huko Zurich, Uswis ilitumia Franc 500 (sawa na Sh
1,145,500) hivyo Simba pia imeagizwa kuzilipa ikiwa ni gharama za kikao
cha kufuatilia utekelezaji sakata la mchezaji huyo, raia wa Kenya.
Simba
imeelezwa kupuuza kumlipa mchezaji Donald Musoti Omanua kwa wakati tangu
mkataba wake uvunjwe. Musoto aliyesajiliwa na Simba msimu wa 2014/15 na kuachwa alilalamika FIFA ambayo iliona ana hoja na hivyo Simba kutakiwa kumlipa dola 29,250 (sawa na Sh 62.8
milioni) na kiasi kingine anachodai ni Dola 600 (Sh 1,290,000)
zilizobaki katika usajili ambapo jumla yake ni Sh 64.2 milioni. Pia
Mosoti anamlipa Mwanasheria wake dola 2,000 (Sh 4.3 milioni) kwa ajili
ya kusimamia kesi hiyo.
Felix Majani, Mwanasheria wa
Musoti, ambaye pia ni mmoja wa wanasheria wa FIFA, alifungua kesi katika
shirikisho hilo kuwashitaki Simba kwa kukiuka makubaliano ya mkataba na
mteja wake.
Kwa kosa hilo
Simba inatakiwa kulipa faini ya kiasi hicho cha fedha ndani ya siku 30
kuanzia tarehe ya kupokea barua hiyo ya FIFA iliyoandikwa Mei 3, mwaka
huu na kufika Tanzania leo Mei 6, 2016. TFF imekuwa nakala na maagizo kuisimamia Simba inalipa kiasi hicho cha fedha.
Simba imeagizwa kulipa stahiki
zote za Mosoti ndani ya siku 30 kuanzia tarehe ya kupokea barua hiyo ya
FIFA iliyoandikwa Mei 3, mwaka huu na kufika Tanzania leo Mei 6, 2016.
Katika barua hiyo ambayo TFF ina
nakala yake, Simba imepewa amri ya kuhakikisha inalipa na isipotekeleza
agizo hilo mara moja itakatwa pointi tatu katika mechi zake Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara –VPL.
FIFA imekwenda mbali zaidi
ikisema ikiwa klabu hiyo kama haitalipa katika muda uliopangwa yaani
siku 30 kutoka sasa, FIFA itaishusha Simba daraja kutoka Ligi Kuu
Tanzania Bara hadi Ligi Daraja la Kwanza au zaidi.
Kwa upande wake, TFF imagizwa
kuhakikisha uamuzi huo unasimamiwa vema utekelezwaji wa maagizo hayo
vinginevyo itachukuliwa hatua stahiki ikiwamo kuiondoa Tanzania katika
mashindano ya kimataifa.
UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE, (JNIA), WAPATA SHIRIKA LINGINE LA NDEGE, NI MAURITIUS AIRLINES
Mfanyakazi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini, TAA, akiielekeza ndege ya Shirika la
Ndege Mauritius Airlines, kuegesha kwenye daraja la kushukia abiria (Bridge),
kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mei
6, 2016. Ndege hiyo aina ya Airbus 319 yenye uwezo wa kubeba abiria 130, imetua
kwa mara ya kwanza na itakuwa ikifanya safari zake kila Ijumaa ikiruka moja kwa
moja kutoka Mauritius kuja Dar es Salaam kasha Nairobi, nchini Kenya.
Ndege Mauritius Airlines, kuegesha kwenye daraja la kushukia abiria (Bridge),
kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Mei
6, 2016. Ndege hiyo aina ya Airbus 319 yenye uwezo wa kubeba abiria 130, imetua
kwa mara ya kwanza na itakuwa ikifanya safari zake kila Ijumaa ikiruka moja kwa
moja kutoka Mauritius kuja Dar es Salaam kasha Nairobi, nchini Kenya.
Magari ya zimamoto yakiipokea ndege hiyo kwa kuimwagia maji ikiwa ni ishara ya ukaribisho
NA
K-VIS MEDIA/Khalfan Said, JNIA
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini, TAA, kupitia uwanja wake wa ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere, imeongeza idadi ya mashirika ya ndege yanayotumia uwanja huobaada ya ndege ya kwanza ya Shirika la Ndege la Mauritius (Mauritus Airlines),
kutua kwenye uwanja huo leo Mei 6, 2016.
Ndege
hiyo aina ya Boeng Airbus 319, yenye kubeba abiria 130, ilitua kwenye uwanja
huo majira ya saa 5;20 asubuhi ambapo kama ilivyoada ya kupokea ndege mpya
inayoanza shughuli zake kwenye uwanja huo, magari mawili ya zimamoto yalipiga
(saluti), kumwagilia maji ndege hiyo wakati ikielekea kuegesha kwenye daraja la
kushukia abiria.
Kwa
mujibu wa maafisa wa Shirika hilo, ndege hiyo itakuwa ikiruka kutoka Mauritius
moja kwa moja na kutua kwenye uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere
ambapo itashusha abiria na kuelekea
uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta.
“Safari ya kutoka Mauritius kuja Dar es Slaam ni kiasi ya masaa matatu .”alisema rubani
mkuu wa ndege hiyo, Parikshant Nundlol
Maafisa wa TAA walisema kuwa ndege hiyo itakuwa ikifanya safari yake mara
moja kwa wiki kila siku ya Ijumaa.

Rubani mkuu wa ndege hiyo, Parikshany Nundlol, akizungumza na waandishi wa habari wa Mauritius waliofuatana na ndege hiyo
Warembo wa Kitanzania walioshiriki kuipokea ndege hiyo
Wafanyaakzi wa shirika la ndege la Mauritius na wale wa Swissport wakiwa katika picha ya pamoja
Abiria wa kwanza waliowasili na ndege hiyo
Mahakama Kuu imefuta rufaa ya Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP)
Na JacquilineMrisho – MAELEZO
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam imetupilia mbali rufaa iliyokatwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)
iliyokuwa ikipinga kuondolewa kwa shitaka la 8 la utakatishaji fedha
linalomkabili aliyekuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania
(TRA) Harry Kitilya na wenzake wawili.
Uamuzi huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mheshimiwa Moses Mzuna alipokuwa akitoa majibu ya rufaa iliyokuwa imekatwa na DPP.
“Ninafahamu kila kesi inaamuliwa kutokana na mazingira yake lakini nimefuta rufaa hii kwa kuwa hoja zilizotolewa hazina nguvu kisheria” alisema Jaji Mzuna.
Aidha Jaji Mzuna amefafanua kuwa hata kama amefuta rufaa hiyo lakini upande wa Jamuhuri bado una nafasi ya kubadilisha shitaka au hati nzima ya mashtaka inayowakabili washtakiwa hao.
Kwa upande wake Wakili Mkuu wa Serikali Timony Vitalis amekubaliana na uamuzi uliotolewa na Mahakama hiyo juu ya pingamizi lake ingawa bado anasimamia watuhumiwa kutofutiwa shitaka la utakatishaji wa fedha.
Naye Wakili wa Utetezi Majula Magafu amesema kuwa wao wanasubiri maamuzi yatakayotolewa na Wakili wa Serikali ili wajue namna ya kuikabili kesi hiyo.
Uamuzi huo umetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Mheshimiwa Moses Mzuna alipokuwa akitoa majibu ya rufaa iliyokuwa imekatwa na DPP.
“Ninafahamu kila kesi inaamuliwa kutokana na mazingira yake lakini nimefuta rufaa hii kwa kuwa hoja zilizotolewa hazina nguvu kisheria” alisema Jaji Mzuna.
Aidha Jaji Mzuna amefafanua kuwa hata kama amefuta rufaa hiyo lakini upande wa Jamuhuri bado una nafasi ya kubadilisha shitaka au hati nzima ya mashtaka inayowakabili washtakiwa hao.
Kwa upande wake Wakili Mkuu wa Serikali Timony Vitalis amekubaliana na uamuzi uliotolewa na Mahakama hiyo juu ya pingamizi lake ingawa bado anasimamia watuhumiwa kutofutiwa shitaka la utakatishaji wa fedha.
Naye Wakili wa Utetezi Majula Magafu amesema kuwa wao wanasubiri maamuzi yatakayotolewa na Wakili wa Serikali ili wajue namna ya kuikabili kesi hiyo.
Mtafiti wa Hesabu aomba Milioni 12 kufanikisha safari ya Marekani kuwasilisha Utafiti wake.
Anitha Jonas – MAELEZO
Dar es Salaam.
Mtanzania aliyevumbua Fomula ya
Hesabu yenye uwezo wa kutumika katika Hesabu za Viwandani Mhandisi
Mazoleka Maziku awaomba watanzania, Taasisi za Serikali na zisizo za
Kiserikali,Kimataifa na za watu binafsi kumchangia kiasi cha Shilingi
Milioni 12 kwa ajili ya kuwasilisha utafiti wake katika Mkutano wa Mwaka
wa wataalamu wa Hesabu za Viwandani nchini Marekani.
Bw. Maziku ameomba msaada huo
alipokuwa akizungumza na waaandishi wa Habari kuhusu utafiti huo
aliyoufanya kwa lengo la kuboresha fomula zinazotumika sasa hivi ambapo
kama utafiti huu utakubalika na kuanza kutumika basi unaweza kurahisisha
ukokotoaji wa hesabu zinazotumika viwandani.
Mbali na hayo mtafiti huyo
alisema fomula hiyo aliyogundua inauwezo wa kukokotoa hesabu za aina
mbili ambazo hujulikana kama (Arithmetic Progression na Sums of Powers)
ambapo hapo mwanzo zilikuwa zikitumia fomula tofauti.
“Baada ya kuwasilisha utafiti
wangu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Kitivo cha Hesabu (UDSM)kwa
ajili ya kufanya uchunguzi na uhakiki, wataalam hao walijiridhisha na
kuona vyema watume utafiti huo katika Chuo Kikuu cha Manchester
Uingereza, ambapo chuo hicho ni miongoni mwa vyuo bora Duniani na ndipo
nilipotumiwa mwaliko huu,” alisema Mhandisi Maziku.
Hata hivyo mtafiti huyo amewasihi
watanzania watakaoguswa kumchangia wanaweza kuwasiliana naye kupitia
namba 0686-632 262 au 0713 037 123 kwa ajili ya kufanikisha safari hiyo,
kwani safari hiyo itasaidia kuitangaza nchi yetu pamoja na kupata
mtandao wa wanasayansi Duniani.
Mkutano huo unatarajiwa kufanyika
huko Marekani kuanzia tarehe Julai 11 hadi 15 mwaka huu katika Chuo
Kikuu cha Massachusetts na Utahushisha wanachama zaidi ya 13,000 Duniani
pamoja na Vyuo Vikuu vya Kisayansi takribani 500 Duniani kote.
Wizara ya Afya yapokea vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi bilioni 1.4
Mwakilishi
wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro
(kulia) akikabidhi jokofu kwa kwa jaili ya huduma za chanjo kwa
Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila leo 6 Mei, 2016 jijini
Dar es Salaam.
Mwakilishi
wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt. Rufaro Chatoro
(kulia) akikabidhi jokofu kwa kwa jaili ya huduma za chanjo kwa
Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii,
Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila leo 6 Mei, 2016 jijini
Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imepokea msaada wa vifaa tiba vyenye
thamani ya shilingi bilioni 1.4 ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kutoa
chanjo kwa akina mama na watoto dhidi ya magonjwa mbalimbali nchini.
Akiongea na waandishi
wa habari Wizarani hapo, Mkurugenzi wa Huduma za Kinga, Wizara ya Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Neema Rusibimayila
ameeleza kuwa vifaa tiba hivyo vitasaidia uhifadhi wa chanjo katika
mikoa mbalimbali pamoja halmashauri nchini.
‘’Ni msaada mkubwa tulioupata
toka WHO na nina amini kuwa utatusaidia sana katika kufanikisha suala la
chanjo kwa akina mama na watoto nchini na pia tunaamini wataendela
kushirikiana na Wizara ili tuweze kufikia malengo tuliyojiwekea’’,
alisema Dkt. Rusibimayila.
Ameongeza kuwa, kwa sasa vituo
vipya vinavyofunguliwa nchini vikiwemo vile ambavyo havikuwa na majokofu
vitakuwa na uwezo wa kupata vifaa hivyo kama vile majokofu na vifaa
vingine vya tiba ili huduma za chanjo ziweze kutolewa katika kila kituo
nchini.
Akikabidhi vifaa hivyo Wizarani
hapo, Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzania Dkt.
Rufaro Chatoro amesema kuwa vifaa hivyo vyenye thamani ya shilingi
bilioni 1.4 ni pamoja na majokofu 200 pamoja na vifaa vitumikavyo kwa
ajili ya kutolea chanjo.
Kwa upande wake Mratibu Chanjo
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bwana
Emmanuel Yohana ameeleza kuwa, majokofu hayo pia yatapelekewa katika
wilaya ambayo yana upungufu wa majokofu pamoja na vituo vipya kwa ajili
ya kupunguza umbali kwa wagonjwa wa chanjo na pia ni moja ya kuweka
huduma karibu na wananchi nchini.
Aidha, ameongeza kuwa spesimeni
za polio na surua zilizotolewa na WHO zitapalekwa pia katika vituo kwa
jili ya kuchukua damu kwa ajili ya vipimo na kuletwa Dar es Salaam kwa
uchunguzi zaidi wa maabara.
‘’Wanufaika wa huu msaada
kutoka WHO ni wananchi wote wa Tanzania kwani utaenda katika vituo vyote
vya chini zikiwemo Zahanati’’, alisema Yohana.
Kupitia wadau mbalimbali Wizara
ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto inaendelea
kushirikiana na wadau hao katika kutafuta vifaa tiba mbalimbali kwa
lengo la kuhakikisha kuwa sekta ya afya nchini inaimarika kwani Tanzania
kwa sasa imeweza kudhibiti polio kwa kiasi kikubwa.
TUZILINDE HAKI ZA BINADAMU.
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
Tanzania
imechukua hatua kadhaa za kulinda na kuhifadhi haki za binadamu nchini.
Hatua hizo zinajumuisha kuridhia mikataba kadhaa muhimu ya Kimataifa na
Kikanda ya haki za binadamu, kuingiza baadhi yake kwenye sheria za nchi
na kuanzisha Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB).
Aidha, Serikali imeendelea kuimarisha Mahakama, Bunge na Vyombo vyote vinavyosimamia utekelezaji wa Sheria nchini.
Kwa mujibu
wa mapendekezo ya Azimio la Vienna la mwaka 1993 na Programu yake ya
utekelezaji, kila serikali ulimwenguni inapaswa kuandaa Mpango Kazi wa
Kitaifa wa Haki za Binadamu, ambapo kwa upande wa Serikali ya Tanzania
iliamua kuanzisha mchakato huu.
Mnamo mwaka
2009, THBUB iliongoza warsha ya Kitaifa ya Mashauriano yenye lengo la
kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa wa Haki za Binadamu ambapo warsha hiyo
ilijumuisha wajumbe mbalimbali kutoka Serikalini, Wanataaluma, Asasi za
Kiraia pamoja na Ofisi ya Umoja wa Mataifa (UN).
Mpango Kazi
huu unajumuisha mapendekezo mengi ya kimataifa na unatoa mwongozo wa
utekelezaji ulio wazi kwa Wizara mbalimbali katika kukuza haki za
binadamu nchini. Unaelezea malengo ya jumla na hatu za msingi
zinazopaswa kuchukuliwa huku ukibainisha Wizara zinazohusika.
Aidha,
Mpango huu unajumuisha Mfumo wa Ufuatiliaji na Tathmini (M&E) wenye
viashiria vinavyopimika, ambao pia unaimarisha utekelezaji wa Mpango
Kazi.
Mpango Kazi
huu utaimarisha haki za binadamu nchini Tanzania kupitia baadhi ya
malengo yakiwemo kufanya tathmini kuhusu masuala ya haki za binadamu na
kuandaa mikakati ya kukuza utoaji elimu ya haki za binadamu na kuongeza
uelewa kwa Watanzania wote.
Halikadhalika,
Mpango umebainisha haki 23 zilizoko katika makundi manne ya kimada kama
maeneo ya kipaumbele katika kuimarisha ukuzaji na ulinzi wa haki za
binadamu nchini. Haki na makundi hayo yanajumuisha Haki za kiraia na
Kisiasa, Haki za kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni, Makundi yenye
Mahitaji Maalumu, Kuimarisha Taasisi na Msuala yaliyopo ambapo Tume ya
Haki za Binadamu na Utawala Bora ikisaidiwa na Wizara ya Katiba na
Sheria pamoja na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali itafuatilia
utekelezaji wa Mpango huo.
Continue reading →TRA kugawa EFD’S 5700 kwa wafanyabiashara
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata akizungumza na
waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mwenendo wa makusanyo ya
mapato nchini kulia ni Kamishna wa kodi za ndani Bw. Yusufu Salum.
(Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO)
(Picha na Raymond Mushumbusi MAELEZO)
…………………………………………………………………………………………………
Na Lilian Lundo MAELEZO
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
imejipanga kugawa jumla ya mashine 5700 za (Electronic Fiscal Devices)
EFD’s kwa wafanyabiashara wadogo wadogo nchini ikiwa ni jitihada za
Serikali katika kukusanya mapato nchini.
Akizungumzia mipango hiyo leo, Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) Alphayo Kidata amesema wameamua kuanza kugawa mashine hizo kwa wafanyabiashara wadogowadogo ambao wengi wao hawana uwezo wa kugharamia manunuzi ya mashine hizo.
Akizungumzia mipango hiyo leo, Jijini Dar es Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) Alphayo Kidata amesema wameamua kuanza kugawa mashine hizo kwa wafanyabiashara wadogowadogo ambao wengi wao hawana uwezo wa kugharamia manunuzi ya mashine hizo.
“ Mamlaka imeona changamoto
wanayoipata wafanyabiashara wadogo hivyo imeamua kuanza kugawa mashine
hizi ili kuondokana na tatizo la kutotoa risiti za mauzo kwa
wafanyabiashara hao ambao walio wengi walikuwa na kisingizio cha
kutokuwa na mashine hizo”. Alisema Kidata.
Kamishna Kidata ameongeza kuwa
Mamlaka yake imeshaagiza mashine hizo na zipo tayari kuanza kugawiwa
mwezi huu kwa wafanyabiashara hao ikiwa ni awamu ya kwanza ya ugawagaji
wa mashine hizo ambao utafanyika nchi nzima.
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
imeazimia kugawa mashine laki mbili kwa wafanyabiashara wadogo wadogo
nchini ikiwa ni jitihada za kuweza kukusanya mapato yatokanayo na kodi
za biashara kwa urahisi na ufanisi mkubwa.
Wafanyabiashara zaidi ya 300 wakamatwa kwa kutotoa risiti za EFD’S.
Kamishna
Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata akizungumza na
waandishi wa habari (Hawapo pichani) kuhusu mwenendo wa makusanyo ya
mapato nchini.
……………………………………………………………………………………………….
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
imewakamata zaidi wafanyabiashara 300 kwa kosa la kutotumia mashine za
(Electronic Fiscal Devices) EFD’S katika biashara zao.
Akizungumzia na waandishi wa
habari Jijini Dare s Salaam, Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania(TRA) Alphayo Kidata amesema mamlaka yake imefanya uchunguzi wa
kina na kuwabaini wafanyabiashara hao katika maeneo mbalimbali nchini
wakikiuka agizo la kuwa na mashine hizo.
“ Tumeshaanza kuwapeleka
mahakamani wafanyabiashara ambao wanakwepa kulipa kodi kwa kuuza bidhaa
bila risiti na pia tumetaifisha bidhaa mbalimbali zilizoingizwa nchini
kwa njia ya magendo na kukwepa kodi “ Alisema Kidata.
Kamishna Kidata amefafanua kuwa mamlaka haitowavumilia wafanyabiashara wanaoikosesha mapato Serikali kwa kuuza na kutoa huduma bila risiti za EFD’s kwa makusudi na hasa wale wafanyabiashara wanaouza kazi za wasanii bila stempu za kodi pamoja na wafanyabiashara wanaojihusisha na magendo.
Kamishna Kidata amefafanua kuwa mamlaka haitowavumilia wafanyabiashara wanaoikosesha mapato Serikali kwa kuuza na kutoa huduma bila risiti za EFD’s kwa makusudi na hasa wale wafanyabiashara wanaouza kazi za wasanii bila stempu za kodi pamoja na wafanyabiashara wanaojihusisha na magendo.
Vilevile amefafanua kuwa, kwa
wafanyabiashara waliopelekwa mahakamani mara baada ya kumalizika kwa
kesi zao na kupewa adhabu ya kulipa faini, wakibainika tena kurudia
makosa hayo adhabu kali zaidi zitachukuliwa dhidi yao ikiwemo kifungo
cha miaka mitatu jela kwa kukaidi agizo la Serikali.
Aidha, Mamlaka imetoza faini ya
Shillingi Mil 746 kwa wafanyabiashara waliokutwa na makosa mbalimbali
yakiwemo kutotumia mashine za kielotroniki za EFD’s , kuingiza bidhaa
kimagendo na kuuza kazi za wasanii bila ya stempu ya kodi.
Mamlaka inatoa wito kwa wananchi
wote kuwa mabalozi wa kodi na kichocheo cha ukusanyaji wa mapato
kwakutimiza wajibu wao wa kudai risiti wanaponunua bidhaa au kupatiwa
huduma mbalimbali.Na Raymond
TUHUMA DHIDI YA CHUO CHA USIMAMIZI WA FEDHA (IFM) KUHUSU UTAFUNAJI WA MAMILIONI YA FEDHA
Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) kimesikitishwa na habari zilizochapishwa na gazeti la RAI Toleo la 1249 la tarehe 5 – 11 Mei 2016 ambazo ni za upotoshaji.
Tunapenda kufafanua kuwa taarifa
za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) zinaeleza kuwa,
Chuo cha Usimamizi wa Fedha kilipokea fedha za ziada kutoka Wizara ya
Fedha kwa ajili ya mishahara na fedha hizo zilishapangwa kurudishwa
ndani ya mwaka wa fedha 2015/2016 kama ripoti ya Mkaguzi ilivyoagiza
katika mwaka wa fedha wa 2014/2015. Kwa hiyo fedha hizo hazijatafunwa
wala kupotea.
Kuhusu ukusanyaji wa madeni
yaliyoripotiwa, nusu ya deni ni karo ya wanafunzi wanaolipiwa na Bodi ya
Mikopo na fedha hiyo ililipwa Chuoni ndani ya mwaka wa fedha 2014/2015.
Madeni mengine ni ya wanafunzi walioshindwa kuendelea na masomo kwa
sababu mbalimbali na madeni hayo yanafutwa kwa kufuata taratibu za
kifedha (Financial Regulation) kama Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu
za serikali alivyoelekeza.
Ufanunuzi huu ulitolewa kwa
mwandishi wa gazeti hili (Bwana Gabriel Mushi) mnamo tarehe 04-05-2016
alipoongea na Naibu Mkuu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala.
Kwa kumalizia Chuo cha Usimamizi
wa Fedha kinafanya kazi zake kwa kufuata taratibu zilizowekwa na kwa
zaidi ya miaka 30 mfululizo Chuo kimepata hati safi za mahesabu (Clean
Audit Report) kwa mujibu wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za
Serikali (CAG).
Taarifa hii imetolewa na
3 ZA AZAM FC SAWA, BADO ZA COASTAL UNION
Muda mfupi uliopita Mapunda ameimbia mbeyacityfc.com kwamba kwa kosa hilo City ilistahili kupata ushindi huo wa bao 3 na pointi 3 kama ambavyo kanuni za ligi zinavyoelekeza na kutoa angalizo kwa vilabu vyote vinavyoshiriki ligi kuu Tanzania bara kuongeza umakini katika kutunza kumbukumbu za adhabu au makosa mbalimbali kwa wachezaji wake.
“Kwenye hili nalipongeza shirikisho, hakika wametenda haki, na ninawaomba waendelee kusimama kwenye misingi ya haki, ni haki yetu kupata pointi 3 baada ya Azam fc kuchezesha mchezaji mwenye adhabu ya kadi 3 ambaye ni wazi hakustahili kucheza mchezo ule, hata sisi tumekutana na hali hii katika nyakati tofauti lakini hatukuwahi kuthubutu kumchezesha mchezaji mwenye adhabu hata kama alikuwa ni muhimu kikosini” alisema.
Akiendelea zaidi Mwenyekiti Mapunda alisisitiza vilabu kuwa makini na matukio ya aina hii huku pia akiikumbusha TFF kuendele kuchukua hatua kama hizi.
Katika hatua nyingine Mapunda amesema kuwa bado anaamini TFF itaitendea haki City kwa kuchukua hatua kama hizi kwenye mchezo dhidi ya Coastal Union uliovunjika dakika mwisho za kipindi cha pili baada ya kutokea kwa vurugu kubwa uwanjani zilizosababishwa na mashabiki wa timu hiyo ya Tanga.
“Naamini TFF watatutendea haki kwenye hili pia,mchezo ule ulikuwa na matukio mengi ya ajabu ambayo yalimfanya mwamuzi kushindwa kumaliza mchezo, risasi za moto zilipigwa uwanjani, , sisi bado tunasubiri pointi tatu zingine kutoka kwenye mchezo ule, kwa sababu mnyonge mnyongeni haki yake mpeni”, alimaliza.
Timu ya Taifa ya mchezo wa Roll yaenda Kenya
……………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
Na Mwandishi Wetu
TIMU ya Taifa ya Mchezo wa mpira
wa kuteleza(Roll Ball) imeondoka jana ikiwa na wachezaji 12 kwenda Kenya
kwenye mashindano ya kimataifa ya Afrika yatakayoanza leo mjini
Nairobi.
Kocha Mkuu wa timu hiyo,Arthur
Haule alisema jana Dar es Salaam kuwa wamejiandaa kutwaa ubingwa wa
mchezo huo utakaoshirikisha timu kutoka mikoa sita.
Alisema safari yao ambayo imedhaminiwa na Kampuni ya Nadia House of Beuty inaondoka na wachezaji 12 na viongozi wawili.
Aliwataja wachezaji
watakaowakilisha Tanzania kwenye mashindano hayo ni Mohammed Athumani,
Emmanuel Thomas, Hamisi Salum, Rajab Kassim, Omari Madohola, Yakhe
Shaaban,Jonas Emmanuel, Fahadi Waziri, Said Abdallah,Kassim Rajab,
Feruzi Juma na Clement Andrea.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Nadia
House of Beuty, Nadia Azmat akikabidhi vifaa vya michezo kwa safari hiyo
aliwataka watanzania wengine kusadia michezo ambayo haina umaarufu ili
kuibua vipaji mbalimbali vya vijana.
Nchi zinazoshiriki mashindanoi hayo ni wenyeji Kenya, Rwanda, Uganda, Tanzania, Afrika Kusini na Zambia.
MTOTO WA KITANZANIA ASHIRIKI KATIKA FILAMU YA KIMAREKANI
Tasnia ya filamu Tanzania inazidi kukua kwa kasi, si tu nyumbani hata nje ya nchi watanzania wanazidi kungara.
Safari hii mtoto wa watanzania
wenzetu aitwaye Evan Byarushengo amabahatika kupata nafasi ya kushiriki
katika filamu ya kimarekani iitwayo THE REAL MVP: The Wanda Durant
Story.
Filamu hii inajaribu kuonyesha
jinsi mama wa mchezaji nyota wa mpira wa kikapu Kevin Durant
alivyohangaika kuwakuza watoto wake mpaka kufikia kuwa mastaa. Evan
anaigiza kama Kevin Durant akiwa mtoto wa miaka 7. Waigizaji wakuu wa
filamu hii ni pamoja na Cassandra Freeman anayeigiza kama mama Evan;
Pauletta Washington (mke wake Denzel Washington) ambaye anaigiza kama
bibi
yake Evan na wengine wengi.
Juu, katika clip
mojawapo Evan akifanya mazoezi ya kucheza mpira wa kikapu. Nyuma ni
director wa filamu George Nelson na wasaidizi wake.
Juu, Evan akiwa anaongea na bibi yake (Pauletta) na mtoto anayeigiza kama kaka yake Kevin aitwaye Tony.
Juu Evan(aliyechuchumaa) akipitia script mbele ya wenzake.
Evan na mwenzake mwishoni walipata bahati ya kuonana na mama yake Kevin ambaye stori ya filamu inamuigiza.
Unaweza kuona clips za hiyo movie kupitia links hizi za youtube.
Kwa walio Marekani na Canada, movie hiyo itaonyeshwa siku ya Ijumaa na Jmosi kupitia Lifetime Channel 8/7c
Tuendelee
kumwombea mtanzania mwenzetu aende mbele zaidi ili tuzidi kuipeperusha
bendera yetu. Evan amefanya audition nyingi kwahiyo Mungu akipenda
ataonekana kwenye matangazo ya kibiashara na filamu zaidi.
Asante sana,
Dr. Philomena Ishengoma & Godfrey Byarushengo
Wazazi wa Evan
JAJI MFAWIDHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA MWANZA AFUNGUA MAFUNZO MAALUMU KWA WATUMISHI WA MAHAKAMA MKOANI MWANZA.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Mhe.Robert Vicent Makaramba akiongea katika Ufunguzi wa Mafunzo
Maalumu ya huduma kwa Wateja yanayotolewa kwa Watumishi wa Mahakama za
Mkoani Mwanza. Mafunzo hayo yameanza leo na yanatarajia kufikia tamati
kesho Mei 07,2016.
……………………………………………………………………………………
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya
Mwanza, Mhe.Robert Vicent Makaramba, amewataka watumishi wa Mahama Mkoani
Mwanza kutimiza wajibu wao kwa wananchi kwa kutoa huduma bora na kwa wakati.
Mwanza, Mhe.Robert Vicent Makaramba, amewataka watumishi wa Mahama Mkoani
Mwanza kutimiza wajibu wao kwa wananchi kwa kutoa huduma bora na kwa wakati.
Mhe.Makaramba ameyasema hayo hii leo Jijini
Mwanza, wakati akifungua Mafunzo Maalumu ya huduma kwa Watumishi
wa Mahakama za Mkoa wa Mwanza.
Mwanza, wakati akifungua Mafunzo Maalumu ya huduma kwa Watumishi
wa Mahakama za Mkoa wa Mwanza.
Amesema Mafunzo hayo yamekuja kwa
wakati ikizingatiwa kwamba Mahakama ya Tanzania kwa sasa inaendelea na
maboresho ya Utendaji kazi wake kama sehemu ya kuhakikisha kwamba inatoa huduma
iliyo bora kwa wananchi.
wakati ikizingatiwa kwamba Mahakama ya Tanzania kwa sasa inaendelea na
maboresho ya Utendaji kazi wake kama sehemu ya kuhakikisha kwamba inatoa huduma
iliyo bora kwa wananchi.
Simon Berege, amesema mafunzo hayo yanaendeshwa katika Kanda zote za
Mahakama nchini, baada ya utafiti uliofanyika mwaka 2014 kuonyesha kwamba kuna ugumu
katika upatikanaji wa habari za mahakama kwa umma hata kama habari hizo siyo za
siri.
“Tunaipongeza Mahakama kwa hatua hii
ya kukubali kutoa mafunzo kwa watumishi wake na kutoa taarifa muhimu kwa
wananchi maana mihimili mingine imekuwa ikiminya upatikanaji wa taarifa zake
hata kama taarifa hizo siyo za siri”. Amesema Berege.
ya kukubali kutoa mafunzo kwa watumishi wake na kutoa taarifa muhimu kwa
wananchi maana mihimili mingine imekuwa ikiminya upatikanaji wa taarifa zake
hata kama taarifa hizo siyo za siri”. Amesema Berege.
Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo
hayo wamesema wanatarajia kujifunza mambo mengi ikiwemo kuongeza ujuzi zaidi wa
namna ya kuwahudumia wateja (Wananchi) ili kuwafanya watambue kwamba Mahakama nchini
zinatenda haki.
hayo wamesema wanatarajia kujifunza mambo mengi ikiwemo kuongeza ujuzi zaidi wa
namna ya kuwahudumia wateja (Wananchi) ili kuwafanya watambue kwamba Mahakama nchini
zinatenda haki.
Mafunzo hayo ambayo yanafadhiriwa na
Shirika la Misaada la Ujerumani FES, yamefanyika Mkoani Mwanza baada ya mafunzo
kama hayo yaliyofanyika katika Mikoa ya Dodoma, Morogoro na Tabora kuonyesha
yameongeza ufanisi na utendaji wa Watumishi wa Mahakama katika kuwahudumia
wananchi hususani katika utoaji wa taarifa kwa umma ambapo yanawajumuisha
Mahakimu, Watunza Kumbukumbu pamoja na Maafisa Utumishi wa Mahakama.
Shirika la Misaada la Ujerumani FES, yamefanyika Mkoani Mwanza baada ya mafunzo
kama hayo yaliyofanyika katika Mikoa ya Dodoma, Morogoro na Tabora kuonyesha
yameongeza ufanisi na utendaji wa Watumishi wa Mahakama katika kuwahudumia
wananchi hususani katika utoaji wa taarifa kwa umma ambapo yanawajumuisha
Mahakimu, Watunza Kumbukumbu pamoja na Maafisa Utumishi wa Mahakama.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Mwanza, Mhe.Robert Vicent Makaramba akiongea katika Ufunguzi wa Mafunzo Maalumu ya huduma kwa Wateja yanayotolewa kwa Watumishi wa Mahakama za Mkoani Mwanza.
Washiriki wa Mafunzo ya Maalumu ya huduma kwa Wateja yanayotolewa kwa Watumishi wa Mahakama za Mkoani Mwanza.
Continue reading →RAIS DK. SHEIN AZUNGUMZA NA BALOZI MTEULE NCHINI JAPAN
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akiagana na Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini
Japan Mhe,Mathias M.Chikawe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo baada ya mazungumzo yao,[Picha na ikulu.]
…………………………………………………………………………………………………
TAHAFE YATANGAZA TAASISI 31 ZITAKAZO PELEKA MAHUJAJI KWENDA KUHIJI MAKKA
Mwenyekiti
wa Shirikisho la Taasisi za Hijja Tanzania (TAHAFE), Sheikh Abdallah
Khalid (katikati), akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam
jana, kuhusu mchakato wa kwenda kuhiji mwaka huu 2016. Kushoto ni Katibu
wa Taasisi hiyo, Dk. Ahmed Twaha na kulia ni Mjumbe, Hassan Ali.
Katibu wa Shirikisho la Taasisi za Hijja Tanzania (TAHAFE), Sheikh Abdallah Khalid , akizungumza katika mkutano huo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
……………………………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kutoa Taarifa ya vifo vya uzazi kila robo mwaka.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
akiongea na Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya
Afya katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam 5 Mei,
2016.
Balozi
wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen akiongea na
Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya katika
Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam, 5 Mei, 2016.
Balozi
wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen akiongea na
Wajumbe wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya katika
Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam, 5 Mei, 2016.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu (kushoto) pamoja na Balozi wa Denmark nchini Tanzania, Mhe. Einar Hebogard Jensen wakifurahia burudai toka kwa Vijana wakiotumbuiza stejini (hawapo pichani) wkaati wa Mkutano wa Viongozi Wanawake katika masuala ya Afya uliofanyika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam 5 Mei, 2016.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA-MAELEZO.
MAMIA WAMZIKA ANDREW NICKY SANGA (KING DREW) DODOMA
Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga Enzi za Uhai wake
Mwili
wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga (King Drew) ukiwa unawasili katika
uwanja wa Mashujaa kwa ajili ya Ibada na Kutoa kutoa Heshima za mwisho
Ibada ikiwa inaanza Baada ya Mwili wa Mpendwa wetu Andrew Nicky Sanga kuwasili
Kwaya wakiwa wanaimba wimbo wao wakati wa kujiandaa na ibada
ZANZIBAR YAADHIMISHA SIKU YA WAKUNGA DUNIANI
Waziri
wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohammed ambae
alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani
akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Baraza la Wauguzi na Wakunga
Zanzibar Profesa Amina Abdulkadr, (kulia) Waziri wa Afya Mahmoud Thabit
Kombo na (kushoto) Naibu Katibu Mkuu Wizara hiyo Halima Maulid Salum.
Waziri
wa Afya Mahmoud Thabit Kombo akimkaribisha Mgeni rasmi Waziri wa
Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi Hamad Rashid Mohammed katika
maadhimisho ya siku ya Wakunga Duniani.
WAAMUZI MECHI YA YOUNG AFRICANS, ESPERANCAWAAMUZI MECHI YA YOUNG AFRICANS, ESPERANCA
Mwamuzi Joseph Odartei Lamptey,
Jumamosi Mei 7, 2016 anatarajiwa kuwa mwamzi wa kati katika mchezo wa
kimataifa kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaozikutanisha
timu za Young Africans ya Dar es Salaam, Tanzania na GD Sagrada
Esperanca ya Angola.
Lamptey kutoka jiji la Accra,
Ghana atasaidiwa na raia wenzake wa nchi hiyo kuchezesha mchezo huo Na.
99. Mwamuzi Msaidizi Na. 1 (line 1) ni David Laryea wakati Mwamuzi
Msaidizi Na. 2 (line 2) ni Malik Alidu Salifu.
Mwamuzi Msaidizi mezani (Fourth
Official) ni Cecil Amately Fleischer huku Kamishna wa mchezo huo, akiwa
ni Asfaw Luleseged Begashaw wa Ethiopia.
Viingilio na upatikanaji wa
tiketi utatangazwa kesho Ijumaa Mei 6, 2016 na uongozi wa klabu ya Young
African mara baada ya mkutano kati ya makocha wa timu zote mbili.
Mkutano wa makocha hao utafanyika saa 5.00 mchana kwenye Ukumbi wa
mikutano wa TFF.
Mwamuzi Joseph Odartei Lamptey,
Jumamosi Mei 7, 2016 anatarajiwa kuwa mwamzi wa kati katika mchezo wa
kimataifa kuwania Kombe la Shirikisho Barani Afrika utakaozikutanisha
timu za Young Africans ya Dar es Salaam, Tanzania na GD Sagrada
Esperanca ya Angola.
Lamptey kutoka jiji la Accra,
Ghana atasaidiwa na raia wenzake wa nchi hiyo kuchezesha mchezo huo Na.
99. Mwamuzi Msaidizi Na. 1 (line 1) ni David Laryea wakati Mwamuzi
Msaidizi Na. 2 (line 2) ni Malik Alidu Salifu.
WAFANYAKAZI WA NHC WAPANDA MITI KATIKA MAKAZI YALIYOUZWA WANANCHI KIBADA NHC
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Susani Omari
akizungumza na Mameneja wa NHC na Wakurugenzi wakati wa zoezi la kupanda
miti katika Estate ya Kibada ikiwa ni jitihada za NHC kuboresha
mazingira ya eneo hilo linalokaliwa na wakazi takribani 1,000 katika
nyumba zipatazo 218 za gharama nafuu. EMT wote(Directors, Regional
Managers & Line Managers) pia wametembelea miradi ya Kawe,
Morocco Square, Victoria Place, Eco Residence na Kibada ambako
kumefanyika shughuli hiyo ya upandaji miti.
Mkurugenzi
wa Rasilimali Watu wa Shirika la Nyumba la Taifa, James Rhombo akipanda
mti wa mchikichi katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu
kama Kigamboni Housing Estate.
Mwenyekiti
wa Chama cha Wafanyakazi (TAMICO), Lilian Reuben na Meneja wa NHC,
Mtwara, Joseph John wakipanda mti katika eneo la makazi la NHC Kibada
Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.
Zoezi la kupanda miti likiendelea katika eneo la makazi la NHC Kibada Kigamboni maarufu kama Kigamboni Housing Estate.
Mandhari
ya kupendeza ya nyumba za makazi za NHC Kibada Kigamboni maarufu kama
Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara,
mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
Mandhari
ya kupendeza ya nyumba za makazi za NHC Kibada Kigamboni maarufu kama
Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara,
mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
Wajumbe
wa ziara hiyo wakisikiliza kwa makini maenelezo kutoka kwa Mkurugenzi
wa Uendelezaji Miliki wa Shirika la Nyumba la Taifa, NHC, Haikamen
Mlekio wakati wajumbe hao walipotembelea eneo hilo la makazi.
Mandhari
ya kupendeza ya nyumba za makazi za NHC Kibada Kigamboni maarufu kama
Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara,
mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
Mandhari
ya kupendeza ya nyumba za makazi za NHC Kibada Kigamboni maarufu kama
Kigamboni Housing Estate inavyoonekana mchana huu, hizo ni barabara,
mataa na mitaro ya nyumba hizo zinavyoonekana leo hii.
Timu ya Menejimenti ya NHC nchi nzima yatembelea miradi ya shirika hilo jijini Dar es salaam
Meneja
Mradi wa Shirika la nyumba la Taifa NHC Kawe unaokwenda kwa jina la 711
Injinia Samwel Metil akitoa maelezo kwa Timu ya Menejimenti ya NHC
wote(Directors, Regional Managers & Line Managers) wakati
walipotembelea miradi ya 711 Kawe , Morocco Square, Victoria Place, Eco
Residence na Kibada ambapo ambapo pia watafanya pia kazi katiia miradi
hiyo Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kuwafahamisha juu ya maendeleo na
changamoto za miradi hiyo.
Mmoja wa Mainjinia wa Mradi wa
711 Kawe Bw.Kishor Hirani akimelezea jambo Meneja mradi Injinia Samwel
Metil wakati menejimenti ya shirika hilo ilipotembelea katika mradi huo.
Wakuu wa vitengo mbalimbali na mameneja wa mikoa wakitembelea mradi wa 711 Kawe leo.
Mmoja wa Mameneja wa NHC kutoka
mkoani Dodoma Bw. Itandula Gambalagi pamoja na wenzake wakiwasili
kutembelea mradi wa Morocco Square.
Mameneja hao wakifuatilia maelezo ya mradi wa Morocco Square
Muungano Saguya kulia Yahya
Charahani kushoti na Itandula Gambalagi wakijadiliana jambo wakati
walipotembelea mradi wa 711 Kawe pamoja na wenzao.
Jengo la Mradi wa Eco Residents ambalo limekamilika kwa asilimia 99%.
Ujenzi wa mradi wa 711 Kawe ukiendelea.
CCM YAKANUSHA UZUSHI ULIOENEA KUHUSU MCHAKATO WA UENYEKITI WA CCM
Baadhi
ya vyombo vya habari vimekuwa vinatoa taarifa potofu kuhusu mchakato wa
Mwenyekiti wa sasa wa CCM Dkt. Jakaya Kikwete kukabidhi kijiti cha
uongozi wa CCM kwa Rais John Pombe Magufuli kama ilivyo mila na desturi
ya Chama Cha Mapinduzi.
Yamekuwepo madai eti Mwenyekiti amekataa au anachelewesha kukabidhi kijiti.
Habari hiyo sio kweli kabisa na
ni kinyume chake, kwani Dkt. Kikwete amekuwa akisisitiza kukabidhi
madaraka mapema iwezekanavyo. Kwa ajili hiyo kwenye kikao cha Mei 3,
2016 alikataa kusiongezwe agenda nyingine ambazo zitalazimisha Mkutano
Mkuu Maalum kuchelewa kufanyika kwa sababu ya kukamilisha maandalizi ya
agenda hizo. Alisisitiza agenda iwe moja tu.
Dhamira ya kufanyika Mkutano Mkuu
maalum mwezi Juni, 2016 iko pale pale. Kilichoelezwa kwenye kikao ni
kutaka kukamilisha utaratibu wa kupata fedha za kugharamia mkutano huo.
Taratibu zikikamilika tarehe itapangwa. Mipango ya kutafuta pesa
inaendelea na ikikamilika tarehe itatangazwa.
Tunawataka wana-CCM wasihamanike
wala kubabaishwa na taarifa za upotoshaji zinazofanywa na watu wenye nia
mbaya na CCM. Hawa ni wale wale ambao wamekuwa wakiiombea mabaya CCM
bila ya mafanikio.
Pia tunapenda kukanusha madai ati
kuwa Mwenyekiti Kikwete aliwatahadharisha Wajumbe wa Kamati Kuu kuhusu
ukimya wa Ndugu Edward Lowassa. Hakuna wakati wowote kauli kama hiyo
aliitoa. Ni uzushi mtupu. Jina la Ndugu Lowassa halikutajwa kabisa.
Aidha, tunapenda kukanusha madai
ya kufanyika mkutano baina ya Mwenyekiti wa CCM, Rais wa Jamhuri ya
Muungano, Makamu wa Rais na Katibu Mkuu wa CCM kuhusu uchaguzi wa Katibu
wa Kamati ya Wabunge wa CCM. Hapajawahi kufanyika mkutano wa aina hiyo
siku yoyote na mahali popote. Hivyo madai ya kuwepo kwa tofauti baina ya
Viongozi wakuu kuhusu nani achaguliwe kuwa Katibu wa Wabunge wa CCM
hayana msingi wowote.
Kamati Kuu iliteua Wabunge wanne
kugombea na kuwaachia Wabunge wa CCM kuamua. Kuhusisha Viongozi na hasa
kuzua kuwepo kutokuelewana ni jambo la kusikitisha. Ni taarifa ya uongo
yenye nia ovu kwa CCM na Viongozi wake.
Tunapenda kuwatahadharisha
waandishi wa habari kuandika habari za ukweli. Waache kuzua mambo yenye
kupandikiza chuki na mgawanyiko usiostahili kuwepo ndani ya CCM na
kuyaeneza kwa watu. Waheshimu maadili ya kazi zao.
Napenda kuwahakikishia na kusisitiza kuwa hakuna mgogoro wa kukabidhi kijiti cha uenyekiti katika CCM na wala hautakuwepo.
Imetolewa na;
Ndugu Christopher Ole Sendeka
MSEMAJI WA CCM
MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
MJUMBE WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,
05/05/2016










No comments :
Post a Comment