LAPF
imedhamini kongamano la Jeshi la Polisi (Vikosi vya masuala ya tiba)
uliofanyika mjini Tabora. Mfuko wa Pensheni wa LAPF umetoa kiasi cha
Shilingi milioni 6,200,000/= katika kufanikisha kongamano la Maafisa
wa Polisi kutoka mikoa yote Tanzania maalum kwa ajili ya kujipima na
kujadili changamoto mbalimbali za kitengo cha tiba ndani ya jeshi la
polisi (medical wing) Wawakilishi kutoka mikoa yote Tanzania walishiriki
katika kongamoano hilo wakiwa ni maofisa waandamizi wa jeshi hili la
polisi. katika kongamano hilo Mfuko ulipata wasaa wa kuwasilisha mada
kuhusu fursa mbalimbali zitolewazo na Mfuko lakini pia mada ya
maandalizi kabla ya kustaafu ilitolewa katika mkutano huo , udhamini huu
una synergy kubwa na mfuko katika kusajili wanachama wapya ndani ya
jeshi la polisi.
Mkurugenzi
wa Huduma kwa Wanachama Mfuko wa Pensheni LAPF Bw. Valerian Mablangeti
akitoa mada kuhusu Mfuko ikijumuisha maandalizi kabla ya kustaafu,
Maafisa waandamizi wa jeshi la Polisi wakisiliza kwa makini katika
kongamano la jeshi hili lililofanyika mjini Tabora hivi karibuni.
Kamanda
wa Jeshi la Polisi ACP Paul Kasabago akipokea mfano wa hundi yenye
thamani ya TZS. 6,200,000/= iliyotolewa na Mfuko wa Pensheni LAPF
kuwezesha kongamano la Maafisa wa Polisi kutoka mikoa yote Tanzania
(medical wing) mjini Tabora. Wanaokabidhi kutoka LAPF ni Mkurugenzi wa
Huduma kwa wanachama Bw. Valerian Mablangeti, Mkurugenzi wa Utawala na
Rasilimali Watu Bw. Desdery Sigonda pamoja na Meneja Kanda ya Dar es
Salaam Bi. Amina Kassim.
Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Polisi wakifuatilia kwa makini mada toka Mfuko
wa Pensheni LAPF kwenye kongamano la Jeshi hili lililofanyika mjini
Tabora ambapo maafisa hao walivutiwa na kujiunga na mfuko wa uchangiaji
wa hiari ikiwa ni maandalizi kabla ya kustaafu.
Mmoja
ya Maafisa waandamizi walioshiriki kongamamo la jeshi la Polisi mkoani
Tabora hivi karibuni akiuliza namna ya kujiunga kwa hiari na Mfuko wa
Pensheni wa LAPF mara baada Mkurugenzi wa Huduma kwa Wanachama
kuwasilisha mada kuhusu fursa mbalimbali zitoleawazo na Mfuko wa
Pensheni wa LAPF.
Visa na mikasa,Vilio na majonzi kumbukumbu ya makovu katika filanu ya Scars
MATUKIO ZAIDI RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI UZINDUZI WA MAJENGO YA NSSF NA PPF MKOANI ARUSHA LEO
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli
akiwahutubia na wafanyakazi wa PPF na NSSF pamoja na wananchi wa jiji la
Arusha kabla ya kufungua rasmi jengo la la Kitega uchumi la Mfuko wa
Pensheni wa PPF jijini Arusha. PICHA NA IKULU
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza
jambo na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mipango kabla ya
kufungua rasmi jengo la la Kitega uchumi la Mfuko wa Pensheni wa PPF
jijini Arusha.
Meya
jiji la Arusha mstahiki Calist Lazaro Bukhai akimshukuru Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya
ufunguzi rasmi wa Jengo la Kitega uchumi la Mfuko wa Pensheni wa PPF
jijini Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia
wakati kikundi cha ngoma za asili cha kimasai kilipokuwa kikitumbuiza
pembezoni mwa jengo la kitega uchumi la NSSF jijini Arusha.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisikiliza
maelezo ya mradi wa ujenzi wa Jengo la kitega uchumi la NSSF Mafao House jijini Arusha
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mipango, Waziri wa Kazi wa nchi
ofisi ya Waziri Mkuu,Sera, Bunge kazi ajira na vijana Jenista Mhagama
wakifunua pazia kuashiria ufunguzi rasmi wa jengo la kitega uchumi la
NSSF Mafao House jijini Arusha.
MAPITIO YA HOJA MBALIMBALI ZA WABUNGE MJINI DODOMA.
| Naibu Waziri, Wizara ya Nishati na Madini, Mhe. Medard Kalemani akijibu baadhi ya hoja za Wabunge zilizoihusu Wizara ya Nishati na Madini wakati wa kipindi cha jioni Bungeni mjini Dodoma. |
| Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mwigulu Nchemba (Mb) (kulia) akijibu baadhi ya hoja za baadhi ya Wabunge wakati wa mapitio ya hoja mbalimbali jioni bungeni mjini Dodoma. |
| Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Charles Mwijage (Mb) akijibu hoja za Wabunge mbalimbali wakiochangia hotuba ya Wizara yake leo jioni Bungeni mjini Dodoma. |
(Picha zote na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma)
SHAKA: KIKWETE AMETOA JASHO JINGI KUITUMIKIA TANZANI
Kaimu katibu mkuu wa UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka akiwa anaongea na wananchi wa tanga
…………………………………………………………………
Na Woinde Shizza,Tanga
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM )umevitaka vyama vya
upinzani wanaopika maneno ya kipuuzi yenye lengo la kuwagongajisha viongozi wa CCM wakome na wamuache Mwenyekiti wa CCM Dk Jakaya
Kikwete astaafu kwa heshima kwasababu ameitumikia nchi yake kwa kutoa jasho jingi miaka kumi iliopita
Aidha umoja huo umesisitiza kuwa kazi aliyoifanya Dk Kikwete katika uongizi wake wa miaka kumi kisiasa na kiserikali utabaki kwenye vitabu
vya kumbukumbu ya historia iliotukuka hususan kila utakapokumbukwa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM mwaka 2015.
Kaimu katibu mkuu wa uvccm shaka hamdu shaka ameyasema hayo wakati alipozungumza na viongozi na wanachama wa uvccm na ccm kwenye ukumbi
wa TANU Hall mjini Tanga.
Alisema baada ya upinzani sasa kujiona hawana hoja na hakubaliki
katika jamii maadui wa kisiasa wanotimiwa na nafisadi wamekuwa
wqkijaribu kupika uzushi na kutaka kuionyesha jamii kwamba viongizi wa
chama tawala hawana maelewano.
“Nakupeni usia viongozi wa Ukawa ambao sasa mmekuwa wakiwa , mambo ya
ngoswe waachieni ngoswe wenyewe, viongozi wa ccm hawagombani,
hawajawahi kugombana na kamwe hawatagombana milele “alisema shaka
Aliwataka viongozi hao kutazama mustakabali wao kisiasa na kuachana na
ccm kwasababu chama hicho tawala haiwezekani kubomoka kwa maneno ya
jikoni , vijiweji au vichochoroni.
Shaka alisisitiza kuwa mwenyekiti wa ccm Dk Kikwete wakati akiwa Rais
ameitumikia nchi yake kwa kadri ya uwezo wake kama ambavyo
walivyotenda na kuitumikia nchi viongozi watangulizi wake akiwemo
baba wa Taifa Mwalimu julius Nyerere, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee
Benjamin Mkapa na yeye ametenda kwa uwezo wake kama atakavyotenda Rais
Dk John Magufuli katika kipindi chake.
“Mtu mwenye akili timamu kila atakaposafiri akiizunguuka nchi yetu na
kupita juu ya barabara za lami, ujenzi wa madaraja, kutanuka kwa
mawasiliano, kukua uchumi wa Taifa na wa mtu mojmoja na wananchi iushi
katika nyumba za kisasa lazima utamkunbuka Kikwete taka usitake
“alieleza Kaimu huyo katibu mkuu .
Alisema kila zama ina kitabu na Nabii wake hivyo mema yaliofanywa na
kiongozi mmoja aliyemaliza muda wake yanahitaji kuheshimiwa kwasababu
Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli wote ni watoto wa baba na
mama mmoja.
Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM )umevitaka vyama vya
upinzani wanaopika maneno ya kipuuzi yenye lengo la kuwagongajisha viongozi wa CCM wakome na wamuache Mwenyekiti wa CCM Dk Jakaya
Kikwete astaafu kwa heshima kwasababu ameitumikia nchi yake kwa kutoa jasho jingi miaka kumi iliopita
Aidha umoja huo umesisitiza kuwa kazi aliyoifanya Dk Kikwete katika uongizi wake wa miaka kumi kisiasa na kiserikali utabaki kwenye vitabu
vya kumbukumbu ya historia iliotukuka hususan kila utakapokumbukwa mchakato wa kumpata mgombea urais wa CCM mwaka 2015.
Kaimu katibu mkuu wa uvccm shaka hamdu shaka ameyasema hayo wakati alipozungumza na viongozi na wanachama wa uvccm na ccm kwenye ukumbi
wa TANU Hall mjini Tanga.
Alisema baada ya upinzani sasa kujiona hawana hoja na hakubaliki
katika jamii maadui wa kisiasa wanotimiwa na nafisadi wamekuwa
wqkijaribu kupika uzushi na kutaka kuionyesha jamii kwamba viongizi wa
chama tawala hawana maelewano.
“Nakupeni usia viongozi wa Ukawa ambao sasa mmekuwa wakiwa , mambo ya
ngoswe waachieni ngoswe wenyewe, viongozi wa ccm hawagombani,
hawajawahi kugombana na kamwe hawatagombana milele “alisema shaka
Aliwataka viongozi hao kutazama mustakabali wao kisiasa na kuachana na
ccm kwasababu chama hicho tawala haiwezekani kubomoka kwa maneno ya
jikoni , vijiweji au vichochoroni.
Shaka alisisitiza kuwa mwenyekiti wa ccm Dk Kikwete wakati akiwa Rais
ameitumikia nchi yake kwa kadri ya uwezo wake kama ambavyo
walivyotenda na kuitumikia nchi viongozi watangulizi wake akiwemo
baba wa Taifa Mwalimu julius Nyerere, Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mzee
Benjamin Mkapa na yeye ametenda kwa uwezo wake kama atakavyotenda Rais
Dk John Magufuli katika kipindi chake.
“Mtu mwenye akili timamu kila atakaposafiri akiizunguuka nchi yetu na
kupita juu ya barabara za lami, ujenzi wa madaraja, kutanuka kwa
mawasiliano, kukua uchumi wa Taifa na wa mtu mojmoja na wananchi iushi
katika nyumba za kisasa lazima utamkunbuka Kikwete taka usitake
“alieleza Kaimu huyo katibu mkuu .
Alisema kila zama ina kitabu na Nabii wake hivyo mema yaliofanywa na
kiongozi mmoja aliyemaliza muda wake yanahitaji kuheshimiwa kwasababu
Nyerere, Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli wote ni watoto wa baba na
mama mmoja.
MATUKIO KUTOKA BUNGENI MIJINI DODOMA
Mbunge
wa Jimbo la Muleba Kusini Mhe.Profesa Anna Tibaijuka na Katibu wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Thomas Kashilila
wakibadilishana mawazo leo mjini Dodoma .
Mbunge
wa Jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe akichangia mjadala wa hoja
ya hotuba ya bajeti ya Wizara ya Viwanda , Biashara na Uwekezaji leo
mjini Dodoma.
Picha na MAELEZO-Dodoma.
MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WAENDELEA KUPUNGUA.
Mtaalam
wa Uchumi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam Prof. Haji Semboja
akifafanua kwa waandishi wa Habari kuhusu mwenendo wa uchumi wa
Tanzania.
Waandishi
wa Habari wakiwa kazini, wakati Ofisi ya Taifa ya Takwimu ikitangaza
Mfumuko wa Bei Mwezi Aprili 2016 leo jijini Dar es salaam.
……………………………………………………………..
Na. Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dar es salaam.
Ofisi ya Taifa ya Takwimu
imetangaza Mfumuko wa Bei wa Taifa wa mwezi Aprili 2016 na kusema kuwa
umepungua kidogo hadi kufikia asilimia 5.1 kutoka asilimia 5.4
iliyokuwepo mwezi Machi, 2016.
Hii inamaanisha kuwa kasi ya
upandaji wa bei ya bidhaa na huduma kwa mwezi Aprili 2016 imepungua
kidogo ikilinganishwa na kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa na huduma
iliyokuwepo mwezi Machi mwaka huu.
Mkurugenzi wa Sensa ya Watu na
Takwimu za Jamii wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Ephraim
Kwesigabo ametoa taarifa hiyo leo jijini Dar es salaam na kueleza kuwa
kupungua kwa mfumuko huo kumesababishwa na kupungua kwa kasi ya bei ya
bidhaa za vyakula na bidhaa zisizo za vyakula katika maeneo mbalimbali
nchini.
Amesema Takwimu zilizokusanywa
katika mikoa yote ya Tanzania Bara kwenye bidhaa zinazotumika kupima
mfumuko wa bei kwa mwezi Aprili 2016 zimeainisha kuwa bidhaa zisizo za
vyakula katika soko zikiwemo Gesi , dizeli na mafuta ya taa zimechangia
kupungua kwa mfumuko huo.
Amesema kuwa pamoja na kupungua
kwa kasi ya upandaji wa bei ya bidhaa hizo kwa mwezi Aprili 2016, baadhi
ya bidhaa za vyakula ikiwemo mchele, unga wa Mahindi na mkaa ilionyesha
kuongezeka katika kipindi hicho.
Akizungumzia Kuhusu Fahirisi za
Bei ambacho ni kipimo kinachotumika kupima mabadiliko ya bei ya bidhaa
na huduma zinazotumiwa na kaya binafsi hapa Tanzania kwa mwezi Machi na
Aprili Bw. Kwesigabo amesema kuwa zimeongezeka hadi kufikia 102.46
kutoka 101:93 za mwezi Aprili.
Amesema kuwa tofauti na mwezi
Machi bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi kwa mwezi
Aprili ni unga wa muhogo, dagaa, choroko, maziwa ya ungana na matunda
aina ya machungwa.
Aidha,bidhaa zisizo za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa fahirisi za bei ni pamoja na mvinyo, bia kuni na mazulia.
Kwa upande wa uwezo wa shilingi
100 ya Tanzania katika kununua bidhaa na huduma za mlaji kwa mwezi
Aprili, 2016 umefikia shilingi 97 na senti 60 ikilinganishwa na uwezo wa shilingi 98 na senti 11 wa mwezi Machi 2016.
“Uwezo wa shilingi 100 ya
Tanzania katika kununua bidhaa na huduma zilezile kwa mlaji kwa mwezi
Aprili 2016 umepungua, hii ina maana kuwa sasa mtu anahitaji kuongeza
ya shilingi 2.40 ili aweze kununua bidhaa na huduma sawa na zile
alizokuwa na uwezo wa kuzinunua mwezi Machi ” Amesema Kwesigabo.
Kwa upande wa mfumuko wa Bei kwa nchi za Afrika Mashariki mwezi Machi, 2016, Kwesigabo amesema una mwelekeo unaofanana; Kenya umepungua
kidogo hadi kufikia asilimia 5.27 kutoka 6.45 huku Uganda ukifikia
asilimia 5.1 kutoka asilimia 6.2 zIlizokuwepo mwezi Machi 2016.
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete AAGWA LEO NA BALOZI WAPYA CHIKAWE NA KISAMBA
Mwenyekiti
wa CCM, Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akiagana na Balozi Mpya wa Tanzania
nchini Japani, Balozi Mathis Chikawe, baada ya mazungumzo yao, Balozi
huyo alipofika kumuaga katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM,
Lumumba, Dar es Salaam, leo, Mei 9, 2016.
Balozi
wa Tanzania nchini Urusi, Balozi Mathew Kisamba akisaini kitabu cha
wageni, alipofika kumuaga Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya
Kikwete, katika Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es
Salaam, leo.
(Picha na Bashir Nkoromo).
RAIS DKT. MAGUFULI AZINDUA JENGO LA KITEGAUCHUMI LA MFUKO WA PENSHENI PPF JIJINI ARUSHA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akikata utepe
kuzindua rasmi, Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni (PPF) lililopo Mtaa
wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016. Wa pili (kushoto) ni Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira,
Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenister Mhagama, (kushoto) ni Meya wa jiji
la Arusha, Calist Lazaro (wa kwanza kutoka kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini
ya PPF, Ramadhan Kijjah, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio na Waziri wa Fedha
na Mipango, Dkt. Phillip Mpango.
kuzindua rasmi, Jengo la Kitegauchumi la Mfuko wa Pensheni (PPF) lililopo Mtaa
wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016. Wa pili (kushoto) ni Waziri wa Nchi
Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Uratibu na Bunge, Kazi, Ajira,
Vijana na Watu wenye Ulemavu, Mhe. Jenister Mhagama, (kushoto) ni Meya wa jiji
la Arusha, Calist Lazaro (wa kwanza kutoka kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini
ya PPF, Ramadhan Kijjah, Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio na Waziri wa Fedha
na Mipango, Dkt. Phillip Mpango.
Picha zote na Mafoto Blog
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akimpongeza Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, baada ya kuweka Jiwe la Msingi
la uzinduai wa Jengo la Kitegauchumi la Mfuko huo lililopo Mtaa wa Korido
Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio, baada ya kuweka Jiwe la Msingi
la uzinduai wa Jengo la Kitegauchumi la Mfuko huo lililopo Mtaa wa Korido
Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
Jengo hilo lililozinduliwa leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, akihutubia wakazi
wa arusha na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakati alipozindua rasmi, Jengo
la Kitegauchumi la Mfuko huo (PPF)
lililopo Mtaa wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
wa arusha na wadau wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakati alipozindua rasmi, Jengo
la Kitegauchumi la Mfuko huo (PPF)
lililopo Mtaa wa Korido Jijini Arusha leo Mei 9, 2016.
Sehemu ya wadau kutoka NSSF waliohudhuria uzinduzi huo wa wenzao wa PPF.
Sehemu ya wadau wakimsikiliza Mhe. Rais Dkt. Magufuli…..
Baadhi ya wafanyakazi wa PPF Kanda yas Arusha wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Sehemu ya wananchi wa Jiji la Arusha wakimsikiliza Mhe. Rais Dkt. Magufuli…..
Wananchi wakimshangilia Mhe Rais wakati akihutubia…..
Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mhe Rais.
Baadhi ya Wakurugenzi wa Mfuko wa Pensheni wa PPF wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Baadhi ya Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Pensheni PPF na
Wakurugenzi wa Mfuko wa huo wakimsikiliza Mhe Rais wakati akihutubia.
Baadhi ya viongozi na wadau wa Mfuko huo na Meya wa Jiji la Arusha Calist Lazaro (kushoto) wakimsikiliza Mhe Rais.
Continue reading →WATANZANIA KUSHUHUDIA COPA AMERICA LIVE KUPITIA STARTIMES
Meneja
Uhusiano wa Kampuni ya StarTimes Tanzania, Mohamed Kimweri (kushoto),
akizungumza katika na waandishi wa habari Dar es Salaam leo, kuhusu
kampuni hiyo kupata haki za kuonesha michuano ya Copa Amerika moja kwa
moja ambayoitafanyika nchini Marekani kuanzia Juni 3 mpaka Juni 26 mwaka
huu. Kulia ni Meneja Maudhui wa kampuni hiyo, Paulina Kimweri.
Meneja Maudhui wa kampuni hiyo, Paulina Kimweri, akizungumza katika mkutano huo.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
…………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
KAMPUNI
ya StarTimes Tanzania imefanikiwa kupata haki za kuonyesha michuano ya
Copa America moja kwa moja ambayo itafanyika nchini Marekani kuanzia
Juni 3 mpaka Juni 26 mwaka huu.
Akizungumza
na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi wakati wa uzinduzi huo
Makamu wa Rais wa kampuni hiyo nchini, Zuhura Hanif alisema kuwa
kupatikana kwa haki za kuonyesha michuano hiyo mikubwa na mikongwe
ulimwenguni ikiwa inatimiza miaka 100 tangu kuanzishwa kwake ni jitihada
za kuhakikisha kuwa wateja wao wanafurahia vipindi bora vya michezo na
burudani.
“Leo
StarTimes inayo habari njema kuwataarifu kuwa tumepata haki maalum za
kuonyesha michuano ya Copa America moja kwa moja kutoka nchini Marekani
kuanzia Juni 3 mpaka Juni 26 mwaka huu. Ninaposema haki maalumu manake
ni kwamba watanzania hawataweza kushuhudia michuano hii sehemu yoyote
isipokuwa kupitia king’amuzi cha
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.
MWANAFUNZI
WA DARASA SITA SHULE YA MSINGI TUYOMBO AFARIKI DUNIA NA MWINGINE
KUJERUHIWA BAADA YA PIKIPIKI WALIOKUWA WAKISAFIRIA KUGONGWA NA GARI.
MTEMBEA KWA MIGUU AFARIKI DUNIA PAPO HAPO BAADA YA KUGONGWA NA GARI.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATANO WAKIWA WANASAFIRISHA NA KUPAKIA SUKARI BILA KIBALI.
Katika Tukio la Kwanza:
Mwanafunzi wa Shule ya Msingi
Tuyombo darasa la sita iliyopo Wilaya ya Mbeya Vijijini aliyefahamika
kwa jina la TIMOTH PHILIMON (14) amefariki dunia baada ya Pikipiki
waliyokuwa wakisafiria ikiendeshwa na dereva aitwaye MATHIAS TIELI
MARIRA (32) mkazi wa Inyala yenye namba za usajili T. 791 BPM aina ya
T-Better kugongwa kwa nyuma na Gari.
Ajali hiyo ilitokea mnamo tarehe
08.05.2016 majira ya saa 19:15 jioni huko Kijiji cha Shamwengo, Kata ya
Inyala, Tarafa ya Tembela, Wilaya ya Mbeya Vijijini, Mkoa wa Mbeya.
Inadaiwa kuwa Gari yenye namba za
usajili T. 126 BEL aina ya Mitsubishi Fuso ikiendeshwa na dereva
aliyefahamika kwa jina la FRANSIS S/O ALEX NYIGU (48) mkazi wa Makambako
ilimgonga mwendesha Pikipiki huyo ambaye aliyekuwa mbele yake
kusababisha kifo cha mwanafunzi TIMOTH PHILIMON ambaye alikuwa abiria
kwenye Pikipiki hiyo.
Aidha katika ajali hiyo mwendesha
pikipiki MATHIAS TIELI MARIRA alijeruhiwa na anaendelea na Matibabu.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Mbeya. Chanzo cha
ajali ni mwendo kasi. Mtuhumiwa amekamatwa.
Katika Tukio la Pili:
Mtembea kwa miguu mwanamke
asiyefahamika jina umri kati ya miaka 30 hadi 40 alifariki dunia papo
hapo baada ya kugongwa na Gari yenye namba za usajili T. 696 yenye Tela
namba T.589 BCG aina ya Scania ikiendeshwa na dereva DAVID MALILA (28)
mkazi wa Makambako.
Ajali hiyo ilitokea mnamo tarehe
08.05.2016 majira ya saa 08:00 asubuhi huko eneo la Nsalaga, Kata ya
Nsalaga, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya.
Inadaiwa kuwa chanzo cha ajali
hiyo ni baada ya tairi ya Gari hilo kuchomoka na kwenda kumgonga
mwanamke huyo ambaye alikuwa akitembea kwa miguu pembezoni mwa Barabara.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Mbeya. Dereva
alikimbia mara baada ya tukio, upelelezi unaendelea.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya
Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi JUSTUS A. KAMUGISHA anatoa wito
kwa madereva kuwa makini wanapotumia vyombo vya moto ikiwa ni pamoja na
kufuata na kuheshimu sheria na alama za usalama barabarani ili kuepuka
ajali zinazoweza kuepukika. Lakini pia anatoa wito kwa watumiaji wengine
wa barabara wakiwemo watembea kwa miguu nao wachukue tahadhari pindi
wanapotumia barabara.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya kwa
kushirikiana na Maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(PCCB) na Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tawi la Mbeya
linawashikilia watu watano ambao ni PIUS KIKO (43) mkazi wa Sae Jijini
Mbeya ambaye alikuwa akisafirisha sukari katoni 52 kwenye Gari yenye
namba za usajili T.724 DCF aina ya Toyota Coaster bila kibali.
Mtuhumiwa akiwa na wenzake
alikamatwa mnamo tarehe 08.05.2016 majira ya saa 11:00 asubuhi katika
Operesheni hiyo maalum iliyofanyika eneo la Kabwe, Kata ya Ruanda,
Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya.
Aidha Jeshi la Polisi kwa
kushirikiana na Maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(PCCB) na Maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) tawi la Mbeya
waliendelea na Operesheni hiyo eneo la Soweto na kufanikiwa kumkamata
mfanyabiashara aitwaye BUSHIRI BONIFACE (45) mkazi wa Soweto akiwa na
mifuko 27 ya sukari kila mmoja ukiwa na uzito wa kilogram 50 akiweka
katika mifuko midogo ya kilo moja bila kibali.
Mtuhumiwa alikamatwa mnamo tarehe
08.05.2016 majira ya saa 15:00 alasiri huko eneo la Soweto, Kata ya
Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jiji na Mkoa wa Mbeya katika Operesheni
maalum. Watuhumiwa watafikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi
kukamilika.
Imesainiwa na:
(JUSTUS A. KAMUGISHA – SACP)
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA
Dar Kuongeza madampo kukabiliana na uchafu Jijini
Na Lilian Lundo – Maelezo
………………………………………
Baraza la Madiwani la Halmashauri
ya Jiji la Dar es Salaam limeazimia kuongeza idadi ya madampo na
kurekebisha miundombinu ya dampo la Pugu ili kuhakikisha jiji linakuwa
safi.
Akiongea na waandishi wa habari
leo jijini Dar es Salaam Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam Mhe.
Isaya Mwita alisema Baraza hilo limeazimia kuongeza na kurekebisha
miundombinu baada ya ziara walioifanya na kugundua mapungufu katika
dampo la Pugu.
“Tumegundua kuna udhaifu mkubwa
katika dampo la Pugu, magari yanayopeleka taka yananasa barabarani hivyo
tukaona kuna sababu ya kutengeneza miundombinu, hivyo tumetenga milioni
700 kwenye bajeti hii ili kutengeneza barabara hiyo,”alisema Mhe.
Mwita.
Aidha, alisema kwamba baraza
limetenga kiasi cha shilingi milioni 200 katika bajeti ya 2016/17 ili
kununua eneo Mkuranga kwa ajili ya dampo, huku wakiendelea na mchakato
wa kuongeza madampo mengine Kigamboni na Kisarawe ili kuhakikisha taka
zote zinazozalishwa ndani ya jiji la Dar es Salaam zinapelekwa kwenye
madampo badala ya kuzagaa mitaani.
Kwa upande wake, Naibu Meya wa
jiji la Dar es Salaam Mhe. Mussa Kafana alisema kuwa, suluhisho la
kumaliza taizo la uchafu si kuwa na dampo tu bali ni kuwepo kwa vifaa
maalumu vya kuhifadhi taka. Hivyo baraza likaamua kuwepo na vyombo vya
kuhifadhia taka katika mitaa yote ya jiji la Dar es Salaam ili kudhibiti
uzagaaji wa taka.
Usafi ni moja ya kipaumbele cha
Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambapo kwa mara ya
kwanza alitangaza siku ya Uhuru wa Tanzania (Tisa Desemba) iazimishwe
kwa kufanya usafi nchi nzima ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko
ikiwemo Kipindupindu pamoja na kuiweka Tanzania katika hali ya usafi.
`
Wawekezaji Sekta Binafsi wahimizwa kuwekeza katika biashara ya matunda mkoani Tanga.
Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
……………………………………
Wawekezaji kutoka Sekta Binafsi
nchini wenye nia ya kufungua Viwanda vya juisi mkoani Tanga ikiwemo
Wilaya ya Muheza wamehimizwa kuwekeza katika biashara hiyo mkoani humo.
Hayo yamesemwa leo na Waziri wa
Viwanda na Biashara, Mhe. Charles Mwijage wakati wa kipindi cha maswali
na majibu, ambapo Mhe. Mwijage alikuwa kijibu swali lililoulizwa na
Mheshimiwa Balozi Adadi Mohamed Rajabu, Mbunge wa Muheza lililotaka
kujua ni lini Serikali itajenga kiwanda cha matunda wilayani hapo na
kuwaondolea usumbufu wakulima katika utafutaji masoko.
Mhe. Mwijage amesema kuwa
tafsiri ya Serikali katika kujenga viwanda ni kwa serikali kuweka
mazingira sahihi na wezeshi ili kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje wa
sekta binafsi kujenga viwanda.
Aidha, aktika kutekeleza hilo
Mhe. Mwijage ameeleza kuwa Sera na Mikakati mbalimbali shirikishi inatoa
fursa kwa Sekta na Taasisi za uwekezaji kujenga viwanda na kunufaika na
vivutio mbalimbali.
“Mkoa wa Tanga ikiwemo Wilaya ya
Muheza wamejaaliwa kuwa na utajiri wa matunda aina mbalimbali ikiwa ni
pamoja na machungwa, maembe, machenza, mafenesi na mananasi, kwa
kutambua upatikanaji wa matunda hayo, Wizara yangu inahimiza na
kuhamasisha wawekezaji kutoka Sekta Binafsi wenye nia ya kufungua
viwanda vya juisi mkoani Tanga wafanye hivo’’, alisema Mhe. Mwijage.
Amefafanua kuwa, mpaka sasa
Kampuni ya M/s Sasumua Holding imeanzisha mradi mkubwa wa kulima matunda
katika utaratibu utakaoshirikisho wananchi na kufikia mwezi Novemba,
2018 kiwanda cha juisi kitakuwa tayari kinafanya kazi.
“Mradi huu uko kwamsisi, Handeni
mkoani Tangam hivyo ni tegemo langu kuwa mafaniko ya Mwekezaji huyo
yatawavutia wawekezaji wengine”, alisema Mhe. Mwijage.
Ameongeza kuwa, Wizara kupitia
Shirika la Viwanda Vidogo (SIDO) ina utaratibu wa kutoa ushauri jinsi ya
kuanzisha mitaa ya viwanda kila mkoa ikiwa ni jitihada za kuweka
mazingira wezeshi kwa sekta binafsi kuendeleza uzalishaji katika mikoa
husika.
Wananchi wahamasishwa kuwekeza kwenye dhamana za Serikali.
Meneja
Msaidizi Masoko ya Ndani wa Benki kuu ya Tanzania (BOT) Bw. Genes
Kimaro (kushoto) akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo
Jijini Dar es Salaam kuhusu aina na faida za uwekezaji kwenye dhamana za
Serikali.
PICHA NA FATMA SALUM-MAELEZO
SUMATRA YATANGAZA NAULI ZA USAFIRI WA MABASI YAENDAYO HARAKA.
PICHA NA FATMA SALUM-MAELEZO
Serikali Mkoani Manyara kujenga Kituo cha Michezo cha Mkoa.
………………………………………………………………………………..
Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
Serikali inaendelea kuendeleza
sekta ya michezo nchini ikiwemo kutafuta maeneo ya kuwawezesha vijana
kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya vijana ikiwemo kuwapatia ajira
vijana.
Kauli hiyo imetolewa leo Bungeni
mjini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe.
Nape Nnauye wakati akijibu swali toka kwa Mheshimiwa Martha Umbulla
ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum lililokuwa likiuliza ni lini Serikali
itasikiliza kilio cha muda mrefu na kujenga Senta ya michezo ya riadha
mkoani Manyara ili vijana wengi wenye vipaji waweze kunufaika.
Mhe. Nnauye amesema kuwa Mkoa wa
Manyara pamoja na Wilaya zake una vijana wenye vipaji vya riadha na
michezo ambapo Serikali inatambua pia umuhimu wa kuwa na kituo kikubwa
cha michezo hasa ya riadha ambacho pamoja na mambo mengine kitasaidia
kuibua, kukuza na kuviendeleza vipaji vya vijana ikiwa ni pamoja na
kuwapatia ajira vijana mkoani humo.
Amesema kuwa, Serikali ya Mkoa
wa Manyara imepanga kujenga Kituo cha Michezo cha Mkoa, mara bada ya
kukamilisha mazungumzo na kukiubaliana na wananchi wanaomiliki ardhi
mkoani humo.
Aidha, ameeleza kuwa kwa kipindi
hiki ambacho Uongozi wa mkoa hauna Kituo cha Michezo, mkoa umepanga
kutumia kambi ya michezo ya Hifadhi ya Taifa ya Tarangire kwa muda,
wakati wanasubiri kupatikana kwa eneo la kudumu la mkoa.
“Hii inatokana na sababu kuwa
hifadhi ya Taifa ya Tarangire ina hosteli za kutosha na viwanja vya
michezo vya kutosha”, alisema Mhe. Nnauye.
Aliongeza kuwa, kujengwa kwa
kituo hicho kutaongeza ajira na kupanua shughuli za kibiashara na hata
kukua kwa uchumi wa mkoa wa Manyara.
“Serikali inaendelea na mazungumzo na wananchi wamiliki wa ardhi ili kupata eneo la ujenzi”, aliongeza Mhe. Nnauye.
Kwa upande mwingine ameziomba
Halmashauri kuisadia Serikali katika kulinda maeneo ya michezo ambayo
baadhi ya watu pasipo utaaratibu wanavamia na kugeuza kuwa maeneo yao ya
kufanyia shughuli zao ikiwemo makazi.
NI 5000 TU,DAKIKA 90 ZA CITY VS YANGA KESHO – Mbeya City Council FC
Kwa mujibu wa msimamizi wa
kituo cha Mbeya ambaye pia ni katibu mkuu wa chama cha soka mkoa, Haroub
Suleiman, mchezo huo utafanyika kama ulivyopangwa kwa sababu timu zote
mbili tayari zisharipoti (kuwepo) kituoni na tayari makubaliano juu ya
kiingilia yashafikiwa.
“Yanga wamewasili asubuhi ya
leo, hii ina maana kuwa mchezo upo kama ulivyopangwa, kutokana na uzito
wa mchezo wenyewe,tumekubaliana kiingilio kitakuwa shilingi 5000,
nawaomba mashabiki wote wa soka katika kanda hii ya nyanda za juu
kusini wajitokeze kwa wingi kuzishangilia timu zao huku pia
wakitakiwa kudumisha amani kabla na baada ya mchezo” alisema.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa
Mbeya City Fc, Mussa Mapunda amewatakia kila la kheri na kuwashukuru
mashabiki wote wa timu yake popote walipo ndani na nje ya nchi kwa jinsi
walivyojitolea kuisapoti timu yao tangu ilipopanda daraja na
kuwataka kujitokeza kwa wingi hapo kesho kuja kuisapoti na
kushuhudia City ikiandikisha ushindi wa kwanza mbeya ya Yanga.
TIB imetoa mikopo ya bilioni 550 kwa Watanzania.
Naibu
Waziri, Wizara ya Fedha na Mipango, Mhe. Ashatu Kijaji akijibu maswali
mbalimbali kuhusu Benki ya TIB na TADB katika kupunguza umaskini, leo
Bungeni mjini Dodoma.
Picha na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
………………………………………………………………………………
Na Benedict Liwenga-MAELEZO, Dodoma.
Hadi kufikia mwaka jana (2015) Benki ya Uwekezaji Tanzania
(TIB) imewawezesha Watanzania wengi kupambana na umaskini kwa kutoa
mikopo ya zaidi ya shilingi bilioni 550 katika sekta mbalimbali za
kiuchumi.
Taarifa hiyo imetolewa leo Bungeni Mjini Dodoma na Naibu
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Ashatu Kijaji wakati akijibu swali toka
kwa Mbunge wa Karagwe, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) lililotaka kujua
Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa Benki za TIB na TADB
zinajielekeza kwenye utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.
Mhe. Kijaji ameeleza kuwa, madhumuni ya kuanzishwa kwa
benki ya TIB na TADB kama benki za maendeleo ni kutoa mikopo ya muda wa
kati na muda mrefu kwa lengo la kufadhili miradi ya kimkakati, hivyo
katika kutimiza azma ya kufadhili miradi ya kimkakati ya kufungua fursa
za kiuchumi na kupunguza umaskini, TIB imetoa mikopo katika maeneo ya
miji kupitia NHC, Viwanda vya kubangua korosho, maghala, mabomba ya
maji, sukari na kilimo cha miwa, kukoboa na kusindika kahawa, kusindika
matunda, mifuko ya kuhifadhia mazao na nyaya za umeme; vinu vya pamba na
uzalishaji wa mafuta yatokanayo na mbegu za pamba na hoteli.
Aidha, TIB imetoa mkopo wa shilingi bilioni 489.2 kwa ajili
ya utekelezaji wa miradi 181 ya kusambaza umeme vijijini kupitia REA na
kaya 257,000 zimenufaika na mradi huo. Pia vikundi 17 vya wachimbaji
wadogo wadogo vimenufaika na mikopo jumla ya shilingi bilioni 8.
“Mikopo ya TIB kwa sekta na taasisi mbalimbali imesaidia
kwa kiasi kikubwa kutoa ajira na kuendeleza zilizopo. Pia mikopo ya TIB
imetumika kuongeza uzalishaji wa bidhaa zinazouzwa nje kama vile maua,
kahawa na dhahabu”, alisema Kijaji.
Aliongeza kuwa pamoja na benki ya Kilimo kuchelewa kuanza
kutoa mikopo, ni wazi kuwa benki ya TIB imejielekeza kwenye utekelezaji
wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM pamoja na utekelezaji wa Mipango na mikakati
mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Dira ya Taifa ya 2025, FYDB, SDGs 2030
pamoja na Afrika 2063.
TIB imewekeza katika mashirika ya umma kama vile Shirika la
Reli (TRL), pia imeiwezesha TPDC katika mradi wa gesi na kuipatia
Shirika la Ugavi Umeme Tanzania (TANESCO) mkopo kwa ajili ya fidia kwa
wananchi ili kuweka njia mpya ya kusafirisha umeme.
Serikali yawataka wananchi kutumia mpango wa msaada wa kisheria.
Wakili
wa Serikali Mkuu kutoka Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Charles Mmbando
akiwaeleza waaandishi wa Habari (Hawapo pichani) kuhusu huduma za msaada
wa kisheria kwa wananchi ambao ni wahitaji wa msaada hiyo juu ya
masuala mbalimbali yanayowakabili, Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha
Mawasiliano wa Wizara hiyo Bi. Sheiba Bulu.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia Mkutano huo
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.
Kipaumbele chetu ni kuboresha reli ya TAZARA- Balozi Kijazi
Na. Immaculate Makilika- MAELEZO
………………………………….
Serikali imesema iko tayari
kuboresha reli ya Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia(TAZARA) ili
iweze kufanya kazi kwa ufanisi kwani ni jambo la msingi na itashirikiana
na nchi za Zambia na China ili kufanikisha azma hiyo.
Akizungumza leo jijini Dar es
salaam Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi wakati akizindua kikao
kazi kilicho shirikisha nchi tatu ambazo ni Tanzania, Zambia na China
kuhusu maboresho ya kiutendaji ya reli ya TAZARA.
“Kipaumbele chetu ni kuboresha
reli ya TAZARA ili iweze kufanya kazi kwa ufanisi, kikao hiki kitajadili
kwa kina changamoto mbalimbali zinazoikabili reli hii, pamoja na fursa
zilizopo na namna ya kutatua changamoto hizo ili kufufua uchumi wetu
kupitia reli ya TAZARA” amesema Balozi Kijazi.
Balozi Kijazi amesema kwa muda
sasa reli hii imekua ikifanya kazi bila ufanisi kutokana na sababu
mbalimbali licha ya kuwa kiwango cha mizigo kutoka bandari ya Dar es
salaam kimeongezeka kutoka tani milioni 6 mwaka 2006 hadi kufikia tani
milioni 15 mwaka 2015, reli ya TAZARA imeshindwa kuwa na uwezo wa
kusaidia kusafirisha mizigo hiyo, ambapo mwaka kila mwaka uwezo wake
unashuka kutoka kusafirisha mizigo tani 601,229 mwaka 2005/2006 hadi
tani 87,860 kwa mawaka 2014/2015.
Vile vile, licha ya kuwa nchi za
Zambia na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimeongeza uzalishaji wa
shaba bado TAZARA haikuwa na uwezo wa kuhudumia ama kusafirisha shaba
hiyo, utendaji huu wa kiwango cha chini lazima ubadilike.
Aidha, Serikali imesema ina ya
dhati ya kuibadilisha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati, na yenye
viwanda, kwa kujua kuwa uanzishwaji mzuri wa mtandao wa miundombinu hasa
reli, barabara, usafiri wa anga, usafiri wa majini ni chanzo muhimu ya
kutimiza azma hiyo.
Kwa upande wake, Katibu wa
Baraza la Mawaziri la Zambia Dkt. Rowland Msiska amesema kuna haja kubwa
ya kuboresha reli ya TAZARA kwa kuwa reli hiyo ina msaada mkubwa
kiuchumi si tu kwa nchi za Tanzania, Zambia na China bali hata nchi za
Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na nchi za Ukanda wa
Maziwa Makuu.
Aidha, amesema kuna faida nyingi
za kuboresha reli ya TAZARA ikiwemo ya gharama nafuu. Usafirishaji
mizigo kwa njia ya reli ni wa gharama nafuu kuliko barabara kwani
inagharimu senti 5 kwa tani moja kwa umbali wa kilometa moja, huku
gharama za usafirishaji kwa barabara ikiwa ni senti 12 kwa tani moja kwa
umbali wa kilometa moja.
Naye, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa
Wizara ya Biashara ya China, Bwana. Liu Junfeng amesema Serikali yake
itaendelea kushirikiana na nchi za Tanzania na Zambia ili kuboresha
utendaji wa reli hiyo, huku akisisitiza uhusiano wa nchi hizi tatu
umeendelea kuimarika na unazalisha fursa nyingine za ushirikiano.
Reli ya TAZARA ilijengwa mwaka
1970 hadi 1976 kwa msaada wa Jamhuri ya watu wa China kama zawadi kwa
mataifa ya Tanzania na Zambia, kwa lengo la kusaidiza kuongeza njia za
usafirishaji wa bidhaa mbalimbali.
Wadau wa maji kujadili rasilimali za bonde la Mto Rufiji.
Na Jacquiline Mrisho MAELEZO
………………………………………….
Wizara ya Maji na Umwagiliaji
imeandaa warsha kwa wadau wake juu ya tathmini ya kimkakati ya athari za
kimazingira na jamii juu ya mpango jumuishi wa usimamizi na maendeleo
ya rasilimali maji za bonde la Mto Rufiji zitakayofanyika Jijini Dar es
salaam na mkoani Iringa.
Taarifa hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo
Mhandisi Mbogo Futakamba alipokua akifafanua kuhusu mpangilio wa warsha
hizo zitakazofanyika katika mikoa miwili ambapo kwa Jijini Dar es salaam
warsha hiyo itafanyika Mei 20 mwaka huu na mkoani Iringa itafanyika Mei
23 mwaka huu kuanzia sa 3 kamili asubuhi hadi sa 10:30 jioni.“Wizara yetu inawakaribisha wadau wake wote kushiriki warsha hii na mada zitakazotolewa zitahusisha maelezo ya jumla juu ya mipango ya maendeleo ya muda mrefu ya rasilimali za maji ya bonde la mto Rufiji na athari zake tarajiwa za kimazingira na kijamii, kuwapa fursa ya kutoa maoni na mitazamo yao juu ya mipango inayokusudiwa pamoja na kutoa ufafanuzi kuhusu maamuzi na taratibu zinazofuata,”alisema Mhandisi Futakamba.
Aidha, Mhandisi Futakamba ameongeza kuwa warsha hizo zitaandaliwa na kuwezeshwa na washauri elekezi kutoka Kampuni ya uingereza ijulikanayo kama Environmental Resource Management ikishirikiana na kampuni za JSB Envi-Dep na eMjee Consult za Tanzania.
Warsha hizo zitaruhusu wadau kujadiliana kwa pamoja na kutoa maoni ya kutosha juu ya mada zitakazoongelewa ili kusaidia kuinua uchumi wa Tanzania kupitia rasilimali maji zilizopo kwenye bonde la mto huo.
KATIBU MKUU KIONGOZI BALOZI, ENG. JOHN WILLIA MKIJAZI AFUNGUA MKUTANO WA WATAALAM KUTOKA NCHI YA CHINA, TANZANIA NA ZAMBIA
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya
Uchukuzi), Dkt. Leonard Chamuriho (kulia), akimkaribisha Katibu Mkuu
Kiongozi, Balozi, Eng. John William Kijazi kwenye Jengo la Ukumbi wa
Mikutano la Mwl. Julius Nyerere, wakati alipofika kufungua Mkutano wa
siku nne wa kujadili namna ya kuboresha utendaji wa Shirika la Reli la
Tanzania na Zambia (TAZARA).
Katibu
Mkuu Kiongozi, Balozi, Eng. John WilliamKijazi (kushoto), akisalimiana
na ujumbe kutoka Nchini China ambao wanahudhuria Mkutano wa siku nne wa
kujadili namna ya kuboresha utendaji wa Shirika la Reli la Tanzania na
Zambia (TAZARA) unaofanyika katika Ukumbi wa Mikutano la Mwl. Julius
Nyerere. Kushoto kwake ni Balozi wa China NchiniDkt. LU Youqing.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Uchukuzi),
Dkt. Leornard Chamuriho (kulia), akitoa hotuba yake kabla ya ufunguzi wa
Mkutano wa siku nne wa kujadili namna ya kuboresha utendaji wa Shirika
la Reli la Tanzania na Zambia (TAZARA) unaofanyika katika Ukumbi wa
Mikutano la Mwl. Julius Nyerere.














No comments :
Post a Comment