Tuesday, May 24, 2016

TANZANIA KUIUZIA UMEME ZAMBIA – MAJALIWA l

lu6 
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Tanzania ina mpango wa kujenga njia ya umeme kutoka Mbeya hadi Zambia kupitia Tunduma ili kupunguza tatizo la umeme linaloikabili nchi hiyo.
“Serikali ya Tanzania inajenga njia ya umeme ya msongo wa KV 400 kutoka Iringa – Dodoma – Singida – Shinyanga ambayo ni sehemu ya mradi mkubwa wa umeme unaolenga kuunganisha Zambia, Tanzania na Kenya,” amesema.
Amesema  upembuzi yakinifu kwa ajili KV400 kutoka Iringa hadi Mbeya umekwishakamilika tangu mwaka 2012, na hivi sasa Serikali inatafuta fedha kwa ajili kuunganisha kipande cha kutoka Mbeya na gridi ya Taifa ya Zambia.
Waziri Mkuu ambaye anahudhuria mkutano huo kwa niaba ya Mheshimiwa Rais, Dk. John Pombe Magufuli, ametoa ufafanuzi huo leo mchana (Jumanne, Mei 24, 2016) wakati akichangia hoja kwenye mjadala wa wakuu wa nchi na Serikali uliohusu Nishati na Mabadiliko ya TabiaNchi kwenye ukumbi wa mikutano cha kimataifa wa Mulungushi.
Amesema ili kukabiliana na changamoto ya nishati barani Afrika, nchi za bara hili zinahitaji kuwa na fedha ama mitaji, teknolojia ya kisasa na wataalamu wenye ujuzi wa kutosha jambo ambalo amesema ni gumu kulikamilisha kila nchi peke yake.
Amesema ili kukaribisha wawekezaji kwenye sekta ya umeme, Tanzania inafanyia marekebisho sheria zake ili kuruhusu uwekezaji kwenye sekta hiyo.

NAPE AFUNGUA MASHINDANO YA KOMBE LA MKUU WA MAJESHI YA ULINZI ( CDF CUP – 2016) JIJINI DAR ES SALAAM

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akihutubia wakati wa
kufungua mashindano ya tatu ya kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF Cup – 2016) kwenye
uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Mkuu wa Mafunzo na Utendaji Kivita Meja Jenerali Issa Nassor akihutubia wanamichezo
wa kijeshi kwenye sherehe za ufunguzi wa  mashindano ya tatu ya kombe la
Mkuu wa Majeshi (CDF Cup – 2016) kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.


Mwakilishiwa Mnadhimu Mkuu wa Majeshi Meja jenerali Simoni Mumwi akihutubia wakati wa
ufunguzi wa  mashindano ya tatu ya kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF Cup –
2016) kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akiangalia picha yake aliopewa na kikundi cha sanaa  wakati wa kufungua mashindano ya tatu ya kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF Cup – 2016) kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akipiga penati ikiwa ishara ya kufungua mashindano ya tatu ya kombe la Mkuu wa Majeshi (CDF Cup – 2016) kwenye uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA ARDHI KWA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 YAPITISHWA.

 
ar1 
Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi na naibu waziri wake Mhe. Angelina Mabulla wakifuatilia hoja za wabunge wa mapitio makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya Aridh kwa mwaka wa fedha 2016/20
ar2 
Waziri wa Ardhi Mhe. William Lukuvi akijibu hoja bungeni wakati wa mapitio ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara ya Aridh kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ar3 
Naibu waziri wa Ardhi, Mhe. Angelina Mabulla akipongezwa na watendaji wa Wizara nje ya ukumbi wa bunge baada ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara kupitishwa na bunge   kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
ar4 
Naibu Waziri wa Ardhi Mhe. Angelina Mabulla akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Yamungu Kayandabila Nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya bajeti ya Wizara hiyo kupitishwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017
ar5 
Mhe. William Lukuvi Waziri wa Ardhi na Naibu Waziri Mhe. Angelina wakiwa na baadhi ya watendaji wa Wizara Nje ya Ukumbi wa Bunge baada ya makadirio ya mapato na matumizi ya wizara hiyo kupitishwa na bunge   kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Kampuni ya TBL Group yaendesha zoezi la kutathmini wafanyakazi wake

index1 
 Afisa Rasilimali watu katika kiwanda cha TBL mkoani Mwanza, Dorah Nyambalya akifanya tathimini ya kazi kwa baadhi ya wafanyakazi wa kiwanda hicho jana.
index2 
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL kiwanda cha Mwanza wakiwa katika picha ya pamoja baada ya zoezi la tahmini kiwandani hapo leo
……………………………………………………………………………………………………….
Kampuni ya TBL Group kuanzia leo imeanza kuendesha zoezi la kutathmini wafanyakazi wote katika viwanda vyake vyote vilivyopo katika mikoa ya Dar es Salaam,Mwanza,Mbeya,Arusha na Kilimanjaro.
Lengo kubwa la kuendesha zoezi hilo limeelezwa kuwa ni kujua changamoto wanazokabiliana nazo wafanyakazi katika majukumu yao ya kila siku ili kuzitafutia ufumbuzi kwa lengo la kuleta ufanisi wenye tija katika kazi.
Katika kutekeleza zoezi hilo wafanyakazi walijaza fomu maaalumu zenye maswali ya kiutendaji chini ya usimamizi wa watendaji wa idara ya Raslimali watu ambao yalihusu utendaji wao,changamoto wanazokutana nazo pia walipata fursa ya kutoa maoni yao ni jinsi gani ya kuboresha mazingira ya kazi na kuwaendeleza wao ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi.

Mfumo wa usimamizi wa nyaraka kidijiti kuongeza kasi ya utendaji Serikalini.

images 
Na Daudi Manongi.
Mfumo wa usimamizi wa nyaraka kidijiti utaongeza kasi serikalini na hivyo kuchochea maendeleo chanya katika kila nyanja.
Hayo yamesemwa leo na Katibu mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Prof.Elisante Ole Gabriel wakati wa mafunzo yanayotolewa na Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano kwa Menejimenti ya wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo wakati walipotembelea mfumo wa usimamizi wa nyaraka wa kidijiti.
Alisema pia kuwa mfumo huu una faida nyingi na ndio ambazo zimeifanya wizara hii kutaka kujifunza ni pamoja na suala la gharama na kwa kuwa serikali ya awamu ya tano iko katika jitihada kubwa za kupunguza matumizi na kwa kuwa bajeti ya shajala ni kubwa katika taasisi nyingi za serikali hivyo mfumo huu wa kidijiti utasaidia kupunguza garama kwani hapatakuwa na haja ya kutumia karatasi na hivyo kupunguza gharama kubwa.
Prof Elisante pia aliongeza kuwa mfumo huu utaongeza usiri wa nyaraka hizi na kwa sasa zitakuwa zinasomwa na yule tu aliyekusudiwa na kutoa pongezi kwa ofisi ya rais manejimenti ya umma kwa kuhamasisha matumizi ya mfumo huu kwani ukitumiwa vyema utakuwa na manufaa sana.
Kwa upande wake Katibu mkuu wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Faustin Kamuzora alisema kuwa mfumo huo ulijengwa miaka mitatu iliyopita na unaweza kutumika katika wizara yeyote kwani una ufanisi mkubwa sana kwani kwa sasa utaweza kuangalia mafaili gani yameingia  kwa mfumo wa kidijitali na  kwa namna hii itapunguza garama na muda kwani hatutakuwa tunatumia karatasi tena.
Prof.Kamuzora alizitaka Taasisi na Wizara mbalimbali kuwapa elimu ya kutosha watunza kumbukumbu kwani wao ndio wahusika wakuu wa kwanza wa mfumo huu na hivyo kuwataka wahusika kuwapa mafunzo ya kompyuta na kuboresha vifaa kama scanner maofisini mwao.
Nae mmoja wa watunza kumbukumbu kutoka wizara Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bi.Felomena Swai alisema amenufaika na mafunzo hayo na yatawasaidia katika utunzaji wa kumbukumbu kwani sasa watapeleka barua kwa wakati  na kurahisisha utunzaji wa mafaili.

Serikali kuboresha mazingira ya biashara ili kuongeza uwekezaji

tp1 
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu,Bunge,kazi,Ajira na watu wenye ulemavu Dkt. Hamis Mwinyimvua(Kushoto) akizungumza wakati wa akifungua mkutano wa wadau wa biashara nchini uliolenga kujadili namna ya kuboresha mazingira ya biashara katikati ni Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania Godfrey Simbeye na kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Raymond Mbilinyi.
tp2 
Wadau wa biashara kutoka sekta za umma na binafsi wakifatilia mkutano uliofanyika leo uliolenga kujadili namna ya kuboresha mazingira ya biashara nchini.
tp3 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Raymond Mbilinyi(Kulia) akijibu maswali toka kwa wadau wa bishara(hawapo pichani) wakati wa mkutano wa wadau wa biashara nchini uliolenga kujadili namna ya kuboresha mazingira ya biashara kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu,Bunge,kazi,Ajira na watu wenye ulemavu Dkt. Hamis Mwinyimvua na katikati ni Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania Godfrey Simbeye. Picha zote na Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
……………………………………………………………………………………………………….
Na Raymond Mushumbusi MAELEZO
Serikali imedhamiria kuboresha mazingira ya biashara nchini ili kuongeza uwekezaji na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa Kati.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu,Bunge,kazi,Ajira na watu wenye ulemavu Dkt. Hamis Mwinyimvua wakati akifungua mkutano wa wadau wa biashara nchini uliolenga kujadili namna ya kuboresha mazingira ya biashara.
Dkt. Hamis Mwinyimvua amesema Serikali imeazimia kuboresha mazingira ya biashara nchini kwa kuandaa sera ambazo zitawasaidia wafanyabishara kuwekeza katika sekta mbalimbali.
“Tutahakikisha tunaboresha mazingira ya biashara kwani hakuna uwekezaji utakaowezekana kama mazingira ya ufanyaji wa biashara yatakuwa hayaridhishi.” Alisisitiza Dkt Mwinyimvua.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) Raymond Mbilinyi amesema kuwa kuna haja ya Taasisi zote za umma na binafsi kufanya kazi kwa pamoja ili kuboresha mazingira ya biashara.
Naye Mkurugenzi Mtendaji  wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania Godfrey Simbeye amesema kuwa Serikali ya awamu ya tano imeanza kufanya maboresho katika mazingira ya uwekezaji.
Akifafanua kuhusu maboresho hayo Simbeye alisema kwasasa ujasili wa makampuni unafanyika kwa kutumia mfumo wa kieletroniki ambapo muombaji anaweza kusajili kampuni pasipo kufika katika Ofisi za BRELA katika kipindi cha muda mfupi.
Mkutano huu uliondaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu ikishirikiana na Baraza la Taifa la Biashara, Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania wakishirikiana na taasisi za umma na binafsi umedhamiria kuwezesha wafanyabiashara na wawekezaji kuwa mazingira mazuri ya kufanya biashara

MWAMKO MDOGO WA WATANZANIA KUTEMBELEA HIFADHI ZA TAIFA WAATHIRI UTALII WA NDANI.

index 
Na. Aron Msigwa – Dodoma.
Mwamko mdogo wa Watanzania kutembelea hifadhi za Taifa zilizo katika maeneo mbalimbali nchini umeathiri kiwango cha idadi ya watu wanaotembelea hifadhi hizo kwa mwaka hivyo kuzorotesha mapato yanayotokana na watalii wa ndani ya nchi.
Kauli hiyo imetolewa Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe wakati akiwasilisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Amesema kuwa licha ya Serikali kuweka gharama ndogo za viingilio katika hifadhi za Taifa kwa watanzania na raia wa Jumuiya ya Afrika Mashariki  bado mwamko ni mdogo hasa idadi ya watanzania wanaokwenda kutembele hifadhi hizo jambo linalopunguza mapato yanayotokana na utalii wa ndani wa watanzania.
Ameeleza kuwa kwa sasa watanzania kwa maana ya watu wazima wanaotembelea hifadhi za ndani zilizoko eneo la Kaskazini hutakiwa kulipa  kiingilio cha  shilingi  elfu kumu (10,000) na shilingi elfu 5000 hadi 15,000 kwa hifadhi zote zilizoko kusini mwa Tanzania huku watoto wakilipia shilingi 2000 kutembelea hifadhi yoyote nchini.
Prof. Maghembe ameeleza kuwa kufuatia hali hiyo Wizara yake inaendelea na kampeni mbalimbali ili kuwahamasisha Watanzania Wengi zaidi  kushiriki katika  shughuli za utalii ndani ya nchi hivyo kuongeza patoa la Taifa.
Amesema katika kulinda na kutunza hifadhi za Taifa ili kuhakikisha  zinakuwa endelevu na kutoa mchango mkubwa katika maendeleo ya taifa, Serikali ya awamu ya tano imejipanga kikamilifu ujangili wa wanyama pori kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa uhifadhi.
Amefafanua kuwa katika kupambana na ujangili nchini Wizara kwa kushirikiana na wadau wa uhifadhi imeshawabaini na kuwashughulikia baadhi ya wananchi wanaoishi kwenye maeneo yanayopakana na hifadhi wanaoshirikiana na watumishi wasio waaminifu kushiriki vitendo vya ujangili pia kuwashughulikia wawindaji haramu wanaojihusisha moja kwa moja kuua wanyama  kufanya udalali na kusafirisha wanyama hao.
Aidha, amesema kuwa katika kupambana na ujangili Serikali inaendelea  kufanya doria ili kuwashughulikia wawezeshaji ngazi ya nchi wanaonunua nyara, kusambaza silaha, watakatishaji fedha , majangili nguli wa kimataifa kwa kukitumia na kukiimarisha kitengo cha Intelijensia ili kiweze kutimiza majukumu ya kiulinzi kwa ufanisi zaidi.
Pia amesema kuwa Wizara hiyo imeendendelea kuongeza idadi ya askari wanyamapori 447 na maafisa 111 na kufanya idadi ya watumishi waliopo kwa sasa kufikia 2,064 pamoja na kuanzisha kada nane za doria za ushirikiano katika mifumo ya ikolojia ya Selous-Niassa-Mikumi, Ruaha- Ruangwa, Katavi -Rukwa , Moyowosi -Kigosi, Tarangire- Manyara-Simanjiro na Ngorongoro – Serengeti.

MAJALIWA AMWAKILISHA JPM MKUTANO WA ADB – LUSAKA

lu1 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais wa Zambia, Edgar Lungu katika Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi kilichopo Lusaka Zambia , Mei 24, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu.
lu3 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri Mkuu wa Msumbiji, Carlos Agostino do Rosario katika Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi kilichopo Lusaka Zambia , Mei 24, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
lu4 
Rais wa Zambia, Edgar Lungu akifungua Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi kilichopo Lusaka Zambia , Mei 24, 2016.Kushoto kwake ni Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa ambaye alimwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano huo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
lu6 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika Mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi kilichopo Lusaka Zambia , Mei 24, 2016. Wengine pichani kutoka kushoto ni Makamu wa Rais wa Nigeria, Prof. Yemi Osinbojo, Rais wa Chad,  Idriss Debyo, Rais wa Zambia, Edgar Lungu na Waziri Mkuu wa Msumbiji,  Carlos Agostino do Rosario (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
lu8 
Wasanii wa Lusaka wakicheza ngoma ya asili ya Zambia katika mkutano wa Benki ya Maendeleo ya Afrika – ADB uliofanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Mlungushi Zambia Mei 24, 2016. Tanzania iliwakilishwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

SERENGETI BOYS YAWANIA NAFASI YA TATU

Timu ya soka ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti Boys’ kesho Mei 25, 2016 kesho inaingia tena Uwanja wa Tilak, Maidan mjini Goa India kukipiga na Malaysia katika mchezo wa kuwania nafasi ya tatu kwenye michuano maalumu ya kimataifa yaliyoandaliwa na Shirikisho la Soka nchini humo (AIF Youth Cup 2016 U-16).
Katika mchezo wa kuwania kucheza fainali, Serengeti Boys iliruhusu sare ya mabao 2-2 Malaysia hivyo kufikisha sare ya tatu baada ya kushinda mechi moja. Serengeti Boys imemaliza hatua ya awali ikiwa na pointi sita sawa na Korea Kusini, lakini ikazidiwa bao moja hivyo kushika nafasi ya tatu katika michuano ambayo Marekani iliongoza kwa kufikisha point nane.
Licha ya kuwa wenyeji, India ilitupwa mbali hivyo kwa kesho watakuwa watazamaji katika michezo yote miwili ukianzia wa Serengeti Boys na Malaysia utakaopigwa saa 7.30 mchana kwa saa za Tanzania kabla ya fainali kuchezwa saa 11.30 jioni kati ya Marekani na Korea Kusini.
India kimeandaa mashindano ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikosi chao kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia kwa Vijana zitakazofanyika nchini humo mwaka 2017.

NI FAINALI YA KUKATA NA SHOKA, VIINGILIO VYATAJWA

Fainali za Kombe la Shirikisho maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) zinatarajiwa kufanyika kesho Mei 25, 2016 kwa kuzikutanisha timu za Young Africans na Azam FC; zote za Dar es Salaam katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Taifa jijini.
Sherehe za mchezo huo zitaanza rasmi saa 8.00 mchana kwa mchezo wa awali wa kuburudisha kuzikutanisha timu za soka za kituo cha Televisheni cha Azam ‘Azam Tv’ na wafanyakazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) na kurushwa live na kituo hicho kilichotokea watazamaji wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.
Viingilio katika mchezo huo itakuwa ni Sh 25,000 kwa VIP A wakati VIP B na C ni Sh 20,000 wakati majukwaa yenye viti vya rangi ya chungwa, mzunguko wenye viti vya rangi ya bluu na kijani ni Sh 5,000.
TFF inajivunia nyota wake kama Jemedari Said, Wilfred Kidao, Salum Madadi, Alfred Lucas, Danny Msangi, Michael Ngogo na Jonas Kiwia, lakini Meneja wa timu ya Wafanyakazi wa TFF, Eliud Mvella anasikitika kumkosa nyota wake Mwesigwa Selestine.
Azam Tv wanatamba na nyota wao waliopata kufanya kazi nje ya nchi katika vyombo vya kimataifa kama vile Charles Hilary, Tido Mhando, Yahaya Mohammed, Baruan Muhuza na Rhys aliyetajwa kwa jina moja.
Mbali ya burudani hiyo, pia Mwakilishi wa Azam Tv, Baruan Muhuza alisema kwamba mara baada ya mchezo huo utakaomalizika saa 9.00 alasiri, itafuata burudani ya wasanii mbalimbali ambao pia wataburudisha wakati wa mapumziko ya mchezo huo.
Alisema kwamba burudani hiyo itakuwa ni ya nusu saa kabla ya kuziacha timu kufanya maozezi ya kupasha moto viungo kabla ya mchezo huo kuanza saa 10.30 jioni na wakati wa mapumziko burudani itaendelea kabla ya kutolewa taji ambalo timu zitakuwa zikiliwania.
Kwa mujibu wa kanuni bingwa wa michuano hiyo atatwaa kombe, medali na fedha Sh 50,000,000 wakati mshindi wa pili atazawadiwa tuzo na medali. Kadhalika kutakuwa na tuzo kwa mchezaji bora, mfungaji bora na mchezaji bora wa michuano hiyo ambayo waaandaaji wamepanga kuiboresha mwakani.
Mwamuzi wa mchezo huo atakuwa Israel Mujuni Nkongo wa Dar es Salaam kwa mujibu wa Kamati ya Waamuzi ya TFF huku akisaidiwa na Ferdinand Chancha wa Mwanza upande wa kulia (line 1) na upande wa pili ni Soud Lila wa Dar es Salaam (line 2) na mwamuzi wa akiba mezani ni Frank Komba wa Dar es Salaam pia. Kamishna wa mchezo huo anatakuwa Juma Mgunda wa Tanga.
Kwa mujibu wa kanuni za Ligi Kuu msimu 2015/16, mabingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu 2015/16 wataiwakilisha nchi katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu wa 2016/17. Nafasi hiyo imechukuliwa na Young Africans.
Kadhalika Azam ina tiketi tayari ya kushiriki Kombe la Shirikisho Barani Afrika kwa kufika fainali za ASFC ingawa kanuni zinataka bingwa ambako kwa upande wa Yanga wana tiketi ya michuano ya juu zaidi ya shirikisho. Mvuto wa mchezo wa Jumatano ni ushindani wa soka na zawadi kwa bingwa.
Fainali za Kombe la Shirikisho zinakuja baada ya mchuano ulioshindanisha timu 64 za Ligi Kuu Tanzania Bara – VPL (16); Ligi Daraja la Kwanza -FDL (24), Ligi Daraja la Pili – SDL (24).

Aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam aagwa

ji2 
Baadhi ya Mawakili na Wanasheria wakiingiza mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bwa. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho.(PICHA NA BEATRICE LYIMO-MAELEZO)
ji3 
Familia ya aliyekuwa Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe wakifuatilia ibada ya kutoa heshima za mwisho ya kuuaga mwili huo.
ji4 
Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene akiwakisha salamu za rambirambi kutoka Serikalini wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa  aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee, leo jijini Dar es salaam.
ji5 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaa Paul Makonda akiwasilisha salamu za rambirambi kutoka ofisi ya Mkuu mkoa wa Dar es salaam wakati wa kutoa heshima za mwisho kwa  aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee, leo jijini Dar es salaam
ji6 
Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI George Simbachawene akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Raymond Mushi akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.
ji8 
Meya wa jiji la Dar es salaam Isaya Mwita akitoa heshima za mwisho kwa aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe katika viwanja vya Karimjee kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.
ji9 
Baadhi ya Ndugu, jamaa na marafiki waliohudhuria ibada ya heshima za mwisho kwa  aliyekuwa  Mkurugenzi wa jiji la Dar es salaam Bw. Mbonea Wilson Kabwe kabla ya safari ya kuelekea Mamba, Wilayani Same mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi.
ji1

14 wakamatwa mauaji ya watu watatu msikitini Mwanza

Image00003-CopyNa Lorietha Laurence-Maelezo
Jeshi la Polisi Nchini linawashikilia watuhumiwa 14 kufuatia tukio la mauaji ya watu watatu lililotokea katika msikiti wa Rahman eneo la Ibanda relini mkaoni Mwanza, Mei 18 mwaka huu.
Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Kamishna Msaidizi Advera Bulimba alisema kuwa msako wa kuwakamata watuhumiwa wengine unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini.
Hivyo amewaomba wananchi kutoa ushirikiano mkubwa kwa jeshi hilo ili kufanikisha kuwakamata wale wote wanaotuhumiwa kuhusika na tukio hilo.
“Nitoe wito kwa wananchi kushirikiana kikamilifu na vyombo vya usalama katika kufichua wahalifu kwa kuwa ni watu tunaoishi nao, hivyo hakuna budi kutoa taarifa zao ili usalama na mali zetu uendelee kuimarika”, aliongeza Kamishna Msaidizi Bulimba.
Hata hivyo, alieleza kuwa hali ya usalama nchini iko shwari na kuwatoa hofu wananchi kwamba jeshi hilo limejipanga kikamilifu katika kuhakikisha hali ya usalama inaendelea kuwepo.
“Niwaombe wananchi kuondoa hofu juu ya hali ya usalama na wasiwasi na watoe ushirikiano kwa vyombo vya dola ili kuhakikisha kwamba wote wanaojihusisha na uhalifu wanakamatwa haraka”, alisema Kamishna Msaidizi  Bulimba.
Aliongeza kuwa uchunguzi zaidi wa matukio ya uhalifu nchini unaendelea ikiwemo matukio ya mkoani Tanga, Dar es Salaam na mikoa mingine ili kubaini na kuwakamata wahusika na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Hivi karibuni kumeripotia matukio mbalimbali ya uvunjifu wa amani katika mikoa mbalimbali  nchini ikiwemo mauaji ya watu watatu waliouawa wakiwa msikitini jijini Mwanza.

Wamiliki wa silaha watakiwa kuhakiki silaha zao kabla ya Juni 30

index
Na Lorietha Laurence-Maelezo
Jeshi la Polisi nchini limetoa wito kwa wamiliki wa silahi  kujitokeza na kuhakiki silaha zao katika Wilaya wanazoishi kabla ya kumalizika kwa zoezi hilo mnamo Juni 30 mwaka huu.
Hayo yalisemwa na Msemaji wa Jeshi hilo Kamishna Msaidizi Advera Bulimba alipokuwa  akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
“Serikali imetoa muda wa miezi mitatu kukamilisha zoezi hili muhimu na tayari miezi miwili imepita hivyo wale ambao bado hawajahakiki silaha zao kuzikakiki sasa kabla ya Juni 30 ili kuepukana na usumbufu” alisema Kamshna Msaidizi Bulimba na kuongeza kuwa:
“Natoa wito kwa watu wote wanaomiliki silaha kinyume na sheria kusalimisha silaha hizo katika vituo vya polisi, ofisi za serikali na kwenye nyumba za ibada  na watakaofanya hivyo ndani ya muda ulipangwa hawatachukuliwa hatua zozote za kisheria”.
Aliongeza kuwa baada ya muda ulipangwa na Serikali kupita na wamiliki hawajahakiki silaha zao Jeshi la Polisi  nchini litaendesha operesheni kali kuwakamata  wale ambao hawakujitokeza katika zoezi la uhakiki na hatua kali zitachukuliwa ikiwemo kufutiwa leseni na silaha zao kutaifishwa na kuwa mali ya Serikali.
Aliwaomba ndugu wa wale walikuwa wakimiliki silaha ambao wamefariki au ni wagonjwa wasalimishe silaha hizo katika vituo vya Polisi kwa niaba ya ndugu zao ndani ya kipindi cha uhakiki wa silaha.
Zoezi la uhakiki wa silaha lilianza Machi 21 mwaka huu kufuatana na sheria ya usimamizi wa silaha na risasi ya mwaka 2015, ambapo kifungu cha 66 cha sheria hiyo kinamtaka kila mmiliki kuhakiki kumbukumbu za silaha yake au risasi  pale anapoamriwa na mamlaka.
Lengo la kuhakiki kumbukumbu za wamiliki wa silaha ni kupata taarifa sahihi za wamiliki hao zitakazosaidia kubaini wale wote wanaomiliki kinyume na sheria, kuwafahamu wamiliki waliohama na kuhamia makazi mapya, kuwafahamu wamiliki waliofariki ili kuzuia vitendo vya uhalifu na uvunjwaji wa amani nchini.

SHERIA MPYA YA USHIRIKA YAWANUFAISHA WAKULIMA WA TUMBAKU

index
Na Fatma Salum- MAELEZO, Dodoma.
Serikali imebainisha kuwa Sheria Mpya ya Ushirika (Sheria namba 6 ya mwaka 2013) imesaidia kupunguza changamoto za wanachama wa Vyama vya Ushirika pamoja na wakulima wa Tumbaku nchini.
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi  Mhe. Tate William Ole-Nasha aliyasema hayo leo bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu maswali ya wabunge kwenye kipindi cha maswali na majibu.
Mhe. Ole-Nasha alisema kuwa baadhi ya marekebisho ya Sheria hiyo yanayowanufaisha wanachama wa Vyama vya Ushirika wakiwemo wakulima wa tumbaku ni pamoja na kuwachukulia hatua viongozi wabadhirifu wa vyama hivyo.
“ Katika maeneo yanayolima tumbaku viongozi wabadhirifu wa Vyama vya Ushirika 26 Mkoani Ruvuma  wakiwemo Maafisa Ushirika wawili wamesimamishwa kazi na kufikishwa mahakamani.” alisema Ole-Nasha.
Pia Mhe. Ole-Nasha alifafanua kuwa sheria ya sasa inakataza vyama kukopa zaidi ya asilimia 30 ya mali zake (Own Capital) ili kuzuia vyama hivyo kuingia kwenye madeni makubwa yasiyolipika  na hatimaye kusababisha migogoro ndani ya vyama.
Akizungumzia mafanikio upande wa tozo, Ole-Nasha lisema kuwa kuanzia sasa Mkutano Mkuu utakuwa chini ya uenyekiti huru utakaochaguliwa na wajumbe wa mkutano huo kinyume na awali ambapo Mwenyekiti wa Bodi ya Tumbaku ndiye aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu. 
“Lengo ni kulinda maslahi ya wakulima ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa tozo zote zinazoidhinishwa na Mkutano Mkuu zinakuwa na maslahi kwa wakulima wa Tumbaku.” Aliongeza Ole-Nasha.
Kwa mujibu wa Ole-Nasha Serikali inatambua uwepo wa kodi nyingi na tozo kwenye mazao mbalimbali ya chakula na biashara hivyo kwa kushirikiana na wadau imedhamiria kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara katika sekta ya kilimo kwa kupitia upya taratibu, vibali, tozo, kodi, ushuru na ada nyingine zinazotozwa ili kutoa nafuu kwa wakulima.    

SERIKALI YAENDELEA NA MPANGO WA KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA VIJIJINI.

Na Fatma Salum- MAELEZO, Dodoma.index
Serikali imewahakikishia wananchi kuwa inaendelea na utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa zahanati kila kijiji, vituo vya afya kila kata na Hospitali katika kila Wilaya ikiwa ni mkakati wake wa kuboresha huduma za afya kote nchini.
Hayo yamesemwa leo bungeni mjini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Suleiman Jafo wakati akijibu swali la Mbunge wa Busokelo Mhe. Fredy Mwakibete kuhusu Mpango wa kujenga zahanati kila Kijiji na kituo cha afya kila Kata. 
Mhe. Jafo alisema kuwa Serikali kwa kushirikisha nguvu za wananchi inaendelea na ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na Hospitali kila Wilaya ambapo ujenzi huo unafanyika chini ya Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM).
“Utekelezaji wa Mpango huo unaendelea na kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri zimetengewa shilingi bilioni 182.5 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya afya na kipaumbele kitatolewa katika kukamilisha miradi viporo badala ya kuanzisha miradi mpya.” alisema Jafo.
 Kwa mujibu wa Mhe. Jafo, Ofisi ya Rais TAMISEMI inafanya tathmini ya utekelezaji wa mpango wa MMAM ili kujua idadi ya Vijiji ambavyo havina zahanati, Kata ambazo hazina vituo vya afya na Wilaya ambazo hazina Hospitali lengo likiwa ni kuhakikisha maeneo hayo yanapewa kipaumbele na kutengewa fedha ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi.
Akieleza mafanikio ya mpango wa MMAM, Mhe. Jafo alisema kuwa chini ya mpango huo vituo vya kutolea huduma za afya vimeongezeka kutoka 5,255 mwaka 2006/2007 hadi 6,935 mwaka 2014/2015 sawa na ongezeko la asilimia 39.9 hivyo kuna matumaini makubwa ya kuvifikia vijiji vingi kupitia mpango huo.

TAWLA yasisitiza mabadiliko ya sheria za Usalama Barabarani ili kupunguza ajali na vifo

images 
Jonas Kamaleki-Maelezo
Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Kamanda Mohamed Mpinga amesema mabadiliko ya sheria ya usalama barabarani hayaepukiki ili kupunguza vifo na majeruhi vitokanavyo na ajali za barabarani.
Kamanda Mpinga amayesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa Uzinduzi wa Programu ya Usalama Barabarani inayoratibiwa na  Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) kwa kushirikiana na wadau mbali mbali wa Usalama Barabarani.
“Sheria zinazohusu masuala ya Usalama barabarani inabidi zifanyiwe marekebisho ili ziweze kusaidia kupunguza vifo na majeruhi kwani zilivyo sasa hazitoi adhabu kali kwa wanaokiuka sheria hizo”alisema Kamanda Mpinga.
Aidha Kamanda huyo alisisitiza kuwa suala la Usalama Barabarani ni la kila mmoja hivyo inabidi litiwe mkazo na watu wote.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa TAWLA, Bi Tike Mwambipile amesema chama hicho kwa kuzingatia umuhimu wa kushughulikia masuala ya Usalama Barabarani kimeona ni vyema kikafanya kikao hicho ili kupata mawazo ya wadau.
Bi Mwambipile amesema vifo vingi vinavyotokana na ajali za barabarani vinawaacha wanawake wengi wakiwa wajane na watoto yatima wanaongezeka.
 Ameongeza kuwa fedha nyingi zinatumika kuwahudumia majeruhi badala ya kufanya shughuli nyingine za maendeleo ya jamii.
Naye Mwenyekiti wa TAWLA, Bi Aisha Bade amesema mabadiliko makubwa ya sera na sheria za usalama barabarani  ni lazima yafanyike ili kupunguza athari zitokanazo na ajali za barabarani.
Bi Bade amesema TAWLA kwa kushirikiana na wadau wengine inafanya juhudi za makusudi ili kuhakikisha sheria hizi zinabadilishwa ili kukabiliana na janga hili.
Visababishi vya ajali kwa hapa nchini vimetajwa na Mratibu wa Mradi Bloomberg wa Usalama Barabarani, Bi Mary Kessy kuwa ni ulevi, kutofunga mkanda, kutoweka vizuizi vya watoto kwenye magari, mwendo kasi na kutovaa kofia ngumu kwa waendesha pikipiki.

Kampuni ya Vision Investiments yatoa fursa kwa makampuni mengine.

indexMkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Vision Investiments  Ally Nchahaga (katikati) akifafanua juu ya fursa zitolewazo na Kampuni yao leo Jijini Dar es Salaam, kulia ni Afisa Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Aisha Mohammed na kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mauzo cha Kampuni ya Mafuta ya Oil com Aluwy Amar.
…………………………………………………………………………………………………………………..
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Kampuni ya Vision Investments imetoa fursa kwa makampuni mengine kushiriki kutoa huduma mbalimbali wakati wa makutano baina ya wanunuzi na wauzaji wa magari yanayoandaliwa na Kampuni hiyo yatakayofanyika Mei 29 mwaka huu.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni hiyo Ally Nchahaga ambaye amewaomba wauzaji na wanunuzi wa magari pamoja na makampuni mbalimbali kushiriki katika makutano hayo ili kutimiza mahitaji yao ya magari.
“Kama ilivyo ada kila Jumapili ya mwisho wa mwezi Kampuni yetu inawakutanisha wauzaji, wanunuzi wa magari pamoja na makampuni tofauti kutoa huduma shirikishi zinazokwenda sambamba na biashara hii ya magari ya watu binafsi” alisema Nchahaga.
Kwa mujibu wa Kampuni ya Vision Investments makutano hayo yatafanyika nchini kwa mara ya sita ambapo mwaka huu yatafanyika katika viwanja vya Coco Mihogo kuanzia sa 4 asubuhi.
Nchahaga alizitaja baadhi ya kampuni zinazotoa huduma shirikishi zikiwemo Benki ya watu wa Zanzibar (PBZ), Kampuni ya Mafuta ya Oil com, Kampuni ya Coca cola, pamoja na Kampuni ya Simply Elegant ambazo zinatoa huduma za mikopo ya magari, mafuta ya magari, vinywaji pamoja na vilainishi vya magari kwa wateja watakaokuwepo katika makutano hayo.
Aidha, Nchahaga amesisitiza kuwa kampuni yao sio ya maonyesho ya magari wala wao sio madalali bali ni kampuni inayotoa fursa yenye gharama nafuu kwa wanachi kutimiza mahitaji yao ya magari.
Ameongeza kuwa elimu kuhusu magari na vifaa vyake itatolewa bure na mtu yeyote atakayehitaji kuuza gari lake atachangia shilingi elfu 50 ikiwa ni mchango wa kuweka gari lake katika viwanja hivyo pamoja na kufanyiwa matangazo katika mitandao ya kijamii kwa mwezi mzima.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Mauzo cha Kampuni ya Mafuta ya Oil com Aluwy Amar amesema kuwa Kampuni yao inatoa huduma mpya ya kulipa kwa kutumia kadi itakayomrahisishia mteja kupatiwa huduma za mahitaji ya mafuta ya magari yao kwa hiyo, watashiriki katika makutano hayo ili kutoa elimu kwa wateja hao kuhusu matumizi ya kadi hizo.
“Huduma hii tumeianza kuitoa kwa mikoa ya Dar es Salaam na Pwani, huduma za kupatiwa kadi pamoja na kufanya miamala yote ni bure pia mwisho wa mwezi tutatoa huduma ya punguzo la bei kulingana na matumizi ya mteja”,alisema  Amar.
Kwa upande wake Afisa Mahusiano wa Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Aisha Mohammed amesema kuwa wamefurahi kupata fursa hii ya kushiriki katika makutano hayo kwakua anaamini ni njia moja wapo kwa benki hiyo kuwapa mikopo au kuwanunulia magari wateja wao ili kutimiza ndoto zao kwa muda muafaka.

‘TUNASAKA’ NYOTA WAPYA– Mbeya City Council FC

DSC_0301
SIKU  chache baada ya pazia  la ligi kuu ya soka Tanzania  bara kufungwa,Kocha mkuu wa Mbeya  City Fc  Kinnah Phiri ameanza zoezi maalumu la kusaka nyota wapya ambao atawajumuisha  moja kwa moja kwenye vikosi vya timu yake  msimu ujao.
Akizungumza muda mfupi baada ya majaribio ya siku ya kwanza  kwa wachezaji wapya vijana waliofika kujaribu bahati zao kwa kuonyesha  vipaji walivyonavyo navyo, afisa habari wa City Dismas Ten amesema kuwa muitikio umekuwa mzuri katika siku hii kwanza ambayo nyota hao wa baadae wamefika kuonysha  uwezo wao mbele ya kocha huyo raia wa malawi.
“Leo ni siku ya kwanza, kitu kizuri mwitikio umekuwa mkubwa, takribani vijana 50 wamejitokeza kujaribu  bahati zao kulingana na vipaji walivyonavyo, haya ni majaribio ambayo kocha Phiri ameyaitisha ili kusaka vipaji vipya ambavyo moja kwa moja vitaingia kwenye timu yetu kubwa na ile ya U20, alisema.
Akiendelea zaidi, Ten  alisema kuwa,  hii  imekuwa ni kawaida kwa City kila inapofika mwisho wa msimu kuwaleta  pamoja vijana wote wanaoamini wanauwezo wa kucheza mpira, kufichua  vipaji vyao ili waje kuwa wachezaji wakubwa  baadae.
“Hii ni kawaida yetu, kila tunapomaliza msimu huwa tunafanya hivyi, vijana wote wenye umri kuanzia miaka 17-22 ni fursa kwao kujitokeza, zoezi hili la kusaka vipaji  litakuwepo kwa juma zima, leo hatukuwa na kocha Phiri kwa sababu  alikuwa kwenye majukumu mengine lakini kesho tutakuwa  kwenye uwanja Sokoine na mwalimu  atakuwa, kwa hiyo vijana wote ndani ya jiji la Mbeya na mikoa ya jirani waje kujaribu bahati zao.
Kwa upande wa vijana waliojitokeza siku ya leo, walishukuru kuwepo kwa zoezi hili kwa sababu limerahisisha  uwezekano wa vipaji walivyonavyo kuonekana mapema hatimaye waweze kutimiza ndoto zao za kuwa wachezaji wakubwa  siku za usoni

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZINDUA KAMPENI YA LONGA NASI LEO

mak1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akihutubia kwenye uzinduzi wa kampeni ya LONGA NASI inayomaanisha Sema au ongea na TAKUKURU kwa kutoa Taarifa za vitendo vya Rushwa au maoni ya kuboresha mapambano dhidi ya Rushwa ambapo uzinduzi huo umeambatana pamoja na uzinduzi wa matumizi mapya ya simu ya Dharura ya 113. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 24,2016 katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es salaam.
mak2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki kabla ya kuzindua mpango wa kampeni ya LONGA NASI inayomaanisha Sema au ongea na TAKUKURU kwa kutoa Taarifa za vitendo vya Rushwa au maoni ya kuboresha mapambano dhidi ya Rushwa ambapo uzinduzi huo umeambatana pamoja na uzinduzi wa matumizi mapya ya simu ya Dharura ya 113. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 24,2016 katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es salaam.
mak3 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki kabla ya kuzindua mpango wa kampeni ya LONGA NASI inayomaanisha Sema au ongea na TAKUKURU kwa kutoa Taarifa za vitendo vya Rushwa au maoni ya kuboresha mapambano dhidi ya Rushwa ambapo uzinduzi huo umeambatana pamoja na uzinduzi wa matumizi mapya ya simu ya Dharura ya 113. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 24,2016 katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es salaam.
mak4 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akivuta kamba kuondoa kitambaa kuzindua mpango wa kampeni ya LONGA NASI inayomaanisha Sema au ongea na TAKUKURU kwa kutoa Taarifa za vitendo vya Rushwa au maoni ya kuboresha mapambano dhidi ya Rushwa ambapo uzinduzi huo umeambatana pamoja na uzinduzi wa matumizi mapya ya simu ya Dharura ya 113. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 24,2016 katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es salaam. Kushoto Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki, kushoto Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Valentino Mlowola.
mak5 
Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiagana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuwia na kupambana na Rushwa Nchini TAKUKURU Valentino Mlowola baada ya kuzindua mpango wa kampeni ya LONGA NASI inayomaanisha Sema au ongea na TAKUKURU kwa kutoa Taarifa za vitendo vya Rushwa au maoni ya kuboresha mapambano dhidi ya Rushwa ambapo uzinduzi huo umeambatana pamoja na uzinduzi wa matumizi mapya ya simu ya Dharura ya 113. Uzinduzi huo umefanyika leo Mei 24,2016 katika viwanja vya Mwembe Yanga Temeke jijini Dar es salaam. (Picha na OMR)

Taasisi ya Mbalawala yaipongeza Nishati na Madini kuwezesha shughuli zake kufahamika

index 
Meneja Uendeshaji   kutoka  Taasisi ya Wanawake ya Mbalawala Women Organization inayojishughulisha na uzalishaji wa briketi  za makaa ya  mawe wilayani Mbinga mkoani  Ruvuma, Hajiri Kapinga (kulia)  akielezea mafanikio ya  taasisi hiyo mara baada ya  taarifa zake kuanza kuchapishwa katika Jarida la  Wizara. Kushoto ni Kaimu Mkuu  wa Kitengo cha Mawasilano  Serikalini Wizara ya Nishati na Madini, Asteria Muhozya.
………………………………………………………………………………………………………………
Na Greyson Mwase, Dar es Salaam
Taasisi ya  Wanawake ya Mbalawala inayojishughulisha na  uzalishaji wa braketi za makaa ya mawe ijulikanayo kama Mbalawala Women Organization yanye makazi yake katika kijiji cha Ruanda wilayani Mbinga mkoani  Ruvuma imeipongeza  Wizara ya Nishati na Madini kupitia Kitengo cha Mawasiliano Serikali kwa kutangaza shughuli zake hali iliyopelekea wateja wa makaa ya mawe katika taasisi hiyo kuongezeka kadri  siku zinazokwenda.
Taasisi hiyo inayofanya  shughuli zake karibu na Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka inajishughulisha na utengenezaji  wa briketi bora za makaa ya mawe kwa ajili ya kupikia
Pongezi hizo zilitolewa na  Meneja Uendeshaji  wa Taasisi hiyo Hajiri Kapinga aliyekutana na  Kaimu Mkuu  wa Kitengo cha Mawasilano  Serikalini Wizara ya Nishati na Madini, Asteria Muhozya jijini  Dar es Salaam na kusema kuwa  tangu  Kitengo cha Mawasiliano Serikalini kianze kuchapisha  habari zinazohusu  taasisi hiyo kupitia Jarida lake linalochapishwa kila wiki lijulikanano  kama MEM Newsbulletin  wameshuhudia idadi kubwa ya  wateja  ikiongezeka na  kuzidi  uzalishaji wa taasisi hiyo.
Alisema kabla ya  habari zake kuchapishwa na  Jarida la Wizara,  taasisi hiyo ilikuwa ikiwauzia briketi za  makaa ya mawe wateja wake  walioko katika  vijiji  vinavyozunguka mgodi wao  wilayani Mbinga mkoani  Ruvuma.
“Mara baada ya   taarifa zetu kuanza kuchapishwa na Jarida la  Wizara ya Nishati na Madini  tumeshuhudia mabadiliko makubwa kwani tumekuwa  tukipokea simu kutoka mikoa mbalimbali  hususan  Dar es Salaam,  Mbeya, Iringa wateja wakihitaji bidhaa,  hali inayopelekea  mahitaji kuwa makubwa kuliko  kiasi tunachozalisha,.” alisema Kapinga.
“Jarida limetufanya  tujulikane, hata wahisani wetu wameahidi kuongeza nguvu  na misaada katika kuwezesha  mradi huu  kuendelea vizuri; Jamii inasoma habari zetu na sisi tumesoma masuala mengi  kuhusu nishati na madini,” aliongeza
Kapinga aliendelea kusema kuwa ili kukabiliana na  mahitaji makubwa ya wateja taasisi hiyo imeweka mkakati wa kununua mtambo mwingine kutoka nje ya nchi  ili kuongeza uzalishaji utakaoendana na mahitaji ya wateja.
Alisema mikakati mingine ni pamoja na ujenzi wa ghala la kuhifadhia makaa ya mawe, ununuzi wa magari  kwa ajili ya usambazaji wa bidhaa ya briketi za makaa ya mawe katika  vituo vya uwakala  vitakavyoanzishwa nchini karibu kila mkoa.
“Mara baada ya kuanzisha vituo hivyo, wateja wetu watakuwa wanapata bidhaa  kutoka kwa mawakala badala ya kukutana na sisi moja kwa moja,” alisema Kapinga.
Alisema kuwa pia wamejipanga kutoa elimu ya matumizi ya briketi za matumizi ya makaa ya mawe na  utafutaji wa masoko  kwa kushirikiana na wadau wa utengenezaji wa majiko  sanifu yanayotumia briketi za makaa ya  mawe kwa matumizi ya majumbani.
Akielezea uanzishwaji wa taasisi hiyo, Kapinga alisema kuwa  taasisi hiyo  ilianzishwa chini ya ufadhili wa Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Ngaka (Tancoal Energy Limited)  unaomilikiwa na kampuni ya Intra Energy ya Australia kwa asilimia  70 na Serikali ya  Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo  la Taifa (NDC) kwa asilimia 30 ambao wanafurahishwa na   hatua iliyofikiwa na  taasisi hii  katika uzalishaji  ya briketi za makaa ya mawe.
Aliongeza sambamba na uzalishaji wa briketi za makaa ya mawe, taasisi hiyo imekuwa ikitoa mafunzo juu  ya utumiaji wa briketi ya makaa ya mawe katika  vijiji na miji  jirani na mgodi wake pamoja na ushiriki katika maonesho mbalimbali ndani ya mkoa  wa Ruvuma.
“Lengo letu ni kuhakikisha briketi za makaa ya mawe zinazoendelea kuzalishwa katika mgodi wetu  zinatumika majumbani, shuleni , vyuoni na taasisi mbalimbali  na kupunguza uharibifu wa mazingira kwa kutumia kuni” alisema Kapinga
Aliendelea kusema kuwa lengo la uanzishwaji wa taasisi hiyo lilikuwa ni  kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kupitia  briketi za makaa ya mawe na kuachana na matumizi ya kuni ambayo ni chanzo  cha uharibifu wa mazingira.
Naye Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Asteria Muhozya alisema kuwa  lengo la  Jarida la Wizara ni kutangaza shughuli za nishati na madini  ikiwa ni pamoja na  taasisi zake
Muhozya aliongeza kuwa  jarida la Wizara  lipo  tayari kutangaza shughuli za wadau wa Madini  na Nishati ili kuhakikisha kuwa sekta  hizo zinakuwa na kuwa na mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa nchi

SERIKALI KUZITAMBUA NA KUZIRASIMISHA BANDARI BUBU ZILIZOKIDHI VIGEZO KWA LENGO LA KUKUSANYA KODI.

images MAELEZO
.DODOMA.
Serikali imesema kuwa inaendelea na utaratibu wa kuzitambua na kuzirasimisha bandari Bubu zote zilizokidhi vigezo ambazo zinatumiwa na wafanyabiashara kupitisha bidhaa mbalimbali ili ziweze kuchangia katika Pato la Taifa kulingana na  wingi wa bidhaa zinazopitishwa katika bandari hizo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Edwin Ngonyani ametoa kauli hiyo bungeni mjini Dodoma leo wakati akijibu maswali ya Wabunge waliotaka kujua mkakati wa Serikali katika kudhibiti bidhaa zinazoingizwa nchini na wafanyabiashara wasio waaminifu kupitia bandari bubu hali inayoikosesha  serikali mapato.
Mhe. Ngonyani amekiri kuwepo kwa ongezeko la wafanyabiashara wasio waaminifu wanaotumia bandari hizo katika maeneo mbalimbali nchini hasa ukanda wa Pwani wa Bahari ya Hindi, Ziwa Tanganyika, Ziwa Victoria na maeneo ya mipakani ambayo yanaingia moja kwa moja kwenye makazi ya watu akieleza kuwa wengi wa wafanyabiashara wanakwepa kodi na kutafuta urahisi wa kupitisha mizigo yao.
Amesema maeneo hayo yamekuwa chanzo kikubwa cha upitishaji wa bidhaa zisizokidhi viwango, Silaha na Biashara haramu na kubainisha kuwa baadhi ya wafanyabiashara wa ndani wasio waaminifu wamekuwa wakishirikiana na raia wa kigeni kuagiza na kuingiza bidhaa hizo kupitia bandari hizo kwa lengo la  kukwepa kodi.
Amesisitiza kuwa  Serikali ya Awamu ya tano inalishughulikia kwa nguvu zote suala hilo kupitia watendaji wake wakiwemo wakuu wa mikoa wa maeneo husika ambao hushirikiana na mamlaka zinazohusika vikiwemo vyombo vya ulinzi na usalama kudhibiti njia na maeneo yote yanayotumiwa na wafanyabiashara hao.
” Kama Serikali tunaendelea kufanya vikao kwa kushirikiana na wakuu wa mikoa na mamlaka zinazohusika kuangalia namna ya kurasimisha bandari bubu zilizobaki ili tuweze kukusanya mapato ya Serikali yaliyokuwa yakipotea kutokana na wingi wa mizigo inayopitishwa” Amesema Mhandisi Ngonyani.
Amefafanua kuwa mwaka katika kipindi cha mwaka 2015 na mwezi Januari,  2016, doria zilizofanyika katika maeneo yanayotumiwa na wafanyabishara hao zilifanikisha kukamatwa kwa wafanyabiashara 98 ambao wote walichukuliwa hatua za kisheria ikiwem mali zao kutaifishwa pamoja na  kuwafikisha mahakamani.
Kuhusu bandari bubu zilizotambuliwa na kuzirasimishwa na Serikali katika  Pwani ya Bahari ya Hindi ni  Mbweni ya jijini Dar es salaam, Mlingotini mkoani Pwani, Kisiju na Nyamisati mkoa wa Pwani na Bandari bubu ya Kilambo mkoani Mtwara.
Aidha, amesema Serikali inaendelea na utaratibu wa kurasimisha bandari binafsi umefanyika katika ziwa Victoria mkoani Mwanza na maeneo mengine ambayo serikali inaendelea kuyafanyia kazi.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Masauni  amesema kuwa Serikali inaendelea kuvijengengea uwezo vikosi vyake vya ulinzi na usalama kwa kuviongezea vifaa vya kisasa ili viweze kuimarisha doria nchi nzima ili kukabiliana na vitendo vyote vya uvunjaji wa sheria.
Amesema Jeshi la Polisi linaendelea kushirikiana na wananchi kukusanya taarifa za kiharifu ili kuwabaini na kuwakamata wafanyabishara wote wanaojihusisha na uagizaji na uingizaji wa bidhaa kupitia bandari bubu  ambaoumekua ukiisababishia serikali ikose mapato.
” Vyombo vyetu vya ulinzi na usalama vinaendelea kukusanya taarifa za kiharifu kutoka kwa wananchi ili kukabiliana na wimbi hili, pia tunaendelea kuviongezea nguvu vikosi vyetu vya ulinzi na usalama ili viweze kutimiza majukumu yao ipasavyo” Amesisitiza Mhe.Masauni.

Serikali yaombwa kusaidia uingizwaji wa mafuta ya watu wenye ualbino

maxresdefault 
Na: Lilian Lundo – MAELEZO
Taasisi ya Josephat Torner Foundation inayojishughulisha na watu walemavu wameiomba Serikali kusaidia uingizaji wa mafuta ya ngozi kwa watu wenye albino nchini.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo Josephat Torner alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam ambapo alibainisha changamoto mbalimbali zinazo wakabili watu wenye ualbino.
“Watu wengi wenye ualbino wanaishi chini ya miaka 40 kutokana na kukosa mafuta ya kulinda ngozi dhidi ya miale ya jua, mafuta hayo huwasaidia kutoathilika na magonjwa ikiwemo kansa ya ngozi,” alisema Torner.
Torner alisema kuwa mafuta ya ngozi kwa watu wenye ualbino yanauzwa kati ya shilingi 30,000 na 40,000 kwa chupa ambapo mtu mwenye ualbino mmoja anatumia wastani wa chupa tano kwa mwaka.
Mkurugenzi huyo alisema kuwa gharama ya mafuta hayo ni kubwa kwa watu wenye ualbino ambao wengi wao wanaishi maisha ya chini na hasa wale wanaoishi vijijini ambao hawawezi kumudu kuyapata na kununua mafuta hayo.
Aidha, aliongeza kuwa kama Serikali itasaidia uingizwaji wa mafuta hayo na kupunguza ushuru ili yaingie nchini kama madawa kupitia Bohari Kuu ya Dawa (MSD) tofauti na hali ilivyo sasa ambapo yanatozwa kodi kama vipodozi, hatua hiyo itasaidia kupunguza kwa kiasi kubwa kushuka bei mafuta hayo na kuwafikia walengwa.
Kwa upande wake, Mratibu wa taasisi ya Afrikan Albino Foundation kutoka Netherland nchini Tanzania Bas Kreukniet amesema kuwa ikiwa Serikali itashiriki katika uingizaji wa mafuta hayo kuna uwezekano wa mafuta hayo kuuzwa shilingi 4,000 kwa chupa.
Aliongezea kuwa ikiwa bei ya mafuta hayo itapungua itawasaidia watu wengi wenye ualbino hasa wa kipato cha chini na wale waishio vijijini kutumia mafuta hayo na kuwasaidia kujikinga na miale ya jua.
Hadi sasa taasisi ya Afrikan Albino Foundation imeweza kuwasaidia watu wenye ualbino wapatao 13,000 tangu waanze kuleta mafuta hayo nchini mwaka 2004 ambapo kila mwezi jumla ya chupa 5,200 huingizwa nchini kwa ajili ya kuwasaidia watu wenye ualbino.

Jamii yahimizwa kuwatunza vizuri wanyama wafugwao

index 
Na Mahmoud Ahmad ,Arumeru
JAMII hapa nchini imehimizwa kuhakikisha kuwa inawapa matunzo mazuri
wanayama wafugwao,ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa inawapatia lishe
bora,makazi mazuri na kuwapatia huduma za afya.
Kaimu ofisa mifugo wa Halimashauri ya Wilaya ya Meru,Dkt.Asha Ali
aliyasema hayo juzi alipokuwa akifungua mafunzo ya namna ya kuwatunza
mifugo,kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali ya mifugo kutoka maeneo
mbalimbali hapa nchini.
Mafunzo hayo ya wiki moja ambayo yalilenga kuwapatia mbinu bora za
utunzaji wa waqnyama, yaliratibiwa na shirika la kuhudumia wanyama
Meru(MAWO) kwa ufadhili wa shirika la wanyama la WTG la Ujerumani
yalifanika katika Kata ya Kikatiti wilayani hapa
.
Wanyama waliolengwa  katika mafunzo hayo ni wale ambao wanaonekana
kutokupewa kipaumbele katika jamii licha ya umuhimu wao kwa jamii
ambapo wanayama hao ni punda paka na mbwa.
Dkt.Ali ametoa wito kwa wanachuo hao kuhakikisha kuwa wanazingatia na
kushika kwa makini yale yote wanayofundishwa ili waweze  kutumia ujuzi
huo kuelimisha jamii mbinu mbalimbali za kuwatunza wanyama hao.
Kwa upande wao wakufunzi wa mafunzo hayo,Dkt. Solomon Onyango na
Dkt.Amos Suppet kutoka taasisi Donkey Sanctuary ya Kenya(DSK),wamesema
kuwa katika mafunzo hayo wanachuo hao watafundishwa namna ya kuboresha
maisha ya wanyama ikiwa ni pamoja na kukabiliana na magonywa ya
mifugo.
Kadhalika wakufunzi hao wametoa wito kwa jamii kuhakikisha kuwa
wanawahudumia vizuri punda kutokana na umuhimu wao wa kubeba
mizigo,kutokuwapiga sana na kuhakikisha kuwa wanawatandikia tandiko
mgongoni ili wasiweze kuchumbuka na kupata vidonda pindi wabebeshapo
mizigo.
Kwa unde wake mratibu wa mafunzo hayo kutoka shirika la MAWO.Johnson
Lyimo amesema kuwa mpaka sasa Shirika lake kwa kushirikiana na WTG la
Ujerumani wameshatoa mafunzo hayo kwa wanachuo zaidi ya miambili
kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Pia tumekuwa tukizunguka katika vijiji mbalimbali hapa nchini ambapo
tumekuwa tukitoa elimu hii kwa wafugaji ikiwa ni pamoja na kuitibu
mifugo hiyo hususani punda ambao tumewakuta wakiwa na magonjwa
mbalimbali.Na Mahmoud Ahmad ,Arumeru
JAMII hapa nchini imehimizwa kuhakikisha kuwa inawapa matunzo mazuri
wanayama wafugwao,ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kuwa inawapatia lishe
bora,makazi mazuri na kuwapatia huduma za afya.
Kaimu ofisa mifugo wa Halimashauri ya Wilaya ya Meru,Dkt.Asha Ali
aliyasema hayo juzi alipokuwa akifungua mafunzo ya namna ya kuwatunza
mifugo,kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali ya mifugo kutoka maeneo
mbalimbali hapa nchini.
Mafunzo hayo ya wiki moja ambayo yalilenga kuwapatia mbinu bora za
utunzaji wa waqnyama, yaliratibiwa na shirika la kuhudumia wanyama
Meru(MAWO) kwa ufadhili wa shirika la wanyama la WTG la Ujerumani
yalifanika katika Kata ya Kikatiti wilayani hapa
.
Wanyama waliolengwa  katika mafunzo hayo ni wale ambao wanaonekana
kutokupewa kipaumbele katika jamii licha ya umuhimu wao kwa jamii
ambapo wanayama hao ni punda paka na mbwa.
Dkt.Ali ametoa wito kwa wanachuo hao kuhakikisha kuwa wanazingatia na
kushika kwa makini yale yote wanayofundishwa ili waweze  kutumia ujuzi
huo kuelimisha jamii mbinu mbalimbali za kuwatunza wanyama hao.
Kwa upande wao wakufunzi wa mafunzo hayo,Dkt. Solomon Onyango na
Dkt.Amos Suppet kutoka taasisi Donkey Sanctuary ya Kenya(DSK),wamesema
kuwa katika mafunzo hayo wanachuo hao watafundishwa namna ya kuboresha
maisha ya wanyama ikiwa ni pamoja na kukabiliana na magonywa ya
mifugo.
Kadhalika wakufunzi hao wametoa wito kwa jamii kuhakikisha kuwa
wanawahudumia vizuri punda kutokana na umuhimu wao wa kubeba
mizigo,kutokuwapiga sana na kuhakikisha kuwa wanawatandikia tandiko
mgongoni ili wasiweze kuchumbuka na kupata vidonda pindi wabebeshapo
mizigo.
Kwa unde wake mratibu wa mafunzo hayo kutoka shirika la MAWO.Johnson
Lyimo amesema kuwa mpaka sasa Shirika lake kwa kushirikiana na WTG la
Ujerumani wameshatoa mafunzo hayo kwa wanachuo zaidi ya miambili
kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini.
Pia tumekuwa tukizunguka katika vijiji mbalimbali hapa nchini ambapo
tumekuwa tukitoa elimu hii kwa wafugaji ikiwa ni pamoja na kuitibu
mifugo hiyo hususani punda ambao tumewakuta wakiwa na magonjwa
mbalimbali.

CBE yatoa ufafanuzi tuhuma za upostoshaji.

cb1 
Mkuu wa Chuo cha Elimu Biashara (CBE) Prof. Emmanuel Mjema akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) ripoti ya Mamlaka ya Udhibiti ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ya Mwaka huu inayoonesha chuo hicho ni moja kati ya Taasisi 14 zilizofanya vizuri kwa kushika nafasi ya kwanza kwa kupata alama 95.8 katika kufuatilia sheria ya manunuzi ya umma na kuutaka umma kupuuza taarifa za upotoshaji zinazotolewa na baadhi ya watu kuwa wanakiuka sheria hizo.PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO.
cb2 
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano huo
cm3 
Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Prof. Emmanuel Mjema akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani) ripoti ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) inayoonesha kuwa chuo hicho kimepata ziada ya bilioni 1.2 kati ya mwaka huu na kufanya chuo kujiendesha kwa faida tofauti na baadhi taarifa za upotoshaji zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari.
………………………………………………………………………………………………………………………
Frank Mvungi-Maelezo
Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kimewataka wananchi kupuuza taarifa za upotoshaji zilizoripotiwa na Baadhi ya vyombo vya Habari Hapa nchini kuhusu chuo hicho.
Akizungumza na vyombo vya Habari leo jijini Dar es salaam Mkuu wa chuo hicho Prof. Emmanuel Mjema amesema tuhuma za  kuwa chuo hicho kina ubadhirifu wa kutisha si za kweli na zinalenga kuchafua taswira ya chuo hicho.
“Chuo kinafanyiwa ukaguzi wa Hesabu zake na Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikali na kwa kipindi cha miaka minne tumepata hati safi (Clean Audit Report) kuanzia mwaka 2010/2011 hadi 2014/2015 .” alisisitiza Prof. Mjema.
Katika ukaguzi huo ripoti hiyo ilionyesha kuwa Taasisi hiyo imekuwa ikizingatia sheria na kanuni za matumizi ya fedha za umma hali iliyopelekea kupata hati safi kwa kipindi chote.
Pia Chuo hicho kilifanyiwa ukaguzi na Mamlaka ya Udhibiti wa manunuzi Serikalini (PPRA) kwa mwaka unaoishia 2014/2015 na Chuo hicho kupata alama 95.8 hivyo kuwa moja ya Taasisi za Umma zinazofanya vizuri katika kuzingatia sheria na kanuni za manunuzi ya umma.
Prof. Mjema amesema kuwa chuo hicho kimekuwa kikijiendesha bila kupata ruzuku toka Serikalini na pia kuzalisha mapato ya ziada zaidi ya bilioni moja kwa kwa kila mwaka wa fedha kuanzia mwaka 2013 hadi 2015.
Kutokana na Mafanikio hayo chuo hicho kimeweza kuanzisha Kampasi ya Mbeya ambapo chuo hicho kimenunua eneo lenye ukubwa wa ekari 54.9 na pia maboresho katika maktaba ya chuo yamefanyika.
Mafanikio mengine ni kujenga hema kubwa lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 740 na kuboresha karakana ya vipimo na mizani chuoni hapo.

VIJANA WATAKIWA KUACHANA NA UTUMIAJI WA MADAWA YA KULEVYA

Muandaaji wa tamasha la michezo kwa vijana wa mkoa wa Arusha Neema Mollel ambaye pia ni  Mwenyekiti wa CCM Kata ya Sakina pamoja na  mlezi wa Timu za mpira kata ya Sakina Jijini Arusha akiongea katika fainali za Tamasha la vijana lililofanyika katika viwanja vya kumbukumbu ya Sheikh Amri Abeid jijini hapa.
 
Martini Shimweta( Mdau) ambaye ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa  Olmatejoo A.
 
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Arusha Mjini Wilfred Soilel.
Diwani wa kata ya Ungalimited akiwa anawaasa vijana kuachana na madawa ya kulevya katika fainali hizo
 
Kiongozi wa Intersport Club akipokea kombe baada ya ushindi.
 …………………………………………………………………………………………………
Na Woinde Shizza,Arusha
 
Timu ya Intersport Club yaibuka kidedea katika Tamasha la vijana  mara baada ya  kuifunga Club ya mairiva bao 3 kwa 1 katika fainali iliyofanyika katika uwanja wa Shekhe Amir Abeid uliopo Jijini Arusha.
 Tamsha hilo ambalo lilianza mapema mwanzoni mwa mwezi huu limeweza kufikia tamati huku vijana wakiwatoa wito kwa wadau mbalimbali wa michezo kujitokeza kuanzisha mashindano kama haya kwani yanawasiadia kwa kiasi kikubwa 
Akizungumza wakati wa fainali za mashindano hayo muuandaaji wa mashindano hayo ambaye ni mwenyekiti wa CCM kata ya Sakina Neema Mollel alisema kuwa lengo la kuanzisha tamasha hili la vijana ni kuwaleta pamoja vijana na kuwapa elimu  ya jinsi ya kupiga vita utumiaji wa madawa ya kulevya kwa vijana 
Alisema kuwa vijana wengi wamekuwa wanajishirikisha na utumiaaji wa madawa ya kulevya ivyo aliona ni bora akatumia muda huu kuwaleta pamoja ili kuwapa elimu pamoja na kuwashirikisha katika tamasha hili la michezo ambalo limeweza kuwafundisha vijana wengi huku wengine wakiwa wameamua kuaachana kabisa na kutumia madawa haya ya kulevya badala yake wameamua kushiriki katika mazoezi pamoja na michezo
 
 “nia alisi ya  kuandaa mashindano haya ni kuwaleta kwa pamoja vijana pamoja na kupiga vita madawa ya kulevya kwa vijana,kuwaleta vijana pamoja,kuwaondoa vijana wasiendelee kukaa mitaani bila kazi kwani michezo ni ajira”Alisema Neema Mollel
 
Aidha aliwataka wazazi na jamii kwa ujumla kuwajengea vijana misingi Imara ilikuwajengea mtizamo mzuri wa maisha ya mbeleni badala ya kuwatupia lawama ambazo baadae zinajenga uadui kati yao na wazazi na
jamii.
 
Akikabidhi kombe kwa washindi ambao ni Interspot Club ,mwenyekiti wa CCM wilaya ya Arusha Wilfred Soilel amesema kuwa Michezo hujenga hujenga urafiki kati ya vijana ,wanafahamiana pia afya ya mwili inaimarika, pia itamfanya kijana ufahamu wake kuchangamka.
 
Sambamba ugawaji wa zawadi katika fainali hizo mshindi wa kwanza Intersport club kutoka kata ya Ungalimited, amekabidhiwa Kombe pamoja na  Tsh 100,000 ,Mshindi wa pili Mairiva club Tsh 75,000 na mshindi wa tatu ni Black Eagle Tsh 50,000. 

Twanga Pepeta kuzindua Albamu ya 13 Mwanza Jumamosi, kuchangia madawati

indexMkurugenzi wa bendi ya African Stars, Asha Baraka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  kuhusiana na uzindua albamu yake ya 13 ijulikanayo kwa jina la (Usiyaogope Maisha) mkoani Mwanza kwenye ukumbi wa Villa Park Jumamosi Mei 28.
……………………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
Bendi ya muziki ya African Stars “Twanga Pepeta” itazindua albamu yake ya 13 ijulikanayo kwa jina la Usiyaogope Maisha mkoani Mwanza kwenye ukumbi wa Villa Park Jumamosi.
Akuzungumza jijini jana, Mkurugenzi wa bendi hiyo, Asha Baraka alisema kuwa maandalizi ya uzinduzi huo yamekwisha kamilika na wanamuziki wake wapo kwenye maandalizi ya mwisho kwa ajili ya uzinduzi huo.
Mbali ya wimbo wa Husiyaogope  Maisha uliotungwa na Ali Choki, nyimbo nyingine zinazounda albamu hiyo ni Ndoa (Luizer Mbutu), Uso Chini, (Choki), Michepuko (Msafiri Diouf), Mapenzi Yanaumiza (Haji Ramadhani) na Ganda la Mua uliotungwa na Saleh Kupaza ambaye kwa sasa hayupo kwenye bendi hiyo.
Asha alisema kuwa wamekwisha rekodi nyimbo zote na mauzo ya CD 1000 ya kwanza, yatatumika kuchangia ununuzi wa madawati mkoani humo. Alisema kila CD itauzwa Sh3, 000 na Sh 1,000 watatumia kununua madawati.
 “Hii ni heshima kwa wapenzi wa muziki wa Mwanza, bendi inafanya uzinduzi wa albamu hii kwa mara ya kwanza mkoani, albamu zote 12 zilizinduliwa  hapa Dar es Salaam, hii ni mara ya kwanza katika historia ya bendi yetu,”
“Tunataka tuwe tofauti, mpango wa kununua madawati pia utafanyika katika uzinduzi wa albamu hiyo kwa mkoa wa Dar es Salaam katika siku itakayopangwa, tumepiga hesabu na kujua dawati moja ni Sh50,000 (kama utatengeneza mwenyewe), “ alisema Asha.
Alisema kuwa albamu hii ni ya aina yake kwani wanamuziki wake wametunga nyimbo ambazo mbali ya kuburudisha, pia zinatoa mafundisho mbalimbali.
Albamu za nyuma ya bendi hiyo ni  Kisa Cha Mpemba, Jirani, Fainali Uzeeni, Chuki Binfasi, Ukubwa Jiwe, Mtu Pesa,  Safari 2005, Password, Mtaa wa Kwanza, Mwana Dar es Salaam, Dunia Daraja na Nyumbani ni Nyumbani.
 Mwisho….
Caption:
Mkurugenzi wa bendi ya African Stars, Asha Baraka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)  kuhusiana na uzindua albamu yake ya 13 ijulikanayo kwa jina la Husiyaogope Maisha mkoani Mwanza kwenye ukumbi wa Villa Park Jumamosi Mei 28.

MAJALIWA AWASILI LUSAKA

MAJA 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Ulinzi wa Zambia, Christopher Mulenga baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Keneth Kaunda uliopo Lusaka  Mei 23, may 2016 ambako leo atamwakilisha Rais John Magufuli kwenye mkutano wa  Benki ya Maendeleo ya Afrika _ADB. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MATUKIO KATIKA PICHA LEO KUTOKA BUNGENI, DODOMA

NG1\
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira ambaye pia ni Mbunge Jimbo la Kisesa, Mhe. Luhaga Joelson Mpina (kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge wa CHADEMA Jimbo la Iringa Mjini, Mhe. Mchungaji Peter Simon Msigwa wakielekea Bungeni kwa ajili ya vikao vya asubuhi ndani ya bunge hilo leo 24 Mei, 2016.
NG2 
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Sospeter Mwijarubi Muhongo akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG3 
Mbunge wa CHADEMA Jimbo la Mikumi, Mhe. Joseph Leonard Haule akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG4 
Naibu Waziri, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Mb), Mhe. Eng. Edwin Amandus Ngonyani (kushoto) akiwa ameongozana na Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Eng. Hamad Yusuf Masauni wakielekea ndani ya Bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016.
NG5Mwenyekiti wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi, Mhe. Andrew John Chenge (kulia) akiwa ameongozana na Mbunge mwenzie wakielkea ndani ya Bunge kwa ajili ya vikao vya asubuhi ndani ya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG6 
Naibu Waziri, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Mbunge Jimbo la Ngorngoro, Mhe. William Tate Ole-Nasha akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG7 
Mbunge wa Viti Maalum CCM, Mhe. Mary Machuche Mwanjelwa akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG8 
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Mhe. Prof. Joyce Lazaro Ndalichako akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
NG9 
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ambaye pia ni Mbunge wa CCM Muleba Kaskazini, Mhe. Charles John Mwijage akiwasili Bungeni kwa jili ya kuhudhuria vikao vya bunge hilo leo 24 Mei, 2016 mjini Dodoma.
PICHA ZOTE NA BENEDICT LIWENGA, MAELEZO, DODOMA.

UPUNGUFU WA WAFANYAKAZI HOSPITALI YA WETE UNAWEZA KULETA ATHARI KWA MAMA WAJAWAZITO

index 
Na Masanja Mabula –Pemba .
UPUNGUFU  wa wafanyakazi   kwenye  wodi ya wazazi katika Hospitali ya Wete unaweza kuleta athari kwa mama wajawazito na wazazi  kutokana na kitendo cha kutumia kitanda kimoja watu wawili .
Hayo yalibanika baada ya Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Omar Khamis Othman kufanya ziara ya kushitukiza katika Hospitali , na kuelezea kusikitishwa na kitendo cha mama wazazi kuchangia kitanda kwa wakati mmoja .
Akizungumzia changamoto hiyo Dk Mbwana Shoka Salim alisema kuwa pamoja na uwepo wa jengo jengine ambalo limejengwa kwa ajili ya wazazi , lakini limeshindwa kutumika kutokana na upungufu wa wafanyakazi .
Awali Mkuu wa Mkoa alitaka ufafanuzi wa mama wazazi kuchangia kitanda kimoja wakiwa wawili , wakati jengo lina nafasi kubwa kutosheleza mahitaji ya mama wanakwenda kujifungua katika hospitali hiyo .
Dk Mbwana alisema , mama mzazi na mtoto  anatakiwa kuwa chini ya uangalizi wakati wote , na kwamba kitendo cha kuhamia jengo jengine itakuwa ni ufumbufu katika kutoa hudumia kwa daktari atakaye kuwa zamu .
“Jengo lipo lakini tatizo ni wafanyakazi , unajua mama mzazi na mtoto anatakiwa kuwa chini ya uangalizi wakati wote , hivyo kuwahamishia jengo jengine itakuwa ni usumbufu katika utojai wa huduma ”alifahamisha.
Naye daktari Bikombo Abdalla alikiri kwamba kitendo cha kuchangia kitanda kimoja wazazi wawili kunahatarisha maisha ya mama na mtoto kwani baadhi yao wamejifungua kwa njia ya upasuaji .
“Ni kweli hali hii inahatarisha maisha ya mama na mtoto kwani baadhi yao wamejifungua kwa njia ya upasuaji , tunaiomba Serikali ya Mkoa kusaidia kupatikana wataalamu wa kutosha ili tuweze kutoa huduma vyema ”alieleza.
Katika nasaha zake , Mkuu wa Mkoa mbali na kusikitishwa na kitendo cha wazazi kuchangia kitanda watu wawili , pia aliwataka  madaktari kutumia lugha nzuri wakati wanapotoa huduma kwa wateja wao .
Alisema , baadhi ya madaktari wanapohudumia wagonjwa hutumia lugha chafu jambo ambalo husababisha lawama kwa Serikali kutokana na kosa la mtu mmoja .
“Tumieni lugha nzuri wakati mnapohudumia wagonjwa , ili kupunguza lawama kutoka kwa wagonjwa pamoja na wananchi wanaoleta wagonjwa wao hospitalini hapa ”alisema Mkuu wa Mkoa .
Hivyo ameahidi kumchukulia hatua za kisheria daktari ambaye atabainika kutumia lugha mbaya na vitisho kwa wagonjwa .

WASHIRIKI WA SHINDANO LA AJIRA YANGU BUSINESS PLAN COMPETITION WAANZA MAFUNZO

1 
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la  Uwezeshaji (NEEC)Bi Beng’i Issa akigungua mafunzo ya washiriki wa shindano la andiko la Biashara la ajira yangu Ajira Yangu Business Plan Competition yaliyoanza jana kwenye ukumbi wa Makumbusho ya Taifa jijini Dar es salaam ambapo vijana 50 wamefanikiwa kuendelea na shindano hilo baada ya mchujo kufanyika na kuwapata hao 50, Mchujo huo utaendelea ili kupata maadiko mengine bora ya kibishara bora 20 na kisha baadaye kupata maandiko bora  10 ambapo washindi hao 10 watapatiwa mitaji kwa ajili ya kundeleza bishara zao na kuanzisha biashara pia.
Katika picha kutoka kulia ni Mwezeshaji Mkuu wa Mafunzo Dkt. ThobiasSwai, Mwakilishi wa ILO Anna Marie Kiaga na kushoto ni mwakilishi  kutoka ILO, Bw. Geras Shirove
2 4Mwakilishi  kutoka ILO, Geras Shirove akizungumza katika wa ufunguzi wa mafunzo hayo kulia ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la  Uwezeshaji (NEEC)Bi Beng’i Issa na kushoto ni Mkurugenzi wa Uwezeshaji Bi Anna Lyimo.
5
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wakiwa kwenye ufunguzi rasmi wa mafunzo yanayofanyika kwenye ukumbi wa Makumbusho ya taifa jijini Dar es salaam.
6 Mkurugenzi wa Uwezeshaji Bi Anna Lyimo akitambulisha wageni mbalimbali waliohudhuria katika mafunzo hayo kabla ya kuyazindua rasmi

 E. African Parliament starts budget session

 
MEMBERS of the East African Legislative Assembly have gathered here for their Sixth Meeting in the Fourth Session of the Third Assembly, which has commenced here yesterday and is expected to climax next month.

This is the regional assembly which is supposed to table the Budget of the East African Community Operations for the fiscal year 2016-2017. It will be the first budget to be calculated with the EAC new member aboard.
South-Sudan joined the community last March making the regional bloc to have six member states, including the founding three - Kenya, Uganda and Tanzania, as well as Rwanda and Burundi who joined later.
The East African Parliament is being presided by the EALA Speaker, Mr Daniel Kidega. The Budget Speech is expected to be delivered next Thursday, by the Chair of the Council of Ministers, Dr Augustine Mahiga.
The Assembly is then expected to debate and approve the Budget as part of its mandate. The Budget Speech is a key activity of the EAC calendar. Last year, EALA debated and approved EAC Budget estimates for the Financial Year 2015/2016 totalling to US $ 110, 660,098.
The 2015/2016 Budget prioritised on the operationalisation of the Single Customs Territory, enhanced implementation of the EAC Common Market Protocol with particular focus on implementation of the new generation EAC internationalised e-Passports and development of the EAC trading, payments and settlement systems.
Debate on the recent State of EAC Address, is also on the menu. On March 8th, 2016, The Tanzanian Prime Minister, Mr Kassim Majaliwa delivered the State of EAC Address to EALA at the 5th Meeting of the 4th Session in Dar es Salaam where he informed the House that progress had been realised following the entry of the Single Customs Territory.
He said that finalisation of key operational instruments, revision of business manuals, development of Monitoring and Evaluation tool framework, deployment of staff and revision of an enforcement framework had opened the path for the operationalisation of the Single Customs Territory in the Partner States. There are also two Bills on the table at the EALA meeting: the EAC Persons with Disabilities (PWD) Bill, 2015 and the EAC Supplementary Appropriation Bill, 2016.
The object of PWD Bill, 2015 is to provide a comprehensive legal framework for the protection of the rights of persons with disability in the Community. The Bill is premised under the provisions of Article 120 (c) of the EAC Treaty under which, Partner States closely co-operate amongst themselves in the field of social welfare with respect to the development and adoption of a common approach towards disadvantaged and marginalised groups.
Such groups include children, the youth, the elderly and persons with disability through rehabilitation and provision of among others, foster homes, health care, education and training. The House is also expected to receive and to debate on a number of Committee reports.
On the other side, its Committees shall hold consultative meetings with the EAC Council of Ministers. The Communications, Trade and Investments Committee has a date with the EAC Council of Ministers to review the EAC Sectional Properties Bill, 2016 and the EA Customs Management (Amendment Act) 2016.
On its part, the General Purpose Committee will consult with the Council on the Supplementary Budget Bill and the PWD Bill respectively, prior to tabling of both Bills in the House

No comments :

Post a Comment