Monday, May 23, 2016

BENKI YA CRDB YAFANYA MKUTANO MKUU WA WANAHISA JIJINI ARUSHA

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Martin Mmari akihutubia mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Benki ya CRDB katika ukumbi wa AICC Arusha. 
 Katibu wa Benki ya CRDB, John Rugambo akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Wanahisa.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akijibu maswali ya wanahisa.
 Manaibu Wakurugenzi Watendaji wa Benki ya CRDB, Esther Kitoka na Saugata Bandyopadhyay wakifurahia jambo wakati wa mkutano huo.
Mwanahisa akiuliza swali.
Wanahisa wakiwa katika mkuano.
Mwenyekiti Abeid Mwasajone akiongoza mkutano wa wanahisa. Katikati ni Katibu wa Benki ya CRDB, John Rugambo na Makamu Mwenyekiti, Steven Mashishanga

TAMASHA LA KUSAKA VIPAJI VYA UTANGAZAJI LA “HHC ALIVE TALENT SEARCH” JIJINI MWANZA LAIBUA VIPAJI VIPYA.

Kushoto ni Meneja wa kituo cha Radio cha 91.9 HHC ALIVE cha Jijini Mwanza, Maganga James Gwensaga, akizungumza katika tamasha la kusaka Vipaji vya Utangazaji (HHC ALIVE TALENT SEARCH 2016) lilizofanyika katika Kanisa la HHC Cathedral, Ilemela Mkoani Mwanza.
 
Watangazaji chipukizi, Hellen Jerome, Ibrahim Mgaya pamoja na Deophinius Salvatory, wameibuka kidedea katika tamasha la kusaka Vipaji vya Utangazaji lililoandaliwa na kituo cha redio cha 91.9 HHC Alive cha Jijini Mwanza.

Mbunge wa Simanjiro amelipotosha bunge juu ya kauli yake ya Tanzanite one

imagesNa Mwandishi Wetu,Dodoma
Uongozi wa Kampuni ya Tanzanite One ya wilayani Simanjiro Mkoani Manyara umesema kuwa Mbunge wa jimbo la Simanjiro ,James Ole Millya amelipotosha bunge na umma kwa ujumla kwa kusema kauli ambazo hakuzifanyia utafiti wa kina.
Millya katika kikao cha Juzi bungeni alisema kuwa kampuni ya Sky Group Associates iliyonunua hisa kwa kampuni ya Tanzanite One na kumiliki kitalu C cha madini ya Tanzanite Mererani wilayani humo hakikufuata taratibu za ununuaji wa hisa hizo na kuwatuhumu baadhi ya Mawaziri kuwa walihusika katika kupindisha taratibu.
Mbali ya hilo Mbunge huyo alienda mbali zaidi na kuituhumu kampuni hiyo kwa kuwafukuza kazi wafanyakazi 201 bila ya kufuata utaratibu na kuwa kampuni ya Tanzanite One inanyanyasa wafanyakazi.
Akizungumza kwa njia ya simu mwanasheria wa kampuni hiyo,Kisaka Mzava alisema uongozi wa Tanmzanite One umesikitishwa na kauli ya Mbunge Millya aliyesomea taaluma ya sheria kwa kusema vitu ambavyo hafanyia utafiti wa kina hatua ambayo uongozi unashaka na taaluma yake kwani vitu kama hivyo hata mtoto mdogo hawezi kusema.
Mzava alisema na kumtaka mbunge huyo kwanza kujilidhisha kwa kufanya utafiti wa kina namna hisa za Tanzanite One zilizouzwa kwa kampuni ya Sky Group inayomilikiwa na wazawa kwa asilimia mia na wamiliki wa hisa wanajulikana na kama anahitaji kujuwa anapaswa kwenda Brella kujilidhisha.
Alisema hakuna Waziri wala kiongozi yoyote mwingine wa serikali anayemiliki hisa katika kampuni hiyo na kulichosemwa na Mbunge Millya kinapaswa kulaaniwa.
Mwansheria huyo alisema Sky Group katika ununuzi wa hisa hizo umeshalipa kodi ya serikali yote bila ya wasiwasi na kampuni hiyo sio kampuni ya mfukoni kama anavyodai kwani mbunge huyo amelipotosha bunge na umma kwa ujumla kwa maslahi yake binafsi.
Mwanasheria huyo alisema shughuli za uzalishaji zinasimamiwa kikamilifu kati ya kampuni ya Sky Group na serikali kupitia Stamico na hakuna madini yanayoibiwa kama Mbunge huyo anavyosema na kama ana ushahidi wa wizi huo anapaswa kuutoa nje ya bunge.
 Alisema hakuna njia ya mkato iliyofanywa katika ununuwaji wa hisa na hakuna Waziri yoyote aliyehusika katika kusaidia kupindisha taratibu kwani kila kitu kipo wazi na alichosema mbunge Millya anapaswa kukitolea ushahidi nje ya bunge na sio ndani ya bunge.
Akizungumzia kufukuzwa kwa wafanyakazi,mwanasheria huyo alisema kuwa wafanyakazi 201 waliofukuzwa kazi ni wafanyakazi hatari kwa mstakabali wa kampuni kwani ni wachochezi,na wenye hila za kutaka kuihujumu kampuni hiyo ili iweze kuleta maafa.
Mwanasheria huyo alisema kugoma ni kosa kisheria kama mgomo hakufuata taratibu sheria lazima zichukue taratibu na ndio uongozi wa Tanzanite One umechukua kwa kuwafukuza kazi wafanyakazi hao 201 walipogoma bila ya kufuata taratibu.
‘’Sheria za kazi ziko wazi kugoma,kuhujumu kampuni na kuchochea wafanyakazi kugoma na kuhujumu kampuni ni kosa kisheria hivyo uongozi wa kampuni haukusita kuwachukulia hatua kwa hilo’’
‘’Wafanyakazi waliofukuzwa kazi walistahili kufukuzwa na kama kampuni ilikiuka taratibu sheria iko na vyombo vya kisheria viko na siasa isiingizwe katika masuala ya kisheria’’
Mwanasheria huyo alisema Waziri wa Nchi,ofisi ya Waziri Mkuu sera,Bunge,kazi ajira vijana na walemavu Jenista Mhagama hana ndugu na mtu anayefanya kazi katika kampuni ya Tanzanite One na kilichosemwa na Mbunge Millya ni kukurupuka na uongo wa kupindukia ambao haukufanyiwa utafiti wa kina.
Mzava alisema Nasibu Mhagama ana mtoto anaitwa Yufuph Mhagama ambaye anafanya kazi Tanzanite One na hawana  uhusiano wowote na Waziri Mhagama na wala hawamujii.
‘’ Yusuph Mhagama ni mtoto wa Nasibu  Mhagama hawana uhusiano wowte na waziri Jenista Mhagama na wala hawamjui’’ Mwanasheria huyo
Kampuni imesikitishwa sana na upotoshwaji ulitolewa ndani ya bunge na mbunge Millya na inashaka na taaluma ya sheria ya mbunge huyo kwani hakufanyia utafiti hoja aliziwasilisha bungeni na kuonekana kutumika kwa maslahi yao watu wengine.

Mkutano Mkuu Wa Mwaka wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya wafanyika Mkoa wa Shinyanga

Hapa ni katika Msikiti wa Masjid Latif Ahmadiyya Muslim Jamaat Nsalala uliopo kijiji cha Nsalala ,kata ya Tinde wilaya ya Shinyanga ambapo leo Jumapili Mei 22,2016 Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Mkoa wa Shinyanga(Ahmadiyya Muslim Jamaat Shinyanga) imefanya mkutano wa Mwaka wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Shinyanga ukiwa na kauli mbiu ya ” Love For All Hatred For None (Mapenzi Kwa Wote Bila Chuki Kwa Yeyote”.
….
Mgeni rasmi alikuwa katibu tawala msaidizi idara ya  uchumi na uzalishaji aliyemwakilisha kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga John Mongella huku waumini wa dini hiyo kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga wakihudhuria mkutano huo.
Mkutano huo uliolenga kuhamasisha amani katika jamii kwa kuwakumbusha waumini kumjua mwenyezi mungu hali itakayosaidia kupunguza hata kumaliza kabisa vitendo vya kihalifu ikiwemo mauaji ya watu wasio na hatia kama vile vikongwe na albino, umehudhuriwa pia na Kiongozi Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry (pichani juu).
Akizungumza katika mkutano huo Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry alieleza kusikitishwa na kitendo cha mauaji ya watu watu msikitini na kuongeza kuwa dini ya kiislam hairuhusu vitendo kama hivyo huku akiviomba vyombo vya dola kufanya uchunguzi ili kubaini wahusika wa kitendo hicho haramu.
Kupitia mkutano huo jamii imeelimishwa juu ya dhana potofu dhidi ya uislamu ambapo baadhi ya watu wamekuwa wakihusisha dini hiyo pamoja na vikundi vya kigaidi mfano wa Boko haram, Isis, Al-shabaab na vingine vingi ambavyo vimekuwa vikidhuru binadamu. 
Mada mbalimbali zimetolewa na viongozi wa jumuiya hiyo ikiwemo nafasi ya dini katika maisha ya binadamu,malezi ya watoto na majukumu ya wazazi sawa na mafundisho ya dini ya kiislamu,umuhimu wa kuwa kiongozi (Khalifa) wa kiroho na barakaza ukhalifa pamoja na masharti ya kujiunga na jumuiya hiyo(masharti 10 ya Baiat na wajibu wa waumini.
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo wakati wa mkutano huo,ametusogezea picha 55 kilichojiri..
Hapa ndipo Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Mkoa wa Shinyanga waumini wa dini ya kiislamu kutoka Jumuiya hiyo kutoka ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga wamejitokeza kwa wingi kusikiliza mawaidha mbalimbali kutoka kwa viongozi wa Jumuiya hiyo pamoja na wageni waalikwa akiwemo kaimu mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mohammed Idd Nchira
Bango likionesha kilichokuwa kinaendelea 
Katibu Mkuu Msaidizi wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya nchini Tanzania Abdulrahman Mohammed Ame akitoa mada kuhusu Haja ya nafasi ya dini katika maisha ya binadamu ambapo alitumia fursa hiyo kuitaka jamii kutenda mambo mema na kujiepusha na vitendo vya kihalifu ikiwemo kuua watu wenye ulemavu wa ngozi na vikongwe.
 
Alisisitiza kuwa uislamu ni dini ya amani hivyo kuwataka binadamu kuishi kwa amani na kwamba kitendo cha kuua mtu mmoja ni sawa na kuua dunia nzima.Hata Hivyo Ame alisema sera ya jumuiya hiyo ni kutochanganya siasa na dini .
Meza kuu,wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya Tanzania Maulana Sheikh Tahir Mahmood Chaudhry,kushoto kwake ni mgeni rasmi Mohammed Idd Nchira,akifuatiwa na rais wa Jumuiya hiyo Kanda ya Ziwa Salim Thani,wa kwanza kushoto ni Naibu rais wa jumuiya hiyo Kanda ya ziwa Yahaya Kamba Ulaya.Wa kwanza kulia ni Mbashiri wa kanda ya ziwa  wa jumuiya hiyo Sheikh Waseem Khan 
Waumini wa dini ya Kiislam kutoka maeneo ya mjini na Vijijini ndani na nje ya mkoa wa Shinyanga waliojitokeza katika mkutano huo
Mgeni rasmi katika mkutano huo Mohammed Idd Nchira akiwahutubia waumini wa dini ya kiislamu wa Jumuiya ya Waislam wa Ahmadiyya.
Continue reading →

AliKiba and Leading TV Cookery Personality

*Music Sensation AliKiba and Leading TV Cookery Personality Marion Elias join the Food Revolution – see them cooking live on Facebook at 4pm local time on Friday 20th May
*9 per cent of boys and 12 per cent of girls under the age of 20 in Tanzania are classed as overweight and obese in 2013.Music Sensation AliKiba and Leading TV Cookery Personality Marion Elias...
Music Sensation AliKiba and Leading TV Cookery Personality Marion Elias…ON Food Revolution Day, Jamie Oliver and numerous famous faces including the campaign’s Global Champions music sensation AliKiba and leading television cookery personality Marion Elias, will be calling for people around the world to sign up to the Food Revolution. Jamie and his army of revolutionaries will be putting pressure on governments at the World Health Assembly meeting in Geneva on 23rd May to tackle the child nutrition crisis.In a move that Jamie Oliver has called a “game-changer”, he and numerous other well-known personalities, will take to Facebook Live on 20thMay for a 7-hour cooking marathon. The aim is to encourage people to join them in a full-scale, global Food Revolution – a major part of which will be giving people power to lobby their own governments to fight diet-related disease. Jamie Oliver says:
“The last 15 years have been tough at times. There were a few of us out there asking questions, wanting answers and making a lot of noise but it often felt like no one was listening. But recently we’ve started making headway, governments are beginning to change policies. This Food Revolution Day we’re going to give governments that extra little nudge by running longest-ever Facebook Live campaign, getting millions of people involved from all around the globe. The World is crying out for action and there has never been a better time to make changes to save millions of lives.”
AliKiba from Tanzania says:
“It’s great to be involved in the Food Revolution this year. It’s particularly important to us here in Tanzania as we are experiencing a child nutrition crisis – on one hand we’ve got millions of kids being severely undernourished, and on the other hand, more and more Tanzanian kids are becoming obese – if we’re going to combat this crisis we have to do it as one.Food Revolution Day 2016 in Tanzania...
Food Revolution Day 2016 in Tanzania Leading Tanzanian TV Cookery Personality Marion Elias says: “I am delighted to be involved in Food Revolution Day, I can’t wait to start cooking some tasty, nutritious food. By having these cooking demonstrations we are doing our part to educate, on a practical level, the people of Tanzania about good nutrition.”
Currently 41 million children under five are overweight while another 159 million are too undernourished to grow properly: we are in the middle of a global health crisis. Food Revolution Day, now in its 5th year, aims to provoke discussion and inspire positive, meaningful change in the way we access, consume and understand food.
Starting in kitchens at home and moving up to the highest levels of business and government, Jamie believes people must work together to empower children with the nutritional knowledge and resources they need to live healthier, happier lives.
Undernutrition is still widespread in Tanzania, obesity is on the rise with 9 per cent of boys and 12 per cent of girls under the age of 20 being classed as overweight and obese in 2013*. The government needs to step up its efforts in tackling the crisis.
That’s why Jamie and AliKiba and Marion Elias want people in Tanzania to join the Food Revolution and ask their government to ensure there is strong Tanzanian leadership at the World Health Assembly meeting on 23rd May where The Minister for Health, Community, Development, Gender, Elderly and Children, Hon. Ummy Ally Mwalimu will represent Tanzania just three days after Food Revolution Day.

No comments :

Post a Comment