Tuesday, April 12, 2016

UJUMBE WA MAWAZIRI NA WAFANYABIASHARA WA CZECH REPUBLIC WAFANYA KONGAMANO LA UWEKEZAJI DAR.


2
Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo na Misitu  wa Serikali ya Czech Republic Bw. Dusan Benza akizungumza katika kongamano la wafanyabiashara wa nchi hiyo na watanzania lililofanyika leo kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
Mawaziri wawili Kilimo na Viwanda wa Jamhuri ya Jamhuri ya Czech  wakiongozana na wafanyabiashara zaidi ya thelathini wako nchini kwa ajili ya kutafuta na kujionea fursa za uwekezaji  nchini Tanzaniam  Mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja na Tanzania Investiment Bank (TIB), Ubalozi wa Szech Republic nchini Kenya na Tanzania House Of Business Company Limited (THB).
Ujumbe huo metembelea wizara ya Kilimo na wizara ya Viwanda na Biashara  na kusaini mikataba ya ushirikiano wa kibiashara na uwekezaji hapa nchini na nchi ya Szech Republic ili kuunganisha masuala ya kibiasha na uwekezaji na kuwezesha wafanyabiashara wa nchi hizi kuwekeza katika masuala ya biashara, Teknolojia  na Kilimo kwa ujumla.

3
Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic hapa nchini  John Chaggama  akizungumza na mmoja wa viongozi wa ujumbe huo huku   Marian Jureck Waziri wa Kilimo wa Czech akisikiliz kwa makini.
4
Injinia Michal Basovnik  wa kampuni ya Impuls  akitoa mada kuhusu shughuli mbalimbali zinazotolewa na kampuni yao ambayo ina tawi pia nchini Zambia.
5 7
Injinia Martin Adamuska  wa kampuni ya NWT kutoka nchini Czech Republic akifafanua jambo wakati alipokuwa akielezea mambo mbalimbali yanayofanya na kampuni yao lakini pia fursa mbalimbali zinazoweza kuwekezwa.
8
Injinia Petr Pawlica wa wa kampuni ya PAWLICA pia ametoa mada katika kongamano hilo na kuelezea teknolojia ya kampuni hiyo katika masuala ya Kilimo.
9
Bw. Godffrey Kirenga wa SAGCOT CENTER LIMITED akiwaelezea wafanya biashara hao juu ya fursa mbalimbali zilizopo hapa nchini katika uwekezaji wa kilimo.
10
 Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza katika kongamano hilo kulia ni  John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania.
11 12
Kutoka kulia ni Mr Charles Chandika Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Tanzania House Of Business Company Limited, Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania, Elipina Makungu na Bahija Salim wakijadiliana jambo wakati wa kongamano hilo la wafanya biashara.
13
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza na Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania  wakimsikiliza mmoja wa maofisa kutoka wizara ya mambo ya nje wakati akizungumza nao.
14
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye na  John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania wakizungumza na Injinia Vladmir Pikora wa benki  ya Czech Export Bank mara baada ya nusu ya kwanza ya majadiliano kati ya wafanya biashara wa Tanzania na Szech Republic katika kongamano lililofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.
15
 John Chaggama Balozi wa Heshima na  Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu ujio wa wafanyabiashara hao.
16
Mkurugenzi mtendaji Mkuu wa Tanzania Private Sector Foundation(TPSF) Godfrey Simbeye akizungumza na waandishi wa habari juu ya umuhimu wa ujio wa wafanyabiashara hao na kongamano hilo kwa wafanyabiashara wa Tanzania ya Czech Republic katika masuala mazima ya kibiashara na uwekezaji.
17
Baadhi ya wafanyabiashara kutoka nchini Czech Republic wakiwa katika kongamano hilo lililofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam
18 19
Baadhi ya wafanyabiashara wa Tanzania wakihudhuria kongamano hilo.
20
Baadhi ya waalikwa kutoka taasisi mbalimbali za Tanzania masuala ya biashara na uwekezaji wakiwa katika kongamano hilo.
21
 John Chaggama Balozi wa Heshima na Mwakilishi wa Ubalozi wa Czech Republic nchini Tanzania akimsikiliza Pan Arnold  Mturi Charge de Affairs at the Szech Consolate  nchini Tanzania.
22
Elipina Makungu na Bahija Salim wakifurahia  jambo wakati wa kongamano hilo la wafanyabiashara wa Czech Republic na Tanzania kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar es salaam.

SENDEKA ATINGA SINGIDA KUPITIA HANANG

 Msemaji wa CCM na Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akisalimiana na baadhi ya viongozi alipowasii Ofisi ya CCM wilaya ya Hanang mkoani  Manyara akiwa njioni kwenda Singida leo
 Katibu wa CCM wilaya ya Hanang, Kajoro Vyohoroka akimpeleka Ofisini, Msemaji wa CCM Ole Sendeka baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya CCM wilaya ya Hanang leo akiwa njiani kwenda Singida
 Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM wilaya ya Hanang mkoani Manyara. Kulia ni Katibu wa CCM  wilaya hiyo, Kajoro Vyohoroka
 Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM wilaya ya Hanang mkoani Manyara. Kulia ni Katibu wa CCM  wilaya hiyo, Kajoro Vyohoroka na kushoto ni Mjumbe wa NEC wa Kigoma, na Ofisa katika Idara ya Itikadi na Uenezi Makao Makuu ya CCM, Kilumbe Ng’enda
 Msemaji wa CCM, Ole Sendeka akisalimiana kwa bashasha na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Manyara, alipowasili kwenye ofisi ya CCM ya wilaya hiyo leo
 Msemaji wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akizungumza na viongozi wa CCM wa Wilaya ya Hanang, alipofika kwenye ofisi hiyo akiwa njiani kwenda Singida leo 
 Msemaji wa CCM na Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akisalimiana na baadhi ya viongozi wa CCM alipowasili leo, Ofisi ya CCM mkoa wa Singia akiwa katika ziara ya kikazi

MAKABIDHIANO YA WAZIRI OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI

ofi1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi (Gavu) akikabidhiana Ofisi na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi IkuluMjini Zanzibar baada ya uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawazi wapya kwa Wizara mbali mbali za Serikali.[Picha na Ikulu.]
ofi2
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini akitoa shukurani kwa wafanyakazi wakati wa kukabidhi Ofisi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi (Gavu) katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu  Mjini Zanzibar baada ya uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya kwa Wizara mbali mbali za Serikali.[Picha na Ikulu.]
ofi3
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini akitoa shukurani kwa wafanyakazi wakati wa kukabidhi Ofisi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi (Gavu) (katikati) katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu  Mjini Zanzibar baada ya uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya kwa Wizara mbali mbali za Serikali.[Picha na Ikulu.]
ofi4
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa haji Ussi (Gavu) akitoa nasaha zake kwa Wafanyakazi wakati wa makabidhiano ya Ofisi na aliyekuwa Waziri ya Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini leo katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu  Mjini Zanzibar baada ya uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya kwa Wizara mbali mbali za Serikali,[Picha na Ikulu.]
ofi5
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi (Gavu) na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini (katikati) wakiombewa dua baada ya makabidhiano ya Ofisi katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu  Mjini Zanzibar baada ya uteuzi wa Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya kwa Wizara mbali mbali za Serikali.[Picha na Ikulu.]
ofi6
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe,Issa Haji Ussi (Gavu) na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini (katikati) wakipeana na Makatibu (kulia) Katibu Mkuu Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Salum Maulid Salum na Katibu wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Haroub Shaibu Mussa kwa kuwatakia Kheri na mafanikio  baada ya makabidhiano ya Ofisi katika ukumbi wa Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu  Mjini Zanzibar,[Picha na Ikulu.]

ZIARA YA SENDEKA BABATI MJINI

Msemaji wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christipher Ole Sendeka akisalimiana na Katibu wa CCM wilaya ya Babati mjini, Benard Ghati alipowasili Ofisi ya CCM wilaya ya Babati mkoani Manyara akiwa katika ziara ya kikazi
Viongozi wa CCM wilaya ya Babati mkoani Manyara wakiwa tayari kumpokea Msemaji wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka alipowasili Ofisi ya CCM wilaya ya Babati
Msemaji wa CCM, Mjmbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni katika Ofisi ya CCM wilaya ya Babati mkoani Manyara
Katibu Mwenezi wilaya ya Babati mjini Reginard Sanga akizungumza maneno ya utangulizi kumkaribisha Msemaji wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka alipofika katika Ofisi ya Wilaya hiyo
Katibu wa CCM, Babati Mjini Bernard Ghaty akizungumza, Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka alipofika katika Ofisi ya CCM wilaya ya Babati mjini mkoani Manyara
Katibu wa CCM mkoa wa Manyara, Ndengaso Ndakubali akimkariisha kuzungumza Msemaji wa CCM, Ole  Sendeka.
Mjumbe wa NEC Kigoma, Kilumbe N’genda akizungumza kabla ya Msemaji wa CCM aliyefuatana naye, Ole Sendeka hajazungumza
Msemaji wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akizungumza na wajumbe wa Sekretarieti wa CCM Wilaya ya Babati mkoani Manyara

Wahandisi Temesa wapigwa msasa

R1 
kaimu Mtendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme(TEMESA) Mhandisi Manase
Ole Kujan (wa pili kushoto) akipata maelekeo juu ya ufungaji wa moja ya
mtambo wa umeme wa nishati ya jua (Solar) kutoka kwa Mhandisi Zuhura
Semboji mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya wiki mbili kwa wahandisi na
mafundi wa Temesa.
R2 
kaimu Mtendaji wa Wakala wa Ufundi na Umeme(TEMESA) Mhandisi Manase
Ole Kujan(katikati) akiangalia moja ya kifaa cha kupimia umeme
kinachotumika katika mafunzo kwa wahandisi na mafundi wa Temesa
yaliyofunguliwa leo.
R3 
Mhandisi Amani Mwanga akitoa maelekezo ya namna ya kufunga moja ya
mitambo ya umeme wa nishati ya jua (Solar) Katika mafunzo ya  wahandisi na
mafundi wa Temesa yaliyofunguliwa leo.
R4 
Baadhi ya wahandisi kutoka Temesa wakiwa katika harakati za kuchuna
na kuunga nyaja katika moja ya mitambo ya umeme wa nishati ya jua (Solar)
Katika mafunzo ya  wahandisi na mafundi wa Temesa yaliyofunguliwa leo.
R5 
Fundi Sanifu kutoka Temesa Mganza Juma (Katikati)akiwa makini kufunga
moja ya mtambo wa umeme wa nishati ya jua (Solar) Katika mafunzo ya  wahandisi
na mafundi wa Temesa yaliyofunguliwa leo.
……………………………………………………………………
Na  Raymond Mushumbusi MAELEZO
Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) ikishirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam wanaendesha mafunzo ya wiki mbili kwa Wahandisi na mafundi wa Temesa
ili kuwajengea uwezo katika kutumia teknolojia ya umeme wa nishati ya jua.
Akifungua mafunzo hayo leo Jijini Dar es Salaam Kaimu Mtendaji Mkuu TEMESA
Mhandisi Manase Ole Kujan amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwaongezea
uwezo wahandisi na mafundi ili kuweza kutumia teknolojia ya umeme wa
nishati ya jua ambao umekuwa na tija kubwa hasa kwa sehemu ambazo umeme wa
kawaida haujafika.
“Nishati ya umeme wa jua imeshika kasi kwa sasa na inatumiwa sana katika
maeneo ambayo umeme wa kawaida haujafika hivyo basi kwa mafunzo haya
wahandisi na mafundi wetu wataweza kushirikiana na wadau mbalimbali katika

RAIS DKT. MAGUFULI ASHIRIKI KUAGA MWILI WA MAREHEMU CHRISTINA LISSU MUGHWAI KATIKA UKUMBI WA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM

P1 
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha Maombolezo kufatia kifo cha Mbunge wa zamani wa Viti Maalum Chadema Christina Lissu Mughwai aliyefariki Aprili 7 mwaka huu.
P5 
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akiaga mwili wa marehemu Christina Lissu Mughwai aliyewahi kuwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Chadema katika ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
J4 J2 
Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji Mwanasheria Tundu Lissu (Mb) kufatia kifo cha mdogo wake Christina Lissu Mughwai aliyefariki Aprili 7 mwaka huu.
J3Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimpa pole Mwanasheria Tundu Lissu (Mb) kufatia kifo cha mdogo wake Christina Lissu Mughwai aliyefariki Aprili 7 mwaka huu.
PICHA NA IKULU

Wizara YA KILIMO yakanusha kodi ya ng’ombe

image.php 
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
……………………………………………
Wizara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi imekanusha kodi ya ng’ombe iliyoripotiwa na Umoja wa wafanyabiashara wa Mifugo na Mazao yake wa Wilaya ya Kinondoni.
Taarifa hii imetolewa na Katibu Mkuu (Mifugo) wa Wizara hiyo Dkt. Mary Mashingo baada ya kuyaona malalamiko ya wafanyabiashara hao kwenye baadhi ya vyombo vya habari nchini.
Katika taarifa hiyo wizara imekanusha kuwa kodi ya ng’ombe siyo shilingi 18,500 kama ilivyoripotiwa na wafanyabiashara hao bali ni shilingi 12,000 ambayo inatambulika kisheria.
“Wizara yetu inapenda kutoa ufafanuzi juu ya kodi inayotozwa katika machinjio ya Kimara kama ifuatavyo: ushuru wa soko shilingi 5000, ushuru wa kusafirisha mifugo shilingi 1500, ushuru wa ukaguzi wa wanyama shilingi 2500 pamoja na gharama za machinjio shilingi 3000 kwa kila  kichwa cha ng’ombe ambapo jumla yake ni shilingi 12,000”alisema Dkt.Mashingo.
Aidha,taarifa  hiyo imeelezea kuhusu kupitisha ng’ombe katika soko la upili la Pugu kabla ya kuwapeleka katika machinjio ya Kimara kuwa ni kwa ajili ya kuwafanyia vipimo vya afya ng’ombe hao kabla ya kuchinjwa pamoja na kulipia tozo ya Serikali.
Taarifa hiyo pia imefafanua baadhi ya sababu za kufungwa kwa machinjio ya Kimara tangu Aprili 9 mwaka huu zikiwemo za baadhi ya wafanyabiashara kupeleka ng’ombe katika machinjio hayo moja kwa moja bila kupitia Pugu ambalo ni kosa kisheria pamoja na uchafu uliokithiri katika machinjio hayo.
Katika kufanya juhudi za kupambana na matatizo haya,Wizara  ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi inajipanga kukutana na wafanyabiashara wa mifugo na mazao yake ili kuwaelimisha zaidi kuhusu Sheria, Kanuni, na Taratibu zinazopaswa kufuatwa katika ufanyaji wa biashara hii.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AZINDUA KONGAMANO LA WANAWAKE KATIKA UONGOZI

c1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mhe. Zakia Meghji alipowasili ukumbi wa Mwalimu Nyerere kwa ajili ya kuzindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016.
C2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.
C3 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katikati akiwa katika picha ya pamoja na Wanawake waliohudhuria Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.
C4 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Waandishi wa Vyombo vya Habari baada ya kuzindua Kongamano la Wanawake katika Uongozi linalojadili kuendeleza Mazingira kuwezesha kuinua Wanawake ambao bado hawajapata fursa kufikia nafasi za Uongozi. Kongamano hilo lililoandaliwa na Taasisi ya Uongozi limefanyika leo April 12, 2016 katika ukumbi wa Mwalim Nyerere.
(Picha na OMR)

FAO JIPYA LA WOTE SCHEME LA PPF LITASAIDIA KUKUZA UCHUMI WA WATANZANIA

 Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya Kinondoni,Pwani na Tanga,Zahra Kayugwa akizungumza wakati wa semina hiyo.
Fao jipya la Wote Scheme ambalo ni mfumo wa hiari kwa wanachama ulioanzishwa na Mfuko wa Pensheni wa PPF utasaidia kuwapa fursa watanzania waliopo kwenye sekta isiyo rasmi kukidhi mahitaji na kutambua mchango na ushiriki wa sekta hizo katika kukuza uchumi.
Fao hilo pia linatoa fursa kwa wafanyakazi waliopo kwenye sekta iliyo rasmi kuwawezesha kunufaika na mfumo huo kwa ajili ya kukuza shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.
Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya Kinondoni,Pwani na Tanga,Zahra Kayugwa alisema hayo juzi wakati semina kwa askari wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Zimamoto mkoani Tanga uliokuwa na lengo la kuwapa uelewa juu ya mafao yanayopatikana kupitia mfuko huo.
 Washiriki wa semina
hiyo
Meneja wa Mfuko wa PPF Kanda ya
Kinondoni,Pwani na Tanga,Zahra Kayugwa
Alisema kupitia fao hilo
mwanachama
anafaidika na huduma za Afya ikiwemo kupata kadi ya Afya mahali popote kwa
kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini (NHIF) mwaka
mzima bure.
Aidha alisema kupitia skimu hiyo mpya ya mfuko huo unachangia na kuwapa uelewa watanzania utamaduni wa kujiwekea
akiba ya baadae ili kuweza kukabiliana na ugumu wa maisha wakati
wanapokuwa wakifikia
umri wa kustaafu.
 “Lakini pia sisi kama PPF
tunarahisisha
uchangiaji kupitia mitandao yote ya simu kwani hii imesaidia kuweza kuepusha
changamoto mbalimbali ambazo wanaweza wakukumbana nazo wanachama wetu ambao
wamejiunga ma Mfuko huu “Alisema.
Hata hivyo alisema kuwa
wanaendelea
kutoa mikopo ya elimu na biashara ili kuweza kuwainua wanachama wao kiuchumi
sambamba na kujiendeleza kielimu ili waweze kukabiliana na changamoto za maisha
na utandawazi.
 
 “Fao hili lilianzishwa mwezi wa saba mwaka jana ambapo mwanachama
anafaidika na huduma za afya (Kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya nchini
NHIF)
,mikopo mbalimbali
na Fao la Uzeeni(Pensheni) Alisema Meneja huyo.
Semina hiyo ililenga kuwapa
uelewa wa mambo mbalimbali kuhusu mfuko
huo ikiwemo uandikishaji wanachama,mafao yatolewayo na mfuko huo,Wote
Scheme (mfumo
wa Hiari),Mikopo ya Saccos na Fao la Elimu.
Picha na Stori kwa Hisani ya blog ya Kijamii ya Tanga Raha

Waziri Makamba akutana na Ujumbe wa Kamati ya Fedha ya Bunge la Finland

indexTTWaziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais ( Muungano na Mazingira) January Makamba akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe wa Wabunge la Finland. Wabunge hao wa Kamati ya Fedha wamefanya mazungumzo na Waziri Makamba hii leo Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli, Jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………….
Na Mwandishi wetu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) January Makamba hii leo amekutana na kufanya mazungumzo na Ujumbe wa Kamati ya Fedha ya Bunge la Finland.
Katika mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ofisi ya Makamu wa Rais, Luthuli Dar es Salaam, wabunge hao wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada inazofanya za kulinda na kuhifadhi mazingira.
Awali, akiwakaribisha wabunge hao Waziri Makamba amesema Tanzania inajivunia uhusiano mzuri uliopo baina ya Tanzania na Finland na kuwashukuru  wabunge hao kwa kufanya ziara hiyo ya kikazi nchini Tanzania.
Waziri Makamba amesema Serikali ya awamu ya Tano imejikita zaidi katika kuimarisha Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira ikiwa ni pamoja na kuandaa Mkakati Mkubwa wa Kitaifa wa kupanda miti nchi nzima hususan maeneo kame ili kunusuru nchi na athari za mabadiliko ya Tabianchi.
“Hivi sasa tuko katika hatua za kuainisha maeneo yatakayopandwa miti hiyo kwa kuangalia aina za udongo na miti itakayoweza kuhimili katika maeneo husika” Alisisitiza Makamba.
Waziri Makamba ameiomba Serikali ya Finland kuendelea kushirikiana zaidi na Serikali ya Tanzania ili kufikia malengo endelevu ya Uchumi na maendeleo ya Viwanda bila kuathiri Mazingira.
Naye Balozi wa Finland Nchini Tanzania Bw Mart Akhtsary aliyeambatana na ujumbe wa wabunge kutoka Finland amemhakikishia Waziri Makamba kuendeleza na kudumisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

WASHTAKIWA WA TUMBILI WASOTEA DHAMANA.

Baadhi ya Washtakiwa katika kesi ya uhujumu uchumi ya usafirishaji wa
wanyama Hai 61 aina ya Tumbili wakiongozwa na asakari Polisi walipokuwa
wakiwasili katika mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Moshi.Washtakiwa katika kesi ya kusafirisha Tumbili raia wa Uholanzi ,Artem
Vardanian na ndugu yake Eduard Vardanyan wakisindikizwa na askari Polisi
kuingia mahakamani,Nyuma yao ni mshtakiwa mwingine Idd Misanya
Washtakiwa katika kesi ya kusafirisha Tumbili raia wa Uholanzi ,Artem
Vardanian na ndugu yake Eduard Vardanyan wakiwa katika viunga vya mahakama kuu kanda ya Moshi ,kulia ni aliyekua Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori Dkt Charles Mulokozi.
Washtakiwa katika kesi ya kusafirisha Tumbili wakiwa katika mahabusu ya
mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, kutoka kulia ni Eduard Vardanyan ,ArtemVardanian na Idd Misanya.
Watuhumiwa katika kesi ya kusafirisha Tumbili wakiwa katika mahabusu ya
mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Moshi, wakizungumza jambo na wakili
Majura Magafu anyewatetea katika shauri hilo.kutoka kulia aliyeshika
nondo ni aliyekua Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Wanamapori Dkt Charles
Mulokozi, mfanyabiashara raia wa Uholanzi Artem Vardanian na ndugu yake
Eduard Vadanyan.

KAMPUNI YA TRICSTER YAANDAA SHINDANO LA WAZO LA BIASHARA

_MG_5119Na Lorietha Laurence-Maelezo
………………………….
Kampuni ya Kijapani inayofanya shughuli zake nchini (Tricster)  imeandaa shindano la wazo la biashara  litakalozishirikisha  nchi tano  za Afrika zikiwemo Kenya,Rwanda,Zambia,Zimbabwe na Tanzania mwenyeji wa  mashindano hayo kwa mwaka 2016.
Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam Meneja Mradi kutoka kampuni ya Afrika New Business Development Department(DMM)  Bw.Alex Kapungu ambao ndio  wadhamini wa shindano hilo ameeleza kuwa lengo la shindano hilo ni  kusaidia kuboresha ujasiriamali katika bara la Afrika.
“Shindano hili linafanyika kwa mara ya kwanza na hivyo ni fursa nzuri kwa wajasiriamali na wale wanaotaka kuwa wajasiriamali kushiriki na baadaye kufanikisha wazo hilo kiutendaji kwa kuwa biashara halisi”alisema Bw.Alex.
Aidha ameongeza kuwa vigezo vya kushiriki shindano hilo ni mshiriki awe amefikisha miaka 18 na kuendelea, awe anajua kuongea na kuandika lugha ya kiingereza na kuwa na hati ya kusafiria.
Naye Mkurugenzi wa Trickster Bw.Sonobe Atsushi amesema washindi watakaoingia nusu fainali watapata fursa  ya kutembelea nchi ya japani ambapo mshindi wa kwanza atapata fedha taslimu  Dola elfu tano za kimarekani.
Pia ametoa wito kwa watanzania kujitokeza na kushiriki kwa wingi ili wapate fursa ya kuanzisha biashara kupitia mawazo watakayoyatoa na hivyo kupanua wigo wa biashara.

fastjet yashinda kwenye Tuzo Za Usafiri Duniani

TAARIFA KWA NYOMBO VYA HABARI
…………………………………
Dar es Salaam – 11 April 2016 –fastjet, shirika la  ndege la gharama nafuu barani Afrika imeshinda Tuzo ya Shirika la Ndege Linaloongoza Afrika kwa Gharama Nafuu kwenye Tuzo ya  23 ya Mwaka  ya  Usafiri Duniani iliyotolewa Zanzibar, Tanzania  Aprili 9, 2016.
Tuzo ya Usafiri ambayo inatambulika  duniani  imepangwa kwa kutambua, kutuza na kusherehekea  mafanikio kwenye  sekta zote muhimu  za usafirishaji  wa kwenye sekta ya utalii.
 Tuzo ya Shirika la Ndege Linaloongoza kwa Gharama Nafuu  ambayo hutolewa kwa wataalamu wa  usafiri na utalii pamoja an watumiaji duniani kote  inatokana na kutambua  huduma za fastjet za kufanya watu wamuumudu usafiri wa anga, usalama na kuaminika  kwenye mtandao yote barani Afrika.
“Kutambuliwa na kupata tuzo hii sio tu kunaonesha  kujituma kwa ufanisi kwenye usafiri wa anga, lakini kunaonesha matokeo ya juhudi zetu  tunazojaribu kulifanyia bara la Afrika,” alisema Meneja Mkuu wa fastjet Tanzania,  John Corse na kuongeza, “tunajivunia sana  kupokea kutambuliwa huko na sekta hii kubwa  na fastjet itaendelea  kuufanya usafiri wa anga  kuwa wa gharama za chini ambazo watu wengi watazimudu  barani Afrika.”
Shirika hilo la ndege la bei nafuu  lilizinduliwa  Novemba 2012 na linafanya safari kadhaa za ndani ya Tanzania  kutoka Dar es salaam kwenda Mbeya, Mwanza na Kilimanjaro. Kukua kwa mtandao wa fastjet  pia kunatoa huduma  kwa njia ya kutoka Dar es Salaam na Zanzibar na kwenye vituo vya kimataifa  kama vile Johannesburg, Harare, Victoria falls, Entebbe, Nairobi na Lusaka.
Fastjet inatarajia  abiria wake wengi kwenye njia hizo inakotoa huduma  kuwa ndio wanasafiri kwa mara ya kwanza kwa kutumia ndege  kutokana na sababu ya kukwazwa na tozo za nauli ya juu  ambazo awali  hawakumudu kulipa kwa ajili ya usafiri huo.
Huduma hii ya nauli nafuu imeungwa mkono kwenye utafiti uliofanywa na shirika hilo hivi karibuni, unaoonesha kuwa asilimia 40 ya abiria  kwenye njia zote walikuwa ndio mara yao ya kwanza kusafiri kiumudu kusafiri kwa ndege  kwa mara ya kwanza  hivyo pongezi ziende kwa gharama nafuu za fastjet.
Jambo jingine ambalo linapatikana kwenye  njia inamopita fastjet ni kuboreshwa kwa mbadala wa mzigo  ambako kunajulikana kama ‘freighty’ kunakoruhusu abiria  kusafirisha  hadi kilo 80 zilizofungwa kwenye mabegi kwa  gharama ya shillingi 88,000. Mbadala huo wa kusafirisha mizigo kimsingi umekuwa ni maarufu kwa wafanya biashara wanaosafiri na fastjet  kwenda kununua bidhaa za jumla kimataifa na kuzisafirisha kwa ajili ya kuziuza  kwenye masoko ya  nyumbani mwao.
 Tuzo hii inaongeza  idadi ya tuzo  ambazo fastjet imeshazipata  zikiwemo kushinda Tuzo ya Ubunifu kwenye Usafiri kwenye utoaji wa nane wa tuzo hiyo mwaka 2015, na hali kadhalika  kutangazwa kuwa  shirika la ghama  nafuu barani Afrika katika kulinganishwa  mengine kwenye usafiri wa anga kupitia mtandao wa safiri  WhichAirline.com in 2016.

Waandishi wa habari waaswa kujiendeleza kuelimu

SONY DSC 
Na Beatrice Lyimo – MAELEZO
…………………………………………
Waandishi wa habari waaswa kujiendeleza kielimu katika fani ya uandishi wa habari na taaluma nyingine ili waweze kukabiliana na kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.
Wito huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mhadhiri Chuo Kikuu Huria Dr. Hamza Kondo alipokuwa akizindua kitabu chake kiitwacho Watchdog Journalism in Tanzania a Sustainable Struggle ambapo kwa Kiswahili ni “Uandishi Habari Huru Tanzania ni mapambano endelevu”.
Dr Kondo amesema lengo la kitabu hicho ni kuwaelimisha na kuwaasa waandishi wa habari na wataaluma ya habari kuzidi kuithamini taaluma hiyo licha ya changamoto zinazowakabili.
Amesema kitabu hicho kinazungumzia uhalisia wa uhuru wa habari nchini, hivyo kinafaa kufundishia taaluma ya habari katika vyuo vikuu na vyuo vya kati nchini.
Aidha, Mhadhiri huyo ameongeza kuwa ili fani ya taaluma ya habari iheshimike ni lazima iwe na bodi ya wataalamu waliobobea ambayo itaundwa na wasomi wa taaluma husika ili kusimamia maadili ya taaluma hiyo na kuchukua hatua kwa wanataaluma watakaokiuka maadili.
Mbali na hayo Dr Kondo ametoa zawadi ya vitabu kwa baadhi ya vyombo vya habari nchini likiwemo gazeti la Jamuhuri, gazeti la majira, gazeti la Habari Leo, gazeti la Mwananchi na gazeti la Nipashe.

mhe. January Makamba akutana na balozi wa Ireland Bi. Fionnuala Gilsenan

index
index 
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais- Muungano na Mazingira Mh. January Makamba akiwa na balozi wa Ireland Bi. Fionnuala Gilsenan aliyemtembelea Ofisini kwake leo mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam.

LANCET TANZANIA LIMITED YAFUNGUA MAABARA YA KISASA MJINI MOSHI.

Maabara ya kisasa ya Lancet  iliyofunguliwa mjini Moshi jirani na YMCA kwa ajili ya kufanya vipimo vya magonjwa mbalimbali ikiwemo magonjwa ya Saratani.
Mtafiti wa Magonjwa,Dkt Hemed Kalebu akimuonesha Kaimu mganga mkuu wa mkoa ,Dkt Japhet Boniface ,maeneo mbalimbali alipotembelea maabara hiyo iliyofunguliwa mjini Moshi.
Dkt Kalebu akileza jambo kwa kaimu mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro,Dkt Josephat Boniface katika eneo ambalo hutumika kumpokea mgonjwa anayefika kwa ajili ya kufanyiwa vipimo.
Dkt Kalebu akionesha sehemu ya vifaa mbalimbali katika maabara hiyo ambavyo vimekuwa vikitumika kwa ajili ya kufanya vipimo.
Baadhi ya vifaa mbalimbali vilivyoko katika maabara hiyo ya kisasa iliyofunguliwa mjini Moshi itakayotumika kufanya vipimo vya magonjwa mbalimbali ambayo baadhi ya wagonjwa wamekuwa wakivifuata nje ya nchi.
Kaimu Mganga mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro ,Dkt Josephat Boniface akiwa katika picha ya pamoja na Dkt Hemed Kalebu pamoja na watumishi wengine wa maabara hiyo .
 
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

TANZANIA OMAN BUSINESS FORUM TO BE HELD ON 13TH APRIL, 2016 AT HYATT REGENCY KILIMANJARO HOTEL, DAR ES SALAAM

New Picture NEMBO YA TAIFA 
On the occasion of the state visit by the Minister for Industry and Trade of Oman Dr. Ali Masoud Al Sunaid, the Ministry of Foreign Affairs Regional and International Corporation and the Ministry of Industry, Trade and Investment with corroboration with Tanzania Chambers of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) are co-organizing a business forum which will take place on Wednesday, 13th April, 2016 starting from 9:00 AM at Hyatt Regency Kilimanjaro Hotel.
The objective of the forum is to create a convenient platform for Tanzanian business community to meet, share experiences and establish business relations with the Oman business community. The forum will be graced by Her Excellence Samia Suluhu Hassan the Vice President of United Republic of Tanzania and Dr. Ali Masoud Al Sunaid Minister for Industry and Trade of Oman.
The Forum will also provide the opportunity for business to business (B2B) meetings between the Oman businessmen and  their Tanzanian counterparts in various sectors such as; Banking &  Finance, Oil  & Gas, Construction & Real Estates, Posts & Telecommunications, Information Technology, Electrical & Electronics, Furniture, Tourism, :Agriculture& Agro Processing, Food & Beverages, Pharmaceuticals, Textiles, Footwear and General Trading.
As we value your participation in the growth of trade and investment in Tanzania, we feel honoured to extend this invitation to you and we hope you will reserve a place to exchange useful information to participants during the B2B Meetings Session.
You are kindly requested to confirm your participation to TCCIA via; Fatma Hamisi (fhamisi@tccia.com ) or to Mr. James W. Kyejo (james.kyejo@mit.go.tz, +255 675 417 813)


No comments :

Post a Comment