Tuesday, April 19, 2016

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA RASMI DARAJA LA KIGAMBONI, ALIBATIZA JINA LA DARAJA LA NYERERE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli akikata utepe huku viongozi wengine wakiushikilia kuashiria uzinduzi rasmi wa Daraja la Kigamboni katika wilaya mpya ya Kigamboni jijini Dar es salaam leo Aprili 19, 2016

MLIPUKO KATIKA JIJI LA KABUL WASABABISHA VIFO VYA WATU KADHAA

MTOTO MCHANGA AFARIKI DUNIA AKIWA ANGANI KWENYE NDEGE

OSCAR DE LA HOYA AMPATIA USHAURI BONDIA AMIR KHAN

Bondia Oscar De La Hoya amemshauri bondia Amir Khan kutumia kasi yake ya kurusha masumbwi ili kumshinda kirahisi Canelo' Alvarez

Amir Khan amekuwa akijifua vikali kujiandaa na pambano hilo litakalofanyika Jijini Las Vegas Marekani mwezi Mei mwaka huu.
                           Amir Khan akijifua katika kambi yake kujiandaa na pambano 
                               Amir Khan akifanya mazoezi huku akijiangalia kwenye kioo

VIJANA WA CHELSEA WATWAA TENA UBINGWA WA UEFA

VICHAKA HATARISHI KATIKA KITUO CHA AFYA BUZURUGA JIJINI MWANZA VYAFYEKWA.

RAIS MAGUFULI ATUMBUA JIPU LINGINE, AMSIMAMISHA KAZI MKURUGENZI WA JIJI LA DAR ES SALAAM

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ametangaza kumsimamisha kazi kuanzia leo Mkurugenzi wa jiji la Dar es Salaam, Wilson Kabwe kutokana na kuingia mikataba tata ambayo imeisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 3. 

Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo wakati akilizindua daraja la Kigamboni ambalo amependekeza liitwe daraja la Nyerere. 

Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. Paul Makonda kuweka hadharani mikataba mibovu iliyoingiwa na Mkurugenzi huyo

SERIKALI KUCHUNGUZA MKATABA WA JENGO LA MACHINGA COMPLEX

 Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Paul Makonda (kulia), akikagua vizimba katika Jengo la Machinga Complex Dar es Salaam jana, baada ya kufanyika kikao cha kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kilichoketi jana kujadili uendeshaji wa biashara wa katika jengo hilo pamoja na kamati ya mkoa iliyoundwa kuchunguza mkataba wa jengo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaa, Paul Makonda akizungumza na wafanyabiashara katika Jengo la Machinga Complex Dar es Salaam jana, kuhusu uendeshaji wa jengo hilo.
Makonda akiwasili katika viwanja vya Jengo la Machinga Complex kuzungumza na wafanyabiashara na wadau wengine. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Raymond Mushi wengine ni viongozi wa jengo hilo.
       Makonda akiangalia Uwanja wa Karume akiwa jengo la Machinga Complex.

KILA LA KHERI AZAM, YANGA

UCHUKUZI WAENDELEA KUJIFUA KWA KASI

Hawa Senkondo (mbele) akikiongoza kikosi cha wanawake cha kuvuta kamba cha Uchukuzi SC katika mazoezi. Wengine ni Germana Vicent, Janeth Komba na Tatu Cosmas


Kocha Abuno Issa (kustoto) akitoa maelekezo kwa timu ya wanawake ya Uchukuzi SC.
Kocha Abuno Issa (kulia) akitoa maelekezo kwa timu ya wanaume ya Uchukuzi SC.
Sharifa Mustafa (mwenye mpira) akiangalia wa kumrushia wakati (katikati) Mayasa Hamidu akitazama.

MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR BALOZI SEIF AWATEMBELEA WAATHIRIWA WA MAFURIKO WALIOPO KATIKA KAMBI MAALUM YA SEKONDARI YA NYERERE

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na wananchi waliopata majanga ya kuingiliwa na maji katika nyumba zao wakati alipotembelea kambi maalum iliowekwa katika Skuli ya Sekondari ya Nyerere, alipofika kuwafariji na kuwapa pole na mtihani huo.
Baadhi ya Wananchi wa maeneo ya Nyerere, Kwahani Kwa Wazee na Sebleni wakiwa katika Kambi maalum ilioandaliwa kwa Wananchi waliopata maafa ya kuingiliwa na Maji Nyumba zao wakati wa mvua ilionyesha juzi jumapili katika maeneo ya Visiwa vya Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiwafariji Wananchi waliopata maafa ya mvua katika baadhi ya maeneo ya Visiwa vya Unguja, Katika Kituo hicho kuna Wananchi zaidi ya mia nne waliopata maafa hayo wakiishi kwa muda katika kituo hicho.

No comments :

Post a Comment