Waziri
wa Fedha Dkt.Philip Mpango akizungumza na wadau (hawapo
pichani) wakati wa ufunguzi wa Kongamano la uwajibikaji katika sekta ya
Mafuta na Gesi lililoandaliwa na taasisi ya WAJIBU – Institute of Public
Accountability leo Aprili 11,2016 jijini Dar es Salaam.
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt.Philip Mpango (kulia) akikata utepe kuashiria
ufunguzi rasmi wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public
Accountability na (kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo
Bw.Ludovick Utouh,sherehe hizo zimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wadau waliyoshiriki Kongamano linahusu Uwajibikaji katika sekta ya
Gesi na Mafuta wakifuatilia mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Mkurugenzi
wa Taasisi ya TWAWEZA Bw.Aidan Eyakuze (hayupo pichani) wakati wa
ufunguzi wa kongamano hilo lililofanyika leo jijini Dar es Salaam
Waziri
wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa
Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability Bw.Ludovick
Utouh wakiwa wanaonesha kibao kinacho onyesha ufunguzi rasmi wa taasisi
hiyo leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango (wanne kushoto)akiwa
katika picha ya pamoja na wadau waliyoshiriki Kongamano la Uwajibikaji
katika sekta ya Mafuta na Gesi,(watatu kulia ni)aliyekuwa Katibu Mkuu
Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na (watatu kushoto) ni Mkurugenzi Mtendaji
wa Taasisi ya WAJIBU – Institute of Public Accountability Bw.Ludovick
Utouh.
Picha na Anitha Jonas – MAELEZO.
Mhe. Kairuki afungua Mafunzo JUU YA Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS) Dodoma
Waziri
wa Nchi,Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki
(Mb) akifungua Mafunzo juu ya Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi
na Mishahara (HCMIS) kwa Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Mamlaka za
Serikali za Mitaa Tanzania yaliyofanyika mjini Dodoma.
Katibu
Mkuu Utumishi Dkt. Laurean Ndumbaro akizungumza wakati wa Mafunzo
kuhusu Mfumo Shirikishi wa Taarifa za Kiutumishi na Mishahara (HCMIS)
kwa Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa
Tanzania yaliyofanyika mjini Dodoma.
Mmoja
wa washiriki wa Mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya
Manispaa ya Tabora Bibi. Sipora J. Liana akiuliza swali wakati wa
mafunzo yaliyofanyika mjini Dodoma.
Mkutano ukiendelea
KAMATI YA BUNGE YA VIWANDA YAKUTANA NA WAZIRI WA MUUNGANO NA MAZINGIRA
Waziri
wa nchi Ofis ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh.January
Makamba akielezea jambo kwa wajumbe wa Kamati ya bunge ya
Viwanda,Biashara na Mazingira wakati Wakijadili bajeti ya Ofisi ya
Makamu wa Rais-Mazingira kwa mwaka wa fedha 2016/ 2017.
Wajumbe
wa Kamati ya Bunge ya Viwanda,Biashara na Mazingira Wakimsikiliza kwa
Makini Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mh.Dkt. Dalaly P. Kafumu walipokutana
Kujadili taarifa ya Utekelezaji wa bajeti ya Ofisi ya Makamu wa
Rais-Mazingira kwa Mwaka wa fedha 2016/2017.
MKE WA WAZIRI MKUU ATOA MSAADA WA MASHUKA KWA AKINAMAMA WALIOJIFUNGUA
Waziri
Mkuu, Kassim Majalaiwa akizungumza na Madaktari, Wauguzi na watumishi
wa hospitali ya wilaya ya Ruangwa Aprili 11, 2016. Kushoto ni Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa
Lindi, Mzee Mtopa.
Mke
wa Waziri Mkuu, Mary Majalaiwa akizungumza baada ya kukabidhi msaada
wa shuka kwa wazazi wanaosubiri kujifungua na waliojifungua kwenye
hospitali ya wilaya ya Ruangwa Aprili 11, 2016. Kushoto ni Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na wapili kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wa mkoa
Lindi, Mzee Mtopa.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akiagana na wanwake wa Ruangwa baada ya
kuzungumza nao kwenye ukumbi wa Chama cha Walimu mjini Ruangwa
Aprili 11, 2016.
Waziri
Mkuu, Kassim Majliwa akitembelea soko kuu la mji wa Ruangwa kukagua
hali ya chakula na bei zake Aprili 11, 2016. Alikuwa katika ziara ya
jimbo lake la uchaguzi la Ruangwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na mabingwa
wa soka wa mkoa wa Lindi , timu ya Namungo FC ya Ruangwa baada ya
kukabidhiwa kombe la ubingwa huo na kuzungumza nao kwenye uwanja wa
michezo wa Ruangwa akiwa katika ziara jimboni kwake , Aprili 11, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
…………………………………………………………………………………………………….
AFRICA DIGITAL BANKING SUMMIT WILL BE HELD ON 13TH & 14TH APRIL, 2016 AT JNICC, DAR ES SALAAM
Africa
Digital Banking Summit will be held on 13th & 14th April, at Julius
Nyerere International Convention Centre, Dar es Salaam from 8.30am-
4.30pm.
Topics that will be discussed:
1. E- commerce/M-commerce in East Africa,
2. Mobile Money & Digital Payment,
3. Payment Security & Regulation ,
4. The Future of Mobile Money & Digital Platforms.
Guest
of Honour: Dr. Ashatu Kijaji, Assistant Minister, Ministry of Finance.
Speakers include: Mr. Bernard Dadi, Director, National Payment System,
Bank of Tanzania, Kelvin Twissa, Telecommunications Expert, Imeke
Bassemaker, CEO, NMB, Sameer Hirji, Executive Director, Selcom Tanzania.
Visit www.africadbs.com for registration detail
SENDEKA AZUNGUMZA NA WAJUMBE WA HALMASHAURI BABATI
Msemaji
wa CCM, Mjumbe wa NEC, Christopher Ole Sendeka akionyshwa na Katibu wa
CCM mkoa wa Manyara, Ndengaso Ndakubali (kulia), jinsi Jengo la Ofisi ya
CCM mkoa huo, lilivyoungua moto hivi karibuni, Sendeka alipokagua jengo
hilo, leo Aprili11, 2016, akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Manyara.
(Picha na Bashir Nkoromo).
KIKAO CHA BARAZA LA MAPINDUZI (BLM)
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein
akiongoza kikao cha kwanza cha Baraza la Mapinduzi (BLM) mara baada ya
kuwaapisha Viongozi hao hapo jana, kikao kilichofanyika leo
kiliwajumuisha Mawaziri pamoja na Naibu Mawaziri wote wa wizara 13
katika ukumbi wa Baraza hilo Ikulu Mjini Unguja,
[Picha na Ikulu.]
WATANZANIA WATAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZILIZOPO AFRIKA MASHARIKI
Mbunge
wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Makongoro Nyerere (katikati)
akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya Habari
Maelezo, jijini Dar es Salaam.
.
Mbunge wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji akizungumza jambo.
Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo wakichukua habari.
JESHI LA MAGEREZA NA SUMA – JKT WAKABIDHIWA JUKUMU LA KUTENGENEZA MADAWATI YENYE THAMANI YA BILIONI 6, JIJINI DAR
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akionesha mfano wa hundi
aliyokabidhiwa na Ofisi ya Bunge leo Ikulu, Jijini Dar es Salaam ambapo
fedha hizo ameelekeza zitumike kutengenezea madawati ya shule hapa
nchini(kulia)ni Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.
Muonekano wa Madawati ambayo
yanatarajiwa kutengenezwa na yaliyoidhinishwa na Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi kama yanavyoonekana katika picha.
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, CGP John Casmir Minja(kushoto) akiwa na Mkuu wa Jeshi la Kujenga
Taifa, Bregedia Jenerali, Michael Isamuhyo(katikati) wakifuatilia
hotuba ya Rais Magufuli(kulia) ni Mtendaji Mkuu wa SUMA – JKT, Bregedia
Jenerali C.Yateri.
Kamishna Jenerali wa Magereza
nchini, CGP John Casmir Minja akiongea na Wandishi wa Habari kuhusu
namna Jeshi hilo lilivyojipanga kutekeleza jukumu lililopewa.
Baadhi ya Maafisa Waandamizi wa
Jeshi la Magereza pamoja na Maafisa Waandamizi kutoka Makao Makuu ya
Jeshi la Kujenga Taifa waliohudhuria hafla hiyo.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP John Casmir Minja akisalimiana
na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashilila wakipokutana katika Viwanja
vya Ikulu, Jijini Da es Salaam(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la
Magereza).
……………………………………………………………………………………………….
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu azindua taasisi ya (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation)
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa
Taasisi ya Basila Mwanukuzi (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation)
yenye lengo la kusaidia wanawake kuinua uwezo wao wa kibunifu ili
kujiinua kiuchumi hasa Mama Lishe kwa kushirikiana na wadau mbali
mbali. Uzinduzi huo umefakika leo Aprili 11, 2016 kwenye Ukumbi wa
Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni
Mwanzilishi wa Taasisi hiyo, Basila Mwanukuzi (kulia), Kaimu Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Jinsia, Timoth Mgonja pamoja na Mwakilishi wa Mama
Lishe, Bi. Grace Foya.
Mwalimu (wa pili kulia), akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa
Taasisi ya Basila Mwanukuzi (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation)
yenye lengo la kusaidia wanawake kuinua uwezo wao wa kibunifu ili
kujiinua kiuchumi hasa Mama Lishe kwa kushirikiana na wadau mbali
mbali. Uzinduzi huo umefakika leo Aprili 11, 2016 kwenye Ukumbi wa
Makumbusho ya Taifa, Jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni
Mwanzilishi wa Taasisi hiyo, Basila Mwanukuzi (kulia), Kaimu Mkurugenzi
wa Maendeleo ya Jinsia, Timoth Mgonja pamoja na Mwakilishi wa Mama
Lishe, Bi. Grace Foya.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Mwalimu akizungumza na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi huo uliofanyika leo jijini Dar es salaam.
Basila Mwanukuzi Mkurugenzi wa
Taasisi ya (Basila Mwanukuzi Empowerment Foundation) akimkaribisha
Waziri Ummy Mwalimu ili kuzungumza na wageni waalikwa na kisha kuzindua
rasmi taasisi hiyo.
Baadhi ya ndugu na wanafamilia wa Basila Mwanukizi wakiwa katika hafla hiyo
Mrisho Mpoto kushoto na Miriam Ikoa mmoja wa waliowahi kuwa Miss Tanzania wakiwa pamoja na wageni wengine katika hafla hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu akisalimiana na Basila Mwanukuzi mara baada ya kuwasili katika uzinduzi huo Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Timoth Mgonja
Mwalimu akisalimiana na Basila Mwanukuzi mara baada ya kuwasili katika uzinduzi huo Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Maendeleo ya Jinsia, Timoth Mgonja
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu akisalimiana na baadhi ya akina mama Lishe waliohudhuria katika hafla hiyo ya uzinduzi.
Mwalimu akisalimiana na baadhi ya akina mama Lishe waliohudhuria katika hafla hiyo ya uzinduzi.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio katika hafla hiyo.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga.
Mwalimu akisalimiana na Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Ummy
Mwalimu na Basila Mwanukuzi wakipiga picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.
Mwalimu na Basila Mwanukuzi wakipiga picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi huo.

No comments :
Post a Comment