Thursday, April 14, 2016

ISMAIL ADEN RAGE AJIUNGA NA MPANGO WA UCHANGIAJI WA HIARI WA MFUKO WA PENSHENI WA PSPF


 RAIS wa zamani wa Klabuya Simba ya Dar es Salaam, Alhaj Ismail Aden Rage, (kushoto), akipokea kadi yake ya uanachama wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, kupitia mpango wa uchangiaji wa hiari yaani PSS, kutoka kwa Meneja Masoko, Mawasiliano na Uhusiano wa PSPF, Bi.Costantina Martin, makao makuu ya PSPF, katikati ya jiji la Dar es Salaam, Aprili 14, 2016.
 Alhaj Rage akionyesha kadi hiyo
 Meneja wa Mpango wa Uchangiaji wa Hiari, (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Mwanjaa Sembe, (kushoto), akipokea fomu za kujiunga na uanachama kutoka kwa aliyekuwa Rais wa Klabu ya soka ya Simba, Alhaj Ismail Aden Rage, makao makuu ya PSPF, katikati ya jiji la Dar es Salaam, Aprili 14, 2016
 Alhaj Rage, (kushoto), akiweka dole gumba kwenye fomu yake ya uanachama huku akisaidiwa na Bi. Mwanjaa Sembe, (kulia) na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw.Abdul Njaidi
 Alhaj Rage akijaza fomu, kuliani Bi. Mwanjaa Sembe
 Alhaj Rage, akikabidhi fomu kwa Bi. Mwanjaa Sembe, huku Njaidi akishuhudia
 Rage akizungumza baada ya kukabidhi fomu kwa Bi. Mwanjaa Sembe (kushoto)
 Meneja wa Mpango wa uchangiaji wa hiari yaani PSS, wa Mfuko wa Pensehni wa PSPF, Bi. Mwanjaa Sembe, akiwa mwenye furaha baada ya kupokea mwanachama mpya, Alhaj Ismail Aden Rage
 Alhaj Rage akipokewa na Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Bw. Njaidi alipowasili kujiunga na Mfuko huo
Alhaj Rage, akibadilishana mawazo na Bi. Costantina Martin, na Njaidi baada ya kuwa mawanachama wa Mfuko huo
…………………………………………………………………………………………………
RAIS wa zamani wa Klabu ya Simba ya Dar es Salaam, Alhaj Ismael Aden Rage, amejiunga
na mpangowa uchangiaji wa Hiari (PSS), wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Aprili 14,
2016.
Rage ambaye pia ni Mbunge wa zamani wa Jimbo la Tabora mjini, kufuatia kujiunga huko,
amefaidika kuingizwa kwenye fao la huduma ya afya litolewalo na Mfuko huo
kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, NHIF ambao una ushirikiano wa kutoa
huduma za afya kwa wanachama wa PSPF wanaotaka kufaidikana huduma hiyo.
“Nitoe wito kwa wanamichezo wakiwemo wa mpira wa miguu, kuchangamkia fursa hiyo kwani
mambo sasa yamebadilia kujiunga na PSPF kupitia mpango huu wa hiari ambao
unamruhusu mtu binafsi au vikundi kujiunga na uanachama, lakini pia kutokana na
kupanda kwa huduma za afya, ukiwa mwanachama wa PSPF unaweza kupata huduma ya
afya wewe na familia yako, hii ni faida kubwa.” Alisema Rage wakati
akikabidhiwa kadi yake ya uanachama na Meneja Masoko, Mawasiliano na Uenezi wa
PSPF, Bi. Costantina Martn.
Rage alisema, yeye kama mwanamichezo atahamasisha wanamichezo hususan wacheza mpira
kujiunga na mpango huu kwani maisha ya sasa yanahitaji kwenda kisasa, na jambo
muhimu ni kuwa na afya bora, na afya bora utaipata kama unapata huduma bora,
nimeambiwa kupitia mpango huu ninaweza kupata matibabu kwenye hospitali yoyote
nchini na wakati wowote, Alisema.
Awali Rage alijaza fomu za kujiunga na uanachama ambapo alipokewa na Meneja wa Mpango
wa Uchangiaji wa Hiari, PSS, wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Bi. Mwanjaa Sembe. Ambaye
alimshukuru Rage kwa kuwa mwanachama wa Mfuko huo.

WAZIRI WA ARDHI AKUTANA NA WAMILIKI WA MABENKI NCHINI

LUK1 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwasisitiza Wamiliki wa Mabenki Nchini kuzitambua Hati Miliki za Ardhi za Kimila katika kutoa mikopo kwa Wakulima, wajenzi na Wajasiliamali, kushoto ni Bibi Medelina Kiwayo Meneja Usimamizi wa Taasisi za Fedha-Benki Kuu na Tuse Joune Kaimu Mkurugenzi Mkuu Chama cha Wenye Mabenki Tanzania (TBA).
LUK2 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwasisitiza Wamiliki wa Mabenki Nchini kuzitambua Hati Miliki za Ardhi za Kimila katika kutoa mikopo kwa Wakulima, wajenzi na Wajasiliamali alipo kutana nao leo jijini Dar es salaam.
LUK3 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwasisitiza Wamiliki wa Mabenki Nchini kuzitambua Hati Miliki za Ardhi za Kimila katika kutoa mikopo kwa Wakulima, wajenzi na Wajasiliamali alipo kutana nao leo jijini Dar es salaam.
LUK4
LUK5
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akiwa katika kikao na Wamiliki wa Mabenki Nchini ili kuzitambua Hati Miliki za Ardhi za Kimila katika kutoa mikopo kwa Wakulima, wajenzi na Wajasiliamali, kulia ni Bibi Medelina Kiwayo Meneja Usimamizi wa Taasisi za Fedha-Benki Kuu na Tuse Joune Kaimu Mkurugenzi Mkuu Chama cha Wenye Mabenki Tanzania (TBA), kushoto ni David Shambwe Mkurugenzi wa Hazina na Maendeleo ya Biashara-NHC na Mary Makondo Kaimu Kamishna wa Ardhi.
LUK6Baadhi ya Wamiliki wa Mabenki Nchini wakiwa katika kikao hicho.

Rais Magufuli atengua uteuzi wa Nderumaki

NDER
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mhariri Mtendaji wa Magazeti ya Serikali (TSN) Bw. Gabriel Nderumaki.
Taarifa iliyotolewa leo tarehe 14 Aprili, 2016 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John Kijazi, imeeleza kuwa Rais Magufuli ametengua uteuzi huo kuanzia tarehe 18 Machi, 2016.
Kufuatia kutenguliwa kwa uteuzi huo, Rais Magufuli amemteua Bi. Tuma Abdallah kukaimu
nafasi hiyo.
Bi. Tuma Abdallah ni Mhariri Mtendaji Msaidizi wa Magazeti ya Serikali (TSN)
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
14 Aprili, 2016

ASILIMIA 71 YA WATANZANIA HAWATAKI KUFANYA KAZI.

JEN1
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu),Jenista Mhagama,akizungumza katika katika uzinduzi wa matokeo ya utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014. Uzinduzi huo ulifanyika katika Viwanja vya Karimjee,Dar es Salaam, jana. Kulia ni Mkurugenzi wa Sensa ya watu na Takwimu za Jamii,Ephraim Kwesigabo na Mkurugenzi Mkuu wa Takwimu nchini,Dk.Albina Chuwa.
JEN2
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu),Jenista Mhagama,akionesha ripoti ya matokeo ya utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014 katika Viwanja vya Karimjee,Dar es Salaam, jana. Wengine wanaoshuhudia ni kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Takwimu nchini,Dk.Albina Chuwa, Mkurugenzi wa Sensa ya watu na Takwimu za Jamii,Ephraim Kwesigabo na Mwakilishi kutoka Shirika la Kazi Duniani,Marry Kawar.
JEN3
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge,Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu),Jenista Mhagama,akizindua ripoti ya matokeo ya utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa mwaka 2014 katika Viwanja vya Karimjee,Dar es Salaam, . Wengine wanaoshuhudia ni kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa Takwimu nchini,Dk.Albina Chuwa, Mkurugenzi wa Sensa ya watu na Takwimu za Jamii,Ephraim Kwesigabo na Mwakilishi kutoka Shirika la Kazi Duniani,Marry Kawar.
………………………………………………………………………………………………………………..
Na Raymond Mushumbusi – MAELEZO
Utafiti uliofanyika hivi karibuni na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) umebaini kwamba asilimia 71 ya watanzania wanatumia muda mwingi kufanya shughuli zisizokuwa za uzalishaji mali wala tija binafsi kwao na Taifa kwa ujumla
Akizundua taarifa ya utafiti huo leo jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi,Ajira,Vijana na watu wenye ulemavu Mhe. Jenista Mhagama  amesema kuwa idadi hiyo hufanya kazi zisizoleta tija kwao na taifa na muda mwingi huutumia kujihudumia binafsi kwa kulala na starehe nyingine.
Ameeleza kuwa takwimu hizo zinaonesha wazi ni kwa namna gani watanzania wanashindwa kujishughulisha katika kufanya kazi zenye kuwaingizia kipato na badala yake wanatumia muda wao mwingi kufanya shughuli zisizo za uzalishaji hasa kufanya starehe mbalimbali.
 “ Ndugu zangu watanzania unakuta mtu amekaa baa au anacheza “poll table” kuanzia asubuhi mpaka jioni na hujui anafanya kazi gani ya uzalishaji, ndugu zangu tuone aibu basi tujishugulishe tulijenge taifa letu ili kujiletea maendeleo yetu na nchi yetu.”
Aidha, matokeo hayo yamebainisha kuwa asilimia 18.5 ya wananchi wanafanya kazi za uzalishaji na asilimia 10.6 ni wale wanaofanya shughuli za nyumbani zisizo na malipo huku uchambuzi wa kijinsia ukionesha kuwa wanaume asilimia 23.8, wanatumia muda mwingi kwenye shughuli za kiuchumi ikilinganishwa na asilimia 13.5 ya wanawake.
Amefafanua kuwa wanawake ambao ni asilimia 16.5 katika utafiti huo wanatumia muda mwingi kufanya kazi za nyumbani zisizo na malipo ikilinganishwa na asilimia 4.4 ya wanaume.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Ofisa ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa amesema kuwa upatikanaji wa Takwimu hizo utaisaidia Serikali kupata mbinu sahihi za kuondokana na tatizo la ajira nchini kwa kuunganisha nguvu kutoka sekta isiyo rasmi ili kuleta changamoto katika soko la ajira nchini.
Amesema kuwa hii ni mara ya tano Tanzania inafanya utafiti huo na kubainisha kuwa ulianza  mwezi Januari hadi Desemba,  2015 ukitumia sampuli ya Sensa  ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 iliyotumika kupata taarifa sahihi ya takwimu hizo.
Aidha, amebainisha kuwa ili kufanikisha utafiti huo NBS imeshirikiana na wadau mbalimbali ikwemo Wizara ya kazi na Ajira,Shirika la Kazi Duniani (ILO),Benki ya Dunia (WB),Benki ya Maendeleo ya Afrika(ADB) na Asasi zisizo za Kiseikali.

Tigo sasa ya pili kwa ukubwa katika kampuni za simu Tanzania

 
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez
Ushindani unazidi kupamba moto miongoni mwa kampuni za simu nchini ambapo katika kipindi cha miezi mitatu cha kati ya Oktoba na Desemba mwaka 2015, ni jumla ya watumiaji wapya 1,448,782 tu ambao walijisali kutumia huduma zao za mawasiliano.
Ushindani huu ambao umechochewa na kuingia kwa kampuni mpya katika sekta ya mawasiliano Tanzania, umefikisha jumla kuu ya watumiaji wa huduma ya mawasiliano nchini kufikia 39.8 milioni kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa hivi karibuni na Mamlaka ya Mawasilano Tanzania, (TCRA).
Kampuni ya MIC Tanzania Ltd- ijulikanayo kwa jina lingine kama Tigo – ilisajili juma ya wateja wapya 488,886 katika kipindi hicho cha miezi mitatu sawa na asilimia 34.  Idadi hii ya wateja wapya inaifanya Tigo kuwa na jumla ya wateja 11,115,991 na kuifanya kampuni hiyo kuwa katika nafasi ya pili kwa ukubwa imiliki asilimia 28 la soko la mawasiliano nchini na hivyo kuipita
Airtel ambayo imekuwa katika nafasi hiyo kwa kipindi cha takriban muongo mmoja.
Airtel kwa upande mwingine ilisajili jumla ya wateja wapya wapatao 32, 839 katika kipindi hicho cha miezi mitatu na kufikisha jumla ya wateja wake kuwa  11,047, 505 ambayo ni sawa na asilimia 28 lakini kiwa imezidiwa na Tigo kwa idadi ya wateja 68,486. Licha ya kuendelea kupungua kwa idadi ya wateja wake mwaka hadi mwaka, kwa mujibu wa takwimu za TCRA, Vodacom bado inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wateja wapatao 12,714,297 sawa na asilimia 32 ya jumla
ya watumiaji wote wa huduma za mawasiliano Tanzania.
Idadi ya wateja wa Vodacom imeonekana kushuka kutoka asilimia 45 mwaka 2007 hadi asilimia 41 mwaka 2008 na kufikia asilimia 39 Desemba 2009.
Wadadisi wa sekta ya mawasiliano wanaelezea hali hii kushuka kwa idadi ya wateja wapya miongoni mwa kampuni hizi kuwa kunachangiwa na mabadiliko ya kimikakati ambapo msizitizo mkubwa miongoni mwa kampuni ni kuwalenga Zaidi wateja watumiaji wa huduma za Intaneti kupitia simu zao kama nyenzo kuu ya kukuza mapato tofauti na matumizi ya kuongea na kutuma sms kama ilivyokuwa siku za nyuma.
Meneja Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez, kwa upande wake ameelezea kukua haraka kwa kampuni hiyo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita na kusema kumechangiwa na sababu mbalimbali zikiwemo ubunifu mkubwa ambao unafanywa katika kendesha kampuni kibiashara.
“Mafanikio ya Tigo yameletwa na sababu nyingi kama vile kuwapa wateja wetu huduma bora na kwa bei nafuu, upatikanaji wa mtandao wetu nchi nzima, utumiaji wa teknolojia ya kisasa, ubunifu na kuwa karibu na wateja,” Gutierrez anasema.
Akifafanua Zaidi kuhusu ubunifu huo, Gutierrez ametaja baaadhi ya huduima na bidhaa zilioanzishwa na kampuni hivi karibuni kama vile kuwapa wateja uwezo wa kufanya miamala ya kibenki kupitia simu zao za mikononi, uwezo wa kutuma na kupokea fedha kutoka mitandao mingine ya mawasiliano, kutuma na kupokea fedha kimataifa na mgao wa faida utolewao kwa watumiaji wa huduma ya Tigo Pesa kila baada ya miezi mitatu.
 Aidha meneja huyo mkuu ametaja vichocheo vingine vya kukua hara kwa Tigo kuwa ni “kubuni
huduma zinazolenga kuwapa wateja wetu fursa ya kuishi maisha ya kidijitali zikiwemo
huduma kama vile upatikanaji wa Facebook kwa lugha ya Kiswahili, simu zenye menu ya Kiswahili, WhatsApp ya bure na zinginezo,” amesema. 
Kampuni ya Tigo kwa mujibu wa Gutierrez inawekeza kiasi cha dola za kimarekani $ 120 milioni  kwa mwaka katika kuboresha mtandao wake na kupanua upatikanaji wa huduma zake
nchini.
Ametoa mfano wa huduma ya 4G LTE ya Tigo ambayo kwa sasa inapatikana katika miji sita – Dar es Salaam, Arusha, Tanga, Dodoma, Morogoro, Moshi na Mwanza – na kuelezea kuwepo kwa mkakati wa kufikisha huduma hii katika mji mikubwa yote nchini ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
Kwa upande wake kampuni ya Zantel ambayo ni kampuni dada ya Tigo, zote kiwa zinamilikiwa na Millicom, ilirekodi wateja wapya 320, 483 katika kipindi cha miezi mitatu ya mwisho ta mwaka 2015 na kufikisha jumla ya wateja 1, 839, 391. Nayo kampuni mpya ya Haloteli ndiyo iliyoongoza kwa kuvuna wateja wengi kipindi hicho wapatao 793, 383 na hivyo kufikisha jumla kuu
ya waetja wake kuwa 1,226,678 hadi kufikia mwisho wa Desemba 2015.
Ikiwa na wateja milioni 1.56 hadi kufikia mwishoni mwa Desemba 2015, Smart ilikuwa na asilimia nne (4) la soko la mawasiliano ya simu nchini sawa na Zantel wakati kampuni inayomilikiwa na serikali (TTCL) ikiwa inashikilia asilimia moja (1) ya soko hilo.

MAKABIDHIANO YA OFISI KATIBA NA SHERIA ZANZIBAR

of1
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini akitoa shukurani kwa wafanyakazi wa Wizara ya Katiba,Sheria,Utumishiwa Umma na Utawala Bora  wakati wa makabidhiano ya Ofisi na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishiwa Umma na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman leo katika ukumbi wa Jengo la Wizara ya Utumishi wa Umma Shangani  Mji Mkongwe wa Zanzibar, baada ya uteuzi uliofanywa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Sheun,[Picha na Ikulu.]
of2
Aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Ikulu na Utawala Bora Dkt.Mwinyihaji Haji Makeme Mwadini  akikabidhiana Ofisi na  Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Katiba,Sheria,Utumishiwa Umma na Utawala Bora Mhe Haroun Ali Suleiman leo katika ukumbi wa Jengo la Wizara ya Utumishi wa Umma Shangani  Mji Mkongwe wa Zanzibar, baada ya uteuzi uliofanywa na  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Sheun,[Picha na Ikulu.]

Mwakilishi WHO atembelea Wizara ya Afya Zanzibar kupata tarifa za Kipindupindu

kidu
Waziri wa Afya Mhe, Mahmoud Thabit Kombo kulia akisalimiana na Muakilishi wa Shirika la Afya Duniani WHO alioko Zanizbar Dk, Ghirmay Andemichael mara baada ya kuwasili Ofisini kwake Mnazi mmoja Mjini Zanzibar, kupata taarifa ya  maradhi ya kipindupindu yalioanza mwezi Septemba mwaka jana hapa  Zanzibar.
kidu1
Waziri wa Afya Mhe, Mahmoud Thabit Kombo akizungumza na muakilishi wa Shirika la Afya Duniani WHO nchini Tanzania Dk, Rufaro Chatora kushoto yake pamoja na ujumbe aliofuatana nao Ofisini kwake Mnazi mmoja Mjini Zanzibar. Muakilishi huyo alifika kuangalia hali ya maradhi ya kipindupindu  Zanzibar.
kidu3
Muakilishi wa Shirika la Afya Duniani WHO Dk, Rufaro Chatora katikati akizungumza na Wakuu wa sekta mbalimbali katika Wizara ya Afya Zanzibar kuhusiana na Maradhi ya Kipindupindu  Zanzibar. Kushoto yake ni Muakilishi wa WHO aliopo Zanzibar Dk, Ghirmay Andemichael na kulia yake ni Katibu Mkuu wizara ya Afya Zanzibar Mohd Saleh Jidawi.
………………………………………………………………………………………………….
NA RAMADHANI ALI/MAELEZO ZANZIBAR 
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Tanzaia Dkt. Rufaro Chatora amezishauri taasisi za Serikali, taasisi za kiraia na watu  binafsi kila mmoja kutekeleza wajibu wake katika kukabiliana na maradhi ya kipindupindu nchini.
Amesema maradhi ya kipindupindu yanapotokea katika nchi moja yanagusa nchi nyingi duniani kutokana na watu kusafiri kutoka nchi moja kwenda nyengine katika harakati zao za maisha.
Dkt. Chatora ameeleza hayo alipokuwa akizungumza katika mkutano na watendaji wakuu wa Wizara ya Afya na waandishi wa Habari katika ziara yake ya kuangalia hali ya maradhi ya kipindupindu Zanzibar tokea yalipoanza mwezi Septemba mwaka jana hadi hivi sasa ambapo  watu 2703 wamepata ugonjwa  huo.
Amesema maradhi ya kipindupindu ni rahisi kutibika iwapo kila mtu atatimiza wajibu wake na kufuata ushauri wa wataalamu wa afya ikiwa ni pamoja na kuacha  kutumia maji yasiyo salama ambayo ni moja ya chanzo kikubwa cha kupata maradhi hayo.
Mwakilishi huyo wa WHO amesema Shirika hilo kwa kushirikiana na mashirika mengine ya Kimataifa litaendelea kuunga mkono juhudi za  Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kukabiliana na maradhi hayo ili kuhakikisha yanamalizika.
Akieleza hali ya kipindupindu ilivyo hivi sasa Zanzibar katika mkutano huo uliofanyika Wizara ya Afya Mnazimmoja, Mkurugenzi Kinga na ELimu ya Afya Dkt. Mohd Dahoma amesema hali  bado sio nzuri na wanaendelea kupokea wagonjwa wengi katika kambi ya Chumbuni.
“Tunapokea  wagonjwa kati ya  10 hadi 15 kwa siku katika kambi ya Chumbuni, kwa bahati mbaya jana tulipokea wagonjwa 20  na kambi moja mpya imefunguliwa  katika kisiwa cha Tumbatu,’’ alisema Dkt. Dahoma.
Amesema jumla ya Kambi 17 za wagonjwa wa kipindupindu zimefunguliwa katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba na kumi kati yao zimefungwa baada ya kukosa mgonjwa wa maradhi hayo.
Ameongeza kuwa kati ya wagonjwa 2703 waliogunduliwa na maradhi hayo 34 wamefariki ikiwa ni  sawa na asilimia 1.3 na vijana wenye umri kuanzia miaka 17 ndio walioathirika zaidi.
Dkt. Dahoma amesema kisiwa cha Unguja kimekuwa na wagonjwa wengi  zaidi wa kipindupindu  asilimia 52.3 na Pemba ni asilimia 47.3 huku Mkoa Mjini Magharibi ukiongoza ukifuatiwa na Mkoa Kaskazini Pemba.
Mkurugenzi Kinga na Elimu ya Afya amewashauri wananchi kuwawahisha  mapema vituo vya afya  watu wanaobainika na  dalili za maradhi ya kipindupindu kwa vile imeonekana wagonjwa wengi wanapopelekwa vituoni afya zao zinakuwa mbaya na matibabu yanakuwa magumu.

Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Fionnuala Gilsenan amtembelea Waziri Mh. Angellah Kairuki

fin
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mh. Angellah Kairuki (Mb) (kulia) akizungumza na Balozi wa Ireland nchini Tanzania Mhe. Fionnuala Gilsenan alipotembelea ofisini kwake mapema leo

Wizara ya Afya Zanzibar yaadhimisha siku ya afya Duniani kwa kutoa elimu ya maradhi yasiyoambukiza skuli mbali mbali.

za1
Mkuu wa Kitengo cha maradhi yasiyoambukiza (NCD) Omar Mwalimu Omar akitoa elimu  kwa wanafunzi wa Skuli ya Sekondari ya Kiembesamaki juu ya njia bora za kujikinga na  maradhi yasiyoambukiza ikiwa ni maadhimisho ya siku ya afya Duniani. 
za2
Muuguzi kutoka kliniki  ya wagonjwa wa kisukari Hospitali ya Mnazimmoja Bi. Mwanaharusi Shaaban akitoa elimu ya ugonjwa wa kisukari kwa wanafunzi wa Skuli ya Mwanakwerekwe C katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ifikapo tarehe 7 April.  Zanzibar imeadhimisha siku hiyo April 13 kwa kutoa elimu skuli za serikali na binafsi.
za3
Baadhi ya wanafunzi wa Skuli ya Mwanakwerekwe C wakimskiliza kwa makini mtoa elimu ya maradhi yasiyo ambukiza Bi. Mwanaharusi Shaaban (hayupo pichani) wakati wa sherehe za siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ikifika tarehe 7 kila mwaka.
za4
Mwanafunzi Shadia Issa Juma akiuliza swali kwa Muuguzi kitengo cha wagonjwa wa kisukari Bi. Mwanaharusi Shaaban.
za5
Mkufunzi kutoka kitengo cha maradhi yasiyoambukiza (NCD) cha Wizara ya Afya Rabia Ali Makame akifundisha wanafunzi wa Skuli ya SOS kuhusiana na visababishi vinavyopelekea maradhi yasiyo ya kuambukiza katika sherehe za kuadhimisha siku ya Afya Duniani. 
Baadhi ya wanafunzi wa Skuli ya Mwanakwerekwe C wakimskiliza kwa makini mtoa elimu ya maradhi yasiyo ambukiza Bi. Mwanaharusi Shaaban (hayupo pichani) wakati wa sherehe za siku ya Afya Duniani zinazoadhimishwa kila ikifika tarehe 7 kila mwaka.Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. DKT. JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI KUWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA BARABARA YA JUU (FLYOVER) YA TAZARA NA KUFUNGUA DARAJA LA KIGAMBONI JIJINI DARA ES SALAAM

taza
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano inapenda kutaarifu Umma kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa barabara ya juu (Flyover) katika makutano ya TAZARA na ufunguzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Siku ya Jumamosi tarehe 16 Aprili, 2016 Mheshimiwa Rais ataweka jiwe na msingi la ujenzi wa barabara ya juu katika makutano ya barabara Nyerere na Mandela (Flyover ya TAZARA).
Jumanne tarehe 19 Aprili, 2016 Mheshimiwa Rais atafungua rasmi Daraja la Kigamboni lenye urefu wa mita 680 na barabara unganishi (approach roads) upande wa Kurasini na Kigamboni zenye urefu wa kilometa 2.5.  Ujenzi huu umefanywa na Kampuni ya China Railway 15 Group ilishirikiana na Kampuni ya China Bridge Engineering Group.
Aidha wakati tunasubiri uzinduzi rasmi, Wananchi na magari yenye uzito usiozidi tani 10 yataruhusiwa kutumia Daraja la Kigamboni kuanzia Jumamosi tarehe 16 Aprili, 2016 ili kuwawezesha kuelewa vizuri miundombinu na matumizi ya daraja.
Utekelezaji wa miradi hii ni mojawapo ya jitihada za Serikali za kuboresha miundomninu na kupunguza msongamano wa magari katika jiji la Dar es salaam.
Imetolewa na;
Eng. Joseph M. Nyamhanga
Katibu Mkuu  (Ujenzi)
Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
14 Aprili, 2016

NAIBU WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KUTEMBELEA MRADI WA MABWAWA YA SAMAKI GEREZA KWAMUGUMI, KOROGWE

ole
Naibu Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mhe. William Ole Nasha (Mb) anatarajia kufanya ziara ya kikazi Gereza Kwamugumi, Korogwe Mkoani Tanga.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na kusainiwa na Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja inaeleza kuwa lengo kuu la ziara hiyo ni kujionea maendeleo ya mradi wa mabwawa ya samaki yaliyopo gerezani hapo ambayo hadi sasa yamepandwa vifaranga wa samaki 18,800 tangu tarehe 16/12/2015.
Kabla ya kutembelea eneo la mradi wa mabwawa ya samaki, Naibu Waziri, Mhe. Ole Nasha atapokea taarifa fupi ya maendeleo ya mradi wa uzalishaji samaki Gereza Kwamugumi, Korogwe.
Miradi ya ufugaji samaki ipo katika Magereza ya Karanga, Njombe, Masasi, Tukuyu ambapo nia ya Uongozi wa Jeshi la Magereza ni kuieneza katika Magereza mbalimbali yenye fursa za kuendesha mradi huo.
Mradi wa uzalishaji samaki katika Gereza Kwamugumi ni mojawapo ya miradi mbalimbali ya uzalishaji mali iliyoanzishwa na Uongozi wa Jeshi katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazolikabili Jeshi la Magereza, hususan katika kuipunguzia Serikali gharama za kuhudumia Magereza na kuongeza pato la kodi kwa Taifa.

Dk. Kigwangalla akutana na afisa miradi kutoka Shirikala la Kimataifa la nguvu za Atomiki (IAEA)

kig1
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla (wa pili kushoto) akisikiliza kwa makini mazungumzo na Afisa  miradi anayesimamia miradi ya mionzi barani Afrika kutoka wakala wa Kimataifa wa nguvu za Atomiki (IAEA), Bw. Solomon Haile (wa kwanza kulia). Wengine ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Tiba anayeshughulikia magonjwa yasiyo ambukiza, Profesa Ayoub Magimba (katikati),  akifutiwa na Mkurugenzi  taasisi ya Ocean Road, Dk. Julius Mwaisalage na kushoto Mratibu wa Magonjwa ya Saratani Kitaifa pamoja na magonjwa yasiyoambukiza kwa watu wazima, Dk. Sara Maongezi. (Picha na mpiga picha wetu).
kig2
……………………………………………………………………………………………….
Na Mwandishi Wetu
NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla amekutana na   Afisa  miradi anayesimamia miradi ya mionzi barani Afrika kutoka wakala wa Kimataifa wa nguvu za Atomiki (IAEA), Bw. Solomon Haile  katika mazungumzo yaliyofanyika leo asubuhi Aprili 14.2016, Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Katika mazungumzo hayo, Dk. Kigwangalla ameomba Tanzania ipatiwe kibali cha kununua mashine mpya ya kutibu saratani (LINAC) Sambamba na sehemu ya msaada iliyoahidiwa na Mkurugenzi Mkuu wa IAEA, Bw.Yukiko Amano mbele ya Waziri Mkuu Mstaafu, Mh. Mizengo Kayanda Pinda miaka mitatu iliyopita.
Tanzania tayari imetenga kiasi cha Euro 1.65 Milioni kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya mchango wake kwa asilimia 50  kama mradi ulivyokuwa awali.
Mh. Kigwangalla alisema: “Bahati mbaya sana kutokana na ucheleweshwaji, Bajeti ya msaada huo kutoka IAEA ilipitwa na wakati  na kusababisha Tanzania kukosa fursa hiyo. Malengo ya Tanzania ni kununua mashine hizo mbili  kwa ajili ya kuboresha huduma za tiba ya Mionzi nchini”.
Ujenzi wa jengo kwa ajili ya kufunga mashine hizo mbili umesha kamilika na mashine moja itakamilika mwaka huu na ya pili mwakani ili kuboresha huduma za Saratani nchini.
Katika mazungumzo hayo, Maafisa waandamizi wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Woto walishiriki, akiwemo  Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Tiba anayeshughulikia magonjwa yasiyo ambukiza, Profesa Ayoub Magimba, Mratibu wa Magonjwa ya Saratani Kitaifa pamoja na magonjwa yasiyoambukiza kwa watu wazima, Dk. Sara Maongezi pamoja na Kaimu Mkurugenzi taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dk. Julius Mwaiselage.

WAZIRI UMMY MWALIMU AZINDUA BARAZA LA USAJILI LA MAZINGIRA

um1
Waziri  afya ,maendeleo ya jamii,jinsia ,wazee na watoto Ummy Mwalimu akiongea na wajumbe wa  baraza jipya  la usajili wa wataalam wa afya ya mazingira nchini(hawapo pichani) kushoto ni Mganga  Mkuu wa Serikali Prof: Bakari Mohammad
um2
Baadhi ya wajumbe wa baraza hilo pamoja na maofisa mazingira wakifuatilia hotuba ya Mh. Waziri Ummy Mwalimu
um3
Mwenyekiti mpya wa baraza la usajili wa wataalam wa afya ya mazingira nchini  Bartholomayo Ngaeje(katikati) akitoa neon la shukrani kwa waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto(hayupo pichani) mara baada ya kuzinduliwa kwa baraza hilo,kulia ni msajili wa baraza hilo Iddy Hoyange na kulia ni njumbe wa baraza hilo toka ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,hafla hiyo imefanyika kwenye ukumbi wa wizara hiyo
um4
Waziri wa afya,maendeleo ya jamii,jinsia,wazee na watoto Ummy Mwalimu akimkabidi cheti cha Uongozi kwa kuthamini mchango wake kwa baraza hilo aliyekuwa mwenyekiti wa awamu ya pili Bi.Mary Swai

Filamu za Bi Kidude kuoneshwa katika kumbukumbu ya kifo chake

kidu2
Kushoto ni mmiliki wa ukumbi wa ZANCINEMA Mohammed Bajbeir, akiwa pamoja na Andy Jones, raia wa Uingereza, mtengenezaji wa filamu za ‘As Old sa My Tongue’ na ‘I shot Bi. Kidude’, zinazoonesha historia ya maisha hadi kufa kwa msanii mkongwe marehemu Fatma Baraka ‘Bi. Kidude’, wakizungumza na waandishi wa habari juu ya kumbukumbu ya msanii huyo aliyefariki dunia Aprili 17, 2013. (Picha na Yussuf Simai-MAELEZO, ZANZIBAR.

Kamati ya Muda ngumi za kulipwa yaundwa.

ust1
Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Taifa(BMT) Bw. Mohamed Kiganja wa kwanza kushoto akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani leo jijini Dar es salaam kuhusu viongozi waliochaguliwa wa kamati ya muda ya mchezo wa Ngumi za kulipwa , kulia ni Katibu Mkuu wa kamati hiyo Bw. Yassin Ustaadh.
ust2
Katibu Mkuu mpya wa Kamati ya Muda ya Mchezo wa Ngumi za kulipwa Bw. Yassin Ustaadh akisisitiza jambo mbele ya  waandishi wa habari hawapo pichani baada ya kukabidhiwa kamati hiyo leo jijini Dar es salaam.
ust3
Waandishi wa habari wakimsikiliza kwa makini  Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Taifa(BMT) Bw. Mohamed Kiganja hayupo pichani  alipotambulisha  viongozi waliochaguliwa wa kamati ya muda ya mchezo wa Ngumi za kulipwa , kulia ni Katibu Mkuu wa kamati.

WAZIRI MKUU AKUTANA NA WAZIRI WA BIASHARA WA OMAN

maj2
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imedhamiria kuendeleza sekta ya viwanda kama mkakati wa kukuza uchumi ili nchi iweze kutoka kwene umaskini na kufikia uchumi wa kati.
buli

TAARIFA YA JESHI LA POLISI KUHUSU UTAPELI WA AJIRA KATIKA TAASISI MBALIMBALI

Katika siku za hivi karibuni katika maeneo mbalimbali hapa nchini, kumejitokeza makundi ya watu ama mtu binafsi kutumia mwamvuri wa taasisi fulani kujipatia kipato kwa njia za udanganyifu (utapeli) kwa kuwaahidi vijana kwamba watawapatia ajira katika taasisi hizo.
Makundi haya ya kihalifu imebainika kwamba yapo katika maeneo mbalimbali, hivyo, ni suala ambalo linahitaji ushirikiano mkubwa kutoka kwa wananchi ili kukomesha vitendo hivyo. Juhudi za makusudi zinaendelea kufanyika na jeshi la polisi ili kuwatia mbaroni watu wote wanaojihusisha na vitendo hivyo vya kitapeli.
Aidha, kufuatia kuibuka kwa vitendo hivyo, tayari Jeshi la Polisi limewakamata matapeli wawili wakiwa wamekusanya vijana katika mikoa ya Kilimanjaro na Mbeya, uchunguzi dhidi yao unaendelea na pindi utakapokamilika watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabiri.

SENDEKA AWASILI MKOANI KILIMANJARO LEO

 Msemaji wa CCM, Christopher Ole Sendeka akisalimiana na Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Deogratius Ruta alipowasili Ofisi ya CCM mkoa wa Kilimanjaro, mjini Moshi leo
 Mjumbe wa NEC na Ofisa Mwandamizi katika Idara ya Mawasilino na Umma Makao Makuu ya CCM, Kilumbe Ng’enda akisalimiana na Mwenyekiti wa CCN mkoa wa Kilimanjaro Iddi Juma alipowasili na Sendeka, Ofisi ya CCM mkoa huo leo. Katikati ni Mkuu wa Wialaya ya Moshi Novatus Makunga
 Msemaji Mkuu wa CCM, Christopher Ole Sendeka akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Juma Iddi alipowasili katika Ofisi ya CCM mkoa huo leo kuanza ziara ya kikazi. Kulia ni Mkuu wa wilaya ya Moshi Novatus Makunga.
 Msemaji Mkuu wa CCM, Christopher Ole Sendeka akiiingia ukumbini kuzungumza na wajumbe wa  Sekretarieti ya CCM kutoka wilaya za mkoa wa Kilimanjaro, leo.
 Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM kutoka wilaya za mkoa wa Kilimanjaro wakimpokea Ole Sendeka alipoingia ukumbini
 Ole Sendeka baada ya kuingia ukumbini
 Msemaji Mkuu wa CCM, Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili ukumbini kuzungumza na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM kutoka wilaya za mkoa wa Kilimanjaro leo
Msemaji Mkuu wa CCM, Ole Sendeka akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili ukumbini kuzungumza na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM kutoka wilaya za mkoa wa Kilimanjaro leo 
Wajumbe wakiwa ukumbini kusmikiliza Ole Sendka
 Msemaji wa CCM, Cheristopher Ole Sendeka akizungumza na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM wilaya za mkoa wa Kilimanjaro baada ya kuwasili akiwa katika ziara ya kikazi leo.
Msemaji wa CCM, Cheristopher Ole Sendeka akizungumza na wajumbe wa Sekretarieti ya CCM wilaya za mkoa wa Kilimanjaro baada ya kuwasili akiwa katika ziara ya kikazi leo. Picha na Bashir Nkoromo).

TAKUKURU MKOANI PWANI YAZITAJA TAASISI NA IDARA 11 ZINAZOONGOZA KWA MALALAMIKO YA VITENDO VYA RUSHWA

ki1
Kamanda wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa Takukuru Mkoa wa Pwani Suzan Rymond  akiwaonyesha waandishi wa  habari ofisini kwake hawapo pichani orodha ya  majina ya taasisi na idara ambazo  zimeongoza kwa malalamiko ya vitendo vya rushwa (Picha na Victor Masangu)
ki2
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika mkutano huo wa Takukuru.
……………………………………………………………………………………………
 NA VICTOR MASANGU, PWANI
TAASISI ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU Mkoani Pwani imezitaja taasisi na idara zipatazo 11 ambazo zimelalamikiwa  kuhusika katika  matukio mbali mbali  ya vitendo vya kupokea rushwa kinyume kabisa na

TAMISEMI MKOANI MWANZA YAONGOZA KWA RUSHWA.

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rusha Mkoani Mwanza (Pichani) Mhandisi Ernest Makale, leo ametoa taarifa ya Utendaji kazi wa taasisi hiyo mbele ya Wanahabari katika kipindi cha robo mwaka (Januari hadi Machi) mwaka huu.

Katika taarifa hiyo, Mhandisi Makale amebainisha kuwa Takukuru imepokea jumla ya malalamiko 45 yanayohusiana na vitendo vya rushwa kutoka kwa wananchi ambapo katika malalamiko hayo, 27 yameelekezwa kwa watumishi wa idara za Serikali za Mitaa TAMISEMI hiyo ikiwa ni sawa na asilimia 60. Kati ya malalamiko hayo 27, malalamiko 13 yameelekezwa katika idara ya ardhi.

(TUMA) KIMELITAKA BARAZA LA SANAA LA TANZANIA KUTOFUNGIA MATAMASHA YA WASANII BILA KUSHIRIKISHWA

1Katibu Mkuu wa CHAMA cha Muziki wa kizazi kipya Tanzania Urban Music Association (TUMA), Samweli Andrew Mbwana maarufu kama Briton (kulia) akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jijini Dar es Salaam juu ya uundaji wa kamati na viongozi wa kamati ndani ya chama hicho, kushoto ni Afisa uhusino wa Chama hicho, Bagdad Kweka.
2Katibu Mkuu wa TUMA, Samweli Andrew Mbwana maarufu kama Briton (kulia) akionesha baadhi ya kadi za wanachama waliojiunga na chama cha wasanii TUMA,kushoto ni Afisa Uhusino wa Chama hicho, Bagdad Kweka.

RAIS SHEIN AKUTANA MAKAMO WA RAIS WA KOICA

DK1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Makamo wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea Kusini “KOICA GLOBAL” Bw.Kwon  Taemyon akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo pamoja na mwenyeji wa Ujumbe huo Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe,Hamad Rashid Mohamed(hayupo pichani),[Picha na Ikulu.]
DK2
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)  akizungumza na  Makamo wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea Kusini “KOICA GLOBAL” Bw.Kwon  Taemyon akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo pamoja na mwenyeji wa Ujumbe huo Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe,Hamad Rashid Mohamed(hayupo pichani),[Picha na Ikulu.]
DK3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati)  akizungumza na  Makamo wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea Kusini “KOICA GLOBAL” Bw.Kwon  Taemyon (wa pili kushoto) akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo pamoja na mwenyeji wa Ujumbe huo Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe,Hamad Rashid Mohamed(wa pili kulia) akiwepo Katibu Mkuu Kiongozi Dkt.Abdulhamid Yahya Mzee(kulia),[Picha na Ikulu.]
DK4
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia)  akiagana na   Makamo wa Rais wa Shirika la Maendeleo la Korea Kusini “KOICA GLOBAL” Bw.Kwon  Taemyon baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika ukumbi wa  Ikulu Mjini Zanzibar leo (katikati) Waziri wa Kilimo,Maliasili,Mifugo na Uvuvi Mhe,Hamad Rashid Mohamed,[Picha na Ikulu.]

MBUNGE WA CHAMA CHA WAZALENDO ACT-TANZANIA AKUTANA NA WATANZANIA NEW YORK CITY

Zitto Kabwe Mbunge wa Kigoma Kaskazini akisisitiza jambo mbele ya vijana wa Kitanzania waishio New York. Zitto alipata nafasi ya kuongea na vijana hao waliotaka kujua maendeleo ya nchi yao na changamoto zake ndani ya bunge la jamhuri anavyowakilisha hoja zake kwa faida ya wananchi kupitia upinzani, pia yeye kama mwana siasa alie upande wa upinzani nini mtazamo wake juu ya kasi ya rais wa wamu ya 5. Zitto ni mmoja ya vijana kwenye Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania na ni Mbunge mwenye nguvu na uwezo wa kuwakirisha hoja zenye mashiko ndani ya bunge la jamhuri na kuitikisa serikali ya chama tawala. Mfano mmoja ni suala la Escrow yeye ndiyo alikuwa chanzo cha habari hiyo iliyotikisa serikali na kupelekea wananchi kukosa imani na mwenendo mzima wa serikali ya chama tawala. Na pia alisha wasilisha hoja ya Buzwagi ilisababisha Zitto kusimamishwa ubunge kwa miezi 4. Zitto yupo New York City kwa kivuli cha World Bank na pia alipata nafasi ya kutembelea Columbia University  New York na kuongea na wasomi wa huko na pia atapata nafasi ya kutembelea Harvard University huko Boston. MA.  Picha na Vijimambo Blog New York
Zitto akipata ukodak baada ya kukutana na Watanzania New York City. Kwa taswira   zaidi nenda soma zaidi.

MWAKILISHI MPYA WA UNHCR NCHINI AJITAMBULISHA KWA WAZIRI KITWANGA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI

W1 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (katikati), akimkaribisha ofisini kwake Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati alipokuwa anawasili ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha kwa Waziri huyo mara baada ya kuteuliwa na Shirika lake kuja kuiongoza UNHCR nchini. Hata hivyo, viongozi hao katika mazungumzo yao walijadiliana masuala mbalimbali jinsi wa kuwahudumia wakimbizi waliopo nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke.
W2 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kulia), akimfafanulia jambo Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya wakati Mwakilishi huyo alipomtembelea Waziri Kitwanga ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha baada ya kuteuliwa na UNHCR kuja kuwa kiongozi wa Shirika hilo nchini.
W3 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto), akimfafanulia jambo Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (kulia) wakati Mwakilishi huyo alipomtembelea Naibu Waziri huyo ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha baada ya kuteuliwa na UNHCR kuja kuwa kiongozi wa Shirika hilo nchini. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke. Katikati ni Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika hilo, Yoko Akasaka, na Afisa wa Shirika hilo nchini, Daria Santoni (wa pili kulia).
W4Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (kushoto) akimfafanulia jambo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga wakati Mwakilishi huyo mpya nchini alipomtembelea Waziri huyo ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha mara baada ya kuteuliwa na UNHCR kuwa kiongozi wa Shirika hilo nchini.
W5 
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mwakilishi Mkazi mpya wa Shirika la Kimataifa la Kuwahudumia Wakimbizi (UNHCR), Chansa Kapaya (katikati), pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Wakimbizi nchini, Harrison Mseke. Kapaya ameteuliwa na UNHCR kuwa Mwakilishi wa Shirika hilo nchini na amemtembelea Waziri Kitwanga ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha, hata hivyo katika mazungumzo yao walijadiliana masuala mbalimbali ya jinsi ya kuwahudumia Wakimbizi waliopo nchini.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA AFUNGUA MKUTANO WA KWANZA UNAOJADILI SEKTA BINAFSI KATIKA KULETA MAENDELEO ENDELEVU NCHINI

M2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua mkutano wa kwanza unaojadili kuhusu kuangalia Biashara na Sekta Binafsi katika kuleta Maendeleo endelevu Nchini kwa ajili ya kufikia malengo 17 ya Maendeleo kwa Jamii. Mkutano huo ulioandaliwa na AFRIKA SUSTAINABLE BUSINESS umefunguliwa Leo April 14,2016 katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar es salaam.     
M1 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Afisa Mtendaji Mkuu wa AFRIKA SUSTAINABLE BUSINESS Bw. Raymond Mubayiwa kabla ya kufungua mkutano wa kwanza unaojadili kuhusu kuangalia Biashara na Sekta Binafsi katika kuleta Maendeleo endelevu Nchini kwa ajili ya kufikia malengo 17 ya Maendeleo kwa Jamii. Mkutano huo umefunguliwa Leo April 14,2016 katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar es salaam.  
M3 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na watendaji na washiriki wa Mkutano wa kwanza unaojadili kuhusu kuangalia Biashara na Sekta Binafsi katika kuleta Maendeleo endelevu Nchini kwa ajili ya kufikia malengo 17 ya Maendeleo kwa Jamii baada ya kufungua Mkutano huo Leo April 14,2016 katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar es salaam.
(Picha na OMR)    

MUDA WA UZIMAJI SIMU FEKI HAUTAONGEZWA- Makame Mbarawa

index 
Waziri  wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiiano Profesa Makame  Mbarawa amesema Serikali haitaongeza muda katika zoezi zima la uzimaji wa simu feki ifikapo Juni 16 mwaka huu.
Ameyasema hayo ofisini kwake leo jijini Dar es salaam wakati wa mahojiano na kituo kimoja cha habari hapa nchini .

KAIMU KATIBU MKUU WA UVCCM TAIFA SHAKHA HAMDU SHAKA AWASILI WILAYA YA NGORONGORO KUHUTUBIA MKUTANO WA HADHARA

 Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa Shakha Hamdu Shakha akihutubia wafugaji
katika wilaya ya Ngorongoro katika wilaya hiyo
Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM Shakha Hamdu Shakha (wanne kushoto)  akiwasili
katika wilaya ya Ngorongoro ambapo alifanya mkutano wa hadhara na kuzindua
matawi ya chama  katika wilaya hiyo.wakwanza mstari wa mbele ni Mwenyekiti
wa UVCCM Arusha Lengai Ole Sabaya .
(PICHA NA WOINDE SHIZZA,NGORONGORO)

CZECH KUBORESHA UHUSIANO NA TANZANIA


N1 
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kutoka Jamhuri ya Czech, Zdenek Adamec ak
iweka sahihi kwenye kitabu cha wageni Ofisini kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani (Hayupo pichani).
N2 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Medard Kalemani akizungumza katika kikao chake na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Czech, Zdenek Adamec (Hayupo pichani) kilichofanyika jijini Dar es Salaam.
DORNALD
Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Dk. Meldad Kalemani akizungumza na Dk. Mturi Arnold Meneja miradi ya Czech Republic katika kampuni ya Tanzania House of Business Company Limited huku Bw. Zdenek Adamec  katikati Naibu Waziri wa Viwanda wa Jamhuri ya Czech akisikiliza. 
N3 
Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Dkt Medard Kalemani (mwenye tai nyekundu), akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara kutoka Jamhuri ya Czech, Zdenek Adamec (Kushoto kwake), Meneja Mradi wa Czech nchini, Dkt. Mturi Arnold (mwenye suti ya kahawia), kulia ni Mrs. Olivia Maboko  wa idaraya Ulaya na Americas katika  wizara ya mambo ya nje wakiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji wa wizara ya Nishati na Madini.
……………………………………………………………………………………

TAA WATANZANIA WATAKIWA KUTUMIA MIFUMO YA PESA KWA NJIA YA SIMU ILI WAWEZE KUKUZA UCHUMI WAO

Mwenyekiti wa Africa Digital Banking Summit, Baraka Mtavangu akizungumza kuhusu mkutano huo.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji akitoa hotuba katika mkutano huo.
Baadhi ya washiriki walioshiriki mkutano huo unaofanyika kwa siku mbili.
Meneja Mifumo ya Malipo wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Bernard Dadi akitoa taarifa kuhusu matumizi ya mobile banking nchini.
Mkurugenzi mkazi wa Kupatana.com, Makusaro Tesha akiwasilisha mada katika mkutano huo.
Mkurugenzi Mkakati wa Jackson Group Ltd, Kelvin Twissa akitoa mada katika mkutano huo.

Fastjet yatoa ofa nauli za Kilimanjaro, Mbeya na Mwanza

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Dar es Salaam, 12 Aprili 2016-Shirika la ndege la bei nafuu, fastjet, limetangaza punguzo la nauli la sh. 22,000/- kwa mwezi huu wa Aprili kwenye safari zake za Kilimanjaro, Mbeya na Mwanza.
Kulingana na Afisa Masoko na Uhusiano wa Umma wa fastjet, Lucy Mbogoro, ofa hiyo ijulikanayo kama JET10 imeanza kuanzia mwanzo wa April na itamalizika tarehe 30 Aprili 2016.
“Ofa hii kutoka fastjet inaashiria kwa mara nyingine tena jinsi shirika letu linavyosikiliza matakwa ya wateja wake”, alisema Mbogoro.
Mbogoro alisema kwamba wateja wanaweza kilipia nauli zao kupitia mitandao ya Tigo-Pesa, Airtel Money, M-Pesa and pia kupitia NMB Mobile Cash katika tawi lolote la Benki ya NMB.
“Wateja wanashauriwa kukata tiketi mapema ili kufurahia nauli za bei nafuu zaidi na pia wanaweza kulipia kupitia m.fastjet.com or www.fastjet.com.” alishauri Mbogoro.

No comments :

Post a Comment