Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto),
wakipongezana Mara baada ya kutiliana saini makubaliano ya usafiri wa
anga baina ya nchi hizo mbili jijini Dar es Salaam leo Machi 29, 2016.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto) wakielekezwa na wanasheria wao jinsi ya kusaini hati
za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla
hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es
Salaam, leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto)
wakibadilishana hati za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait
na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara
hiyo jijini Dar es Salaam, leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kulia) akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto) mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kusaini makubaliaono
ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika
katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Kulia) akimsikilza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait Mhandisi Yousef Al Fozan (kushoto) wakati wa hafla ya kusaini makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania, jijini Dar es Salaam, leo
Baadhi ya maofisa wa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakimsikiliza kwa makini waziri wa wizara hiyo Profesa Makame Mbarawa wapili (kutoka kushoto) wakati wa hafla ya kusaini makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania, jijini Dar es Salaam, leo
Baadhi
ya wadau wa masuala ya usafiri wa Anga wakiwa katika hafla ya
utilianaji saini ya makubariano ya usafiri wa Anga baina ya Tanzania na
Nchi ya Kuwait.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (wapili kulia) akisisitiza jambo kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Kuwait Mhandisi Yousef Al Fozan , (kushoto) aliyeongozana na maofisa wake wakati walipowasili ofisini kwake jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kusaini makubaliano ya safari za Anga baina ya Tanzania na Kuwait. Wapili kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya kati wa Wizara hiyo,Balozi Abdallah Kilima na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ua Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa na Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Kuwait Mhandisi Yousef Al Fozan ,
wakipongeza na mara baada ya kutiliana makubakliano ya Usafiri wa Anga
baina ya Tanzania na Kuwait.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma
za Jamii, Peter Serukamba (kushoto), Wajumbe wa kamati hiyo na
Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Banakunu (kulia), wakitembea
wakati kamati hiyo ilipotembelea MSD Makao Makuu Keko Dar es Salaam leo
asubuhi.
Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi wa MSD, Mary
Lingo (wa pili kulia), akiwaelekeza wajumbe wa kamati hiyo jinsi dawa
zinavyotunzwa katika maghala.
Mkurugenzi wa MSD, Laurean Banakunu (katikati mbele), akiwaongoza wajumbe wa kamati hiyo walipotembelea MSD leo.
Mjumbe wa kamati hiyo, Azani Zungu akiuliza swali juu ya kuharibika kwa dawa.
Na Mwandishi Wetu
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Huduma ya
Jamii imetembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa Keko na kuipongeza kwa
utendaji wake kazi pamoja na mazingira magumu yanayoikabili.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Peter
Serukamba amesema Kamati yake itasimamiana kuyafanyia kazi masuala
makubwa manne ambayo ni pamoja na bajeti finyu ya dawa, ulipwaji
wa deni la serikali, mfumo wa uwajibikaji kati ya Tamisemi na Wizara ya
Afya ambao unasababisha utekelezaji na usimamizi wa masuala ya Afya
kutokuwa na mtiririko kutoka juu kwenda chini.
Jambo la nne ni kuhakikisha utekelezaji wa kuongeza uzalishaji dawa ndani ya nchi kupitia sekta binafsi (PPP).
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya,
Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kingwangala
alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha Bohari ya Dawa inanunua
dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji kwa bei nafuu, hivyo Serikali
imeweka kipaumbele kuhakikisha deni la MSD linalipwa mapema
iwezekanavyo.
Alisema tayari Wizara ya Afya imeiagiza
MSD kuandaa bei elekezi kwa maduka maalum ya dawa (prime vendor) ili
vituo vinavyokosa dawa MSD vinunue huko bila usumbufu na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa dawa na vifaa tiba.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu ameviomba vituo vya Afya kuleta mahitaji yao kwa wakati.
Mfanyabiashara
Davis Mosha akiwa na mshindi wa kwanza katika mashindano ya Mbio za
magari yaliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Moshi,Gurjit Dhan (kushoto)
akiwa na msoma ramani wake Shameer Yusuf (kulia).
Mshindi wa pili katika mbio za magari ,Piero Canobbio (kushoto) akiwa na msoma ramani wake Silvia Frigo.
Mshindi wa tatu katika mashindano hayo Gurpa Sandhu (kushoto) akiwa na msoma ramani wake Davie Sihoka.
Mshiriki wa Mbiio za magari kutoka Morogoro Bob Taylor akipokea kikombe baada ya kumaliza akiwa katika top ten.
Zawadi mbalimbali zilizotolewa kwa washiriki wa mashindano hayo ya Vaisakh Rally ambayo hufanyika kila mwaka mkoani Kilimanjaro.
Mshindi
wa kwanza katika Mashindano ya mbio za magari ,Gurjit Dhan (Kulia)
akizungumza jambo na mshindi wa pili wa mbio hizo Piero Canobbio kutoka
nchini Kenya.
Wageni rasmi katika mkutano huo,
Wa kwanza kushoto ni Mtafiti kutoka Taasisi ya Mtandao wa Kutathimini
Sera za Chakula, Kilimo na Maliasili (FANRPAN), Njongenhle Nyoni,
Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF),
Dkt. Tausi Kida na Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya
Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande Natai.
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara
ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhakikisha inawasaidia wakulima
kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yanaonekana kuendelea
kuikabili nchi.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo
cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande
Natai alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano
ulioandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) na Taasisi
ya Mtandao wa Kutathimini Sera za Chakula, Kilimo na Maliasili (FANRPAN)
ili kujadili mpango wa Kilimo Salama (CSA).
Bi. Natai alisema serikali inatambua
uwepo wa mabadiliko ya Tabia ya Nchi na kwasasa tayari wataalamu
wanafanya tafiti ili waone ni jinsi gani wanaweza kuwasaidia wakulima
kupambana na mabadiliko hayo.

























No comments :
Post a Comment