Wednesday, March 30, 2016

TANZANIA NA KUWAIT, WASAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA USAFIRI WA ANGA





Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (kulia)  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan  (kushoto), wakipongezana Mara baada ya kutiliana saini makubaliano ya usafiri wa anga baina ya nchi hizo mbili jijini Dar es Salaam leo Machi 29, 2016.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (kulia)  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan  (kushoto) wakielekezwa na wanasheria wao jinsi ya  kusaini  hati za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (kulia)  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi Yousef Al Fozan  (kushoto) wakibadilishana hati za makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (kulia)  akikabidhiwa zawadi na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini Kuwait ,Mhandisi  Yousef Al Fozan  (kushoto)   mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kusaini makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania , hafla hiyo ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam, leo.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (Kulia) akimsikilza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga nchini Kuwait  Mhandisi  Yousef Al Fozan  (kushoto)    wakati wa hafla ya kusaini  makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania, jijini Dar es Salaam, leo
Baadhi ya maofisa wa  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wakimsikiliza kwa makini waziri wa wizara hiyo Profesa Makame Mbarawa   wapili (kutoka kushoto) wakati wa hafla ya kusaini  makubaliaono ya Usafiri wa Anga baina ya Kuwait na Tanzania, jijini Dar es Salaam, leo
Baadhi ya wadau wa masuala ya usafiri wa Anga wakiwa katika hafla ya utilianaji saini ya makubariano ya usafiri wa Anga baina ya Tanzania na Nchi ya Kuwait.
 
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa   (wapili kulia) akisisitiza jambo   kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga Kuwait Mhandisi  Yousef Al Fozan , (kushoto)   aliyeongozana na maofisa wake wakati walipowasili ofisini kwake jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya  kusaini makubaliano ya safari za Anga baina ya Tanzania na Kuwait.  Wapili kutoka kulia ni  Mkurugenzi wa Idara  ya Mashariki ya kati  wa Wizara hiyo,Balozi Abdallah Kilima na  Mkurugenzi  Mkuu wa Mamlaka ua Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) Hamza Johari.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa  na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Usafiri wa Anga  Kuwait Mhandisi  Yousef Al Fozan , wakipongeza na mara baada ya kutiliana makubakliano ya Usafiri wa Anga baina ya Tanzania na Kuwait.

 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, Peter Serukamba (kushoto), Wajumbe wa kamati hiyo na Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean Banakunu (kulia), wakitembea wakati kamati hiyo ilipotembelea MSD Makao Makuu Keko Dar es Salaam leo asubuhi.
 Kaimu Mkurugenzi wa Ugavi wa MSD, Mary Lingo (wa pili kulia), akiwaelekeza wajumbe wa kamati hiyo jinsi dawa zinavyotunzwa katika maghala.
 Mkurugenzi wa MSD, Laurean Banakunu (katikati mbele), akiwaongoza wajumbe wa kamati hiyo walipotembelea MSD leo.
Mjumbe wa kamati hiyo, Azani Zungu akiuliza swali juu ya kuharibika kwa dawa.

Na Mwandishi Wetu

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Huduma ya Jamii imetembelea Makao Makuu ya Bohari ya Dawa Keko na kuipongeza kwa utendaji wake kazi pamoja na mazingira magumu yanayoikabili.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Peter Serukamba amesema Kamati yake itasimamiana kuyafanyia kazi masuala makubwa manne ambayo ni pamoja na bajeti finyu ya dawa, ulipwaji wa deni la serikali, mfumo wa uwajibikaji kati ya Tamisemi na Wizara ya Afya ambao unasababisha utekelezaji na usimamizi wa masuala ya Afya kutokuwa na mtiririko kutoka juu kwenda chini. 

Jambo la nne ni kuhakikisha utekelezaji wa kuongeza uzalishaji dawa ndani ya nchi kupitia sekta binafsi (PPP).

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamis Kingwangala alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha Bohari ya Dawa inanunua dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji kwa bei nafuu, hivyo Serikali imeweka kipaumbele kuhakikisha deni la MSD linalipwa mapema iwezekanavyo.

Alisema tayari Wizara ya Afya imeiagiza MSD kuandaa bei elekezi kwa maduka maalum ya dawa (prime vendor) ili vituo vinavyokosa dawa MSD vinunue huko bila usumbufu na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa dawa na vifaa tiba.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu ameviomba vituo vya Afya kuleta mahitaji yao kwa wakati.

Mfanyabiashara Davis Mosha akiwa na mshindi wa kwanza katika mashindano ya Mbio za magari yaliyofanyika mwishoni mwa wiki mjini Moshi,Gurjit Dhan (kushoto) akiwa na msoma ramani wake Shameer Yusuf (kulia).
Mshindi wa pili katika mbio za magari ,Piero Canobbio (kushoto) akiwa na msoma ramani wake Silvia Frigo.
Mshindi wa tatu katika mashindano hayo Gurpa Sandhu (kushoto) akiwa na msoma ramani wake Davie Sihoka.
Mshiriki wa Mbiio za magari kutoka Morogoro Bob Taylor akipokea kikombe baada ya kumaliza akiwa katika top ten.
Zawadi mbalimbali zilizotolewa kwa washiriki wa mashindano hayo ya Vaisakh Rally ambayo hufanyika kila mwaka mkoani Kilimanjaro.
Mfanyabiashara Davis Mosha akizungumza mara baada ya kukabidhi zawadi kwa washindi.
Washindi wakiwa katika picha ya pamoja na waandaaji wa mbio hizo.
Zawadi mbalimbali zilizotolewa kwa washindi pamoja na waandaaji.
Mshindi wa kwanza katika Mashindano ya mbio za magari ,Gurjit Dhan (Kulia) akizungumza jambo na mshindi wa pili wa mbio hizo Piero Canobbio kutoka nchini Kenya.
Baadhi ya magari yaliyoshiriki mbio hizo.
Mashabiki wakiwa katika eneo mojawapo wakifuatilia mbio hizo.
Moja ya gari la mashindano kikivutwa mata baada ya kupata hitilafu.
Baadhi ya magari yakiwa katika mbio hizo.
Magari mengine yalilazimika kutembea bila ya gurudumu baada ya kupata hitilafu.
DSC_1667
Wageni rasmi katika mkutano huo, Wa kwanza kushoto ni Mtafiti kutoka Taasisi ya Mtandao wa Kutathimini Sera za Chakula, Kilimo na Maliasili (FANRPAN), Njongenhle Nyoni, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida na Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande Natai.
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi imejipanga kuhakikisha inawasaidia wakulima kupambana na mabadiliko ya tabia ya nchi ambayo yanaonekana kuendelea kuikabili nchi.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Mazingira kutoka Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Bi. Shakwaanande Natai alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano ulioandaliwa na Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF) na Taasisi ya Mtandao wa Kutathimini Sera za Chakula, Kilimo na Maliasili (FANRPAN) ili kujadili mpango wa Kilimo Salama (CSA).
Bi. Natai alisema serikali inatambua uwepo wa mabadiliko ya Tabia ya Nchi na kwasasa tayari wataalamu wanafanya tafiti ili waone ni jinsi gani wanaweza kuwasaidia wakulima kupambana na mabadiliko hayo.

No comments :

Post a Comment