Friday, March 25, 2016

MKURUGENZI MKUU MPYA WA NSSF ATEMBELEA DARAJA LA KIGAMBONI


Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara  akisalimiana na Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi wa NSSF, Yacoub Kidula.
Wataalamu wa ujenzi wa daraja la Kigamboni wakisalimiana na Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara.
Barabara za kuingilia darajani upande wa Kurasini.
Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo akionyesha njia za kuingia na kutoka darajani
Barabara ya kuingilia darajani upande wa kushoto na barabara ya kutokea mjini upande wa kulia. 
Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Prof. Godius Kahyarara  (wa tatu kushoto) akipata maelezo kutoka kwa wahandisi wa ujenzi wa daraja la Kigamboni wakati wa ziara yake ya kutembelea daraja la Kigamboni. 
Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo akifafanua jambo
kwa Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),
Prof. Godius Kahyarara  (katika) alipotembelea daraja wa Kigamboni
jijini Dar es Salaam, daraja hilo linatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni baada ya kumalizika kwa ujenzi wake

MABADILIKO YA RATIBA SHUGHULI ZA KAMATI ZA BUNGE

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BUNGE LA TANZANIA
index 
TAARIFA KWA UMMA
Kufuatia mabadiliko ya tarehe ya kupokea Mapendekezo ya Mpango na kiwango cha Ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017, Ofisi ya Bunge imefanya mabadiliko ya tarehe za shughuli za Kamati za Bunge kuelekea Mkutano wa tatu wa Bunge (Mkutano wa Bajeti) ili kuendana na masharti ya Kanuni za Bunge kuhusu shughuli hizo. Kwa mabadiliko hayo , ratiba ya shughuli za Kamati itakuwa kama ifuatavyo:-
  1. Tarehe 29/3/2016 hadi tarehe 4/4/2016 Kamati za Kudumu za Kisekta zitatembelea na kukagua utekelezaji wa miradi iliyotengewa Fedha kwa Mwaka wa Fedha 2015/2016 kwa mujibu wa Kanuni ya 98(1) ya Kanuni za Bunge. Hapo awali kazi hii ilipangwa kufanyika tarehe 31/3/2016 hadi 6/4/2016.
  1. Tarehe 5/4/2016 – Kwa mujibu wa Kanuni ya 96 ya Kanuni za Bunge, Serikali itawasilisha Dondoo na Randama za Vitabu vya Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. Awali kazi hii ilipangwa kufanyika tarehe 29/3/2016;
  1. Tarehe 6/4/2016 – Kwa mujibu wa Kanuni ya 97(1)-(2) ya Kanuni za Bunge kutakuwa na Mkutano wa Wabunge wote ambapo Serikali itawasilisha Mapendekezo ya Mpango na kiwango cha ukomo wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017. Awali kazi hii ilipangwa kufanyika tarehe 30/3/2016;
  1. Tarehe 7/4/2016 hadi 15/4/2016 – Kwa mujibu wa Kanuni ya 98 (2) ya Kanuni za Bunge, kwa kipindi cha siku tisa (9) Kamati za Kudumu za Kisekta zitachambua taarifa za utekelezaji wa Bajeti za Wizara zinazosimamiwa na Kamati hizo. Katika kipindi hicho, Kamati ya Bajeti itafanya uchambuzi wa Mapendekezo ya Mpango na kiwango cha ukomo wa Bajeti kwa Mwaka
wa fedha 2016/2017. Awali Kamati ya Bajeti ingefanya kazi hii kuanzia tarehe 31/3/2016 hadi 6/4/2016;
  1. Tarehe 15/4/2016 – Kwa mujibu wa Kanuni ya 98(3) ya Kanuni za Bunge kutakuwa na Kikao cha pamoja kati ya Kamati ya Uongozi na Kamati ya Bajeti ili kujadili mambo muhimu yaliyojitokeza kwenye Kamati za Kisekta wakati wa kujadili utekelezaji wa Bajeti za Wizara mbalimbali;
  1. Tarehe 16 na 17 Aprili, 2016 kama ilivyokuwa imepangwa awali Wabunge wataelekea Dodoma tayari kwa Shughuli za Mkutano wa Tatu wa Bunge ambao utaanza tarehe 19 Aprili, 2016.
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano Ofisi ya Bunge
DAR ES SALAAM
25 Machi, 2016.

Zaidi ya watu 150 wamejitokeza kuhakiki silaha zao.

diwani_athumaniNa. Immaculate Makilika –MAELEZO
……………………………………..
Mkurugenzi  wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi Diwani Athumani amesema hadi kufikia sasa zaidi ya watu 150  wamejitokeza  kuhakiki wa  silaha zao, katika hatua ya  kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul  Makonda.

WAGOMBEA USPIKA BUNGE LAWAWAKILISHI ZANZIBAR WAMKATAA KIFICHO

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
……………………………………….
HEKAHEKA zimeanza Visiwani Zanzibar ambapo wagombea nafasi ya Uspika wa Bunge la Wawakilishi wameanza kupigana vikumbo kuwania nafasi hiyo huku sura mpya za vijana wenye damu mbichi zikijitokeza kuchuana na mkongwe aliyechukua tena fomu ya kutetea nafasi yake Mhe Pandu Ameri Kificho.
Kificho ni Spika wa Bunge la Wawakilishi kwa muda wamiaka 25 sasa ambapo wanachama wa CCM Zanzibar tayari wameanza kutilia mashaka uamuazi wa spika huyo aliyechukua fomu za kugombea tena akitaka kuendelea na kuongoza kiti cha uspika kwa kipindi cha miaka mitano ijayo, jambo, inalozua maswali mengi yasiyo na majibu.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO ASHUHUDIA KUORODHESHWA KWA HISA STAHILI ZA MAENDELEO BANK PLC, KATIKA SOKO LA HISA LA DAR ES SALAAM (DSE)

Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji, Mwenyekiti wa Maendeleo Benki, Amulike Ngeliama (kushoto) na Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na Mipango wa(CMSA) Nicodemus Mukama wakifuatilia jambo katika hafla hiyo.
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji akipiga kengele kuashiria uorodheshwaji rasmi wa Maendeleo Benki katika soko la hisa DSE jana. Kushoto ni Mwenyekiti wa Maendeleo Benki, Amulike Ngeliama na Mkurugenzi wa Capital Markets na Securities Authoriy (CMSA) Nicodemus Mukama 
Emmanuel Nyalali, Mkuu wa Kitengo cha Uendeshaji DSE akizungumza katika hafla hiyo. 
Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Dkt. Ashatu Kijaji akiongea wakati wa hafla ya kuorodheshwa kwa Maendeleo Benki katika soko la hisa DSE
Mkurugenzi mtendaji wa Maendeleo Benki, Ibrahim Mwangalaba akitoa hotuba yake kabla ya kumkaribisah Mwenyekiti wa Benki hiyo kuzungumza na washiriki wa hafla hiyo. 
……………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
Bank PLC ni benki iliyoanzishwa na Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mashariki na Pwani na inamilikiwa na Wananchi mbalimbali kwa njia ya HISA bila kujali, kabila, itikadi, dini wala rangi, kwani benki hii imesajiliwa na soko la hisa la Dar es Salaam (DSE), kupitia dirisha dogo yaani Enterprise Growth Market (EGM) na inaendeshwa kwa kufuata taratibu zote za BOT na Soko la Hisa la Dar es S alaam. Maendeleo Bank ilianza kutoa huduma za kibenki tarehe 9/9/2013 baada ya kupewa leseni na Benki Kuu ya Tanzania na tarehe 05/11/2013 ilisajiliwa rasmi katika soko la hisa la Dar es Salaam baada ya kukidhi vigezo vyote vilivyowekwa na mamlaka husika. Benki hii ilianza na mtaji wa shilingi bilioni 4.5 kutoka kwa wanahisa zaidi ya 3,000 wa rika na itikadi mbalimbali walionunua wakati wa mauzo ya awali (IPO) yaliyofanyika mwaka 2013.
Tarehe 9/11/2015 benki ilipata kibali cha kuuza hisa stahili ambapo matarajio yake yalikuwa kupata shilingi bilioni 3.06 ambazo zitatumika kuimarisha shughuli za uendeshaji wa benki pamoja na kuongeza matawi. Katika zoezi la uuzaji wa hisa stahili benki imeweza kupata jumla ya shilingi bilioni 2.8 na kufikisha jumla ya mtaji wa benki kuwa shilingi bilioni 7.3.
Kusudi kubwa la kuanzishwa kwa Maendeleo Bank PLC ni kufikisha huduma za kibenki kwa wananchi wa kipato cha chini na cha kati kwani hao ndio walio wengi na upatikanaji wa huduma za kibenki kwao ni changamoto kubwa. Benki hii imepata mafanikio mengi tangia kuanzishwa kwake takribani miaka miwili iliyopita ambapo mpaka tarehe 31/12/2015, benki imefikisha wateja zaidi ya 12,000, amana zaidi ya shilingi bilioni 46.0, mali za benki zimefikia zaidi ya shilingi bilioni 55, imetoa mikopo zaidi ya shilini bilioni 21.0 na mwaka 2015 imepata faida ya takribani shilingi milioni 200.0 baada ya kodi. 
Benki hii inatoa huduma mbalimbali za ubunifu ambazo zinawalenga wananchi wa kada mbalimbali, zikiwemo: huduma za kibenki kwa njia ya simu, huduma za BIMA, ATM kupitia mtandao wa UMOJA Switch, akaunti mbalimbali zenye gharama rafiki, kutuma na kupokea pesa kutoka nje na ndani ya nchi, na kutoa mikopo ya aina mbalimbali, ikiwemo kwa wajasiliamali wadogo ambayo haina dhamana, yaani mikopo ya vikundi. 

DAKTARI BINGWA WA MAGONJWA YA MOYO, STEPHAN P. MASATU KUENDESHA HUDUMA YA UCHUNGUZI WA MARADHI YA MOYO MKOANI KIGOMA

DAKTARI bingwa wa magonjwa ya moyo, Dkt. Stephan P. Masatu
………………………………………………………………………
 NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
WATU wanaosumbuliwa na maradhi ya Moyo mkoani Kigoma, watapata faraja kubwa mapema Aprili 4 hadi 9, 2016, kufuatia uwepo wa huduma za uchunguzi wa maradhi hayo utakaofanywa na Daktari Bingwa wa magonjwa ya Moyo, Dkt. Stephan P. Masatu, kutoka jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jijini Dar es Salaam, Dkt. Masatu alisema, huduma zote za magonjwa ya moyo ikiwa ni pamoja na vipimo vya ECG na ECHO zitatolewa kuanzia asubuhi kwenye hospitali ya kibinafsi ya Upendo iliyo jirani na soko kuu la mkoani Kigoma.
Mkoa wa Kigoma ni miongoni mwa mikoa iliyo pembezoni mwa nchi na zinakabiliwa na upungufu wa wataalamu wa kushughulikia magonjwa kama ya Moyo na kutokana na uchache wa wataalamu hao, itakuwa ni nafasi nzuri kwa wananchi wa mkoa huo pamoja na vitongoji vyake, kujitokeza ili kuhudumiwa ambapo kliniki hiyo itadumu kwa muda wa siku sita mfululizo.
Dkt. Masatu akitumia mashine ya kupima ECHO, mmoja wa wagonjwa wa moyo

WANAFUNZI WA FEZA BOYS HIGH SCHOOL WATEMBELEA VIRGINIA INTERNATIONAL UNIVERSITY

Wanafunzi wa Feza Boys High School kutoka jijini Dar es Salaam wakipata picha ya pamoja walipokua Virginia International University iliyopo jimbo la Virginia siku ya Alhamisi March 24, 2016, wanafunzi hao wapo kwa ziara maalum ya kuangalia uwezekano wa kujiunga na chuo hicho katika masomo ya juu.
 Makamu Rais wa Chuo hicho Dr. Suleyman Bahceci (kulia) akiwaeleza wanafunzi hao taratibu za kufuata kwa ajili ya kujiunga na VIU
Kushoto ni Alex Luketa Mtanzania anayefanyakazi chuoni hapo kwa ajili ya kusajili wanafunzi kutoka Afrika Mashariki akiwa pamoja na wanafunzi wa Feza Boys High School wakimsikiliza Makamu Rais wa chuo (hayupo pichani) alipokua akielezea wanafunzi hao utaratibu wa kujiunga na masomo VIU.
Wanafunzi wa Feza Boys wakipata mulo.
Mazungumuzo yakiendelea.
 Picha ya pamoja

No comments :

Post a Comment