KAMATI
ya Kudumu ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu, imefanya ziara ya
kutembelea mradi wa upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius
Nyerere (Terminal Three- TBIII), jijini Dar es Salaam, Machi 29, 2016
ambapo awali wajumbe wa kamati hiyo inayoongozwa na Profesa Norman
Adamson Sigalla King, walipatiwa maelezo ya kina ya maendeleo ya mradi
huo unaohusisha jengo la kisasa la abiria na sehemu ya kuegesha ndege
kwa ajili ya kupakia na kushusha abiria na sehemu ya maegesho ya magari.
Baada ya maelezo hayo ya kina yaliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Nchini, (TAA), Mhandisi George Sambali
akisaidiana na baadhi ya wakurugenzi wengine wa Mamlaka hiyo, wajumbe
hao walitembelea mradi huo na kujionea hatua mbalimbali za ujenzi ambapo
kwa sasa ujenzi umefikia karibu asilimia 60. Pichani, Kaimu Mkurugenzi
Mkuu wa TAA, Mhandisi George Sambali, (kushoto), akitoa maelezo kwa
Mwenyekiti wa Kamati hiyo ya Bunge, Norman Adamson Sigalla King,
(kulia), na baadhi ya wajumbe na maafisa wa TAA
Mwenyekiti wa Kamati, akizungumza
Kaimu
Mkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere (JNIA), Paul Rwegasha,
akizungumza na wajumbe wa Kamati hiyo ya Bunge kabla ya kutembelea mradi
Baadhi
ya wajumbe wa Kamati hiyo na maafisa wa TAA, wakisikiliza maelezo
yaliyokuwa yakitolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Mhandisi George
Sambali (hayupo pichani)
Mkurugenzi
wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed Millanga, (kulia), akitoa
maelezo ya maeneleo ya mradi huo. (kushoto) ni Mkurugenzi wa Utawala na
Rasilimali Watu wa TAA, Laurent Mwigune
Mjumbe wa Kamati, Anna Richard Lupembe, akizungumza
Mjumbe
wa Kamati ya Bunge ya Maendeleo ya Miundombinu, na Mbunge wa Fuoni,
Zanzibar, Abbas Ali Hassan Mwinyi, (kulia), akisalimiana na Mkurugenzi
wa Sheria na Mahusiano wa TAA, Ramadhan Maleta, na Mkurugenzi wa Utawala
na Rasilimali Watu, Laurent Mwigune (kushoto)
Mkurugenzi
wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed Millanga(kushoto), akimueleza
Mwenyekiti wa Kamati, Profesa Sigalla, sehemu ya maegesho ya ndege
Mkurugenzi wa Mradi huo wa TBIII, Mhandisi Mohammed
Millanga(kushoto), akimueleza Mwenyekiti wa Kamati, Profesa Sigalla,
(kulia kwake) na baadhi ya wajumbe na maafisa wa TAA, wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Sambali, (wakwanza kulia), sehemu ya maegesho ya ndege
Millanga(kushoto), akimueleza Mwenyekiti wa Kamati, Profesa Sigalla,
(kulia kwake) na baadhi ya wajumbe na maafisa wa TAA, wakiongozwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu Mhandisi Sambali, (wakwanza kulia), sehemu ya maegesho ya ndege
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ndege Tanzania, ATCL, Johnson Mfinanga akizungumzia hali ya shirika hilo
Afisa Mkuu wa Masoko wa TAA, Scholastica Mukanjanga, akizungumza
Mjumbe wa Kamati akizungumza
Mjumbe wa Kamati akizungumza
Mjumbe wa Kamati, Abass Ali Hassan Mwinyi, (katikati), akizungumza
Sehemu ya jengo la uwanja huo
KAMATI YA BUNGE YAIOMBA SERIKALI KUTOA VIBALI VYA UINGIZAJI SUKARI KUTOKA NJE YA NCHI
Mwenyekiti
wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Maji, Dk. Mary Nagu
(kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es
Salaam leo asubuhi, kuhusu Serikali kutoa mapema vibali vya uingizwaji
wa sukari kutoka nje ya nchi ili kuweza kuziba upungufu ya bidhaa hiyo
nchini. Kulia ni Mjumbe wa Kamati hiyo, Mahmoud Mgimwa.
Mjumbe wa Kamati hiyo, Mahmoud Mgimwa akizungumza katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Maji, Dk. Mary Nagu (katikati), akiwa na wajumbe wa kamati hiyo.
Mkutano na wanahabari ukiendelea.
Mwanahabari kutoka TBC, Angela Msangi (kulia), akiuliza suala katika mkutano huo.
ASKOFU CHARLES GADI NA WACHUNGAJI WENZAKE WALIOMBEA TAIFA LIPATE MVUA
Askofu
wa Kanisa la God News for all Ministry, Dk. Charles Gadi, akizungumza
katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhu kabla ya
kuliombea taifa lipate mvua akiwa na wachungaji mbalimbali. Kulia ni
Mchungaji Palemo Masawe.
Mchungaji Martini Ndaki (kushoto), akizungumza katika
mkutano huo.
Meza kuu kabla ya maombi.
Askofu
Charles Gadi (wa tatu kutoka kushoto), akiongoza maombi ya kuliombea
taifa lipate mvua. Kutoka kushoto ni Mchungaji Denis Komba, Mchungaji
Martin Ndaki, Mchungaji Palemo Masawe, Mchungaji Denis Kumbilo,
Mchungaji James Manyama na Mchungaji Leonard Kajuna
Wizara ya Habari yateua Wajumbe wa Kamati ya Maudhui kwa kipindi cha miaka 3
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye (MB), amewateua wafuatao kuwa
Wajumbe wa Kamati ya Maudhui kwa kipindi cha miaka mitatu (3) kuanzia
Machi 11, 2016.
- Joseph Method Mapunda (Mwandishi wa Habari/Mhariri Mtendaji mstaafu wa Magazeti ya Serikali (TSN);
- Abdul Ngalawa (Mwandishi wa Habari/Mkurugenzi mstaafu wa Redio Tanzania Dar Es Salaam (RTD);
- Derek Kaitira Murusuri (Mwandishi wa Habari/Mhadhiri); na
- Zainabu Mrisho Mwatawala (Mwandishi wa Habari na Mwanasheria).
RAIS DK.JOHN MAGUFULI ATOA HATI YA KIWANJA KWA BOHARI YA DAWA (MSD)
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu (kulia), akisalimiana Naibu Katibu Mkuu wa Ardhi
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Moses Kusiluka wakati wa hafla hiyo ya
kukadhiana hati hiyo ya kiwanja. Katikati ni Waziri wa Wizara hiyo,
William Lukuvi.
Salamu zikiendelea. Hapa Mkurugenzi Mkuu wa MSD, akisalimiana na Mkurugenzi wa Mipango Miji, Profesa John Modestus.
Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu (mbele kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo.
Waziri Lukuvi na Mkurugenzi wa MSD, wakiangalia hati hiyo.
Viongozi
wa wizara hiyo wakiwa kwenye mkutano hafla hiyo. Kutoka kushoto ni Mkuu
wa Idara ya Usanifu Majengo, Amina Ramadhani, Ofisa Ardhi Mkuu,
Mwamasage na Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani, Justo Lyamuya.
Na Dotto Mwaibale
RAIS
Dk. John Magufuli kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
ametoa kiwanja chenye ukubwa wa ekari 5 kwa Bohari ya Dawa (MSD)
kilichopo Luguluni nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, kwa ajili ya
ujenzi wa Bohari ya Dawa ili kuondoa upotevu wa fedha kwa maghala ya
kukodi.
Ujenzi
wa maghala katika kiwanja hicho utaokoa kiasi cha sh. bilioni 4
zilizokuwa zikitumika kila mwaka kwa ajili ya malipo ya maghala ya
kukodi yaliyopo Mabibo Ubungo jijini pamoja na kanda mbalimbali nchini.
Akizungumza
wakati wa akikabidhi hati hiyo kwa Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean
Bwanakunu Dar es Salaam leo mchana, Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo
ya Makazi, William Lukuvi alisema, Rais ametoa ardhi hiyo ili kuepusha
gharama zisizo na sababu kwa MSD.
Rais Magufuli aingia Chato kwa mara ya kwanza ataka watanzania washikamane kujitegemea badala ya kutegemea misaada
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Geita
Meja Jenerali Ezikiel Elias Kyunga mara baada ya kuwasili katika viwanja
wa Chato Mkoani Geita. Rais aliwasili Wilayani Chato kwa mara ya kwanza
tangu achaguliwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja
Jenerali Mstaafu Ezikiel Elias Kyunga kulia ,Mbunge wa Geita Vijijini
Joseph Kasheku Msukuma kushoto na Naibu waziri wa Nishati na Madini
ambaye pia ni mbunge wa Chato Dkt. Medard Kalemani watatu kutoka kulia
wakielekea kwenye uwanja wa Mkutano wa mazaina kwa ajili ya kuwasalimia
mamia ya wakazi wa Chato Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga ngoma na kikundi cha ngoma za
asili cha Chato mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Mkutano Chato
Mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwasalimia wakazi wa Chato mara
baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Mazaina Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwashukuru wakazi wa Chato waliofika
kumpokea kwenye Uwanja wa Michezo wa Mazaina Wilayani Chato.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu wa wageni mara baada
ya kuwasili Wilayani Chato.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia mamia ya wakazi wa Chato mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo katika hotuba yake.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na wananchi wa Chato mara
baada ya kumaliza kuwahutubia katika mkutano wa hadhara.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasalimia wananchi wa Chato mara baada ya kuwasili uwanjani hapo.
Wakazi wa Chato wakifurahia
Hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli katika uwanja wa Michezo wa Mazaina Wilayani
Chato. PICHA NA IKULU
……………………………………………………………………………………………………….
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefika nyumbani kwake katika kijiji
cha Mlimani, Wilaya ya Chato Mkoani Geita kwa mara ya kwanza tangu
achaguliwe kuwa Rais, ambapo akizungumza na wananchi katika Mkutano wa
hadhara uliofanyika katika uwanja wa shule ya sekondari Chato, ametoa
wito kwa kila mtanzania kuchapa kazi kwa juhudi ili nchi iondokane na
utegemezi wa misaada ya wafadhili ambayo huambatana na masharti.
Dkt. Magufuli amesema jukumu
kubwa lililo mbele ya watanzania kwa sasa, ni kushikamana na kujisimamia
katika maendeleo ili kila mmoja ahakikishe anaongeza uzalishaji na
utendaji kazi mahali pake pa kazi.
KAMATI YA BUNGE YA HUDUMA ZA JAMII YATEMBELEA BOHARI YA DAWA MSD JIJINI DAR ES SALAAM LEO
Mwenyekiti
wa Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii, Peter Serukamba (kushoto),
Wajumbe wa kamati hiyo na Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Laurean
Banakunu (kulia), wakitembea wakati kamati hiyo ilipotembelea MSD Makao
Makuu Keko Dar es Salaam leo asubuhi.
Kaimu
Mkurugenzi wa Ugavi wa MSD, Mary Lingo (wa pili kulia), akiwaelekeza
wajumbe wa kamati hiyo jinsi dawa zinavyotunzwa katika maghala.
Mkurugenzi wa MSD, Laurean Banakunu (katikati mbele), akiwaongoza wajumbe wa kamati hiyo walipotembelea MSD leo.
Mjumbe wa kamati hiyo, Azani Zungu akiuliza swali juu ya kuharibika kwa dawa.
……………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
KAMATI
ya Kudumu ya Bunge ya Huduma ya Jamii imetembelea Makao Makuu ya Bohari
ya Dawa Keko na kuipongeza kwa utendaji wake kazi pamoja na mazingira
magumu yanayoikabili.
Mwenyekiti
wa Kamati hiyo, Peter Serukamba amesema Kamati yake itasimamiana
kuyafanyia kazi masuala makubwa manne ambayo ni pamoja na bajeti finyu
ya dawa, ulipwaji wa deni la
serikali, mfumo wa uwajibikaji kati ya Tamisemi na Wizara ya Afya ambao
unasababisha utekelezaji na usimamizi wa masuala ya Afya kutokuwa na
mtiririko kutoka juu kwenda chini.
Jambo la nne ni kuhakikisha utekelezaji wa kuongeza uzalishaji dawa ndani ya nchi kupitia sekta binafsi (PPP).
Kwa
upande wake Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Dk. Hamis Kingwangala alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha
Bohari ya Dawa inanunua dawa moja
kwa moja kutoka kwa wazalishaji kwa bei nafuu, hivyo Serikali imeweka
kipaumbele kuhakikisha deni la MSD linalipwa mapema iwezekanavyo.
Alisema
tayari Wizara ya Afya imeiagiza MSD kuandaa bei elekezi kwa maduka
maalum ya dawa (prime vendor) ili vituo vinavyokosa dawa MSD vinunue
huko bila usumbufu na kuhakikisha upatikanaji endelevu wa dawa na vifaa tiba.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa MSD, Laurean Bwanakunu ameviomba vituo vya Afya kuleta mahitaji yao kwa wakati.
Waziri Mbarawa azitaka taasisi na idara kutumia kituo cha kuifadhi taarifa cha Taifa
![]() |
| Mkuu wa Idara ya Compyuta NSSF, Yahaya Madenge (kulia) akiuliza swali kupata ufafanuzi juu ya usalama wa Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Taarifa ‘National Information Data Centre’. |
![]() |
| Baadhi ya mashine kubwa za kisasa za kufua umeme katika Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Taarifa ‘National Information Data Centre’. |
![]() |
| Baadhi ya mitambo ya kuhifadhia taarifa katika Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Taarifa ‘National Information Data Centre’. |
![]() |
| Baadhi ya mitambo ya kuhifadhia taarifa katika Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Taarifa ‘National Information Data Centre’. |
![]() |
| Baadhi ya mashine zinazofanya kazi ya kupooza mitambo katika Kituo cha Taifa cha Kuhifadhia Taarifa ‘National Information Data Centre’ kilichopo jijini Dar es Salaam. |
Vivuko vya MV Magogoni na MV Kigamboni viko katika hali nzuri
Tunapenda
kuutarifu umma kuwa Vivuko vya MV Magogoni na MV Kigamboni viko katika
hali nzuri na vinaendelea na kazi yake ya kuhudumia wananchi kama
kawaida.
Kumekuwa
na malalamiko kuwa Vivuko vya MV Kigamboni na MV Magogoni havifanyi
kazi kwa muda sasa hivyo kusababisha usumbufu kwa wananchiwanaotu
mia huduma hiyo.
mia huduma hiyo.
Tunapenda
kuutarifu umma kuwa taarifa hizo sio za kweli na kwamba Vivuko vyote
viwili yani MV Magogoni na MV Kigamboni vinaendelea na kazi zake za
kutoa huduma kwa wanachi kama kawaida na kusisitiza kuwa katika kipindi
cha usiku kutokana na kutokuwepo kwa wananchi kwa muda huo vivuko hivyo
hupumzika.
MV.
Magogoni ina uwezo wa kubeba tani 500, ambayo ni sawa na kubeba abiria
2000 na magari madogo 60 kwa wakati mmoja. Kivuko hiki kiko katika hali
nzuri, kinafanya kazi saa 20 kwa siku, na kupumzika kuanzia saa 6:00
usiku mpaka saa 10:00 alfajiri kila siku ili kufanyiwa matengenezo ya
kinga (service).
Vile
vile MV. Kigamboni inauwezo wa kubeba tani 160, ambayo ni sawa na
kubeba abiria 800 na magari madogo 21 Kwa wakati mmoja. Kivuko hiki
kinafanya kazi kwa saa 22 kwa siku, na kupumzika kuazia saa 4:00 usiku
mpaka saa 6:00 usiku kila siku ili kufanyiwa matengenezo ya kinga
(service).
Aidha
TEMESA inatoa rai kwa watu wote wanaotumia mazingira ya vivuko vya MV
Magogoni na Kigamboni kuyatunza mazingira ya vivuko hivyo katika kuvipa
maisha marefu, ili kuepusha adha ya usafiri wa vivuko na inawashauri
watumiaji wa Vivuko vya MV Magogoni na Kigamboni kufuata taratibu zote
za kivuko kama inavyoelekezwa ili kutoathiri utoaji wa huduma hiyo.
Vivuko
vya Mv Magogoni na Kigamboni vinasimamiwa na Wakala wa Ufundi na Umeme
(TEMESA) katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya usafiri kutoka
katika maeneo ya katikati ya Jiji la Dar es Salaam na Kigamboni.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano
KUFUTWA USAJILI KWA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (110) KWA KUJIENDESHA KINYUME CHA SHERIA KUANZIA TAREHE 30/03/2016
Msajili wa Mashirika
Yasiyo ya Kiserikali amefuta usajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiesrikali
(NGOs) 109 kwa kuendesha shughuli zao kinyume cha Sheria ya NGOs Na. 24
ya mwaka 2002 kama ilivyorekebishwa mwaka 2005. Mashirika hayo ni yale
ambayo hayajawasilisha taarifa za mwaka kwa kipindi cha miaka miwili
pasipo kutoa sababu za msingi, kutolipa ada ya mwaka au kuendesha
shughuli za NGOs bila kusajiliwa chini ya Sheria ya NGOs.
Kwa taarifa hii, Mashirika
yaliyotajawa hapa chini yamefutiwa usajili na yataarifiwa kusitisha
shughuli zao kuanzia tarehe ya tangazo hili (30/03/2016). Baada ya
kipindi hicho, Msajili wa NGOs atayachukulia hatua stahiki Mashirika
ambayo yatakaidi amri hii na kuendelea na shughuli za NGOs kinyume na
Sheria husika.
| MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI (109) YALIYOFUTIWA USAJILI KUANZIA TAREHE 30/3/2016 NI KAMA IFUATAVYO: |
|
1. THE MEDICAL WOMEN ASSOCIATION OF TANZANIA (MEWATA) 2. AFRICAN GENDER AND GOOD GOVERNANCE ALLIANCE 3. AFRICAN WILDLIFE FOUNDATION 4. AGENDA FOR ENVIRONMENTAL AND SUSTAINABLE DEVELOPMENT 5. ANTIOKIA MISSION INTERGRATED SOCIAL DEVELOPMENT 6. BUSEGWE DEVELOPMENT ASSOCIATION 7. BUTIAMA DEVELOPMENT ASSOCIATION 8. CARE FOR THE CHILD (CFC) 9. CHAKUFAA DEVELOPMENT FOUNDATION 10. CHAMA CHA KUSAIDIA WATOTO YATIMA MAKAMBAKO 11. COMFORT WOMEN RELIEF FOUNDATION 12. COMMUNITY AGRICULTURAL ACTION SERVICES CENTRE 13. COMMUNITY SERVICES SUPPORT OF TANZANIA (COSESU-T) 14. DAUGHTERS OF ZION FOUNDATION LTD 15. DEFENCE OF HUMAN RIGHTS CITIZEN RIGHTS 16. DEVELOPERS OF SUSTAINABLE COMMUNITY BASED ACTIVITIES (DESCOBA) 17. DIANA WOMEN EMPOWERMENT ORGANIZATION 18. EDNA DEVELOPMENT FOUNDATION 19. EMPOWERMENT AGAINST POVERTY AND HIV/AIDS 20. EMPOWERMENT FOR THE DISADVANTAGED COMMUNITY (EDC) 21. ENVIRONMENTAL MANAGEMENT AND NUTRITIONAL SERVICES AGENCY (EMA-NUSA) 22. GLOBAL VISION TANZANIA (GVT) 23. GRASSROOTS INITIATIVE FOR YOUTH AND ELDERLY DEVELOPMENT ORGANIZATION (GIYEDO) 24. HOPE MISSION OF DEVELOPMENT FOR THE DISABLED (HOMIDED) 25. HURUMA CHILD MINISTRY CENTRE 26. HURUMA REHABILITATION PROGRAMME 27. IMANI WOMEN ECONOMIC EMPOWERMENT ASSOCIATION (IWEA) 28. INTERNATIONAL MEDICAL CORPS 29. IZAAZ MEDICAL PROJECT 30. JUMUIYA EDUCATION BAGAMOYO (JEBA) 31. JUNIOR ACHIEVEMENT OF TANZANIA 32. KAMACHUMU IN NGEMU AGENDA (KINGA) 33. KILIMO HAI TANZANIA (KIHATA) 34. KUZA EDUCATION DEVELOPMENT 35. MANDATE AFRICA FOUNDATION 36. MASASI FARMERS ADVOCACY ASSOCIATION (MAFADA) 37. MAZINGIRA INSTITUTE OF TANZANIA (MAI-TANZANIA) 38. SUMBAWANGA ESCARPMENT ENVIRONMENTAL CONSERVATION ORGANIZATION (SEECO) 39. MFUKO WA MAENDELEO YA WAISLAM MKOA WA RUVUMA 40. MKONGO MLOKA DEVELOPMENT ASSOCIATION 41. MOROGORO ENVIRONMENTAL CONSERVATION ACTION GROUP 42. MOROGORO ENVIRONMENTAL CONSERVATION ACTION GROUP 43. MUUNGANO DEVELOPMENT ASSOCIATION (MUDEA) 44. MWAKALELI COMMUNITYDEVELOPMENT ORGANIZATION (MWACODO) 45. MWALIMU NYERERE UWC FOR SELF RELIANCE 46. MWANANYAMALA WOMEN LDEVELOPMENT GROUP (MWAWODE) 47. NATIONAL LIFE DEVELOPMENT ASSOCIATION 48. NJOMBE DEVELOPMENT ORGANIZATION (NDO) 49. NORWEGIAN PEOPLE AID 50. OLOF PALME ORPHANS CENTRE 51. DEVELOPMENT AGENCY PROBATION TIME RESEARCH 52. PANGOLIN ELITE SPORTS FOUNDATION 53. PARTGAGE TANZANIA 54. PERIPHERY AREAS DEVELOPMENT ASSOCIATION (PADA) 55. POVERTY ALLEVIATION AND AGRICULTURAL DEVELOPMENT (PADEFO) 56. POVERTY FIGHTERS AND CHARITABLE GROUP 57. POVERTY FIGHTERS AND DEVELOPMENT SOCIETY OF TANZANIA (POFIDESO) 58. PRICESS AGNES FOUNDATION 59. PROGRESS ASSOCIATION TANZANIA (PATA) 60. PROMOTION OF FARMING AND ORPHANS EDUCATION IN TANZANIA (PROFOET) 61. RESTE YOUTH TRAINING TRUST FUND 62. RIDHIKA SHIRIKA LA ULINZI NA MAZINGIRA 63. RURAL ACCESS TECHNOLOGY INORMATION AND INSTITUTIONAL SERVICES (RATHS) 64. RURAL FAMILY LIFE PLANNING ASSOCIATION 65. RURAL INITIATIVES FOR DEVELOPMENT OF TANZANIA – RIDE(T) 66. RURAL ORIENTED SUSTAINABLE DEVELOPMENT ORGANIZATION (ROSDO) 67. RURAL WOMEN DEVELOPMENT ASSOCIATION 68. SAMORSES EDUCATION FOUNDATION 69. SANTA MERINA EDUCATION FOUNDATION 70. SAVE LIFE ASSOCIATION 71. SHINYANGA FOUNDATION FUND (SFF) 72. SOCIETY FOR RURAL DEVELOPMENT INITIATIVES (SRDF) 73. SOLIDARITY WOMEN GROUP (SWG) 74. SOLUTION AND OPPORTUNITIES FOR DISADVANTAGED IN AFRICA (SODA) 75. SOUTH DEVELOPMENT IN TANZANIA (YODIT) 76. SUSTAINABLE INTERGRATED FARMING AND HEALTH IMPROVEMENT 77. TAMADA 78. TANZANIA ACTION FOR PASTORAL EDUCATION ADVOCACY (TACEA) 79. TANZANIA ASSOCIATION OF ENVIRONMENTAL ENGINEERS (TAEES) 80. TANZANIA DEVELOPMENT AND AIDS PREVENTION (TADEPA) 81. TANZANIA GIRL’S EMPOWERMENT (TAGE) 82. TANZANIA HURUMA AIDS ORGANIZATION (THAO) 83. TANZANIA INITIATIVES FOR POVERTY ALLEVIATION (TIPA) 84. TANZANIA JOURNALIST ASSOCIATION (TAJA) 85. TANZANIA MANGROVE PROTECTION ASSOCIATION (TAMPA) 86. TANZANIA MARGINALIZED AREAS COMMUNITY SERVICES FOUNDATION 87. TANZANIA ROAD ASSOCIATION (TRA) 88. TANZANIA SOCIETY FOR THE BLIND (TASODEB) 89. TANZANIA SUPPORT AND TRAINING YOUTH AND WIDOWS ASSOCIATION 90. TANZANIA TENANTS ASSOCIATION 91. TANZANIA YOUTH MUSLIM ASSOCIATION (TAYMA) 92. TARIME – SIRARI GROUP (TARSI) 93. TAX SERVICES TANZANIA 94. TECHNOWLEDGE TANZANIA (TKTZ) 95. TELECOMS AND ELECTRONICS TECHNICIANS ASSOCIATION (TETA) 96. TEMEKE DISTRICT YOUTH FOUNDATION (TEYOFO) 97. THE HUMAN DEVELOPMENT PROJECTS AND TANZANIA 98. NAMTUMBO NETWORK OF CIVIL SOCIETY (NANECISO) 99. THE SURVIVAL AFRICA TRUST (SAT) 100. THE TANZANIA HERALDS YOUTH SERVICES (THEYS) 101. THE VOICE OF THE AIDS AND ORPHANS (VOTAO) 102. THE WOMEN WIDOW CHILDREN AND FISHERIES DEVELOPMENT 103. TUMAINI ORPHANS AND VULNERABLE CHILDREN CENTRE 104. UMOJA WA DOUYA NA MAKANGAWE (UDOMA) 105. UMOJA WA MADEREVA WA MABASI TANZANIA (UWAMATA) 106. WATOTO CARE ORGANIZATION (WACO) 107. WOMEN AND YOUTH ECONOMIC DEVELOPMENT INITIATIVE (WOYEDE) 108. WOMEN DEVELOPNMENT AND GENDER 109. SAIDIA JAMII YA WAZEE KAGERA SAJAWAKA) 110. UKIMWI ORPHANS ASSISTANCE (UKOA) |
| Imetolewa na,
M.S. Katemba MSAJILI WA NGOs WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO 29 Machi, 2016 |
RAIS MAGUFULI APATA CHAKULA CHA MCHANA MGAHAWANI UWANJA WA NDEGE WA MWANZA AKIWA NJIANI KUELEKEA CHATO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
pamoja na viongozi wa mkoa wa Mwanza wakijipatia chakula cha mchana
katika mgahawa wa Victoria uliopo nye ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza
alipopumzika kwa muda kabla ya kuelekea nyumbani kwake Chato mkoani
Geita kwa mapumziko mafupi. Pamoja nao mezani hapo ni Meya wa Ilemela
Mstahiki Renatus Mulunga, Meya wa jiji la Mwanza Mstahiki James Bwire,
Mkuu wa Mkoa wa MWanza Mhe John Mongella na Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo
Ndg Anthony Diallo.PICHA NA IKULU
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
pamoja na viongozi wa mkoa wa Mwanza wakijipatia chakula cha mchana
katika mgahawa wa Victoria uliopo nye ya Uwanja wa Ndege wa Mwanza
alipopumzika kwa muda kabla ya kuelekea nyumbani kwake Chato mkoani
Geita kwa mapumziko mafupi. Pamoja nao mezani hapo ni Meya wa Ilemela
Mstahiki Renatus Mulunga, Meya wa jiji la Mwanza Mstahiki James Bwire,
Mkuu wa Mkoa wa MWanza Mhe John Mongella na Mwenyekiti wa CCM Mkoa huo
Ndg Anthony Diallo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Joseph Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
pamoja na viongozi wa mkoa wa Mwanza wakiondoka baada ya kupata chakula
cha mchana katika mgahawa wa Victoria uliopo nye ya Uwanja wa Ndege wa
Mwanza alipopumzika kwa muda kabla ya kuelekea nyumbani kwake Chato
mkoani Geita kwa mapumziko mafupi.
RAIS MAGUFULI AWASILI MWANZA, AAMURU BARABARA UWANJA WA KAYENZE IFUNGULIWE MARA MOJA
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akishuka kwenye ndege mara baada
kwasili kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza wakati alipopitaka mkoani humo
akielekea Nyumbani kwake Chato mkoani Geita kwa ajili ya mapumziko, hii
ni mara ya kwanza kwenda kupumzika kijijini kwake toka alipchaguliwa na
kauapishwa kushika madaraka ya kuongoza Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
mwezi Oktoba mwaka jana.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. John
Mongela amemshukuru Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya
kuamuru kufunguliwa kwa barabara inayopita kandokando ya uwanja wa ndege
kuelekea Kayenze iliyokuwa imefungwa kwa miezi miwili na kuleta adha
kubwa kwa wananchi wanaoishi maeneo hayo.
Mara baada ya Rais Magufuli
kuamuru barabara hiyo ifunguliwe mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela
pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama mkoani Mwanza Uongozi mzima wa
mkoa huo waliongozana kwenda Kayenze na kuwatangazia wananchi kwamba
wako huru kutumia barabara hiyo kwakuwa Mh. Rais ameamuru ifunguliwa na
sisi tumekuja kutekeleza agizo la rais na sasa barabara hii
imefunguliwa.
(PICHA NA JOHN BUKUKU- FULLSHANGWE-MWANZA)
Mke wa Rais Mama Janet Magufuli
akishuka kwenye ndege wakati Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli
alipowasili uwanjani hapo akielekea Chato Mkoani Geita kwa mapumziko.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mkuu wa mkoa wa Mwanza
Mh. John Mongela mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa mwanza
leo.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana Mkuu wa wilaya ya
Nyamagana Mh. Baraka Konisaga kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza leo.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na viongozi wa kamati ya
Amani mkoani Mwanza wakati alipowasili uwanjani hapo akielekea Chato.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mh.Altaf Mansour
mlezi wa shirikisho la Vyuo vikuu CCM Kanda ya Ziwa, Kushoto ni Mkuu
wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na Mh.Altaf Mansour
mlezi wa shirikisho la Vyuo vikuu CCM Kanda ya Ziwa, Kushoto ni Mkuu
wa mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana wana CCM waliofika
uwanjani hapo kumpokea, Kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh. John
Mongela.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akipigiwa saluti na mmoja wa wakuu wa
vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Mwanza waliofika uwanjani hapo
kumpokea.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana afisa habari wa ofisi ya
mkuu wa mkoa wa Mwanza Bw. Atley Kuni .
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akielekea kukagua vikundi vya ngoma na kwaya.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli na Mkewe mama Janet Magufuli
wakiangalia vikundi vya ngoma wakati walipowasili kwenye uwanja wa Ndege
wa Mwanza leo wakielekea Chato kwa mapumziko.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli na Mkewe Mama Janet Magufuli
wakiwapungia wachenza goma wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa Ndege wa
Mwanza.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akisalimiana na askari wa kikozi cha Zimamoto uwanjani hapo.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiangalia kwaya ya AIC Makongoro
ambayo iliimba wimbo wa kuhamasisha kuitunza amani ya nchi na
kumhamasisha kiasi cha kumfanya kujumuika nao na kuimba pamoja na
wanakwaya hao.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa AIC
Makongoro ya jijini Mwanza wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa
Mwanza.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akiimba pamoja na wanakwaya wa AIC
Makongoro ya jijini Mwanza wakati wa mapokezi kwenye uwanja wa ndege wa
Mwanza.
Wadau Issa Michuzi kulia na Pius Lugonzibwa kushoto walikuwepo katika mapokezi hayo.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akwapungia mkono wafanyakazi wa uwanja wa ndege wa Mwanza.
Rais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Dk. John Pombe Magufuli akizungumza na baadhi ya wananchi
waliofika kumpokea kwenye uwanja wa ndege wa mwanza katikati ni Mkuu wa
mkoa wa Mwanza Mh. John Mongela na kushoto ni Mkuu wa wilaya ya
Nyamagana Mh. Baraka Konisaga.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh. John
Mongela akimshukuru Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli mara baada ya
kuamuru kufunguliwa kwa barabara inayopitka kandokando ya uwanja wa
ndege kuelekea Kayenze.
Mh.Altaf Mansour mlezi wa
shirikisho la Vyuo vikuu CCM Kanda ya Ziwa alikuwepo katika mapokezi
hayo , Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mh. Baraka Konisaga.
Baadhi ya wanahabari waliokuwepo
uwanjani hapo wakifurahia kwa kugonganisha chupa za soda kinywaji
ambacho Mh. Rais Dk John Pombe Magufuli alitoa ofa kwa wananchi wote
waliokuwepo uwanjani hapo, kulia ni Shila Kutoka ITV Mwanza na kushoto
ni Atley Kuti afisa habari wa ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Mwanza.
Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli
akiondoka kwenye kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza mara baada kupata
kifungua kinywa kwenye mgahawa wa Victoria Catering.
Mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli
akipiga picha ya pamoja na kwaya ya AIC Makongoro na baadhi ya viongozi
wa mkoa wa Mwanza kabla ya kuelekea Chato mkoani Geita.
TANZANIA NA KUWAIT ZASAINI MAKUBALIANO YA SAFARI ZA ANGA
Picha na Eleuteri Mangi –MAELEZO.
Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo imepanga kufanya mikutano ya kusikiliza maoni ya wadau
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BUNGE LA TANZANIA
TAARIFA KWA UMMA
Katika kutekeleza majukumu yake,
Kamati ya Bunge ya Sheria Ndogo imepanga kufanya mikutano ya kusikiliza
maoni ya wadau (Public Hearing) kwa mujibu wa Kanuni ya 117 (9)
kuhusiana na Sheria Ndogo zilizowasilishwa na Serikali katika Mkutano wa
Pili wa Bunge uliomalizika Februari 2016.
Mikutano hiyo ya kusikiliza maoni
ya wadau kuhusu Sheria Ndogo inatarajiwa kufanyika Jumatatu tarehe 4
Aprili, 2016 na Jumanne tarehe 5 Aprili, 2016 katika Ukumbi wa Mikutano
wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Sheria Ndogo
ambazo Kamati inakaribisha wadau na umma kwa ujumla kutoa maoni yao ni
pamoja na zifuatazo:-
- The Petroleum (Bulk Procurement) Regulations, 2015
- The Public Private Partnership Regulations, 2015
- The Copyright and Neighboring Rights (Copyrighted Works – Communication to the Public) Regulations, 2015
- The National Examinations Regulations, 2015
- The Institute of Judicial Administration Lushoto (Students’ General Welfare, Conduct and Disciplinary Matters) Regulations, 2015
- The Institute of Judicial Administration Lushoto (Students’ Performance Assessment) Regulations, 2015
- The Fire and Rescue Force (Fire Precautions in Buildings) Regulations, 2015
Sheria Ndogo zilizotajwa hapo juu
pamoja na nyingine ambazo zinashughulikiwa na Kamati, zinapatikana kwa
kupakua (downloadable) katika tovuti ya Bunge la Tanzania ya
www.parliament.go.tz pamoja na tovuti ya Serikali ya www.tanzania.go.tz
Aidha, maoni ya wadau yanaweza kuwasilishwa kwa njia ya posta au barua pepe kwa anuani ifuatayo:-
Katibu wa Bunge, Ofisi ya Bunge,
- L. P. 9133, DAR ES SALAAM
Barua pepe: cna@bunge.go.tz
Imetolewa na:
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano Ofisi ya Bunge
DAR ES SALAAM
29 Machi, 2016.
SUMATRA KWA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI, KIKOSI CHA USALAMA BARABARANI WAFANIKIWA KUKAMATA MABASI 105
(Picha na Maelezo)
……………………………………………………………………………………………..
Frank Mvungi-Maelezo
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri wa
Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi,Kikosi
cha Usalama Barabarani wamefanya ukaguzi katika Jiji la Dar es
salaam,ambapo wamefanikiwa kukamata mabasi 105 na kati hayo 36
yamefikishwa mahakamani baada ya kukiuka wa masharti ya leseni ya
usafirishaji abiria.
Hayo yamwebainishwa leo na Meneja
Mawasiliano wa SUMATRA Bw. David Mziray wakati wa mkutano na vyombo vya
habari uliolenga kutoa ufafanuzi kuhusu hatua zinazochukuliwa na
Mamlaka hiyo katika kutatua kero zinazowakabili abiria nyakati za
asubuhi na Jioni.
Akifafanua Mziray amesema kati ya
Machi 21-24 , 2016 ilifanya ukaguzi huo na ili sheria iweze kuchukua
mkondo wake Kwa wale wanaokwenda kinyume na taratibu zilizowekwa.
“Katika kuimarisha huduma za
usafiri Mamlaka imeweka utaratibu maalum wa kufanya ukaguzi katika
maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es salaam ikiwemo katikati ya
jiji,Ubungo,Buguruni na Kariakoo ili kubaini wale wote wanaovunja
sheria”.alisisistiza Mziray.
Akizungumzia baadhi ya makosa
yalibainika kutendwa na mabasi hayo Mziray alisema kuwa ni pamoja na
kuongeza nauli,kukata njia,kutoa huduma bila leseni ya
usafirishaji,kutoa huduma katika njia ambazo hawakupangiwa.
Wamiliki na wafanyakazi katika
sekta ya usafirishaji kote nchini hasa wa mabasi ya daladala wametakiwa
kuzingatia sheria na kanuni za usafirishaji wanapotoa huduma hiyo kwa
umma.
Mziray aliongeza kwamba wananchi
wametakiwa kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa pale wanapobaini basi
walilopanda linakiuka masharti ya leseni ikiwemo kuongeza nauli,kukata
njia,kutoa huduma bila leseni ya usafirishaji na kutoa huduma katika
njia ambazo hawakupangiwa ambapo wananchi wanaweza kutoa taarifa kupitia
namba za simu za bure ambazo ni 0800110019 na 0800110020.
TANESCO MKOANI PWANI YAWANASA WEZI SABA KWA TUHUMA ZAKUIBA UMEME KINYEMELA
(PICHA NA VICTOR MASANGU)
………………………………………………………………………………………..
Serikali ya Tanzania kujenga bomba la mafuta kutoka Tanga hadi Uganda
Picha na Ally Daud- Maelezo
……………………………………………………………….
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
Imeelezwa kuwa Tanzania ina vigezo mbalimbali ambavyo vinaifanya nchi ijiamini kwa asilimia 98 kuwa mradi wa bomba la kusafirishia mafuta kutoka Ziwa Albert nchini Uganda utapitia Kaskazini mwa Tanzania hadi Bandari ya Tanga badala ya nchini Kenya.
Hayo yameelezwa na Katibu Mkuu
wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa wakati wa kikao
chake na wafanyabiashara wa mafuta nchini ambacho kililenga kujadiliana
nao kuhusu fursa za uwekezaji zitakazotokana na mradi huo endapo utapita
nchini.
Profesa Ntalikwa alivitaja
vigezo hivyo kuwa ni uzoefu wa Tanzania katika ujenzi wa mabomba ya
kusafirisha nishati mbalimbali ikiwemo Bomba la
Mafuta la kutoka Tanzania hadi Zambia (TAZAMA), Bomba la kusafirisha
gesi kutoka SongoSongo hadi Dar es Salaam, Bomba la kusafirisha gesi
kutoka eneo la Mnazi Bay hadi Mtwara, pamoja na Bomba kuu la gesi kutoka
mkoani Mtwara hadi Dar es Salaam lenye kipenyo cha inchi 36 hivyo
uzoefu huo utasaidia katika kupunguza muda wa ujenzi wa bomba la mafuta
ambalo kipenyo chake ni inchi 24.
“Tumewaeleza
wenzetu kuwa Serikali ya Tanzania pia ilishajenga uwezo mkubwa katika
masuala ya kutwaa, kumiliki na kulipa madai ya wananchi wanaopisha
miradi ya mabomba na shughuli hizi zimekuwa zikifanywa kwa wepesi na
umakini mkubwa ikiwemo umakini katika kufuata kanuni na sheria za
mazingira, hivyo haitatuwia ngumu katika kutekeleza mradi huu,” alisema
Profesa Ntalikwa.
Continue reading →RAIS MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA UKAGUZI WA HESABU ZA SERIKALI KUTOKA KWA MKAGUZI NA MDIBITI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) IKULU DAR ES SALAAM LEO
PICHA NA IKULU
waogealeaji nane wa Tanzania kushindana kesho (jumanne)
Kocha
wa TSS, Alex Mwaipasi akiwafundisha waogeaji wa TSS, kwenye bwawa la
Ellis Park mjini Johannesburg Afrika Kusini kwa ajili ya Kusini tayari
kushindana katika mashindano ya South Africa level 2
Viongozi
wa timu ya Tanzania Swim Squad (TSS), Thauriya Diria (wa kwanza
kushoto) na Inviolata Itatiro (Katikati) wakiwa katika picha ya pamoja
na kocha Michael Livingstone wakiwa katika picha ya pamoja TSS kwenye
bwawa la kuogelea la Ellis Park kabla ya mashindano ya South Africa
level 2
IZZO BIZNESS APAGAWISHA WAKAZI WA MBEYA KWENYE TAMASHA LA PASAKA
![]() |
|
Msanii Emmanuel Simwinga maarufu “ Izzo Bizness “ akitumbuiza
kwenye tamasha la pasaka la home sweet home lililodhaminiwa Tigo jijini Mbeya jumapili iliyopita. |
![]() |
|
Izzo Bizness akishow love kwa mashabiki zake tamasha la pasaka la home Sweet Home lililodhaminiwa Tigo jijini Mbeya
jumapili iliyopita |
![]() |
| Mamia ya mashabiki wakifurahia burudani toka kwa Izzo Bizness |
![]() |
| Yani
ilikuwa shangwe wakati Izzo Bizness akitumbuiza jukwaani
kwenye tamasha la pasaka la home sweet home lililodhaminiwa Tigo jijini
Mbeya jumapili iliyopita. . |
Milioni 37 zatengwa kukarabati barabara ya Kata ya Panzuo/Mkuranga
Na Mwandishi Wetu,
Mkuranga
Mkuranga
JUMLA ya Sh Milioni 37 zimetangwa kwa ajili ya kukarabati
barabara ya Mbogo na Mbezi Muungwana, inayopita katika vijiji kadhaa vya Kata
ya Panzuo, wilaya Mkuranga, mkoani Pwani kwa ajili ya kupunguza adha za ubovu
wa barabara wanazokutana nazo wananchi wa maeneo hayo hali inayopelekea wakati
mwingine akina mama kujifungulia njiani.
barabara ya Mbogo na Mbezi Muungwana, inayopita katika vijiji kadhaa vya Kata
ya Panzuo, wilaya Mkuranga, mkoani Pwani kwa ajili ya kupunguza adha za ubovu
wa barabara wanazokutana nazo wananchi wa maeneo hayo hali inayopelekea wakati
mwingine akina mama kujifungulia njiani.
Mwendesha
bodaboda Ramadhan Rajab akijaribu kupita katika barabara mbovu
inayotokea Kimanzichana kuelekea vijiji vya Mnyonzole na Kibesa, Kata ya
Panzuo, wilayani Mkuranga, mkoani Pwani.











































No comments :
Post a Comment