Tuesday, January 26, 2016

MATUKIO MBALIMBALI YA PICHA KATIKA KIKAO CHA BUNGE MJINI DODOMA LEO

bu1
 Spika wa Bunge Job Ndugai (kulia)  akimwapisha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa  , bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
bu2
Spika wa Bunge Job Ndugai (kulia)  akimwapisha Waziri wa  Fedha na Mipango, Dkt.Philip Mpango, bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu3
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Dkt. Abdallah Possi akijibu maswali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu4
Waziri  wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Jenista Mhagama  akijibu swali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu5
Wabunge wakisikiliza hoja mbalimbali bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu6 bu7
Baadhi ya Mawaziri wa wizara mbalimbali wakisikiliza maswali na majibu Bengeni leo.
bu8
Profesa Sospeter Muhongo Waziri wa Nishati na Madini kulia na Dk Philip Mpango Waziri wa Fedha na Mipango wakifuatilia mambo mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea bungeni leo.
bu9
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Walemavu, Anthony Mavunde  akijibu maswali Bungeni Mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu10
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akijibu maswali Bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu11
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitoa hoja ya kutaka Bunge lijadili  Hotuba ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli aliyoitoa wakati alipofungua Bunge la Kumi na Moja Novemba 20, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
bu12
Mbunge wa Mvomero, Murad Sadiq akichangia  bungeni mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

MWESIGWA AFUNGUA KOZI YA NGAZI YA JUU KWA WANAWAKE

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Mwesigwa Selestine leo amefungua kozi ya ngazi ya juu ya ukocha kwa wanawake (High Level Coaching Course) iliyoandaliwa na TFF kwa kushirikiana na FIFA.
Akiongea na waandishi wa habari wakati wa ufunguzi wa kozi hiyo, Mwesigwa amewataka washiriki wa kozi hiyo kuzingatia mafunzo hayo na kuitumia vyema fursa hiyo adimu waliyoipata.
Mwesigwa amewataka washiriki kuhakikisha kozi hiyo ya siku tano, inawasaidia na kwenda kuwa walimu wa mpira wa miguu kwa wanawake, na kuongeza mwamko kwa wanawake wengi kuupenda na kuucheza mpira wa miguu.
Aidha Mwesigwa, amewataka washiriki wa kozi hiyo kuzingatia maelekezo ya mkufunzi, nidhamu ya ndani na nje ya uwanja kwani imekua ni bahati nzuri kwao kupata nafasi ya kushiriki kozi hiyo ya ngazi ya juu.
Naye mkufunzi wa kozi hiyo anayetambulika na FIFA/CAF, Sunday Kayuni amesema atatumia uwezo wake wote kuhakikisha washiriki wa kozi hiyo wanajifunza na kuelewa vizuri mafunzo yake, ili waweze kuwa walimu wazuri watakapokwenda kuanza kufundisha.
Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Wanawake ya TFF, Amina Karuma ameishukuru TFF kwa kuendesha kozi hiyo  na kusema kupatikana waalimu wengi wa kike kutaongeza mwamko wa wanawake kuucheza mpira wa miguu.
Jumla ya washiriki 25 wanashiriki kozi hiyo kutoka mikoa mbalimbali nchini ambao ni Fatuma Omary, Esther Chabruma, AMina Mwinchum, Sweetie Charles, Pendo John, Berlina Mwaipungu, Mariam Mchaina, Elizabeth Sokoni, Sophia Mkumba, Marry Masatu, Aziza Mbwele, Fadhila Yusuph.
Wengine ni Veneranda Mbano, Mariam Aziz, Hilda Masanche, Chichi Mwidege, Sophia Edward, Asha Rashid, Fatuma Khatibu, Neema Sanga, Hindu Muharami, Tatu Malogo, Komba Alfred, Veroinca Ngonyani, Judith nyatto na Ingfridy Kimaro.

AZAM, SIMBA, YANGA ZAFUZU 16

Timu za Azam FC, Simba SC, Yanga zimeungana na timu zingine saba kufuzu kwa hatua ya 16 Bora ya michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mzunguko wa nne utakaochezwa mwishoni mwa mwezi Februari, huku michezo mine ikichezwa leo katika viwanja mbalimbali nchini.
Jumla ya michezo 10 mpaka sasa imeshachezwa na timu kumi kujikatia tiketi ya kucheza mzunguko wa nne, ambao utazikutanisha jumla ya timu 16 mwezi ujao kusaka timu nane zitakazosonga mbele hatua ya nane bora (Robo Fainali).
Timu zilizofuzu hatua ya 16 bora mpaka sasa ni Azam FC, JKT Mlale, Mwadui FC, Ndanda FC, Panone FC, Rhino Rangers, Simba SC, Tanzania Prisons, Toto Africans na Young Africans.
Leo michezo minne itachezwa, Mtibwa Sugar v Abajalo (Jamhuri – Morogoro), Geita Gold v Mgambo Shooting (Nyankumbu – Geita), Lipuli FC v JKT Ruvu (Wambi – Mafinga), na African Sports v Coastal Union (Mkwakwani – Tanga).
Bingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) mwaka huu, ataiwakilisha Tanzania mwaka 2017 kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF-CC)

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA KOCHA MINGANGE

Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa Kocha Mkuu wa klabu ya Mbeya City inayoshiriki Ligi Kuu ya Vodacom, Meja Mstaafu Abdul Mingange kufuatia kifo cha mke wake Fatma Juma kilichotokea mwishoni mwa wiki jijini Dar es salaam.
Katika salamu zake kwenda kwa familia ya marehemu, TFF imempa pole mme wa marehemu Meja Mingange, ndugu jamaa, marafiki pamoja na klabu ya Mbeya City kufuatia kifo hicho.
Mazishi ya marehemu Fatma Juma yamefanyika Jumapili iliyopita katika makaburi ya Matombo mkoani Morogoro

VYAMA VYA SIASA VYAASWA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA ZANZIBAR

mutungi 
Na mwandishi wetu
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini Mhe.Jaji Francis Mutungi ameviasa Vyama vya Siasa kushiriki chaguzi zinazotangazwa na tume za uchaguzi nchini ikiwemo uchaguzi wa Machi 20, mwaka 2016 uliotangzwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).
 Kwa mujibu wa barua iliyotolewa  kwa vyama hivyo leo na kusainiwa na  Jaji Mutungi  ilieleza kwamba,  kimsingi Sheria ya Vyama Vya Siasa Sura ya 258 inasisitiza vyama vya siasa  kushiriki katika chaguzi zote zinazotangazwa na tume za uchaguzi ili kufikia malengo yake ya kushika dola.
“Katika nchi kidemokrasia na kwa chama cha siasa kinachoamini misingi ya kidemorasia ya vyama vingi vya siasa, hakuna njia mbadala kwa chama cha siasa kufikia malengo yake zaidi ya kushiriki uchaguzi.
“Ni wajibu wa kila chama cha siasa nchini  kama wakala wa kukuza demokrasia, utawala wa sheria na amani ya nchi, kuwa wa kwanza kutii matamko ya kisheria yanayotolewa na mamlaka husika . Kama kuna chama cha siasa hakiridhiki au kimekwazwa kwa njia moja au nyingine na suala lolote kuhusu masuala ya uchaguzi, njia stahiki na inayonyesha ukomavu wa kisiasa si kuhamasisha kugomea uchaguzi, bali ni vema kikafuata utaratibu uliowekwa katika sheria za uchaguzi,” alisema Jaji Mutungi.
Aidha Msajili huyo amesema kwa mujibu wa Sheria za Nchi bado ni suala la hiari kwa chama kushiriki uchaguzi lakini utashi huo wa hiari unaenda sanjari na umuhimu wa kila chama kushiriki kila uchaguzi unaotangazwa na tume ya uchaguzi.
“Hivyo ni muhimu basi kila chama cha siasa kuelewa kuwa,uchaguzi ni kipimo cha uhai wa chama cha siasa. Chama cha siasa kisiposhiriki uchaguzi kinaua uhai wake katika mtazamo wa harakati za kisiasa,” alisisitiza.
 
Aliongeza kwamba hivi sasa, mfumo wa demokrasia ya vyama vingi na vyama vya siasa vimeimarika, hivyo sio vyema kwa chama cha siasa kujirudisha nyuma au kujiua kisiasa kwa kutoshiriki uchaguzi wakati kina uwezo wa kufanya hivyo.

MAJALIWA ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWANASHERIA WA BUNGE

kas1
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitoa heshima za mwisho kwa  aliyekuwa Mshauri Mkuu wa Masuala ya Sheria wa Bunge, marehemu Oscar Mtenda  nyumbani kwa marehemu mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
kas2
Waziri  Mkuu  Kassim Majaliwa akiwapa pole wafiwa  baada ya kutoa heshima za mwisho kwa  aliyekuwa Mshauri Mkuu wa Masuala ya Sheria wa Bunge, marehemu Oscar Mtenda nyumbani kwa marehemu mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
kas3
Baadhi ya waombolezaji walioshiriki katika ibada ya kumwombea aliyekuwa Mshauri Mkuu wa Masuala ya Sheria wa Bunge, maerehemu Oscar Mtenda iliyofanyika nyumbani kwake mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
kas4
Baadhi ya waombolezaji walioshiriki katika ibada ya kumwombea aliyekuwa Mshauri Mkuu wa Masuala ya Sheria wa Bunge, maerehemu Oscar Mtenda iliyofanyika nyumbani kwake mjini Dodoma Januari 26, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

KAIMU MKURUGENZI MKUU WA TAKUKURU ATANGAZA KIAMA KWA WALA RUSHWA HASA WATUMISHI WA UMMA

 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (Takukuru), Kamishna Valentino Mlowola akizungumza na wanahabari.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (Takukuru), Kamishna Valentino Mlowola (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini jijini Dar es Salaam leo asubuhi kuhusu mikakati mbalimbali ya taasisi hiyo ya kupambana na rushwa nchini hasa kwa watendaji wa Umma na kesi zinazochunguzwa ili watuhumiwa wafikishwe mahakama wakati wowote baada ya kukamilika kwa uchunguzi wake.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo. Kulia ni John David wa Gazeti la Majira.
 Mwendeshaji wa Mtandao wa Fullshangwe, John Bukuku (kulia), akiuliza swali katika mkutano huo.

Broad Based InterSect Organisation yatangaza tuzo mpya za AMAN

index1
Katibu Mtendaji wa Broad Based Intersect Organization (BBIO) Amani Joram Mgullo (katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya utambulisho wa Tuzo mpya za AMAN AWARD katika tasnia ya Muziki, Filamu na Habari. Kushoto ni Afisa Mahusiano Balozi Gepard na kulia ni Afisa Habari Salesi Malusa.
index2
Afisa Habari wa Broad Based Intersect Organization (BBIO) Salesi Malusa (Kulia) akitoa ufanunuzi kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) namna ambavyo wananchi watashiriki kuchagua washindi wa tuzo hizo kwa kuwapigia kura. Kushoto ni Katibu Mtendaji wa (BBIO) Amani Joram.
Picha na Beatrice Lyimo
…………………………………………………………….
Na Lilian Lundo-Maelezo Dar es Salaam
Taasisi isiyo ya kiserikali “Broad Based Intersect Organization” (BBIO) ambayo inaratibu uhamasishaji na uimarishaji wa mikakati ya maendeleo, yenye makao makuu mjini Dodoma imetambulisha tuzo mpya ziitwazo AMAN Awards katika tasnia za muziki, filamu na habari.
Tuzo hizo zimetambulishwa leo, jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa taasisi hiyo Aman Joram Mgullo.
Mgullo alisema kuwa, tuzo hizo zimetokana na mradi uitwao “Advocacy Mission Awards Network” (AMAN) unaohusika na uhamasisha na uimarishaji wa juhudi za utekelezaji wa mikakati ya maendeleo
“Wazo la utoaji wa tuzo za AMAN limekuja baada ya Tanzania pamoja na mataifa mengine ulimwenguni kuzindua mkakati mpya wa maendeleo (the Agenda 2030 of Sustainable Development Goals) ikiwa na adhima ya kutengeneza Maisha bora na Dunia bora kwa kila mwanadamu ulimwenguni,” alisema Mgullo.
Mgullo aliongeza kwa kusema kuwa, kutokana na mikakati mingi iliyotangulia kutofanikiwa kufikia malengo yake na kufanya jamii nyingi kuendelea kuishi katika hali duni ndicho kilichopelekea taasisi ya BBIO kufanya juhudi za ushawishi na uwezeshaji kupitia wasanii na wanahabari ili mradi huo wa maendeleo ufikie malengo yake kupitia tuzo za AMAN.
Kutokana na tafiti nyingi kuthibitisha kuwa tasnia za muziki na filamu, kupitia vyombo vya habari zinauwezo mkubwa wa ushawishi na uwezeshaji kwa jamii. Hivyo kwa kuwashilikisha wasanii kutoa ujumbe wa maendeleo kwa jamii kupitia tuzo za AMAN kutaleta mabadiliko kwa jamii ya Tanzania.
Mgulla alizitaja tuzo zitakazowaniwa kuwa ni Aman Music Awards, Aman Film Awards na Aman Media Awards ndani ya kila Tuzo kutakuwa na vipengele tofauti tofauti, na wananchi watashiriki kwa kupigia kura na kuchagua msanii au mwanahabari ambaye amefikisha ujumbe wa maendeleo katika jamii.
Lengo la tuzo za AMAN ni kuhakikisha dhima ya maisha bora na dunia kwa kila mwanadamu kwa kuchochea umahiri katika kutoa, kueneza na kufikisha ujumbe wa maendeleo endelevu kupitia tasnia za muziki, filamu na habari.

TAARIFA YA UFAFANUZI KUHUSU MALIPO YA UMEME KWA ASKARI POLISI

indexaa 
Katika gazeti la Tanzania Daima ukurasa wa 5, toleo namba 4070 la tarehe 25 Januari, 2016, lilichapisha habari yenye kichwa cha habari Polisi “waisoma” namba. Sehemu ya taarifa hiyo inaeleza kuwa askari Polisi hivi sasa wanatakiwa kujilipia gharama za umeme.
Jeshi la Polisi nchini, linakanusha vikali taarifa hiyo kwamba siyo sahihi. Ukweli ni kwamba askari polisi wote makambini wanalipiwa umeme na serikali, ikiwemo wale ambao nyumba zao zimefungiwa luku kama njia ya kuboresha huduma na matumizi sahihi ya umeme. Baada ya askari kununua umeme hutakiwa kuwasilisha stakabadhi ya malipo ya umeme kwa ajili ya kurudishiwa kiasi cha fedha walichonunulia umeme kila mwisho wa mwezi.
Aidha, habari iliyochapishwa na Tanzania Daima ililenga kupotosha umma na mwandishi wa habari hiyo hakutafuta ufafanuzi kutoka kwenye mamlaka husika.
Kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi nchini, linamtaka mhariri wa gazeti la Tanzania Daima na waandishi wake wa habari kuwa makini na habari wanazoziandika hasusani taarifa zinazohusu vyombo vya ulinzi na usalama ili kuepuka madhara ya kiusalama yanayoweza kutokea kutokana na habari wanazozitoa zisizo na usahihi.
Imetolewa na:-
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi,
Makao Makuu.

UDA YAKANUSHA JUU YA TAARIFA ZA KUFIRISIKA

Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Simon Group, Robert  Simon Kisena

Basata: Tamasha la Pasaka liwe njia ya jamii

BNa Mwandishi Wetu
……………………………….
BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) limeipongeza Kampuni ya Msama Promotions kwa utekelezaji wake wa majukumu yake kwa jamii.
Basata walieleza hayo baada ya kufanikisha kibali cha Tamasha la Pasaka linalotarajia kuanza kufanyika Machi 26-28 hapa nchini.
Kwa Mujibu wa Katibu Mtendaji Godfrey Mungereza,  Msama ameliandaa tamasha hilo kufanikisha waimbaji wa injili kupanda jukwaa moja bila kuchagua imani kwa kuamrishana  mema.
Mungereza alisema, waimbaji wa muziki wa injili wanabadilishana uzoefu hasa na waimbaji kutoka nje ya Tanzania ambako muziki huo unapiga hatua kimataifa.
Mungereza alisema kupitia tamasha hilo kutambulika zaidi ndani na nje ya mipaka ya Tanzania hiyo  ni ishara ya  kuendelea kufahamiana zaidi.
Aidha Mungereza alisema Tamasha la Pasaka linaiweka Tanzania katika sura ya kimataifa zaid i jambo  ambalo ni   la msingi kwa serikali.
Aliongeza kuwa  jamii inapata mafunzo mbalimbali kwani jamii kwani waimbaji na jamii wanaunganisha uelewa kupitia tamasha hilo.
Sambamba na hayo Mungereza alisema Tamasha la Pasaka ni sehemu ya jamii hasa katika uwakilishaji wa pato linalotokana na viingilio vya tamasha hilo.

TRA yawaomba wananchi kutoa ushirikiano

index 
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
……………………………………..
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) yawaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa za Maafisa wanaofanya kazi kinyume na maadili.
Akiongea na mwandishi wa habari hii leo Jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi Richard Kayombo amesema kuwa TRA ina Idara Maalumu ijulikanayo kama Idara ya Mambo ya Ndani ya TRA ambayo inashughulika na kufuatilia maadili ya watumishi wa sekta hiyo nchi nzima.
“Tunawaomba wananchi kushirikiana na Idara ya Mambo ya Ndani ya TRA kwa kuwapa taarifa juu ya maafisa wa TRA wanaokwenda kinyume na Maadili ya Utumishi wa Umma,”alisema Kayombo.
Mkurugenzi Kayombo ameongeza kuwa wananchi wanaweza kutoa taarifa kwa kupiga simu kwa namba 0689122515 au kwa kutuma ujumbe mfupi kwa simu namba 0689122516  na kuwahakikishia kuwa taarifa zao zitakua zimefika sehemu husika na zitafanyiwa kazi.
Aidha Kayombo amependa kuwatoa wasiwasi wananchi kuwa namba hizo ni za siri na hakuna mwananchi atakayepata tatizo lolote kwa kutoa taarifa za maafisa wasio na maadili.
TRA kupitia Idara yake ya Mambo ya Ndani imepokea malalamiko mengi kutoka kwa wananchi juu ya watumishi wa TRA wanaoenda kinyume na maadili, wameyafanyia uchunguzi na baadhi ya watumishi wamefukuzwa na wengine kupewa adhabu kali.

MADAKTARI BINGWA KUTOKA CHINA WAKISHIRIKIANA NA MADAKTARI WA ZANZIBAR WATOA HUDUMA ZA MATIBABU KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MATEMWE UNGUJA

S2Dokta Abdull Maulid Abdull akimpima Miwani ya kuonea Mwananchi Chale Muumin Fumu mkaazi wa Kijiji cha Matemwe Tunda ngaa katika matibabu yalio fanyika skuli ya matemwe mkoa wa Kaskazini unguja.
S3Dokta Rajab Mohd Haj akimkagua Jicho Mzee Muhidin M Ali Mkaazi wa Kijiji cha Matemwe katika matibabu yaliofanyika Skuli ya Matemwe Mkoa wa Kaskskazini Unguja.
S4Dokta Fei Jie kutoka China akimpima Masikio Bi Fatma Khamis Jaku mkaazi wa Kijiji cha Matemwe  Mfuruni katika matibabu yalio fanyika Skuli ya Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja.
S5Mtoto Iddi Khamis Juma akipatiwa huduma ya kupimwa uzito.
S6Daktari Bingwa kutoka China Yun Lai Gao kushoto na  Mwanafunzi kutoka Zanzibar School of Health Machano M Ali kwa pamoja wakipata maelezo kutoka kwa Mgonjwa anaesumbuliwa na maradhi ya Ganzi Haji Ali Mcha kabla ya kumtibu huko Skuli ya Matemwe.
S7Dokta Yu Lu akimgonga ngumi Mgonjwa anaesumbuliwa na maradhi ya Mgongo Mkadam Vuai kwaajili ya kumpatia matibabu ambayo yamekua yakimsumbua kwa muda mrefu.
S1Mwandishi wa habari wa Star TV Abdalla Pandu akimuhoji Mwanchi wa Kijiji cha Matemwe Mbupurini Chida Pili Khamis Juu ya Huduma za Afya zilizowafikia katika kijiji chao cha Matemwe Mkoa wa Kaskazini Unguja.
Picha na Abdalla Omar-Maelezo Zanzibar

UBALOZI MDOGO WA INDIA ZANZIBAR WAADHIMISHA MIAKA 67 YA UHURU WA JAMHURI YA INDIA

02Kaimu Balozi Mdogo wa India Govind Sharan Gupta akisalimiana na Wananchi mbalimbali wenye asili ya India wanaoshi Zanzibar waliohudhuria katika hafla ya kuadhimisha miaaka 67 ya Uhuru wa Jamhuri ya India iliyofanyika katika Ubalozi huo Migimbani mjini Zanzibar.
01Kaimu Balozi Mdogo wa India Govind Sharan Gupta akiwahutubia wananchi mbalimbali wanaoishi Zanzibar waliohudhuria katika kuadhimisha siku ya Uhuru wa Jamuhuri ya India kuadhimisha miaka 67 katika ofisi za Balozi migombani Zanzibar.
03Wananchi mbalimbali wanaioshi Zanzibar wenye asili ya India wakiimba wito wa Taifa la India
04Kaimu Balozi Mdogo wa India Govind Sharan Gupta akipandisha Bendera ya India kuashiria kuifungua sherehe ya Uhuru wa Jamuhuri ya India ya kutimiza miaka 67  katika Sherehe iliofanyka katika ubalozi huo Migombani Zanzibar
05Wananchi waliohudhuria katika hafla hiyo wakisherehekea baada ya kupandishwa Bendera ya Nchi ya India kuadhimisha miaaka 67 ya Uhuru wa Jamhuri ya India iliyofanyika katika Ubalozi huo Migimbani mjini Zanzibar.
Picha na Abdallah Omar-Maelezo Zanzibar 

Dk Shein Ashiriki Mazishi ya Marehemu Ramadhani Nyonje Pandu Zanzibar.

D1
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akishiriki dua ya kuuombea Mwili wa Marehemu Ramadhani Nyonje Pandu wakati alipofika nyumbani kwa marehemu fuoni michezani Unguja kutoa mkono wa pole kwa wanafamilia leo asubuhi.
D2
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akimfariji Mjane wa Marehemu Ramadhani Nyonje Panda alipofika nyumbani kwao fuoni michezani kutowa mkono wa pole kwa wana familia, kulia Kadhi Mkuu wa Zanzibar Shekh Khamis Haji Khamis.
D3
WANANCHI wakiwa katika msiba wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu aliyewahi kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni Zanzibar.
D4
WANANCHI wakiwa katika msiba wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu wakiwa nyumbani kwa marehemu fuoni michezani Unguja wakisubiri taratibu za mazishi ya marehemu  Ramadhani Nyonje Pandu  yaliyofanyika  Kijiji kwao Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja..
D5
WANANCHI wakisoma hitma ya marehe katika msiki wa fuoni kabla ya kusaliwa kwa ajili ya marehemu  Ramadhani Nyonje Pandu  yaliyofanyika  Kijiji kwao Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja…
  D7
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akijumuika na Wananchi katika kisomo cha hitma ya Marehemu Ramadhani Nyonje Pandu, iliosomwa katika msikiti wa fuoni.
D9
WANANCHI wakiitikia dua baada ya kusomwa kwa hitma ya marehemu Ramadhani Nyonje Pandu wakati ikisomwa na Shekh Soraga.
D8
WANANCHI wakiwa na jeneza likiwa na mwili wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu kwa ajili ya kusaliwa katika msikiti wa fuoni
D11
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein, akishiriki katika kubeba jeneza lililokuwa na mwili wa marehemu Ramadhani Nyonje Pandu aliyewahi kuwa Mwakilishi wa Jimbo la Muyuni Zanzibar na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM.
D12
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein na Viongozi na Wananchi wakishiriki katika Sala ya kumsalia marehemu Ramadhani Nyonje Pandu iliofanyika katika msikiti wa fuoni  marehemu  Ramadhani Nyonje Pandu  amezikwa Kijiji kwao Jambiani Wilaya ya Kusini Unguja..
(Picha na Ikulu)

MAJALIWA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI

1 2
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kwenye ukumbi wa TAMISEMI mjini Dodoma Januari 25, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

DTB YAAGA MWAKA KWA STYLE YA KIPEKEE


Wafanyakazi wa Tawi la Benki ya DTB Makao Makuu wakiwa katika picha ya pamoja baada ya tawi lao kupata tuzo ya Tawi Bora Tanzania 2015 kati ya matawi 24 ya benki hiyo ambapo 10 yapo Dar es Salaam na 14 mikoani. Meneja wa Tawi hilo, Shahista Karim (katikati) akiwa ameshikilia tuzo hiyo aliyokabidhiwa na Mkurugenzi Mkuu (hayupo pichani) katika sherehe za kufunga mwaka zilizofanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Ledger Plaza ulioko Bahari Beach.
PITON CHINI: Wanawake wa benki ya DTB wakicheza muziki wa asili katikasherehe za kuaga mwaka katika usiku uliokuwa na kauli mbiu ya ‘Usiku wa Afrika’. Sherehe hiyo ilifanyika katika ukumbi wa Ledger Plaza ulioko katika Hoteli ya BahariBeach jijini Dar es Salaam. Kati ya mambo ambayo sherehe hiyo ilisherehekea ni pamoja na kutambua mafanikio benki hiyo ilipata katika mwaka 2015. Kati ya matawi yote 24 nchini, Tawi la Masaki na lile la Makao makuu yaliibuka washindina kujizotea tuzo. DTB ina matawi 10 Jijini Dar es Salaam na 14 mikoani.

Buddha ya washiriki wakipakua chakula katika ghafla hiyo

Dance ilisakatwa chapati maelezo, JUU na CHINI baadhi ya wafanyakazi wa DTB kutoka katika matawi mbalimbali ya Benki hiyo wakiwajibika ipasavyo
KWA HISANI YA IMMA MATUKIO

Watumishi wa Umma wahimizwa kuvaa beji zianazoonesha majina yao.

indexKatibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue (akiwa amevaa beji inayoonesha jina lake) amewahimiza watumishi wote katika Utumishi wa Umma kuvaa beji zenye majina yao kila wakati wa kutekeleza majukumu yao ambapo amesisitiza kuwa ofisi zote zisimamie na kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu kila mtumishi awe na beji hiyo inachoonesha jina lake.
(Picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
………………………………………………………
Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue ameagiza na kusisitiza ofisi zote Umma kusimamia na kuhakikisha kuwa hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Machi mwaka huu kila watumishi awe na kitambulisho (beji) kinachoonesha jina lake.
Akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Balozi Sefue alisema hatua hiyo ya watumishi wa umma kuvaa beji zenye majina kila wakati wanapotekeleza majukumu yao itasaidia wananchi kuwatambua kwa majina watumishi wanaowahudumia na kuwasaidia kulingana na mahitaji yao kwenye ofisi hizo.
Ili kutekeleza azma ya kuwahudumia wananchi, Balozi Sefue alisema kuwa kuanzia sasa watumishi wote wa umma wavae beji zenye majina yao iwe rahisi kwa mwananchi kumtambua anayemhudumia na hivyo kumsifu mtumishi wa umma anayewahudumia kwa weledi, uaminifu na kwa wakati na kumtolea taarifa yule anayefanya mambo ya hovyo.
Zaidi ya hayo, Balozi Sefue amewahimiza viongozi na watumishi wote katika Utumishi wa Umma kubadilika kwa dhati kwenye utendaji na uadilifu wao na kuwahudumia wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na heshima.
“Rais na sisi wote tunaomsaidia hatuoni raha kuchukua hatua dhidi ya viongozi na watumishi wengine, tungependa kila mtu mwenyewe ajirekebishe na kutomfikisha Rais mahali ambapo inabidi amchukulie hatua” alisema Sefue.
Mambo muhimu yanayopaswa kuzingatiwa ni pamoja na kila kiongozi na mamlaka ya nidhamu isipate kigugumizi kusimamia utendaji na maadili ya kazi ili kuchukua hatua za nidhamu, lakini afanye hivyo kwa kuzingatia kwa ukamilifu sheria, kanuni na taratibu katika Utumishi wa Umma.
Balozi Sefue amewahimza viongozi na watumishi wa umma kuwahudumia wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na heshima ambapo kila ofisi ya Serikali inapaswa kuwa na dawati la kusikiliza shida za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
Kwa upande wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wote nchini wametakiwa kujenga uwezo wa kushughulikia shida za wananchi kwa ukamilifu na kwa wakati.
“Kwa muundo wa Serikali yetu hakuna sababu kwa mwananchi kufunga safari mpaka Ikulu Dar es Salaam kwa kuamini kuwa ni Rais tu ndiye anayeweza kumaliza matatizo yake, maana wawakilishi wa Rais wako kila pembe ya nchi yetu, ikibidi wananchi wafike Ikulu inamaana hao wawakilishi wa Rais hawakutimiza wajibu wao” aliongeza Balozi Sefue.
Aidha, Balozi Sefue alisema kuwa ofisi zote za Serikali zinatakiwa kuwa na dawati la kupokea maoni ya wananchi kuhusu huduma inayotolewa kwenye ofisi hizo na kushughulikia haraka maeneo yote ambayo wananchi wataonesha kutoridhika na huduma inayotolewa.

No comments :

Post a Comment