Sunday, December 6, 2015

Umoja wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika (CPA) wakutana leo Jijini Dar es Salaam CP1

CP1  
Mweka hazina wa Umoja wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Request Muntanga (Zambia) akiongoza kikao cha Bajeti cha Umoja huo kilichokutana leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu wa Bunge la Tanzania Dkt. Thomas Kashililah ambae pia ni Katibu wa Umoja huo Afrika.
CP2 
Mweka hazina wa Umoja wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Request Muntanga (Zambia) akipitia Jarida la Umoja huo wakati wa kikao cha Bajeti cha Umoja huo kilichokutana leo Jijini Dar es Salaam.
CP3 
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika ambaye pia ni Katibu wa Bunge la Tanzania Dkt. Thomas Kashililah akijadili jambo na msaidizi wake Ndg. Demitrius Mgalami wakati wa kikao cha Bajeti cha Umoja huo kilichokutana leo Jijini Dar es Salaam.
CP4 
Mwenyekiti wa Kamati tendaji ya Umoja wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola Kanda ya Afrika Mhe. Lindiwe Maseko (Afrika Kusini) akifafanua jambo wakati wa wa kikao cha Bajeti cha Umoja huo kilichokutana leo Jijini Dar es Salaam.

POLISI KUTUMIA “WHATSAPP” KUDHIBITI UHALIFU

AR1 
Mkuu wa Operesheni wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha (ACP) Edward Balele akifungua kikao kati ya Jeshi hilo na Taasisi za ulinzi kujadili mustakabali wa usalama ndani ya mkoa huu. Kikao hicho kilifanyika katika ukumbi wa Bwalo la Polisi Jijini hapa (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
AR2 
Meneja Mkuu wa Kampuni ya Ulinzi ya KK kanda ya Kaskazini Claude Herssens akichangia mada katika kikao kilichoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoani hapa na kuziusisha taasisi mbalimbali za ulinzi (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
AR3 
Baadhi ya washiriki wa Taasisi za Ulinzi wakiwa wanasikiliza moja ya mada kwa umakini ili baadae waweze kutekeleza kwa vitendo. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
AR4 
Katibu wa TUPSE kanda ya Kaskazini Aisha Masoud akielezea umuhimu wa mikataba baina ya waajiri na waajiriwa wa Makampuni ya Ulinzi. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)
AR5 
Mkuu wa Upelelezi ya Makosa Jinai Mkoa wa Arusha (SSP) Muliro Jumanne Muliro akielezea athari za kuwa na waajiriwa ambao hawana sifa kwenye kazi za ulinzi. (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi.
AR6 
Mkuu wa Kitengo cha Polisi Jamii Mkoa wa Arusha (SSP) Mary Lugola akitoa elimu ya Huduma bora kwa mteja kwa Makampuni ya Ulinzi (Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
……………………………………………………………………………………………………..
Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha
Jeshi la Polisi mkoani hapa limeazimia kushirikiana na Makapuni binafsi ya Ulinzi na taasisi za Ulinzi kutoka UN-ICTR, UNMICT, kitengo cha Ulinzi cha B.O.T pamoja na   Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu katika kupeana baadhi ya taarifa za uhalifu na wahalifu mara kwa mara kwa njia mtandao wa kijamii wa “whatsApp”.
Hayo yalisemwa na Mkuu wa Operesheni wa Jeshi hilo mkoani hapa (ACP) Edward Balele wakati akifungua kikao kilichofanyika katika Bwalo la Polisi mjini hapa alipokuwa anazungumza kwa niaba ya Kamanda wa Polisi Mkoani hapa mwishoni mwa wiki kati ya Jeshi hilo na wawakilishi wa Makampuni 31 ya Ulinzi, Benki Kuu Kanda ya Kaskazini, Mahakama ya Afrika ya Haki za Kibinadamu,UN-ICTR na UNMICT.
Mkuu huyo wa Operesheni alisema kwamba imefika wakati sasa kwa taasisi hizo kuzidi kuimarisha mahusiano kwa ukaribu huku njia za kisasa za mawasiliano zikitumika katika kupeana taarifa za uhalifu na pia kubadililishana uzoefu katika masuala ya ulinzi na usalama.
Alisema awali taarifa juu ya matukio mbalimbali sio kwamba zilikuwa hazipatikani bali zilikuwa zinawafikia walengwa kwa mtindo wa ujumbe mfupi yaani SMS lakini kwa kutumia mfumo wa kikundi cha “WhatsApp” ambacho kitapewa jina maalum, taasisi hizo zitakuwa zinapata na kutoa taarifa kwa pamoja na kila mhusika atakuwa anachangia mawazo yake huku wanachama wengine wa kikundi hicho wakiwa wanaona ushauri wa kila mchangiaji.
Aidha mbali na uundaji wa kundi hilo litakalotumia mtandao huo wa kijamii mbao umeshika kasi katika mawasiliano pia aliyaomba Makampuni hayo kutoa ushirikiano zaidi hasa kwa kutoa rasilimali vifaa pamoja na askari katika kuelekea mwisho wa mwaka kwa nia ya kufanya doria ya pamoja hivyo kudhibiti vitendo vya uhalifu ndani ya Mkoa wa Arusha.
Kwa upande wake Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Arusha (SSP) Muliro Jumanne Muliro alisema kwamba Jeshi la Polisi na Makampuni hayo kila chombo kikiwa kinawajibika ipasavyo katika nafasi yake mafanikio ya kudhibiti vitendo vya uhalifu yatakuwa makubwa.
Alisema anathamini mchango mkubwa unaotolewa na Makapuni hayo ya Ulinzi kwani matukio mengi ya uvunjaji wa Maghala ya viwanda, Ofisi mbalimbali na Makampuni yamepungua ukilinganisha na miaka ya nyuma kabla Makapuni hayo ya Ulinzi kukubaliwa kisheria.
Mkuu huyo wa Upelelezi alisema kwamba wakati wa uajiri wa askari hao wanatakiwa waangalie mambo mablimbali ikiwemo akili ya kuweza kugundua kitu kinachoashiria uhalifu, kuwa mwaminifu, kuwa mtulivu na kuwa mvumilivu na kusema kwamba huwa anafadhaishwa sana pale anapopata shauri linalomhusisha askari yoyote katika uhalifu hali ambayo inatia doa na aibu kwa taasisi zote za Ulinzi.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Polisi Jamii Mkoa wa Arusha Mrakibu Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SSP) Mary Lugola ambaye alizungumzia juu ya huduma bora kwa Mteja ambapo aliwataka Wawakilishi wa Makampuni hayo kuwaelekeza askari wao kuwa, wawe na lugha nzuri kwa wateja wao jambo ambalo pengine litakuwa linazidi kuwavutia wengine na hatimaye kupata malindo mengi ambayo yatawaongezea kipato, mbali na hilo pia aliwataka kutotumia nguvu kupita kiasi katika ukamataji ili kupunguza madhara makubwa yanayoweza kutokea.
Kwa upande wake Mkuu wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) Mkoa wa Arusha (SSP) Ramadhani Giro yeye aliyataka makampuni hayo kufanya mazoezi ya mara kwa mara na alisema baadhi ya Makampuni  ya Ulinzi huwa yanapata mafunzo mbalimbali kama vile matumizi sahihi ya silaha, ukakamavu na mbinu mbalimbali za kuweza kubaini uhalifu na wahalifu toka kwa askari waliopo katika kikosi hicho na kutoa wito kwa askari wa makapuni mengine kujitokeza ili waweze kupata mafunzo hayo na kupunguza madhara yanayoweza kutokea huko mbeleni.
Wakichangia katika kikao hicho baadhi ya wawakilishi wa Makampuni ya Ulinzi, Mwakilishi toka Kampuni ya KK Security ambaye pia ni Meneja Mkuu wa mikoa ya Kanda ya Kaskazini Bw. Claude Herssens alilisifu Jeshi la Polisi mkoani hapa kwa kuitikia wito kwa haraka pindi wanapoomba msaada na kuongeza kwamba mtandao huo utawasaidia sana na hivyo kuwafanya wajue tukio ambalo wanatakiwa kwenda kutoa msaada nje ya mipaka yao ya kazi na tukio ambalo litakuwa linawahusu Polisi pekee.
Naye Katibu wa Chama Cha waajiriwa wa Makampuni Binafsi Kanda ya Kaskazini (TUPSE) Aisha Masoud alizidi kusisitiza kwamba bado baadhi ya Kampuni hizo zinachangamoto hasa katika suala zima la mishahara ya wafanyakazi wao japokuwa serikali  toka mwaka 2013 mwezi Agosti ilishatangaza mishahara mipya lakini baadhi yao hawajatekeleza hilo na kuwataka wafanye hivyo pamoja na kuwaingiza katika mifuko ya Jamii.
Mara kwa mara Jeshi la Polisi Mkoani hapa limekuwa likifanya vikao na Makapuni ya Ulinzi lengo likiwa ni kukumbushana majukumu ya utendaji wa kazi za kila siku hali ambayo inasababisha kuimarika kwa hali ya usalama.

Serikali ya awamu ya tano yapongezwa

index 
Frank Mvungi-MAELEZO
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Magufuli amepongezwa kwa hatua ambazo Serikali yake imeanza kuzichukua ikiwemo kubana matumizi.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es salaam na Mfanyabiashara maarufu nchini Bw. Mohamed Raza wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliolenga kuipongeza Serikali kwa hatua inazochukua katika kuwaletea watanzania maendeleo.
Akifafanua Raza amesema sasa ni wakati muafaka kwa watanzania kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano kwa kuwa Mh. Rais John Pombe Magufuli ameonyesha dhamira ya dhati ya kuwakomboa watanzania kwa kujenga Tanzania mpya.
“Tumeshuhudia kwa dhati kabisa Mh. Rais akionyesha kwa vitendo dhamira yake ya kuwainua wanyonge kwa kubana matumizi ya Serikali ili fedha zitakazopatikana zitumike kuboresha huduma za jamaii na tayari ameshaanza kutekeleza hilo” alisisitiza Raza.
Katika kuimarisha huduma za jamii kama afya,elimu na miundo mbinu Raza amaesema kuwa tayari Serikali imeanza kufanya kazi kwa juhudi kubwa ili kuimarisha huduma hizo kote nchini.
Kwa kuzingatia umuhimu wa rasilimali za Taifa Raza amebainisha kuwa Serikali imeshaonyesha msimamo wake kuwa ni lazima zitumike kuwanufaisha watanzania wote na si vinginevyo .
Sambamba na juhudi za Serikali Raza amebainisha kuwa chama cha mapinduzi (CCM) kina ilani inayojibu changamoto za watanzania na itawanufaisha wote bila kujali itikadi za vyama na ndio maana CCM imeendelea kuaminiwa na watanzania kwa kupewa nafasi ya kuongoza nchi.
Pia Raza alitoa wito kwa watanzania wote bila kujali itikadi zao,rangi, wala maeneo wanayotoka kufanya kazi kwa bidii na kujituma ili kujiletea maendeleo kwa Kuwa Serikali ya awamu ya tano imeonyesha kwa vitendo dhamira hiyo na ni jukumu la kila mwananchi kuiunga mkono.
Baadhi ya hatua zilizochukuliwa na Serikali ya awamu ya tano ni kubana matumizi kwa kuondoa matumizi yasiyo ya lazima,kufuta safari za nje zisizo na ulazima, kusimamia kwa dhati ukusanyaji wa kodi na kusimamia kwa karibu utendaji Serikalini ili kuongeza tija kwa kutoa huduma bora kwa wananchi.

MTU MMOJA AFARIKI DUNIA KWA MOTO

blogger-image--1791117579
Na Mahmoud Ahmad Arusha
MTU moja amefariki dunia , na vyumba vinne vya madarasa na ofisi mbili za walimu zikiteketea wa moto usiku wa kuamkia leo.
Kaimu kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Arusha, Edward  BaleLe, amesema matukio hayo yanatokana na yanzo tofauti .
Amesema mtu mmoja ambae ni kijana amefariki kwa kuteketea kwa moto alipokuwa amelala kwenye nyumba ya mzazi  wake eneo la Njiro jijini Arusha.
Amesema kulingana na maelezo ya baba yake na marehemu, ambae ni mhadhiri mstaafu wa chuo ,mtoto wake alirejea majira ya saa tisa usiku  na kuingia ndani ya chumba chake na baada ya muda mfupi moto ulizuka na kuteketeza nyumba hiyo .
Amesema bado jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi kuhusiana na chanzo cha tukio hilo.
Amesema moto huo unasadikiwa ulizuka majira ya saa kumi usiku wa kuamkia leo muda mfupi tu baada ya marehemu kuingia ndani ya nyumba hiyo na kulala na ndipo moto ulipozuka na kuteketeza nyumba hiyo.
Katika tukio lingine vyumba vinne vya madarasa vimeteketea kwa moto kwenye shule ya msingi ya Daraja mbili ya jijini Arusha.
Kamanda Balele, amesema  chanzo ni hitilafu ya umeme ambayo imesababisha pia  ofisi mbili za walimu kuteketea kwenye tukio hilo na hasara kamili bado haijajulikana.
Wakati huo huo kamanda wa umoja wa vijana wa chama cha mapinduzi UVCCM mkoa wa Aruha, Philemon Mollel, ambae pia ni mgombea ubunge jimbo la Arusha, amefika kwenye shule hiyo na kuahidi tofali 2000 za Saruji.

Zaidi ya wagonjwa 200 kutoka maeneo mbalimbali mkoa wa Arusha wapewa elimu kutambua vyanzo vya magonjwa

02-2_organizing_help_for_major_operations 
Na Gladness Mushi,Arusha
ZAIDI ya wagonjwa 200 kutoka maeneo mbalimbali katika mkoa wa Arusha wamefanikiwa kupewa elimu ya kutambua vyanzo vya magonjwa yao pamoja na kuepukana na mbinu mbalimbali ambazo zinafanywa na wataaalamu wa afya kwa malengo ya kupata faida
Hataivyo Elimu hiyo imetolewa na Hospitali ya Shree Hindu Union Charitable iliopo maeneo ya Faya jijini Arusha ambapo elimu hiyo inatolewa bure kwa kila siku.
Akiongea na waandishi wa habari kuhusiana na mpango huo wa utoaji wa elimu, mganga mkuu wa hospitali hiyo Dkt Rajendra Patama alisema kuwa lengo halisi la kuanzisha mpango huo ni kuweza kuwaokoa watanzania ambao mara nyingi wanadanganyika kuwa wanaumwa na kumbe hawaumwi.
Rajendra alifafanua kuwa mpango huo umeanza hivi karibuni kwani kwa sasa wapo baadhi ya wataalamu wa afya ambao wanatumia mwanya wa wagonjwa kuumwa na kisha kuwabambikiza magonjwa ambayo sio yao ili waweze kuapata viapato vyao vya kila siku
Dkt huyo alidai kuwa hali hiyo inawafanya wagonjwa wengi kuishi kwa wasiwasi huku kwa upande wa wengine nao wakijikuta wanatumia dawa ingawaje hawaumwi na chochote hali ambayo nayo inasababisha miili kujaa sumu kubwa sana.
“Hapa kila siku lazima tutoe elimu ya magonjwa mbalimbali lakini hata kiiini cha magonjwa yanayoambukiza na yale ambayo hayaambukizi na ambao wameshapata elimu hii kwa kweli hawawezi kutapeliwa bali wanachukua tahadhari tuu wao na jamii zao”aliongeza.
Wakati huo huo alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa tiba kwa watanzania wameshaweza kuwasafirisha wagonjwa 6 nje ya nchi kwa ajili ya kuweza kufanyiwa vipimo na tiba kubwa na mpaka sasa hali za wagonjwa hao zinaenedelea vema.
“Huu mkakati wetu wa kuepukana na vifo visivyo vya lazima pamoja na kutoa elimu umeweza kuwasafirisha wagojwa 6 na bado tupo kwenye mchakato wa kuwasidia walio wengi zaidi”alisisitiza Dkt huyo.
Alimalizia kwa kuwataka watanzania hususani wanawake kuhakikisha kuwa wanajiwekea utaratibu wa kupima afya zao kila mara na pia kujitokeza kwa wingi kwani wanatarajia kutoa wataalamu wa masuala mbalimbali ya afya kutoka Nchini India.

WAFADHILI KUTOKA MAREKANI WATOA MSAADA WA MADAWATI YA MILIONI 6

images 
Na Gladness Mushi, ARUSHA
ASASI ya Joy Moja kutoka nchini Marekani imefanikiwa kutoa msaada wa madawati yenye thamani ya zaidi ya milioni 6 katika shule ya msingi ya Kisongo kwa malengo ya kuboresha elimu shuleni hapo
Akikabidhi msaada huo mapema jana mkurugenzi wa asasi hiyo hapa nchini,Gidion fanuely alisema kuwa msaada huo umetoka moja kwa moja marekani ambapo umelenga kuwasaidia watoto katika changamoto mbalimbali ambazo wanakabiliana nazo
Fanuely alisema kuwa asilimia kubwa ya wanafunzi wa kitanzania wanashindwa kufikia malengo yao kutokana na changamoto hususani za uhaba wa vifaa kama vile madawati hali ambayo inasababisha madhara  kwao
Alidai kuwa ili elimu iweze kuwa nzuri kuna hitajika kuwepo na vifaa vya uhakika ambapo moja ya vifaa hivyo ni kama vile madawati, lakini kama kukiwa hakuna madawati basi hata miandiko ya watoto itakuwa mibaya sana
Mbali na hayo fanueli alisema kuwa ufike wakati sasa wataalamu lakini wafadhili mbalimbali  wan chi mbalimbali waone changamoto ambazo zinaikabili sekta ya elimu hapa Tanzania na kamwe mzigo huo usibaki kwa serikali pekee kwani bado kuna changamoto lukuki.
‘asasi yetu ipo hapa Tanzania lakini hata marekani na tuliona kuwa watoto wa shule hii wanakabiliwa na changamoto kubwa sana hasa kwenye suala zima la madawati yaliyokuwepo ni michache ukilinganisha na uhitaji halisi na tumehaidi kuendelea kutoa msaada lengo tukimaanisha kuwa watoto wanatakiwa kuwa na ndoto na ndoto hizo zinaanzia kuanza shule za msingi’aliongeza
Naye mkuu wa shule hiyo Cosmas Lyimo alisema kuwa hapo awali madawati yalikuwa 171 na kwa sasa wafadhili hao wameleta madawati 80 ila bado kuna uhitaji wa madawati mengine 35
Lyimo alisema kuwa msaada huo wa madawati utakuwa ni chachu kubwa sana shuleni hapo kwani hapo awali watoto walikuwa wanaelekea kukaa chini kutokana na wingi wa watoto na madawati yakiwa machache
Alisema kuwa mbali na upungufu huo wa madawato lakini bado shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya uhaba wa viti vya walimu hali ambayo nayo inawafanya walimu washindwe kufanya kazi zao kwa raha hasa wanapokuwa madarasani.
“Kwa sasa tunaitaji viti 36 vilivyopo ni 16 pekee hivyo basi tunawaomba wafadhili wengine nao waje kututatulia changamoto hiyo ili tufundishe wanafunzi kwa raha zaidi na wapte elimu bora zaidi.

BALOZI WILSON MASILINGI AANZA ZIARA YA KUTEMBELEA VYAMA VYA SIASA DMV AHUDHURIA MKUTANO WA HALMASHAURI YA CCM DMV

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani Mhe. Wilson Masilingi leo Jumamosi Desemba 5, 2015 alihudhuria mkutano wa Halmashauri ya CCM tawi la DMV ikiwa ni moja ya ziara zake anazotarajiwa kuzifanya kutembelea matawi ya vyama vya siasa nchiMarekani yenye lengo la kudumisha mshikamano na ushirikiano wa Watanzania bila kujali itikadi za vyama vyao.
Akiongea kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV Mhe. Wilson Masilingi amesema lengo kuu ni kuwa karibu na vyama vya siasa kwa lengo la kuleta umoja na mshikamano ndani ya Jumuiya za Watanzania nchini Marekani na pia kuvitambua kama sehemu na sura ya Diaspora na kutoa wito kwa Watanzania waishio Marekani kuelekeza nguvu katika kuwekeza nyumbani bila kujali ufuasi wa chama unachoamini au kushabikia, wote ni Watanzania.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi aliiomba Halmashauri hiyo ya CCM DMV kusaidia katika maendeleo ya Tanzania kwa kupanua wigo wao pamoja na kwamba lengo lao ni siasa na siasa ni sehemu ya maisha ya jamii na maendeleo ya jamii yanategemea siasa, kwa hiyo basi mnaposikia kuna muwekezaji yupo tayari kuwekeza Tanzania msisite Ubalozi upo wazi na utafanya kila liwezekanalo kuhakikisha muwekezaji huyo hapati vikwazo vyovyote.
Mwisho Balozi Wilson Masilingi aliwashukuru Watanzania kwa kuwa mabalozi wazuri nchini Marekani na kuwaasa kuishi kwa kufuata misingi na sheria za nchi ya Marekani.
 Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea jambo na mwenyekiti wa tawi CCM DMV Bwn. George Sebo kwenye mkutano wa Halmashauri ya CCM DMV siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 mkutano uliofanyika Hampton Inn, College Park, Maryland. Picha na Kwanza 
Mkutano ulianza kwa sala na kuwakumbuka wote waliotangulia mbele ya haki.
Mwenyekiti tawi la CCM DMV Bwn. George Sebo akifungua kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV kilichofanyika siku ya Jumamosi Desemba 5, 2015 katika ukumbi wa Hampton Inn, College Park, Maryland.
Mhe. Balozi Wilson Masilingi akiongea machache kwenye kikao cha Halmashauri ya CCM DMV
Picha ya pamoja.
Bwn. John Mbatta katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Given  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Tino Malinda  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Aunty Grace Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Grace Mlingi  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mzee Joel  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Dr. Secelela Malecela  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Katibu wa CCM DMV Bi.Jesca Mushala  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.
Mwenyekiti wa CCM DMV Bwn. George Sebo  katika picha ya pamoja na Balozi Wilson Masilingi.

ABDALLAH LUWANJE NA SHEDRACK IGNAS WATAMBIANA KUPIGANA KATIKA MPAMBANO WA KUFUGUA MWAKA JANUAR 2 /2016

Mabondia Hassan Salumu kushoto na Hassan Mgosi wakitunishiana misuli baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Januari 2 katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es a salaam Picha na SUPER D BOXING NEWS
Na Mwandishi Wetu
MABONDIA mbalimbali wa ngumi za kulipwa wamesaini mkataba wa mpambano wa kufungua mwaka  kuzipika siku ya januar 2 mwakani katika ukumbi wa Frends Corner Manzese Dar es salaa
Akizungu wakati wa kusaini mikataba hiyo mratibu wa mpambano uho Rajabu Mhamila ‘Super D’ amesema kuwa mabondia walio wasainisha kuwa ni Shedrack Ignas atakaepambana na Abdallah Luwanje na
Hassan Salumu atakabiliana na
Hassan Mgosi nae Shomari Mirundi atapambana na Husein Mbonde na Ramadhani Maonya atakumbana na Said Faraji wakati Kelvin Majiba atakumbana na Ibrahimu Hamis mabondia wengine walio saini ni Mohamed Muhunzi na Mohamed Kashinde
Abdallah Pazi ‘Dula Mbabe’ atakumbana na Zumba Kukwe
Mpambano huo umeandaliwa na kampuni ya Butamanya General Tredes and Boxing Promotion imeandaa mpambano huo kwa ajili ya kukuza viwango vya mabondia chipukizi na kuimarisha zaidi wale wenye uwezo kwa ajili ya kuwapatia mipambano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi
Super D aliongeza kwa kusema kuwa siku hiyo kutakuwa na burudani za nguvu pamoja na ulinzi wa kutosha na ngumi zitaanza mapema ili wapenzi wa mchezo wa masumbwi warudi majumbani mapema wakiwa na furaha ya mchezo utakaochezwa siku hiyo.

WALIMU WA SKULI MBALI MBALI ZA WILAYA WAPATIWA MAFUNZO YA MICHEZO NA KAMATI YA OLIMPIKI TANZANIA (TOC) MJINI ZANZIBAR

ol1 
Mkufunzi wa Mafunzo ya Walimu wa Michezo wa Skuli yaliyoandaliwa na   Kamati ya  Olimpiki Tanzania  (TOC) Suleiman Mahmoudu Jabiri  akitowa maelezo kwa washiriki  katika siku ya mwisho ya mafunzo hayo yaliyoanza  tarehe 01 mwenzi huu.
ol2 
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu mbadala na Watu wazima Mashavu  Fak akifunga mafunzo ya walimu wa michezo wa Skuli katika  Skuli ya Elimu Mbadala Rahaaleo Mjini Zanzibar.
ol3 
Mkurugenzi wa Idara ya Elimu mbadala na Watu wazima Mashavu  Faki  akiwakabidhi vyeti washiriki  wa mafunzo  yaliyoandaliwa na Kamati ya  TOC  katika Ukumbi wa Elimu Mbadala Rahaleo Mjini Zanzibar.
……………………………………………………………………………………………………………..
Na Rahma Khamis Maelezo Zanzibar 
Idara ya ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar imeshauriwa kuwaandalia michezo nje ya nchi walimu wa michezo wa skuli kwa lengo la kujipatia taaluma zaidi na kukukuza mechezo nchini ,
Hayo yameelezwa huko Rahaleo katika Ukumbi wa Elimu Mbadala na Watu wazima na Mkurugenzi Idaraya hiyo Zanzibar Mashavu Faki  wakati akifunga mafunzo yalioandaliwa na  Kamati ya Olimpiki Tanzania  (TOC) yaliyofunguliwa tarehe 1 mwezi huu.
Amesema iwapo walimu wa michezo watapatiwa mafunzo zaidi nje ya nchi wataweza kuwasomesha wanafunzi wao wa skuli na kuinua sekta  ya michezo Zanzibar.
Mkurugenzi Mashavu amesema katika mwaka 2013 kulifanywa utafiti wa kimchezo na kuonekana kuwa nchi zinazoimarisha michezo maskulini ndizo zinazofanya  vizuri zaidi katika masomo yao.
Aidha amesema michezo huimarisha afya, kujenga  upendo, udugu na uzalendo katika jamii hivyo hakuna budi kuendelezwa  kwa manufaa ya wanamichezo wenyewe na Taifa kwa jumla.
Sambmba na hayo Mkurugenzi huyo amewashauri waalimu waliopata mafunzo hayo kwa kushirikiana na Idara husika  kuandaa mafunzo kila baada ya miezi mitatu.
Nae mkufunzi wa mafunzo hayo Suleiman Mahamoud Jabir amewataka washiriki wa mafunzo hayo kujenga moyo wa kujitolea kwani katika kufundisha mara nyingi hujitokeza matatizo mengi.
Kwa upande wao waalimu waliopata mafuzo hayo Mussa Abdulrab na Arafa Talib Omar wamesema   wamejifunza mambo mengi wasioyajua na kuahidi kuwa watayafanyia kazi.
Mafunzo hayo ya siku tano ya walimu wa michezo wa skuli mbali mbali za  Zanzibar yameandaliwa na Kamati  Tanzania.

RICHARD MWAIKENDA WA KAMANDA WA MATUKIO BLOG AACHANA NA UKAPERA

 Bibi harusi Mary Michael Mbaya (kushoto), akimvisha pete ya ndoa mume wake Richard Mwaikenda ambaye ni mpiga picha mkuu wa gazeti la Jambo Leo na mmiliki wa Kamanda wa Matukio Blog, baada ya kubariki ndoa yao katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kivule Dar es Salaam mchana huu.
 Bwana harusi Richard Mwaikenda akiwa amepozi na mke wake Mary Michael Mbaya wakati wa ibada yao ya ndoa.
 Mchungaji wa Kanisa hilo, Naory Chuma (kushoto), akiwabariki maharusi hao.
 Baba  wadogo wa bwana harusi Richard Mwaikenda wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Wazazi wa bibi na bwana harusi wakiwa kwenye ibada hiyo. 
 Ndugu na jamaa wa maharusi hao wakiwa katika ibada hiyo.
 Hapa ni furaha tupu kwa ndugu wa maharusi.

 Baadhi ya Waandishi wanaofanyakazi na bwana harusi wakijumuika katika ibada hiyo. Kutoka kushoto ni Peter Mwenda (Majira), Anicetus Mwesa, Said Mwishehe na Peter Ambilikile wote kutoka gazeti la Jambo Leo.
 Maharusi na wapambe wao wakiwa mbele ya kanisa.
 Wanandoa hao wakionesha shahada ya ndoa yao baada ya kukabidhiwa.
 Waumini wakiwa kwenye ibada hiyo.
 Maharusi hao wakitoka kanisani na wanandoa wenzao baada ya kufunga ndoa. Ndoa 11 zilifungwa katika kanisa hilo.
 Wanahabari wakiwa katika picha ya pamoja na maharusi hao.

Hapa ni furaha tupu. Wa tatu kulia ni mwanahabari, Nyakasagani Masenza.

WATENDAJI WA TAMISEMI WATAKIWA KUSIMAMIA SHERIA KUHUSU USAFI, UJENZI HOLELA, WANAOFANYA BIASHARA MAENEO YA DART

tam1 
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Jumanne  Sagini  wakati akizungumza na watendaji mbalimbali wa ofisi hiyo leo  katika mkutano wa kikazi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Karimjee jijini Dares Salaam , ambapo lengo kuu lilikuwa ni kutoa maelekezo ya utendaji kazi kama ilivyoagizwa na  Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa.Kulia ni  Naibu Katibu Mkuu Afya -TAMISEMI ,Dkt .Deo Mutasiwa .
tam2 
Baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) wakimsilikiza  Katibu Mkuu wa ofisi ambaye hayupo pichani.
tam3
Baadhi ya watendaji wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) wakimsilikiza  Katibu Mkuu wa ofisi ambaye hayupo pichani.
 Picha namba Magreth Kinabo- MAELEZO.
………………………………………………………………………………………………………………………..
Na Magreth Kinabo – maelezo
Serikali  imewataka  watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini kuhakikisha kwamba wanafanyakazi kwa uadilifu weledi wa taaluma zao na kufuata sheria zilizopo  katika kusimimia suala la usafi wa mazingira, likiwemo la kudhibiti biashara holela, gereji bubu,uegeshaji wa magari holela.
Pamoja na hayo wasimamie, upigaji holela wa muziki katika vilabu, baa  na kumbi  zaidi  ya saa zilizopangwa na kuzuia bodaboda  zinazosafirisha abiria hadi maeneo  ya miji katikati, pia kuzuia ujenzi holela.
Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Jumanne  Sagini  wakati akizungumza na watendaji mbalimbali wa ofisi hiyo  katika mkutano wa kikazi uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Karimjee, jijini Dar es Salaam ambapo lengo kuu lilikuwa ni kutoa maelekezo ya utendaji kazi kama ilivyoagizwa na  Waziri Mkuu Majaliwa Kassim Majaliwa.
 Akizungumzia kuhusu suala la usafi wa mazingira kufuatia  ziara iliyofanyika hivi karibuni imeonekana kuwa na changamoto mbalimbali  alisema;
“Kazi zetu  haziendi vizuri  kwa sababu hatusimamii  sheria zilizopo ndio kumekuwa na malalamiko katika utendaji wa kazi zetu, mfano katika suala la  gharama za usimamizi wa usafi wa mazingira ni kubwa . Lakini kinachofanyika ni kweli  kinalinganishwa na gharama  hizi?” alihoji  Katibu Mkuu huyo.
 Akitolea mifano  gharama zinazotumika  katika suala hilo, kwa kipindi cha mwaka wa fedha wa 2014/2015  alisema kwa upande wa manispaa ya Kindondoni wanatumia Sh. bilioni 2.6, Ilala  ni Sh. bilioni 2.6, wakati Temeke wanatumia Sh. bilioni 1.2 .
“Kilichobainika  ni kwamba  mikataba ya watu wanaojishughulisha na  usimamizi wa usafi wa mazingira ni ya mwaka mmoja na wanaopewa  mikataba hiyo ni watu ambao hawana uwezo wa kutosha wa kutekeleza jukumu hilo.
“ Ama  watu wasio na uwezo ama mnaofahamiana nao.  Au kampuni zenye mahusiano na baadhi ya watumishi wa mamlaka za serikali za mitaa au  wenye uhusiano  na viongozi wenu, Jiepusheni  na kuwapa watu hawa kwa sababu  kutokana na hali hiyo hamtaweza kukabiliana  nao. Kama   kuna kiongozi ambaye  mmepatia nafasi hii  lazima athibitishe kuwa na uwezo. Na kama pia ni miongoni  mwenu  hakikisheni kuwa ni mtu mwenye uwezo. Kazi zetu haziendi vizuri kwa sababu ya nasaba au viongozi wenu,” alisisitiza  Katibu Mkuu huyo, huku akisema lazima  wabadilike na kuangalia kama  hawana  uwezo wajitoe au wafukuzwe.
 Aliongeza kwamba katika suala hilo kumekuwa na migongano  ya watumishi  wa halmashauri ambao wanatakiwa kufanya kazi kama timu;  mfano maafisa  afya, mazingira na usafishaji,  lakini akasema wanaonana kama maadui.
“ Hawa  wangepaswa kufanya kazi kwa kushirikiana ,lakini ni maadui kwa sababu ya maslahi … hili ni lenu wakurugenzi  kwani hata watoto wako  wakisambaratika ni lazima huwaketishe chini  ili mambo yaende,  asiyekubali unamwajibisha,” alisema.
Sagini alisema watendaji hao , wote ni wadau wa usafi, hivyo wanapaswa kufanya kazi kwa ushirikiano, hivyo aliwataka wapeane  mikono katika kikao hicho, ambapo walifanya hivyo ikiwa ni hatua ya kuonesha ushirikiano.
Pia alisema watu wanaosafirisha  bidhaa za vyakula kwa kutumia  majani ya migomba au matenga wasiruhusiwe kufanya hivyo wapewa muda wa wiki moja au mbili kutumia utaratibu mwingine.
 Aliwataka pia watendaji mbalimbali wa TAMISEMI kuwa na ushirikishwaji katika ngazi za chini kwenye halmashauri kwa kuwa haliko vizuri.
 Sagini alisema ni vizuri kukawekwa mfumo wa TAMISEMI  wa  kushirikisha ngazi za chini kama ilivyo kwa mjumbe wa nyumba kumi kwenye masuala ya vyama .
“ Ni lazima tuingie katika mfumo huu wa  kuwa na watendaji  wa kaya 30  ambao watakuwa  chini ya TAMISEMI . Suala hili lina faida  ya ulinzi na  usalama  na kuwatambua wageni…  tunaangalia jinsi ya kulitekeleza,” alisema.
Aliwataka wakurugenzi wasikae maofisini kwenye madawati bali watembelee maeneo mbalimbali  ili kutatua kero za wananchi na kuangalia mipangilio ya miji na majiji.
Katika suala hilo la usafi wa mazingira alisema mtu mwenye uwezo wa kusafisha jiji liwe safi apewe nafasi huku akisisitiza suala la kushirikisha sekta binafsi ni muhimu katika mambo mbalimbali  likiwemo la ujengaji wa maegesho ya magari, ambapo sasa  yanahitajika kwa ajili ya mradi wa mabasi yaendayo haraka(DART).
“ Kwenye  eneo hili la DART lazima  mbadilike tunataka barabara za DART ziwe nyeupe yaani watu wasifanye biashara,” alisisitiza huku akitaka kuanzia Jumatatu wiki ijayo  yatekelezwe.
Aliwataka watu wanaohusika  na vyombo vya usafiri na usafirishaji kutovunja sheria, akatolea mfano boda boda.

RED AVENUE PARTY RELOADED DESEMBA 26, 2015

Michango ya wasamaria wema yafanikisha Dada Joyce wa Mbeya kuwasili Muhimbili kwa matibabu

 Dada Joyce akiwa ameketi kwa utulivu kwenye siti yake ndani ya ndege
…………………………………………………………………………………………………………

 Mpiganaji Deo Kakuru akiwa na dada Joyce ndani ya FastJet wakitoka Mbeya keuelekea Dar es salaam 
 Mpiganaji Deo Kkuru akiwa na dada Joyce mara baada ya kuwasili  Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es salaam
 Msamaria mwema Mama Rozi akimhudumia dada Joyce akiwa kitandani kwake Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha mifupa cha MOI katika wodi ijulikanayo kama Wodi ya Magufuli ghorofa ya tatu
 Dada Joyce akiwa wodini Moi


MATUKIO YA PICHA ZA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU SEMINA YA MAGONJWA YASIYOPEWA KIPAUMBELE

VC1 
Mwezeshaji wa Semina hiyo Andreas Nshala ambaye ni Afisa Mipango akitoa elimu juu ya magonjwa yasiyopewa kipaumbele jana wakati semina kwa waandishi wa habari kuhusu magonjwa yasiyopewa kiupaumbele iliyofanyika hivi karibuni  kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini  Dare Salaam.(Picha zote na Magreth Kinabo – maelezo)
VC2 
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo.
VC4 
Mkurugenzi wa Idara ya  Kinga kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Neema Rusibamayila akifungua semina kwa waandishi wa habari kuhusu magonjwa yasiyopewa kiupaumbele iliyofanyika  hivi karibuni  kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini  Dare Salaam.
VC5 
Mratibu wa Kitaifa wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele, Dkt. Upendo Mwingira akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jana kuhusu magonjwa yasiyopewa kiupaumbele katika semina  iliyofanyika hivi karibuni  kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini  Dare Salaam.

TGDC NA KAMPUNI YA TOSHIBA WATILIANA SAINI MKATABA WA MAELEWANO (MOU) WA UTAFUTAJI WA NISHATI YA JOTOARDHI

tg1 
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakiweka saini Mkataba wa wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.
tg2 
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) akikabidhi zawadi ya kinyago cha Twiga kwa Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara mara baada ya kusaini Mkataba wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.
tg3 
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kulia) akikabidhi zawadi ya kinyago cha Kimasai kwa Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara mara baada ya kusaini Mkataba wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.
……………………………………………………………………………………………
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC) pamoja na Kampuni ya TOSHIBA ya nchini Japan zimetiliana saini Mkataba wa Maelewano wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi.
Utiaji saini wa mkataba huo umefanyika Desemba 4, 2015 Jijini Dar es Salaam katika Ofisi za TGDC ambapo hatua hiyo itaiwezesha TGDC kuweza kupata msaada wa kitaalam ambao utaliwezesha shirika hilo kuweza kuchimba ardhini kwa lengo la kupata mvuke utakaoweza kuzalisha umeme.
Akiongea ofisini kwake, Meneja Mkuu wa TGDC, Mhandisi Boniface Njombe amesema kuwa kupitia Serikali ya Japan hususani Shirika la Maendeleo Japan (JICA), Kampuni ya TOSHIBA watasaidia kuomba ufadhili wa Serikali yao ili kuweza kuendeleza ujenzi wa kituo cha kuzalisha umeme pamoja na matumizi mengine yanayoendana na nishati hiyo.
“Katika utafiti wa nishati ya jotoardhi tunahitaji watu wenye elimu na uzoefu na ujuzi wa kutosha, miongoni mwa makubaliano ndani ya mkataba huu tuliosaini leo ni wafanyakazi wetu kadhaa kuwapeleka nchini Japan kwenye vyuo vyao ili kuweza kupata mafunzo ya darasani na kutembelea maeneo ambayo Japan wana vituo vya jotoardhi ili wapate ujuzi wa kufanya kazi na Wajapan na kutuletea ujuzi huo hapa nchini”, alisema Njombe.
Aidha, ameeleza kuwa kupitia ushirikiano huo na Serikali ya Awamu ya Tano, nchi ya Japan itaendelea kuisadia Tanzania katika kuendeleza nishati ya jotoardhi kwakuwa ni nishati yenye tija katika kutimiza ndoto za Tanzania kwa kuifanya kuwa nchi yenye kipato cha kati kufikia mwaka 2020.
Mhandisi Njombe aliongeza kuwa kwa niaba ya Serikali TGDC iko tayari kushirikiana na TOSHIBA ambapo Januari mwakani wataanza kuaninisha maeneo ya ushirikiano huo na kuyawekea muda wa utekelezaji na mwezi Machi Wataalam toka TGDC wataweza kwenda nchini Japan kwa ajili ya kwenda kupata elimu zaidi ya nishati hiyo.
Kwa upande wake Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara ameeleza kuwa kampuni yao iko tayari kuisaidia Tanzania katika masuala yanayohusu jotoardhi na iko tayari kuomba ufadhili kupitia Serikali ya Japan ikiwemo kuwapa Wataalam wa TGDC elimu ya kutosha inayohusu nishati hiyo ili waweze kuhkikisha kuwa nishati hiyo inapatikana na kuleta maendeleo kwa Tanzania.
“Tunafuraha ya kushirikiana na TGDC katika kufanya tafiti zinazohusu jotoardhi kama mkataba wetu tuliousaini unavyosema, kupitia Serikali ya Japan na Shirika la JICA tutaomba ufadhili kwa ajili ya TGDC ili muweze kuleta wataalam wenu kuja kujifunza Japan pamoja kuwasaidia katika masuala mengine yanayohusu shughuli ya utafutaji wa nishati hii”, alisema Kurahara.
TGDC ni Shirika Tanzu lililopo chini ya Kampuni ya Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) ambapo limepewa lengo na Serikali la kuharakisha upatikanaji wa nishati ya jotoardhi kufikia Megawati 200 mwaka 2020.

KONGAMANO LA MSAFARA LILILOFANYIKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM LAWAJENGA VIJANA WENGI

 Msanii
wa sanaa za Maonesho Vanensia Shule, ambaye pia ni Mkufunzi wa Chuo
kikuu cha Dar es salaam upande wa sanaa na Filamu akielezea jinsi Sanaa
inavyoweza kumkomboa kijana,na kutoa mifano ya baadhi ya wasanii
walioanzia chini na sasa wanamafanikio makubwa.
Baadhi ya vijana wakionesha ishara ya ushindi  
Alphonse
Matata ambaye anajihusisha na kilimo pia Mjasiliamali kupitia ufugaji
wa nyuki akielezea safari yake ya mafanikio ,na kuwashauri vijana
wasingoje kuajiliwa bali wawe wabunifu na kujiunga katika ujasiliamali, jana tarehe 4.12.2015
 Rais
wa Serikali ya wanafunzi Chuo kikuu cha Dar es salaam Kitaponda Ahadi,
akielezea kuhusu elimu na changamoto alizo zipata wakati wa akiwa Shule
mpaka ndoto yake ilivyotimia ya kuja kusoma chuo kikuu na kuwa kiongozi,
amewasihi vijana wenzake wasikate tamaa wafanye bidii katika masomo
watafikia malengo.
……………………………………………………………….
Vijana
mbalimbali wamejitokeza katika kongamano la msafara kusikiliza baadhi
ya vijana wenzao ambao wametoa historia zao kuhusu walipotokea mpaka
wamefanikiwa kufika hapo walipofikia na kuwatia moyo vijana wengine
wasikate tamaa kwa sababu mafanikio yapo.
Msafara
ambao unalenga kuibua na kurudisha ndoto za vijana katika sekta zote
kwa kutambua kuwa kila eneo lina mchango mkubwa katika mafanikio na
maendeleo ya vijana. Wazungumzaji tofauti tofauti walijikita katika
maeneo makuu yafuatayo Sayansi na Teknolojia,Kilimo, Biashara, Sanaa na
usanii, Elimu, Uongozi, Michezo, utunzaji Mazingira, haki sawa za
kijinsia pamoja na harakati.
Maeneo
hayo yalikuwa ni nguzo kuu ya kufanya vijana kuwa na fursa ya
kukabiliana na changamoto za kimaisha katika kufikia mafanikio na
malengo yao. Katika safari hii ya Msafara matukio mbalimbali yatafanyika
ikiwemo kuwaleta vijana wa rika moja wenye umri wa miaka 15-24 ili
kuwaleta kwa pamoja wapate kujifunza kutoka kwa wengine waliofanikiwa,
wenye fani mbalimbali/Taaruma zao, hii itawajengea ujasili wengine
katika kufikia mafanikio yao.
Progamu
hii inaendeshwa na muungano wa Mashirika na Makundi Matano yaliyopo
hapa Tanzania ikiwa ni pamoja na DARUSO, YouthCAN, NGAO YOUTH na Young
Feminist Forum na inaratibiwa na Oxfam Tanzania, msafara itakuwa ni moja
ya fursa kwa vijana kutangaza na kuonesha ubunifu wao na mafanikio
waliyofikia kimaisha ingawa kuna changamoto na vikwazo mbalimbali. Safari ya
msafara itaendelea Ifakara mkoani Morogoro tarehe 12.12.2015

No comments :

Post a Comment