Tuesday, December 8, 2015

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA MABALOZI WA MALAWI NA SWEDEN IKULU JIJINI DAR ES SALAAM

 
bal1
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Balozi wa Malawi hapa nchini Mhe. Hawa Ndilowe  Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 8, 2015
bal2 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika mazungumzo  na Balozi wa Malawi hapa nchini Mhe. Hawa Ndilowe  Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 8, 2015
bal3 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimsindikiza  na Balozi wa Malawi hapa nchini Mhe. Hawa Ndilowe baada ya mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 8, 2015
bal5 
Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akipokea barua za salamu toka na Balozi wa Sweden hapa nchini Mhe. Katarina Rangnitt alipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Jumanne Desemba 8, 2015.
PICHA NA IKULU

Muhimbili Yaendelea Kupokea Misaada

mse1 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Mseru akizungumza leo katika mkutano uliowajumuisha viongozi wa Jumuiya ya Australia na Tanzania kabla ya hospitali hiyo kukabidhiwa vifaa vya wagonjwa vikiwamo vitanda na baiskeli za magurudumu matatu.
mse2 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Australia na Tanzania, Didier Murcia akimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Mseru leo wakati wa mkutano na viongozi wa jumuiya hiyo na wataalamu wa hospitali hiyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Upasuaji, Dk John Kimario wa MNH.
mse3 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Wateja, Aminieli Aligaesha akiwa katika mkutano huo uliofanyika leo kabla ya kukabidhiwa kwa vifaa vinavyotumika kuwasaidia wagonjwa wakati wa kupatiwa matibabu.
mse7 
Mkuu wa Idara ya Uuguzi na Mazingira ya Ndani, Bi. Zuhura Mawona akisalimiana na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Australia na Tanzania, Didier Murcia kabla ya kupokewa kwa msaada huo leo katika hospitali hiyo.
mse8 
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Australia na Tanzania, Didier Murcia akiwa katika picha ya pamoja na wauguzi wa hospitali hiyo baada ya kukabidhiwa msaada huo leo.
mse5 
Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Bi. Agness Mtawa akipokea msaada wa vitanda na vifaa vingine leo kwenye hospitali hiyo. Katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Australia na Tanzania, Didier Murcia akimkabidhi Sister Mtawa vifaa hivyo na kulia ni Mkurugenzi wa jumuiya hiyo, Thierry Murcia.
……………………………………………………………………………………
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imepokea msaada wa vifaa mbalimbali vitakavyotumika kuwahudumia wagonjwa katika hospitali hiyo.
Msaada wa vitanda kumi utatumika katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) pamoja na wodi nyingine. Msaada huo umetolewa na Jumuiya ya Australia na Tanzania.
Vifaa vingine vilivyotolewa ni pamoja na  Stretcher’  nne zitakazotumika kusafirishia wagonjwa ambao hawawezi kukaa, kifaa cha kufanyia  mazoezi  kwa wagonjwa  na baiskeli ya magurudumu matatu.
 Akipokea msaada huo  Mkurugenzi wa Huduma za Uuguzi katika hiyo Agness Mtawa ameishukuru Jumuiya hiyo na kutoa rai kwa wadau wengine kuendelea kutoa msaada katika hospitali hiyo.

SERIKALI YA JPM KIBOKO, “UKIBEEP WANAPIGA”, DKT MPANGO ATINGA TRA SAMORA BAADA YA MWANANCHI KUTUPIA UJUMBE MTANDAONI

KUNA ule msemo wa watu wa mjini, “Uki-beep, napiga” na kweli leo hii Desemba 8, 2015 pale Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA, barabara ya Samora katikati ya jiji la Dar es Salaam, mlipa kodi mmoja alitupia ujumbe kwenye mtandao wa kijamii akiomba wataalamu wa IT wa TRA, wafike haraka kwenye ofisi zao za TRA Barabara ya Samora kwani mitambo ya ku-print Motor Vehicles License ime-collapse”, na watu wamekaa tu wasijue la kufanya.
 
ilichukua kama dakika 15 au 20 hivi, watu wawili waliovalia suti maridhawa na dada mmoja “aliyeshiba”, walitinga kwenye ofisi hizo, na kukuta walipa kodi wakiwa wamejazana kwenye mabenchi wakijipepea tu, kutokana na joto kali.
 
Mmoja wa watu hao waliovaia suti, alianza kuwauliza walipa kodi, “Jamani vipi huduma za hapa mnaridhika nazo.”? Aliuliza mmoja wao.
 
Walipa kodi hao kwanza walimtazama, na mmoja “akajilipua”, hapana haturidhiki nazo, hapa unapotuona tumeshakaa sana, huduma hakuna tunaambiwa mtandao haupo, tumeshindwa kuchapishiwa stika za malipo ya kodi ya barabarani.
 
Mwingine akasema, hata hali ya hewa humu ndani kama unavyoiona joto kali, hakuna viyoyozi, na tumekuja kulipa kodi hii ni sawa??, akahoji mlipa kodi huyo.
 
Baada ya majibu hayo, Mlipa kodi mmoja aliibuka na kuwaambia wenzake, jamani semeni huyo ndiye bosi mpya wa TRA, “tiririkeni” yaani semeni, na hapo malalamiko yakawa mengi, naye bosi huyo ambaye si mwingine bali ni Dkt. Philip Mpango, ambaye hivi karibuni,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, alimteua kukaimu nafasi ya Kamishna Mkuu wa TRA, akiziba nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Kamishna Rished Bade, akawajibu, nimeyapokea malalamiko yenu, na ndiyo maana mmeniona niko hapa, nilipokea ujumbe kutoka kwa mlipa kodi akilalamika kuwa hapa kwenye tawi letu huduma zimesimama, nikaona nfike kujua nini kimetokea. Alisema Dkt. Mpango akiwaambia walipa kodi hao ambao walionekana kufurahishwa na maneno hayo.
Wakati akiwaeleza hayo, mitambo hiyo ghafla ikaanza kufanya kazi na waliokuwa jirani na madirisha walianza kuitwa mmoja mmoja na kupatiwa huduma.
Hiyo ndiyo serikali mpya ya awamu ya tano yenye kauli mbiu “Hapa Kazi Tu”, hakuna kulala kila mtu anapiga kazi tu.
 “figisu figisu” ya kile wafanyakazi wa hapo waliwaambia wateja wao kuwa “system iko down”, yaani kwa maana ambayo wao wamezoea kuwaambia wateja kuwa mtandao wa computer haufanyi kazi kwa hivyo walipa kodi kibao waliokuwepo kwenye ofisi hizo, walilazimika kukaa tu kwenye mabenchi wakimuomba mungu mtandao huo upone ili waweze kupata “stika” za magari yaani Motor Vehicles License.
Pichani Dkt. Mpango (kushoto), akizungumza na walipa kodi hao kwenye tawi la TRA, barabara ya Samora Desemba 8, 2015
 Khalfan Said Photojournalist K-VIS MEDIA P.Box 77807 Mobile; +255 646-453/+255-653-813-033 Blog:http//khalfansaid.blogspot.com Dar es Salaam, Tanzania

KAMPUNI YA MAFUTA YA PUMA YATEKELEZA AGIZO LA RAIS YAKABIDHI VIFAA VYA USAFI VYA MILIONI 5.5 MANISPAA YA TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM LEO

 Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti (wa tatau kulia), akimkabidhi vifaa mbalimbali vya usafi wa mazingira vyenye thamani ya sh.milioni 5.5, Katibu Tawala (DAS), wa Wilaya ya Temeke, Laurence Mlangwa Dar es Salaam leo mchana, kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Sophia Mjema kwa ajili ya kusaidia kufanyia usafi leo hii ikiwa ni kuunga mkono agizo la Rais Dk. John Magufuli la kutumia Sikukuu ya Uhuru kufanya usafi nchini kote. Kulia ni Ofisa Usalama na Mazingira wa Puma, Jonathan Mmari na wengine ni maofisa kutoka Manispaa ya Temeke
 Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti, akizungumza kabla ya kukabidhi vifaa hivyo.
 Ofisa Usalama na Mangira wa Puma, Amani Mmari (kulia) akizungumza katika mkutano huo wa makabidhiano wa vifaa hivyo. Wa pili kulia ni Meneja Rasimali Watu (HR) wa Puma, Loveness Hoyange.
 Vifaa hivyo vikikaguliwa.
 Mkurugenzi wa Puma akitoa maelekezo wakati wakikabidhi vifaa hivyo.
 Vifaa hivyo vikipangwa katika toroli.
 Mazungumzo ya hapa na pale yakiendelea wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo.
 Baadhi ya vifaa hivyo.
 Matoroli yaliyokabidhiwa na Puma kwa Manispaa ya Temeke.
Matoroli yakipakiwa katika gari la Manispaa ya Temeke baada ya kukabidhiwa.
…………………………………………………………………………….
Na Dotto Mwaibale
 
KAMPUNI ya Mafuta ya Puma imetoa vifaa vya usafi wa mazingira vyenye thamani ya sh.milioni 5.5 kwa manispaa ya Temeke ili kutekeleza agizo la Rais John Magufuli alilotaka kila mmoja wetu kushiriki kufanya usafi katika kilele cha Sikukuu ya Uhuru ambayo inafanyika nchini kote leo.
 
Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo kwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Temeke, Laurence Mlangwa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Sophia Mjema Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Puma Energy Tanzania, Philippe Corsaletti alisema aliguswa mno na agizo la Rais na kuona ni vema Puma nao wakamuunga mkono rais.
 
“Baada ya kusikia katika vyombo vya habari kuwa rais ameagiza katika sikukuu ya uhuru mwaka huu badala ya kufanya sherehe  hufanyike usafi niliguswa na kuamua kumuunga mkono” alisema Corsaletti.
 
Alisema wameamua kutoa vifaa hivyo kwa manispaa ya Temeke ili kusaidia kazi ya usafi katika maeneo mbalimbali ambao utafanyika leo nchini kote.
 
Alitaja baadhi ya vifaa hivyo kuwa ni matoroli 10, mipira ya kuvaa mikononi wakati wa kufanya usafi, viatu vya mvua, vizibao na vinginevyo vyote vikiwa na thamani ya sh.milioni 5.5
 
Kwa upande wake Katibu Tawala wa Manispaa hiyo Laurence Mlangwa akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya hiyo, aliishukuru Kampuni hiyo kwa kutoa vifaa hivyo ambapo alisema vifika wakati muafaka ambapo leo vitatumika kufanyia usafi kama Rais Magufuli alivyo agiza.
 
Alisema shughuli za usafi huo zitaanzia viwanja vya Mbagala Zakhem na kutawanyika kuelekea maeneo mengione mbalimbali.
 

KAMISHNA JENERALI WA JESHI LA MAGEREZA NCHINI AONGOZA KIKAO MAALUM CHA KUPITIA RASIMU YA MPANGO WA WA JESHI LA MAGEREZA

min1 
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza, John Casmir Minja akifungua Kikao Maalum cha Wadau kutoka nje ya Magereza(hawapo pichani) cha kujadili rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani. Kikao hicho kimefanyika leo Desemba 8, 2015 katika Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi hilo Jijini Dar es Salaam.
min2 
Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Beatus Kundy(aliyesimama) akiwasilisha rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani. Jeshi la Magereza limeandaa rasimu hiyo ili kuipunguzia Serikali gharama za kuwalisha wafungwa waliopo magerezani.
min3 
Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakifuatilia kwa makini uwasilishaji wa Andiko hilo(wa kwanza kulia) ni Kamishna wa Huduma za Urekebishaji, Eng. Deonice Chamulesile(wa pili kulia) ni Kamishna wa Sheria na Uendeshaji wa Magereza, Dkt. Juma Malewa(wa pili kushoto) ni Kamishna wa Fedha na Utawala wa Magereza, Gaston Sanga.
min4 
Mwakilishi kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Hashim Kimmwe akitoa mchango wake wakati wa kujadili rasimu ya Mpango wa Jeshi la Magereza wa kujitosheleza kwa chakula cha Wafungwa waliopo Magerezani.
min5 
Wataalam wa Jeshi la Magereza walioshiriki kikamilifu katika maandalizi ya Andiko la Mpango wa Jeshi la Magereza kujitosheleza kwa chakula kwa kushirikiana na Mshauri Mwelekezi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakifuatilia majadiliano ya rasimu hiyo(Picha zote na Lucas Mboje wa Jeshi la Magereza).

Katibu mtendaji BAKITA amkabidhi kamusi kuu mpya ya kiswahili katibu mkuu wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo.

index 
Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel(kulia) akikabidhiwa kamusi kuu mpya ya Kiswahili kutoka kwa Katibu Mtendaji kutoka baraza la Kiswahili la Taifa(BAKITA) Dkt Selemani Sewangi.Kamusi hiyo mpya ina jumla ya maneno makuu Zaidi ya elfu thelathini na sita(36000) na kurasa 1264.
index2 
Katibu Mtendaji kutoka baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Dkt Selemani Sewangi(kushoto) akitoa ufafanuzi kwa Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Profesa Elisante Ole Gabriel kwa baadhi ya maneno ambayo yapo katika kamusi mpya iliyotolewa na Baraza hilo leo jijini Dar es Salaam.

TFF YATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI

baf 
Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limetuma salamu za rambirambi kwa familia ya marehem Willie Chiwango aliyefariki dunia mwishoni mwa wiki na mazishi kufanyika eneo la Buguruni jijini Dar e salaam.
Katika salam zake, TFF inawapa pole familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki na kusema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu nchini, wako pamoja katika kipindi hiki cha maombolezo.
Marehemu Willie Chiwango ni miongoni mwa waandishi wa habari wa michezo wakongwe kabisa, aliambatana na timu ya taifa ‘Taifa Stars’ iliyoshiriki michuano ya Mataifa Afrika mwaka 1980 nchini Nigeria.
TFF ilimpa cheti cha heshima marehemu Chiwango katika zoezi la kuwakumbuka na kutambua mchango wa viongozi, wachezaji, waandishi wa habari za michezo waliojitoa katika sekta ya mpira wa miguu nchini.

U15 YAREJEA DAR

u15camp 
Ziara ya timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 15 (U15) iliyoanzia kanda ya ziwa na kanda ya Magharibi kisha kuendelea katika nchi za Rwanda, Uganda na Kenya mwezi huu imesitishwa kutokana na kufungwa akaunti za Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF) na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).
Timu hiyo ya vijana iliondoka wiki iliyopita kuelekea jijin Mwanza, ambapo iliagwa na kukabidhiwa bendera ya Taifa na katibu mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Profesa Elisante Ole Gabriel, ilicheza mchezo mmoja wa kirafiki na timu ya Alliance kabla ya kuelekea mkoani Kigoma.
Ikiwa Kigoma U-15 ilicheza michezo miwili ya kirafiki na timu ya kombaini ya mkoa wa Kigoma U-15, jumapili ikacheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya Burundi U-17, na jana asubuhi kuanza safari ya kurejea jijini Dar essalaam.
Awali ziara ya timu hiyo ya U-15 ilikua iendelee katika mji wa Kigali kwa kucheza na U17 ya Rwanda, Kampala kucheza na Uganda U17, jijini Nairobi kwa kucheza na U17 ya Kenya na kumaliza ziara hiyo kwa kuchez ana U15 kombaini ya mkoa wa Arusha Disemba 23, na kurejea jijin Dar es salaam Disemba 24, 2015.
U-15 inajiandaa na michuano ya Viajana U17 kuwania kufuzu kwa Mataifa ya Afrika mwaka 2017 nchini Madagascar itakayoanza kutimua vumbi Juni 2016.

Naibu Inspekta jenerali wa polisi aanzisha mpango wa kuboresha usalama wa jamii

index
Na. Tamimu Adam – Jeshi la Polisi.
Jeshi la polisi nchini, limeanzisha mpango wa kuboresha usalama wa jamii nchi nzima ambao unalenga kuboresha utoaji wa huduma bora kwa wananchi, kuboresha mawasiliano ya ndani na nje ya Jeshi la polisi kwa kuwashirikisha wadau mbalimbali wa usalama ambapo mpango huo utaanza kutekelezwa katika mkoa wa kipolisi kinondoni ambapo lengo lake ni kupunguza uhalifu kwa asilimia kumi ifikapo mwaka 2019.
Akihitimisha maabara ya mpango huo iliyofanya kazi kwa wiki sita, Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Abdulrahmani Kaniki aliwahakikishia washiriki wa maabara ya kuboresha usalama wa jamii, kuwa Jeshi la polisi litatekeleza kwa vitendo mapendekezo yote yaliyotokana na maabara hiyo, kwani baadhi ya mapendekezo hayahitaji bajeti hivyo utekelezaji wake utaanza mara moja.
“Kazi iliyofanywa na maabara hiyo ni kubwa na umuhimu katika kuboresha usalama wa jamii katika nchi yetu hivyo mapendekezo yote ni lazima yafanyiwe kazi ili kuleta mafanikio chanya”. Alisema Kaniki.
Aliongeza kuwa mpango huo umeanzia katika mkoa wa kipolisi kinondoni na baadaye utaenea nchi nzima, ambapo alizitaja sababu zilizopelekea kuanza na kinondoni kuwa ni pamoja na kuongezeka kwa makosa, kupanuka mji, idadi kubwa ya watu na uwepo na shughuli nyingi za kiuchumi ukilinganisha na maeneo mengine.
Naye, Mtendaji mkuu wa ofisi ya Rais ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi (PDB), Omari Issa alisema mpango huo wa uboreshaji wa usalama wa jamii ambao unaanza na mkoa wa Kinondoni uliandaliwa kwa kuwashirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali za serikali na kijamii ambao kwa pamoja walishirikiana kwa pamoja katika kuangalia namna ya kuboresha usalama wa jamii ili kuwezesha jamii kuwa salama.
Aliongeza kuwa mpango wa matokeo makubwa sasa unahitaji kuzingatia vitu vikuu vitatu katika utekelezaji wake ambavyo ni kujiwekea vipaumbele, nidhamu ya utekelezaji na uwajibikaji hivyo alisema hana wasiwasi na Jeshi la Polisi katika utekelezaji wa mpango huo hapa nchini.
Mpango wa uboreshaji wa usalama wa jamii unalenga kuboresha na kurahisisha huduma mbalimbali zinazotolewa na Jeshi la polisi ikiwemo kuboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa askari, usimamizi wa rasirimali watu na vifaa na kuweka mikakati ya kuwashirikisha wadau wa kada mbalimbali ndani ya jamii katika kuboresha usalama wa jamii.
Maabara hiyo ya kuboresha usalama wa jamii ripoti yake inatarajiwa kukabidhiwa kwa Inspekta Jenerali wa Polisi hivi karibuni ili kuanza utekelezaji wake kwa kuanza na mkoa wa kipolisi wa Kinondoni.

PANAFRICAN ENERGY YATOA YAFADHILI UJENZI WA WODI YA ‘MAMA NGONJEA’ HOSPITALI YA WILAYA KINYONGA KILWA KIVINJE NA KUKARABATI WODI ZA UZAZI NA CHUMBA MAALUM CHA UANGALIZI WA AKINA MAMA

Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni
ya PanAfrican Energy Andrew
Kangashaki  (kushoto ) na
Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa
Twalib Mbasha wakikabidhiana mkataba wa miradi  ya ujenzi wa nyumba ya mama ngojea  katika hospital ya Kinyonga  na ukarabati wa wodi  ya uzazi  mara baada ya kumaliza kusaini mikataba hiyo katika hafla fupi iliyofanyika jana Kilwa Kivinje.
Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni
ya PanAfrican Energy Andrew
Kangashaki(wa tatu kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa
Twalib Mbasha (wa tatu kulia) wakisaini makubaliano ya miradi miwili ya ujenzi
wa mama ngojea ‘maternity waiting home’ yaani nyumba maalum kwa kina mama
wajawazito watakaokua wakisubiri kujifungua itakayojengwa katika hospitali ya
Kinyonga – Kilwa Kivinje na kukarabati wodi ya uzazi na chumba maalum cha
uangalizi wa akina mama mara tu baada ya kujifungua katika kituo cha afya cha
Kilwa Masoko. Huku wakishuhudiwa na Mwanasheria wa Wilaya Mh. Godfrey Makary
(wapili kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Juma Abdalah Njwayo(wa pili
kushoto), Mbunge wa jimbo la Kilwa Kaskazini kupitia chama cha CUF Mh. Vedasto
Edgar Ngombale(wakwanza kushoto) pamoja na Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama
cha CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wakwanza kulia).
Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha
CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wapili kulia) akitoa neno la shukrani kwa
Kampuni ya PanAfrican Energy kwa niaba ya wananchi wa Kilwa Kusini mara baada
ya makabidhiano ya mkataba wa miradi itakayowanufaisha wananchi wa kilwa.
Wafadhili wa mradi wa ujenzi wa wodi ya
wazazi Kampuni ya PanAfrican Energy pamoja wakiwaonesha wanahabari chumba cha
uzazi katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko ambacho kipo katika mradi uliosainiwa
kati ya wilaya ya Kilwa na kampuni hiyo. Hii ni katika kuunga jitihada za
serikali za kuboresha huduma za afya.
Hali
halisi ya mazingira ya wodi ya wagonjwa katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko,
hii ni wodi ya wanaume. Kiyuo hichi cha afya
kilijengwa mwaka 1952 enzi za ukoloni mpaka sasa hakijawahi
kukarabatiwa.

Wakisaini makubaliano ya miradi ya ujenziwa mama ngojea na ukarabati wa chumba cha uzazi na wodi maalum ya uangalizi wakina mama mara tu baada ya kujifungua wilayani Kilwa ni Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni ya PanAfrican Energy Andrew Kangashaki (wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa Twalib Mbasha (wa pili kulia) wanaowashuhudiwa ni Mwanasheria wa Wilaya ya Kilwa Mh. Godfrey Makary ( kulia), Mkuu wa Wilaya ya hiyo Juma Abdalah Njwayo (kushoto) jana katika hafla fupi iliyofanyika jana katika hospitali ya Kinyonga Kilwa Kivinje.

WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUWAPELEKA WATOTO SHULE

index 
Mkuu wa Divishen ya Elimu ya msingi Zanzibar Ahmed Abdul Majid akifafanuwa jambo kwa washirikiwa wa mafunzo hayo  juu ya Umuhimu wa Elimu ya Maandalizi yaliyofanyika Kituo cha Walimu Kiembesamaki (TC), (kuliya) Mkuu wa Mohamed Othman Dau.
…………………………………………………………………………………………………….
Na Majda Kasid –Maelezo Zaznzibar 
Wazazi na Walezi wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika  kuwapeleka watoto wao waliyofikiwa umri wa miaka minne katika skuli za maandalizi kwa lengo la kuwakuza kielimu.
 Hayo yameelezwa na  Mkuu wa Divishen ya Elimu ya  Msingi Zanzibar Ahmed Abdul Majid wakati alipokuwa  akitowa  mafunzo  kwa wazazi katika  Kituo cha Walimu (TC) Kiembe Samaki  juu ya umuhimu wa Elimu ya Maandalizi.  

Amesema  wazazi na walezi  ndio wanao hitajika kufanya bidii kwa  kila  hali kuhakikisha watoto wanawapa  kipaumbele  ili kuhakikisha wanapatiwa  elimu  ya  maandalizi na  kujiandaa na    elimu  ya msingi na sekondari.

Amewataka walimu wanaofundisha Wanafunzi kuanzia Elimu ya Maandalizi hadi Elimu ya Sekondari kutowatolesha ada wanafunzi  kwani  hilo ni agizo lililotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr. Ali Mohammed Shein.

Alifahamisha  kwamba  mafunzo  hayo yaliyowashirikisha  Walimu wa skuli  za  maandalizi , Walimu  wa  madrasa , Masheha  pamoja  na  Wazazi  yanalengo la   kutoa elimu kwa jamii .
Nae Mkuu wa Kituo cha Maendeleo ya  awali  ya Makuuzi  ya  watoto (ECD) Muhammed Othman Dau amesema  lengo la  mafunzo hayo ni kuwaandaa  wazazi  wa watoto ili waweze  kuanzishwa skuli  za maandalizi mapema  kuwajengea  mfumo mzuri  wa  masomo  ya   baadae.

Amesema  watoto    wanapopatiwa  elimu ya  maandalaizi  huwajengea mustakabali  mzuri  wa maisha ikiwemo  upeo  wa maadili  mema   pamoja  na kuwa na uwezo wa kubuni  mambo  ambayo yatawakuza kiakili na kielimu.

Mohammed Othman Dau amesema hadi hivi sasa watoto waliofikia umri wa miaka mine wanaoandikiswa skuli za maandalizi imefikia   asilimia 50  na lengo ni kuhakikisha watoto wote  wanapelekwa skuli za maandalizi.

Mmoja  ya  wazazi  walioshiriki  mafunzo  hayo Othman Khamis amesema ni  vyema  wanafunzi  wa  maandalizi  kupatiwa walimu wa  masomo  ya  dini.

KAMATI KUU CCM: RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI KANYAGA TWENDE

index 
Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 8, 2015, katika Ukumbi wa Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba jijini Dar es Salaam.
………………………………………………………………………………
Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa ilifanya kikao chake cha kawaida mjini Dar es salaam kwa siku moja. Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.

Kamati Kuu pia ilipokea taarifa juu ya utendaji wa Serikali katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015-2020.  Kwa ujumla na kwa kauli moja Kamati Kuu ya CCM Taifa iliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu na Waziri Mkuu Mhe. Kassim M. Majaliwa kwa kasi nzuri waliyoanza nayo katika utekelezaji wa Ilani hiyo.

Kamati Kuu kwa niaba ya Chama imeunga mkono hatua kadhaa zinazochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuhakikisha Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020 inatekelezwa kwa ufanisi. Aidha, inapongeza na kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali katika maeneo ya:-

(1) Kusimamia vyanzo vya mapato ya Serikali:
Kamati Kuu inapongeza na kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano katika kuhakikisha kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) zinasimamia ukusanyaji wa kodi za Serikali ipasavyo. Juhudi hizi za Serikali ya Awamu ya Tano kwa muda mfupi zimezaa matunda yanayoonekana wazi. Aidha, Kamati Kuu inawataka wahusika mbalimbali kwenye maeneo hayo ya udhibiti wa vyanzo vya mapato kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa Serikali ili lengo liweze kutimia.

(2) Kudhibiti matumizi ya Serikali:
Kama ilivyoagizwa na Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2015-2020, Serikali ya Awamu ya Tano imeanza vizuri na kwa kasi kusimamia udhibiti wa matumizi yasiyo ya lazima katika Serikali, ili kutumia fedha hizo kwenye utoaji wa huduma kwa wananchi. Kamati Kuu inaunga mkono juhudi hizi na kuwataka wote wanaohusika kwa namna moja ama nyingine na udhibiti wa matumizi hayo wamuunge mkono Rais Dkt. John Pombe Magufuli na Serikali yake katika jitihada hizi.

(3) Uhimizaji wa wananchi katika kufanya kazi kwa bidii:
Kamati Kuu inawataka wanaCCM na wananchi wote kwa ujumla nchini kumuunga mkono Rais na Serikali yake kwa kuitikia wito wa kufanya kazi kwa bidii, kwa maarifa na uzalendo. Kamati Kuu inawahimiza watu wote kwenye maeneo yao ya kazi kujituma na kuchapa kazi ili kujenga nchi yetu na kumuunga mkono Rais Magufuli.

(4) Kusimamia na kuhimiza uwajibikaji katika Serikali, Taasisi na Mashirika yake:
Kamati Kuu pia inapongeza na kuunga mkono juhudi zinazoendelea za kuhakikisha kunakuwa na uwajibikaji mkubwa Serikalini ili kuongeza kasi na ubora wa utoaji huduma. Katika kipindi cha muda mfupi matunda yake yameanza kuonekana na hivyo kuweka msingi mzuri wa kuboresha huduma kwa umma kwa njia endelevu.

(5) Juhudi na jitihada hizi za Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Uongozi wa Rais Dkt. Magufuli zimeleta matumaini mapya kwa sehemu kubwa ya wananchi na kukuza imani kwa Serikali yao.  Hivyo, kila Mtanzania ana wajibu wa kuunga mkono jitihada hizi.

Pamoja na kuunga mkono na kupongeza kasi waliyoanza nayo Rais Magufuli, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu, Kamati Kuu inawataka Viongozi wengine wote kuiga mfano huu mzuri na kuhakikisha wanatimiza wajibu wao ipasavyo ili kutekeleza kwa haraka zaidi Ilani ya Uchaguzi ya CCM na kuleta maendeleo nchini.

Aidha, Kamati Kuu inawatakia Watanzania wote kheri ya Krismas na mwaka mpya wa 2016, na inaamini mwaka ujao utakuwa wa kuchapa kazi na wenye mafanikio zaidi.
Imetolewa na:-
Abdulrahman O. Kinana,
KATIBU MKUU WA CCM 08/12/2015

Tume ya Haki za Binadamu yaandaa Mpango Endelevu kufikia malengo ya Millenia

hk1 
Mgeni Rasmi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Tume ya Haki za Binadamu Bi. Rehema Ntimizi akiongea na wadau hawapo pichani walioshiriki katika kongamano la kujadili malengo endelevu kufikia malengo ya Milenia jijini Dar es salaam leo.
hk2 
Mkurugenzi wa Tume ya Haki za Binadamu Bw. Francis Nzuki akiongea na waandishi wa habari katika kongamano la kujadili malengo endelevu kufikia malengo ya Milenia jijini Dar es salaam leo.
hk3 
Wadau kutoka sehemu mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja waliposhiriki kongamano la kujadili malengo endelevu kufikia malengo ya Milenia jijini Dar es salaam leo.
hk4 
Wadau kutoka sehemu mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja waliposhiriki kongamano la kujadili malengo endelevu kufikia malengo ya Milenia jijini Dar es salaam leo.
………………………………………………………………………………………..
Na Shamimu Nyaki¬¬-Maelezo
Dar es salaam
Katika kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya Haki za Binadamu duniani ambayo ni tarehe10 Disemba mwaka huu,Tume ya haki za binadamu na Utawala bora leo imeandaa kongamano la siku moja kujadili Mpango wa Maendeleo Endelevu unaotarajia kuanza rasmi januari mwaka2016.
Mgeni Rasmi katika kongamano hilo Bi Rehema Ntimizi kutoka Tume ya haki za binaadamu ameiomba jamii kushiriki kwa ukamilifu katika kuleta maendeleo yao wenyewe na taifa kwa ujumla kwa kuwa maendeleo yanaanza na watu wenyewe kwa kuhakikisha wanaondokana na umasikini,kuwa na afya bora ,pamoja na elimu na kutambua kuwa ni haki yao kuwa na uwelewa wa suala hilo.
“Binadamu wote huzaliwa huru na wote ni sawa hivyo wote tuwajibike katika maendeleo”Alisema bi Ntimizi.
Bi Rehema ameongeza kuwa dunia nzima kwa sasa inashirikisha makundi yote katika jamii katika kutoa maamuzi hasa yale yaliyosahaulika kama wanawake,wazee na watoto waishio vijijni hivyo wakati umefika sasa kwa kila mtu katika jamii kushiriki hatua zote za maendeleo.
Akizungumza na waandishi wa habari katika kongamano la kujadili mpango huo leo jijini Dar es salaam Mkurugenzi wa Tume ya haki za Binaadamu bw Francis Nzuki ameeleza kuwa lengo la kongamano hilo ni kujadili mpango huo wa maendeleo endelevu jinsi gani utaleta matokeo chanya katika kufikia malengo ya millenia ifikapo mwaka 2030.
Ameongeza kuwa mpango huo umejikita katika malengo kumi na saba ambayo miongoni mwao ni kuondoa umaskini,kutoa Elimu bora, afya bora pamoja na maji safi kwa kila kundi lililopo katika jamii ambao ni vijana,wazee, wanawake, pamoja na watoto katika jamii ya Watanzania ili kuweza kufikia malengo ya millenia.
Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa Tume itaanzisha utaratibu wa kutembelea hospitali za umma kuanzia ngazi ya mkoa hadi kijiji ili kuweza kubaini malalamiko na changamoto wanazopata wananchi ,lakini pia kutoa elimu jinsi watakavyoweza kusaidiwa na tume pale wanakutana na changamoto katika suala linalohusu haki na utu wao.
Kauli mbiu katika kongamano hilo ni “Haki zetu uhuru wetu daima”.
Aidha mshiriki kutoka shirika linalowahudumia wazee linaloitwa Helpage Intanational Fund Bw Joseph Mbasha amesema kuwa wazee wanapaswa kushirikishwa katika masuala yote ya maendeleo kwa kuwa nao ni binaadamu na wana uhuru wa kutoa mawazo na kupewa afya bora, kuondokana na umaskini lakini pia kumiliki ardhi.
“Kila mmoja ashiriki katika maendeleo yake na Taifa kwa ujumla”Alieleza Mbasha.
Kongamano hilo limehudhuriwa na wadau mbalimbali wa haki za binaadamu wakiwemo Haki Elimu,YUNA,Shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP),Chuo kikuu cha Dar es salaam pamoja na Chuo cha Uhasibu.

MASHINDANO YA BASEBALL KUANZA KUTIMUA VUMBI IJUMAA WIKI HII JIJINI DAR ES SALAAM

bas1 
Nahodha wa Timu ya Baseball ya Kibasila Pius Peter (kulia) akiwaonyesha waandishi wa habari  leo jijini Dar es salaam jinsi ya mchezo huo unavyochezwa. Kushoto ni  Nahodha wa Timu ya Baseball ya Tigers  Mussa Mbugi.
bas3 
Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Alpherio Nchimbi(kushoto) akitoa ufafanuzi kwa  waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu Mashindano ya Kitaifa ya Awamu ya Tatu ya Mchezo wa Baseball yanayotarajia kuanza Ijumaa ya wiki hii jijini Dar es salaam. Wengine ni Nahodha wa Timu ya Baseball ya Kibasila Pius Peter (wa pili kulia) ,Nahodha wa Timu ya Baseball ya Tigers  Mussa Mbugi( wa pili kushoto) na Nahodha wa Timu ya Baseball ya Giants Douglas Stanslaus(kulia).
bas4 
Nahodha wa Timu ya Baseball ya Kibasila Pius Peter (wa pili kulia ) akizungumza na  waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu Mashindano ya Kitaifa ya Awamu ya Tatu ya Mchezo wa Baseball yanayotarajia kuanza Ijumaa ya wiki hii jijini Dar es salaam . Wengine Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Alpherio Nchimbi(kushoto) ,Nahodha wa Timu ya Baseball ya Tigers  Mussa Mbugi( wa pili kushoto) na Nahodha wa Timu ya Baseball ya Giants Douglas Stanslaus( kulia).
……………………………………………………………………………………………
Na Nyakongo Manyama-MAELEZO-Dar es salaam.
Mashindano ya Kitaifa ya Awamu ya Tatu ya Mchezo wa Baseball yanatarajiwa kuanza Ijumaa ya wiki hii jijini Dar es salaam.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Alpherio Nchimbi leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari.
Amesema kuwa mashindano yatashirikisha timu tisa kutoka Tanzania bara na Visiwani na yanatarajiwa kufunguliwa na Balozi wa Japani nchini Tanzania Mhe. Masaharu Yoshida.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo , mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika katika shule ya Sekondari ya Azania iliyopo jijini  Dar es salaam.
Amesema kuwa mashindano hayo yanayojulikana kama 3rd Koshien  Tanzania National Championship yatafanyika kwa muda wa siku tatu kuanza tarehe 11 hadi 13 mwezi huu.
Nchimbi amezitaja timu zitakazoshiriki kuwa ni Shule za Sekondari  ya Azania, Kibasila , Iyunga, Sanya Juu, Londoni , na Mwanza Baseball Club, Mwanakwerekwe “C” , Tigers na Giants.
Amesema kuwa mshindano ya mwaka huu yanatarajiwa kusimamiwa na wataalamu kutoka nchini Japan wakishirikiana na wataalam kutoka nchini katika kutoa uamuzi na masuala mengine ya kiufundi.
Nchimbi amesema lengo la mashindano hayo ni kupata timu ya Taifa ya umri wa chini ya miaka 21 kwa ajili ya kuanza maandalizi ya kushiriki mashindano yatakayofanyika Afrika kusini hapo mwezi wa pili(February ) mwakani (2016).
Kwa upande wa Nahodha wa Timu ya Giants Douglas Stanslaus ametoa wito kwa wananchi wajitokeze kwa wingi kwa ajili kuona mashindano hayo na kuwatia moyo ili waweze kukuza mchezo huo nchini.
Naye Nahodha kwa timu ya Kibasila Pius Peter amewaomba vijana wengi kujitokeza kuona na kujifunza jinsi mchezo huo unavyochezwa ili hatimaye mchezo huo umeweze kuenea sehemu mbalimbali nchini kama fursa ya vijana kushirikiana na kujenga umoja.
Aidha Katibu Mkuu wa Katibu wa Chama cha Mchezo wa Baseball nchini Nchimbi amewaomba wadau mbalimbali kuthamini mchezo wa Baseball kama ilivyo michezo mingine na kujitokeza kuufadhili ili uweze kukua na kutengeneza ajira kwa vijana.

Viingilio Tamasha la Krismasi 50,000/-

index
KAMPUNI ya Msama Promotions ambayo ni waandaaji wa Matamasha ya Pasaka na Krismasi, imetangaza viingilio vya juu kwenye Tamasha la Krismasi kuwa ni Shilingi 50,000 kwa viti maalum, Tamasha ambalo litafanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo linalokwenda na shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 ambako kabla, Msama waliandaa tamasha la Kuombea Amani uchaguzi Mkuu lililofanyika Oktoba 4 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama VIP watachangia shilingi 10,000 na viti vya kawaida watachangia shilingi 5000.
Msama alisema watoto watakaohudhuria tamasha hilo watachangia shilingi 2000, alitoa wito kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi katika tamasha hilo ambalo lina lengo la kurudisha shukrani kwa Mungu baada ya kupita kwenye uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu.
“Watanzania tujitokeze kwa wingi ili turudishe shukrani kwa Mungu baada ya kutupitisha katika uchaguzi Mkuu ambao ulikuwa tofauti na chaguzi zilizopita, hivyo ni nafasi yetu kumwambia Mungu asante baada ya kutupitisha katika tukio hilo muhimu,” alisema Msama.
Aidha Msama michango inayopatikana kupitia viingilio hivyo hurudisha kwa Jamii yenye uhitaji maalum kama yatima, walemavu, wajane na wengineo wenye uhitaji kama huo.
Msama alisema maandalizi ya kuelekea tamasha hilo yanakwenda vizuri, huku waimbaji kama Rose Muhando, Upendo Nkone, Ephraim Sekeleti, Rebecca Malope, Kwaya ya Wakorintho Wapili, Joshua Mlelwa na Christina Shusho wamethibitisha kushiriki tamasha hilo.

TGDC NA MKAKATI WA UZALISHAJI WA UMEME KUPITIA JOTOARDHI

index 
Meneja Mkuu Shirika la Uendelezaji wa Nishati ya Jotoardhi Tanzania (TGDC), Mhandisi Boniface Njombe (kushoto) pamoja na Mtaalamu Mkuu toka Kampuni ya TOSHIBA Bwana Kentaro Kurahara wakikabidhiana Mkataba wa Maelewano (MOU) wa kufanya tafiti kwa pamoja zinahusu maeneo yenye viashiria ya upatikanaji wa nishati ya jotoardhi katika Ofisi za TGDC zilizopo Jijini Dar es Salaam.
……………………………………………………………….
Na Benedict Liwenga-MAELEZO.
 
Kutokana na ongezeko la mahitaji ya nishati ya umeme nchini, nishati itokanayo na jotoardhi (Geothermal Energy) imetajwa kuwa ni muhimu katika kuepukana na hasara kubwa na isiyo ya lazima inayotokana na matumizi ya mitambo ya mafuta katika kuzalisha umeme na kuifanya Tanzania kuondokana na tatizo la umeme usiokuwa na uhakika pamoja na kuleta maendeleo nchini.
 
Ili kuleta Maendeleo haya katika sekta ya nishati, Tanzania hainabudi kugeukia katika vyanzo vingine vya uzalishaji umeme ikiwemo nishati hiyo ambayo kwa kutumia mvuke wa maji yaliyochemshwa na joto la asili lililopo chini ya ardhi, nishati ya umeme inaweza kuzalishwa na kukidhi mahitaji ya nishati ambayo yatasaidia kuwa kiunganishi cha ukuaji wa uchumi nchini.
 
Tanzania iko katika ukanda wa Bonde la Ufa (Rift Valley), hivyo kuna uwezekano mkubwa wa uwepo wa hifadhi kubwa ya nishati itokanayo na jotoardhi ambayo inaweza kutumika katika uzalishaji wa umeme na kuinua uchumi wan chi yetu.
 
Nishati hii itakuwa mkombozi kwa taifa letu hususani kwa mwananchi wa  kipato cha chini kwani tunaamini kuwa matumizi ya nishati hiyo yatapelekea kupungua kwa gharama za manunuzi ya umeme na kutokana na ukweli kwamba nishati hiyo pindi ipatakinapo haitarajiwi kuisha.
 
Unafuu wa umeme utakaozalishwa na jotoardhi unatokana na ukweli kwamba mitambo inayotumika kuzalisha umeme  huo kuendeshwa kwa mvuke ambao unatokana na majimoto toka ardhini tofauti na uzalishaji wa umeme uliokuwa unatumika kwa kutumia mitambo yenye kutumia mafuta ambayo gharama yake ilikuwa juu kwa Serikali.
 
Hapa nchini, kuna viashiria vingi vinaonyesha uwepo wa jotoardhi hasa kwa maeneo ya vijijini ambako umeme sehemu nyingi haujafika, kutokana na hilo sasa Serikali yetu hainabudi kutupia macho katika nishati hii kwa kuhakikisha kwamba wananchi ambao wnaaishi maeneo ambayo nishati hiyo inapatikana wananufaika na umeme huo.
 
Jotoardhi ina matumizi mengi kwa jamii yetu, mfano majimoto yatokayo ardhini yanaweza kutumika katika kukaushia mazao mfano matumizi ya Vitalu shamba (Green Houses) badala ya kutegemea jua. Mwananchi wa kipato wa chini anaweza kutumia majimoto kukausha mazao yake kwa mfano mpunga, maharage, mahindi, karanga katika ubora ule ule kama wa jua.

No comments :

Post a Comment