TAARIFA YA WAZIRI MKUU KWA WATANZANIA ALIPOZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI OFISINI KWAKE
Waziri
Mkuu Mh. Majaliwa, Kassim Majaliwa akizungumza na waandishi wa habari
katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu leo wakati alipotoa taarifa ya
serikali kuhusu hatua zilizochukuliwa dhidi ya watumishi wa TPA, TRA,
Wizara ya Uchukuzi na TRL. kulia ni Katibu Mkuu Kiongozi Mh. Ombeni
Sefue.
Waziri
Mkuu Mh. Majaliwa, Kassim Majaliwa akisisitiza jambo wa kwa utulivua
wakati akitoa taarifa hiyo mbele ya waandishi wa habari , Kalia ni
Katibu Mkuu Kiongozi Ombeni Sefue.
Waziri Mkuu Mh. Majaliwa, Kassim Majaliwa akiingia kwenye ukumbi wa mikutano tayari kwa kuzungumza na waandishi wa habari.
…………………………………………………………………………………………………………….
Mnamo tarehe 27 Novemba, 2015
nilifanya ziara ya kushitukiza Bandari ya Dar es Salaam ambapo
nilifichua mwanya wa ukwepaji kodi kwa makontena 329 yaliyopitishwa
bandarini kinyume cha utaratibu.
Mtakumbuka pia tarehe 4 Desemba,
2015 nilirudi tena kufanya ufuatiliaji wa hatua ya udhibiti wa
upitishaji wa bidhaa mbalimbali kinyume cha utaratibu.
Ziara yangu ilinipitisha hatua
zote za upitishaji mizigo ambazo pia kwa mujibu wa Taarifa ya Ukaguzi wa
Ndani wa tarehe 30 Julai 2015 Mamlaka ya Bandari uligundua kuwepo kwa
mianya mingi ya ukwepaji kodi ikiwemo na makotena 2387 yaliyopitiahwa
kati ya Machi – Septemba 2014 kinyume cha utaratibu, vitendo hivi
vinaonyesha kuwa bandari yetu hupitisha makontena mengi bila ya kulipiwa
kodi na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa.
Upotevu huo unaenda sambamba na
mfumo usiokidhi wa kupokelea malipo (BILLING SYSTEM) ambao unatoa mwanya
mkubwa wa kupoteza mapato ya Serikali. Bandari ni eneo muhimu ambako
kama panasimamiwa vizuri panaweza kukusanya fedha nyingi na kuchangia
Pato la Taifa.
Serikali haitavumilia kuona watu
wachache au kikundi chochote kilichojipanga kuhujumu mifumo au kuiibia
Serikali kwa namna yoyote ile kwa manufaa ya wachache.
Matokeo ya ziara hizo ni haya yafuatavyo:-
1. Nimeagiza mfumo wa kupokelea malipo ubadilishwe kutoka Billing System na uwekwe mfumo wa e-payment ambao tayari ulianza kuwekwa na uwe umekamilika kufikia tarehe 11 Disemba 2015.
2. Kwa kuwa ripoti iliwataja waliohusika na upitishaji makontena hayo na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa, kuanzia muda huu nawasimamisha kazi wale wote waliohusika kupitisha makontena kinyume na utaratibu.
1. Nimeagiza mfumo wa kupokelea malipo ubadilishwe kutoka Billing System na uwekwe mfumo wa e-payment ambao tayari ulianza kuwekwa na uwe umekamilika kufikia tarehe 11 Disemba 2015.
2. Kwa kuwa ripoti iliwataja waliohusika na upitishaji makontena hayo na hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa, kuanzia muda huu nawasimamisha kazi wale wote waliohusika kupitisha makontena kinyume na utaratibu.
1. Wasimamizi wa Bandari Kavu (ICD)
(i) Happygod Naftari
(ii) Juma Zaar
(iii) Steven Naftari Mtui
(iv) Titi Ligalwike
(v) Lydia Prosper Kimaro
(vi) Mkango Alli
(vii) John Elisante
(viii) James Kimwomwa – ambaye amehamishiwa Mwanza.
(i) Happygod Naftari
(ii) Juma Zaar
(iii) Steven Naftari Mtui
(iv) Titi Ligalwike
(v) Lydia Prosper Kimaro
(vi) Mkango Alli
(vii) John Elisante
(viii) James Kimwomwa – ambaye amehamishiwa Mwanza.
2. Wafuatao ni Viongozi wa sekta
zilizotoa ruhusa ya makontena kutoka ndani ya Bandari ambao hawamo
kwenye ripoti ila ni wahusika wakuu.
1. Shaban Mngazija – Aliyekuwa Meneja Mapato ambaye kwa sassa amehamishiwa Makao Makuu kitengo cha Fedha.
2. Rajab Mdoe – Aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha na Mkuu wa Bandari Kavu (ICD) – ambaye amehamishiwa Makao Makuu kwa Naibu Mkurugenzi Co-operate Services.
3. Ibin Masoud – Kaimu Mkurugenzi wa Fedha.
4. Apolonia Mosha – Meneja Bandari Msaidizi – Fedha.
5. James Kimwomwa.
2. Rajab Mdoe – Aliyekuwa Mkurugenzi wa Fedha na Mkuu wa Bandari Kavu (ICD) – ambaye amehamishiwa Makao Makuu kwa Naibu Mkurugenzi Co-operate Services.
3. Ibin Masoud – Kaimu Mkurugenzi wa Fedha.
4. Apolonia Mosha – Meneja Bandari Msaidizi – Fedha.
5. James Kimwomwa.
Kutokana na utendaji mbovu wa Mamlaka ya Bandari kwa muda mrefu na kwa kitendo cha kutochukua hatua kwenye vyanzo.
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amevunja Bodi yote ya
Bandari na kutengua uteuzi wa wafuatao:-
1. Mwenyekiti wa Bodi ya Bandari – Prof. Joseph Msambichaka.
2. Mkurugenzi Mkuu wa Bandari – Bw. Awadhi Massawe.
2. Mkurugenzi Mkuu wa Bandari – Bw. Awadhi Massawe.
Ndugu Waandishi wa Habari
mtakumbuka pia nilifanya ziara pia TRL ambako kwa awali nimegundua
matumizi mabaya ya fedha Shilingi Bilioni 13 nje ya utaratibu ambako
uchunguzi unakamilishwa.
Mheshimiwa Rais, pia ametengua
uteuzi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaban Mwinjaka kuanzia
tarehe ya leo na atapangiwa kazi nyingine.
Waogeaji wa Dar Swim Club watamba kutwaa medali, kwenda Dubai Jumatano
Wachezaji wa klabu ya Dar Swim Club wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuondoka
……………………………………………………………………..
Na Mwandishi wetu
Kocha wa klabu ya kuogolea ya
Dar Swim Club, Michael Livingstone ametamba kuwa waogelaji wake
chipukizi watatwaa medali mbalimbali katika mashindano ya kuogelea ya
kimataifa ya Dubai yanayojulikana kwa jina la “Hamilton Aquatics Dubai
Long Course” yaliyopangwa kuanza Desemba 11.
Akizungumza jijini jana,
Livingstone alisema kuwa waogeleaji wote 13 wapo katika morali ya hali
ya juu baada ya kupata maandalizi ya miezi miwili.
Livingstone alisema kuwa
mashindano hayo ambayo yanashirikisha waogelaji kutoka nchi mbalimbali
duniani, mbali ya kusaka medali, pia yatawapa uzoefu wachezaji wao ambao
ni bado chipukizi.
Alisema kuwa mashindano hayo ni
makubwa sana katika mchezo huo na hivyo watatumia fursa ili kuwapa
uzoefu wa kimatafa waogelaji wao ambao ni hazina ya Tanzania katika
mashindano ya kimataifa katika miaka ijayo.
“Timu yetu inaundwa na
waogeleaji chipukizi sana, wengi wao chini ya miaka 15, mbali ya
kushindana, pia watakuwa wanapata uzoefu wa kimataifa kwa ajili ya
kuiwakilisha nchi katika mashindano mengine ya kimataifa kama,
Mashindano ya Dunia, Jumuiya ya Madola namichezo ya Olimpiki,” alisema
Livingstone.
Alisema kuwa waogeleaji wamesema
kuwa hakuna cha kuogopa katika mashindano hayo ambayo yatamalizika
Desemba 12, Livingstone, Kocha mwingine wa klabu hiyo,
Kocha mwingine wa timu hiyo,
Ferick Kalengela alisema kuwa pamoja na kujiandaa katika katika bwawa la
kuogelea la mita 25, wataweza kushindana katika Bwawa la Mita 50 kwani
waliongeza muda na umbali wakati wa mashindano.
Kalengela alisema kuwa
wamejifunza stamina, kasi ya kuogelea na mambo mengine mengi yanayohusu
mashindano hayo na kupata majina ya waogeleaji bora 13.
Katibu Mkuu wa klabu hiyo,
Inviolata Itatiro alisema kuwa maandalizi yote ya safari hiyo
yamekamilika na wanatarajia kuondoka nchini kesho Jumatano kuelekea
kwenye mashindano hayo.
Inviolata aliwataja waogeleaji
hayo kuwa ni Lidia Janik, Deeptti Venugopal, Maia Tumiotto, Ursula
Khimji, Anna-Clara Azzoni, Maya Somaiya and Niki Somaiya. Also in the
list are Smriti Gokarn, Anjani Taylor, Kayla Temba, Celina Itatiro,
Peter Itatiro na Marin de Villard.
Viongozi ni Michael Livingstone na Kanis Mabena ambao ni makocha na Inviolata ambaye ni meneja na mkuu wa msafara.
WAPINGA COCO BEACH KUUZWA
Mwenyekiti
wa Jukwaa Huru la Wazalendo Tanzania (JUHWATA), Ally Hapi akizungumza
na waandishi wa habari, katika ukumbi wa Hoteli ya Travertine Ubungo
jijini Dar es Salaam, kupinga hatua ya Mfanyabiashara mmoja wa jijini
Dar es Salaam kutaka kuuziwa na Jiji Ufukwe wa Coco Beach, uliopo
Oysterbay. Kulia ni Katibu Mkuu wa JUHWATA, Mtela Mwampamba. (Picha na
Bashir Nkoromo).
REBECCA MALOPE KUTIKISA TAMASHA LA KUSHUKURU
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion Bw. Alex Msama akizungumza na waandishi
wa habari ofisini kwake Kinondoni jijjini Dar es salaam wakati
akitambulisha ujio wa mwimbaji wa muziki wa injili Rebecca Malope kutoka
Nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya kutumbuiza kwenye tamasha la
Kushukuru linalotarajiwa kufanyika Desemba 25 kwenye uukumbi wa Diamond
Jubilee jijini Dar es salaam , kulia ni Mratibu Tamasha la Kushukuru
masuala ya usalama Bw. Hamisi Pembe.
Mratibu
Tamasja la Kushukuru masuala ya usalama Bw. Hamisi Pembe akifafanua
jambo kuhusu usalama wa mashabiki wa muziki wa injili pamoja na mali zao
wakati wa tamasha hilo, kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama
Promotion Bw. Alex Msama.
……………………………………………………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu
MWIMBAJI nguli wa muziki wa
Injili barani Afrika, Rebecca Malope ambaye ni raia wa Afrika Kusini
anatarajia kuongeza nguvu katika Tamasha la Krismasi linalotarajia
kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es
Salaam.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati
ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama muimbaji huyo atakuwa jukwaa
moja na wenzake Sarah K wa Kenya na Ephraim Sekeleti wa Zambia ambao
watafikisha shukrani za Watanzania baada ya kufanya uchaguzi Mkuu kwa
amani na utulivu, uchaguzi uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Msama alisema Kamati yake
inaendelea na mchakato wa kufanikisha tamasha hilo ambalo ni muendelezo
wa Tamasha la Amani lililofanyika Oktoba 4 uwanja wa Taifa jijini Dar es
Salaam.
Aidha Msama alisema Watanzania
walichukilie tamasha hilo kama sehemu ya kurudisha shukrani kwa Mungu
baada ya kutupitisha katika kipindi kigumu cha uchaguzi Mkuu ambao
ulifanyika kwa amani na utulivu ingawa kulikuwa na viashiria vya
uvunjifu wa amani.
Msama alisema waimbaji wa Tanzania
watakaosindikiza tamasha hilo ni pamoja na Rose Muhando, Upendo Nkone,
Joshua Mlelwa, Kwaya ya Wakorintho wapili huku kamati ikiendelea na
mchakato wa kufanikisha tamasha hilo.
“Tumejipanga vilivyo na tamasha la
Krismasi, hivyo tujiandae kupiga goti la kumrudishia Mungu Shukrani
baada ya uchaguzi Mkuu ambao ulikuwa na mguso wa aina yake kutoka kwa
vijana walioonesha kutaka maendeleo kutoka kwa serikali,” alisema Msama.
Naye mjumbe wa Kamati ya
maandalizi ya Tamasha hilo, Khamis Pembe aliwahakikishia Watanzania
watakaohudhuria tamasha hilo ulinzi wa uhakika kupiia Jeshi la Polisi.
CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI (MoCU) CHAFANYA MAHAFALI YA KWANZA.
![]() |
| Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU) Pius Msekwa akitunuku Shahada ,Stashahada na Astashahada kwa wahitimu wa Chuo hicho wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho. |
![]() |
| Wahitimu wa kozi mbalimbali waliohitimu katika Chuo Kikuu cha Ushirika mjini Moshi,(MoCU) |
![]() |
| Miongoni mwa wageni waalikwa alikuwepo pia Mbunge wa jimbo la Moshi mjini ,Jafary Michael. |
![]() |
| Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Profesa Faustine Bee akizungumza wakati wa sherehe za mahafali ya kwanza ya Chuo hicho yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Chuo hicho. |
MKUU WA MAJESHI MSTAAFU,JENERALI GEORGE WAITARA AONGOZA TIMU YA MAAFISA 24 WA JESHI KUPANDA MLIMA KILIMANJARO.
![]() |
| Baadhi ya washiriki wa zoezi la kupanda Mlima Kilimanjaro. |
![]() |
| Mkuu wa majeshi Mstaafu,Jenerali George Waitara akizungumza katika hafla hiyo. |
![]() |
| Baadhi ya wapandaji. |
![]() |
| Mhifadhi Mkuu ,Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro,( KINAPA) akizungumza wakati wa hafla hiyo. |
![]() |
| Washiriki. |
![]() |
| Afisa Masoko wa KINAPA,Antypas Mgungusi akieleza jambo wakati wa hafala hiyo. |
![]() |
| Mgeni rasmi katika hafla hiyo ,Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi,Fulgence Mponji akikabidhi bendera kwa Mkuu wa majeshi mstaafu ,Jenerali George Waitara ambaye ndiye kiongozi wa msafara huo. |
![]() |
| Washiriki wakijiandaa kuanza safari. |
![]() |
| Mhifadhi mkuu KINAPA,Erastus Lufunguro akiongozana na mgeni rasmi kwa ajili ya kukabidhi bendera kwa wapandaji mlima hao. |
![]() |
| Safari ya kuelekea kilele cha Mlima Kilimanjaro ikaanza kwa maafisa 24 wa JWTZ . Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii kada ya Kaskazini (0755659929). |
JUMUIYA YA KIMATAIFA YAOMBWA KUSAIDIA HUDUMA KAMBI YA NYARUGUSU
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (wa pili kulia) na ujumbe wake
aliombatana nao Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa
linaloshughulikia Idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini, Dkt. Natalia
Kanem (wa pili kushoto) pamoja na Ofisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya
Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Maulidah Hassan (kushoto) kabla ya kuelekea kambi ya
Nyarugusu walipita ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Gerald Guninita
kumsalimia pamoja na kusaini kitabu cha wageni. (Picha zote na Zainul
Mzige wa Modewjiblog).
Na Mwandishi Wetu, Kigoma
JUMUIYA
ya Kimataifa imekumbushwa kuisaidia Tanzania katika kuhudumia wakimbizi
kutoka Burundi na Kongo ambao wanaishi katika kambi ya Nyarugusu mkoani
Kigoma.
Kauli
hiyo imetolewa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na
Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez wakati
akizungumza na waandishi wa habari mara tu baada ya kukamilisha ziara
yake mkoani Kigoma.
Alisema
kwamba serikali ya Tanzania kwa miaka mingi imekuwa na moyo wa huruma
wa kusaidia majirani zake kwa kuhifadhi wakimbizi na kuitaka Jumuiya ya
Kimataifa kuona hilo na kusaidia Tanzania kufanikisha hifadhi ya
wakimbizi.
Alisema
Umoja wa Mataifa umekuwa ukishuhudia namna ambavyo serikali ya Tanzania
inahudumia wakimbizi na kuridhika na hata pale ilipowapatia haki za
kuwa Watanzania kwa kuwapa uraia na pia kusaidia kuwarejesha makwao
wakati hali ilipokuwa njema.
Hata hivyo amesema kwa sasa hali ya Burundi na Kongo si njema na hivyo Watanzania kupata tena kazi yakuhifadhi wakimbizi.
Alisema
Tanzania kwa huruma yake imetoa ardhi zaidi ili kupunguza msongamano
katika kambi ya Nyarugusu na kuitaka Jumuiya ya Kimataifa kusaidia
kukamilisha makazi hayo mapema kabla ya mvua za masika ili wananchi hao
waweze kuishi kwa amani.
Mkuu
wa Wilaya ya Kasulu, Gerald Guninita akimsikiliza kwa makini Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez (hayupo pichani) alipomtembelea
ofisini kwake kabla ya kuelekea kambi ya Wakimbizi Nyarugusu.
Alisema
kambi ya Nyarugusu ni ya tatu kwa ukubwa duniani na inahifadhi zaidi ya
wakimbizi 150,000 wakiwemo watoto na wanawake na wanahitaji huduma za
shule, afya, maji na mengine.
Aidha
wanahitaji nishati na hali hiyo haiwezi kuwezeshwa na serikali ya
Tanzania pekee kwani watakuwa wakielemewa na huruma yake na moyo wa
upendo kwa majirani zake.
“Dunia
ikumbuke wema wa watanzania kwa miaka yote hii, na isaidie kuweka sawa
hali ya kambi hiyo ili huduma zote muhimu za wananchi zipatikane”
alisema mratibu huyo.
Akizungumza
kuhusu wajibu wa Umoja wa Mataifa, alisema mashirika yake yamekuwa
yakishirikiana na serikali ya Tanzania katika kuhakikisha kwamba wanatoa
huduma kwa wakimbizi hao na kutaka wadau duniani kusaidia mashirika
hayo na serikali ya Tanzania kufanikisha mahitaji muhimu kwa wakimbizi
hao hadi hali itakapokuwa shwari katika nchi zao na kurejea kuishi
makwao.
Tanzania
imetoa maeneo matatu zaidi ya kupunguza msongamano katika kambi ya
Nyarugusu na maeneo hayo yanahitaji huduma za msingi kama barabara,
maji, vituo vya afya na shule.
Katika
ziara hiyo ambayo aliambatana na Ofisa wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya
Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa, Maulidah Hassan, pamoja na kukagua maendeleo ya kambi ya
Nyarugusu pia walikagua miradi inayofadhiliwa na Shirika la Kazi Duniani
ILO na ile ya Shirika la Mpango wa idadi watu duniani UNFPA.
ILO
Kigoma inaendesha mafunzo ya ujasirimali kwa vijana kwa lengo la
kuwawezesha kujiajiri wenyewe na kuhudumia familia zao kwa kuziwezesha
kupata huduma bora za elimu na afya kutokana na kipato chao.
Katika
msafara huo walikuwepo maafisa kutoka Shirika la linalohudumia
Wakimbizi (UNHCR) ofisi ya Kasulu mkoani Kigoma (walioipa mgongo
kamera).
Alisema
kwamba amefurahishwa na mradi huo ambao unawawezesha vijana kutambua
fursa mbalimbali zilizopo na kuzitumia vyema kufanikisha maendeleo ya
familia zao.
“Naona
uwezekano wa vijana hawa kujiajiri na kuziwezesha familia zao
kuondokana na tatizo la kipato.. elimu hii inaweza kutanzua mambo mengi
na kuondoa changamoto nyingine zinazoambatana na kukosa kipato” alisema
mratibu huyo.
Mkoa
wa Kigoma una mashirika mengi ya Umoja wa Mataifa yakifanya kazi
mbalimbali za maendeleo na za kutoa huduma za kibinadamu kwa wakimbizi.
Mashirika
hayo ya Umoja wa Mataifa yanayotekeleza miradi mbalimbali mkoani Kigoma
ni pamoja na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR), Shirika la Afya
Duniani ( WHO), Shirika la Mpango wa Uzazi (UNFPA), Shirika la Kazi la
Kimataifa ( ILO), Shirika la Kuhudumia Watoto ( UNICEF), Shirika la
Kuhudumia Wahamiaji ( IOM), Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP)
na Shirika la maendeleo (UNDP).
Akizungumza
Afisa anayeshughulikia Ustawi na Usalama UNHCR, Kasulu, Bi. Zenobia
Mushi, alisema shirika lake litaendelea kushirikiana na serikali ya
Tanzania na ya mkoa wa Kigoma katika kuhudumia wakimbizi kwa kuhakikisha
kwamba mahitaji yao ya msingi yanapatikana.
Naye
Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Kanali Mstaafu Issa Machibya alishukuru
Mashirika ya Umoja wa Mataifa kwa kuwa tayari kusaidia mkoa wake.
“
Tunashukuru kwa mambo yanayofanywa na Umoja wa Mataifa katika dhima
nzima ya ushirikiano katika kuhakikisha kwamba pengo la maskini na
matajiri linazibwa na umaskini unaondolewa katika mkoa wa Kigoma.”
Ofisa
wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan akipiga
picha kwenye bango linaloonyesha Serikali zinazofadhili misaada kwa
Wakimbizi nchini Tanzania lililopo katika ofisi za UNHCR Kasulu.
Naye
Mkuu wa wilaya ya Kasulu, Gerald Guninita akizungumza kuhusu hali ya
kambi ya Nyarugusu alisema kwamba hali ya kambi si nzuri na wakati msimu
wa masika ukikaribia ni vyema Jumuiya ya Kimataifa ikaharakisha
kukamilisha miundombinu ili kupunguza msongamano Nyarugusu.
Serikali
imetoa maeneo mengine ya Nduta yaliyoko Kibondo na na Ntendeli, Kakonko
kwa ajili ya kupunguza uwingi wa watu katika kambi hiyo.
DC
huyo pia alisema kwamba kuna uharibifu mkubwa wa mazingira na lazima
wadau wote washirikiane kuhakikisha kwamba mazingira yanaboreshwa pamoja
na kupokea wakimbizi na kuwapa makazi.
Alisema kambi hiyo ilipangwa kuwa na watu elfu 50 kwa miaka ya 1996 lakini sasa inaweka wakimbizi wengi zaidi.
Aidha
alisema kwamba pamoja na kupokea wakimbizi hao, inaonekana baadhi yao
wameingia kufanya uhalifu na kuomba wakimbizi kushirikiana na polisi
kuwataja wahalifu hao ili wadhibitiwe.
Kuwepo
kwa kundi kubwa la wakimbizi kunasababisha uharibifu wa mazingira kama
inavyoonekana pichani wakimbizi wakitoka kukata kuni kwenye misitu
iliyopo karibu na kambi ya Nyarugusu wilayani Kasulu mkoani Kigoma.
Aidha
katika mazungumzo ya shukurani kwa namna serikali ya Kigoma inavyotoa
ushirikiano kwa Mashirika ya Umoja wa Mataifa katika miradi ya maendeleo
na misaada kwa wananchi na kwa wakimbizi, Mwakilishi wa Shirika la
mpango wa idadi ya watu duniani (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem alisema
kwamba kumekuwepo na mafanikio mengi kutokana na ushirikiano huo.
Alisema
anachokiona yeye anaona hali ya baadae ya taifa la Tanzania kuwa bora
zaidi kutokana na kuwapo kwa ushirikiano mzuri kati ya serikali,
mashirika ya umma na kundi kubwa la vijana ambalo kwa sasa linapokea
elimu mbalimbali kwa manufaa yao na ya baadae.
“Taifa
la Tanzania nusu yake ni vijana na sehemu kubwa ni chini yake, taifa
hili lina hali njema kabisa ya siku za usoni kutokana na ushirikiano
wenye lengo la kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na wengi” alisema
Kanem.
Anasema
kwa kuangalia program zilizopo zinazotekelezwa kwa pamoja na mashirika
ya Umoja wa Mataifa na serikali anaona mafanikio ya mafunzo ya
ujasiriamali na pia elimu inayotolewa kwa watu kwa malengo ya
kufanikisha maendeleo.
Alisema
UNFPA imefurahishwa sana namna mafunzo yanavyoendeshwa kwa vijana
mafunzo ambayo yanaleta mshikamano wa pekee katika kufanikisha ustawi wa
jamii na taifa kwa jumla.
Aidha
alifurahi kuona kwamba wanawake wanashiriki katika kutoa elimu hivyo
kuingiza sauti katika mafanikio ya jamii na uongezaji wa uelewa miongoni
mwa jamii.
Mratibu
huyo Mkazi wa UN Tanzania, Alvaro Rodriguez na timu yake wamerejea Dar
es Salaam baada ya ziara ndefu kuangalia miradi ya Umoja wa Mataifa
inavyoleta tija na ufanisi wa maisha katika jamii.
Mratibu huyo alitembelea mikoa ya Manyara, Singida, Tabora na Kigoma.
Katika
ziara yake alioneshwa kufurahishwa na miradi hiyo inavyobadili jamii
husika na kusema kwamba umoja huo utaendelea kufadhili miradi ya
maendeleo nchini Tanzania.
Mkuu
wa Kambi ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile (kulia) akielezea changamoto
mbalimbali zinazowakabili kambini hapo kwa Mratibu Mkazi wa Mashirika
ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP), Alvaro
Rodriguez (wa pili kulia) na ujumbe wake aliombatana nao Mwakilishi wa
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani
(UNFPA) nchini, Dkt. Natalia Kanem (wa pili kushoto) pamoja na Ofisa wa
Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan (kushoto)
kabla ya kutembelea makazi ya wakimbizi hao.
Mwakilishi
wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani
(UNFPA) nchini, Dkt. Natalia Kanem (kulia) na Ofisa wa Mambo ya Nje
kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan wakirekodi mambo muhimu
wakati wa kupokea taarifa ya maendeleo ya kambi ya Wakimbizi ya
Nyarugusu kutoka kwa Mkuu wa Kambi ya Nyarugusu B, Fredrick Nisajile
(hayupo pichani).
Kutoka
kushoto ni Afisa mahusiano wa UNHCR, Ofisi ya Kasulu, Agnes Mwangoka,
Mshauri na Mtaalum wa Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Hoyce
Temu, Mwandishi wa Habari, Prosper Kwigize pamoja na Ofisa wa Mambo ya
Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan wakielekea kwenye kambi
za Wakimbizi baada ya kupokea taarifa.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez pamoja na Mwakilishi wa Shirika la
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu duniani (UNFPA) nchini,
Dkt. Natalia Kanem wakikagua ndani ya mahema wanakoishi Wakimbizi wapya
wanaoendelea kuwasili katika kambi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu
mkoani Kigoma.
Mmoja wa Wakimbizi akiwa na mwanae nje ya chumba chake na mwanae katika kambi ya Nyarugusu.
Kuni zikitumika kupikia chungu cha Maharage kambini hapo.
Mtoto
ambaye jina lake halikuweza kupatikana kiurahisi akikoleza moto
ulioonekana kufifia wakati akijiandalia chakula chake cha mchana kama
alivyonaswa na kamera yetu.
Moja
ya familia ya Wakimbizi katika kambi ya Nyarugusu wakiangalia msafara
wa Mkuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini uliotembelea kambini
hapo mwishoni mwa juma.
Ofisa
wa Mambo ya Nje kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara
ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Maulidah Hassan akipozi na
moja ya familia katika kambi ya Wakimbizi ya Nyarugusu.
Mratibu
Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la
Maendeleo (UNDP), Alvaro Rodriguez akisalimiana na Rais wa kambi ya
Wakimbizi ya Nyarugusu, Bi. Abilola Angelique wakati wa ziara yake ya
kutembelea kambi ya wakimbizi ya Nyarugusu iliyoko wilayani Kasulu
mkoani Kigoma.Kwa matukio zaidi ya picha bofya link hii
KESI RUFAA YA TALAKA DHIDI YA MTEMBEI YAAHIRISHWA
Na Mwandishi wetu
KESI
ya rufaa ya madai ya talaka dhidi ya mfanyabiashara na Mkurugenzi wa
shule ya sekondari ya St Mathew, Thadei Mtembei imeahirishwa baada ya
wakili wa Mtembei, Mussa Kyoboya kudai mrufaniwa yuko India kwa
matibabu.
Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Temeke, Tarimo.
Katika
kesi hiyo, mpeleka rufaa, Magreth Mwangu anawakilishwa na wakili Chacha
Mrungu. Kesi hiyo ilikuja mahakamani juzi ambapo mrufaniwa alitakiwa
kupeleka majibu ya rufaa.
Hata
hivyo, wakili wake alisema majibu hayako tayari kwani kuna vipengele
ambavyo alitakiwa kusaini, lakini ilishindikana kutokana na kuwa nchini
India kwa matibabu. Kesi hiyo imepangwa kuendelea Desemba 16 mwaka huu.
Awali,
kesi hiyo ilisikilizwa katika Mahakama ya Mwanzo Kizuiani mbele ya
hakimu Rajab Tamaambele, ambapo Mwangu na watoto wake walionekana hawana
haki, kwa madai sio mke halali na watoto hao ni wa zinaa kutokana na
kuzaliwa nje ya ndoa.
Katika madai ya msingi, Mwangu anataka talaka, mgawanyo wa mali na matunzo ya watoto.
Katika
sababu za rufaa, mrufani alieleza kusikitishwa na maamuzi yaliyotolewa
na Mahakama ya Mwanzo Kizuiani Septemba Mosi mwaka huu, kwa hakimu
kukosea kisheria kwa kutosaini nakala ya hukumu ikiwa ni pamoja na
kukosekana kwa saini za wazee wa baraza.
Sababu
nyingine ni Mahakama kukosea kisheria kwa kunyang’anya haki ya watoto
kwa kutotoa matunzo ya watoto kwa mama, ambaye anaishi na mrufaniwa kwa
miaka 20 na kuvunja Sheria ya Mtoto Namba 21 ya mwaka 2009. Maamuzi ya
Mahakama ya Kizuiani yalishindwa kufuata sheria kwa wazee wa baraza
kushindwa kutoa maoni yao.
























No comments :
Post a Comment