Afisa wa Operesheni wa Mfuko wa Pensheni wa PPF,
Kanda ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, Saluna Aziz Ally, (kushoto),
akimeuelekezea mwanachama wa Mfuko huo jinsi ya kupata taarifa za michango yake
iliyopelekwa na mwajiri wake PPF kupitia
simu ya mkononi, huduma ijulikanayo kama “PPF Taarifa’’.
Christian Gaya Mwananchi Alhamis26 Novemba 2015
Wiki iliyopita tuliona ya kuwa mara
nyingi waajiri wanatoa sababu zinazofanana zinazowafanya wasipeleke michango ya
wafanyakazi wao
Lakini kutokana na utafiti
uliofanywa unaonyesha ya kuwa waajiri wengi huchukulia michango kama gharama
kubwa kwao ambapo wakati mwingine inasababisha hata kupandisha bei za bidhaa
zao wanazopeleka sokoni na hivyo kufidiwa na mlaji ambapo unakuta ndiyo huyo
huyo mwanachama wa mfuko wa hifadhi ya jamii.
Na mara nyingi hupunguza hata idadi
ya wafanyakazi wake wanapotoa taarifa kwa wakaguzi wa mifuko ya hifadhi ya
jamii. Madharani ana wafanyakazi 100 lakini utakuta walioandikishwa kama
wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii ni 50 tu.
Na wakati mwingine wanapunguza hata
kuonyesha mishahara kamili ya wafanyakazi wao kwa wakaguzi wa mifuko hii ya
pensheni kwa kukubaliana na baadhi ya wafanyakazi ya kwamba atakuwa anachukua
tofauti ili kukwepa makato ya michango ya pensheni.
Kwa kawaida mfanyakazi ambaye ni
mwanachama wa mfuko wa pensheni hukatwa asilimia 10 ya jumla ya mapato yake
yote kwa mwezi na mwajiri analazimika huchangia asilimia 10 ya mapato yote ya
mshahara wa mfanyakazi hivyo na kufanya kuwa jumla ya asilimia 20 na yote
kupelekwa kwenye akaunti ya mwanachama wa mfuko wa pensheni wa hifadhi.
Au mwajiri huweza kuchangia asilimia
15 na mwajiriwa asilimia 5 au asilimia yote 20 inaweza kutolewa na mwajiri kwa
mfanyakazi wake kulingana na makubaliano.
Mfano jumla ya pato la mshahara wa
mfanyakazi kwa mwezi ni shilingi 700,000.00 hiyo asilimia kumi ya mchango wa
mfanyakazi utakuwa shilingi 70,000.00 na mwajiri naye lazima atachangia
asilimia kumi ya shilingi 700,000.00 ambayo ni shilingi 70,000.00. kwa hiyo
mchango wa pensheni wa kila mwezi wa mfanyakazi huyo itakuwa shilingi
140,000.00.
Hivyo basi kwa kujiunga na mfuko
wowote wa pensheni wa hifadhi ya jamii unapata faida ya kuongezwa pato kutoka
kwa mwajiri wako kwa kuchangiwa kwenye pensheni yako ya sasa na ya baadaye.
Na tambua ya kuwa makato yako ya
pensheni hukatwa kabla ya makato yoyote ya kodi ili kutunisha pensheni yako
wewe mwanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii.
Na nadharia nyingi na kutoka kwa
baadhi ya wafanyakazi wamekuwa wakisema ya kuwa baadhi ya wakaguzi
wanashirikiana na waajiri wasio waaminifu kudidimiza michango ya pensheni
kutokusanywa ipasavyo na hata kupunguza idadi ya wafanyakazi wanaotakiwa
kuandikishwa na mifuko ya pensheni ya hifadhi ya jamii ukiwemo na ujanja
mwingine uliotajwa hapo juu ingawa hauna ushahidi wowote.
Na hata wakati mwingine kesi za
jinai na madai ya michango ya pensheni ya hifadhi ya jamii kucheleweshwa kwa
muda mrefu kusababishwa na ucheleweswaji wa uendeshwaji wa kesi ambapo huchukua
muda mrefu sana mpaka kupatikana kwa
michango wa wanachama.
Na hapa inaonyesha ya kuwa watu
wengi wamekuwa wakilipwa michango ya pensheni pungufu kwa wakati wote huu wa
kuondoa michango ya pensheni kabla ya wakati wake na kwa sababu wengi wamekuwa
wakikimbilia kwenye akaunti zao za michango ya pensheni ya hifadhi ya jamii kwa
kutatua shida zao za kijamii na za kiuchumi kwa kuwa na mitazamo tofauti juu ya
jambo hili.
Lakini wakati mwingine imekuwa ni
faida kwa upande wa mifuko kwa kuwalipa pungufu wateja wao na kubakiwa na idadi
kubwa ya michango ambayo haitafuatiliwa na wadai.
Ikumbukwe ya kuwa utafiti unaonyesha
michango mingi ya pensheni inayotolewa na wanachama ni ya uwongo au kudanganya
kwa sababu idadi kubwa ya wanachama waliojitoa bado wako kazini aidha kwa kushirikiana
na waajiri wenyewe.
Jambo la kujiuliza hapa ni kwamba ni
wajibu wa nani kukusanya michango. Na inaonyesha ya kuwa mpaka Machi 2015 mifuko
ilikuwa inadai shilingi bilioni 18 zikiwa kama michango ya pensheni ambayo
haijawasiliswa kwenye mifuko ya jamii ya NSSF na PPF.
Mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii
(NSSF) na mfuko wa pensheni wa PPF wanasema mpaka kufikia mwezi Septemba 2013
zaidi ya waajiri wapatao 230 walikuwa hawajawasisha michango ya pensheni ya
wafanyakazi wao ambayo kwa kweli ni makosa ya jinai kisheria
Kulingana na gazeti la The Guardian
la tarehe 17 Novemba 2013 mkuu wa idara ya uhusiano na huduma kwa wateja wa
NSSF Bi. Eunice Chiume alisema zaidi ya waajiri 200 walikuwa wameshidwa
kuwasilisha michango na kusababisha
hasara ya bilioni 16.
Kati ya hizi zote, bilioni 6 zilikuwa zimesabishwa na Mamlaka ya
Reli ya Tazara. Wakati kwa upande wa mfuko wa pensheni wa PPF Bi Vupe
Ligate ambaye ni mkurugenzi wa sheria alisema ya kuwa zaidi ya waajiri 30 nao walikuwa
wameshidwa kuwasilisha makusanyo ya michango ya wafanyakazi wao ambayo ni kama
jumla ya bilioni 6 kwenye mfuko wa pensheni wa PPF
Ingawa mifuko imeweza kuwafunguliwa
mashtaka ya jinai karibu waajiri wote wanalioshidwa kuwasilisha michango ya
wafanyakazi wao. Lakini pamoja na hayo baadhi ya waajiri walisha waachisha kazi
wafanyakazi wao kwa sababu mbalimbali
Na ndio maana Bi. Chiume wa NSSF alisema
NSSF wameanzisha mfuko unaitwa akaunti ya hasara ya kuwalipia baadhi ya
wanachama wanaodai au wanaotaka kutoa michango yao ya pensheni aidha baada ya
kuachishwa kazi, au kufikisha umri wa kustaafu au kumaliza mkataba wake.
Kwa vile wajibu wa kufuatilia
michango ya pensheni ya mwanachama ya
kuwa inawasilishwa na waajiri ilikuwa ni NSSF na mkataba ulikuwa kati ya NSSF
na mwanachama kwa kumpatia hata kadi ya uwanachama imemlazimu NSSF kuwalipia wanachama wake kama wateja wake kiasi cha bilioni 2.
Na mpaka wakati huo mzigo ulikuwa
kwa mfuko wa pensheni wa NSSF kupambana na waajiri hao kuhakikisha ya kuwa
wanawasilisha michango yote ya wanachama wao kisheria
No comments :
Post a Comment