Mwenyekiti
wa Jukwaa Huru la Wazalendo Ndugu Salum Ally Hapi akizungumza na
waandishi wa habari kwenye hotel ya Travetine ,Magomeni jijini Dar es
Salaam, kulia ni Katibu wa Jukwaa hilo Ndugu Mtela Mwampamba.
……………………………………………………………………………….
Ndugu wanahabari,
Mbele yenu sisi tuliowaita hapa ni Jukwaa Huru la Wazalendo ambalo
limeitisha mkutano huu ili kufikisha yale tuliyoyakusudia kuwaeleza umma wa
watanzania.
Sote tunatambua kuwa nchi yetu imetoka katika uchaguzi mkuu ambao umetupatia
viongozi wapya wa awamu ya tano ya uongozi wa taifa letu chini ya Dr. John
Pombe Joseph Magufuli. Tunapenda kuwapongeza watanzania wote kwa uchaguzi wa
amani na utulivu. Aidha kwakua ndio mara yetu ya kwanza kuzungumza nanyi
tunapenda kuwapongeza wanahabari wote kwa kazi nzuri ambayo mmekua mkiifanya
kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchini. Tunawashukuru sana.
Mkutano wetu huu umebeba madhumuni makubwa mawili.
Kwanza ni kumpongeza Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
hotuba yake aliyoitoa Bungeni siku ya ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 19/11/2015. Tunaiunga mkono Hotuba yake
ambayo kwa kweli ilikuwa imebeba Uzalendo, Ujasiri, dira ya kweli ya maendeleo
ya taifa letu na muuelekeo mpya wa Serikali ya awamu ya tano. Mambo yote
aliyozungumzia Mh. Rais yamebeba maslahi mapana ya nchi yetu na yanalenga
kuijenga Tanzania mpya ambayo waasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere na Abeid Amani Karume walikusudia kuijenga.
Pili, pamoja na mambo mengi yaliyogusiwa na hotuba ya Mh. Rais, eneo la
kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa Serikali ni
moja katika mambo ambayo Jukwaa hili limeamua kuyaunga mkono kwa vitendo.
Mh. Rais alitoa mchanganuo wa eneo moja tu la safari za nje na jinsi lilivyo
ligharimu Taifa mabilioni ya shilingi na kuahidi kuwa serikali ya awamu ya tano
chini ya uongozi wake itajikita katika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Aidha Mh. Rais ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake hiyo ya kupunguza
matumizi yote yasiyo ya lazima Serikalini, ikiwemo hafla, warsha, makongamano
na safari za nje.
Jukwaa Huru la Wazalendo, linatambua kuwa kwa miaka kadhaa mbunge wa Kigoma
Mjini Mh. Zitto Kabwe amekuwa na msimamo wa kutokupokea posho za kitako tangu
akiwa mbunge wa Kigoma Kaskazini katika Bunge la 10. Pamoja na mh. Zitto,
Jukwaa pia limepokea taarifa za baadhi ya wabunge wa Bunge la 11 la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania walioamua kuunga mkono juhudi za Mh. Rais za kupunguza
matumizi yasiyo ya lazima serikalini kwa kukataa hadharani kupokea posho ya
kitako ya mbunge (sitting allowance).
Mnamo tarehe 23/11/2015, mbunge wa Singida Magharibi (CCM) Mh. Elibariki
Imanuel Kingu alimwandikia barua Katibu wa Bunge akieleza msimamo wake wa
kukataa kulipwa posho ya kitako ya Bunge (sitting allowance) katika kipindi
chote cha miaka mitano (2015 – 2020). Huyu anakuwa ni mbunge wa pili
baada ya Mh. Zitto Kabwe kutoka hadharani na kukataa posho ambazo msingi wake
ni unyonyaji wa wanyonge na ubadhirifu wa kodi za wananchi.
Jukwaa linapenda kumpongeza Mh. Kingu Mbunge kwa ujasiri wake na Uzalendo
kwa Taifa lake, uliomfanya kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa vitendo.
Jukwaa linatambua ya kwamba, mapambano ambayo Mh. Kingu Mbunge ameyaanzisha
ni makubwa, magumu na yanahitaji kuungwa mkono na watanzania wote wanaoipenda
nchi yao bila kujali itikadi za vyama. Tunafahamu, wapo baadhi ya wabunge
wabinafsi na wasio na huruma na wanyonge wa Taifa letu ambao hawajafurahishwa
na hatua hii ya wabunge kama Zitto na Kingu ya kukataa posho ya kitako. Baadhi
ya wabunge wameanza kumpigia simu na kumtumia jumbe (sms) za vitisho mh.
Elibariki Kingu (MB) na wengine wakibeza kuwa anatafuta cheo.
Jukwaa linalaani hatua za wabunge hao wanaopinga nia njema ya Mh. Elibariki
Kingu na Mh. Zitto Kabwe kwa uamuzi wao wa kukataa posho za kinyonyaji na hivyo
basi, Jukwaa linawaomba wananchi wote majimboni, kuwataka wabunge wao
waliowachagua kueleza misimamo yao hadharani juu ya kuunga mkono hatua ya
kukataa posho kama njia ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima.
Jukwaa linafahamu ya kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye
mwenye mamlaka ya mwisho ya kuidhinisha masharti ya kazi za kibunge na stahiki
wanazopaswa kulipwa katika kazi hiyo.
Continue reading →Ndugu wanahabari,
Mbele yenu sisi tuliowaita hapa ni Jukwaa Huru la Wazalendo ambalo
limeitisha mkutano huu ili kufikisha yale tuliyoyakusudia kuwaeleza umma wa
watanzania.
Sote tunatambua kuwa nchi yetu imetoka katika uchaguzi mkuu ambao umetupatia
viongozi wapya wa awamu ya tano ya uongozi wa taifa letu chini ya Dr. John
Pombe Joseph Magufuli. Tunapenda kuwapongeza watanzania wote kwa uchaguzi wa
amani na utulivu. Aidha kwakua ndio mara yetu ya kwanza kuzungumza nanyi
tunapenda kuwapongeza wanahabari wote kwa kazi nzuri ambayo mmekua mkiifanya
kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu nchini. Tunawashukuru sana.
Mkutano wetu huu umebeba madhumuni makubwa mawili.
Kwanza ni kumpongeza Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa
hotuba yake aliyoitoa Bungeni siku ya ufunguzi wa Bunge la 11 la Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania mnamo tarehe 19/11/2015. Tunaiunga mkono Hotuba yake
ambayo kwa kweli ilikuwa imebeba Uzalendo, Ujasiri, dira ya kweli ya maendeleo
ya taifa letu na muuelekeo mpya wa Serikali ya awamu ya tano. Mambo yote
aliyozungumzia Mh. Rais yamebeba maslahi mapana ya nchi yetu na yanalenga
kuijenga Tanzania mpya ambayo waasisi wa Taifa letu Mwalimu Julius Kambarage
Nyerere na Abeid Amani Karume walikusudia kuijenga.
Pili, pamoja na mambo mengi yaliyogusiwa na hotuba ya Mh. Rais, eneo la
kubana matumizi na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima kwa Serikali ni
moja katika mambo ambayo Jukwaa hili limeamua kuyaunga mkono kwa vitendo.
Mh. Rais alitoa mchanganuo wa eneo moja tu la safari za nje na jinsi lilivyo
ligharimu Taifa mabilioni ya shilingi na kuahidi kuwa serikali ya awamu ya tano
chini ya uongozi wake itajikita katika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima.
Aidha Mh. Rais ameanza kutekeleza kwa vitendo ahadi yake hiyo ya kupunguza
matumizi yote yasiyo ya lazima Serikalini, ikiwemo hafla, warsha, makongamano
na safari za nje.
Jukwaa Huru la Wazalendo, linatambua kuwa kwa miaka kadhaa mbunge wa Kigoma
Mjini Mh. Zitto Kabwe amekuwa na msimamo wa kutokupokea posho za kitako tangu
akiwa mbunge wa Kigoma Kaskazini katika Bunge la 10. Pamoja na mh. Zitto,
Jukwaa pia limepokea taarifa za baadhi ya wabunge wa Bunge la 11 la Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania walioamua kuunga mkono juhudi za Mh. Rais za kupunguza
matumizi yasiyo ya lazima serikalini kwa kukataa hadharani kupokea posho ya
kitako ya mbunge (sitting allowance).
Mnamo tarehe 23/11/2015, mbunge wa Singida Magharibi (CCM) Mh. Elibariki
Imanuel Kingu alimwandikia barua Katibu wa Bunge akieleza msimamo wake wa
kukataa kulipwa posho ya kitako ya Bunge (sitting allowance) katika kipindi
chote cha miaka mitano (2015 – 2020). Huyu anakuwa ni mbunge wa pili
baada ya Mh. Zitto Kabwe kutoka hadharani na kukataa posho ambazo msingi wake
ni unyonyaji wa wanyonge na ubadhirifu wa kodi za wananchi.
Jukwaa linapenda kumpongeza Mh. Kingu Mbunge kwa ujasiri wake na Uzalendo
kwa Taifa lake, uliomfanya kuunga mkono juhudi za Mh. Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kwa vitendo.
Jukwaa linatambua ya kwamba, mapambano ambayo Mh. Kingu Mbunge ameyaanzisha
ni makubwa, magumu na yanahitaji kuungwa mkono na watanzania wote wanaoipenda
nchi yao bila kujali itikadi za vyama. Tunafahamu, wapo baadhi ya wabunge
wabinafsi na wasio na huruma na wanyonge wa Taifa letu ambao hawajafurahishwa
na hatua hii ya wabunge kama Zitto na Kingu ya kukataa posho ya kitako. Baadhi
ya wabunge wameanza kumpigia simu na kumtumia jumbe (sms) za vitisho mh.
Elibariki Kingu (MB) na wengine wakibeza kuwa anatafuta cheo.
Jukwaa linalaani hatua za wabunge hao wanaopinga nia njema ya Mh. Elibariki
Kingu na Mh. Zitto Kabwe kwa uamuzi wao wa kukataa posho za kinyonyaji na hivyo
basi, Jukwaa linawaomba wananchi wote majimboni, kuwataka wabunge wao
waliowachagua kueleza misimamo yao hadharani juu ya kuunga mkono hatua ya
kukataa posho kama njia ya kupunguza matumizi ya Serikali yasiyo ya lazima.
Jukwaa linafahamu ya kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ndiye
mwenye mamlaka ya mwisho ya kuidhinisha masharti ya kazi za kibunge na stahiki
wanazopaswa kulipwa katika kazi hiyo.
SERIKALI YAAHIDI KUSHIRIKIANA NA MASHIRIKA NA WADAU WA HABARI KUTOKOMEZA VITENDO VYA UKATILI KWA WAANDISHI WA HABARI
Mkuu
wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues
(katikati) akisalimiana na Mjumbe wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio
Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi Mstaafu, Christopher Liundi alipowasili
katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa
waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa
habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO. Kulia
ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof.
Ole Sante Gabriel.
Na Rabi Hume, Modewjiblog
Serikali
mpya ya awamu ya tano iliyochini ya rais Dr. John Magufuli, imeahidi
kushirikiana na mashirika na wadau mbalimbali ambao wamekuwa wakipambana
kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa salama na kufanya kazi zao kwa
uhuru bili kuingiliwa ufanyaji wa kazi zao na mtu yoyote.
Ahadi
hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Prof. Ole Sante Gabriel katika mkutano wa kitaifa wa
mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa
kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia
maadili ulioandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia na
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Prof. Gabriel amesema
serikali ya awamu ya tano ipo tayari kushirikiana na mashirika na wadau
mbalimbali ambao wapo kuwasaidia waandishi wa habari ili haki zao ziweze
kutekelezwa kutokana na kuwepo kwa uvunjaji wa haki za wanahabari.
Amesema
wanatambua kuwepo kwa changamoto hizo kwa waandishi wa habari na kwa
serikali ya awamu ya tano itahakikisha kushirikiana na mashirika na
wadau ili kutetea haki za wanahabari kwa kuwa na uhuru katika utendaji
wa kazi zao bila kuingiliwa na mtu.
“Naahidi
kuanzia sasa serikali itakuwa ikishirikiana nanyi kusaidia kuhakikisha
kunakuwa na uhuru wa vyombo vya habari, nchi yetu kwa sasa haina sababu
ya kuacha kuungana na ninyi kutokomeza vitendo hivyo kwa wanahabari,
serikali ni mpya na tutalitekeleza jambo hilo kila tumaposhirikishwa
kuhusu vitendo vibaya kwa wanahabari,” amesema Prof. Gabriel.
Mkuu
wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akitoa
neno la ufunguzi katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi
kufungua.
Aidha
Katibu Mkuu huyo amewata waandishi wa habari kuwa pamoja na usaidizi
ambao wizara imeamua kujitoa kuwasaidia pia wanapaswa kuandika habari
zenye weledi na zilizo sahihi kwani kumekuwepo na kundi kubwa la
waandishi wa habari ambao wamekuwa wakiandika habari ambazo hazina
uhakika wala weledi na hivyo kuupotosha umma kwa habari wanazoandika ila
kuanzia sasa wanabidi kubadilika kwa kuandika habari ambazo zitakuwa na
fadia kwa jamii inayowazunguka.
Kwa
upande wa UNESCO, kupitia kwa Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la
Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)
nchini, Zulmira Rodrigues, amesema kumekuwepo na vitendo vingi ambavyo
sio vya kibinadamu ambavyo wamekuwa wakifanyiwa waandishi wa habari na
wao wameamua kujitoa kuhakikisha wanatokomeza vitendo hivyo.
Amesema
kama jamii ikiungana kwa pamoja kutokomeza vitendo hivyo inawezekana
kwani kutokuwepo uhuru wa waandishi wa habari katika utendaji wao wa
kazi kunapelekea jamii kukosa baadhi ya taarifa muhimu ambazo kama
kukipatikana uhuru wa habari kutawapa fursa wanahabari wa kuzitoa
taarifa hizo.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante
Gabriel akisisitiza jambo wakati akifungua rasmi mkutano wa kitaifa wa
mashauriano kuhusu hali ya usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa
kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa habari na uandishi unaozingatia
maadili ambao umeandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na
Elimu, Sayansi (UNESCO).
“UNESCO
tunapenda kuona vitendo hivyo havifanyiki kwa waandishi wa habari kama
kuweka sheria ambazo zinawabana na kusababisha wanashindwa kufanya kazi
zao kwa uhuru na tunaweza kuona kama serikali na kila mtu akiwa tayari
tunaweza kumaliza tatizo hilo,” amesema Rodrigues.
Nae
Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS),
Flaviana Charles amesema imekuwa ngumu kesi zinazokuwa zikiwahusu
waandishi wa habari juu ya vitendo vya kikatili wanavyotendewa kutokana
na ucheleweshwaji wa upelelezi unaofanywa na Jeshi la Polisi Tanzania
akitolea mfano kesi ya mwandishi wa zamani wa Chaneli 10 mkoani Iringa,
Daudi Mwangosi ambapo mpaka sasa ina miaka 4 na bado upelelezi
haujakamilika.
Makamu wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika, Bi. Flaviana Charles akifafanua jambo wakati wa mkutano huo.
Pichani
juu na chini ni wahariri wa vyombo vya habari, waandishi wa habari,
wadau wa tasnia ya habari pamoja na maafisa wa UNESCO na taasisi
mbalimbali walioshiriki mkutano huo.
Mhadhiri
wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) katika tasnia ya Habari na
Mawasiliano, Ayub Rioba akiwasilisha mada ya wajibu wa vyombo vya habari
huku akitolea mfano wa moja ya habari iliyobeba kichwa cha habari
“Uhuru wa habari watikiswa Zimbabwe” katika moja ya magazeti ya Serikali
wakati wa mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa
waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa
habari na uandishi unaozingatia maadili ulioandaliwa na UNESCO.
Ofisa
Miradi katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama UNESCO, Nancy Kaizilege
akiwasilisha mada ya Uhuru wa vyombo vya Habari katika mkutano huo.
Mratibu
wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),
Mwanasheria Onesmo Olengurumwa akielezea jinsi mtandao wake unavyotoa
msaada kwa wanahabari wanaokumbwa matukio mbalimbali katika utendaji wao
hususan msaada wa kisheria.
Mhariri
Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena akiuliza swali kwa
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene (hayupo pichani)
katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya usalama wa
waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa waandishi wa
habari na uandishi unaozingatia maadili sambamba na kuadhimisha
“International Day to #EndImpunity” ulioandaliwa na UNESCO.
Mkurugenzi
wa Idara ya Habari (MAELEZO), Assah Mwambene akitolea ufafanuzi wa
swali la Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima, Neville Meena
(hayupo pichani).
Mkuu
wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia
Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues akitoa
maoni katika katika mkutano wa kitaifa wa mashauriano kuhusu hali ya
usalama wa waandishi wa habari, uzinduzi wa kikosi kazi cha usalama wa
waandishi wa habari na uandishi unaozingatia maadili sambamba na
kuadhimisha “International Day to #EndImpunity” ulioandaliwa na UNESCO.
Mjumbe
wa bodi udhamini ya Mtandao wa Radio Jamii Tanzania (COMNETA), Balozi
Mstaafu, Christopher Liundi akitoa pongezi kwa Shirika la UNESCO katika
kuhamasisha Amani kupitia, Redio za Jamii, makongamano mbalimbali pamoja
na kuwashirikisha viongozi wa dini kuhubiri Amani nchini katika mkutano
huo.
Mwandishi wa habari mkongwe, Halima Sharrif akitoa maoni katika mkutano huo.
Kutoka
kushoto ni Ofisa miradi katika kitengo cha Mawasiliano na Tehama
UNESCO, Nancy Kaizilege, Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za
Binadamu Tanzania (THRDC), Mwanasheria Onesmo Olengurumwa, Mkuu wa ofisi
na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Elimu,
Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Zulmira Rodrigues pamoja na Makamu
wa Rais wa Chama cha Kijamii cha Wanasheria wa Tanganyika, Bi. Flaviana
Charles katika picha ya ukumbusho.
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Ole Sante
Gabriel (kushoto) akifurahi jambo na Mhariri Mtendaji wa Gazeti la
Tanzania Daima, Neville Meena mara baada ya zoezi la picha ya pamoja.
Jumia.co.tz partners with Ecobank Tanzania for the launch of Black Friday in Tanzania
Jumia Tanzania (www.jumia.co.tz), Africa’s largest online shopping mall, launches its first edition of Black Friday on 27th November, in partnership with Ecobank Tanzania.
Dar es Salaam, November 24th, 2015 –Be ready for unbelievable discounts! On 27th November
a unique online flash sale event, Black Friday, will take place on
Jumia Tanzania (www.jumia.co.tz). Black Friday, one of the most popular
shopping events in the world, is all about deals and bargain hunting
during only one day. This year, Black Friday on Jumia Tanzania will
start on Friday 27th November and will be extended until Monday 30th November.
Jumia
is the first online mall in Africa (present in 11 countries in Africa)
where customers can choose between a large range of products from
fashion, to electronics such as phones and TVs. Jumia introduced Black
Friday to the African market in 2013 and made it become the first and
largest event of its kind in Africa. During this day, Africans search
for the best deals and discounts that they would otherwise not get on a
regular day.
“Originally
established in the U.S. more than 50 years ago, Black Friday, which
take place after Thanksgiving day, is now a well-known sales day both in
the U.S. and Europe. People go mad for it. This year, we bring the
concept to Tanzania. We’ve got mind blowing deals for our customers. And
can’t wait to share them!” stated Jean-Philippe Boul, Managing Director of Jumia Tanzania.
For the 1st edition
of Jumia Black Friday in Tanzania;Jumia has decided to partner with
Ecobank Tanzania which isa Subsidiary of Ecobank Transnational
Incorporated (ETI), a multinational bank presents in 36 African
Countries.“With its wide network and a wide range of advanced electronic
offering Ecobank is the right partner. The partnership will go beyond
Black Friday, whereby Ecobank Customers will be able to purchase
merchandise on Jumia.co.tz at a special discount of rate. The two
companies will join their efforts to make payments on Jumia.co.tz an
afterthought. Ecobank’s mission is to bring services closer to our all
customers while connecting them to the rest of Africa through our wide
network and diverse offering” said Eric Luyangi (Head of Altenative
Channels)
In
2014, while more than 100 million Americans were shopping over the
Black Friday holiday, millions more were shopping online on Jumia. Last
year, Jumia reached an all-peak in sales within 24 hours and had over
1,500,000 online visitors. Over 50% of the visitors accessed the site
through a mobile device viaAndroid oriOS. These sales represented an extraordinary tenfold order increase compared to 2013’s Black Friday.
“Africa’s
disposable income & online consumption is growing at an
extraordinary rate. In Tanzania, we expect to sell more in this year’s
Black Friday than in the whole of 2014. But this is just the start. We
are here for the long term and have plenty more surprises to come”,
added Jean-Philippe Boul
Last year’s Black Friday sales
primarily focused on consumer electronics, with particular interest in
digital products such as flatscreen TVs, digital cameras and ventilation
systems. This year, Jumia predicts that it will sell a lot more fashion
& cosmetics too, with great deals such as all kinds of stylish
dresses at 50% off. Jumia positions itself as the leading marketplace
for high-end local and international brands. They work with everyone
from local fashion brands such as Footstep (50% off!), to established
mobile brands such as Samsung, Tecno or itel (up to 23% off –Tecno C8 below 274,000 TSH). On Jumia’s Black Friday,
you will be able to get your hands on the Samsung Tab4 7” tablet for
less than 345,000 TSH (that’s 18% off!) and Sony 32” TV at 23% off.
Black
Friday will also be a great occasion for Jumia Tanzania to launch
InnJoo phones and tablet. InnJoo had already experienced a massive
success in the other Jumia markets and is now ready to enter the
promising Tanzanian market (InnJoo tablet F3, InnJoo Halo and Fire
smartphones).
“By
tapping into this global shopping phenomenon, with the support of our
partner Ecobank Tanzania, we have created a powerful event that our
customers will love.” concluded Jean-Philippe Boul.
About Black Friday
Black
Friday is a popular label attached to the Friday following Thanksgiving
Day in the US. This day marks the beginning of the busy shopping season
during which most consumers typically start their Christmas/holiday
shopping.
An
explanation of the name « Black Friday » is that during that day so
many people went out to shop that it caused traffic accidents and
sometimes even violence. « Black Friday » officially opens the Christmas
shopping season in center city, and it usually brings massive traffic
jams and over-crowded sidewalks as the downtown stores are mobbed from
opening to closing.”
Doorcrashers,
special deals and heavy discounts on the most highly sought after
holiday gifts are often offered by retailers in order to lure consumers
into their stores in the hope that they will purchase other, more
expensive, goods. Some bargain hunting consumers have even been known to
camp out overnight in order to secure a place in line at a favorite
store.Www.jumia.co.tz/black-friday
About Jumia
Jumia
is Africa’s leading online shopping destination. Customers across the
continent can shop amongst the widest assortment of high quality
products at affordable prices – offering everything from fashion,
consumer electronics, home appliances to beauty products. Jumia was the
first African company to win an award at the World Retail Awards 2013 in
Paris as the “Best New Retail Launch” of the year.
About Africa Internet Group
Africa
Internet Group, the leading internet platform in Africa, promotes
sustainable online growth that benefits both businesses and consumers.
Firmly rooted in Africa’s startup ecosystem, the group provides
easy-to-use services and smart solutions across the African internet
sector. AIG is invested in furthering regional entrepreneurship and
innovation through a passion for Africa, its culture and its people. AIG
is the parent group of ten successful and fast-growing companies in
more than 30 African countries. Its network of companies includes
Carmudi, Easy Taxi, Everjobs, hellofood, Jovago, Jumia, Kaymu, Lamudi,
Vendito and Zando.
About Ecobank Tanzania
Ecobank
Tanzania is a Subsidiary of Ecobank Transnational Incorporated (ETI), a
multinational bank Present in 36 African Countries. Ecobank began its
operations in Tanzania on the 19th January 2010; the bank currently has 9
branches (Dar-es-salaam branches include: Mwenge, Sokoine Drive,
Uhuru, Msimbazi-Kariakoo, Quality Centre and Acacia- Kinondoni.
Upcountry: Arusha, Mwanza and Mtwara); these branches are strategically
located bringing financial advice closer to Tanzanians and ease of cross
border trade due to the bank’s wide network. Ecobank Tanzania currently
has 22 ATMs all accepting VISA, MasterCard’s, China Union Pay and Pan
African Cards (PAC).
WANAHARAKATI WA TANZANIA WANATOA WITO KWA JAMII KUCHUKUA HATUA ILI KUMLINDA MTOTO APATE ELIMU BORA NA SALAMA
Eda
Malick kutoka Tanzania Women and Children Welfare center akizungumza na
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia
Malick kutoka Tanzania Women and Children Welfare center akizungumza na
waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia
Afande
Christina Onyango, Afisa wa Polisi, mkoa wa kipolisi Ilala akielezea
namna ambavyo dawati la jinsia wamejipanga kufikisha ujumbe wa siku 16
za kupinga ukatili wa kijinsia.
Christina Onyango, Afisa wa Polisi, mkoa wa kipolisi Ilala akielezea
namna ambavyo dawati la jinsia wamejipanga kufikisha ujumbe wa siku 16
za kupinga ukatili wa kijinsia.
Waandishi
wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini Tanzania wakihudhuria mkutano
na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
wa habari kutoka vyombo mbalimbali nchini Tanzania wakihudhuria mkutano
na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
Bahati
Mandago kutoka shirika la Tanzania Human Rights fountain akielezea
mikakati ya shirika lake katika kufikisha ujumbe wa Funguka. Chukua
Hatua Mlinde Mtoto apate elimu.
Mandago kutoka shirika la Tanzania Human Rights fountain akielezea
mikakati ya shirika lake katika kufikisha ujumbe wa Funguka. Chukua
Hatua Mlinde Mtoto apate elimu.
Wadau
kutoka katika mashirika mbalimbali wanaoshiriki kikamilifu katika
utekelezaji wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari
kutoka katika mashirika mbalimbali wanaoshiriki kikamilifu katika
utekelezaji wa maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia
wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari
Dr.
Judith Odunga Mkurugenzi wa Shirika la WiLDAF akisoma taarifa kwa
vyombo vya habari kuhusiana na kuanza kwa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
Judith Odunga Mkurugenzi wa Shirika la WiLDAF akisoma taarifa kwa
vyombo vya habari kuhusiana na kuanza kwa siku 16 za kupinga ukatili wa
kijinsia.
FUNGUKA! CHUKUA HATUA MLINDE MTOTO APATE ELIMU
Katika kuadhimisha Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia kuanzia
tarehe 25 Novemba mpaka 10 Desemba, WiLDAF, Mashirika ya Haki za Binadamu,
Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia watatoa elimu na kuhamasisha umma
kuchukua hatua kumlinda mtoto ili apate elimu bora na salama. Ulinzi wa mtoto ni
pamoja na kuzuia vitendo vyote vya ukatili
wa kijinsia.
tarehe 25 Novemba mpaka 10 Desemba, WiLDAF, Mashirika ya Haki za Binadamu,
Wadau wa Maendeleo na Asasi za Kiraia watatoa elimu na kuhamasisha umma
kuchukua hatua kumlinda mtoto ili apate elimu bora na salama. Ulinzi wa mtoto ni
pamoja na kuzuia vitendo vyote vya ukatili
wa kijinsia.
Maadhismisho ya SIku 16 za kupinga Ukatili wa kijinsia mwaka
huu yanalenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama mashuleni, lengo kuu ikiwa kuhamasisha umma
kuhusu ukubwa wa tatizo la ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu
mashuleni, kwani vitendo vingi vya ukatili wa kijinsa vimekuwa vikiripotiwa.
huu yanalenga zaidi kuzungumzia suala zima la usalama mashuleni, lengo kuu ikiwa kuhamasisha umma
kuhusu ukubwa wa tatizo la ukatili wa kijinsia kwa vijana na watoto wetu
mashuleni, kwani vitendo vingi vya ukatili wa kijinsa vimekuwa vikiripotiwa.
Utafiti uliyofanywa na Chuo cha Tiba Cha Muhimbili (MUHAS)
kwa kushirikiana na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika,
(WiLDAF) umetambua hatari zinazochangia ukatili wa kijinsia ikiwa ni pamoja na
wazazi kutowajali watoto na kutoa adhabu kali kwao na hivyo kuwafanya watoto
kuwa na hofu. Wakati mwingine watoto kufanyiwa ukatili bila wao kufahamu. Aidha,
adhabu ya viboko inahusishwa kama moja ya aina za ukatili dhidi ya watoto. Hii
inaathiri maendeleo ya elimu ya watoto katika taifa letu.
kwa kushirikiana na Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika,
(WiLDAF) umetambua hatari zinazochangia ukatili wa kijinsia ikiwa ni pamoja na
wazazi kutowajali watoto na kutoa adhabu kali kwao na hivyo kuwafanya watoto
kuwa na hofu. Wakati mwingine watoto kufanyiwa ukatili bila wao kufahamu. Aidha,
adhabu ya viboko inahusishwa kama moja ya aina za ukatili dhidi ya watoto. Hii
inaathiri maendeleo ya elimu ya watoto katika taifa letu.
Kukosekana kwa usawa kati ya watoto wa kiume na wa kike hunapelekea
kuwajengea hofu watoto wa kike, na wakati
huo kuwajengea watoto wa kiume ujasiri wa kuona kuwa ni sahihi kwao kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Continue reading →kuwajengea hofu watoto wa kike, na wakati
huo kuwajengea watoto wa kiume ujasiri wa kuona kuwa ni sahihi kwao kufanya vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Muhimbili yapatiwa msaada wa vifaa vya kuokoa maisha ya watoto
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa
Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) Tanzania, Dk Juma Gulaid akisoma
taarifa kabla ya kukabidhi vifaa vya kuhudumia watoto katika hafla fupi
iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Kushoto ni
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando.Picha
zote kwa hisani ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Baadhi ya wauguzi wakisimsikiliza
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF)
Tanzania, Dk Juma Gulaid katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) .
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando akizungumza katika hafla ya kupokea
vifaa vya kisasa vya kuhudumia watoto katika hospitali hiyo. Vifaa
hivyo vimekabidhiwa na Mwakilishi wa UNICEF Tanzania, Dk Juma Gulaid.
Mwakilishi wa UNICEF Tanzania, Dk
Juma Gulaid akimkabidhi hati ya vifaa vya kuwahudumia watoto kwa Katibu
Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Donan Mmbando.
Naibu Mkurugenzi Mkuu wa
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Mseru akipokea
hati ya vifaa kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa
Jamii, Dk Donan Mmbando. Vifaa hivyo vimetolewa na UNICEF.
Baadhi ya wauguzi wakisimsikiliza
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF)
Tanzania, Dk Juma Gulaid katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH).
Baadhi ya vifaa vilivyokabidhiwa
………………………………………………………………………………….
Hospitali ya Taifa Muhimbili
(MNH) imepatiwa msaada wa vifaa kumi vya tiba vya kuwahudumia watoto
mara wapougua na kufikishwa kwenye hospitali hiyo.
Vifaa hivyo vina thamani ya Dola
za Kimarekani Laki moja sawa na zaidi Sh milioni 2 vimetolewa na
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF),kwa lengo la
kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka mitano.
Baadhi ya vifaa vilivyotolewa
ni Ventilator, medical, adult –child ,w/access pamoja na Warmer system ,
newborn, radiant, w/access.
Akizungumza wakati wa kukabidhi
vifaa hivyo Mwakilishi wa UNICEF Tanzania Dk Jama Gulaid amesema
mchango wa UNICEF na michango ya wadau wengine itawezesha watumishi wa
hospitali ya Muhimbili kuokoa maisha ya watoto ambao wanahitaji huduma
za afya.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando amesema hadi
kufikia mwaka 2013 Tanzania imefanikiwa kupunguza vifo vya watoto hao
kwa theluthi mbili.
Kwa mujibu wa Dk Mmbando, mwaka
2013 Tanzania imepunguza vifo hivyo na kufikia 54 kwa vizazi hai 1,000
na kufikia lengo la Milenia na kwamba mafanikio hayo yametokana na
kiwango kikubwa cha chanjo , matumizi sahihi ya dawa za Malaria pamoja
na vyandarua.
Kwa upande wake Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Profesa Lawrence Mseru amewashukuru UNICEF
kwa msaada huo ambao utachangia kwa kiasi kikubwa kuokoa maisha ya
watoto na kuboresha huduma za afya .
Kipindupindu chapungua DAR
Idadi ya wagonjwa wa kipindupindu jijini
Dar es salaam imepungua kufikia wagonjwa kumi na mbili (12) kwa mkoa
mzima, huku wilaya ya Temeke ikiwa na wagonjwa saba,Kinondoni wagonjwa
wanne na Ilala ikiwa na mgonjwa mmoja
.
Haya yamezungumzwa na Mratibu wa Magonjwa
ya kuambukiza wa Jiji la Dar es salaam Bw. Alex Mkamba ofisini kwake
leo akielezea jinsi gani mkoa umefanikisha kupambana na kipindupindu kwa
kuzingatia usafi katika jiji.
Ameongeza kuwa katika kufanikisha mapambano
dhidi ya kipundupindu wametoa mafunzo juu ya mbinu shirikishi ya namna
ya kujikinga na kipindupindu kwa watendaji wa mitaa na pia imewahimiza
kukagua maeneo yao na kuwapa kibali cha kufunga maeneo ya biashara au
maeneo yatoayo huduma za chakula yasiyozingatia usafi.
Akielezea kuhusu huduma kwa wagonjwa wa
kipindupindu jijini Dar es salaam mratibu huyo amesema jiji lina dawa
za kutosha za kuhudumia wagojwa ipasavyo kwa kuwapatia huduma bora
zaidi kuendana na kasi ya maambukizi yaliyopo.
“ hata leo Shirika la Afya Duniani (WHO)
limetoa dawa za kusafishia maji (Water Guard) maboksi 45 kwa kila
wilaya” Mkamba alifafanua.
Aidha alisema serikali imejipanga katika
kudhibiti maambukizi mapya kwa kuwapima wagonjwa kabla na baada ya
kuruhusiwa kutoka hospitalini na aliwashauri wananchi kubadili tabia
kwa kuhakikisha usafi unafanyika pia kuchemsha maji na kuufanya usafi
kuwa ni tabia yao ya kila siku.
Mpaka sasa jumla ya watu 55 wamefariki dunia kwa ugonjwa wa kipindupindu jijini Dar es salaam.
WANANCHI WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIMA AFYA ZAO KUELEKEA DESEMBA MOSI, 2015.
Mwenyekiti
Mtendaji wa Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI nchini Tanzania Dkt.
Fatma Mrisho akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu Maadhimisho ya
Siku ya Ukimwi Duniani mwaka huu ambayo inaadhimishwa kwa kuwahimiza
wananchi kujitokeza kwa wingi kupima afya zao na kupata elimu ya
kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo.
……………………………………………………………………………………………
Na. Nyakongo Manyama- MAELEZO.
Dar es salaam.
Wito umetolewa kwa wananchi kote
nchini kuyatumia maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani ambayo
huadhimishwa kila ifikapo Desemba 1 ya kila mwaka kupima afya zao ili
kudhibiti maambukizi mapya ya VVU.
Akizungumza na waandishi wa Habari
leo jijini Dar es salaam Mwenyekiti Mtendaji wa Tume ya Taifa ya
Kudhibiti UKIMWI nchini Tanzania Dkt. Fatma Mrisho amesema Siku ya
Ukimwi Duniani nchini itaadhimishwa kwa kuwahimiza wananchi kujitokeza
kwa wingi kupima afya zao na kupata elimu ya kujikinga na maambukizi
ya ugonjwa huo.
Ameeleza kuwa maadhimisho ya
mwaka huu yataambatana na shughuli mbalimbali zikiwemo za Utoaji wa
Elimu ya Afya na Upimaji wa hiari wa VVU katika maeneo mbalimbali kote
nchini kupitia vituo vitakavyowekwa, Kufungua kituo cha maarifa cha
udhibiti UKIMWI eneo la Manyoni mkoani Singida ambayo ni njia kuu
kuelekea mikoa ya Kanda ya Ziwa na nchi za Jirani za Burundi na Rwanda.
Ameongeza kuwa Tume kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali itaendesha mikutano ya kitaalam kuhusu
UKIMWI, Zoezi la upimaji wa hiari wa VVU kwa wananchi, Kupokea tamko
litakalotolewa na Baraza la Watu wanaoishi na VVU pamoja na Uzinduzi wa
taarifa ya tathmini ya Sheria zinazotumika zinazohitaji kurekebishwa
zinazozuia malengo ya sifuri 3.
Aidha Tume itapokea taarifa ya
hali ya maambukizi ya VVU duniani itakayotolewa na Katibu Mkuu wa Umoja
wa Mataifa Ban Ki Moon kuhusu dunia na mapambano dhidi ya VVU.
Dkt. Fatma amefafanua kuwa mgeni
rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli ambapo pamoja na
mambo mengine atazindua Mfuko wa UKIMWI ambao utakuwa chachu ya
kupunguza maambukizi ya VVU nchini.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
ufuatiliaji na tathmini kuhusu UKIMWI wa TACAIDS Dkt.Jerome Kamwela
amesema kuwa kiwango cha maambukizi ya UKIMWI kwa mujibu wa takwimu za
mwaka 2011/2012 kimepungua na kufikia asilimia 5.3 huku mikoa ya nyanda
za juu kusini ya Njombe, Iringa na Mbeya ikiongoza kwa kuwa na
maambukizi zaidi na mikoa ya Manyara, Tanga na Lindi ikiwa na
maambukizi ya chini ya asilimia mbili.
Dkt. Kamwela amesema kuwa
maambukizi ya VVU ni mengi hasa kwa kundi la watu wenye umri wa miaka
19-24 huku makundi ya wanaojidunga, wanaume wanaofanya mapenzi ya jinsia
moja, wanawake wanaofanya biashara ya ngono yakiendelea kuwa katika
hatari ya kuathiriwa zaidi na maambukizi ya VVU.
WAZIRI MKUU ATAKA KILA MKURUGENZI ASOME HOTUBA YA RAIS, AIFANYIE KAZI
WAZIRI
MKUU Majaliwa Kassim Majaliwa amewataka wakurugenzi wa vitengo na wakuu
wa taasisi katika Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) wapate nakala ya
hansard ya hotuba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuzindua Bunge la
11, waisome na kufanyia kazi maeneo yote aliyoyaainisha.
“Katibu Mkuu hakikisha umepata
hansard ya hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati akizindua Bunge na
uhakikishe kila mkurugenzi ana nakala na kila mmoja wenu lazima
ahakikishe anafanyia maeneo ambayo Mheshimiwa Rais ameyaainisha. Ni
lazima tuelewane ni nini tunapaswa tufanye,” alisema.
Ametoa kauli hiyo leo mchana
(Jumanne, Novemba 24, 2015) wakati akizungumza na wakuu wa taasisi,
wakurugenzi na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) kwenye
mkutano uliofanyika ofisi ndogo ya TAMISEMI, barabara ya Kivukoni,
jijini Dar es Salaam.
“Ninatamani kuona mabadiliko ya
utendaji kazi Serikalini katika kipindi kifupi. Natamani kila mmoja
asiridhike na uzembe unaofanywa huku chini. Ni nyote ni wataalamu, kwa
hiyo mnapaswa kudhirisha elimu yenu na ujuzi mlionao,” aliwasisitizia
Wakurugenzi hao.
Alisema kila mkurugenzi na mkuu wa
taasisi anapaswa kuongeza usimamizi na ufuatiliaji wa kazi kwenye sekta
yake kwani hilo litasaidia kukidhi matarajio ya Watanzania ya kuona
mabadiliko ya utendaji kazi kwenye Serikali ya Awamu ya Tano. “Ninyi
wakurugenzi siyo desk officers bali ni field officers. Nataka muweke
utaratibu wa kwenda vijijini mkasimamie watu wenu, pia mhimize uadilifu,
uaminifu na weledi wa kazi,” alisisitiza.
“Mambo ninayotaka mhimize
watendaji waliopo chini yenu ni pamoja na haya yafuatayo: muda wa
kuripoti kazini uzingatiwe, muda wa kukaa kazini uzingatiwe, utokaji
kazini kwenda kwenye chai na chakula cha mchana udhibitiwe, na mipango
na malengo ya kazi kwa siku ni lazima yafikiwe,” alisema.
“Tunataka kujua mtumishi amefanya
nini tangu alipoingia ofisini. Suala siyo kukaa tu ofisini, kwani kuna
mtu anakaa ofisini, hajaenda hata kunywa chai lakini ukiuliza amefanya
nini hupati jibu la kueleweka. Sisi kama vongozi wao ni lazima tujue
wanafanya kazi gani wanapokuwa maofisini,” alisisitiza.
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu
Majaliwa ameitisha kikao ofisini kwake kesho saa 4 asubuhi akitaka
kupatiwa taarifa ni kwa nini mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART)
haujaanza kazi hadi sasa. “Kesho saa 4 asubuhi Katibu Mkuu, Mkurugenzi
Mkuu DART na watendaji wako mje ofisini. Nataka kupata maelezo ni kwa
nini mabasi hayajaanza kazi hadi leo, je ni lini yataanza kazi, je ni
nani anakwamisha. Na hata kama ni sheria, ni kwa nini tusiziharmonise
ili kuondoa hivyo vikwazo,?” alihoji Waziri Mkuu.
“Ninataka kupata haya maelezo kwa
sababu Watanzania na hasa wana-Dar es salaam, wamesubiri kwa muda kuona
mradi ukianza kazi ili uondoe kero ya usafiri. Wao wanajua anayehusika
ni TAMISEMI,” aliongeza.
Mapema, akimkaribisha Waziri Mkuu
kuzungumza na watumishi na viongozi wa TAMISEMI, Katibu Mkuu wa
OWM-TAMISEMI, Bw. Jumanne Sagini alimweleza baadhi ya mafanikio na
changamoto ambazo wizara hiyo imekabiliana nazo katika utendaji wake wa
kazi.
Kuhusu ujenzi wa vyumba vya
maabara kwa ajili ya kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi, Bw.
Sagini alisema vyumba hivyo vimeongezeka kutoka 247 mwaka 2005/2006 na
kufikia 6,161 mwaka 2014/2015. Pia alisema vyumba 4,228 viko kwenye
hatua za kukamilika ujenzi wake.
Kuhusu utengaji wa madirisha ya
kuhudumia makundi yenye msamaha kama wazee na watu wenye ulemavu
hospitalini na kwenye vituo vya afya, Katibu Mkuu alisema nayo
yameongezeka kutoka madirisha 5,074 mwaka 2010 na kufikia 7,903 mwaka
2014/2015 sawa na ongezeko la asilimia 55








No comments :
Post a Comment