Mwenyekiti
wa CCM Taifa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akisalimiana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye mara baada ya
kuwasili kwenye Makao Makuu ya Chama Ofisi Ndogo Lumumba.
Mwenyekiti
wa CCM Taifa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete
akiwa ofisini kwake Makao Makuu ya CCM Ofisi Ndogo Lumumba .
KAMATI YA STARS, YAWASHUKURU WATANZANIA
Mwenyekiti
wa Kamati Taifa Stars, Farouqh Baghozah amewashukuru watanzania kwa
michango yao waliyoitoa kuispaoti timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ katika
michezo ya kuwania kufuzu kwa Kombe la Dunia 2018 nchini Urusi dhidi ya
Algeria.
Farouqh alianza kwa kuwashukuru watanzania kwa kujitokeza kwa
wingi katika mechi ya Taifa Stars na Algeria na kuwashukuru pia wale
wote waliosafiri na timu hiyo ya Taifa, Taifa Stars kwenda Algeria
katika mechi ya marudiano.
Pia Mwenyekiti amechukua fursa
hiyo kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Makamu wa
Raisi Mama Samiha Suluhu, Raisi Mstaafu wa Awamu ya Nne, Mkuu wa Mkoa wa
Dar Es Salaam na Pwani na viongozi wote wa chama na serikali kwa njia
moja au nyingine katika kusapoti timu ya Taifa Taifa Stars kwenye Mchezo
na Algeria
Naye Mkuu wa mkoa Dar es salaa,
ambaye ni mlezi wa kamati hiyo, Mh Mecky Sadick aliwashukuru watu wote,
kuanzia wanakamati kwa jinsi walivyojitoa kwa muda wao wote katika
maandalizi na hasa kuhamasisha watanzania kujitokeza kwa wingi uwanjani
kuishangilia timu yao ya taifa kwa kuomnyesha uzalendo.
Kwa namna ya kipekee Mecky Sadick
amewashukuru watu wote na makampuni yaliyojitokeza katika kuchangia Timu
ya taifa wakiwemo Jubilee Insurance, Equity Bank, PPF, Serena Hotel,
GSM, bila kusahau vyombo vote vya habari ambavyo kwa namna moja au
nyingine waliweza kujitoa na kuhamasisha watanzania wajitokeze kwa wingi
uwanja wa taifa kuishangilia timu yao.
Katika mchakato mzima wa awali wa
mechi ya kufuzu kombe la dunia 2018, Kamati kupitia kwa wadau mbalimbali
iliweza kuchangisha pesa jumla ya milioni 122,640,000 za kitanzania,
dola za kimarekani 19,800 na 177,000 kutoka tigo pesa na airtel money.
Matumizi ni dola za kimarekani 70355, na milioni 47,904, 743 za kitanzania.
Mwisho kamati imewashukuru sana Watanzania na na kuwaomba wadumishe umoja wtue.. Nchi Yangu, Timu Yangu Taifa langu.
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAFANYA MKUTANO NA WADAU WA SEKTA YA MALIASILI NCHINI KUJADILI MAENDELEO YA SEKTA HIYO
Katibu
Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akitoa hotuba ya
ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Maliasili nchini leo tarehe 26
Novemba 2015 katika Ukumbi wa Chuo cha Utalii Kampasi ya Bustani Jijini
Dar es Salaam. Mkutano huo umeshirikisha wadau mbalimbali wakiwemo wa
Wizara zenye muelekeo wa Maliasili, Sekta binafsi, NGOs, Waandishi wa
habari na wadau wengine. Mada mbalimbali kutoka katika Sekta ndogo za
Wanyamapori, Misitu, Utalii, Mambo ya Kale na Uvuvi zimewasilishwa.
Baadhi ya Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa.
Katibu
Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru wa pili kulia
akiwa kwenye picha ya pamoja na balozi wa Ujerumani hapa nchini Mhe.
Egon Kochanke wa pili kushoto muda mfupi baada ya kufungua Mkutano huo.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Mkambusho ya Taifa Prof. Audax Mabula.
Katibu
Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Adelhelm Meru akihojiwa na
Mwandishi wa Habari wa Azam TV, Jamal Hashim muda mfupi baada ya
ufunguzi wa Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Maliasili nchini uliofanyika
leo tarehe 26 Novemba 2015 katika Ukumbi wa Chuo cha Maliasili Jijiji
Dar es Salaam. Mkutano huo umejadili mambo mbalimbali ikiwemo mafanikio,
changamoto na fursa zinazopatikana katika sekta hiyo muhimu
inayochangia kwa kiasi kikubwa katika pato la taifa. Miongoni mwa
changamoto kubwa alizozieleza Katibu Mkuu huyo ni Ujangili na Uharibifu
wa misitu jambo ambalo amesema Serikali na Wizara imejiapanga kupambana
nalo na kuwaomba wadau kushirikiana na Serikali katika vita hiyo.
Baadhi ya wadau walioshiriki Mkutano huo.
Mkurugenzi
wa Idara ya Mipango na Sera Bi. Mary Faini kutoka Wizara ya Maliasili
na Utalii akiwasilisha mada kuhusu Mafanikio, Changamoto na Fursa
zinazopatikana katika Sekta ya Maliasili nchini Tanzania.
Picha ya pamoja.
(Picha na Hamza Temba – Wizara ya Maliasili na Utalii)
DC AAGIZA MUUGUZI ALIYEKAMATWA KWA WIZI WA DAWA SHINYANGA ASIMAMISHWE KAZI MARA MOJ
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro amefanya ziara ya kushtukiza katika kituo cha afya Kambarage mjini Shinyanga ili kujionea hali halisi jinsi huduma zinavyotolewa kwa wananchi siku moja tu baada ya muuguzi wa kituo hicho kukamatwa kwa tuhuma ya kuiba dawa za serikali.Pichani ni mkuu wa wilaya Josephine Matiro na katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga wakiwa katika chumba cha kuhifadhia dawa wakiwa wamepigwa butwaa baada ya kuona chumba kimesheheni dawa wakati mara kwa mara wananchi wamekuwa wakiambiwa hakuna dawa badala yake wanaambiwa wakanunue kwenye maduka ya watu binafsi mtaani-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blogHapa ni ndani ya ofisi ya mganga mkuu/msimamizi wa kituo hicho ambapo mkuu wa wilaya akiwa ameambatana na maafisa wengine wa manispaa ya Shinyanga amekutana na uongozi wa kituo hicho pamoja na wananchi waliomkamata muuguzi mkunga wa kituo hicho Joseph Nkila akituhumiwa kuiba dawa za serikali.Kulia ni Rashid Shaban akimweleza mkuu huyo wa wilaya jinsi walivyofanikisha kufichua wizi huo
Wa pili kutoka kulia ni msimamizi wa kituo cha afya Kambarage Dkt Nassoro Yahya akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga kuhusu suala la upungufu wa dawa katika kituo chake ambapo alisema kituo kina upungufu wa dawa na walishatoa taarifa panapohusika siku nyingi zilizopita.Hata hivyo maelezo yake yalipingana na yale ya kaimu mganga mkuu wa manispaa ya Shinyanga Dkt Mhana Raphael(mwenye suti pichani) aliyedai kuwa mkoa wa Shinyanga hauna tatizo la upungufu wa dawa bali dawa pekee ambayo haipo ni ile ya Antibiotic
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza katika kituo cha afya cha Kambarage mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine amemwagiza mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga kumsimamisha kazi muuguzi Joseph Nkila anayetuhumiwa kuiba dawa za serikali pamoja na msimamizi wa kituo hicho Dkt Nassoro Yahya kwa uzembe unaosababisha mwanya wa upotevu wa dawa katika kituo hicho na kusababisha wananchi kuilalamikia serikali kwa kukosa dawa wakati mkoa wa Shinyanga hauna tatizo la dawa
Mfamasia/mtunza dawa wa kituo cha afya Kambarage Seleman Hamza akitoa maelezo namna anavyofanya kazi katika kituo hicho ambayo hata hivyo mkuu wa wilaya hakuridhika nayo na kumwagiza yeye na msimamizi wa kituo waandae maelezo ya kina ndani ya siku 5
Mmoja wa wasamaria wema waliomkamata muuguzi anayedaiwa kuiba dawa akisimulia jinsi wizi wa dawa unavyofanyika katika kituo hicho na jinsi walivyomkamata Joseph Nkila.Soma hapa Maelezo yake na wenzake
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akiwa katika kituo cha afya Kambarage,nyuma yake ni katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniface Chambi na kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Sande Deogratius
Dawa zikiwa katika chumba cha kuhifadhia dawa cha Kituo
Mfamasia/mtunza dawa wa kituo cha afya Kambarage Seleman Hamza akizungumzia kuhusu tukio la wizi wa dawa katika kituo hicho na changamoto ya dawa katika kituo hicho ambapo alisisitiza kuwa kuna baadhi ya dawa hazipo katika kituo hicho
Dawa zikiwa katika chumba cha kuhifadhia dawa kituo cha afya Kambarage
Dawa katika kituo cha afya Kambarage
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro na katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniface Chambi wakiwa katika chumba cha kuhifadhia dawa
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoka kwenye kituo cha afya Kambarage
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akitoa maelekezo kwa kaimu mganga mkuu wa manispaa ya Shinyanga Dkt Mhana Raphael(mwenye suti),kaimu mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga Sande Deogratius na mfamasia wa manispaa ya Shinyanga Emmanuel Zabron
Mkuu wa wilaya Josephine Matiro akimpa maelekezo kaimu mganga mkuu wa manispaa ya Shinyanga Dkt Mhana-Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog









No comments :
Post a Comment