Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akiwahutubia wananchi wa mji wa Njombe katika mkutano wake wa
kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Sabasaba wa CCM mjini humo, Dr.
Magufuli amewaomba wananchi hao kumpa kura za ndiyo huku akiahidi
kuboresha mambo mbalimbali katika serikali yake ikiwemo Elimu, Kilimo,
Viwanda.
Ameongeza kwamba watu wengi
watajiuliza na kusema hizi ni siasa fedha atapata wapi? ” Mimi si
mwanasiasa ila ni mtendaji zaidi na ninajua mianya inayopoteza fedha za
serikali nipeni kazi nikazibe mianya hiyo” Amesema wakuu wa idara
mbalimbali za serikali wajiandae na kujiweka sawa kabla hajaapishwa
kwani hatavumilia uzembe kazini, Wizi na Ufisadi huku akiahidi kuanzisha
mahakama maalum itakayoshughulikia kesi za ufisadi na ubadhirifu wa
mali za serikalini ili watuhumiwa wahukumiwe haraka.
Uchaguzi mkuu wa jamhuri ya
muungano ya Tanzania wa Rais , Wabunge na Madiwani unatarajiwa
kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu nchini Kote. (PICHA NA JOHN
BUKUKU-FULLSHANGWE-NJOMBE)
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akisisitiza jambo wakati akihutubia katika mkutano huo.
Umati uliohudhuria katika mkutano huo.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Mzee
Philip Mangula akimnadi Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akipunga mkono kwa pamoja na wananchi waliohudhuria katika
mkutano wake wa kampeni mjini Njombe leo.
Wananchi wakipunga mikono yao
juu kama ishara ya kumkubali Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya
Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli.
Mgombea ubunge wa jimbo la Njombe
Kusini: Edward Mwalongo akijinadi mbele ya Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli.
Mabasi maalum yaliyopambwa picha za Dr. John {ombe Magufuli.
Mlemavu huyu ambaye jina lake halikupatikana mara moja alikuwa ni miongozi mwa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.
Mgombea ubunge wa jimbo la Kyela
mkoani Mbeya Dr. Harrison Mwakyembe akimnadi Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Njombe katika
uwanja wa Nanenane.
Shilole akikamu jukwaani kaazi kwelikweli.
Kada wa CCM aliyekuwa mjumbe wa bunge maalum la Katiba akizungumza na wananchi katika mkutano wa kampeni mjini Njombe leo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya Mh. Temba akifanya vitu vyake jukwaani.
Chege naye amekonga nyoyo za wananchi waliohudhuria katika mkutano huo.
Mama Martina Jonas wa Njombe
akiwa na watoto wake ambao ni watumishi wa CCM kulia Edward Mpogolo na
kushoto Rodrick Mpogolo wakati alipohudhuria katika mkutano wa kampeni
wa CCM mjini Njombe
Vijana waendesha Bodaboda wakipiga vuvuzela wakimshangilia Dr. John Pombe Magufuli.
Wana CCM wakishangilia.
Msafara wa Mgombea Urais wa
jamhuri ya Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr.
John Pombe Magufuli ukiwasili kwenye uwanja wa Nanenane.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akizungumza na wananchi wakati akiwa njiani
kuelekeamjini Njombe kwa ajili mkutano wa kampeni.
Akina mama wakimpokea kwa matawi ya miti huku wakicheza ngoma.
Wananchi wakimpokea kwa mabando yenye kumsifu Dr. John Pombe Magufuli.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Njombe Magharibi katika
kijiji cha Ilovi Wanging’ombe.
Vikongwe hawa ambao majina yao
hayakufahamika wanaonekana wakijadili jambo wakati wa mkutano wa kampeni
wa Dr. John Pombe Magufuli katika kijiji cha Ilovi Wanging’ombe.
Wananchi hawa wakifurahia hotuba
ya Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama
Mapinduzi CCM Dr. John Pombe Magufuli alipokuwa akiwahutubia katika
kijiji cha Ilovi Wanging’ombe mkoani Njombe.
Hawa wakifuatilia mkutano huo.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akilimiana na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Mzee Philip
Mangula.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akisalimiana na mmoja wa mwananchi katika kata ya Tandala
mkoani Njombe
Mwenyekiti wa Shirikisho la vyama vya Watu wenye ulemavu Tanzania ( SHIVYAWATA)
Amon Anastaz Mpanju akisalimia wakazi wa Iwawa kwenye mkutano wa
Kampeni za CCM uliofanyika stendi ya Mabehewani Makete.
Huu ni ujumbe wa wananchi wa Makete walioutoa kwa jia ya mabango kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Iwawa Makete.
Wananchi wakishangilia huku wakiwa wameshikilia vipeperushi vyenye picha ya Dr. John Pombe Magufuli.
Mgombea Urais wa jamhuri ya
Muungano ya Tanzania Kupitia Chama Chama Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akisalimiana na Kada wa CCM na mjumbe wa kamati kuu Mh. Pindi
Chana katikati ni Mgombea ubunge wa jimbo la Makete Bw. Norman Sigala.
Mgombea Mwenza MAMA SAMIA ATINGA SINGIDA LEO
Umati
wa wananchi ukimsikiliza Mgombea Mwenza kwa tiketi ya CCM, Mama Samia
Suluhu alipohutubia mkutano wa kampeni katika eneo la Msange, Singida
Kaskazini, leo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, akiwahutubia wananchi katika mkutano huo leo
Umati
wa wananchi ukimsikiliza Mgombea ubunge wa jimbo la Singida Kaskazini,
Lazaro Nyalandu, alipohutubia katika mkutano wa kampeni wa mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, katika eneo la Msange,
Singida Kaskazini, leo.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan
akimnadi Mgombea Ubunge Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, katika
mkutano uliofanyika katika jimbo hilo leo.
Baadhi
ya viongozi na wananchi wakijimwayamwaya kwa furaha wakati wa mkutano
wa kampeni wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia
Suluhu Hassan
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan
akiwasalimiabaadhi ya viongozi, baada ya kuwasili katika mkutano wa
kampeni uliofanyika katika jimbo hilo leo.
Wananchi
waliojawa na furaha wakimkimbilia kumlaki, Mgombea Mwenza wa Urais kwa
tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu, alipowasili kwenye mkutano wa hadhara
uliofanyika leo, katika viwanja vya Kyengege, Iramba mkoani Singida leo
“Baba
hakimbii nyumba” Kijana akiwa na bango linalowasema wanaaokimbia
kutoka CCM kwenda upinzani kutokana na kutochaguliwa katika nafasi za
uongozi, kijana huyo alipokuwa kwenye mkutano wa Mgombea Mwenza wa Urais
kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu, uliofanyika leo Iramba mkoani
Singida.
Mgombea
Ubunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba akiselebuka na baadhi ya
viongozi na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika leo, katika
eneo la Kyengege, Iramba mkoani Singida, leo.
Mgombea
Ubunge jimbo la Iramba Magharibu, Mwigulu Nchemba akiomba kura, wakati
wa mkutano wa kampeni za CCM wa mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya
CCM, uliofanyika leo katika jimbo hilo.
Wananchi
wakimsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia
wakati wa mkutano wa kampeni za CCM wa mgombea Mwenza huyo, uliofanyika
leo katika jimbo hilo.
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimnadi
Mgombea Ubunge jimbo la Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba katika mkutano
uliofanyika katika jimbo hilo leo. Kushoto ni Mgombea wa Ubunge jimbo
la Mkalamo, Allan Kiula
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimnadi
Mgombea Ubunge jimbo la Mkalamo, Allan Kiula, katika mkutano uliofanyika
katika jimbo hilo leo.
Wananchi
wakiwa kwenye mkutano wa kampeni, wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi
ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan uliofanyika leo, kwenye Ofisi ya CCM
mkoa wa Singida. Picha na Bashir Nkoromo).
KARUMA MWENYEKITI MPYA WA TWFA
Uchaguzi wa Chama cha Mpira wa
Miguu nchini (TWFA) umemalizika ambapo Amina Karuma amechaguliwa kuwa
mwenyekiti mpya wa chama hicho, kufuatia uchaguzi uliofanyika leo jijini
Dar es salaam.
Nafasi ya katibu msaidizi
imekwenda kwa mwandishi wa habari za michezo Someo Ng’itu, na nafasi ya
wajumbe wa kamati ya utendaji ya TFWA imekwenda kwa Debora Mkemwa na
Theresia Mng’ongo.
Mgeni rasmi katika uchaguzo huo
alikuwa ni katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine ambapo na uchaguzi
ulisimamiwa na Kamati ya Uchaguzi ya TWFA chini ya uangalizi wa Jeremia
Wambura kutoka kamati ya Uchaguzi ya TFF.
TFF inawapongeza viongozi wapya
waliochaguliwa na kuwatakia kila la kheri katika majukumu hayo mapya, na
kuahidi kuendelea kushirikiana nao katika maendeleo ya mpira wa miguu
ya wanawake nchini.
BANK OF AFRIKA TANZANIA YAKUSANYA ZAIDI YA MILIONI 210 KUSAIDIA MATIBABU YA WOTOTO WANAOZALIWA NA MIGUU ILIYOPINDA
Mkurugenzi
Mkuu wa Bank of Africa nchini Bw. Ammishadai Owusu-Amoah akimkabidhi
Ofisa Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT mfano wa hundi wenye ya dola
za kimarekani 100,000 kwa ajili ya matibabu ya watoto wanaozaliwa na
miguu iliyopinda. Nyuma ni Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Ali
Hassani Mwinyi na Mwenyekiti wa Bodi ya Bank of Afrika Mwanaidi Majaar.
Balozi
Mwanaidi Majaar,Mwenyekiti wa Bodi Bank of Afrika akihutubia wadau
mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo. Balazo anasema BOA wamejizatiti
kurudisha kwa jamii wanayoihudumia na harambee ya kutibu watoto
wanaozaliwa na miguu iliyopinda ni moja ya mafanikia ya taratibu wao.
Matembezi
ya hisani ya pamoja yaliyoandaliwa na BOA na CCBRT hospitali kutoka
Leaders clup mpaka CCBRT kuadhimisha kilele cha uchangiaji wa fedha kwa
ajili ya matibabu ya watoto wanaozaliwa na miguu iliyopinda.
Rais
Mstaafu wa awamu ya pili Mh. Ali Hasssan Mwinyi akihutibia na kupongeza
kwa dhati juhudi zilizofanya na zinazoendelea kufanywa na Bank of
Africa kwa kujali jamii na kuhusia wadau wengine pia kuiga mfano wa BOA
Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mh. Ali Hasssan Mwinyi akimsalimia mtoto aliyeshiriki katika matembezi hayo.
Matembezi ya hisani
kuadhimisha kilele cha ukusanyaji fedha yakiendelea kueleka hospital ya
CCBRT
kuadhimisha kilele cha ukusanyaji fedha yakiendelea kueleka hospital ya
CCBRT
…………………………………………..
NA FRANCIS DANDE
RAIS wa Awamu ya Pili, Ali Hssan Mwinyi, jana
aliongoza matembezi ya hisani ya
kilometa tatu kutoka Leaders Club, Kinondoni hadi Hospitali ya CCBRT Msasani
kwa ajili ya kuchangia matibabu ya
watoto waliopinda miguu.
aliongoza matembezi ya hisani ya
kilometa tatu kutoka Leaders Club, Kinondoni hadi Hospitali ya CCBRT Msasani
kwa ajili ya kuchangia matibabu ya
watoto waliopinda miguu.
Matembezi hayo yaliyodhaminiawa na Benki ya Afrika – Tanzania, lengo kuu
lilikuwa ni kukusanya dola za marekani laki moja kwa madhumuni ya kugharamia
watoto wenye miguu iliyopinda nchini kote. Ilikuwa ni kilele cha kampeni
ya ukusanyaji wa dola za Marekani laki moja
iliyozinduliwa mwezi Aprili mwaka huu.
lilikuwa ni kukusanya dola za marekani laki moja kwa madhumuni ya kugharamia
watoto wenye miguu iliyopinda nchini kote. Ilikuwa ni kilele cha kampeni
ya ukusanyaji wa dola za Marekani laki moja
iliyozinduliwa mwezi Aprili mwaka huu.
Kupatikana kwa fedha hizo kutawezesha CCBRT kutoa matibabu ya gharama nafuu kwa
watoto 400 wenye ugonjwa wa kupinda miguu
nchini kote,ilikuyabadili maisha yao na kuwa
ya kawaida.
watoto 400 wenye ugonjwa wa kupinda miguu
nchini kote,ilikuyabadili maisha yao na kuwa
ya kawaida.
Akizungumzia kuhusu tukio hilo jana,Mwenyekiti wa Bodi ya
Wakurugenzi ya Benki ya Afrika –
Tanzania, Mwanaidi Maajar, alisema: “Benki ya Afrika – Tanzania imedhamiria
kurejesha kwa jamii kile inachopata kwa kuwa inaendesha shughuli
zake, kwa kuchangia mahitaji mbalimbali ya jamii husika. Tumeona umhimu
wa kuhimiza usaidizi katika suala hili
jema, kwa kuwa CCBRT inatoahuduma kawa
jamii maskini kwa kuondoa vikwazo mbalimbali ili jamii husika iweze kupata
matibabu,” alisema Mwanaidi .
Wakurugenzi ya Benki ya Afrika –
Tanzania, Mwanaidi Maajar, alisema: “Benki ya Afrika – Tanzania imedhamiria
kurejesha kwa jamii kile inachopata kwa kuwa inaendesha shughuli
zake, kwa kuchangia mahitaji mbalimbali ya jamii husika. Tumeona umhimu
wa kuhimiza usaidizi katika suala hili
jema, kwa kuwa CCBRT inatoahuduma kawa
jamii maskini kwa kuondoa vikwazo mbalimbali ili jamii husika iweze kupata
matibabu,” alisema Mwanaidi .
Aidha , Ofisa Mendaji mkuu wa CCBRT,Erwin Telemans alisisitiza:
“ CCBRT inatoa shukrani za pekee kwa
Benki ya Afrika –Tanzania kutokana na ukarimu wao katika kipindi
chote cha kampeni hii. Maisha ya a mamia ya
watoto wenye ugonjwa wa kupinda miguu watapona kwa uhakika kutokana na
matibabu watakayopatiwa na CCBRT, na hatutaweza kuya badili maisha ya watoto hao bila kupata msaada kutoka kwa washirika wetu
wakarimu kama Benki ya Afrika – Tanzania.”
“ CCBRT inatoa shukrani za pekee kwa
Benki ya Afrika –Tanzania kutokana na ukarimu wao katika kipindi
chote cha kampeni hii. Maisha ya a mamia ya
watoto wenye ugonjwa wa kupinda miguu watapona kwa uhakika kutokana na
matibabu watakayopatiwa na CCBRT, na hatutaweza kuya badili maisha ya watoto hao bila kupata msaada kutoka kwa washirika wetu
wakarimu kama Benki ya Afrika – Tanzania.”
Rose Mhando athibitisha Tamasha la kuombea Amani katika kuelekea uchaguzi mkuu
…………………………………..
MWIMBAJI wa muziki wa injili Rose
Mhando amethibitisha rasmi kushiriki katika Tamasha kubwa la kihistoria
la kuiombea Amani nchi kuelekea uchaguzi mkuu linarotarajia kufanyika
Oktoba 4 kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaa kabla ya kwenda
mikoani.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa
maandalizi ya tamasha hilo Alex Msama, alisema Mhando tayari
amethibitisha kuimba siku hiyo, ambako tayari ameshaanza maandalizi
ikiwa pamoja na nyimbo mpya ambazo ni maalumu kwa ajili ya kuhamasisha
amani.
Msama alisema kuwa maandalizi ya
tamasha hilo la kihistoria yanaendelea vizuri ikiwa pamoja na waimbaji
kujiandaa vizuri watakuwepo waimbaji kutoka nchi zaidi ya tano kuungana
na watanzania katika tukio hilo ambalo litashirikisha matukio
mbalimbali.
Aidha Msama alisema kuwa mbali ya
kuliombea taifa amani kuelekea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Alisema kuwa waimbaji wengine
wanaendelea kuthibitisha ambapo pia mbali ya kuimba mmojammoja wataimba
wimbo wa pamoja ambao umeandaliwa, hivyo Msama aliwaomba watanzania
kujitokeza katika tukio hilo muhimu la kitaifa.
Naye Mjumbe wa Kamati ya
maandalizi ya tamasha hilo, Beno John Chelele alisema tamasha hilo ni la
muhimu hasa katika kipindi hiki cha uhaguzi ambao umekuwa wa tofauti
na chaguzi zilizowahi kufanyika miaka ya nyuma.
“Kila Mtanzania ashiriki
tuliombee taifa letu kokote litakakopita tamasha hili ni la muhimu hasa
katika wakati huu wa uchaguzi ambao ni wa aina yake,” alisema Beno.
Tamasha hilo litanzia mkoa wa Dar
es Salaam Oktoba 4, Morogoro Oktoba 7, Iringa 9,Mbeya Oktoba 11, Dodoma
Oktoba 14, Shinyanga Oktoba 16 na kumaliziwa na Mwanza Oktoba 18.
MABALOZI WAZUNGUMZA NA Dk.Ali Mohamed Shein.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti
wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi
Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uholanzi Irene Florence
Mkwama alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais leo.
[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi Mteule
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Uholanzi Irene Florence Mkwama
alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kumuaga Rais leo,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi Mpya wa
Jamhuri ya watu wa Algeria Belabed Saad alipofika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha rasmi kwa Rais leo,
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akizungumza na Balozi Mpya wa
Jamhuri ya watu wa Algeria Belabed Saad alipofika Ikulu Mjini Zanzibar
kujitambulisha rasmi kwa Rais leo.
UZINDUZI WA TAMASHA LA KUOMBEA AMANI TAIFA KUELEKEA UCHAGUZI MKUU KUFANYIKA OKTOBA 4, 2015 UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM
Mkurugenzi
wa Kampuni ya Msama Promotion, waandaaji wa matamasha mbalimbali kama
lile la Krismas na Pasaka, Alex Msama (kulia), akizungumza katika
mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo asubuhi
kuhusu uzinduzi wa Tamasha la kuliombea Taifa kuelekea ucahguzi Mkuu
utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu utakaofanyika Oktoba 4, 2015 Uwanja
wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mjumbe wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Benno Chilele (kushoto), akizungumza katika tamasha hilo. Kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion, waandaaji wa Tamasha la Krismas na Pasaka, Alex Msama.
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua taarifa hiyo.
BUNGE LA WATOTO OYSTERBAY SHULE YA MSINGI MKOANI MANYARA WAFANIKIWA KUWARUDISHA WATOTO WA MITAANI SHULE
| Abdallah Waziri, Asia Mtibua na Mwalimu Gaudensia Igoshalimo wakimkaribisha Abdallah Waziri shuleni. |
| Mmoja wa wajumbe akitoa maoni yake katika kikao cha bunge katika shule ya oysterbay mkoani manyara |
| Mbunge Nasri Selemani akifuatilia hoja kwa makini.wakati kikao cha bunge la watoto likiendelea katika shule ya oysterbay mkoani manyara |
Mbunge
Nasri Selemani ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa nyumbani na sasa kwa
jitihada za bunge amerudishwa shuleni,,akichangia hoja.
| Mtangazaji wa Kipindi cha Tafakari Time Benedicta Mrema akizungumza na Abdallah Waziri na kumkabidhi mchango wa shilingi 57,800 aliochangiwa kwa ajili ya kumuwezesha mahitaji ya shule. |
| Raisi wa Bunge la watoto Oysterbay, Manyara – Sarah David akitoa hotuba ya ufunguzi wa bunge la watoto katika shule ya oysterbay mkoani manyara |
| Wabumbe wa Bunge la watoto Oysterbay Manyara akishangilia hoja. |
| Wajumbe a Bunge la watoto Oysterbay Manyara akishangilia hoja. |
| Waliosimama, Abdallah Waziri, Asia Mtibua na Mwalimu Gaudensia Igoshalimo wakimkaribisha Abdallah Waziri shuleni. |
Mtandao
wa Marafiki wa Elimu Babati (BADENET) ulianzishwa mwaka 2012 chini ya
uongozi wa Asia Mtibua, mtandao huu ulianzishwa kwa lengo la kuhamasisha
jamii kushiriki katika shughuli za elimu pamoja na kuanzisha kituo cha
kupashana habari.
Moja
ya mafanikio ya BADENET ni kuanzishwa kwa Bunge la Watoto katika shule
ya msingi Osterbay mkoani Manyara. Bunge hili lilianzishwa kwa lengo la
kuwaleta pamoja watoto waliopo shuleni na ambao wapo nje ya shule ili
waweze kujadili masuala ya elimu ikiwa ni pamoja na kutafuta njia za
kuweza kusikilizwa wao kama watoto. Bunge hili la watoto linajumuisha
wajumbe 43 (26 wasichana na 17 wavulana) na hukutana mara 1 kwa kila
mwezi. Mpaka sasa jumla ya watoto wa mitaani 19 wamerudishwa shuleni na
wanasoma, wapo wanaoingia asubuhi na wengine mchana.
Leo
hii Bunge la watoto Oysterbay mkoani Manyara limekutana kwa lengo la
kujadili changamoto zinazowakabili watoto wa mitaani “Chokoraa” ili
kuzungumza namna ambavyo watawawezesha watoto hao kupata fursa ya elimu
kama watoto wengine waliopo shuleni. Katika kikao cha leo bunge
limefanikiwa kumrudisha shuleni mtoto Abdala Waziri ambapo alichangiwa
na wabunge, marafiki wa elimu na walimu jumla ya shilingi 57,800 ili
zimuwezeshe kununua mahitaji muhimu ya shule.
Mkakati
wa bunge la watoto katika shule ya msingi Osterbay ni kuhakikisha kuwa
kila mbunge anamrudisha shuleni mtoto yoyote ambaye yuko mtaani na
kuhakikisha wanafurahia fursa ya kupata elimu ambayo ni haki yao ya
msingi.
Timu
ya Tafakari Time, kipindi kinachorushwa kila siku ya alhamisi kupitia
ITV ilishiriki kikao cha leo kwa lengo la kujifunza uendeshwaji wa
shughuli za bunge hili la watoto.
Ofisi ya Madini Mtwara kutoa leseni za madini ndani ya siku moja
Mtaalam kutoka Kitengo cha Leseni,
Wizara ya Nishati na Madini, Charles Gombe akielezea hatua za Wizara
katika kuboresha huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online
Mining Cadastre Transactional Portal; OMCTP) kwa wachimbaji wa madini
(hawapo pichani) mjini Mtwara. Lengo la mafunzo hayo lilikuwa ni kuwapa
uelewa wachimbaji wa madini kuhusu huduma hiyo pamoja na kuwasajili.
Baadhi ya wachimbaji wadogo
wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa na
wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini (hawapo pichani)
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini
Kanda ya Kusini, Aidan Mhando akifungua mafunzo kuhusu huduma za leseni
za madini kwa njia ya mtandao yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini
kutoka katika mkoa wa Mtwara.
Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji
wa Madini kutoka Mkoa wa Mtwara (MTWAREMA), Festo Balegele akifafanua
jambo katika mafunzo hayo.
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini
Kanda ya Kusini, Aidan Mhando ( wa pili kutoka kushoto, waliokaa mbele)
akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo.
Mtaalam kutoka Mfuko wa Hifadhi ya
Jamii (NSSF) Mtwara, Juma Namuna akielezea umuhimu wa wachimbaji wa
madini kujiunga na mfuko huo ili kunufaika kwa kupata mikopo.
Mtaalam kutoka Kitengo cha Leseni,
Wizara ya Nishati na Madini, Pendo Elisha akielezea faida za kujiunga
na huduma ya leseni za madini kwa njia ya mtandao katika mafunzo hayo.
Mchimbaji mdogo wa madini ya chumvi, Hussen Abdalah akichangia mada kwenye mafunzo hayo.
Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini
Kanda ya Kusini, Aidan Mhando ( wa nne kutoka kushoto, waliokaa mbele)
akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini
na wachimbaji wa madini kutoka Lindi walioshiriki mafunzo ya huduma ya
leseni za madini kwa njia ya mtandao yaliyofanyika mjini Lindi.
…………………………………………..
Na Greyson Mwase, Mtwara
Ofisi ya Madini, Kanda ya Kusini
yenye ofisi zake mjini Mtwara imeanza kutoa huduma za leseni za
utafutaji na uchimbaji wa madini ndani ya siku moja tofauti na
ilivyokuwa awali.
Hayo yalisemwa na Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Aidan Mhando katika mafunzo kuhusu huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal; OMCTP) yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini mkoani Mtwara.
Mhando alisema kuwa awali maombi yalikuwa yakichukua muda mrefu kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya mtandao na kuongeza kuwa ofisi yake imeboresha mtandao na kuanza kutoa leseni ndani ya siku moja.
Alisema ofisi yake ina uwezo wa kushughulikia ombi moja la leseni ndani ya nusu saa iwapo mwombaji atakuwa amekamilisha vigezo vyote vinavyotakiwa.
Alieleza kuwa tangu huduma ya mtandao iboreshwe ofisi ya madini imekuwa na uwezo wa kushughulikia maombi 20 kwa siku tofauti na awali ambapo ilikuwa inachukua muda mrefu.
Akielezea mikakati ya ofisi yake katika utekelezaji wa mfumo mpya wa utoaji wa huduma za leseni kwa njia ya mtandao, Mhando alisema ofisi imejipanga kwa zoezi la kuhakikisha kuwa wateja wake wote wanaingizwa katika mfumo huu na kunufaika na huduma hiyo
Aliongeza kuwa ili kuwafikia wachimbaji wa madini ya chumvi ambao idadi yako kubwa ni wazee, ofisi yake imeweka utaratibu wa kuwatembelea kwenye maeneo yao ya kazi, kuwapa elimu pamoja na kuwasajili kwenye mfumo huu.
Akielezea faida za mfumo mpya wa huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao Mhando alisema kuwa mfumo utawawezesha wamiliki wa leseni za madini kupata taarifa za leseni zao wakati wowote pamoja na kufanya malipo ya leseni zao kwa njia ya mtandao yaani M-Pesa, Airtel Money na Tigo Pesa
“Mfumo huu utapunguza migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara kati ya wachimbaji na kuondoa dhana ya kwamba kuna upendeleo kwenye utoaji wa leseni za madini.” Alisema Mhando.
Hayo yalisemwa na Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini Kanda ya Kusini, Aidan Mhando katika mafunzo kuhusu huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao (Online Mining Cadastre Transactional Portal; OMCTP) yaliyoshirikisha wachimbaji wa madini mkoani Mtwara.
Mhando alisema kuwa awali maombi yalikuwa yakichukua muda mrefu kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya mtandao na kuongeza kuwa ofisi yake imeboresha mtandao na kuanza kutoa leseni ndani ya siku moja.
Alisema ofisi yake ina uwezo wa kushughulikia ombi moja la leseni ndani ya nusu saa iwapo mwombaji atakuwa amekamilisha vigezo vyote vinavyotakiwa.
Alieleza kuwa tangu huduma ya mtandao iboreshwe ofisi ya madini imekuwa na uwezo wa kushughulikia maombi 20 kwa siku tofauti na awali ambapo ilikuwa inachukua muda mrefu.
Akielezea mikakati ya ofisi yake katika utekelezaji wa mfumo mpya wa utoaji wa huduma za leseni kwa njia ya mtandao, Mhando alisema ofisi imejipanga kwa zoezi la kuhakikisha kuwa wateja wake wote wanaingizwa katika mfumo huu na kunufaika na huduma hiyo
Aliongeza kuwa ili kuwafikia wachimbaji wa madini ya chumvi ambao idadi yako kubwa ni wazee, ofisi yake imeweka utaratibu wa kuwatembelea kwenye maeneo yao ya kazi, kuwapa elimu pamoja na kuwasajili kwenye mfumo huu.
Akielezea faida za mfumo mpya wa huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao Mhando alisema kuwa mfumo utawawezesha wamiliki wa leseni za madini kupata taarifa za leseni zao wakati wowote pamoja na kufanya malipo ya leseni zao kwa njia ya mtandao yaani M-Pesa, Airtel Money na Tigo Pesa
“Mfumo huu utapunguza migogoro ambayo imekuwa ikijitokeza mara kwa mara kati ya wachimbaji na kuondoa dhana ya kwamba kuna upendeleo kwenye utoaji wa leseni za madini.” Alisema Mhando.
Rais Kikwete azindua Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao
Wasanii wa Filamu nchini Wema
Sepetu na Steven Nyerere wakimkaribisha Mwenyekiti wa CCM Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete katika Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini
Dar es Salaam kuzindua Kampeni ya Mama Ongea na Mwanao illi aipigie kura
CCM.Kampeni hiyo imeratibiwa na Wasanii wa filamu wakuongozwa Wema
Sepetu na Steven Nyerere.
Msanii wa Filamu Bi.Wema Sepetu
akimkabidhi Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete tuzo maalum kwa kutambua
mchango wake katika kulinda na kuthamini kazi za wasanii nchini ambapo
katika kipindi chake cha uongozi wamepata manufaa makubwa.Wema
alikabidhi tuzo hiyo kwa niaba ya baadhi wasanii wa filamu na Muziki
nchini wanaoshiriki katika kampeni ya Mama Ongea na Mwanao yenye lengo
la kuwahimiza wanawake kuwahimiza watu kuipigia kura CCM kwa kuwachagua
wagombea wake katika uchaguzi mkuu mwaka huu.

Mwenyekiti wa CCM Rais
Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Kampeni ya
Mama Ongea na Mwanao.(picha na Freddy Maro)
MAGUFULI AMJULIA HALI NA KUMPA POLE MEYA WA JIJI LA MBEYA MH ATHANAS KAPINGA BAADA YA KUPATA AJALI
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akimjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni,Mh Kapunga amelazwa kwenye chumba maalum cha wagonjwa mahututi
(ICU) katika hospitali ya Rufaa mjini humo.
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akimjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni,Mh Kapunga amelazwa kwenye chumba maalum cha wagonjwa mahututi
(ICU) katika hospitali ya Rufaa mjini humo.
Mmoja
wa Wauguzi walioko kwenye chumba maalum cha wagonjwa mahututi
(ICU),akimpa maelezo mafupi Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli
alipokwenda kumjulia hali n kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya
Mh.Athanas Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa
mbio za maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya Wauguzi walioko katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya,mara baada ya kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya Wauguzi walioko katika chumba maalum cha wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali ya Rufaa Mbeya,mara baada ya kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli
akisalimiana na Mke wa Meya Mama Kapinga mara baada ya kutoka
kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi (CCM),Ndugu John Pombe Magufuli
akisalimiana na Mke wa Meya Mama Kapinga mara baada ya kutoka
kumjulia hali na kumpa pole aliyekuwa Meya wa jiji la Mbeya Mh.Athanas
Kapunga aliyepata ajali wilayani Momba mkoani Mbeya wakati wa mbio za
maandalizi ya Kampeni hivi karibuni.
PICHA NA MICHUZI JR-MBEYA
DK, FAUSTINE NDUGULILE AKIHUTUBIA MKUTANO VIJIBWENI
Mgombea Ubunge Jimbo la Kigamboni kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)
DK.Faustine Ndugulile akihutubia Mkutano wa kampeni uliofanyika katika
Uwanja wa Mzimu Kata Vijibweni Kigamboni Dar es Sallam (PICHA ZOTE NA
KHAMISI MUSSA).
Wananchi wakifurahia alipokuwa akipanda jukwaani Mgombe ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi CCM DK.Faustine Ndugulile
Wananchi wakimsikiliza kwa makini Mgombea
Mwenyekiti
wa CCM Wilaya ya Temeke na Mjumbe Halmashauri kuu Mkoa, Yahaya
Sikunjema (kulia) akimkabidhi Ilani ya Chama hicho Mgombea nafasi ya
Udiwani kupitia Chama hicho Zacharia Mkundi katika mkutano wa kampeni
ulio fanyika Kata ya Vijibweni Dar es Sallam
Rais Kikwete akutana Alpha Konare Mjumbe wa AU Sudan ya Kusini
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akimkaribisha na kufanya mazungumzo na Mhe.Alpha Oumar Konare ambaye ni
msuluhishi wa Umoja wa Afrika(AU) katika mgogoro wa Sudan ya Kusini
ikulu jijini Dar es Salaam jana.Mbali na majadiliano yaliyohusu vita vya
wenyewe kwa wenyewe katika taifa changa la Sudan ya Kusini Bwana Konare
ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Mali(1992-2002) na mwenyekiti mstaafu wa
Kamisheni ya Umoja wa Afrika alimweleza Rais Kikwete umuhimu wa kutumia
Kiswahili katika mikutano ya Umoja wa Afrika.(picha na Freddy Maro)
Rais Kikwete amjulia hali Bwana Charles Kizigha
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete
akimjulia hali mwandishi wa habari Mkongwe wa magazeti ya Serikali ya
Daily News na Sunday News Bwana Charles Kizigha nyumbani kwake Mbezi
Beach jijini Dar es Salaam jana jioni.Aliyesimama kulia ni mtoto wa
mwandishi huyo wa habari Mhe.Angela Kizigha ambaye ni Mbunge wa Afrika
Mashariki.Rais Kikwete alimtembelea Bwana Kizigha nyumbani kwake baada
ya kupata taarifa kuwa ni mgonjwa(picha na Freddy Maro)
WAANDISHI HABARI WA ZANZIBAR WAPATIWA MBINU BORA ZA KURIPOTI HABARI ZA UCHAGUZI MKUU.
Mwandishi Mkongwe wa Tasnia ya
Habari Tanzania ambae pia ni Mkurugenzi wa Internews Tanzania Valerie N.
Msoka akifafanua kitu kwa wandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa
mafunzo ya kuwajengea uwezo juu ya kuripoti uchaguzi Mkuu.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
Mkurugenzi wa Shirika la Internews
kanda ya Afrika Ian Noble akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa Habari juu
ya kuripoti habari za Uchaguzi, alipotembelea katika mafunzo hayo huko
ukumbi wa watu wenye ulemavu Kikwajuni Weles Mjini Zanzibar.
Afisa Mwandamizi Baraza la Habari
Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said Hassan (aliesimama)akifahamisha
kitu katika mafunzo ya siku tano yalimaliza jana Agosti
28 yaliyoandaliwa na Shirika la Habari la Marekani Internews kwa
waandishi wa Habari wa Zanzibar katika Ukumbi wa Umoja wa watu wenye
Ulemavu Kikwajuni Mjini Zanzibar. Picha na Makame Mshenga-Maelezo
Zanzibar.
Badhi ya waandishi wa habari
walioshiriki mafunzo juu ya kuripoti Habari za Uchaguzi Mkuu
wakisikiliza nasaha zilizotolewa na Mkurugenzi wa Internews Tanzania
Valerie N. Msoka (hayupo pichani) katika mfunzo yaliofanyika Ukumbi wa
Umoja wa watu wenye ulemavu Kikwajuni Mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Shirika la Internews
kanda ya Afrika Ian Noble (wakatikati) katika picha ya pamoja na
washiriki na wasimamizi wa mafunzo hayo (kulia) aliekaa ni Afisa
Mwandamizi Baraza la Habari Tanzania Ofisi ya Zanzibar Shifaa Said
Hassan na kushoto ni Mwandishi Mkongwe wa Tasnia ya Habari
Zanzibar Salim Said Salim.Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.
sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali mpya ya Abdalla Mzee
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa hutuba yake kwa Wananchi
jana wakati sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Hospitali
mpya ya Abdalla Mzee iliyopo Mkoani Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba akiwa
katika ziara ya Moahuo kufungua miradi ya maendeleo.
,[Picha na Ikulu.]
Waziri wa Afya Rashid Suleiman
akisalimiana na Wananchi wakati wa Sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi
ujenzi mpya wa Hospitali ya Abdalla Mzee pia kumkaribisha Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein kutoa
hutuba yake katikasherehe hiyo jana,
Balozi Mdogo wa China nchini Tanzania
anayeishi Zanzibar Xie Yunliang akitoa salamu zake kwa wananchi na
Viongozi wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi Ujenzi mpya wa
Hospitali ya Abdalla Mzee inayojengwa na Kampuni kutoka China Mkoani
Mkoa wa Kusini Pemba wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipoweka jiwe la msingi katika ziara
ya kufungua miradi ya maendeleo.
Baadhi ya wananchi wa Mji na Vitoji vya
Wilaya ya Mkoani Kusini Pemba wakiwa katika sherehe za Uwekaji wa jiwe
la Msingi wa ujenzi mpya wa Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani inayojengwa
na kampuni kutoka China jiwe hilo lililowekwa na Rais wa Zanzibar na
Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein jana.
Wanawake Wamlilia Maji Mgombea Mwenza wa CCM
Mgombea mwenza wa CCM nafasi ya
urais, Bi. Samia Suluhu akiwasikiliza akinamama wakimuelezea kero ya
maji baada ya kumsimamisha na kumpa kero hizo Jimboni Longido.
Wakinamama wilayani Longido
wakiendelea kuteka maji kwa zamu baada ya kumaliza kumueleza kero zao
Bi. Samia Suluhu aliepita maeneo hayo.
Baadhi ya wanaCCM na wananchi wa
Jimbo la Monduli wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
nafasi ya urais wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
Baadhi ya wanaCCM na wananchi wa
Jimbo la Monduli wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
nafasi ya urais wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
Baadhi ya wanaCCM na wananchi wa
Jimbo la Monduli wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
nafasi ya urais wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
Mgombea mwenza wa CCM nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu akiwa katika vazi la kimasai alilopewa kama zawadi na wanaMonduli.
Baadhi ya wajumbe wa kamati ya kampeni ya CCM taifa wakiwa katika mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza Bi. Suluhu.
Baadhi ya wanaCCM na wananchi wa
Jimbo la Monduli wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
nafasi ya urais wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
Bi. Samia Suluhu akimnadi mgombea ujumbe wa Jimbo la Monduli, Bi. Namelok Sokoine (kushoto) kwenye mkutano wa hadhara.
Baadhi ya wanaCCM na wananchi wa
Jimbo la Monduli wakiwa kwenye mkutano wa hadhara wa mgombea mwenza
nafasi ya urais wa CCM, Bi. Samia Suluhu.
……………………………………………
Na Joachim Mushi, Longido
WANAWAKE wa Wilayani Longido
wamemsimamisha mgombea Mwenza wa urais Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bi.
Samia Suluhu njiani akielekea jukaani kuhutubia wananchi wakimlilia
kuwatatulia kero ya maji katika Kata ya Longido ambapo kila familia
imekuwa ikipata huduma hiyo mara moja kwa wiki hali ambayo wamesema
haikidhi mahitaji.
Bi. Samia alilazimika kusimama
eneo ambalo wanawake walikuwa wamefurika wakichota maji kwa zamu huku
kila familia ikipewa idadi ya ndoo kumi mara moja kwa kila wiki kiwango
ambacho akinamama wengi walisema akikidhi mahitaji kwa familia zao.
Mgombea huyo wa CCM
aliwahakikishia akinamama hao kuwa yeye kama mwanamke anajua shida ya
maji inavyowatesa akinamama katika familia ikiwa huduma hiyo inapokuwa
tatizo katika upatikanaji wake, hivyo atalisimamia suala hilo. Alisema
Serikali ya CCM itakapoingia madarakani imetenga shilingi bilioni 13 kwa
ajili ya kupeleka maji eneo la Longido mradi ambao utamaliza kero ya
maji eneo hilo.
Akizungumza katika mkutano wa
hadhara Longido Bi. Suluhu alisema kwa kuwawezesha wafugaji wa eneo hilo
wamepanga kujenga mabwawa ya kuvuna na kuhifadhi maji kwa ajili ya
matumizi ya nyakati za ukame kwa baadhi ya maeneo, ikiwa ni pamoja na
kujenga majosho ya mifugo na kuwezesha madawa ya mifugo kwa wafugaji ili
kuwaendeleza.
“…Kazi hii tutaifanya ndani ya
kipindi kifupi mara tu baada ya kufanikiwa kurudi madarakani, Serikali
inayomaliza muda wake imefanya mengi na sisi tutaendeleza na kuboresha
zaidi. Alisema wanajua kilio cha mahakama katika wilaya ya Longido hivyo
mara baada ya kuingia madarakani wataijenga.
Alisema akiwa njiani katika
mikutano ya kampeni zake ameshuhudia uwepo wa ukame katika vijiji lakini
anawahakikishia hakuna mwananchi ambaye atakufa na njaa endapo hali
hiyo ya ukame itaendelea, kwani serikali ya CCM katika ghala la chakula
ina akiba ya kutosha.
Mgombea huyo mwenza wa CCM pia
alifanya mkutano wa hadhara katika Jimbo Monduli aliwaomba wanaMonduli
kumpigia kura ya ndio mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Pombe
Magufuli ili aweze kutekeleza ilani ya chama hicho ambayo pia
imejumuisha ujenzi wa barabara ya Sanya Juu hadi Longido na Longido hadi
Mto wa Mbu wilayani Longido.
Aliwaomba wanaMonduli kumchagua
mgombea ubungw wa Jimbo la Monduli kwa tiketi ya CCM, Bi. Namelok
Sokoine kwani mgombea huyo anarekodi na historia nzuri ya utendaji kama
alivyokuwa babayake marehemu, Edward Moringe Sokoine. Aliwaomba pia
kuwachagua madiwani wa CCM ili waweze kufanya kazi kwa ushirikiano kama
timu.
MAMA SAMIA AHUTUBIA LEO MBULU NA BABATI
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia
umati wa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo, kwenye
Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani Manyara.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan
akihutubia umati wa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo,
kwenye Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani Manyara.
Mgombea ubunge jimbo la Mbulu Vijijini, kwa tiketi ya CCM, Fraten
Maasai, akiomba kura baada ya kutambulishwa na Mgombea Mwenza wa Urais
kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni
uliofanyika leo, kwenye Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani
Manyara.
Umati
wa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa
Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, leo kwenye Uwanja wa mikutano wa
Mbulu mjini mkoani Manyara.
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan
alipokuwa akiingia kwenye mkutano wake wa kampeni uliofanyika leo,
kwenye Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani Manyara.
Kijana akionysha bango la kumfagilia Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi
ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan, kwenye mkutano wa kampeni za CCM za
Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan
uliofanyika leo, kwenye Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani
Manyara.
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia
umati wa wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo, kwenye
Uwanja wa mikutano wa Mbulu mjini mkoani Manyara.
Mgombe
mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia akimsalimia kijana
Augustine Male, mwenye ulemavu, ambaye alihudhuria mkutano wa kampeni wa
mgombea mwenza huyo, leo Mbulu Mjini.
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia, akimnadi mgombea Ubunge
jimbo la Karatu, kwa tiketi ya CCM, Wilbard Lorri, wakati wa mkutano wa
kampeni uliofanyika leo katika kijiji cha Mbulumbulu katika jimbo hilo.
Mwananchi akiwa na mabango ya kuwafagilia mgombea Urais kwa tiketi ya
CCM, Dk. John Magufuli na Mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,
Mama Samia, wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika leo, Mbulu mjini.
Wananchi katika Kijiji cha Mbulumbulu, wakimshangilia Mgombea Mwenza wa
Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan alipowasili kufanya
mkutano wa kampeni katika eneo hilo leo
Kina mama wakimzawadia mavazi, Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya
CCM, Mama Samia, baada ya kuhutubia mkutano wa kampeni katika kijiji cha
Mbulumbulu, wilayani Karatu, mkoani Arusha.
Wananchi
wakiwa wamezuia msafara wa mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,
katika eneo la Karatu mjini, Mama Samia ambapo alilazimika kuwasalimia,
wakati akiwa njiani kwenda Mbulu leo
Mgombea
Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia akiwasalimia wananchi
waliosubiri msafara wake kkwenye makutano ya mkoa wa Arusha na Manyara,
wakati akitoka Arusha kuingia Manyara
Wananchi
wakiwa wamezuia msafara wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM,
Mama Samia Suluhu Hassan katika eneo la Magugu, wilayani Bbati mkoani
Manyara leo.
PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO
MBUNGE WA LUDEWA DEO FILIKUNJOMBE APINGWA KUPITA BILA KUPINGWA MCHAKATO WA UCHAGUZI MKUU
Mgombea
Ubunge Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Msambichaka Mkinga (kushoto), akizungumza katika mkutano na
waandishi wa habari Dar es Salaam leo asubuhi, wakati akipinga
kupitishwa bila kupingwa mgombea mwenzake wa jimbo hilo kupitia Chama
Cha Mapinduzi (CCM), Deo Filikunjombe na kudai kulikuwa na hujuma. Kulia
ni Wakili wake, Paulo Kalomo.
Mgombea
Ubunge Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Msambichaka Mkinga, akionesha fomu namba 10 ambazo alikabidhi
kwa Msimamizi wa Uchaguzi.
Wakili wake, Paulo Kalomo, akizungumza katika mkutano huo kuhusu sheria inavyoelekeza.
Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.
……………………………………………………
Na Dotto Mwaibale
MGOMBEA
Ubunge wa Jimbo la Ludewa kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Msambichaka Mkinga amepinga vikali kupitishwa bila kupingwa
mgombea mwenzake wa jimbo hilo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Deo
Filikunjombe na kudai kulikuwa na hujuma.
Mkinga
alitoa malalamiko hayo mbele ya waandishi wa habari Dar es Salaam leo
asubuhi na kueleleza kuwa sababu zilizotolewa na msimamizi wa uchaguzi
wa jimbo hilo kuwa hakupeleka fomu namba 10 hazikuwa na ukweli wowote.
“Nilipofika
ofisi ya msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Ludewa nilisaini na kukabidhi
tamko la kuheshimu na kutekeleza maadili ya uchaguzi ya mwaka 2015 (fomu
namba 10) na baada ya kusaini nilimkabidhi msimamizi wa uchaguzi pamoja
na fomu namba 8B,picha, stakabadhi ya malipo ya dhamana ambapo
vilihakikiwa na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi, Gervas Lupembe” alisema
Mkinga.
Mkinga
alisema katika jambo lisilo la kawaida msimamizi wa uchaguzi wa jimbo
hilo hilo hakubandika kwenye ubao wa matangazo tamko hilo na alipomfuata
msimamizi huyo kumuulizia msaidizi wake Lupembe alikiri kupokea na
kuziwasilisha kwa kiongozi wake ili kutia saini ambaye naye alikiri
kuzipokea lakini wakati ana bandika tamko hilo la Mgombea wa CCM fomu
hiyo hakuiona.
Alisema
katika pingamizi alilowekewa dai mojawapo ni kutokuwepo tamko hilo
kwenye fomu zake hali inayoonesha wazi kuwa kulikuwa na mchezo mchafu
uliofanyika ili kumpitisha Filikunjombe bila kupingwa.
Mkinga
alisema kuwa kuwaondoa wagombea kwa sababu zisizo za msingi ni kuiminya
demokrasia na kuirudisha nchi nyuma kwani kunaweza kusababisha kukosa
viongozi wazuri na kubakia na viongozi wasiofaa na wasiotaka
kushindanishwa kwa kuwapa nafasi wananchi ya kumchagua kiongozi
wanayemtaka.
Mgombea
huyo alisema kutokana na sintofahamu hiyo alimuomba msimami wa uchaguzi
wa jimbo hilo kutupiliambali pingamizi lililotolewa dhidi yake na
mgombea mwenzake ambapo anasubiri majibu baada ya kuandika barua ya
malalamiko.
WHO YATOA DAWA ZA MILIONI 42.2 ILI KUPAMBANA NA KIPINDUPINDU NCHINI.
Picha na Ally Daud
…………………………………………………
Na Ally daud-Maelezo
Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii imepokea msaada wa dawa
za kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu nchini kutoka
Shirika la Afya Duniani zenye thamani ya shilingi milioni 42.2.
Msaada huo umepokelewa leo jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Nchini Dkt. Donan Mmbando.
Akizungumza mada baada ya kupata msaada huo amesema dawa
hizo ambazo ni katoni 1000 za water guard, lita 100 za Cresol Saponated
zitasaidia kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo.
Naye mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani(WHO) nchini
Tanzania Dkt.. Rufaro Chatora amesema kuwa ni wajibu wao kusaidia
kupamabana na maambukizi ya ugonjwa huo ili kuhakikisha unatokomea
nchini.
Ameongeza kuwa ni jukumu la wananchi la kupambana na
maambukizi ya ugonjwa huo kwa kudhibiti hali ya usafi kuanzia mwili ,
chakula na mazingira yanayowazunguka kwa ujumla.
Dkt. Chatora amesema kuwa ni vema wananchi wakapigwa
marufuku kuuza vyakula sehemu za kampeni ili kupunguza maambukizi ya
ugonjwa huo.
Aidha , Mwakilishi huyo wa WHO amesema kuwa Shirika lake
litatoa msaada wa shilingi milioni 159.8 kwa ajili ya kusaidia kampeni
ya kuzuia ugonjwa wa KipindupinduNchini .
TWIGA KUFUNGA DIMBA NA IVORY COAST
Twiga Stars iliyoweka kambi
kisiwani Zanzibar kwa takribani mwezi mmoja sasa, itacheza mchezo wake
pili Septemba 9, dhidi ya Nigeria kabla ya kumalizia mchezo wake wa
mwisho hatua ya makundi dhidi ya wenyeji Congo-Brazzavile Septemba 12,
2105.
Jumla ya timu nane za Wanawake
kutoka Barania Afrika zinashirki fainali hizo ambazo ni Nchi za Afrika
Kusini, Cameroon, Ghana, Misri (wamejitoa) kundi B, na wenyeji
Congo-Brazzavile, Ivory Coast, Nigeria na Tanzania kutoka kundi A.
Timu mbili za juu kutoka kila kundi zitafuzu kwa hatua ya nusu fainali.
A Fraudster Suspect in Dar ES SALAAM Court
Wadau wa Maendeleo ya Viwanda Watangaza vyema Fursa za Uwekezaji nchini
Naibu katibu mtendaji kutoka Ofisi
ya Rais Tume ya Mipango anayesimamia klasta ya Miundombinu na huduma,
mhandisi Happiness Mgalula akitoa hotuba katika mkutano uliowahusisha
ujumbe wa wadau wa maendeleo ya viwanda kutoka Tanzania na ujumbe wa
wawekezaji kutoka nchini China.
Wajumbe wa mkutano wakiwa wanasikiliza kinachoendelea ndani ya mkutano wa wadau wa maendeleo ya viwanda.
Wajumbe wa mkutano wakiwa wanasoma kwa makini baadhi ya nyaraka katika mkutano huo.
Picha ya pamoja kati ya wadau wa maendeleo ya viwanda kutoka Tanzania na ujumbe wa wawekezaji kutoka nchini China.
…………………………………………………..
Na Adili Mhina.
Wadau wa maendeleo ya viwanda
nchini wametumia vyema fursa ya kutangaza na kuwashawishi wawekezaji wa
kigeni kutoka nchini China kuwekeza katika maeneo muhimu yatakayohimiza
maendeleo ya viwanda na kupunguza umaskini miongoni mwa wananchi.
Hayo yametokea katika mkutano wa
siku mbili mfululizo kati ya wadu wa maendeleo ya viwanda kutoka
serikalini, sekta binafsi nchini pamoja na ujumbe wa wawekezaji kutoka
nchini China uliomalizika jana. Mkutano huo ulioandaliwa na kituo cha
kimataifa cha kupunguza umaskini cha nchini China, Mfuko wa maendeleo wa
China-Afrika kwa kushirikiana na kituo cha uwekezaji Tanzania na Ofisi
ya Rais, Tume ya Mipango ulibeba ujumbe usemao, “punguza umaskini
kupitia maendeleo ya viwanda”.
Katika hotuba yake kwa niaba ya
katibu mtendaji wa Ofisi ya Rais Tume ya mipango, naibu katibu mtendaji
anayesimamia klasta ya miundo mbinu na huduma mhandisi Hapness Mgalula
alisema Mkutano huo umekuja wakati muafaka ambapo Tanzania ipo katika
maandalizi ya kuandaa mpango wa maendeleo wa miaka mitano
(2016/17-2020/21) ambao umebeba dhima ya kuendeleza uchumi wa viwanda.
“mkutano huu sio kwamba tu umekuja wakati muafaka lakini pia ni muhimu
kwa sababu miongoni mwa yatakayojadiliwa hapa yatatumika katika
kuboresha huo mpango”, alisema Mgalula.
Kwa upande wake mkurugenzi
mtendaji wa kituo cha uwekezaji Tanzania (TIC), bi Juliet Kairuki
aliueleza ujumbe kutoka China kuwa kuwa Tanzania kuna maeneo mbali mbali
ya uwekezaji ambayo yanaweza kuleta tija kubwa kwa Taifa pamoja na
wawekezaji. Alisisitiza zaidi kwa wawekezaji hao kuwekeza katika
kujenga viwanda nchini ili kuondokana na usafirishaji bidhaa ghafi
kwenda nchi za nje. Miongoni mwa maeneo aliyoyawekea msisitizo katika
uwekezaji wa ujenzi wa viwanda ni pamoja na; ubanguaji wa korosho,
usindikaji wa mbegu za mafuta, utengenezaji wa nguo, ngozi, utengenezaji
wa nyama bora na maziwa.
Alisisitiza kuwa pamoja na kuwa
uwekezaji wa ujenzi wa viwanda katika maeneo hayo utasaidia kukuza
ajira kwa wanachi vilevile utasaidia kuongeza thamani ya bidhaa
zinazotoka nchini kwenda kuuzwa nchi za nje. “kwa sasa bidhaa nyingi
zinauzwa zikiwa ghafi na hii inafanya kuuza bidhaa bei ya chini wakati
kama tukifanikiwa kujenga viwanda na kuuza bidhaa za viwandani thamani
ya mazao yetu itaongezeka na italeta faida upande wa serikali na
vilevile kwa muwekezaji,”.
Nae mkurugenzi wa viwanda kutoka
wizara ya viwanda na biashara mhandisi Elli Palangyo aliwahakikishia
wawekezaji kuwa Tanzania ni sehemu salama kwa uwekezaji hivyo yeyote
anayekuja kuwekeza ajue kuwa yupo katika eneo salama na lenye tija
kibiashara. Alieleza kuwa Tanzania ina faida nyingi za kuwavutia
wawekezaji ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa amani na utulivu wa taifa toka
kipindi cha uhuru, uwepo wa maliasili za kutosha kama vile madini na
gesi asilia, upatikanaji wa ardhi ya kutosha na yenye rutuba kwa ajili
ya kilimo, kuwepo kwa bahari inayotumika kupitisha bidhaa mbalimbali
hususani kwenye nchi zisizo na bahari, na zingine nyingi.
Kwa upande wa Zanziabar Mkurugenzi
wa uwekezaji kutoka mamlaka ya uwekezaji vitega uchumi Zanzibar (ZIP)
Nasriya Nassor alieleza wadau kuwa Zanzibar ina fursa mbalimbali za
uwekezaji katika sekta za utalii, uvuvi, kilimo pamoja na maeneo mengine
kama huduma za kifedha, usafirishaji, nishati pamoja na huduma
mbalimbali za jamii.
Wawekezaji hao kutoka nchini China
walionesha kuridhishwa na uwepo wa fursa mbalimbali zilizopo nchini na
kueleza kuwa katika kutimiza azma ya kupunguza umaskini kupitia
maendeleo ya viwanda Tanzania, China ina jukumu kubwa hususani katika
kutoa mawazo, uzoefu, elimu, fursa na kuwekeza katika maeneo mbalimbali
ya Tanzania.
DR. JOHN POMBE MAGUFULI ATIKISA JIJI LA MBEYA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akiwahutubia maelfu ya wananchi wa mkoa wa Mbeya katika mkutano
wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Nzovwe jijini Mbeya huku
akiwaambia wananchi hao kwamba anawaomba kura za ndiyo ili aweze kuingia
Ikulu kuwatumikia watanzania wote bila kujali itikadi zao za vyama,
ukabila, Dini wala ukanda.
Akisisitiza kauli yake Dr.
Magufuli amesema nipeni kazi kwani mimi sio mwanasiasa bali ni mtendaji,
mkweli na Mchapakazi yaani “Hapa Kazi Tu”(PICHA NA JOHN
BUKUKU-FULLSHANGWE-MBEYA)
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akisisitiza jambo wakati alipokuwa akihutubia katika mkutano
huo
Mwigulu Nchemba akimpigia debe Mh. John Pombe Magufuli katika mkutano huo.
Mgombea ubunge jimbo la Kyela Mh. Dr. Harrison Mwakyembe akihutubia katika mkutano huo.
Kada wa CCM Bw. Richard Kasesela akimpigia Debe Dr. John Pombe Magufuli.
Maelfu ya wananchi wakipunga mkono kama ishara ya kumkubali Dr. John Pombe Magufuli.
Msami msanii wa muziki wa kizazi kipya akitumbuiza katika mkutano huo.
Msanii Matonya akifanya vitu vyake jukwaani.
Msanii Sheta akikamua.
Shilole naye amekamua vya kutosha katika mkutano huo.
Baadhi ya wana CCM wakiwa wameshikilia mabango yenye picha za Dr. John Pombe Magufuli.
Wanamuziki wa bendi ya TOT wakifanya vitu vyao jukwaani.
Jamaa huyu naye akitoa burudani ili mradi CCM Mbele kwa mbele.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akipuga mkono kwa wananchi mara baada ya kuwasili kwenye
uwnanja wa Nzovwe tayari kwa mkutano wake wa kampeni.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akiwaaga wananchi mara baada ya kuwahutubia mjini Mbeya leo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akitembea kwa miguu na wananchi mara baada ya kushuka kwenye
gari lake wakati alipokuwa akiondoka katika uwanja wa mkutano mjini
Mbeya.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akiwanadi wagombea udiwani wa Mbeya mjini.
Mjumbe wa Kamati Kuu CCM Ndugu William Lukuvi kushoto , Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mh. Abas Kandoro katikati na Mwigulu Nchemba.
Baadhi ya wana CCM wakifuatilia mkutano huo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya
Muungano ya Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dr. John Pombe
Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Mbeya mjini Bw. Sambwee
Shitambala kwenye mkutano wa kampeni iliofanyika kwenye viwanja vya
Nzovwe jijini Mbeya.
NHC YATILIANA SAINI YA MAKUBALIANO YA MIKOPO YA NYUMBA NA BENKI NNE ZA HAPA NCHINI
Tayari
NHC inafanya kazi na benki kumi na mbili ambazo ni Azania Bank, Bank of
Africa, Bank ABC, Commercial Bank of Africa, CRDB Bank, Dar es Salaam
Community Bank, Exim Bank, KCB Bank, National Bank of Commerce, NIC
Bank, National Microfinance Bank na Stanbic Bank.
PICHA ZOTE ZA KITENGO CHA MAWASILIANO NA HUDUMA KWA JAMII CHA NHC.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi akizungumza
katika hafla ya utiaji saini iliyofanyika Hyatt Regency, The Kilimanjaro
Hotel, Dar-es-Salaam leo asubuhi. Leo NHC imetiliana rasmi saini na
benki na taasisi za Diamond Trust Bank Tanzania Limited, Equity Bank
Tanzania Limited, First National Bank Tanzania Limited, International
Commercial Bank Tanzania Limited.
Tayari
NHC inafanya kazi na benki kumi na mbili ambazo ni Azania Bank, Bank of
Africa, Bank ABC, Commercial Bank of Africa, CRDB Bank, Dar es Salaam
Community Bank, Exim Bank, KCB Bank, National Bank of Commerce, NIC
Bank, National Microfinance Bank na Stanbic Bank.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Taasisi ya mikopo ya nyumba ya Tanzania Mortgage Refinance
(TMRC), Oscar Mgaya akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya NHC na
mabenki manne iliyofanyika Hyatt Regency, The Kilimanjaro Hotel,
Dar-es-Salaam leo asubuhi.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa,Felix Maagi pamoja
na Mwakilishi wa benki ya Diamond Trust Bank Tanzania
Limited wakitiliana saini ya makubaliano kuwezesha kutoa mikopo ya
Nyumba kwa wananchi hapa nchini.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa,Felix Maagi akipena mkono
na Mwakilishi wa benki ya Diamond Trust Bank Tanzania
Limited mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano.hayo.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa , Felix Maagi pamoja na
Meneja Mkuu wa Mikopo wa Equity Bank wakitiliana saini ya makubaliano
kuwezesha kutoa mikopo ya Nyumba kwa wananchi hapa nchini.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania,Felix Maagi akipena mkono
na Meneja Mkuu wa Mikopo wa Equity Bank mara baada ya kutiliana saini
ya makubaliano hayo.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi pamoja na
Mkuu Huduma za Wateja wa Benki ya First National Bank Tanzania Limited,
Francois Bank wakitiliana saini ya makubaliano kuwezesha kutoa mikopo ya
Nyumba kwa wananchi hapa nchini.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania,Felix Maagi akipena mkono
na Mkuu Huduma za Wateja wa Benki ya First National Bank Tanzania
Limited, Francois Bank mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano
hayo.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi pamoja na
Mwakilishi wa International Commercial Bank Tanzania
Limited wakitiliana saini ya makubaliano kuwezesha kutoa mikopo ya
Nyumba kwa wananchi hapa nchini.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi akipena
mkono na Mwakilishi wa International Commercial Bank Tanzania
Limited mara baada ya kutiliana saini ya makubaliano hayo.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi akiwa katika
picha ya pamoja na wawakilishi wa benki nne zilizoingia mkataba na NHC.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Felix Maagi akiwa katika
picha ya pamoja na wawakilishi wa benki nne zilizoingia mkataba na NHC.
Kaimu
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania,Felix Maagi akijadiliana
jambo na Mkuu Huduma za Wateja wa Benki ya First National Bank Tanzania
Limited, Francois Bank kabla ya kutiliana saini ya makubaliano hayo.
Wafanyakazi wa Shirika la Nyumba la Taifa wakifuatilia utiaji saini huo uliofanyika leo asubuhi jijini Dar es Salaam.
TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
JESHI LA POLISI TANZANIA.
“PRESS RELEASE
• MTU MMOJA ANAYEDHANIWA KUWA NI MHALIFU AFARIKI DUNIA KWA KUPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI.
• MTEMBEA KWA MIGUU AFARIKI DUNIA B AADA YA KUGONGWA NA GARI WILAYANI RUNGWE.
• JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WAWILI KWA KUCHANA BENDERA YA CHAMA NA KUBANDUA BANGO LA MGOMBEA.
• JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATATU WAKIWA NA DAWA YA KULEVYA [BHANGI].
• JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATATU WAKIWA NA DAWA YA KULEVYA [BHANGI].
KATIKA TUKIO LA KWANZA:
MTU MMOJA ANAYEDHANIWA KUWA NI MHALIFU ALIYEFAHAMIKA KWA JINA MOJA LA ATHUMANI ALIJERUHIWA KWA KUPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI WALIOKUWA DORIA ENEO MLIMA NYOKA NJE KIDOGO NA JIJI LA MBEYA NA KUFARIKI DUNIA MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA MATIBABU.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 22:30 USIKU HUKO ENEO LA MLIMA NYOKA, KATA YA ITEWE, TARAFA YA TEMBELA, WILAYA YA MBEYA VIJIJINI, MKOA WA MBEYA.
UCHUGUZI UNAFANYIKA KUPATA UKWELI WA SABABU ZILIZOPELEKEA MAUAJI HAYO, KWANI ZIPO TAARIFA ZINAZODAI KUWA MAREHEMU NA WENZAKE WATATU NI BODABODA NA WALIKUWA WAKISINDIKIZA LORI LILILOKUWA LIMEBEBA SHABA BILA KUWASILIANA NA ASKARI WALIOKUWA DORIA ENEO HILO AMBALO UWA NA MATUKIO YA UHALIFU YA MARA KWA MARA.
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. ASKARI POLISI WALIOKUWA KWENYE ENEO LA TUKIO PAMOJA NA WALIOSHUHUDIA TUKIO HILO WANAHOJIWA KUPATA UKWELI. UPELELEZI UNAENDELEA.
MTU MMOJA ANAYEDHANIWA KUWA NI MHALIFU ALIYEFAHAMIKA KWA JINA MOJA LA ATHUMANI ALIJERUHIWA KWA KUPIGWA RISASI NA ASKARI POLISI WALIOKUWA DORIA ENEO MLIMA NYOKA NJE KIDOGO NA JIJI LA MBEYA NA KUFARIKI DUNIA MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA KWA MATIBABU.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 22:30 USIKU HUKO ENEO LA MLIMA NYOKA, KATA YA ITEWE, TARAFA YA TEMBELA, WILAYA YA MBEYA VIJIJINI, MKOA WA MBEYA.
UCHUGUZI UNAFANYIKA KUPATA UKWELI WA SABABU ZILIZOPELEKEA MAUAJI HAYO, KWANI ZIPO TAARIFA ZINAZODAI KUWA MAREHEMU NA WENZAKE WATATU NI BODABODA NA WALIKUWA WAKISINDIKIZA LORI LILILOKUWA LIMEBEBA SHABA BILA KUWASILIANA NA ASKARI WALIOKUWA DORIA ENEO HILO AMBALO UWA NA MATUKIO YA UHALIFU YA MARA KWA MARA.
MWILI WA MAREHEMU UMEHIFADHIWA KATIKA HOSPITALI YA RUFAA MBEYA. ASKARI POLISI WALIOKUWA KWENYE ENEO LA TUKIO PAMOJA NA WALIOSHUHUDIA TUKIO HILO WANAHOJIWA KUPATA UKWELI. UPELELEZI UNAENDELEA.
KATIKA TUKIO LA PILI:
MTEMBEA KWA MIGUU ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA AMBINISYE MWANDOBO (65) MKAZI WA KISEGESE ALIFARIKI DUNIA MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALI YA MISSION ITETE KWA MATIBABU BAADA YA KUGONGWA NA PIKIPIKI ISIYOFAHAMIKA IKIENDESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA.
AJALI HIYO IMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 15:00 ALASIRI HUKO KATIKA KIJIJI CHA KISEGESE, KATA YA KISEGESE, TARAFA YA PAKATI, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. MTUHUMIWA ALIKIMBIA NA PIKIPIKI MARA BAADA YA AJALI. UPELELEZI UNAENDELEA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA MOTO KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO HIVYO IKIWA NI PAMOJA NA KUZINGATIA SHERIA/KANUNI/ALAMA NA MICHORO YA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
KATIKA TUKIO LA TATU:
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA AMANI JOHN @ MWAKASEGE KWA KOSA LA KUHARIBU MALI [KUCHANA PICHA] YA MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 14:30 MCHANA HUKO ILOMBA, KATA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MTUHUMIWA ALIONEKANA AKIWA AMEBEBA MABANGO YA PICHA ZA MGOMBEA WA URAIS HUKU YAKIWA YAMECHANWA VIPANDE VIPANDE NA NDIPO JITIHADA ZA KUMKAMATA ZILIFANYIKA NA KUMFIKISHA KATIKA KITUO KIDOGO CHA POLISI ILOMBA.
AIDHA KATIKA TUKIO JINGINE, MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FADI MWASHIMAHA ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA KOSA LA KUHARIBU MALI [KUCHANA BENDERA YA CHAMA CHA MAPINDUZI].
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 12:00 MCHANA HUKO IYUNGA, KATA NA TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MTUHUMIWA NA VIJANA WENGINE WALIITOA BENDERA HIYO ILIYOKUWA JUU YA MTI NA KISHA KUICHANA KWA MADAI KUWA MTI HUO ULIOKUWA UMEFUNGWA BENDERA HIYO NI MALI YAO.
WATUHUMIWA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI LEO HII KUTOKANA NA MAKOSA HAYO.
MTEMBEA KWA MIGUU ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA AMBINISYE MWANDOBO (65) MKAZI WA KISEGESE ALIFARIKI DUNIA MUDA MFUPI BAADA YA KUFIKISHWA HOSPITALI YA MISSION ITETE KWA MATIBABU BAADA YA KUGONGWA NA PIKIPIKI ISIYOFAHAMIKA IKIENDESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA.
AJALI HIYO IMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 15:00 ALASIRI HUKO KATIKA KIJIJI CHA KISEGESE, KATA YA KISEGESE, TARAFA YA PAKATI, WILAYA YA RUNGWE, MKOA WA MBEYA. CHANZO CHA AJALI NI MWENDO KASI. MTUHUMIWA ALIKIMBIA NA PIKIPIKI MARA BAADA YA AJALI. UPELELEZI UNAENDELEA.
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA WATUMIAJI WA VYOMBO VYA MOTO KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO HIVYO IKIWA NI PAMOJA NA KUZINGATIA SHERIA/KANUNI/ALAMA NA MICHORO YA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.
KATIKA TUKIO LA TATU:
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAMSHIKILIA MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA AMANI JOHN @ MWAKASEGE KWA KOSA LA KUHARIBU MALI [KUCHANA PICHA] YA MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA MAPINDUZI.
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 14:30 MCHANA HUKO ILOMBA, KATA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MTUHUMIWA ALIONEKANA AKIWA AMEBEBA MABANGO YA PICHA ZA MGOMBEA WA URAIS HUKU YAKIWA YAMECHANWA VIPANDE VIPANDE NA NDIPO JITIHADA ZA KUMKAMATA ZILIFANYIKA NA KUMFIKISHA KATIKA KITUO KIDOGO CHA POLISI ILOMBA.
AIDHA KATIKA TUKIO JINGINE, MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FADI MWASHIMAHA ANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA KOSA LA KUHARIBU MALI [KUCHANA BENDERA YA CHAMA CHA MAPINDUZI].
TUKIO HILO LIMETOKEA MNAMO TAREHE 27.08.2015 MAJIRA YA SAA 12:00 MCHANA HUKO IYUNGA, KATA NA TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA.
INADAIWA KUWA, MTUHUMIWA NA VIJANA WENGINE WALIITOA BENDERA HIYO ILIYOKUWA JUU YA MTI NA KISHA KUICHANA KWA MADAI KUWA MTI HUO ULIOKUWA UMEFUNGWA BENDERA HIYO NI MALI YAO.
WATUHUMIWA WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI LEO HII KUTOKANA NA MAKOSA HAYO.
TAARIFA ZA MISAKO:
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATATU WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. NSAJIGWA BROWN (23) MKAZI WA ITUNGE 2. AHOBOKILE RUBEN (21) MKAZI WA ITUNGE NA 3. AYUBU CHURA (25) MKAZI WA BONDENI – WAKIWA NA BHANGI UZITO WA GRAM 25.
WATUHUMIWA YA WALIKAMATWA USIKU WA KUAMKIA LEO MAJIRA YA SAA 00:30 HUKO ENEO LA BONDENI, KATA YA KYELA, TARAFA YA UNYAKYUSA, WILAYA YA KYELA, MKOA WA MBEYA.
Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LINAWASHIKILIA WATU WATATU WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. NSAJIGWA BROWN (23) MKAZI WA ITUNGE 2. AHOBOKILE RUBEN (21) MKAZI WA ITUNGE NA 3. AYUBU CHURA (25) MKAZI WA BONDENI – WAKIWA NA BHANGI UZITO WA GRAM 25.
WATUHUMIWA YA WALIKAMATWA USIKU WA KUAMKIA LEO MAJIRA YA SAA 00:30 HUKO ENEO LA BONDENI, KATA YA KYELA, TARAFA YA UNYAKYUSA, WILAYA YA KYELA, MKOA WA MBEYA.
Imesainiwa na:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.




































No comments :
Post a Comment