Mwanaume anayetuhumiwa kuhusika na
tukio la mabomo katika mbio za marathoni za Boston mwaka 2013,
amekutwa na hatia ya mashtaka yote 30 yanayomkabili ambayo yanaweza
kumfanya akabiliwe na adhabu ya kifo.
Jopo la wazee wa mahakama ya
Massachusetts, wataamua iwapo mtuhumiwa huyo Dzhokhar Tsarnaev,
atapatiwa adhabu ya aina gani.
Watu watatu walikufa na wengine
zaidi ya 260 wamejeruhiwa wakati mabomu yalipolipuka katika eneo la
kumalizia mbio za marathoni Aprili 2013.
LIVERPOOL KUCHEZA NUSU FAINALI KOMBE LA FA NA ASTON VILLA APRIL 19' 2015
Wachezaji
wa timu ya Liverpool wakipongezana baada ya kuifunga Blackburn bao 1-0
na kufanikiwa kusonga mbele hadi hatua ya nusu fainali ya kombe la FA.
Mshambuliaji
wa Liverpool, Philippe Coutinho akikimbia kwa furaha mara baada ya
kuifungia timu yake bao 1-0 katika dakika ya 70 ya mchezo wa robo
fainali wa kombe la FA dhidi ya Blackburn, mchezo uliochezwa usiku wa
kuamkia leo katika uwanja wa Ewood Park.
Kwa matokeo hayo, Liverpool watacheza nusu fainali na Aston Villa,
mchezo utakaochezwa katika uwanja wa Wembley jumapili ya tarehe 19 April
2015.RWANDA YAADHIMISHA MIAKA 21 YA KUMBUKUMBU YA MAUAJI YA KIMBARI
Mgeni
rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dr. Harrison Mwakyembe
na Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Eugene Kayihura wakiwasha mishumaa
maalumu kuwakumbuka raia waliouwawa katika mauaji ya Kimbari.
Mratibu
Mkazi wa UN, Alvaro Rodriguez akizungumza katika Maazimisho ya Miaka 21
ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na
Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na Ubalozi wa Rwanda nchini Tanzania
yamefanyika leo ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Mgeni
rasmi Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dr. Harrison Mwakyembe
(wa pili kulia) akipata maelezo juu ya mwenendo wa mashauri toka ICTR
mara baada ya kuwasili kwenye Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Umoja
wa Mataifa kwa kushirikiana na Ubalozi wa Rwanda nchini Tanzania
yamefanyika leo ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam wakiwa
pichani.
Waziri
wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dr. Harrison Mwakyembe akizungumza
na wageni waalikwa katika Maazimisho ya Miaka 21 ya kumbukumbu ya mauaji
ya Kimbari. Maadhimisho hayo yaliyoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa
kushirikiana na Ubalozi wa Rwanda nchini Tanzania yamefanyika leo ukumbi
wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Rwanda nchini Tanzania, Eugene Kayihura akizungumza katika Maazimisho ya Miaka 21 ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari.
YANGA YAIFUNDISHA SOKA COASTAL UNION, YAIFUNGA 8-0, TAMBWE APIGA 'HAT TRICK'
Kiungo
wa Yanga, Salum Telela, akimiliki mpira mbele ya wachezaji wa Coastal
Union ya Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara
uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imeshinda 8-0. (Picha na Francis Dande).
uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Yanga imeshinda 8-0. (Picha na Francis Dande).
Simon Msuva akishangilia bao aliloifungia timu yake.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia.
Haruna Niyonzima akiruka kihunzi cha, Hamoud Abdulhalim.
Amis Tambwe akiwatoka wachezaji wa Coastal Union.
RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AYAPOKEA MATEMBEZI YA VIJANA YA KUMUENZI MZEE ABEID AMANI KARUME
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu
wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai wakati alipowasili katika viwanja vya
Ofisi Kuu Kisiwandui Mjini Unguja leo kupokea matembezi ya Vijana wa
Chama cha Mapinduzi katika kumuenzi Marehemu Mzee Abeid Amani
Karume,[Picha na Ikulu.] 
Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali
mbali wakati alipowasili katika viwanja vya Ofisi Kuu Kisiwandui Mjini
Unguja leo kupokea matembezi ya Vijana wa Chama cha Mapinduzi katika
kumuenzi Marehemu Mzee Abeid Amani Karume,[Picha na Ikulu.] 
Vijana
wa Chama cha Mapinduzi wakiwa katika matembezi ya kumuenzi Marehemu
Mzee Abeid Amani Karume wakiingia katika viwanja vya Ofisi Kuu ya CCM
Kisiwandui Mjini Unguja leo ambapo yatapokelewa na rasmi na Rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa
CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.] 
Vijana
wa Chama cha Mapinduzi wakibeba Picha la Rais wa Kwanza wa Zanzibar
Marehemu Mzee Abeid Amani Karume katika matembezi ya kumuenzi kiongozi
huyo yaliyoanzia Mwera na kumalizia katika viwanja vya Ofisi Kuu ya
CCM Kisiwandui Mjini Unguja leo ambapo yatapokelewa na rasmi na Rais
wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti
wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein,[Picha na Ikulu.] 
BALOZI SEIF AKUTANA NA BALOZI MDOGO MPYA WA INDIA, AWATAKA WAWEKEZAJI ZAIDI TOKA INDIA KUWEKEZA VISIWANI ZANZIBAR
Balozi
Mdogo Mpya wa India Hapa Zanzibar Bwana Satendar Kumar akisalimiana na
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Ofisini kwake
Vuga Mjini Zanzibar.
Balozi
Mdogo Mpya wa India Hapa Zanzibar Bwana Satendar Kumar akijitambulisha
rasmi kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi.
Balozi
Seif akibadilishana mawazo na Balozi Mdogo Mpya wa India Hapa Zanzibar
Bwana Satendar Kumar Ofisini kwake Mtaa wa Vuga Mjini Zanzibar.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akipokea zawadi kutoka kwa
Balozi Mdogo Mpya wa India Hapa Zanzibar Bwana Satendar Kumar.
Picha na – OMPR – ZNZ.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi ameyashauri
Makampuni na Taasisi za uwekezaji kutoka Nchini India kuwekeza miradi
yao katika Visiwa vya Unguja na Pemba ili kuitikia wito wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar wa kukaribisha wawekezaji mbali mbali kuwekeza
hapa Nchini .
Alisema India bado ina nafasi pana kwa Makampuni yake kuwekeza miradi yao ya Kiuchumi hasa katika Sekta ya Viwanda kama ilivyowahi kutumia fursa hiyo hapa Zanzibar katika miaka ya 80.
Akizungumza na Balozi Mdogo Mpya wa India hapa Zanzibar Bwana Satendar Kumar hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba Sekta ya Viwanda ni eneo muhimu katika kukuza uchumi na kupunguza Umaskini.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa na malengo la kuimarisha sekta hiyo kwa azma ya kulisaidia kundi kubwa la Vijana wasio na ajira ambalo limekuwa likiongezeka kila mwaka baada ya kumaliza masomo yao.
“ Ipo haja kwa wawekezaji wa Sekta ya Viwanda kutoka Nchini India kurejea tena Zanzibar kuwekeza miradi yao ya viwanda ili kusaidia uchumi wa Taifa pamoja na kupnguza wimbi la vijana wasio na ajira “. Alisema Balozi Seif.
Alisema India bado ina nafasi pana kwa Makampuni yake kuwekeza miradi yao ya Kiuchumi hasa katika Sekta ya Viwanda kama ilivyowahi kutumia fursa hiyo hapa Zanzibar katika miaka ya 80.
Akizungumza na Balozi Mdogo Mpya wa India hapa Zanzibar Bwana Satendar Kumar hapo Ofisini kwake Vuga Mjini Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema kwamba Sekta ya Viwanda ni eneo muhimu katika kukuza uchumi na kupunguza Umaskini.
Alisema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imekuwa na malengo la kuimarisha sekta hiyo kwa azma ya kulisaidia kundi kubwa la Vijana wasio na ajira ambalo limekuwa likiongezeka kila mwaka baada ya kumaliza masomo yao.
“ Ipo haja kwa wawekezaji wa Sekta ya Viwanda kutoka Nchini India kurejea tena Zanzibar kuwekeza miradi yao ya viwanda ili kusaidia uchumi wa Taifa pamoja na kupnguza wimbi la vijana wasio na ajira “. Alisema Balozi Seif.
VITA YA UGAIDI KENYA YAFUNGA KAMPUNI 13 ZA KUHAMISHA FEDHA
Serikali ya Kenya imeagiza kufungwa
kwa kampuni 13 za kuhamisha fedha ili kuzuia vikundi vya wapiganaji
wa Kiislam kutotumia kutuma fedha za kufanya mashambulio ya kigaidi.
Waziri wa Mambo ya Ndani Joseph
Nkaissery pia amesema Kenya imefunga akaunti za benki 86 za watu
binafsi pamoja na mali zao kushikiliwa.
Hatua hizo zinaaminika kuilenga
kampuni ya mabasi na hoteli inayodaiwa kuwa na uhusiano na kampuni ya
nchini Somalia.
REPARATIONS FOR THE 7TH EAC-EABC MEDIA SUMMIT IN HIGH GEAR
Dar is set to host the Premier EAC
Media Event on 14-15 May 2015
East African Community Headquarters,
Arusha, 8 April, 2015: The EAC Secretariat together with the East
African Business Council (EABC) and CEOs of Media Houses are
finalizing preparations for the 7th EAC-EABC Media Summit, which is
to be held from 14 to 15 May 2015, at the Hyatt Kilimanjaro Hotel Dar
es Salaam, Tanzania.
The 7th EAC-EABC Media Summit will
bring together over 250 Media owners, CEOs, Publishers, Editors,
prominent Media personalities and practitioners on a round table
discussions under the theme: The Role of the Media in Deeping
Democracy in the Region, with sub-themes on Democracy in the EAC:
Achievements and Challenges; The Role of Media in Electoral
Processes, and Regional Security, Business Environment and Media:
Towards a Common Goal.
“We see the Summit as a vehicle to
increase the visibility of EAC’s flagship in the integration
process and EAC-EABC joint activities through the media is
commendable,” comments Mr. Kajubi Mukajanga, Chair of the Regional
Preparatory Committee of the 7th Media Summit and also the Executive
Secretary of Media Council of Tanzania (MCT). “This will also be a
time to network with and update the Media industry on the latest
developments in the East African regional integration process,” he
said.
The Head of Corporate Communications
and Public Affairs at the EAC Headquarters Owora Richard Othieno
notes that the Media Summit is designed to, among others; advance the
relationship between the EAC/EABC and the media, who have long been
recognized as strategic partners for the Community in achieving its
key objective of deepening and widening regional integration and
development process.
Launching the EAC Media Scholarship
Fund sponsored by EAC-KfW-AKU, and announcing and recognizing Winners
of the EAC Media Award Competition 2013/14 are expected at the Media
Summit over a Gala Dinner.
ZAKHEM FC /FFU SC, KUSAKA BINGWA WA JUMLA MICHUANO YA LIGI YA MKOA DAR ES SALAAM
Baada ya kumalizika kwa michuano ya
ligi ya mkoa wa Dar es salaam na kupata timu tatu zitakazouwakilisha
mkoa katika michuano ya ligi ya mabingwa ya mikoa ya TFF,kesho
Alhamis Aprili 09/2015,katika uwanja wa Karume jijini kutakuwa na
mchezo wa fainali ya kumpata Bingwa wa jumla wa michuano ya ligi ya
mkoa.
Timu zitakazoumana katika fainali
hiyo ni ZAKHEM FC dhidi ya FFU SC,ambazo zitashuka dimbani majira ya
saa kumi jioni zikishuhudiwa na umati wa mashabiki waliokuwa
wakiyafuatilia mashindano hayo tangu yalipoanza kutimua vumbi.
Kwa mujibu wa kamati ya mashindano
ya chama cha soka mkoa wa Dar es salaam DRFA,timu zilizofanikiwa
kuuwakilisha mkoa katika michuano ya ligi ya maabingwa ni pamoja na
ZAKHEM FC,FFU SC na CHANGANYIKENI SC.
Mwenyekiti wa DRFA,Almas
Kasongo,ameipongeza kamati hiyo ya mashindano kwa kusimamia vizuri
uendeshaji wa ligi tangu ilipoanza.
Imetolewa na DRFA,
Mkuu wa kitengo cha Habari na
Mawasiliano DRFA
Omary
Katanga/+255766358585/+255784500028.
KUZIONA TWIGA, SHE-POLOPOLO TSH.2,000/=
Shirikisho
la Mpira wa Miguu nchini TFF limetangaza viingilio vya mchezo kati ya
timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) dhidi ya timu ya
Taifa ya Zambia (She-Polopolo) kiingilio cha juu sh.5,000 kwa VIP na sh.
2,000 kwa majukwaa yaliobakia, mechi hiyo itachezwa ijumaa jioni saa 10
kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Twiga Stars chini ya kocha mkuu Rogasian Kaijage imeendelea kujifua katika hosteli za TFF zilizopo Karume, kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo huo wa kuwnaia kufuzu kwa Michezo ya Afrika nchini Congo- Brazzavile mwezi Septemba mwaka huu.
Katika mchezo wa awali uliofanyika wiki tatu zilizopita jijini Lusaka nchini Zambia, Twiga Stars iliibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya wenyeji Zambia, hivyo katika mchezo wa ijumaa kuhitaji ushindi wa aina yoyote tu ili kuweza kufuzu kwa fainali hizo.
TFF inawaomba wapenzi, wadau na washabiki wa mpira wa miguu nchini, kujitokeza kwa wingi siku ya ijumaa jioni uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuja kuwapa sapoti Twiga Stars watakapokuwa wanapeperusha bendera ya Taifa.
Wakati huo huo, timu ya Taifa ya Wanawake ya Zambia (She-Polopolo) inatarajiwa kuwasili usiku wa saa 7.25 kuamkia alhmisi kwa shirika la Ndege la Ethiopia wakiwa na msafara wa wachezaji 18 na viongozi saba na watafikia katika hoteli ya Tansoma iliyopo eneo la Gerezani Kariakoo.
Msafara wa Zambia (She-Polopolo) unaongozwa na mkuu wa msafara Lenny Khuwa, kocha mkuu Albert Kachinga, kocha msaidizi Kape Saili, kocha wa magolikipa Yona Phiri, daktari wa timu James Nyimbili, mchua misuli Conerlia Chazura, na meneja wa timu ni Besa Chibwe.
Wachezaji wanaotarajiwa kuwasili ni Rachel Nachula, Annie Kibanji, Chiko Nkhoma, Osala Kaleo, Joana Benai, Meya Banda (Nahodha), Misozi CR Chisamu, Jane Nshika Chalwe, Milika Limwanya, Mary Wilombe, Grace Chanda, Barbra Banda, Memory Mwaseba, Hazel Natasha Nali, Martha Tembo, Mary Mwakapila na Ireen Lungu.
Kesho jioni She-Polopolo wanatarajiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa, uwanja ambao ndio utakaotumika kw amchezo huo.
Waamuzi wa mchezo huo kutoka nchini Uganda wanatarajiwa kuwasili leo mchana ambao ni Ms Anna Akoyi , Ms Nakkito Nkumbi , Ms Jane Mutonyi, na Ms Nabikko Ssemambo, Kamishina wa mchezo Ms Nomsa Jacobeth Mhalangu kutoka nchini Afrika Kusini anatarajiwa kuwasili leo jioni.
TFF YAMPONGEZA TENGA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF Jamal Malinzi, amempongeza Bw Leodgar Tenga kwa kuchaguliwa kuendelea kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
Aidha Rais Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa wajumbe waliochaguliwa kuwa wajumbe wapya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu baranai Afrika (CAF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA.
Katika salamu hizo na nakala zake kutumwa kwa Rais wa CAF Bw. Issa Haytou na Rais wa FIFA Bw. Blatter, Malinzi amewatakia kila la kheri katika majukumu hayo mapya,na kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa miguu duniani.
Tenga amechaguliwa nafasi hiyo baada ya kuwa mgombea pekee kutoka kanda ya Afrika Mashariki aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo na kuungwa mkono na nchi zote wanachama wa CECAFA.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
Twiga Stars chini ya kocha mkuu Rogasian Kaijage imeendelea kujifua katika hosteli za TFF zilizopo Karume, kuhakikisha inaibuka na ushindi katika mchezo huo wa kuwnaia kufuzu kwa Michezo ya Afrika nchini Congo- Brazzavile mwezi Septemba mwaka huu.
Katika mchezo wa awali uliofanyika wiki tatu zilizopita jijini Lusaka nchini Zambia, Twiga Stars iliibuka na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya wenyeji Zambia, hivyo katika mchezo wa ijumaa kuhitaji ushindi wa aina yoyote tu ili kuweza kufuzu kwa fainali hizo.
TFF inawaomba wapenzi, wadau na washabiki wa mpira wa miguu nchini, kujitokeza kwa wingi siku ya ijumaa jioni uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam kuja kuwapa sapoti Twiga Stars watakapokuwa wanapeperusha bendera ya Taifa.
Wakati huo huo, timu ya Taifa ya Wanawake ya Zambia (She-Polopolo) inatarajiwa kuwasili usiku wa saa 7.25 kuamkia alhmisi kwa shirika la Ndege la Ethiopia wakiwa na msafara wa wachezaji 18 na viongozi saba na watafikia katika hoteli ya Tansoma iliyopo eneo la Gerezani Kariakoo.
Msafara wa Zambia (She-Polopolo) unaongozwa na mkuu wa msafara Lenny Khuwa, kocha mkuu Albert Kachinga, kocha msaidizi Kape Saili, kocha wa magolikipa Yona Phiri, daktari wa timu James Nyimbili, mchua misuli Conerlia Chazura, na meneja wa timu ni Besa Chibwe.
Wachezaji wanaotarajiwa kuwasili ni Rachel Nachula, Annie Kibanji, Chiko Nkhoma, Osala Kaleo, Joana Benai, Meya Banda (Nahodha), Misozi CR Chisamu, Jane Nshika Chalwe, Milika Limwanya, Mary Wilombe, Grace Chanda, Barbra Banda, Memory Mwaseba, Hazel Natasha Nali, Martha Tembo, Mary Mwakapila na Ireen Lungu.
Kesho jioni She-Polopolo wanatarajiwa kufanya mazoezi katika uwanja wa Taifa, uwanja ambao ndio utakaotumika kw amchezo huo.
Waamuzi wa mchezo huo kutoka nchini Uganda wanatarajiwa kuwasili leo mchana ambao ni Ms Anna Akoyi , Ms Nakkito Nkumbi , Ms Jane Mutonyi, na Ms Nabikko Ssemambo, Kamishina wa mchezo Ms Nomsa Jacobeth Mhalangu kutoka nchini Afrika Kusini anatarajiwa kuwasili leo jioni.
TFF YAMPONGEZA TENGA
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF Jamal Malinzi, amempongeza Bw Leodgar Tenga kwa kuchaguliwa kuendelea kuwa mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika (CAF).
Aidha Rais Malinzi ametuma salamu za pongezi kwa wajumbe waliochaguliwa kuwa wajumbe wapya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu baranai Afrika (CAF) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA.
Katika salamu hizo na nakala zake kutumwa kwa Rais wa CAF Bw. Issa Haytou na Rais wa FIFA Bw. Blatter, Malinzi amewatakia kila la kheri katika majukumu hayo mapya,na kwa ajili ya maendeleo ya mpira wa miguu duniani.
Tenga amechaguliwa nafasi hiyo baada ya kuwa mgombea pekee kutoka kanda ya Afrika Mashariki aliyejitokeza kuwania nafasi hiyo na kuungwa mkono na nchi zote wanachama wa CECAFA.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)
WENGI WANUFAIKA NA SEMINA YA KILIMO NA UFUGAJI WA KISASA ILIYO ENDESHWA NA MJASIRIAMALI BI. MARY DAVID JIJINI DAR
Mmoja
wa wajasiliamali ambaye pia ni Mkulima na Mfugaji akichangia uzoefu
wake wa jinsi alivyo nufaika na mafunzo kama haya na mpaka sasa
anajitegemea na Kupata kipatochake na kuwasaidia wengine.
Wa
kwanza Kulia ni Stella mmoja wa akina dada ambaye amekuwa mfano mzuri
wa kuigwa katika semina hiyo akieleza ujuzi wake umuhimu wa mikutano
kama hii ambapo yeye anafanya kilimo cha Mpunga ambapo alianza na kuvuna
Gunia Mbili na sasa amefikisha mpaka Tani 100 na zaidi baada ya kupata
elimu Bora ya Kilimo.
Bwana Daniel Ambaye ni Mkulima na Mfugaji akichangia uzoefu wake katika maswala ya kilimo.
Mwendeshaji
msaidizi wa Semina Hiyo Bwana Saidi akitoa mafunzo ya juu ya kuanzisha
kilimo kwa kutumia Green House pamoja na faida zake















No comments :
Post a Comment