Friday, April 10, 2015

MKAPA ATOA SOMO JUU YA DIPLOMASIA YA UCHUMI KWA MAAFISA WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA WANAFUNZI WA CHUO CHA DIPLOMASIA

  Ngabwe Mlulu 

RAIS mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, (kulia), akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, akijibu maswali baada ya kutoa "somo" kwenye muhadhara ulioitishwa na wizara ya Mambo ya Nje, ambapo msemaji mkuu alikuwa Rais huyo mstaafu, na mada kuu ilikuwa "Demokrasia ya Uchumi, na takwa jipya la uchumi wa kimataifa. Rais Mkapa, alihadharisha juu ya taifa kuingia "kichwakichwa" kwenye mikataba ya kiuchumi na badala yake wizara ya Mambo ya Nje, inapaswa kuwa mshirika mkubwa katika kufukia mikataba mbalimbali ambayo nchi inaingia na mataifa ya kigeni hususan yaliyoendelea

Mkapa, aksilakiwa na waziri Membe, wakati akielekea ukumbini

Mkapa (katikati), waziri Membe, (kushoto) na balozi Rajab Gamaha

Waziri Membe, akitoa hotuba ya kumkaribisha Rais mstaafu Mkapa, ili atoe mada yake kwa waliohudhuria muhadhara huo

Baadhi ya wafanyakazi wa wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, na wanachuo kutoka chuo cha Diplomasia, wakimsikiliza Rais Mkapa







Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, (kushoto), akisaidiwa na mlinzi wake, kupanda ngazi kjuingia kituo kikuu cha polisi kati jijini Dar es Salaam mapema leo saa moja asubuhi, Aprili 9, 2015. Gwajima aliyefika kuitikia wito wa polisi kjumalizia mahojiano dhidi yake kufuatia kile kinachoelezwa kuwa ni kutoa maneno makali dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarpo Kadinali Pengo, mwishoni mwa mwezi uliopita. Taarifa kutoka kituo kikuu cha kati cha polisi zilizoifikia K-VIS Blog, zinasema, Gwajima alitoka kwenye kituo hicho majira ya saa 6 mchana, na kuwaambia waandishi wa habari kuwa, ameachiwa kwa dhamana yenye masharti kwamba, anatakiwa kuwasilisha nyaraka zinazoonyesha muundo wa uongozi wa kanisa, kueleza umiliki wa helikopta ya kanisa, hati za kanisa, na idadi ya makanisa aliyonayo, majina ya bodi ya wadhamini wa kanisa, idadi ya nyumba zinazomilikiwa na kanisa, na maelezo juu ya mpiga picha wa video wa kanisa 

 

GWAJIMA APEWA MASHARTI 10 YA DHAMANA IKIWEMO KUWASILISHA POLISI MFUMO WA UONGOZI WA KANISA LAKE

Ngabwe Mlulu 
Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, (kushoto), akisaidiwa na mlinzi wake, kupanda ngazi kjuingia kituo kikuu cha polisi kati jijini Dar es Salaam mapema leo saa moja asubuhi, Aprili 9, 2015. Gwajima aliyefika kuitikia wito wa polisi kjumalizia mahojiano dhidi yake kufuatia kile kinachoelezwa kuwa ni kutoa maneno makali dhidi ya Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Muadhama Polycarpo Kadinali Pengo, mwishoni mwa mwezi uliopita. Taarifa kutoka kituo kikuu cha kati cha polisi zilizoifikia K-VIS Blog, zinasema, Gwajima alitoka kwenye kituo hicho majira ya saa 6 mchana, na kuwaambia waandishi wa habari kuwa, ameachiwa kwa dhamana yenye masharti kwamba, anatakiwa kuwasilisha nyaraka zinazoonyesha muundo wa uongozi wa kanisa, kueleza umiliki wa helikopta ya kanisa, hati za kanisa, na idadi ya makanisa aliyonayo, majina ya bodi ya wadhamini wa kanisa, idadi ya nyumba zinazomilikiwa na kanisa, na maelezo juu ya mpiga picha wa video wa kanisa 

No comments :

Post a Comment